My Blog List

Tuesday, December 09, 2008

TAMASHA LA MARIALE CUP LAMALIZIKA MOSHI


Timu ya Kaloleni United ya Kata ya Kaloleni katika Manispaa ya Moshi ambayo iliibuka kidedea jana na kushinda kikombe na ng'ombe katika uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi bao 1-0 dhidi ya Langasani ya Moshi Vijijini.
Nahodha wa Kilimanjaro Queen akipokea kikombe kwa kushinda netiboli katika tamasha la Chifu Mariale
Afisa Tawala wa Wilaya ya Moshi Manispaa akimkabidhi Kikombe Nahodha wa Kaloleni baada ya kushinda bao 1-0 timu ya Langasani kutoka Moshi Vijijini.

Monday, December 08, 2008

MIAKA 47 YA UHURU TANZANIA

Huku tukiwa tumetimiza miaka arobaini na saba ya uhuru, Tanzania ni nchi ambayo inaweza kujivunia mafanikio mengi sana ikilinganishwa na nchi nyingine za kiafrika. Ziko nchi nyingi ambazo zilipata uhuru wake miaka arobaini na saba iliyopita kama Tanzania ambazo kwa sasa ziko hoi kabisa katika nyanja nyingi na pia ziko zingine zimetuacha kabisa. Leo ninaitizama Tanzania ikisherehekea uhuru wake kwa mashaka makubwa sana.
Kama Taifa, naamini tumefanikiwa sana katika kudumisha na kujenga jamii ambayo ni ya amani tangu enzi za awamu ya kwanza, shukrani za pekee zimwendee Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Ila tuna tatizo kubwa ambalo kama litafanyiwa kazi basi uhuru wetu utakuwa na maana kubwa kwa wananchi wengi kwa ujumla kuliko ilivyo sasa. Nasema hivi kwasababu nasikitika sana kuwa jamii ya kitanzania kwa kiasi kikubwa imepotea njia.

Tuna tatizo kuu la “Utawala Bora” ambapo tumeshindwa kabisa kuweza kuiongoza nchi yetu kwa misingi ya kuzingatia uwajibikaji, uwazi, uadilifu na weledi. Hasahasa bado hatujaweza kujenga utamaduni wa Serikali kufanya kazi kwa kuheshimu taasisi (Institutions) zake zifanye kazi bila kuingiliwa na bwana mkubwa. Tatizo hili utaliona kila sekta ya utawala katika nchi yetu na ndio kitu cha pekee ambacho naamini kabisa kama tungaliweza kukishinda basi Tanzania tunayoisherehekea leo hii ya miaka arobaini na saba ingekuwa na mandhari na mielekeo mingine na mizuri kuliko hii tunayodhani ndio mafanikio leo hii.

Kiini kikuu cha kushindwa huku kwa “Utawala Bora” ni mfumo wetu wa elimu naamini una matatizo. Kwa maana nyingine utekelezaji wa sera ya elimu nadhani una mapungufu kiutendaji. Nchi yetu kwa miaka hii arobaini na saba ya uhuru inajivunia idadi kubwa tu ya wasomi kuanzia diploma, shahada, uzamili hadi maprofesa. Ila tatizo ni kwamba wasomi hawa ni wav yeti kuliko matendo. Ukitizama kuongezeka kwa kashfa nyingi za ubadhirifu na za kifisadi zinahusisha watu mbalimbali ambao ni wasomi sana tu.

Mfumo wetu wa elimu kwa kiasi kikubwa unatoa aina ya wataalamu wasio na haiba ya kuzingatia weledi (professionalism) katika utendaji wao wa kazi. Matokeo yake wasomi wengi wanaona ni afadhali wawe wanasiasa kuliko kufanya kazi ambazo wamezisomea. Ndio maana leo hii bunge letu limejaa wasomi lukuki lakini ukitizama na kusikiliza wanapojenga hoja mbalimbali bungeni unagundua kabisa kuwa kuna tatizo la ukosefu wa haiba ya kuhoji (critical) miongoni mwa wabunge wengi. Kwa ujumla, elimu yetu imetuzalishia viongozi na watendaji ambao ni watumwa wa fedha, tumbo na anasa za kila aina. Wao nchi haina nafasi kubwa sana bali maslahi binafsi ndio jambo la msingi.

Uhuru wa miaka arobaini na saba umeshindwa kutupatia mafanikio yanayoendana na muda huo kwa viongozi na wananchi kwa ujumla kushindwa kuwa na haiba ama hulka ya “kuwajibika”. Watu hawataki kukosolewa kabisa, hasa viongozi watendaji mbalimbali wa serikali na wanasiasa wao ndio mwisho wa kila kitu. Kwao mtu akijaribu kuwakosoa basi ni ‘mpinzani’ na anatishwa kuwa atapelekwa mahakamani kwa kumchafulia bwana mkubwa jina. Na ndio maana naweza kusema kuwa kwa kweli uhuru huu wa miaka arobaini na saba kama tusipokuwa makini naufananisha na hali ya kurudi nyuma (retrogressive) tangu tupate uhuru badala ya kwenda mbele(progressive).

Wakati tunasherehekea uhuru ni wakati wa wananchi kwa ujumla wao kuja na mtizamo mpya juu ya maendeleo kama kweli tunataka maendeleo ya nchi na wala si ya mtu binafsi. Lazima nikiri kuwa elimu yetu si bora kwani kwa kiasi Fulani imeshindwa kumfanya anayeipata kuweza kumudu maisha kwa njia za kawaida. Ni dhahiri mafisadi wengi ni watu wenye elimu bora tu lakini wengi wao wameamua kutumia njia za mkato kupata utajiri wa haraka kwa mvuto wa ubinafsi.

Kwa mfano hii hali ya kuongezeka kwa migomo na maandamano hapa nchini siku za karibuni ni kielelezo tosha kuwa kizazi cha viongozi wa sasa bado wameshindwa kuitizama Tanzania katika mtizamo wa kileo na pia kupambana na changamoto za kiutawala za kileo ama kisasa. Matokeo yake bado wanakuwa wagumu sana kukubali mfumo wa demokrasia ufanye kazi inavyotakiwa. Wanahakikisha wanadhibiti vyombo vya habari kwa kila hali ili visiandike baadhi ya habari ambazo wanatumia kisingizi cha usalama wa Taifa. Baadhi ya watawala bado hawajui ama wameamua kutokujali kuwa mfumo wetu wa kisiasa ni wa vyama vingi. Kwao “Chama kushika hatamu bado ndio mawazo na fikra zao”.

Pamoja na udhaifu mkubwa wa mfumo mzima wa kisiasa ambao bado ni mzigo mkubwa wan chi yetu hasa kwa kukosa utashi wa dhati kutekeleza maneno ambayo tunaimbiwa lakini lazima pia tuwaatizame wafanyakazi ama watumishi wa umma. Kwa miaka arobaini na saba ya uhuru, ni dhahiri wafanyakazi wa serikali ni mzigo sana. Nathubutu kusema kuwa serikali ni jamvi la uoza wote wa wafanyakazi wengi ambao hawana kazi za kufanya bali wanapokea fedha tu za bure. Serikali imejaza wafanyakazi wenye elimu haba katika kada mbalimbali ambao kwao hata umuhimu wa kufuata taratibu haupo kabisa. Ndio maana hata mara nyingi tunapopiga kelele kuwa wanasiasa ni mafisadi huwa ninapiga picha wafanyakazi wa umma napatwa na kichaa.

Umefika wakati serikali kama kweli inataka tuingie karne ya sayansi na teknolojia kwa uhakika basi hakuna sababu kuwa na wafanyakazi wasiohitajika katika shughuli zake katika maofisi mbalimbali. Umefika wakati wafanyakazi wahakikiwe uwezo wao kielimu yaani vyeti vyao vya taaluma mbalimbali. Nasema hivi kwani ukienda ofisi mbalimbali utakutana na wafanyakazi wasiojali kazi, wasio na uelewa wa umuhimu wa huduma kwa wateja, wasiokuwa na weledi katika utendaji wao na pia wasiojali kutunza muda. Napendekeza kwa miaka hii arobaini na saba ya uhuru basi serikali iwaondoe watu wa aina hii.

Mwisho kabisa, nampongeza Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na serikali nzima katika kuadhimisha siku hii muhimu kwa Taifa letu. Naamini nchi yetu iko katika wakati mgumu hasa katika vita dhidi ya ufisadi. Bado siamini sana kama kweli kuna utashi wa kisiasa katika mashtaka machache ambayo yameanza kushughulikiwa ila niseme tu ni wakati wa kuamua kikwelikweli kwa Raisi Jakaya Kikwete kutowahurumia baadhi ya maswahiba wake kama kweli anataka kusafisha nchi hii. Ni kwa mantiki hiyo tu ndio atakapoweza kunitoa mashaka pamoja na wengine ambao ni kama mimi.

Mungu Ibariki Tanzania.

Sunday, November 30, 2008

YONA ALIKUWA ANALIA


JE NA FIKRA MPYA ZA VIJANA WA KITANZANIA NI ZA KIPEMBUZI?


Katika mtizamo wangu juu ya mgongano wa fikra nchini Tanzania, leo naendeleza mtizamo wangu juu ya hizi fikra mpya ambazo kimsingi ni za kizazi cha vijana wa leo. Ninadhani kwa mtizamo wa mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma kadhaa hapa nchini ni wazi ni wakati tutizame kwa kina usahihi na uhalali wa kufikiri kwa kizazi hiki.

Moja, hoja kuwa sera ya bodi ya mikopo haifai na ifutwe sidhani kama itakuwa ndio suluhisho la matatizo katika sekta ya elimu ya juu. Vijana wa leo wanadhani kuwa ili wapate maslahi yao katika kila wanachostahiki kupata basi ni kwa kutumia njia za mkato. Wazungu wana msemo usemao: “It takes two to tangle”, na mara nyingine wanasema “Take it all approach”. Nadharia hizi mbili kwa vijana wetu hazipo kabisa. Wanachotaka kipengele cha kukopesha kiwe cha asilimia mia moja.
Kwao maadam ni fedha za serikali basi ni sawa na bure. Inatia mashaka sana unapoona hata wale wenye uwezo wa kulipa viwango katika madaraja mbalimbali kwa mujibu wa sera hiyo wanang’ang’ania wapewe asilimia yote. Kwa vijana hawa inawezekana kabisa wanajua maadam fedha ni za serikali basi kulipa si lazima kwani wamezoea jinsi wanavyoona fedha za serikali zinavyofisadiwa.
Hapa pananipa wasiwasi sana juu ya mtizamo wa vijana wetu hata hawaogopi kuingia kwenye mikopo. Yaani kwa mtu mwenye akili timamu sidhani atapenda kujiingiza katika mikopo ambayo itaathiri mipangilio yake ya baadaye. Niwakumbushe kuwa, mwandishi George Orwel aliwahi kuandika katika Animal Farm: “All Animals Are Equal, But Some Animals Are More Equal than Others”. Wanyama wote ni sawa, lakini baadhi ya wanyama ni sawa zaidi kuliko wengine. Ndio yanayojitokeza na mbinyo wao unaweza usiwe na mafanikio yoyote.

Pili, ni hili suala la kushinikiza kuwa serikali ina uwezo wa kulipa asilimia 100% ya mikopo hiyo. Sijui kama wanafunzi hawa wanajua kuwa kila kitu kinakwenda kwa bajeti. Na bajeti hupangwa mwaka wa serikali unapoanza. Je wanataka serikali ije na bajeti ndogo labda? Basi watoe mapendekezo pia ya juu ya nini kifanyike ili fedha hizo zipatikane kujazia zile zilizokuwa zimetengwa awali. Lakini si kwamba napinga mgomo wao, hii ni haki yao ya msingi lakini nataka nitoe changamoto kwao: Mosi, kama ni kweli kabisa kuna wanafunzi wanaopata mkopo kupitia ngazi (category) wasiyostahili na wanajulikana, je wamechukua hatua gani kuwasema?
Changamoto ya pili, kama kweli serikali yetu ina fedha nyingi za kutosheleza asilimia mia moja kwa wanafunzi, je vipi sekta nyingine za uchumi kama vile afya, miundo mbinu, usalama na ulinzi, kilimo na mifugo n.k, hizi nazo zina mapungufu ya fedha. Hizi nazo si muhimu kama wao wanafunzi? Na kama ni muhimu, kwa uchumi wetu wa Trilioni saba, tufanyeje kwa hili? Tupeleke fedha upande mmoja na sekta nyingine zisimame? Kama si “take it all mentality” hii ni nini? Nimejiuliza kuwa hata kama kuna ongezeko la ufisadi mwingi serikalini, kwa mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kuja na hoja eti fedha zote kwa asilimia mia moja zipelekwe kwenye ufadhili wa mikopo kwa wanafunzi wake. Si sahihi hata kidogo, kama si utoto.
Mgongano huu wa kifikra unalikumba taifa letu ni kielelezo cha kizazi kipya kilichojaa ubinafsi ambao kimeurithi kutoka miongoni mwa wazazi wao. Ni kizazi kinachopenda maendeleo ya haraka bila kuzingatia hatua za ukuaji (gradual) kutoka kiwango Fulani hadi kingine. Ninasema hivi kwani nadhani madai haya ya kulipwa asilimia mia moja bila kuwa na hoja toshelevu kushawishi na kushauri serikali ni wapi hiyo nakisi ya bajeti ya serikali na hata ile inayotengwa kwenye bodi ya mikopo basi vijana wetu wanakuwa kama vile wanaonesha jinsi gani ubinafsi na ushabiki ulivyotawala kizazi hiki kipya.
Jambo la tatu: nimejiuliza hivi inakuwaje sera inaonesha kuwa mtu atalipiwa mkopo kwa makundi kulingana na uwezo wa kifamilia na historia ya mwanafunzi. Hivi kama mtu ni mtoto wa tajiri, kigogo na hata mafisadi mwenye uwezo wake mwenyewe kujilipia analipiwa na bodi asilimia mia moja. Mtu huyu amejaza fomu ya mkopo kwa taarifa za uwongo kuanzia ngazi ya kijiji kwa mtendaji wa kijiji kumjazia baada ya kulipwa hongo. Mtu huyu huyu anajulikana na wanafunzi wenzake lakini hata siku moja hatusikii majina ya watu hawa yakifikishwa kwenye vyombo vya sheria. Vijana wanabaki kulalamika tu lakini hawatoi majina ambayo yangefanyiwa uchunguzi na wanaohusika waadhibiwe. Hili ni tatizo la jamii kulinda maovu, au kuwa na jamii yenye kuogopa kutoa habari za maovu kwa kukosa dhamira safi ya kuishi maisha safi kimaadili. Haiwezekani mtu anapiga kelele kuna watuhumiwa kibao lakini hatoi taarifa za watuhumiwa.
Nadhani pamoja na migomo kuwa na uhalali, tufike mahali tuamue kupenda ukweli wa kimaadili la sivyo tutagoma na kupoteza muda bila sababu. Kama jamii ya wanafunzi ikiamua kuwa watu wakweli kama vile wasomi wanavyotakiwa kuwa, basi naamini hili tatizo la watoto wa matajiri kulipiwa mikopo mikubwa wasiyostahili halitakuwepo. Unapogoma kuilazimisha serikali iwabane watoto wa matajiri wasipate mkopo wasiostahili alafu hauwataji, unataka serikali ifanye nini? Tujenge tabia ya kutaja uovu. Tabia hii ndio inayoua nchi yetu na hakuna shaka kwa kizazi hiki kipya, ule mhimili mzima wa kimaadili wa kitaifa unamomonyoka kwa tabia ya watu kupenda kulalamika bila kuwa na majibu yenye mantiki. Asilimia mia moja si jibu sahihi, ila kufuata maadili mema (prudence) kutatusaidia.
Jambo la nne, kwa hali ilivyo mtizamo wan chi yetu eti kwa kuwa wazee wetu walisomeshwa bure na Nyerere basi ni haki kwa vijana wa leo wasome kwa mikopo ya asilimia mia moja. Hii inanipa wasiwasi kama kweli vijana wetu watarudisha mkopo huu. Kwanini wanajenga hoja hii ambayo ni ya mkopo na kuifananisha na kusoma bure kwa wazazi wao? Kimantiki, wanatumia hoja ya “deduction” kwa kuegemea matokeo ya tukio la kwanza basi na linalofuata nalo liende kwa muelekeo huo huo. Wanasahau historia inabadilika, utekelezaji wa mambo mbalimbali unabadilika, mifumo ya kidunia (World Order) nayo inabadilika, n.k.
Naamini umefika wakati kwa watanzania kwa ujumla wao kutambua ilivyo gharama kusomesha watoto wao na hii habari ya kujizalia bila mpango na bila kuzingatia kipato kwa dunia ya leo ni kuzalisha jamii ambayo itachanganyikiwa na changamoto za kisasa. Kama wewe ni masikini basi kuwa na watoto wachache utakaowamudu kwani sidhani kama kweli tuko katika kipindi ambacho serikali itafanya kila kitu ambacho ni wajibu wa mzazi kwa asilimia mia moja. Serikali isaidie mayatima na watu wa makundi maalum tu.
Mwisho nimeshangazwa kuna vijana wengine wamegoma eti ratiba ya mitihani ibadilishwe. Kuna hatari vijana wetu ni wavivu sana na wanataka kila kitu kifanywe watakavyo. Tusipoangalia ndio hawahawa watakuja kuondoa hata baadhi ya masomo ama kozi kadhaa kwa kisingizio ni ngumu. Ni kizazi kisichozingatia muda wala taratibu. (Laissez Faire). Siamini eti kwa elimu ya Chuo Kikuu kufanya mitihani miwili kwa siku kutachangia mwanafunzi kufeli. Kama ni hivyo basi kuna hatari juu ya upokeaji mafunzo kwa wasomi wetu wapya.
Pamoja na uwezekano mkubwa wa mapungufu kwa migomo hii ya wanafunzi, jambo moja la msingi kwa kizazi cha sasa kufanya ni kufanya utafiti wa kina wakati wa kuandaa madai. Kama utafiti wa kina umefanyika ama ulifanyika basi hii serikali kutoa kauli isiwe ndio mwisho wa madai. Ni lazima waje na mkakati wa kuendeleza madai ambao ni imara wenye mbinyo(pressure) na hamasa (vitality) inayoambatana na utambuzi halisi wa kile wanachokidai. Si kuja na madai nusunusu ambapo hata majina ya wale wote wanaofaidika na mikopo hawako tayari kuyatoa. Bila haya niliyoyataja, nadhani kwa mtu makini inakuwa vigumu kushawishika kuwaunga mkono na hata kuwaamini vijana wa vyuo vikuu.
Kwa kumalizia, nina wasiwasi kama vijana wetu vyuo vikuu wanajifunza namna ya kufikiri kimantiki. Ipo haja somo la mantiki (logic) na hata maadili (morality) lifunzwe kwa wanafunzi wote. La sivyo tutaendelea kushuhudia aibu hii ya matumizi mabaya ya fikra.

Tuesday, November 25, 2008

MAWAZIRI WAANDAMIZI WATUHUMIWA UFISADI KUTOKA KILIMANJARO


Hatimaye JK kaanza kuonesha kuwa hacheki na kima. Jamaa anaanza kutupelekea mahakamani watuhumiwa mawaziri waandamizi katika wizi na kukuza umasikini Tanzania. Pichani juu ni mawaziri Daniel Yona na Bazil Pesambili Mramba ambao leo wamefikishwa kizimbani.
Wamesomewa mashtaka ya kufanya maamuzi bila kujali maslahi ya nchi na wanatakiwa watoe dhamana ya shilingi Bilioni 3.9 kila mmoja. Je watatoa dhamana hiyo?

Je hapa ndio gemu la JK limeanza? Mie sitaki kusapoti sana manake najua hawa jamaa watakuwa nje tu baada ya siku chache kwani walishaiba hela nyingi sana. Na kama watatoka kwa kuweza kumudu dhamana basi namuunga mkono rafiki yangu mmoja aliyesema Tanzania iondolewe katika kundi la nchi Masikini sana duniani. Tutajua jinsi nchi yetu ilivyotajiri sana.

Monday, November 24, 2008

ROSE KABUYE NA UKATILI WA WAZUNGU

Ufaransa ina visa na serikali ya Kagame, na hapa ndipo wameamua kumkamata Bi. Rose Kabuye.
Je ni kweli Rose Kabuye alishiriki kumuua Raisi Kagame?

Monday, November 17, 2008

WAAFRIKA TULIVYO WATU WA MIZENGWE

Kumbe Obama angelikuwa anagombea Africa asingelishinda? Unajua kwanini? Pia hebu ona jinsi ambavyo Obama alivyotimiza ndoto za Martin Luther.

Kwa ushindi wa Obama tunajifunza kuwa siasa pia ni sifa za mgombea si fedha tu na umaarufu wa mtaani na kishabiki.

KIZAZI KIPYA vs KIZAZI CHA ZAMANI TANZANIA

TANZANIA KATIKA MGONGANO WA KIFIKRA (1)

Je fikra kongwe zinatufaa?

Mwaka huu nchi yetu imeshuhudia ongezekao kubwa la migomo katika sekta na hata rika mbalimbali za raia: kuanzia watoto, watu wazima na hata wazee. Sidhani ni kawaida kwa watoto kugoma kudai haki zao ila kwa yanayotokea basi ni wazi kuna tatizo katika utawala na mfumo mzima wa maisha ya watanzania.

Labda nieleze kimtizamo binafsi jinsi ambavyo naamini nchi yetu sasa imepotea njia na kuna watu makini fulani ambao wameamua kusitisha hii hali ya bora liende. Kama raia na mtanzania ninayefuatilia mabadiliko kadhaa kadri yanavyotokea kwa miongo kadhaa, nathubutu kusema kuwa kwa sasa tumefikia wakati muafaka wa mabadiliko (turning point).

Tangu Tanzania ipate uhuru wake mwaka 1961, nchi yetu imeongozwa na kizazi cha wananchi ambao wengi wao sasa ni wazee na wanakaribia kukosa nguvu za kufanya kazi kwa umakini. Nchi yetu kwa ujumla bado haijatoka mikononi mwa viongozi waliopigania uhuru wa nchi yetu wala bado haijatoka mikononi mwa wale wote waliokuwa ndio vijana wakati wa uhuru. Hapa nazungumzia raia wenye umri wa kuanzia miaka hamsini na kuendelea.

Ni kwa mtizamo huo ndio maana nchi yetu imechoka kifikra na ni wakati wa kizazi ambacho si cha uhuru kuichukua nchi na kuipeleka na kuiongoza kwa kuzingatia mahitaji ya wakati. Kwani ni wazi kuwa kwa sasa bado nchi yetu iko katika lepe la usingizi kutokana na kuongozwa na sera, mitizamo na falsafa za kizamani zisizozingatia alama za nyakati. Ninapoona vijana wa vyuo vikuu wanagoma karibu nchi nzima kwa madai ya kutaka serikali yao iwakopeshe fedha za masomo kwa asilimia mia moja lakini wanaonekana ni wakosaji basi ninapata picha kuwa viongozi wetu wamedumaa kifikra.

Kuduma huku kifikra kunaweza kukaelezewa katika mitizamo hii:

Moja, viongozi wetu, inawezekana kabisa mawaziri husika wanadhani kwa kijana mtu mzima wa leo inamuingia akilini eti kuambiwa kuwa serikali haiwezi kusomesha kwa kuwakopesha vijana ili wapate elimu atakuelewa? Mimi binafsi siamini kuwa haiwezekani ila kwasababu viongozi wetu kutokana na mtizamo wa kizazi chao, kwao fedha za umma ni kwa ajili ya kulipana posho, kununua magari ya kifahari yasiyo na ulazima, kufanya starehe na vimwana na mambo mengine mengi yasiyo na maslahi kwa nchi kwa ujumla wake.

Pili, kizazi cha viongozi wetu, yaani wale ambao ni sawa na wazazi wangu wana tatizo kubwa sana la kutopenda mabadiliko. Wako katika kutekeleza ndoto zao za utotoni ambapo inawezekana yale ambayo walikuwa wameyapanga kufanya ukubwani ni lazima wayatimize bila kuzingatia nyakati. Ni wazi, kizazi cha viongozi tulionao hapa Tanzania kwa leo wengi wao si watu wanaojali “KUFIKIRI” yaani matumizi ya akili na ubongo katika kila jambo wanalofanya. Kwao mtu ukifikiri (reasoning) basi hutaweza kuishi kwa raha kwani kwao matakwa ya utashi wa mtu binafsi ama kikundi ndio jambo la msingi zaidi. Kwao mtizamo wa majumuisho (inclusive) haupo kabisa na ndio maana unaona hata wanadiriki kufunga vyuo badala ya kutatua tatizo kwa majadiliano kwa kuzingatia (due process) ambapo pande zote mbili zitasikilizana na kila upande upate keki yake.

Tatu, kizazi cha viongozi wetu kina tatizo la wengi wa viongozi kutokuwa na sifa kabisa za kuwa viongozi wa jamii ya kisasa. Wengi wao hawakuwahi kupata elimu iliyokamilika; yaani walipikika nusu (half cooked), na ndio maana kwao kuwa kiongozi si utumishi bali ni ubabe. Kwao kiongozi lazima awe na nguvu za kutisha ili aweze kutekeleza majukumu yake. Hii yote inasababishwa na wengi wao walisomea uongozi katika zile enzi za ukomunisti na ujamaa ambapo kiongozi alifundwa kuwa kama Mfalme. Kwao kiongozi anapozungumza basi ni amri, hapewi wazo mbadala, hakubali changamoto wala hawana muda wa kuzingatia hoja za upande mwingine. Kwao hoja zao ndio mwisho. Ni tatizo kubwa sana na ndio maana utaona haya mamigomo yanaongezeka kila kukicha.

Nne, viongozi wetu tulionao leo wengi wao hawana tabia ya uwazi (transparency). Yaani kwao kila kitu kinachohusu umma ni siri ya ofisi. Mambo ya umma hasa yanayogusa masuala ya fedha hayashirikishi wananchi wala wadau. Ni siri ya ofisi na ndio maana hata sasa utawasikia wakisema kuwa serikali haina fedha za kuwakopesha vijana ili wasome kama wao walivyosoma bure enzi zao.

Tano, viongozi wengi tulionao si watu wanaoendesha mambo kwa kupanga (planning) na ndio maana hata kwenye uongozi hakuna mipango thabiti ambayo inazingatia jamii kwa tija tarajiwa. Mambo ni bora liende; nitoe mfano tu wa familia za baadhi ya mabwana zetu hawa: wengi wao wana familia kubwa sana ambazo ni mzigo sana kwao. Hapa nazungumzia mke zaidi ya mmoja pamoja na vimada pamoja na ndugu wa karibu (extended family).

Njia pekee kwao kuhakikisha watoto wao wanasoma na kuajiriwa ni kufanya ufisadi wa kila aina ili waweze kumudu matunzo ya watoto wao wengi pamoja na wake zao pamoja na vimada kibao maofisini mwao. Utaona moja kwa moja viongozi wetu wana shinikizo la kifamilia ambalo limebinya akili zao katika kuwatumikia wanachi inavyotarajiwa. Yote hii wataalam wanaita “Poor Planning” ambayo inaanzia majumbani mwao na kuhamia kule wanakokutumikia.

Unapoona migomo inaongezeka basi ujue kuwa tatizo lingine ni serikali kujaza watendaji wasiokuwa na sifa za kitaaluma katika taasisi na idara zake. Kwa mfano, kwanini walimu wanadai madai yao ya muda mrefu? Jibu ni kuwa uhakiki unaendelea. Mimi nashangaa hivi kama kweli walimu wote wa serikali wameajiriwa na orodha na taarifa zao zimehifadhiwa katika mfumo wa kompyuta, kwanini tupate shida kuwahakiki? Ina maana huko wanakohakikiwa, kazi zinafanyika bora liende? Inakuwaje tusubiri mpaka watu wagome ndio tuanze kugundua mapungufu?

Yote hii ni kuwa hizo idara za uhakiki zipo lakini hazifanyi kazi. Na kwa kuongezea, kuna walimu wengi ambao ni marehemu ama waliacha kazi lakini bado wanaendelea kulipwa. Ninaamini kwa kizazi cha viongozi tulionao ambao wao kupendeleana na kuendesha mambo kwa kulindana ndio jadi yao, basi inawezekana kabisa fedha nyingi zinalipa watu hewa kama wafanyakazi halali. Hizi ni fedha ambazo zingeweza kupelekwa kulipa walimu na hata wanafunzi wanaoomba asilimia mia moja ya mikopo.

Liko tatizo kuu ambalo naweza kusema ndio kiini cha ukihiyo wa wengi wa viongozi wetu ambao wengine wana elimu kubwa sana lakini wameshindwa kuitumia. Hapa kuna mambo mawili:

La kwanza ni siasa, ambapo kwa kizazi cha viongozi tulichonacho leo hii kwao maisha hayana maana au hayawezi kuendelea kama Chama Chao kinakosolewa. Hapa nazungumzia hata baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani mkondo ni uleule kama wataingia madarakani. Kwao chama ni chombo kisafi na hakijawahi kuchafuka. Kwao chama lazima kitetewe kwa hali yoyote ile kwani ndio chombo kinacholinda maisha yao. Kwao masuala muhimu ya nchi lazima yazingatie mtizamo wa mteuliwa kwa chama cha siasa. Hata kama mteuliwa ni mbumbumbu maadam anaunga mkono chama chao basi atapewa hata nafasi ambayo ni zaidi ya mteuliwa. Viongozi hawa pia ajira huzingatia urafiki, undugu, uswahiba na mara nyingi tu ni watu wanaotumia ngono katika kuajiri na kuwapa vyeo akina mama. Yaani viongozi wetu wengi imani kuwa Uongozi ni Utumishi kwa Umma ni kiini macho. Kwa viongozi hawa, kwao maslahi ya Chama ni muhimu kuliko Taifa na Umma kwa ujumla wao.

Ni katika mtizamo huu ndio maana sishangai kila panapotokea uchaguzi utawaona wanalazimisha mbinu chafu ili washinde uchaguzi hata kwa kutumia vyombo vya usalama. Na kwasababu hata vyombo vya usalama vimejaa wateule baadhi ambao ni mbumbumbu ila tu mashiko ya chama ndio mbele basi huwatumikia na matokeo yake Taifa linaendelea kubaki kwenye migogoro na migomo isiyokwisha. Viongozi wa aina hii ni wengi sana serikalini na hata ukisema leo tufanye uhakiki wav yeti vyao vya elimu katika ngazi mbalimbali utashangaa hawatakubali manake itashangaza.

Jambo la pili ni kupenda demokrasia ya tumboni (democracy of the belly) ambapo kwao wanachowaza ni fedha tu hata kama hamna tija. Kwa maana nyingine hawa ni wabinafsi sana, wanajipenda kupita kiasi. Ndio maana utashangaa wanakataa watoto wa masikini wasipate mkopo wa asilimia mia moja lakini watoto wao inawezekana kabisa wanasomeshwa kwa asilimia mia moja tena na fedha za umma kwa njia ya mlango wa nyuma. La kushangaza zaidi wengi wa viongozi wetu wanajua tiba ya matatizo ya migomo leo hii lakini kwa makusudi kabisa hawataki kuleta mabadiliko. Wanajua kuwa chakula chao kitapungua na kamwe hawatakubali sera ya mikopo ibadilishwe.

Mwisho, baada ya kuona aina ya viongozi tulionao hapo juu kama tatizo la nchi yetu ni wazi kuwa vijana wana nafasi ya pekee kuhakikisha wanalazimisha mabadiliko. Lazima vijana wasimame imara kuhakikisha kuwa serikali inabadili sera yake ya mikopo kwa elimu ya juu. Kama vijana watashindwa kwa hili basi nasema kabisa kuwa hii ni nafasi ya pekee ambayo haipaswi kuachwa la sivyo itakuwa “Missing opportunity” ambayo haitakaa ijirudie tena.

Ni wakati wa kuwafanya viongozi wetu waelewe kuwa kisingizio cha serikali haina fedha hakina mashiko tena. Ikiwezekana muwashauri waondoe bajeti ya mambo mengi ambayo hayana msingi yanayotumia fedha nyingi bila sababu za msingi. Msipofanya hili mjue Taifa letu litaangamia kabisa na mtawapa mwanya mwingine wa kuwaruhusu baadhi ya viongozi wetu kuendelea kufuja mali za umma wao na familia pamoja na marafiki zao.

Taifa liko kwenye mgongano wa kifikra: yaani kati ya Fikra kongwe za wale wote wenye umri wa miaka hamsini na kuendelea wakisigishana na Fikra mpya za wote walio chini ya umri wa miaka hamsini. Wengi wa viongozi wetu, kwa umri wao hawajatimiza ndoto zao za utotoni sasa ndio maana utaona wanafuja. Wengi wao elimu yao ni wasiwasi sana na ndio maana utaona wanaweka mbele sana masuala ya kuwa na vyeo pasipo elimu stahili inayoendana na mabadiliko ya dunia ya kileo. Katika hali hii nategemea vijana waongeze mbinyo la sivyo hawa jamaa wametuteka sisi wengine kama jamii.

Ili tusiendelee kuwa mateka wa watu wachache ndani ya Taifa huru, natoa rai kuwa vijana wote pamoja na wazee wote wenye mapenzi mema kwa Taifa letu wahakikishe wanaweka mbinyo (pressure) ili kuhakikisha nchi yetu haiendi kuzimu. Migomo iendelee kama viongozi wetu wataendeleza vitisho badala ya kushirikisha wadau pale panatokea hali ya sintofahamu katika masuala mbalimbali.

Saturday, November 08, 2008

KWANINI MUSEVENI ANAKINGIA MAFISADI KIFUA?

Niliwagusia jinsi gani Museveni anavyotumia mbinu za vyama tawala na dola katika kuwahifadhi mafisadi. Hebu ona jinsi gani alijaribu na akafanikiwa kuwakingia kifua mawaziri wake wawili mafisadi. Pia kuna sababu mbalimbali zilizopo nchini Uganda ni kwanini Museveni anahakikisha lazima hawa mabwana wasafishwe.
Si hayo tu, ila kwa wanaoelewa huu mchezo wa Museveni ni kwamba kwa sasa watu ambao wanatarajiwa kumrithi Urais wamebaki mmoja tu baada ya mmojawapo kuwa kati ya hawa mawaziri fisadi wawili.

HOTUBA YA OBAMA KUSHUKURU KUCHAGULIWA

Nimeona ni vyema niweka hii hotuba ili muisome na kuona Obama alisema nini:
Obama victory speech: 'This is your victory'
President elect Barack Obama has addressed supporters in Chicago after beating John McCain to become the next US president. Below is the speech.
Obama:
Hello, Chicago.
If there is anyone out there who still doubts that America is a place where all things are possible, who still wonders if the dream of our founders is alive in our time, who still questions the power of our democracy, tonight is your answer.
It's the answer told by lines that stretched around schools and churches in numbers this nation has never seen, by people who waited three hours and four hours, many for the first time in their lives, because they believed that this time must be different, that their voices could be that difference.
It's the answer spoken by young and old, rich and poor, Democrat and Republican, black, white, Hispanic, Asian, Native American, gay, straight, disabled and not disabled. Americans who sent a message to the world that we have never been just a collection of individuals or a collection of red states and blue states.
We are, and always will be, the United States of America.
It's the answer that led those who've been told for so long by so many to be cynical and fearful and doubtful about what we can achieve to put their hands on the arc of history and bend it once more toward the hope of a better day.
It's been a long time coming, but tonight, because of what we did on this date in this election at this defining moment change has come to America.
A little bit earlier this evening, I received an extraordinarily gracious call from Sen. McCain.
Sen. McCain fought long and hard in this campaign. And he's fought even longer and harder for the country that he loves. He has endured sacrifices for America that most of us cannot begin to imagine. We are better off for the service rendered by this brave and selfless leader.
I congratulate him; I congratulate Gov. Palin for all that they've achieved. And I look forward to working with them to renew this nation's promise in the months ahead.
I want to thank my partner in this journey, a man who campaigned from his heart, and spoke for the men and women he grew up with on the streets of Scranton and rode with on the train home to Delaware, the vice president-elect of the United States, Joe Biden.
And I would not be standing here tonight without the unyielding support of my best friend for the last 16 years the rock of our family, the love of my life, the nation's next first lady Michelle Obama.
Sasha and Malia I love you both more than you can imagine. And you have earned the new puppy that's coming with us to the new White House.
And while she's no longer with us, I know my grandmother's watching, along with the family that made me who I am. I miss them tonight. I know that my debt to them is beyond measure.
To my sister Maya, my sister Alma, all my other brothers and sisters, thank you so much for all the support that you've given me. I am grateful to them.
And to my campaign manager, David Plouffe, the unsung hero of this campaign, who built the best -- the best political campaign, I think, in the history of the United States of America.
To my chief strategist David Axelrod who's been a partner with me every step of the way.
To the best campaign team ever assembled in the history of politics you made this happen, and I am forever grateful for what you've sacrificed to get it done.
But above all, I will never forget who this victory truly belongs to. It belongs to you. It belongs to you.
I was never the likeliest candidate for this office. We didn't start with much money or many endorsements. Our campaign was not hatched in the halls of Washington. It began in the backyards of Des Moines and the living rooms of Concord and the front porches of Charleston. It was built by working men and women who dug into what little savings they had to give $5 and $10 and $20 to the cause.
It grew strength from the young people who rejected the myth of their generation's apathy who left their homes and their families for jobs that offered little pay and less sleep.
It drew strength from the not-so-young people who braved the bitter cold and scorching heat to knock on doors of perfect strangers, and from the millions of Americans who volunteered and organized and proved that more than two centuries later a government of the people, by the people, and for the people has not perished from the Earth.
This is your victory.
And I know you didn't do this just to win an election. And I know you didn't do it for me.
You did it because you understand the enormity of the task that lies ahead. For even as we celebrate tonight, we know the challenges that tomorrow will bring are the greatest of our lifetime -- two wars, a planet in peril, the worst financial crisis in a century.
Even as we stand here tonight, we know there are brave Americans waking up in the deserts of Iraq and the mountains of Afghanistan to risk their lives for us.
There are mothers and fathers who will lie awake after the children fall asleep and wonder how they'll make the mortgage or pay their doctors' bills or save enough for their child's college education.
There's new energy to harness, new jobs to be created, new schools to build, and threats to meet, alliances to repair.
The road ahead will be long. Our climb will be steep. We may not get there in one year or even in one term. But, America, I have never been more hopeful than I am tonight that we will get there.
I promise you, we as a people will get there.
There will be setbacks and false starts. There are many who won't agree with every decision or policy I make as president. And we know the government can't solve every problem.
But I will always be honest with you about the challenges we face. I will listen to you, especially when we disagree. And, above all, I will ask you to join in the work of remaking this nation, the only way it's been done in America for 221 years -- block by block, brick by brick, calloused hand by calloused hand.
What began 21 months ago in the depths of winter cannot end on this autumn night.
This victory alone is not the change we seek. It is only the chance for us to make that change. And that cannot happen if we go back to the way things were.
It can't happen without you, without a new spirit of service, a new spirit of sacrifice.
So let us summon a new spirit of patriotism, of responsibility, where each of us resolves to pitch in and work harder and look after not only ourselves but each other.
Let us remember that, if this financial crisis taught us anything, it's that we cannot have a thriving Wall Street while Main Street suffers.
In this country, we rise or fall as one nation, as one people. Let's resist the temptation to fall back on the same partisanship and pettiness and immaturity that has poisoned our politics for so long.
Let's remember that it was a man from this state who first carried the banner of the Republican Party to the White House, a party founded on the values of self-reliance and individual liberty and national unity.
Those are values that we all share. And while the Democratic Party has won a great victory tonight, we do so with a measure of humility and determination to heal the divides that have held back our progress.
As Lincoln said to a nation far more divided than ours, we are not enemies but friends. Though passion may have strained, it must not break our bonds of affection.
And to those Americans whose support I have yet to earn, I may not have won your vote tonight, but I hear your voices. I need your help. And I will be your president, too.
And to all those watching tonight from beyond our shores, from parliaments and palaces, to those who are huddled around radios in the forgotten corners of the world, our stories are singular, but our destiny is shared, and a new dawn of American leadership is at hand.
To those -- to those who would tear the world down: We will defeat you. To those who seek peace and security: We support you. And to all those who have wondered if America's beacon still burns as bright: Tonight we proved once more that the true strength of our nation comes not from the might of our arms or the scale of our wealth, but from the enduring power of our ideals: democracy, liberty, opportunity and unyielding hope.
That's the true genius of America: that America can change. Our union can be perfected. What we've already achieved gives us hope for what we can and must achieve tomorrow.
This election had many firsts and many stories that will be told for generations. But one that's on my mind tonight's about a woman who cast her ballot in Atlanta. She's a lot like the millions of others who stood in line to make their voice heard in this election except for one thing: Ann Nixon Cooper is 106 years old.
She was born just a generation past slavery; a time when there were no cars on the road or planes in the sky; when someone like her couldn't vote for two reasons -- because she was a woman and because of the color of her skin.
And tonight, I think about all that she's seen throughout her century in America -- the heartache and the hope; the struggle and the progress; the times we were told that we can't, and the people who pressed on with that American creed: Yes we can.
At a time when women's voices were silenced and their hopes dismissed, she lived to see them stand up and speak out and reach for the ballot. Yes we can.
When there was despair in the dust bowl and depression across the land, she saw a nation conquer fear itself with a New Deal, new jobs, a new sense of common purpose. Yes we can.
When the bombs fell on our harbor and tyranny threatened the world, she was there to witness a generation rise to greatness and a democracy was saved. Yes we can.
She was there for the buses in Montgomery, the hoses in Birmingham, a bridge in Selma, and a preacher from Atlanta who told a people that "We Shall Overcome." Yes we can.
A man touched down on the moon, a wall came down in Berlin, a world was connected by our own science and imagination.
And this year, in this election, she touched her finger to a screen, and cast her vote, because after 106 years in America, through the best of times and the darkest of hours, she knows how America can change.
Yes we can.
America, we have come so far. We have seen so much. But there is so much more to do. So tonight, let us ask ourselves -- if our children should live to see the next century; if my daughters should be so lucky to live as long as Ann Nixon Cooper, what change will they see? What progress will we have made?
This is our chance to answer that call. This is our moment.
This is our time, to put our people back to work and open doors of opportunity for our kids; to restore prosperity and promote the cause of peace; to reclaim the American dream and reaffirm that fundamental truth, that, out of many, we are one; that while we breathe, we hope. And where we are met with cynicism and doubts and those who tell us that we can't, we will respond with that timeless creed that sums up the spirit of a people: Yes, we can.
Thank you. God bless you. And may God bless the United States of America.

JANET MUSEVENI MWANAMAMA SHUJAA?


Huko Uganda kuna skandali kubwa juu ya ufisadi wa mawaziri wawili ambao ni watu wa karibu wa Bwana Museveni. Jamaa kaamua lazima wasafishwe na wabunge wa chama tawala hivyo akaitisha wabunge wa NRM ili kuwekwe mkakati wa kuwasafisha mafisadi. Kilichotokea ni kituko kwani Mke wa Museveni ambaye ni mbunge wa chama tawala alipinga maamuzi na ushawishi wa mumewe kuwasafisha mafisadi. Je unajua kwanini?
Pia baada ya Obama kuchaguliwa Rais wa Marekani, sasa ni wakati wa kupambana na chumi zinazokuwa kwa kasi huko Asia.

Tuesday, November 04, 2008

OBAMA RAISI MPYA MAREKANI

Seneta Obama hatimaye ameshinda urais wa Marekani na anakuwa rais wa Kwanza Mweusi kwa historia. John Mc Cain amekuwa wa kwanza kukiri kuwa ameshindwa kiungwana na kumpongeza mwenzake Obama. Hili limekuwa funzo lingine kwa wagombea wetu wa kiafrika na kitanzania wanaposhindwa si kukimbilia mahakamani bali ni kukubali.
Seneta Obama ndio anatoa hotuba ya shukrani kwa sasa ninapoandika hii makala.

Tuesday, October 21, 2008

FURAHA KWA MADIKTETA WA AFRICA

Ni kipindi cha mataifa ya kibepari kupata dhoruba la kiuchumi lakini ni kipindi cha fuaraha kwa madikteta wa Afrika.
Si hayo tu hata wengine wanakumbuka enzi za Iddi Amin kama demokrasia.

Wednesday, October 08, 2008

JAJI KAPOTEZA KIBARUA

Mjue Jaji alilyepoteza kibarua kwa kutimiza wajibu wake.

KUVUJA MITIHANI - MAPROFESA WIZARA YA ELIMU WAACHIE NGAZI

Ni hivi majuzi tu Raisi Jakaya Mrisho Kikwete alikwenda nchini Marekani na kutembeza bakuli na akafanikiwa kuahidiwa misaada lukuki ya vitabu mbalimbali kusaidia sekta ya elimu nchini Tanzania. Nilitizama picha za runinga zikimuonesha Raisin a Waziri wake wa Elimu ambaye walifuatana naye wakishukuru kwa moyo wa ukunjufu misaada hiyo. Kwa kweli nilifarijika angalau na aina ya msaada ambao Raisi alifanikiwa kushawishi wamarikani na kuupata.

Mara mtihani wa kidato cha nne ukaanza siku ya tarehe 6/10/2008 na mtihani wa kwanza wa Hisabati ukafutwa eti umevuja. Yaani ilimaanisha kuwa walioandaa na kuhifadhi mtihani huo hawakuwa makini katika kuutunza na sasa mtihani huo tayari uliwafikia watahiniwa kabla ya mtihani. Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu alionekana akidai eti ni mtihani mmoja tu umevuja na hivyo mitihani mingine iendelee. Alisahau kuwa ile tu mtihani mmoja ambao unaandaliwa na taasisi moja tu umevuja ilitosha kuifuta mitihani yote? Huyu bwana ni Professa, kwa kweli alinishangaza sana na kwa mwendo huu Katibu Mkuu alikosea kabisa. Haiingii akilini eti mtu aibe mtihani mmoja tu na aache mingine.

Mitaani katika sehemu mbalimbali za Tanzania kuna taarifa kuwa mitihani yote iko nje nje na inauzwa kama vile ulivyouzwa ule wa Hisabati. Napenda ieleweke wazi kuwa ni dhahiri kabisa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeshindwa kabisa kusimamia shughuli nzima ya Mitihani ya kidato cha nne. Katibu Mkuu wa Elimu anaeleza vyombo vya habari eti kushuka kwa maadili miongoni mwa watendaji wa Necta kumechangia hili dhahama. Kwa maoni yangu naamini kuwa pia kuna tatizo la kimaadili kwa Waziri wa Elimu na Naibu Wake pamoja na Katibu Mkuu vilevile.

Haiwezekani tatizo la msingi kama la kuvuja kwa mitihani linatokea alafu mtu anabakia akiendelea na kazi yake kama vile hakuna jambo lolote. Msingi wa kimaadili (Moral Fibre) wa viongozi hawa niliowataja una mashaka sana. Jamani kama tunaruhusu wanafunzi wa kidato cha nne waendelee na mitihani hii basi kwa maana nyingine Tanzania inakufa. Katika dunia ya leo ambayo elimu imebakia kama nguzo kuu nay a msingi katika maisha ya mwanadamu, wizara inaachia wanafunzi wanaoiibia mtihani ndio waendelee na masomo yao bila kupimwa sawasawa? Tunaandaa Taifa gani?

Tunaanda Taifa la wataalam mbumbumbu ambao watakuwa wataalam katika kipindi ambacho nadhani Maprofesa hawa wawili wanaoongoza Wizara ya Elimu labda hawatakuwepo na hivyo hawajali lolote. Kwao kila mtu na lake. Sijui Profesa Maghembe na Profesa Dihenga wana taaluma gani ila nabakia nikiamini kama kweli Uprofesa wao ni wa halali basi wasingelivumilia hili la kuvuja mitihani na kubaki kimya. Kama mitihani hii inayoendelea itaachwa imalizike na itumike kama kipimo cha wanafunzi basi itamaanisha katika Tanzania ya leo hakuna tofauti kati ya profesa na mkulima ambaye hajaenda shule.

Maprofesa hawa wanatupeleka kuwa na Taifa ambalo litakuwa na wasomi wasioiva ama waliokamilika nusu (half baked), matokeo yake ni kuwa na wasomi feki. Kama kweli maprofesa wawili wanaiongoza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wangekuwa makini, wasingeichukulia hii hali kimzahamzaha namna hii. Elimu sio kama haya mambo ya EPA na Richmond ambayo yameamuliwa kisaniisanii tu, bali ni sekta ambayo kama utalegeza udhibiti wake basi maana yake matokeo yake yatabakia kwenye jamii husika kwa miongo kadhaa. Ndio maana napendekeza kuwa Maprofesa hawa waifute mitihani hii mara moja na kama si hivyo wapime wenyewe waamue ama kuachia ngazi au kung’ang’ania mkate ikimaanisha watakuwa wameidhinisha vitendo vyote vya wizi wa mitihani. Watakuwa pia wanatekeleza kile alichowahi kunena mwanafalsafa Niccolo Machiaveli: “The End Justifies the Means”. Yaani unapofanya jambo hakuna haja ya kujali unafikiaje malengo yako ila la msingi ni matokeo”.

Baada ya kuwasihi viongozi wakuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, pia nisisahau juu ya huyu Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani (Necta) naye sijui anangoja nini. Yaani kuna madai tumeyasikia karibuni kama vile wizi wa vyeti mbalimbali pamoja na sasa kuvuja kwa mitihani lakini bado anathubutu kukaa kimya nab ado anathubutu kuingia ofisini bila aibu ama hisia za ukosaji wa usimamizi imara. Napenda nishauri huyu Katibu Mkuu apime hili jambo na aamue mwenyewe. Siamini kama nchi yetu tumefika mahali mtu anavurunda lakini hawajibiki.

Hivi nchi yetu ni njaa zinatusumbua ama ni nini? Lakini lazima tumshangae Raisi wa nchi inapata tatizo zito kama hili lakini bado Raisi anawaonea haya wateule hawa wanaosimamia Wizara ya Elimu. Hivi jamani huyu Raisi anakwenda nje ya nchi kuomba misaada ya elimu alafu hapo hapo anaendelea kuwachekea wateule wake ambao wameshindwa kuhakikisha mitihani haivuji. Umefika wakati kama baadhi ya watendaji hawawajibiki pale uoza unapojitokeza katika taasisi zao basi Raisi kama Mtendaji Mkuu wa Serikali achukue hatua, kinyume chake inamaanisha Tanzania inazikwa taratibu kwa Ari Mpya na Kasi Mpya.

Naliona Baraza la Mitihani pamoja na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kama ndio chanzo cha kuifanya Tanzania siku za usoni imezwe na utandawazi. Hebu fikiria tu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, je watanzania hawa wanaofanya mitihani ya kununua mitaani na kwenye mitandao ya kompyuta wataweza kushindana na wenzao wa Kenya na Uganda ama Rwanda? Nashauri Baraza la Mitihani livunjwe kabisa ikiwezekana kwa maana ya utawala mzima na watendaji wake wote waondolewe. Inahitajika damu mpya yenye mawazo mapya yenye utashi wa kujali hatima ya jamii na si hii habari ya kutokujali na kujifanyia mambo kama vile hakuna kizazi kijacho nchini mwetu.

Umefika wakati vyombo vyote vya habari viamue kuwavalia njuga hawa viongozi wa elimu ili wang’oke katika vyeo vyao kwani nadhani wamepoteza mamlaka ya kimaadili (Moral Authority) ya kuongoza sekta husika. Vyombo vya habari navisihi vichukue uamuzi wa dhati kabisa katika kuhakikisha hatuendelei kuishi kwa njia za wizi wa mitihani kwani hiki ni kiama kwa Taifa.

Tuesday, September 16, 2008

TANZANIA INAHITAJI AKINA YOHANA MBATIZAJI

Jumapili ya tarehe 07/0009/2008, nilihudhuria ibada katika kanisa katoliki la “Kristu Mfalme, mjini Moshi. Katika ibada hiyo mara padri aliyekuwa akihubiri kwa kuoanisha na masomo yaliyosomwa siku hiyo alitumia mfano wa kashfa ya EPA kufikisha ujumbe kwa waumini.
Alilaani tabia ya waumini wa siku hizi kuona maovu au watu waovu wakifanya jambo la uvunjaji wa sheria alafu wananyamaza pale wanapotakiwa kuripoti jambo hilo. Padri huyu alikwenda mbali kabisa akadai kuwa hii ni kwasababu ya tabia ya kila mtu kudai “hayo hayanihusu, mimi najali mambo yangu”. Mtizamo huu, padri alidai ndio chanzo cha kukua kwa ufisadi ambao unaliua taifa letu na bara letu la Afrika kwa ujumla.
Padri alidai kuwa wakati mafisadi walipokuwa wanachukua fedha zile za EPA kuna watu wengi waliwaona lakini wamenyamaza na hata sasa hivi wakati mambo yamewekwa hadharani pia wameamua kunyamaza na wala hawatasema. Aliwachekesha waumini kuwa tabia hii ni kwasababu watu tunaogopa tukisema maovu ya mafisadi basi watakuja kutuchoma moto majumbani kwetu ama watatuchinja. Padri alitoa mfano jinsi Yohana Mbatizaji alivyouawa kwa kukatwa kichwa chake na Mfalme Herode kwa kujaribu kumkemea Mfalme alipojaribu kuishi na mjane wa kaka yake alipofariki. Yohana mbatizaji alimkemea Herode na hatima yake ikawa ni kukatwa kichwa chake na kufa.
Padri akasisitiza tuwe tayari kusema ukweli, kumwambia mtu ukweli anapokosea bila woga. Waumini wengi ndani ya kanisa walicheka manake kwa watanzania kwa sasa si rahisi kutekeleza hili.
Mimi kama muumini mahubiri ya padri yalinikuna sana ila nilipata hisia kuwa kwa Tanzania ya leo ni vigumu sana kuweza kuwa wakweli. Mila na desturi za watanzania karibu wote zinakazia zaidi kuficha mambo na kuchukulia kila kitu kinachomhusu mtu mkubwa au mwenye hadhi ni siri. Ni katika mtizamo huu nadhani elimu ya nchi yetu ina changamoto sana kuweza kuwafanya vijana wetu waje na mentalite ya kisasa ambayo ni ya uwazi na ukweli bila kujali ni nani mkosaji. Kama tutaendelea na haya mambo ya kizazi cha kizamani basi tujue haya mambo ya kupiga kelele kuhusu EPA yataendelea kutusumbua bila kupata jibu.
Naamini umefika wakati tuache kubebea bango hili kashfa la EPA na tuanze mchakato mpya wa kufunza watu wetu kwa ujumla wao juu ya suala la kusema ukweli na nini umuhimu wa kusema na kupenda ukweli. Nasema hivi si kwamba ninaunga mkono kashfa ya EPA ilivyozikwa kwa juhudi kubwa na Rais wetu Jakaya Kikwete pamoja na kamati yake ya uchunguzi. Ninaamini kuwa ukweli ni suala tete ambalo ni tatizo letu kama watanzania kwa ujumla wao. Tungekuwa tunapenda ukweli basi usingetarajia kuona makashfa yanafichwa fichwa kama tunavyoshuhudia leo.
Ninasema kutokupenda ukweli ni tabia za kizamani kwasababu mimi binafsi nimepata bahati kufundisha wanafunzi katika shule mbalimbali za msingi na sekondari hapa nchini. Basi inapotokea mwanafunzi kakosea jambo kinyume na sheria za shule na mwalimu umemwona mkosaji akifanya jambo mbele ya wanafunzi bila wao kujua, unapowauliza watakujibu hatujui. Hata uwabane kwa adhabu za aina gain, hutapata jibu kabisa. Ni tabia ambayo watoto wa siku hizi wameirithi kutoka kwa wazazi wao na ni vigumu kuiondoa. Kwa maana nyingine tunayoyashuhudia leo hii ya kuficha ukweli ni matokeo ya aina ya maisha familia nyingi za kitanzania zinavyoishi. Waswahili walisema: “Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo”. Basi kwa hali ilivyo umefika wakati kwanza tufundishane kama jamii umuhimu wa kuheshimu na kupenda ukweli. Bila hivyo, kashfa zitaendelea kwani watenda kashfa hizo wanajua kabisa kashfa zitafichwa kabisa.
Nitoe mifano michache: angalia vyama vyetu vya siasa kwa mfano utaona huku CCM haya mambo ya akina Nape na Lowasa, ukienda Chadema hii kusimamishwa kwa uongozi kwa Chacha Wangwe na hatimaye kufa kuna mambo yanayogusa kusema na kupenda kutenda mambo kwa ukweli ndio yanayosumbua na kusababisha kashfa na mabishano yasiyokuwa na maana utadhani viongozi wetu ni watoto.
Kwa mtizamo wangu, kwa tabia hii ya kutokupenda ukweli basi tusishangae tutaendelea kupata kashfa ambazo kamwe hazitafanyiwa utatuzi wa kitaalamu ili kuficha ukweli kama tulivyoona kwenye EPA, Richmond, na hata mikataba mingi ambayo serikali yetu haitaki watu waichokonoe na inawaona wachokonozi kama ni watu wenye wivu.
Hata hii habari ya Nape Nnaye kuadhibiwa kwa alichokifanya; yaani kuhoji mambo yaliyofanywa na wakubwa ni dalili nyingine ya kutopenda ukweli. Bila kukubali ukosoaji, naamini nchi yetu haifiki popote. Ni kwa mfano wa mahubiri ya Padri wa Kristo Mfalme kwa jumapili iliyopita ambayo kwangu naamini yalilenga nyakati hasahasa. Basi tuamue kuupenda ukweli, la sivyo tusilalamike juu ya mafisadi.
Kutokupenda ukweli imekuwa ni tabia ya watanzania katika nyanja zote. Kwa mfano, hili dhahama la UVCCM, utaona kijana Nape amevuliwa uanachama wa UVCCM, kama adhabu ya kusema uwongo. Mimi kidogo napata taabu sana kuona wachokonozi kama Nape wanapodai jambo na wanaadhibiwa alafu wanaamua kunyamaza kimya. Hii ndio kielelezo cha viongozi wa leo ambao kwao ni bora “status quo” kuliko kuleta mapinduzi. Kwao mapinduzi si hoja ila ni ile wazungu wanaita: “Business as usual”, yaani mambo kama kawaida, hakuna kubadilika.
Mimi naamini viongozi wa aina ya akina Nape tunao wengi ndani ya CCM. Utashangaa bungeni mbunge wa CCM kupiga kelele nyingi dhidi ya ufisadi unaofanywa na viongozi wenzake ndani ya chama. Lakini anabakia kama mwanachama mwaminifu ndani ya chama anachokilalamikia. Yote hii ni kwasababu tumefikia mahali wote ama wengi wetu tunaamini eti bila kuwa mwanachama au mfuasi wa CCM basi hakuna maisha. Hii ni kasumba ambayo ninaiona inawakabili wengi wa tabaka jipya la viongozi linaloibuka kwa sasa. Nadhani ingekuwa vyema kwa watu kama akina Nape waanzishe vyama vipya vya kisiasa ambavyo vitaruhusu mawazo kama yao ili kuleta mabadiliko. Naamini pamoja na CCM na hata vyama vyetu vya upinzani vilivyopo, vyote ni bure tu kama unakuwa mwanasiasa ndani yake na una hii tabia ya uchokonozi au kuhoji mambo yanapokuwa yanakwenda kombo.
Na kwasababu Nape hayuko tayari kuwa kama Yohana Mbatizaji basi tutegemee kuwa hakuna mabadiliko na wala yeye si tabaka jipya la viongozi wanamapinduzi ambao wanaweza kuitoa nchi hapa ilipo katika kipindi hiki. Ni wasanii tuu ambao wanajaribu kufanya kile ambacho mtaani watu wanakiita: kutest zari.

Sunday, September 14, 2008

Rais Museveni anajaribu kutumia viongozi wa kijadi katika kuhakikisha serikali ya NRM inapata sapoti ya karibu kutoka kwa makabila yote Uganda. Hii kwa wachunguzi wa mambo inaonekana ni mbinu isiyo sahihi.http://www.monitor.co.ug/artman/publish/Golooba-Mutebi/Cultural_leaders_shouldn_t_be_political_tools_71486.shtml

Friday, August 22, 2008

VITA YA UKIMWI UGANDA YASHINDIKANA

Uganda ile nchi iliyokuwa inasifiwa vizuri kuwa ndio bingwa wa kudhibiti Ukimwi nayo imeshindwa vita hii.

Thursday, August 21, 2008

KIKWETE AHUTUBIA BUNGE

Hatimaye Kikwete kahutubia Bunge na kama ilivyotarajiwa na wengi wanaomfahamu, hakuna la maana aliloteta sana ukiacha machache.

Tuesday, August 19, 2008

MWANAWASA HATUNAYE DUNIANI

Rais wa Zambia, Levy Mwanawasa amefariki dunia.
Kifo hiki nilikitarajia tangu jana usiku.