Hii ni globu iliyovumbuliwa nchini Uganda inajaribu kukazia matumizi ya lugha ya kiswahili na kuhabarishana kuhusu maswala mbalimbali ya kijamii hasa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kat na kwingineko. Siasa na mambo ya michezo na kijamii kwa ujumla ndio itakayokuwa mada kuu hapa.Nitakaribisha maoni yenu.
My Blog List
Thursday, August 21, 2008
KIKWETE AHUTUBIA BUNGE
Hatimaye Kikwete kahutubia Bunge na kama ilivyotarajiwa na wengi wanaomfahamu, hakuna la maana aliloteta sana ukiacha machache.
Tuesday, August 19, 2008
MWANAWASA HATUNAYE DUNIANI
Rais wa Zambia, Levy Mwanawasa amefariki dunia.
Kifo hiki nilikitarajia tangu jana usiku.
Kifo hiki nilikitarajia tangu jana usiku.
Sunday, August 10, 2008
CHACHA WANGWE LABDA HAKUFAA KUWA MWANASIASA
CHACHA WANGWE HAKUFAA KUWA MWANASIASA
Mara baada ya mazishi ya mbunge wa Tarime kufanyika, nimejiuliza mambo mengi sana kuhusu jamii ya kitanzania. Yaliyotokea Tarime kwa hali ya kawaida yamenifanya nishindwe kujua hivi kweli mtu anaweza kufa alafu wafiwa waamue kuwa mazishi yasifanyike dakika za mwisho? Sina hakika kama hali imewahi kutokea Tanzania hasa kwa watu waheshimiwa kama mbunge. Ila nadhani umefika wakati tuutizame kwa kina mfumo mzima wa uendeshaji wa siasa zetu.
Nimesema hivyo kwani naamini kabisa hisia za mbunge Chacha Wangwe kuuawa zilijitokeza kwa sababu kuna mazingira yanayoonesha kwa sasa jamii ya kitanzania haina imani na mfumo mzima wa uendeshaji siasa. Hii inaweza kujidhihirisha kama ifuatavyo:
Kwanza, kupitia vyombo vya habari vyote viliiripoti habari ya kuwa Chacha aliuawa kwa kushabikia hasa. Hali hii inaonesha ni jinsi gani Tanzania ya leo baadhi ya viongozi wanapokufa basi moja kwa moja kuna kuwa na hisia za kifo cha kupangwa. Tumshukuru rais Kikwete kwa ulegezaji wa sheria za kubana uhuru wa magazeti na vyombo vya habari kwa ujumla, hii inatupa wasaa mzuri kupima na kujua nini hisia za watanzania juu ya matukio mbalimbali nchini Tanzania.
Pili, wanatarime na hasa wanafamilia ya Chacha Wangwe waliamua kwa dhati kabisa kutia shaka kifo kile. Sijui walitaka Chacha afe vipi ama labda walikuwa wanajua kuwa Chacha atakufa je, ila napata mashaka sana kama watanzania tumeamua kuishi kwa kuamini kila jambo lina mchezo mchafu. Kwa maana nyingine nchi yetu imegeuzwa jamvi la wapiga ramli ama watu wasioaminiana kwa jambo lolote. Hila ndio umebaki mchezo pekee katika masuala ya kisiasa.
Tatu, tujiulize alipokufa Amina Chifupa (RIP) yalisemwa mengi na hata baadhi ya wakubwa fulani walihusishwa na kifo kile. Mwisho wa siku mtu alikufa na mpaka leo kifo kile kimebaki na maswali mengi kwa watu wenye akili timamu. Matukio kama haya ya vifo vya viongozi wa kijamii katika utata yanalidhalilisha bunge letu sana na hata jamii nzima ya Tanzania. Inapofikia mahali jamii kwa kiasi kikubwa inapoteza imani na serikali na hata chombo chake kama bunge basi ujue kuna kila dalili za mpasuko.
Kwa upande mwingine, kifo cha Mbunge Chacha kimenifanya nijiulize hivi inakuwaje Mbunge anasafiri safari ya usiku tena na rafiki yake na wala si dereva. Na hata kama itathibitika yule Bwana aliyesafiri naye alikuwa dereva, inakuwaje mbunge aendeshwe na dereva asiyekuwa na sifa kama vile leseni ya udereva. Hii inanipa taabu sana ya umakini wa viongozi wetu. Hebu nikumbushe kuwa Mh. Mudhihir Mudhihir alipata ajali wala hakuwa na dereva; Mh. Kapuya alipata ajali akiwa na dereva, lakini mazingira ya ajali dhahiri yanaonesha ilikuwa kwasababu ya mwendo kasi wa dereva na labda dereva kutozingatia uendeshaji salama wa gari katika barabara ambayo nina hakika hakuwa ameizoea. Ni katika mazingira haya mtu mwenye akili timamu najiuliza : hivi kweli hizi ajira za kuendesha viongozi wetu zinafuata weledi wa dereva ama ni haya masuala ya kuendeshwa na marafiki ama ndugu tu kama alivyokuwa marehemu Wangwe?
Jambo lingine ambalo nadhani kifo cha Wangwe kimetuachia kulidurusu ni juu ya muundo wa vyama vya siasa Tanzania. Inasemwa kuwa aliwahi kutuhumu kuwa Chadema ni chama cha wachaga. Nimeshuhudia mheshimiwa Zitto Kabwe akijitutumua na kuwalaumu wahariri mbalimbali wa vyombo vya habari kwa kuripoti vibaya juu ya vitisho alivyofanyiwa mwenyekiti wa Chadema kule Tarime. Anafananisha uandishi ule kama ule wa Rwanda ambao ulichangia kwa mauaji ya kimbari kwa kusema kuwa wachaga kule Mara sasa wanatishwa.
Kuna kitu ningependa Mheshimiwa Zitto na wapenda demokrasia wajiulize kwa kina: Nacho ni hivi kauli ile ya Chacha ilikuwa na ukweli wowote? Nilipomsikia Wangwe akidai kuwa ni chama cha wachaga sikupata taabu kabisa. Nilimwelewa akimaanisha kuwa ile safu ya uongozi ya juu kabisa, safu ya wadhamini wa chama ndicho alichokuwa analenga. Nani anaweza kubisha kwa muundo wa vyama vya siasa hapa Afrika tangu mageuzi yaanzishwe vimeegemea kwenye nguvu ya kiuchumi ya ama mtu mmoja au kikundi cha watu ambao ndio wenye ushawishi katika Chama? Hili lipo karibu kila nchi ya Afrika kwa mfano: Uganda, NRM ilianzishwa na watu wa magharibi ya Uganda alikozaliwa Museveni. PNU ya Kibaki kule Kenya imeegemea zaidi kabila la Wakikuyu ambako Kibaki katokea. Hapa Tanzania mambo ni hay ohayo, hebu tizama chama kama UDP iko chini ya John Cheyo na yeye ndie mshika dau mkuu pamoja na ukoo wa Cheyo.
Ni katika hali kama hii ambapo nadhani kwa mwanademokrasia wa dhati kama marehemu Wangwe asingeweza kuwa ndani ya Chadema ambacho mhimili wake mkuu ni watu wa kabila la mwenyekiti . Na hata uongozi wa Chadema nani asiyejua kwa mfano wabunge wa kuteuliwa wengi wao ni wa kabila moja na ama wamepata nafasi hizo kwa kigezo cha urafiki ama undugu na baadhi ya wadhamini wa chama? Isitoshe, wabunge baadhi wa kuteuliwa ni ndugu wa karibu wa baadhi ya wadhamini? Ni katika mtizamo huu ambapo ninaamini marehemu Wangwe alikosea mwenyewe kutambua juu ya mifumo ya uundaji wa vyama vya siasa. Nani atakayebisha kuwa kama hao wote ambao Wangwe aliwatuhumu kabla ya kusimamishwa kuwa ni wa kabila fulani ndio mhimili wa Chama? Na kama wakiamua waondoke katika chama hicho na wamwachie marehemu akiendeshe basi chama kitayumba?
Wazungu wana msemo “to go too far” yaani kwenda mbali zaidi. Kwa marehemu Chacha kutuhumu Chama ni cha Kabila fulani ilikuwa sio hatua muafaka kufanywa na mbunge kama yeye ingawa alilotetea ni la ukweli. Matokeo yake Chama kimepatwa na mitikisiko ambayo kwa vyovyote vile kama marehemu Chacha angetafakari kwa kina, nadhani hata kifo chake kisingehusishwa na Chadema. Mara nyingine binadamu ana kasumba tofauti lakini kwa wale wote wenye tabia na kasumba za akina Wangwe; yaani misimamo thabiti isiyoyumbishwa kwa hali yeyote ile inakuwa vigumu sana kuelewana na watu wengi. Watu kama akina Wangwe hawafai kuwa wanasiasa kwani siasa ni mchezo uliojaa unafiki. Na Wangwe na jamii ya watu kama yeye si wanafiki sasa inakuwa taabu sana kuweza kuhimili mizengwe ya kisiasa. Kama Wangwe angekuwa mwanasiasa nina hakika kabisa asingeliwahi kuzua mambo ambayo yalipelekea kusimamishwa uongozi.
Katika hali kama niliyoielezea nadhani tatizo la vyama vyetu ni la kimfumo tulioamua kujiwekea wenyewe ambapo demokrasia ya kweli kwa maana ya kutoa maoni yako mbele ya viongozi wako hayaruhusiwi na yanaonekana ni dharau. Mpaka hapo tutakapoamua kuendesha vyama vya siasa ambavyo havitegemei ruzuku kutoka kwa wenye chama kama kikundi basi tujue migogoro ya aina ya Chacha itaendelea. Ni katika hali hiyo basi umefika wakati tujitizame kama jamii ya watanzania makini na tuamue kuwa na kanuni za kuendesha siasa ambazo zitawekwa kama sheria. Hii itasaidia sana kuwa na vyama kwa maslahi ya nchi na wala si chombo cha kutetea maslahi ya wananchi kijujuu huku wakati huo huo vyama vya siasa vikitumika kama vyombo ama nyenzo za kusaidia ndugu na jamaa ya viongozi kujipatia maslahi ya kazi na maisha yao.
Na tunapokuwa na vyama hivi tulivyonavyo leo hii basi watu wote wa aina ya Wangwe kamwe hawataweza kuishi bila kukumbana na mikasa ya kusimamishwa, kufukuzwa na hata kuonywa mara kwa mara. Si hayo tu, pia kwa zile nchi zenye udikteta watu wa aina hii huuawa ( elimination) ili kuwaondoa katika uso wa kisiasa wa nchi husika. Na ndio maana hadi leo kuna watu wamefariki na kuacha maswali bila majibu. Hawa ni kama vile: Horace Kolimba, Imran Kombe, Amina Chifupa, Ipyana Malecela kwa hapa Tanzania na akina Litvnenko kule Russia, Robert Ouko kule Kenya na wengine wengi ambao wamekufa na watu wakawa na hisia wemeuawa bila kuwa na ushahidi wa dhati kabisa.
Mwisho, binafsi ninaamini kabisa kuwa Wangwe amekufa na baada ya kushindwa kuthibitisha risasi ilitumika basi ni wakati wa kukubali kuwa ilikuwa kazi ya Mungu kwani pamoja na maadui wengi aliokuwa nao bado tumeshindwa kuthibitisha. Lililo mbele yetu ni kuwa umefika wakati kuhakikisha tunaimarisha taasisi za mfumo wa kisiasa Tanzania hasa jinsi gani vyama vya siasa vinapaswa kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya demokrasia ya kweli bila kuweka uzandiki. Tukishindwa haya basi tujue kuwa kila mwaka hasa wakati wa bajeti tutarajie mbunge fulani mwenye misimamo isiyoyumba atatutoka hapa duniani katika mazingira tata ambayo mara nyingi tutashindwa kuthibitisha kama kweli ni kazi ya Mungu.
Mara baada ya mazishi ya mbunge wa Tarime kufanyika, nimejiuliza mambo mengi sana kuhusu jamii ya kitanzania. Yaliyotokea Tarime kwa hali ya kawaida yamenifanya nishindwe kujua hivi kweli mtu anaweza kufa alafu wafiwa waamue kuwa mazishi yasifanyike dakika za mwisho? Sina hakika kama hali imewahi kutokea Tanzania hasa kwa watu waheshimiwa kama mbunge. Ila nadhani umefika wakati tuutizame kwa kina mfumo mzima wa uendeshaji wa siasa zetu.
Nimesema hivyo kwani naamini kabisa hisia za mbunge Chacha Wangwe kuuawa zilijitokeza kwa sababu kuna mazingira yanayoonesha kwa sasa jamii ya kitanzania haina imani na mfumo mzima wa uendeshaji siasa. Hii inaweza kujidhihirisha kama ifuatavyo:
Kwanza, kupitia vyombo vya habari vyote viliiripoti habari ya kuwa Chacha aliuawa kwa kushabikia hasa. Hali hii inaonesha ni jinsi gani Tanzania ya leo baadhi ya viongozi wanapokufa basi moja kwa moja kuna kuwa na hisia za kifo cha kupangwa. Tumshukuru rais Kikwete kwa ulegezaji wa sheria za kubana uhuru wa magazeti na vyombo vya habari kwa ujumla, hii inatupa wasaa mzuri kupima na kujua nini hisia za watanzania juu ya matukio mbalimbali nchini Tanzania.
Pili, wanatarime na hasa wanafamilia ya Chacha Wangwe waliamua kwa dhati kabisa kutia shaka kifo kile. Sijui walitaka Chacha afe vipi ama labda walikuwa wanajua kuwa Chacha atakufa je, ila napata mashaka sana kama watanzania tumeamua kuishi kwa kuamini kila jambo lina mchezo mchafu. Kwa maana nyingine nchi yetu imegeuzwa jamvi la wapiga ramli ama watu wasioaminiana kwa jambo lolote. Hila ndio umebaki mchezo pekee katika masuala ya kisiasa.
Tatu, tujiulize alipokufa Amina Chifupa (RIP) yalisemwa mengi na hata baadhi ya wakubwa fulani walihusishwa na kifo kile. Mwisho wa siku mtu alikufa na mpaka leo kifo kile kimebaki na maswali mengi kwa watu wenye akili timamu. Matukio kama haya ya vifo vya viongozi wa kijamii katika utata yanalidhalilisha bunge letu sana na hata jamii nzima ya Tanzania. Inapofikia mahali jamii kwa kiasi kikubwa inapoteza imani na serikali na hata chombo chake kama bunge basi ujue kuna kila dalili za mpasuko.
Kwa upande mwingine, kifo cha Mbunge Chacha kimenifanya nijiulize hivi inakuwaje Mbunge anasafiri safari ya usiku tena na rafiki yake na wala si dereva. Na hata kama itathibitika yule Bwana aliyesafiri naye alikuwa dereva, inakuwaje mbunge aendeshwe na dereva asiyekuwa na sifa kama vile leseni ya udereva. Hii inanipa taabu sana ya umakini wa viongozi wetu. Hebu nikumbushe kuwa Mh. Mudhihir Mudhihir alipata ajali wala hakuwa na dereva; Mh. Kapuya alipata ajali akiwa na dereva, lakini mazingira ya ajali dhahiri yanaonesha ilikuwa kwasababu ya mwendo kasi wa dereva na labda dereva kutozingatia uendeshaji salama wa gari katika barabara ambayo nina hakika hakuwa ameizoea. Ni katika mazingira haya mtu mwenye akili timamu najiuliza : hivi kweli hizi ajira za kuendesha viongozi wetu zinafuata weledi wa dereva ama ni haya masuala ya kuendeshwa na marafiki ama ndugu tu kama alivyokuwa marehemu Wangwe?
Jambo lingine ambalo nadhani kifo cha Wangwe kimetuachia kulidurusu ni juu ya muundo wa vyama vya siasa Tanzania. Inasemwa kuwa aliwahi kutuhumu kuwa Chadema ni chama cha wachaga. Nimeshuhudia mheshimiwa Zitto Kabwe akijitutumua na kuwalaumu wahariri mbalimbali wa vyombo vya habari kwa kuripoti vibaya juu ya vitisho alivyofanyiwa mwenyekiti wa Chadema kule Tarime. Anafananisha uandishi ule kama ule wa Rwanda ambao ulichangia kwa mauaji ya kimbari kwa kusema kuwa wachaga kule Mara sasa wanatishwa.
Kuna kitu ningependa Mheshimiwa Zitto na wapenda demokrasia wajiulize kwa kina: Nacho ni hivi kauli ile ya Chacha ilikuwa na ukweli wowote? Nilipomsikia Wangwe akidai kuwa ni chama cha wachaga sikupata taabu kabisa. Nilimwelewa akimaanisha kuwa ile safu ya uongozi ya juu kabisa, safu ya wadhamini wa chama ndicho alichokuwa analenga. Nani anaweza kubisha kwa muundo wa vyama vya siasa hapa Afrika tangu mageuzi yaanzishwe vimeegemea kwenye nguvu ya kiuchumi ya ama mtu mmoja au kikundi cha watu ambao ndio wenye ushawishi katika Chama? Hili lipo karibu kila nchi ya Afrika kwa mfano: Uganda, NRM ilianzishwa na watu wa magharibi ya Uganda alikozaliwa Museveni. PNU ya Kibaki kule Kenya imeegemea zaidi kabila la Wakikuyu ambako Kibaki katokea. Hapa Tanzania mambo ni hay ohayo, hebu tizama chama kama UDP iko chini ya John Cheyo na yeye ndie mshika dau mkuu pamoja na ukoo wa Cheyo.
Ni katika hali kama hii ambapo nadhani kwa mwanademokrasia wa dhati kama marehemu Wangwe asingeweza kuwa ndani ya Chadema ambacho mhimili wake mkuu ni watu wa kabila la mwenyekiti . Na hata uongozi wa Chadema nani asiyejua kwa mfano wabunge wa kuteuliwa wengi wao ni wa kabila moja na ama wamepata nafasi hizo kwa kigezo cha urafiki ama undugu na baadhi ya wadhamini wa chama? Isitoshe, wabunge baadhi wa kuteuliwa ni ndugu wa karibu wa baadhi ya wadhamini? Ni katika mtizamo huu ambapo ninaamini marehemu Wangwe alikosea mwenyewe kutambua juu ya mifumo ya uundaji wa vyama vya siasa. Nani atakayebisha kuwa kama hao wote ambao Wangwe aliwatuhumu kabla ya kusimamishwa kuwa ni wa kabila fulani ndio mhimili wa Chama? Na kama wakiamua waondoke katika chama hicho na wamwachie marehemu akiendeshe basi chama kitayumba?
Wazungu wana msemo “to go too far” yaani kwenda mbali zaidi. Kwa marehemu Chacha kutuhumu Chama ni cha Kabila fulani ilikuwa sio hatua muafaka kufanywa na mbunge kama yeye ingawa alilotetea ni la ukweli. Matokeo yake Chama kimepatwa na mitikisiko ambayo kwa vyovyote vile kama marehemu Chacha angetafakari kwa kina, nadhani hata kifo chake kisingehusishwa na Chadema. Mara nyingine binadamu ana kasumba tofauti lakini kwa wale wote wenye tabia na kasumba za akina Wangwe; yaani misimamo thabiti isiyoyumbishwa kwa hali yeyote ile inakuwa vigumu sana kuelewana na watu wengi. Watu kama akina Wangwe hawafai kuwa wanasiasa kwani siasa ni mchezo uliojaa unafiki. Na Wangwe na jamii ya watu kama yeye si wanafiki sasa inakuwa taabu sana kuweza kuhimili mizengwe ya kisiasa. Kama Wangwe angekuwa mwanasiasa nina hakika kabisa asingeliwahi kuzua mambo ambayo yalipelekea kusimamishwa uongozi.
Katika hali kama niliyoielezea nadhani tatizo la vyama vyetu ni la kimfumo tulioamua kujiwekea wenyewe ambapo demokrasia ya kweli kwa maana ya kutoa maoni yako mbele ya viongozi wako hayaruhusiwi na yanaonekana ni dharau. Mpaka hapo tutakapoamua kuendesha vyama vya siasa ambavyo havitegemei ruzuku kutoka kwa wenye chama kama kikundi basi tujue migogoro ya aina ya Chacha itaendelea. Ni katika hali hiyo basi umefika wakati tujitizame kama jamii ya watanzania makini na tuamue kuwa na kanuni za kuendesha siasa ambazo zitawekwa kama sheria. Hii itasaidia sana kuwa na vyama kwa maslahi ya nchi na wala si chombo cha kutetea maslahi ya wananchi kijujuu huku wakati huo huo vyama vya siasa vikitumika kama vyombo ama nyenzo za kusaidia ndugu na jamaa ya viongozi kujipatia maslahi ya kazi na maisha yao.
Na tunapokuwa na vyama hivi tulivyonavyo leo hii basi watu wote wa aina ya Wangwe kamwe hawataweza kuishi bila kukumbana na mikasa ya kusimamishwa, kufukuzwa na hata kuonywa mara kwa mara. Si hayo tu, pia kwa zile nchi zenye udikteta watu wa aina hii huuawa ( elimination) ili kuwaondoa katika uso wa kisiasa wa nchi husika. Na ndio maana hadi leo kuna watu wamefariki na kuacha maswali bila majibu. Hawa ni kama vile: Horace Kolimba, Imran Kombe, Amina Chifupa, Ipyana Malecela kwa hapa Tanzania na akina Litvnenko kule Russia, Robert Ouko kule Kenya na wengine wengi ambao wamekufa na watu wakawa na hisia wemeuawa bila kuwa na ushahidi wa dhati kabisa.
Mwisho, binafsi ninaamini kabisa kuwa Wangwe amekufa na baada ya kushindwa kuthibitisha risasi ilitumika basi ni wakati wa kukubali kuwa ilikuwa kazi ya Mungu kwani pamoja na maadui wengi aliokuwa nao bado tumeshindwa kuthibitisha. Lililo mbele yetu ni kuwa umefika wakati kuhakikisha tunaimarisha taasisi za mfumo wa kisiasa Tanzania hasa jinsi gani vyama vya siasa vinapaswa kuendesha shughuli zake kwa kuzingatia misingi ya demokrasia ya kweli bila kuweka uzandiki. Tukishindwa haya basi tujue kuwa kila mwaka hasa wakati wa bajeti tutarajie mbunge fulani mwenye misimamo isiyoyumba atatutoka hapa duniani katika mazingira tata ambayo mara nyingi tutashindwa kuthibitisha kama kweli ni kazi ya Mungu.
Thursday, July 31, 2008
CHACHA WANGWE ALIUAWA KWA RISASI?
MAZISHI YA CHACHA HAYAKUFANYIKA!
Huwezi amini lakini ndio hivyo, ndugu wa marehemu Chacha Wangwe walizuia mazishi yasifanyike kwa kile kilichoitwa kuwa hawaamini kama kuna ajali bali alipigwa risasi. Kwa mujibu wa redio free Afrika jana usiku, inasemekana familia ilimualika rafiki wa familia kutoka Kenya ambaye ni daktari na akawaambia kuwa jeraha lililopo kisogoni kwa marehemu ni la risasi.
Makubwa ndio haya inaonekana marehemu alipigwa risasi mdomoni na ikatokea kisogoni. Maoni yangu ni kuwa kama hii ni kweli basi marehemu alikuwa anafuatwa na maadui zake ambao naweza kuwaita (firing squad) ambao watakuwa walitumwa. Na inavyoelekea hawa jamaa watakuwa walilipita gari la marehemu na kumpiga risasi wakiwa mbele yake. Hii ndio itakayokuwa sababu ya ajali kwani kishindo ambacho Dennis Mallya alikisikia kabla gari halijabiringika ilikuwa ni risasi.
Kama hiyo sivyo, basi kwa vyovyote vile Dennis Mallya atakuwa ndie muuaji wa mbunge wetu mpendwa. Atakuwa ndie anahusika na mauaji haya na ashughulikiwe ikithibitika ni risasi imemuua Chacha.
Pia ni vyema gari lichunguzwe kama tairi zake zimepasuka kweli.
Nadhani baada ya mafisadi wa kisiasa Tanzania kuzidi kuwaua viongozi bora wa Tanzania sasa mwisho umefika. Alikufa Amina Chifupa alafu tukakaa kimya tu hatukuhoji lakini leo napenda niwapongeze ndugu wa Chacha Wangwe kwa walichokifanya kwani wameonesha kuwa wana akili na wanapenda nchi hii iwe na viongozi wenye weledi.
Mwisho nikumbushie kuwa kabla marehemu hajafariki, alikuwa ametoa maneno mazito dhidi ya hali ya “Ukabila ndani ya chama cha Chadema” na kuanzia hapo amepata misukosuko mingi hata kusimamishwa uongozi. Ni vyema wapenda amani wote Tanzania tujiulize hivi inawezekana maneno haya aliyoyasema ndio chanzo cha kifo chake? Wenye chama chao wamemuua? Je kwa kipindi hiki Chacha alikuwa ni tishio kwa CCM au Chadema? Iwe iwavyo, mojawapo ya hivi viwili ndio chanzo cha kifo hiki.
Huwezi amini lakini ndio hivyo, ndugu wa marehemu Chacha Wangwe walizuia mazishi yasifanyike kwa kile kilichoitwa kuwa hawaamini kama kuna ajali bali alipigwa risasi. Kwa mujibu wa redio free Afrika jana usiku, inasemekana familia ilimualika rafiki wa familia kutoka Kenya ambaye ni daktari na akawaambia kuwa jeraha lililopo kisogoni kwa marehemu ni la risasi.
Makubwa ndio haya inaonekana marehemu alipigwa risasi mdomoni na ikatokea kisogoni. Maoni yangu ni kuwa kama hii ni kweli basi marehemu alikuwa anafuatwa na maadui zake ambao naweza kuwaita (firing squad) ambao watakuwa walitumwa. Na inavyoelekea hawa jamaa watakuwa walilipita gari la marehemu na kumpiga risasi wakiwa mbele yake. Hii ndio itakayokuwa sababu ya ajali kwani kishindo ambacho Dennis Mallya alikisikia kabla gari halijabiringika ilikuwa ni risasi.
