My Blog List

Thursday, November 17, 2005

KIROJA CHA MUSEVENI KUGOMBEA URAISI KWA MARA YA TATU

Haya wajameni, kumekucha hapa Uganda; kama nilivyoeleza mwanzon mwa wiki hii kulikuwa na vurugu sana ila mambo sasa ni shwari.
Leo nataka niwafahamishe kwamba sasa chama tawala hapa kimekuja na staili mpya yaani wajumbe wanajifanya wanamlazimisha Museveni agombee urais.Na yeye atauambia umma wa wananchi kwamba alilazimishwa: hiki ni kiroja cha karne.
Kwa ufupi Museveni kachukua fomu leo soma sasa sijui atarejesha au vipi lakini ndio hali halisi.

No comments: