My Blog List

Sunday, April 27, 2008

HAPA NI WAPI?


Kama unajua hili ni jengo gani mjini Moshi sema.

MASALIA YA AJALI YA NDEGE



Haya ni masalia ya ndege ndogo iliyoanguka Moshi miezi kadhaa.

AJALI YA NDEGE - MOSHI

Nilikuwepo ndege ilipoanguka Moshi maeneo ya jirani na kiwanda cha mafuta BP. Watu wawili walipoteza maisha yao: Rubani (Mbongo) na Mzungu mmoja. Wengine wawili walijeruhiwa.Ilikuwa ni Januari mwaka huu.

VYOO VYA USWAHILINI

Hiki choo kimebomoka lakini kinatumika, ndio mambo ya walalaho wa kitanzania. Nusu kimetoboka na jamaa akija kujisevu hapa inabidi awe makini asije tumbukia.

HILI NALO BAFU


TUONE NA MABAFU YA KUOGEA YA MTANZANIA WA KAWAIDA

Mtanzania wa kawaida ambaye kwake maisha ni magumu na haoni vijisenti hata kidogo. Yeye huwa anaoga mahali kama hapa. Chini ni mchanga tu, hakuna mlango na ujenzi wa bafu ni makaratasi na magunia. Haya yakitokea, wengine wanakomba mafedha "vijisenti" na wala hawachukuliwi hatua. Wanalazimishwa kujiuzulu tu.

HEBU TUJIONEE VYOO VYA WATANZANIA

Hapo chini ni hali halisi ya vyoo vya mtanzania wa kawaida ambaye vijisenti kwake ni ndoto. Mambo ya uswahilini hayo.

Saturday, April 05, 2008

UFISADI HADI JESHINI UGANDA

Wakati ufisadi umetawala Tanzania,kule Uganda hakuna tena woga, mafisadi ambao zamani walikuwa jeuri sasa mkono wa sheria unawakumba. Kuna Jemedari wa jeshi sasa kawekwa jela kwa kosa la ufisadi jeshini. Hebu msome anavyojitetea dhidi ya ufisadi alioufanya.
Majenerali wengine wanaendelea kukanusha ufisadi. Wakati jeshi letu liko Comoro, Waganda nao wako Somalia na kuna tetesi za ufisadi zaidi jeshini.

Tuesday, April 01, 2008

MAJENERALI UGANDA MATUMBO MOTO

Kwa wale masekretary wa vibosile basi wajifunze ni jinsi gani kazi hiyo imejaa ufisadi kutoka kwa sekretary wa Museveni.
Kuna skandali kubwa dhidi ya maafsa wa jeshi la Uganda kwa kuajiri askari hewa: unalijua? Msome pia kinara wa skandali hilo Jenerali James Kazini, ni yule aliyewahi kushtakiwa na Umoja wa Mataifa kwa kuibia DRC rasilimali.