Kama hiyo sivyo, basi kwa vyovyote vile Dennis Mallya atakuwa ndie muuaji wa mbunge wetu mpendwa. Atakuwa ndie anahusika na mauaji haya na ashughulikiwe ikithibitika ni risasi imemuua Chacha.
Pia ni vyema gari lichunguzwe kama tairi zake zimepasuka kweli.
Nadhani baada ya mafisadi wa kisiasa Tanzania kuzidi kuwaua viongozi bora wa Tanzania sasa mwisho umefika. Alikufa Amina Chifupa alafu tukakaa kimya tu hatukuhoji lakini leo napenda niwapongeze ndugu wa Chacha Wangwe kwa walichokifanya kwani wameonesha kuwa wana akili na wanapenda nchi hii iwe na viongozi wenye weledi.
Mwisho nikumbushie kuwa kabla marehemu hajafariki, alikuwa ametoa maneno mazito dhidi ya hali ya “Ukabila ndani ya chama cha Chadema” na kuanzia hapo amepata misukosuko mingi hata kusimamishwa uongozi. Ni vyema wapenda amani wote Tanzania tujiulize hivi inawezekana maneno haya aliyoyasema ndio chanzo cha kifo chake? Wenye chama chao wamemuua? Je kwa kipindi hiki Chacha alikuwa ni tishio kwa CCM au Chadema? Iwe iwavyo, mojawapo ya hivi viwili ndio chanzo cha kifo hiki.
Tuesday, July 29, 2008
UGANDA VS MENGO - UNAIJUA KASHESHE?
Kwa sasa Uganda ina mgogoro mkubwa wa kisiasa na himaya ya Baganda, unajua chanzo chake?
Monday, July 28, 2008
MSIBA BUNGE LA TANZANIA TENA
TANZIA – SASA IMEKUWA ZAMU YA CHACHA WANGWE
Ni saa nne na dakika arobaini na saba, mara nikitizama taarifa ya habari ya ITV usiku nashanga mstari mweusi wa maneno unakatiza katika runinga na maneno: “mbunge wa Tarime, mheshimiwa Chacha Wangwe amefariki dunia usiku kwa ajali ya Gari” habari zaidi fuatilia redio one.
Na kweli ninazima runinga yangu na kuanza kusikiliza redio one. Ninakutana na mahojiano kati ya watangazaji: Asia Mohamed na Jerry Muro akiripoti kutoka Dodoma. Wanahojiwa waheshimiwa mbalimbali kwa masikitiko bado wanaonekana kutaharuki. Mtangazaji anadai eti nyakati za mchana mheshimiwa Chacha alionekana akiteta na mheshimiwa Mudhihir, hii inanikumbusha huyu ni mhanga mwingine wa ajali katika bunge hili. Hisia fulani zinanijia akilini lakini sisemi kitu najinyamazia.
Nikiwa nimekwishaamini kuwa mheshimiwa huyu katutoka, navuta hisia kadhaa juu ya bwana huyu na mara moja nautambua Umachachari wake, ubishi wake hata pale pasipo na Mantiki lakini kwa yote , kauli ya John Cheyo inanikuna akihojiwa na Jerry Muro. Anasema: “Chacha alikuwa na msimamo ambao wengi wetu hatunao” . Nakubaliana na mheshimiwa Cheyo na ninaendelea kusikitika.
Mara ninaamua kumtumia mtu wangu wa karibu sms akiwa Dar es salaam nikimsihi afuatilie habari kuna tukio la kifo cha mbunge mashuhuri. Pia katika message yangu nampa hisia yangu kuwa sasa “ Chadema itachafuka hasa kwani kifo hiki kitatumiwa na wanazi kuonesha kukolimbana hakuko tu CCM”. Ninapoituma message ile mara napata message kutoka kwa rafiki mwingine akinihabarisha juu ya kifo cha Chacha. Ninamrudishia nikimsihi kuwa “Siasa za Afrika ni mchezo mchafu, nina hisia lazima kuna mkono wa mtu awe wa kambi ya marehemu ama kule tulikozoea kukolimba watu wabishi kama Wangwe”.
Hapo hapo napokea message nyingine ambayo inanijibu ile niliyotuma Dar es salaam: “Sio Chadema ni CCM walileta mgogoro alafu wamemuua ili tuone Chadema nao wana mchezo kama wao! Tunaelekea pazuri sana. Tutashuhudia mengi na ukweli utadhihirika mwisho”. Mie sijui kwanini watu wana maoni ya aina hiyo ila ndio jamii ya kitanzania ilipofikia sasa.
Inapofika saa sita na dakika kumi na sita usiku hisia zangu zinashangaa: Jerry Muro, mwandishi wa ITV anaongea na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, mheshimiwa Lukuvi ambaye anasema kuwa gari la Wangwe limepata ajali ya kuanguka baada ya kupasuka gurudumu. Lukuvi anamnukuu rafiki wa Wangwe ambaye alikuwa ndani ya gari la Wangwe na amepata michubuko tu. Anasema gari lenyewe lilibiringika mara nyingi sana na ndipo Israel akachukua roho ya mheshimiwa Chacha. Moja kwa moja hapa ninajenga kanuni za kihisia na chonganishi (conspiracy theories) kadhaa:
Moja, kwanini gari la mbunge kama tuyajuavyo ni magari imara , mazuri na nina hakika yanafanyiwa matengenezo bora, itakuwaje lipasuke tairi tena nyakati za usiku pasipo na joto sana la kupasha hiyo chubu? Inawezekana kirahisi namna hiyo? Au tuseme Chacha anatembelea ulimu?
Pili, hili Bunge letu lina matatizo gani? Ni balaa ama ni nini? Kwanini kila kikao kinapokutana hasa cha bajeti lazima Mbunge afe?
Tatu, kwanini katika bunge hili ukiacha mbunge mmoja tu, wote waliokufa kulikuwa na hali ya kuwa na maadui hasa juu ya misimamo ya marehemu hawa?
Nne, kwanini wabunge wa bunge hili wanapatwa na madhila kama ajali ama vifo mara baada ya kuwa ni watu wenye misimamo yenye kutetea maslahi ya umm a sana ama kudhoofisha maslahi ya umma?
SHUHUDA WA AJALI
Saa sita na dakika thelathini na sita, redio one inaripoti kuwa ndio mwili wa Chacha Unaingia hospitali ya Dodoma kutoka eneo la ajali huko Kongwa. Gari ni Land Cruiser namba: SM.4297 la Halmashauri ya Kongwa. Jerry Muro anaongea na Rafiki wa mheshimiwa Chacha ambaye alikuwa akisafiri na mheshimiwa Chacha, ndugu Deus Mallya, rafiki wa karibu wa Chacha, anaeleza walitoka Dodoma wakienda Dar, anasema alisikia kishindo kikubwa sana kabla ya ajali, ninapata hisia sio ajabu inawezekana gari hilo lilikuwa limetegwa bomu labda, na gari liliruka juu na kufuatiwa na mbiringiko mkubwa sana.
Kuhusu mwendo wa gari Deus Mallya anasema kuwa Mheshimiwa Wangwe hana hakika kama alifunga mkanda. Yeye alifunga mkanda, lakini kimazingira inaonekana marehemu alibanwa kwa hiyo napata hisia alikuwa amefunga mkanda la sivyo kwa mbiringiko huo lazima angerushwa nje.
Je mheshimiwa Wangwe alikuwa kwenye hali gani? Mwanzoni nilidhani ni Land Cruiser, kumbe sio, ila ni gari dogo. Alikuwa anaendesha gari aina ya Corola na anapoulizwa kama marehemu alikuwa mlevi anasema hadhani ila asubuhi alisema alikuwa na malaria.
Je hali ya gari ilikuwaje? Gari limekuwa kama kopo lililofinyangwa. Mheshimiwa Wangwe alikuwa katika hali gani baada ya ajali? Aliumia maeneo ya kichwani na kifuani.
Deus Mallya yeye anasema ameumia mguu wa kushoto kama ameteguka tu na ana maumivu kichwani. Haamini kama amepona, ndio maajabu ya Mungu.
Mwisho, Mkuu wa mkoa wa Dodoma anasema baada ya mwili kuingia Dodoma tusubiri maelezo ya Spika kesho asubuhi. Nami naamua kwenda kulala nitamsubiri Spika aseme zaidi asubuhi.
Binafsi niseme tu, kifo hiki kimenisikitisha na ndio maana nikaamua kuandika makala hii usiku huu wakati nikufuatilia habari zaidi za kifo hiki. Nimalizie kwa maneno ya rafiki yangu katika message yake ambayo yameingia sasa hivi wakati namaliza : “ Aise inasikitisha ubunge sio kazi nzuri kwa sasa afrika hakuna la maana wanalofanya bali kuadhibiana kiainaaina, ngoja tuone mengi yanaweza kufichuka”. Mie nabaki nikijiuliza sijui ni nani atafuata manake nina hakika kabisa kwa mtiririko huu basi kuna mbunge mwingine atakufa kikao kijacho cha bajeti. Kazi kwenu wabunge.
Nimalizie kwa kusema: “ Chacha tulimpenda sana lakini Mafisadi walimchukia sana”. Mungu amlaze mahali pema peponi, Amina.
Ni saa nne na dakika arobaini na saba, mara nikitizama taarifa ya habari ya ITV usiku nashanga mstari mweusi wa maneno unakatiza katika runinga na maneno: “mbunge wa Tarime, mheshimiwa Chacha Wangwe amefariki dunia usiku kwa ajali ya Gari” habari zaidi fuatilia redio one.
Na kweli ninazima runinga yangu na kuanza kusikiliza redio one. Ninakutana na mahojiano kati ya watangazaji: Asia Mohamed na Jerry Muro akiripoti kutoka Dodoma. Wanahojiwa waheshimiwa mbalimbali kwa masikitiko bado wanaonekana kutaharuki. Mtangazaji anadai eti nyakati za mchana mheshimiwa Chacha alionekana akiteta na mheshimiwa Mudhihir, hii inanikumbusha huyu ni mhanga mwingine wa ajali katika bunge hili. Hisia fulani zinanijia akilini lakini sisemi kitu najinyamazia.
Nikiwa nimekwishaamini kuwa mheshimiwa huyu katutoka, navuta hisia kadhaa juu ya bwana huyu na mara moja nautambua Umachachari wake, ubishi wake hata pale pasipo na Mantiki lakini kwa yote , kauli ya John Cheyo inanikuna akihojiwa na Jerry Muro. Anasema: “Chacha alikuwa na msimamo ambao wengi wetu hatunao” . Nakubaliana na mheshimiwa Cheyo na ninaendelea kusikitika.
Mara ninaamua kumtumia mtu wangu wa karibu sms akiwa Dar es salaam nikimsihi afuatilie habari kuna tukio la kifo cha mbunge mashuhuri. Pia katika message yangu nampa hisia yangu kuwa sasa “ Chadema itachafuka hasa kwani kifo hiki kitatumiwa na wanazi kuonesha kukolimbana hakuko tu CCM”. Ninapoituma message ile mara napata message kutoka kwa rafiki mwingine akinihabarisha juu ya kifo cha Chacha. Ninamrudishia nikimsihi kuwa “Siasa za Afrika ni mchezo mchafu, nina hisia lazima kuna mkono wa mtu awe wa kambi ya marehemu ama kule tulikozoea kukolimba watu wabishi kama Wangwe”.
Hapo hapo napokea message nyingine ambayo inanijibu ile niliyotuma Dar es salaam: “Sio Chadema ni CCM walileta mgogoro alafu wamemuua ili tuone Chadema nao wana mchezo kama wao! Tunaelekea pazuri sana. Tutashuhudia mengi na ukweli utadhihirika mwisho”. Mie sijui kwanini watu wana maoni ya aina hiyo ila ndio jamii ya kitanzania ilipofikia sasa.
Inapofika saa sita na dakika kumi na sita usiku hisia zangu zinashangaa: Jerry Muro, mwandishi wa ITV anaongea na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, mheshimiwa Lukuvi ambaye anasema kuwa gari la Wangwe limepata ajali ya kuanguka baada ya kupasuka gurudumu. Lukuvi anamnukuu rafiki wa Wangwe ambaye alikuwa ndani ya gari la Wangwe na amepata michubuko tu. Anasema gari lenyewe lilibiringika mara nyingi sana na ndipo Israel akachukua roho ya mheshimiwa Chacha. Moja kwa moja hapa ninajenga kanuni za kihisia na chonganishi (conspiracy theories) kadhaa:
Moja, kwanini gari la mbunge kama tuyajuavyo ni magari imara , mazuri na nina hakika yanafanyiwa matengenezo bora, itakuwaje lipasuke tairi tena nyakati za usiku pasipo na joto sana la kupasha hiyo chubu? Inawezekana kirahisi namna hiyo? Au tuseme Chacha anatembelea ulimu?
Pili, hili Bunge letu lina matatizo gani? Ni balaa ama ni nini? Kwanini kila kikao kinapokutana hasa cha bajeti lazima Mbunge afe?
Tatu, kwanini katika bunge hili ukiacha mbunge mmoja tu, wote waliokufa kulikuwa na hali ya kuwa na maadui hasa juu ya misimamo ya marehemu hawa?
Nne, kwanini wabunge wa bunge hili wanapatwa na madhila kama ajali ama vifo mara baada ya kuwa ni watu wenye misimamo yenye kutetea maslahi ya umm a sana ama kudhoofisha maslahi ya umma?
SHUHUDA WA AJALI
Saa sita na dakika thelathini na sita, redio one inaripoti kuwa ndio mwili wa Chacha Unaingia hospitali ya Dodoma kutoka eneo la ajali huko Kongwa. Gari ni Land Cruiser namba: SM.4297 la Halmashauri ya Kongwa. Jerry Muro anaongea na Rafiki wa mheshimiwa Chacha ambaye alikuwa akisafiri na mheshimiwa Chacha, ndugu Deus Mallya, rafiki wa karibu wa Chacha, anaeleza walitoka Dodoma wakienda Dar, anasema alisikia kishindo kikubwa sana kabla ya ajali, ninapata hisia sio ajabu inawezekana gari hilo lilikuwa limetegwa bomu labda, na gari liliruka juu na kufuatiwa na mbiringiko mkubwa sana.
Kuhusu mwendo wa gari Deus Mallya anasema kuwa Mheshimiwa Wangwe hana hakika kama alifunga mkanda. Yeye alifunga mkanda, lakini kimazingira inaonekana marehemu alibanwa kwa hiyo napata hisia alikuwa amefunga mkanda la sivyo kwa mbiringiko huo lazima angerushwa nje.
Je mheshimiwa Wangwe alikuwa kwenye hali gani? Mwanzoni nilidhani ni Land Cruiser, kumbe sio, ila ni gari dogo. Alikuwa anaendesha gari aina ya Corola na anapoulizwa kama marehemu alikuwa mlevi anasema hadhani ila asubuhi alisema alikuwa na malaria.
Je hali ya gari ilikuwaje? Gari limekuwa kama kopo lililofinyangwa. Mheshimiwa Wangwe alikuwa katika hali gani baada ya ajali? Aliumia maeneo ya kichwani na kifuani.
Deus Mallya yeye anasema ameumia mguu wa kushoto kama ameteguka tu na ana maumivu kichwani. Haamini kama amepona, ndio maajabu ya Mungu.
Mwisho, Mkuu wa mkoa wa Dodoma anasema baada ya mwili kuingia Dodoma tusubiri maelezo ya Spika kesho asubuhi. Nami naamua kwenda kulala nitamsubiri Spika aseme zaidi asubuhi.
Binafsi niseme tu, kifo hiki kimenisikitisha na ndio maana nikaamua kuandika makala hii usiku huu wakati nikufuatilia habari zaidi za kifo hiki. Nimalizie kwa maneno ya rafiki yangu katika message yake ambayo yameingia sasa hivi wakati namaliza : “ Aise inasikitisha ubunge sio kazi nzuri kwa sasa afrika hakuna la maana wanalofanya bali kuadhibiana kiainaaina, ngoja tuone mengi yanaweza kufichuka”. Mie nabaki nikijiuliza sijui ni nani atafuata manake nina hakika kabisa kwa mtiririko huu basi kuna mbunge mwingine atakufa kikao kijacho cha bajeti. Kazi kwenu wabunge.
Nimalizie kwa kusema: “ Chacha tulimpenda sana lakini Mafisadi walimchukia sana”. Mungu amlaze mahali pema peponi, Amina.
Saturday, July 26, 2008
HABARI ZA JUMAPILI
Kutatokea kupatwa kwa jua wiki ijayo. Kupatwa kwa jua nusu hakutaonekana Afrika siku hiyo.
Kumbe udikteta na ubabe uongozini una faida? Je kuna faida gani kuweka maafisa wa Jeshi kama ndio mabosi wa jeshi la polisi?
Huko Kenya wanafunzi wa sekondari wanagoma, kumbe ni halali kugoma.
ICC imeamua kulia na dikteta wa Sudan, je kwanini ICC inadili na madikteta wa nchi masikini tu?
Kumbe udikteta na ubabe uongozini una faida? Je kuna faida gani kuweka maafisa wa Jeshi kama ndio mabosi wa jeshi la polisi?
Huko Kenya wanafunzi wa sekondari wanagoma, kumbe ni halali kugoma.
ICC imeamua kulia na dikteta wa Sudan, je kwanini ICC inadili na madikteta wa nchi masikini tu?
Monday, July 21, 2008
MAKAMU WA RAIS ANAPOINGILIA NDOA YA DEREVA
Profesa Bukenya ni makama wa rais Uganda. Ana vituko, hebu vione.
MUGABEISM – FALSAFA ILIYOZINDULIWA NA NYERERE
Robert Mugabe hatimaye jana alikutana na hasimu wake wa kisiasa na kusaini makubaliano ya kuanza kujadiliana ili kutanzua mgogoro mkubwa wa kisiasa wa Zimbabwe. Ni hatua ambayo imeendelea kunishangaza juu ya mwenendo mzima wa siasa za Kiafrika kama kweli zinafuata demokrasia ya Kimagharibi au ni demokrasia mpya ya Kiafrika. Morgan Tsavingarai yeye jana kasema ni siku ya kihistoria kukutana na Mugabe tangu miaka kumi.
Kwangu nimeona tukio la hili la kukubali kuzungumza kwa watu hawa wawili kama mwelekeo tata wa siasa za Zimbabwe na pia kama hatua mpya kwa waafrika kujiuliza mambo kadhaa: Moja, nianze na Mugabe mwenyewe ni mtu wa aina yake. Kati ya maraisi wote wanaoitawala Afrika kwa sasa na hata wale waliowahi kutawala bara hili ndiye msomi sana kuliko wote. Mugabe ana shahada (degree) saba za chuo kikuu na wala sio zile zilizoeleka kwa vigogo wetu kutunikiwa za heshima. Huwa nafurahi kumsikiliza kila anapoongea kwa ufasaha lugha ya kiingereza huku akionekana hata kwa umri mkubwa bado ana uwezo mkubwa wa kufikiri.
Pili Mugabe pamoja na akili zote za darasani alizonazo amekosa busara za umri alionao. Nasema hivi kwani nadhani Mugabe ni mwanamapinduzi hasa wa harakati za kiafrika (Pan Africanist) ambaye kateleza sana kwa kile anachokitetea ama labda hajateleza basi ndio mwanzo wa Uwanamapinduzi mpya wa kiafrika. Namfananisha Mugabe na Mwalimu Nyerere ambaye naye alikuwa ni mwanamapinduzi halisi wa kiafrika ambaye hakuwa tayari kuwaruhusu mabepari waimeze nchi yetu chini ya utawala wake. Aliamua aanzishe mfumo wa kisiasa wa kiafrika hasa kwa kutumia mfumo wa kijamaa ambao asili yake ilikuwa ni mfumo mama wa sera za mwanafalsafa wa kijerumani Marx (Marxism).
Mfumo huu wa Ujamaa kwa kiasi fulani haukufanikiwa hadi pale Mwalimu Nyerere alipoamua ang’atuke (1985) kwani alijua wazi hawezi kushindana na mabepari kwa njia yeyote. Kwa kipindi kile nilikuwa nasoma shule ya msingi darasa la tatu nakumbuka jinsi maisha yalivyokuwa magumu kukikosekana hata bidhaa muhimu kama sukari ama sabuni za kuogea ama kufulia na biashara za magendo kushamiri hasa mpakani na Kenya. Nadhani Nyerere hakuwa tayari kuvumilia haya na akaamua akapumzike kwao Butiama.
Tatu, Mugabe pia alikuwa katika imani moja na Nyerere lakini yeye akaamua atofautiane kidogo na Nyerere kwa kuamua kupigana na maadui wakuu yaani mabepari. Ni vita ngumu sana na kuishinda hii mimi binafsi kama mwafrika na mzalendo siamini inawezekana hata kidogo kwa sasa. Nasema hivi kwani naona mfumo wa dunia kwa sasa ni wa unyonyaji kwa nchi kubwa kuzilazimisha nchi masikini kufuata matakwa yao na hata kwa kuruhusu rasilimali zetu kuchukuliwa kwa visingizio vya uwekezaji ama ukosefu wa teknolojia kwa nchi masikini.
Ni katika mtizamo wangu huu nadhani ndio maana Mwalimu Nyerere aliliona hili na ndio maana alikuwa kila akifanya hotuba anakumbushia eti siku zijazo kutakuwa na hali fulani na ambayo ndio tunaiona leo hii hapa Tanzania. Kwa Mugabe yeye ni tofauti na haoni sababu kuwaruhusu mabepari kuzikalia ardhi ya Zimbabwe na kufanya shughuli zao. Hivyo kwake aliona ni bora kuwanyang’anya ardhi na hapo ikawa ndio mwanzo wa dhahama lote hadi leo. Mwenzake Tsavingarai kwa kuona jinsi ambavyo unyang’anyi huo wa ardhi kutoka kwa walowezi ulivyoleta dhahama yeye akaamua kukubali kutumiwa na mabepari. Ni wazi Tsavingarai ni kibaraka (puppet) wa Waingereza; lakini pia naamini anatekeleza matakwa ya mfumo wa kidunia kwa sasa bila kujali ni kiasi gani Wazimbabwe wengi watakavyoumizwa na mfumo wa serikali itakayokuwa chini ya utawala wake kama angelishinda uchaguzi.
Nakubali kuwa Mugabe ndie mwanamapinduzi halisi anayetakiwa Afrika kwa wakati huu. Kwani yeye kaamua ajaribu kuendeleza pale akina Nyerere, Nkrumah, Sekou Toure na Thomas Sankara walipoachia baada ya tawala zao kushindwa kabisa kuhimili mitetemo ya mabepari. Mugabe aliamua avuruge uchaguzi unaoendeshwa kwa taratibu za kimagharibi zilizoanzia kule Athens Ugiriki karne nyingi zilizopita. Yeye kaja na demokrasia mpya kabisa ya kiafrika kwa kuhakikisha watu wanatishwa, kupigwa marungu, na hata kuuawa ili mradi tu wasivutwe na kutekwa na hisia za kupenda sera za mabepari. Hali hii ilifanya uchaguzi uharibike na mpinzani mkuu akaamua kujitoa nah ii ikamruhusu Mugabe kushinda kwa ulaini uchaguzi wa Zimbabwe.
Demokrasia ya Kiafrika haina vigezo vingi; yaani haina mambo ya taratibu za upigaji kura kama kujiandikisha, taratibu za kampeni, uhuru wa kutumia vyombo vya habari kwa wapinzani hauna nafasi kabisa. Ni uchaguzi ambao unazingatia tu ni nani tume ya uchaguzi itamtangaza kama ni mshindi. Hii ni mbinu ambayo hata hapa Tanzania imekuwa ikitumika hasa kule Zanzibar katika chaguzi kadhaa chini ya uasisi wa Mwalimu Nyerere tangu mwaka 1995.
Mugabe alifanikiwa kwa njia hii na hata pale jumuiya ya kimataifa ilipojaribu kuweka vikwazo iligonga mwamba pale Wachina na Warusi walipoamua kupiga kura ya turufu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Huu ukawa ushindi mkubwa kwa Mugabe na sasa ameamua kuanza mazungumzo na Tsavingirai, kwa kiasi fulani ni hatua moja mbele zaidi ya watangulizi waliowahi kupingana na mabepari lakini wakashindwa. Ninasema hivi kwani naamini kwa hotuba aliyoitoa baada ya kusaini na hasimu wake Tsvangira, kuwa sasa “Tuanze kuwaza na kutenda kizimbabwe” ilionesha kuwa hataki mawazo ya kibepari na hii ndio imekuwa shida yake kubwa. Anataka mambo yafanyike Kiafrika kwa kuzingatia mashiko ya kiafrika.
Kufikia hapa ndipo napata maswali ambayo siku zijazo nitayajengea hoja zaidi: Kwanza, Je Mugabe kama atakubali kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na Tsvangira, je ataweza kuwafanya hawa jamaa wa MDC kuwaza na kutenda “Kizimbabwe” ? Hapa nina mashaka sana, sijui itakuwaje.
Pili, je kwa hatua iliyofikiwa hadi leo ya chuki dhidi ya Waingereza na Wamarekani, itawezekana Zimbabwe chini ya Mugabe iwe na ushirikiano wowote wenye manufaa na nchi hizo? Na je nchi zingine zitachukuliaje hatua hii ya maelewano kati ya mafahali hawa wawili, wataweza kuanzisha mashirikiano mapya?
Tatu, Je inawezekana nchi za Kiafrika zikaendelea na utengamano ikiwa hazifuati matakwa ya kiutandawazi ambayo kwayo lengo lake ni “utandawizi” ambao Mugabe na akina Nyerere hawautaki? Na je kama kweli Zimbabwe itatulia je mapinduzi haya mapya ya Mugabe (Mugabeism) yataenea barani Afrika ili kumkomboa mwafrika dhidi ya Utandawizi?
Labda niseme tu ni maoni yangu kuwa sina imani kama kweli hii “Mugabeism” ina tija sana kwa bara letu. Ni falsafa ambayo ni tamu sana kimatamshi lakini kiutekelezaji nadhani ni chanzo cha migogoro hasa ikizingatiwa bado bara letu hatujawekeza ipasavyo katika sekta ya elimu kuweza kuwa na wanataaluma hasa wahandisi ambao wangewezesha nchi zetu kuweza kujitengenezea na kufaidi rasilimali zake kwa asilimia mia moja bila kuibiwa kwa kutumia utandawizi. Ni wazi Zimbabwe na hii “Mugabeism” haitakuwa na tija yeyote ingawa ni tamu masikioni miongoni mwa wazalendo wa kiafrika lakini mtu ukifikiri sana ni bure tu. Ni falsafa inayojaribu kugeuza mwenendo wa dunia pale pasipowezekana.
Naiona Zimbabwe kama ilivyokuwa Kenya kwani mara baada ya Kibaki kukubaliana na Raila, imekuwa kama kuahirisha mwelekeo mpya wa siasa za Kenya na kuendelea mawazo ya kale ( status quo). Mugabe alipaswa atumie busara kwa kuiga wenzake akina Nyerere ama Moi walipoamua kujing’atua pale upepo ulipoonesha wazi kuwa wimbi la dunia lilikuwa dhidi ya falsafa zao na kama wangelijaribu kushinikiza falsafa zao basi wananchi wengi wangeumia sana. Kwa akina Mugabe na Kibaki wao si tija watu kufa ama kuumia ilimradi falsafa zao zinabaki madarakani.
Huku haya yote yakitokea nitabaki najiuliza bila jibu inakuwaje mtu msomi wa shahada saba ang’ang’ane na falsafa potofu (Mugabeism) yake huku uchumi mzima wa nchi ukiangamia? Ni wazi Mugabe atabakia kama mwanamapinduzi halisi ila ameshindwa kuelewa kuwa katika dunia ya utandawizi kamwe mtu huwezi kuwashinda mabepari. Huu ndio ukweli mchungu kwetu wote tunaoipenda Afrika. Na si Wachina wala Warusi ambao watairejesha Zimbabwe katika mafanikio ya kiuchumi kama zamani bali ni hao Waingereza ama Wamarekani ndio tu wanaoweza kurekebisha mambo ya Zimbabwe.
Mwisho, hapa nataka wote tujiulize hivi Ali Hasan Mwinyi kama angeliamua kufuata sera za Nyerere alipopewa jukumu la kuliongoza Taifa la Tanzania je nchi yetu ingelifika hapa ilipo leo? Umefika wakati kwa watawala wetu kujua mipaka ya sera wanazozitetea la sivyo wataharibu kabisa nchi wanazopigania na kujitoa mhanga kuzipigania. Nina mashaka sana bila kufuata kile Watandawizi wanataka basi ni kiama kwa nchi zetu. Kama nimekosea basi naomba nipewe wazo mbadala.
Kwangu nimeona tukio la hili la kukubali kuzungumza kwa watu hawa wawili kama mwelekeo tata wa siasa za Zimbabwe na pia kama hatua mpya kwa waafrika kujiuliza mambo kadhaa: Moja, nianze na Mugabe mwenyewe ni mtu wa aina yake. Kati ya maraisi wote wanaoitawala Afrika kwa sasa na hata wale waliowahi kutawala bara hili ndiye msomi sana kuliko wote. Mugabe ana shahada (degree) saba za chuo kikuu na wala sio zile zilizoeleka kwa vigogo wetu kutunikiwa za heshima. Huwa nafurahi kumsikiliza kila anapoongea kwa ufasaha lugha ya kiingereza huku akionekana hata kwa umri mkubwa bado ana uwezo mkubwa wa kufikiri.
Pili Mugabe pamoja na akili zote za darasani alizonazo amekosa busara za umri alionao. Nasema hivi kwani nadhani Mugabe ni mwanamapinduzi hasa wa harakati za kiafrika (Pan Africanist) ambaye kateleza sana kwa kile anachokitetea ama labda hajateleza basi ndio mwanzo wa Uwanamapinduzi mpya wa kiafrika. Namfananisha Mugabe na Mwalimu Nyerere ambaye naye alikuwa ni mwanamapinduzi halisi wa kiafrika ambaye hakuwa tayari kuwaruhusu mabepari waimeze nchi yetu chini ya utawala wake. Aliamua aanzishe mfumo wa kisiasa wa kiafrika hasa kwa kutumia mfumo wa kijamaa ambao asili yake ilikuwa ni mfumo mama wa sera za mwanafalsafa wa kijerumani Marx (Marxism).
Mfumo huu wa Ujamaa kwa kiasi fulani haukufanikiwa hadi pale Mwalimu Nyerere alipoamua ang’atuke (1985) kwani alijua wazi hawezi kushindana na mabepari kwa njia yeyote. Kwa kipindi kile nilikuwa nasoma shule ya msingi darasa la tatu nakumbuka jinsi maisha yalivyokuwa magumu kukikosekana hata bidhaa muhimu kama sukari ama sabuni za kuogea ama kufulia na biashara za magendo kushamiri hasa mpakani na Kenya. Nadhani Nyerere hakuwa tayari kuvumilia haya na akaamua akapumzike kwao Butiama.
Tatu, Mugabe pia alikuwa katika imani moja na Nyerere lakini yeye akaamua atofautiane kidogo na Nyerere kwa kuamua kupigana na maadui wakuu yaani mabepari. Ni vita ngumu sana na kuishinda hii mimi binafsi kama mwafrika na mzalendo siamini inawezekana hata kidogo kwa sasa. Nasema hivi kwani naona mfumo wa dunia kwa sasa ni wa unyonyaji kwa nchi kubwa kuzilazimisha nchi masikini kufuata matakwa yao na hata kwa kuruhusu rasilimali zetu kuchukuliwa kwa visingizio vya uwekezaji ama ukosefu wa teknolojia kwa nchi masikini.
Ni katika mtizamo wangu huu nadhani ndio maana Mwalimu Nyerere aliliona hili na ndio maana alikuwa kila akifanya hotuba anakumbushia eti siku zijazo kutakuwa na hali fulani na ambayo ndio tunaiona leo hii hapa Tanzania. Kwa Mugabe yeye ni tofauti na haoni sababu kuwaruhusu mabepari kuzikalia ardhi ya Zimbabwe na kufanya shughuli zao. Hivyo kwake aliona ni bora kuwanyang’anya ardhi na hapo ikawa ndio mwanzo wa dhahama lote hadi leo. Mwenzake Tsavingarai kwa kuona jinsi ambavyo unyang’anyi huo wa ardhi kutoka kwa walowezi ulivyoleta dhahama yeye akaamua kukubali kutumiwa na mabepari. Ni wazi Tsavingarai ni kibaraka (puppet) wa Waingereza; lakini pia naamini anatekeleza matakwa ya mfumo wa kidunia kwa sasa bila kujali ni kiasi gani Wazimbabwe wengi watakavyoumizwa na mfumo wa serikali itakayokuwa chini ya utawala wake kama angelishinda uchaguzi.
Nakubali kuwa Mugabe ndie mwanamapinduzi halisi anayetakiwa Afrika kwa wakati huu. Kwani yeye kaamua ajaribu kuendeleza pale akina Nyerere, Nkrumah, Sekou Toure na Thomas Sankara walipoachia baada ya tawala zao kushindwa kabisa kuhimili mitetemo ya mabepari. Mugabe aliamua avuruge uchaguzi unaoendeshwa kwa taratibu za kimagharibi zilizoanzia kule Athens Ugiriki karne nyingi zilizopita. Yeye kaja na demokrasia mpya kabisa ya kiafrika kwa kuhakikisha watu wanatishwa, kupigwa marungu, na hata kuuawa ili mradi tu wasivutwe na kutekwa na hisia za kupenda sera za mabepari. Hali hii ilifanya uchaguzi uharibike na mpinzani mkuu akaamua kujitoa nah ii ikamruhusu Mugabe kushinda kwa ulaini uchaguzi wa Zimbabwe.
Demokrasia ya Kiafrika haina vigezo vingi; yaani haina mambo ya taratibu za upigaji kura kama kujiandikisha, taratibu za kampeni, uhuru wa kutumia vyombo vya habari kwa wapinzani hauna nafasi kabisa. Ni uchaguzi ambao unazingatia tu ni nani tume ya uchaguzi itamtangaza kama ni mshindi. Hii ni mbinu ambayo hata hapa Tanzania imekuwa ikitumika hasa kule Zanzibar katika chaguzi kadhaa chini ya uasisi wa Mwalimu Nyerere tangu mwaka 1995.
Mugabe alifanikiwa kwa njia hii na hata pale jumuiya ya kimataifa ilipojaribu kuweka vikwazo iligonga mwamba pale Wachina na Warusi walipoamua kupiga kura ya turufu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Huu ukawa ushindi mkubwa kwa Mugabe na sasa ameamua kuanza mazungumzo na Tsavingirai, kwa kiasi fulani ni hatua moja mbele zaidi ya watangulizi waliowahi kupingana na mabepari lakini wakashindwa. Ninasema hivi kwani naamini kwa hotuba aliyoitoa baada ya kusaini na hasimu wake Tsvangira, kuwa sasa “Tuanze kuwaza na kutenda kizimbabwe” ilionesha kuwa hataki mawazo ya kibepari na hii ndio imekuwa shida yake kubwa. Anataka mambo yafanyike Kiafrika kwa kuzingatia mashiko ya kiafrika.
Kufikia hapa ndipo napata maswali ambayo siku zijazo nitayajengea hoja zaidi: Kwanza, Je Mugabe kama atakubali kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na Tsvangira, je ataweza kuwafanya hawa jamaa wa MDC kuwaza na kutenda “Kizimbabwe” ? Hapa nina mashaka sana, sijui itakuwaje.
Pili, je kwa hatua iliyofikiwa hadi leo ya chuki dhidi ya Waingereza na Wamarekani, itawezekana Zimbabwe chini ya Mugabe iwe na ushirikiano wowote wenye manufaa na nchi hizo? Na je nchi zingine zitachukuliaje hatua hii ya maelewano kati ya mafahali hawa wawili, wataweza kuanzisha mashirikiano mapya?
Tatu, Je inawezekana nchi za Kiafrika zikaendelea na utengamano ikiwa hazifuati matakwa ya kiutandawazi ambayo kwayo lengo lake ni “utandawizi” ambao Mugabe na akina Nyerere hawautaki? Na je kama kweli Zimbabwe itatulia je mapinduzi haya mapya ya Mugabe (Mugabeism) yataenea barani Afrika ili kumkomboa mwafrika dhidi ya Utandawizi?
Labda niseme tu ni maoni yangu kuwa sina imani kama kweli hii “Mugabeism” ina tija sana kwa bara letu. Ni falsafa ambayo ni tamu sana kimatamshi lakini kiutekelezaji nadhani ni chanzo cha migogoro hasa ikizingatiwa bado bara letu hatujawekeza ipasavyo katika sekta ya elimu kuweza kuwa na wanataaluma hasa wahandisi ambao wangewezesha nchi zetu kuweza kujitengenezea na kufaidi rasilimali zake kwa asilimia mia moja bila kuibiwa kwa kutumia utandawizi. Ni wazi Zimbabwe na hii “Mugabeism” haitakuwa na tija yeyote ingawa ni tamu masikioni miongoni mwa wazalendo wa kiafrika lakini mtu ukifikiri sana ni bure tu. Ni falsafa inayojaribu kugeuza mwenendo wa dunia pale pasipowezekana.
Naiona Zimbabwe kama ilivyokuwa Kenya kwani mara baada ya Kibaki kukubaliana na Raila, imekuwa kama kuahirisha mwelekeo mpya wa siasa za Kenya na kuendelea mawazo ya kale ( status quo). Mugabe alipaswa atumie busara kwa kuiga wenzake akina Nyerere ama Moi walipoamua kujing’atua pale upepo ulipoonesha wazi kuwa wimbi la dunia lilikuwa dhidi ya falsafa zao na kama wangelijaribu kushinikiza falsafa zao basi wananchi wengi wangeumia sana. Kwa akina Mugabe na Kibaki wao si tija watu kufa ama kuumia ilimradi falsafa zao zinabaki madarakani.
Huku haya yote yakitokea nitabaki najiuliza bila jibu inakuwaje mtu msomi wa shahada saba ang’ang’ane na falsafa potofu (Mugabeism) yake huku uchumi mzima wa nchi ukiangamia? Ni wazi Mugabe atabakia kama mwanamapinduzi halisi ila ameshindwa kuelewa kuwa katika dunia ya utandawizi kamwe mtu huwezi kuwashinda mabepari. Huu ndio ukweli mchungu kwetu wote tunaoipenda Afrika. Na si Wachina wala Warusi ambao watairejesha Zimbabwe katika mafanikio ya kiuchumi kama zamani bali ni hao Waingereza ama Wamarekani ndio tu wanaoweza kurekebisha mambo ya Zimbabwe.
Mwisho, hapa nataka wote tujiulize hivi Ali Hasan Mwinyi kama angeliamua kufuata sera za Nyerere alipopewa jukumu la kuliongoza Taifa la Tanzania je nchi yetu ingelifika hapa ilipo leo? Umefika wakati kwa watawala wetu kujua mipaka ya sera wanazozitetea la sivyo wataharibu kabisa nchi wanazopigania na kujitoa mhanga kuzipigania. Nina mashaka sana bila kufuata kile Watandawizi wanataka basi ni kiama kwa nchi zetu. Kama nimekosea basi naomba nipewe wazo mbadala.
Saturday, July 19, 2008
Bashiri Kukamatwa?
Wiki hii ilikuwa siku ya Kupanga Uzazi je unajua kupanga uzazi ni vizuri sana? Pia jambo lililosemwa sana ni hii hatua ya Mahakama ya ICC kutaka kumkamata Rais Bashir.
Friday, July 04, 2008
MUSEVENI KAMA MUGABE?
Saa nyingine serikali za Kiafrika zinajiabisha sana pale zinapowatumia wahuni tu wa mtaani katika shughuli zake. Ona hili la Uganda jinsi lilivyo. Uganda ya Museveni sasa imeanza kumchoka; kuna kila dalili kuwa wapo watu tena wengine wa karibu na Museveni wameanza kupanga jinsi ya kuondokana naye. Hii inachangiwa na kukuwa kwa rushwa na pia jeuri ya baadhi ya maswahiba wa Rais Museveni ambao kwao hata mkaguzi mkuu wa serikali si kitu.
Si hayo tu, kuna hili la Mugabe kufananishwa na Mobutu.
Si hayo tu, kuna hili la Mugabe kufananishwa na Mobutu.
Friday, June 27, 2008
UGANDA YAMPOTEZA MSOMI MWANASIASA
Wiki hii Chama cha Upinzani nchini Uganda kimempoteza Mwenyekiti wake Dr. Kiggundu ambaye amewahi kuwa gavana wa benki kuu.
BARACK OBAMA NA MATUMAINI FEKI YA WAAFRIKA NA WEUSI
Mapema mwezi wa Juni, tarehe 3 mwaka huu, Barack Obama alifikia hatua kubwa katika harakati zake za kuteuliwa mgombea wa Chama cha Democratic. Ni hatua ambayo Wamarekani wanaiita (Nominee designate) mgombea mtarajiwa. Siku hiyo hapa Tanzania mkutano wa nane wa Taasisi ya Sullivan ulikuwa ukifanyika. Aliyewahi kujaribu harakati za kuchaguliwa, Mchungaji Jesse Jackson alinena kwa furaha akijivunia ni ushindi kwa weusi. Karibu waongeaji wote walizungumza juu ya hili kwa maono ya ushindi wa weusi.
Nikiwa kama mtanzania, mtu mweusi, nimefarijika pia kwa ushindi wa Seneta Barack Obama. Kufarijika kwangu si kwa mashiko ya rangi; yaani mweusi kashinda basi nami nifurahi. Kwangu nimeshangazwa karibu weusi wote wanamshabikia Obama eti kwa kuwa ni mweusi. Nina mashaka kama kweli hisia zetu zinaegemea zaidi rangi basi nadiriki kusema kuwa tusipokuwa makini nasi pia ni wabaguzi wa rangi wakubwa.
Nina wasiwasi: wote wanaouchukulia ushindi wa Obama kama ushindi kwasababu ni mweusi basi wamepotea njia. Ni lazima watu tufikiri kwa kina na si kushabikia tu ilihali inawezekana kabisa Obama hatakuwa na maslahi yoyote kwa waafrika na hata kwa watu weusi sehemu mbalimbali za dunia.
Labda niwarejeshe kwenye historia: Raisi wa zamani wa Marekani, Ruthirford Hayes aliwahi kunena kuwa “Us government is a government of the corporations, by corporations for the corporations”. Alimaanisha kuwa serikali ya Marekani ni serikali ya Makampuni, kwa maslahi ya Makampuni na inaendeshwa na Makampuni. Hapa alikuwa anajaribu kutanzua kiza kinene (illusion) kwenye maana ya demokrasia kama ilivyokuwa imeelezwa awali na mtangulizi wake Lincoln pale alipoweka maneno: “Government of the People for the People by the People” yaani: “serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao” katika katiba ya nchi hiyo.
Ni katika msingi wa kuingalia serikali ya Marekani kama inayoongozwa na mtizamo wa Katiba kuheshimiwa bila ubazazi wa aina yeyote kama tunavyoshuhudia hapa kwetu, basi kama Obama atachaguliwa kuwa raisi wa Marekani tujue kabisa atafanya kazi kwa misingi ya Rais wa zamani Ruthirford Hayes. Hapa ndipo panaponifanya nisiwe na matumaini kama kweli mtu mweusi kuwa Rais wa Marekani basi tutafaidika na lolote tofauti na marasi wengine weupe waliokwishapita na kutawala Marekani. Ni vyema tumfurahie Seneta Obama kutokana na wajihi wake: ni jinsi gani ameweza kuchambua masuala mbalimbali kwa ufasaha na kuonesha jinsi gani anavyoweza kufikiri. Ni kigezo hiki tu naweza kufurahia ushindi wa Obama na wala kamwe si rangi yake. Kinyume na hapo naona ni mtizamo wa kibaguzi ambao hauna nafasi katika dunia ya kileo.
USHINDI HARAKATI ZA MTU MWEUSI
Kuna wengine wanauona ushindi wa Seneta Obama kama vile ni ushindi wa harakati za kutafuta haki za mtu mweusi. Hebu nikumbushie harakati za kumkomboa mtu mweusi nadhani zilianza siku nyingi chini ya watu kama akina Willium Du Bois, Marcus Garvey, George Padmore, Malcolm X, Martin Luther King, Nelson Mandela, Julius Nyerere, Jomo Kenyatta, Kenneth Kaunda, Robert Nesta Marley hadi akina Jesse Jackson na Luis Farhani wa leo hii Marekani.
Nimejaribu kupiga picha na nimeona hadi leo hii mtu mweusi kafikia mafanikio mengi katika nyanja nyingi. Kwa mfano, miongo mitatu iliyopita tunaweza kung’amua mafanikio ya mtu mweusi kama ifuatavyo:
Mosi, mwishoni mwa miaka ya 1970, waafrika weusi wa Marekani waliweza kutawala fani ya muziki kimataifa pale mziki aina ya kufokafoka ulikuwa sana kuanzia New York na kuua kabisa muziki wa Rock uliokuwa ukitawala.
Pili, baada ya mafanikio ya muziki, mwafrika asilia alianza kuonesha mafanikio duniani katika mchezo wa soka. Mwaka 1990, timu ya Taifa ya soka ya Cameroon (Indomitable Lions) ilifikia hatua ya robo fainali ya Kombe la dunia kule Italia chini ya Roger Milla. Baadaye mwaka 2002 kule Korea na Japan timu nyingine ya Senegal nayo ilifika hatua kama hiyo.
Jambo la tatu, katika miaka hiyo hiyo ya 1990, kule Afrika ya Kusini, Nelson Mandela na wafungwa wenzake kama akina Govan Mbeki, Walter Sisulu waliachiwa huru. Baadaye mwaka 1994 waafrika walio wengi wakafanikiwa kuunda serikali ndani ya nchi ambayo walinyimwa haki hiyo kwa miongo kadhaa. Si hapa Afrika tu mtu mweusi kafanikiwa, kwa mfano, mwaka 1997, kijana mweusi wa Marekani: Eldrick ‘Tiger’ Woods akaweka historia kushinda mashindano makubwa ya mchezo wa gofu “US Masters” na ametawala mchezo huo kidunia hadi ninapoandika makala hii. Mchezo wa kikapu ndio usiseme, mtu mweusi katawala hasa.
TIJA YA MAFANIKIO YA MTU MWEUSI
Kwa ujumla mtu mweusi kafanikiwa sana kwa miaka ishirini iliyopita si kwenye fani ya sanaa na michezo tu. Bali hata kwenye mambo ya uongozi wa taasisi nyeti za kimataifa, mwafrika tayari anajivunia kuweza kuongoza katika nyadhifa za juu kabisa. Kwa mfano, Umoja wa Mataifa (UN) , mwaka 1991 – 1994 ulikuwa chini ya Butros Butros Ghali raia wa Misri, baadaye akarithiwa na mweusi hasa Koffi Atta Annan wa Ghana mwaka 1995. Ni kipindi hichohicho, Jumuiya ya Madola ilikuwa chini ya Chief Emeka Anyaoku wa Nigeria kama Katibu Mkuu. Haya yote ilikuwa ni kuionesha dunia kuwa mtu mweusi anaweza na anatambulika. Lakini tujiulize: Je kulikuwa na msaada gani mkubwa kwa waafrika pale yote haya yalipojitokeza? Nakumbuka tulifurahi na kushangilia kutokana na hisia zenye mashiko ya rangi.
Watu wengine wanaweza kujiuliza labda mafanikio mengi ya mtu mweusi niliyoyaelezea hayakutokea Marekani bali hapa Afrika chini ya waafrika. Lakini kwa sasa yanatokea kule Marekani, ambalo ndilo Taifa linalotoa mwongozo wa dunia basi hatuna budi kuwa na matarajio. Na hii ndio hisia ninayoiona miongoni mwetu wengi kama “matumaini feki”. Kwangu siamini hivyo na kamwe sitaamini. Labda nikumbushie tu pale Raisi George Bush alipoingia madarakani na kumteua Collin Luther Powel kama mweusi wa kwanza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, yaani cheo cha juu kabisa baada ya Raisi na Makamu wake Marekani. Raisi Bush alimteua baadaye mweusi mwingine Condoleza Rice katika nafasi hiyo ya juu kabisa hadi wakati naandaa makala hii.
Pia ni miaka si chini ya mitatu iliyopita, mwafrika mzaliwa wa Uganda John Sentamu alichaguliwa kuwa Askofu wa jimbo la York huko Uingereza. Hii ni nafasi ya pili kwa cheo ndani ya kanisa la Anglikana duniani. Katika haya yote yanayohusu ukombozi wa mwafrika ni mafanikio ambayo wanaharakati wanatumia mara nyingi neno la kiingereza “African Renaissance” yaani kuzaliwa upya kwa mwafrika.
Kwangu hili naliona pia kwa mtizamo huo kwani mwafrika ameweza kuondokana na kadhia za kibaguzi za zamani. Lakini tujiulize swali: Hivi mafanikio yote hayo yamesaidiaje weusi wa dunia hii? Tuache ukichaa, hebu angalia hata kule Afrika ya Kusini sasa mtu mweusi anapinga mweusi mwenzake kuishi nchini mwake. Umasikini wa mtu mweusi uliosababishwa na ufisadi wa wanaharakati wa zamani umetufikisha hapa tulipo. African Reinassance imepoteza mwelekeo huko Afrika Kusini kwa Madiba. Yote ni kwasababu mtu mweusi amekubali awe mtumishi na wakala wa mfumo wa kiutawala wa aina ya: “ corporate by corporation for the corporation”. Akina Raisi Mbeki na wapigania uhuru wenzake wamegeuka umma wa weusi na kuacha kuwatumikia na kuyatumikia makampuni.
Vivyo hivyo, nadhani hata Seneta Barack Obama atafuata mwelekeo huohuo kwa kuitumikia katiba ya Marekani ambayo imejaa lugha ya giza ikimaanisha mambo ambayo kimatendo ni kinyume na maneno. Yaani ikifuata mwelekeo wa Raisi Hayes badala ya ule sahihi wa Lincoln.
Ndio maana nilishangazwa sana mara baada ya Obama kuthibitisha kuwa ni mgombea mtarajiwa, hotuba yake ya kwanza mjini Washington ilikuwa ni mbele ya umati wa watu 7000 uliojumuisha “Kamati ya Mambo ya Waisraiel – Wamarekani ( Jewish American Israel Public Affairs Committee – AIPAC. Tujiulize ikiwa weusi wengi ndio waliompigia kura ilikuwaje aanze na shukrani kwa Wayahudi?
Dhahiri mwelekeo hapa wa dunia lazima tutumie bongo kufikiri na si kufuata hisia tu. Barack Obama hana njia nyingine ila ataungana na wale wengine niliowataja awali kama alama ya “African Reinassance” ambao wamemtangulia katika kuwatumikia wazungu. Kwani katika demokrasia ya leo, ule mtizamo wa Raisi Lincoln ndivyo sivyo. Mambo ya ‘Serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao’ ni hadithi ya alinacha. Democrasia leo ni kutumikia makampuni makubwa yenye ushawishi. Haya ndiyo yenye kupenyeza rupia kusaidia kampeni za akina Seneta Obama ili wayatumikie pindi watakaposhinda. Ni kama vile hapa kwetu Tanzania vigogo fulani walivyojiundia vikampuni kwa mgongo wa EPA ili kupata fedha za kampeni. Obama yeye hakutumia mbinu za kibazazi za kujiundia vijikampuni feki ila anafadhiliwa na makampuni ambayo lazima alipe fadhila.
Mwisho, Seneta Obama ataungana na waliomtangulia: Koffi Annan, Colin Powel, Condoleza Rice, Chief Emeka Anyaoku na hata mama yetu mpendwa Asha Rose Migiro ambao walitumika na wengine wanatumika kwa sasa kama kielelezo feki cha kioo cha ubinadamu wa serikali za Marekani na Ulaya kukubalika ulimwenguni mbele ya umma wa watu weusi. Kwa mtizamo wangu huu ni lazima wale wote wenye mawazo kuwa Obama atasaidia weusi na hasa sisi waafrika waandike maumivu na masikitiko. Kwani akishakuwa Rais, kipaumbele kitakuwa ni maslahi ya Marekani kwanza kwa kufuata maneno ya Raisi Rutherford Hayes. Yaani kutumikia makampuni mbalimbali kabla ya kutumikia wapiga kura. Je tutarajie kama Raisi wa Marekani hatumikii watu wake, je atatumikia watu walio mbali naye kama sisi waafrika? Tuache ubaguzi tufikiri sana na tuangalie kwa bongo zetu na si kwa mioyo.
Nikiwa kama mtanzania, mtu mweusi, nimefarijika pia kwa ushindi wa Seneta Barack Obama. Kufarijika kwangu si kwa mashiko ya rangi; yaani mweusi kashinda basi nami nifurahi. Kwangu nimeshangazwa karibu weusi wote wanamshabikia Obama eti kwa kuwa ni mweusi. Nina mashaka kama kweli hisia zetu zinaegemea zaidi rangi basi nadiriki kusema kuwa tusipokuwa makini nasi pia ni wabaguzi wa rangi wakubwa.
Nina wasiwasi: wote wanaouchukulia ushindi wa Obama kama ushindi kwasababu ni mweusi basi wamepotea njia. Ni lazima watu tufikiri kwa kina na si kushabikia tu ilihali inawezekana kabisa Obama hatakuwa na maslahi yoyote kwa waafrika na hata kwa watu weusi sehemu mbalimbali za dunia.
Labda niwarejeshe kwenye historia: Raisi wa zamani wa Marekani, Ruthirford Hayes aliwahi kunena kuwa “Us government is a government of the corporations, by corporations for the corporations”. Alimaanisha kuwa serikali ya Marekani ni serikali ya Makampuni, kwa maslahi ya Makampuni na inaendeshwa na Makampuni. Hapa alikuwa anajaribu kutanzua kiza kinene (illusion) kwenye maana ya demokrasia kama ilivyokuwa imeelezwa awali na mtangulizi wake Lincoln pale alipoweka maneno: “Government of the People for the People by the People” yaani: “serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao” katika katiba ya nchi hiyo.
Ni katika msingi wa kuingalia serikali ya Marekani kama inayoongozwa na mtizamo wa Katiba kuheshimiwa bila ubazazi wa aina yeyote kama tunavyoshuhudia hapa kwetu, basi kama Obama atachaguliwa kuwa raisi wa Marekani tujue kabisa atafanya kazi kwa misingi ya Rais wa zamani Ruthirford Hayes. Hapa ndipo panaponifanya nisiwe na matumaini kama kweli mtu mweusi kuwa Rais wa Marekani basi tutafaidika na lolote tofauti na marasi wengine weupe waliokwishapita na kutawala Marekani. Ni vyema tumfurahie Seneta Obama kutokana na wajihi wake: ni jinsi gani ameweza kuchambua masuala mbalimbali kwa ufasaha na kuonesha jinsi gani anavyoweza kufikiri. Ni kigezo hiki tu naweza kufurahia ushindi wa Obama na wala kamwe si rangi yake. Kinyume na hapo naona ni mtizamo wa kibaguzi ambao hauna nafasi katika dunia ya kileo.
USHINDI HARAKATI ZA MTU MWEUSI
Kuna wengine wanauona ushindi wa Seneta Obama kama vile ni ushindi wa harakati za kutafuta haki za mtu mweusi. Hebu nikumbushie harakati za kumkomboa mtu mweusi nadhani zilianza siku nyingi chini ya watu kama akina Willium Du Bois, Marcus Garvey, George Padmore, Malcolm X, Martin Luther King, Nelson Mandela, Julius Nyerere, Jomo Kenyatta, Kenneth Kaunda, Robert Nesta Marley hadi akina Jesse Jackson na Luis Farhani wa leo hii Marekani.
Nimejaribu kupiga picha na nimeona hadi leo hii mtu mweusi kafikia mafanikio mengi katika nyanja nyingi. Kwa mfano, miongo mitatu iliyopita tunaweza kung’amua mafanikio ya mtu mweusi kama ifuatavyo:
Mosi, mwishoni mwa miaka ya 1970, waafrika weusi wa Marekani waliweza kutawala fani ya muziki kimataifa pale mziki aina ya kufokafoka ulikuwa sana kuanzia New York na kuua kabisa muziki wa Rock uliokuwa ukitawala.
Pili, baada ya mafanikio ya muziki, mwafrika asilia alianza kuonesha mafanikio duniani katika mchezo wa soka. Mwaka 1990, timu ya Taifa ya soka ya Cameroon (Indomitable Lions) ilifikia hatua ya robo fainali ya Kombe la dunia kule Italia chini ya Roger Milla. Baadaye mwaka 2002 kule Korea na Japan timu nyingine ya Senegal nayo ilifika hatua kama hiyo.
Jambo la tatu, katika miaka hiyo hiyo ya 1990, kule Afrika ya Kusini, Nelson Mandela na wafungwa wenzake kama akina Govan Mbeki, Walter Sisulu waliachiwa huru. Baadaye mwaka 1994 waafrika walio wengi wakafanikiwa kuunda serikali ndani ya nchi ambayo walinyimwa haki hiyo kwa miongo kadhaa. Si hapa Afrika tu mtu mweusi kafanikiwa, kwa mfano, mwaka 1997, kijana mweusi wa Marekani: Eldrick ‘Tiger’ Woods akaweka historia kushinda mashindano makubwa ya mchezo wa gofu “US Masters” na ametawala mchezo huo kidunia hadi ninapoandika makala hii. Mchezo wa kikapu ndio usiseme, mtu mweusi katawala hasa.
TIJA YA MAFANIKIO YA MTU MWEUSI
Kwa ujumla mtu mweusi kafanikiwa sana kwa miaka ishirini iliyopita si kwenye fani ya sanaa na michezo tu. Bali hata kwenye mambo ya uongozi wa taasisi nyeti za kimataifa, mwafrika tayari anajivunia kuweza kuongoza katika nyadhifa za juu kabisa. Kwa mfano, Umoja wa Mataifa (UN) , mwaka 1991 – 1994 ulikuwa chini ya Butros Butros Ghali raia wa Misri, baadaye akarithiwa na mweusi hasa Koffi Atta Annan wa Ghana mwaka 1995. Ni kipindi hichohicho, Jumuiya ya Madola ilikuwa chini ya Chief Emeka Anyaoku wa Nigeria kama Katibu Mkuu. Haya yote ilikuwa ni kuionesha dunia kuwa mtu mweusi anaweza na anatambulika. Lakini tujiulize: Je kulikuwa na msaada gani mkubwa kwa waafrika pale yote haya yalipojitokeza? Nakumbuka tulifurahi na kushangilia kutokana na hisia zenye mashiko ya rangi.
Watu wengine wanaweza kujiuliza labda mafanikio mengi ya mtu mweusi niliyoyaelezea hayakutokea Marekani bali hapa Afrika chini ya waafrika. Lakini kwa sasa yanatokea kule Marekani, ambalo ndilo Taifa linalotoa mwongozo wa dunia basi hatuna budi kuwa na matarajio. Na hii ndio hisia ninayoiona miongoni mwetu wengi kama “matumaini feki”. Kwangu siamini hivyo na kamwe sitaamini. Labda nikumbushie tu pale Raisi George Bush alipoingia madarakani na kumteua Collin Luther Powel kama mweusi wa kwanza kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, yaani cheo cha juu kabisa baada ya Raisi na Makamu wake Marekani. Raisi Bush alimteua baadaye mweusi mwingine Condoleza Rice katika nafasi hiyo ya juu kabisa hadi wakati naandaa makala hii.
Pia ni miaka si chini ya mitatu iliyopita, mwafrika mzaliwa wa Uganda John Sentamu alichaguliwa kuwa Askofu wa jimbo la York huko Uingereza. Hii ni nafasi ya pili kwa cheo ndani ya kanisa la Anglikana duniani. Katika haya yote yanayohusu ukombozi wa mwafrika ni mafanikio ambayo wanaharakati wanatumia mara nyingi neno la kiingereza “African Renaissance” yaani kuzaliwa upya kwa mwafrika.
Kwangu hili naliona pia kwa mtizamo huo kwani mwafrika ameweza kuondokana na kadhia za kibaguzi za zamani. Lakini tujiulize swali: Hivi mafanikio yote hayo yamesaidiaje weusi wa dunia hii? Tuache ukichaa, hebu angalia hata kule Afrika ya Kusini sasa mtu mweusi anapinga mweusi mwenzake kuishi nchini mwake. Umasikini wa mtu mweusi uliosababishwa na ufisadi wa wanaharakati wa zamani umetufikisha hapa tulipo. African Reinassance imepoteza mwelekeo huko Afrika Kusini kwa Madiba. Yote ni kwasababu mtu mweusi amekubali awe mtumishi na wakala wa mfumo wa kiutawala wa aina ya: “ corporate by corporation for the corporation”. Akina Raisi Mbeki na wapigania uhuru wenzake wamegeuka umma wa weusi na kuacha kuwatumikia na kuyatumikia makampuni.
Vivyo hivyo, nadhani hata Seneta Barack Obama atafuata mwelekeo huohuo kwa kuitumikia katiba ya Marekani ambayo imejaa lugha ya giza ikimaanisha mambo ambayo kimatendo ni kinyume na maneno. Yaani ikifuata mwelekeo wa Raisi Hayes badala ya ule sahihi wa Lincoln.
Ndio maana nilishangazwa sana mara baada ya Obama kuthibitisha kuwa ni mgombea mtarajiwa, hotuba yake ya kwanza mjini Washington ilikuwa ni mbele ya umati wa watu 7000 uliojumuisha “Kamati ya Mambo ya Waisraiel – Wamarekani ( Jewish American Israel Public Affairs Committee – AIPAC. Tujiulize ikiwa weusi wengi ndio waliompigia kura ilikuwaje aanze na shukrani kwa Wayahudi?
Dhahiri mwelekeo hapa wa dunia lazima tutumie bongo kufikiri na si kufuata hisia tu. Barack Obama hana njia nyingine ila ataungana na wale wengine niliowataja awali kama alama ya “African Reinassance” ambao wamemtangulia katika kuwatumikia wazungu. Kwani katika demokrasia ya leo, ule mtizamo wa Raisi Lincoln ndivyo sivyo. Mambo ya ‘Serikali ya watu, kwa watu na maslahi yao’ ni hadithi ya alinacha. Democrasia leo ni kutumikia makampuni makubwa yenye ushawishi. Haya ndiyo yenye kupenyeza rupia kusaidia kampeni za akina Seneta Obama ili wayatumikie pindi watakaposhinda. Ni kama vile hapa kwetu Tanzania vigogo fulani walivyojiundia vikampuni kwa mgongo wa EPA ili kupata fedha za kampeni. Obama yeye hakutumia mbinu za kibazazi za kujiundia vijikampuni feki ila anafadhiliwa na makampuni ambayo lazima alipe fadhila.
Mwisho, Seneta Obama ataungana na waliomtangulia: Koffi Annan, Colin Powel, Condoleza Rice, Chief Emeka Anyaoku na hata mama yetu mpendwa Asha Rose Migiro ambao walitumika na wengine wanatumika kwa sasa kama kielelezo feki cha kioo cha ubinadamu wa serikali za Marekani na Ulaya kukubalika ulimwenguni mbele ya umma wa watu weusi. Kwa mtizamo wangu huu ni lazima wale wote wenye mawazo kuwa Obama atasaidia weusi na hasa sisi waafrika waandike maumivu na masikitiko. Kwani akishakuwa Rais, kipaumbele kitakuwa ni maslahi ya Marekani kwanza kwa kufuata maneno ya Raisi Rutherford Hayes. Yaani kutumikia makampuni mbalimbali kabla ya kutumikia wapiga kura. Je tutarajie kama Raisi wa Marekani hatumikii watu wake, je atatumikia watu walio mbali naye kama sisi waafrika? Tuache ubaguzi tufikiri sana na tuangalie kwa bongo zetu na si kwa mioyo.
AFRIKA MATATIZO YASIYOKWISHA
Umeyasikia haya ya wapigania uhuru (freedom fighters) wa jamii ya akina Mugabe? kwao demokrasia ikifanya kazi yake haina maana kabisa. Mmojawao huko Uganda anadai kuwa hata kama wakishindwa uchaguzi hawataachia wapinzani watawale.
Ndio maana tusishangae kama Uganda itageuka Zimbabwe siku chache zijazo baada ya Museveni maji kumfika shingoni. Saa nyingine tunadhani matatizo ya Afrika ni Ukoloni, je ni kweli? Lakini Museveni anadai tatizo ni IMF na World Bank.
Ndio maana tusishangae kama Uganda itageuka Zimbabwe siku chache zijazo baada ya Museveni maji kumfika shingoni. Saa nyingine tunadhani matatizo ya Afrika ni Ukoloni, je ni kweli? Lakini Museveni anadai tatizo ni IMF na World Bank.
Thursday, May 22, 2008
BALALI – MWISHO WA SINEMA LA BOT?
Ni saa nane za mchana, siku ya tarehe 21/5/2008 mara napokea meseji ya simu inasema hivi: “Hatimaye picha la BoT lafikia patamu! Balali amefariki! Watatuchezea usanii kuwa huu ndio mwisho wa sinema maana stelingi kafa, ila ukweli wenyewe sinema hii haikuwa na stelingi mmoja tu! Nipe mawazo yako.” Habari hii ilinishtua kidogo kwani nilishatarajia huyu bwana angekufa kwani awali iliripotiwa alitiliwa sumu na mamafia wa kibongo. Akili yangu ilikwenda kwenye hisia za sumu na mara moja nikajenga kanuni za kidhahania (conspiracy theories) kadhaa:
Kwanza kabisa ni muhimu sana kuzungumzia na kuchambua kifo mara kitokeapo. Mara nyingi tunapozungumzia kifo inatusaidia kumchambua aliyekufa weledi wake kimaadili. Yaani ni jinsi gani aliishi wakati wa uhai wake. Kifalsafa, na pia kwa kuzingatia mtizamo wa kikristo, kifo ni utengano kati ya raha na mwili. Kwa maana nyingine, ni kusimama (cessation) kwa uhai katika kiumbe chochote kama hayati Balali. Kwa mtizamo wangu nina maswali kadhaa bila majibu ambayo ni kidhahania zaidi.
Pili, hebu wote wenye akili timamu tujiulize kuwa Gavana aliyeomba kujiuzulu akakataliwa na baadaye uteuzi wake ukatenguliwa (kufukuzwa) hatimaye anakufa baada ya hisia kuwa aliwahi kutiliwa sumu. Huyu ndiye shahidi muhimu sana katika sakata la BoT na nadhani kwa mafisadi sasa wanapumua sana. Ndie mtu pekee ambaye kama Gavana alijua michezo yote michafu katika skandali hili kwani yeye alikuwa stelingi kama nilivyokwisha elezwa na mtuma meseji ya simu awali.
Kwa wapenda picha, filamu,kuna msemo kuwa, kwa kawaida stelingi hauawi, akiuawa sinema imeisha; sitarajii tena kama kutakuwa na lolote la maana kuhusu sakata la BoT. Kifo hiki ni pigo kubwa kwa wale wote tuliodhani vita ya mafisadi ni rahisi. Ni vita ngumu sana kwani mara nyingine mafisadi wanawamaliza wale wote watakaoweza kusaidia michezo yao kugundulika ili kupoteza ushahidi.
Tatu, nategemea ile kamati ya kuchunguza dhahama la BoT imalize miezi sita ije na madai kuwa haikuwahi kumuhoji hayati Balali. Nina wasiwasi inawezekana kupewa muda wa miezi sita ilikuwa ni kuvuta muda ili huyu bwana afe kama ni kweli aliwahi kupewa sumu. Na kama niko sahihi basi sitasita kukubali madai ya mwandishi mmoja kuwa dola yetu sasa ni kimafiamafia hivi; yaani inatumikia mafia. Si hili tu ninalolidhania ila niseme tu kifo hiki kimenishangaza sana; yaani kilitokea ijumaa (16/5/2008). Siku tano baada ya kifo habari zake ndipo zinafika nchini yaani jumatano ya tarehe 21/5/2008. Huu mficho wa nini?
Swali lingine la kidhahania ni kuwa hivi huyu Balali alikuwa mtumishi wa serikali au la? Alishafukuzwa (kutenguliwa uteuzi), sasa inakuwaje kifo chake kiwe ni wajibu wa serikali kukitangaza kwa umma? Waandishi wa habari pia walijazana benki kuu kutaka kujua ni vipi kuhusu kifo cha mtu ambaye hakuwa na uhusiano na taasisi ya benki kuu. Inanishangaza kidogo labda nifafanuliwe maana ya kutenguliwa kama si sawa na kufukuzwa. Mtu ambaye alishajiuzulu kwa barua na kujiweka pembeni ingawa baadaye kuonesha kuwa hatakiwi kabisa alitenguliwa uteuzi wake. Jamani naomba nijulishwe maana ya kutenguliwa uteuzi ni kufukuzwa ama vingine? Kwani kifo hiki kinaonesha wazi si kufukuzwa ndio maana BoT waliwajibika kutoa taarifa maalum kama vile huyu bado mtumishi wao.
Kanuni nyingine ya kidhahania: Najiuliza zaidi eti hayati Balali kafia Marekani na mazishi yake hatujui ni wapi japo inaonekana hata familia yake iko huko. Tetesi ni kuwa alikuwa ni raia wa Marekani zinapata ukweli manake huyu mtu kama hata mazishi yatafanyika huko Marekani basi serikali iliyopita itapata doa. Yaani iliajiri Gavana ambaye si raia? Je huu uoza wote wa BoT si inawezekana umechangiwa na kutokuwa raia? Kwani tangu lini nchi yetu ina sheria ya uraia wa nchi mbili? Kiuzalendo mtu ambaye si raia ataweza kujali uzalendo katika maamuzi yake kwa kusimamia sheria na taratibu za nchi? Mamlaka iliyomteua na nyingine ikaendelea naye ina deni kubwa kwa watanzania.
Binafsi, inanishawishi niamini ile sheria ya uraia wa nchi mbili (dual citizenship) kumbe tayari inatumiwa na wateule wachache hapa Tanzania kama akina Jeetu Patel na mwenzie Vithlani pamoja na hayati Balali. Na kama niko sahihi basi si hayati Balali tu anayefaidika na sheria hii bali tutarajie kuwajua wengine wanaofaidika na sheria kama hii vita dhidi ya mafisadi itaendelezwa. Waziri wa fedha kipindi cha uborongaji wa BoT, mama Zakia Meghji ameripotiwa akimsifia marehemu ete alikuwa mchapakazi hodari. Imenishangaza yaani unakuwa kiongozi alafu mafisadi wanajichotea fedha hazina ya serikali ukiangalia tu alafu mambo yakiharibika unaandika barua kujiuzulu eti huo ni uhodari.
Mwisho, kifo cha mtu yeyote ni ukumbusho wa jinsi gani mtu aliishi kimaadili au la. Na kwa Balali ni wazi kama Gavana, uoza wake ulifichuka pale ukaguzi wa Ernst & Young ulipoanika ufisadi wa EPA. Kimaadili namwondoa katika kundi na huyu anatuachia kumbukumbu ya ufisadi. Kama si fisadi basi wanafamilia wake wamsafishe na kutujuza nini hasa zilikuwa hisia zake kabla ya kuondoka. Ila kama wataendelea kushiriki huu usiri wa serikali kuhusu kifo chake ni wazi yeye pamoja na familia yake hawatalikwepa hili limzimu la ufisadi.
Binafsi nadhani hayati Balali kafa kama mtu pekee Tanzania ambaye hakuwahi kufukuzwa kazi ila uteuzi wake ulitenguliwa. La kushangaza kwanini kujiuzulu kwake kukataliwe? Aliogopwa sana? Ama mamlaka ya uteuzi ni ya kishikaji sana na kufukuza wavunja sheria na taratibu ni vigumu kwayo au ina woga kumtia mkosaji kwenye aibu? Sina jibu hapa ila kifo hiki kwa kiasi fulani kinatupa picha halisi ya udhaifu ama uimara wa mamlaka kuu ya utawala wa nchi hii. Na kwa mwono wangu mdogo nadhani kama shahidi muhimu katika suala la BoT basi skandali hiyo imepoteza mwelekeo na ni furaha kwa mafisadi wengi waliohusika.
Mungu amlaze hayati Balali mahali pema peponi, Amina.
Kwanza kabisa ni muhimu sana kuzungumzia na kuchambua kifo mara kitokeapo. Mara nyingi tunapozungumzia kifo inatusaidia kumchambua aliyekufa weledi wake kimaadili. Yaani ni jinsi gani aliishi wakati wa uhai wake. Kifalsafa, na pia kwa kuzingatia mtizamo wa kikristo, kifo ni utengano kati ya raha na mwili. Kwa maana nyingine, ni kusimama (cessation) kwa uhai katika kiumbe chochote kama hayati Balali. Kwa mtizamo wangu nina maswali kadhaa bila majibu ambayo ni kidhahania zaidi.
Pili, hebu wote wenye akili timamu tujiulize kuwa Gavana aliyeomba kujiuzulu akakataliwa na baadaye uteuzi wake ukatenguliwa (kufukuzwa) hatimaye anakufa baada ya hisia kuwa aliwahi kutiliwa sumu. Huyu ndiye shahidi muhimu sana katika sakata la BoT na nadhani kwa mafisadi sasa wanapumua sana. Ndie mtu pekee ambaye kama Gavana alijua michezo yote michafu katika skandali hili kwani yeye alikuwa stelingi kama nilivyokwisha elezwa na mtuma meseji ya simu awali.
Kwa wapenda picha, filamu,kuna msemo kuwa, kwa kawaida stelingi hauawi, akiuawa sinema imeisha; sitarajii tena kama kutakuwa na lolote la maana kuhusu sakata la BoT. Kifo hiki ni pigo kubwa kwa wale wote tuliodhani vita ya mafisadi ni rahisi. Ni vita ngumu sana kwani mara nyingine mafisadi wanawamaliza wale wote watakaoweza kusaidia michezo yao kugundulika ili kupoteza ushahidi.
Tatu, nategemea ile kamati ya kuchunguza dhahama la BoT imalize miezi sita ije na madai kuwa haikuwahi kumuhoji hayati Balali. Nina wasiwasi inawezekana kupewa muda wa miezi sita ilikuwa ni kuvuta muda ili huyu bwana afe kama ni kweli aliwahi kupewa sumu. Na kama niko sahihi basi sitasita kukubali madai ya mwandishi mmoja kuwa dola yetu sasa ni kimafiamafia hivi; yaani inatumikia mafia. Si hili tu ninalolidhania ila niseme tu kifo hiki kimenishangaza sana; yaani kilitokea ijumaa (16/5/2008). Siku tano baada ya kifo habari zake ndipo zinafika nchini yaani jumatano ya tarehe 21/5/2008. Huu mficho wa nini?
Swali lingine la kidhahania ni kuwa hivi huyu Balali alikuwa mtumishi wa serikali au la? Alishafukuzwa (kutenguliwa uteuzi), sasa inakuwaje kifo chake kiwe ni wajibu wa serikali kukitangaza kwa umma? Waandishi wa habari pia walijazana benki kuu kutaka kujua ni vipi kuhusu kifo cha mtu ambaye hakuwa na uhusiano na taasisi ya benki kuu. Inanishangaza kidogo labda nifafanuliwe maana ya kutenguliwa kama si sawa na kufukuzwa. Mtu ambaye alishajiuzulu kwa barua na kujiweka pembeni ingawa baadaye kuonesha kuwa hatakiwi kabisa alitenguliwa uteuzi wake. Jamani naomba nijulishwe maana ya kutenguliwa uteuzi ni kufukuzwa ama vingine? Kwani kifo hiki kinaonesha wazi si kufukuzwa ndio maana BoT waliwajibika kutoa taarifa maalum kama vile huyu bado mtumishi wao.
Kanuni nyingine ya kidhahania: Najiuliza zaidi eti hayati Balali kafia Marekani na mazishi yake hatujui ni wapi japo inaonekana hata familia yake iko huko. Tetesi ni kuwa alikuwa ni raia wa Marekani zinapata ukweli manake huyu mtu kama hata mazishi yatafanyika huko Marekani basi serikali iliyopita itapata doa. Yaani iliajiri Gavana ambaye si raia? Je huu uoza wote wa BoT si inawezekana umechangiwa na kutokuwa raia? Kwani tangu lini nchi yetu ina sheria ya uraia wa nchi mbili? Kiuzalendo mtu ambaye si raia ataweza kujali uzalendo katika maamuzi yake kwa kusimamia sheria na taratibu za nchi? Mamlaka iliyomteua na nyingine ikaendelea naye ina deni kubwa kwa watanzania.
Binafsi, inanishawishi niamini ile sheria ya uraia wa nchi mbili (dual citizenship) kumbe tayari inatumiwa na wateule wachache hapa Tanzania kama akina Jeetu Patel na mwenzie Vithlani pamoja na hayati Balali. Na kama niko sahihi basi si hayati Balali tu anayefaidika na sheria hii bali tutarajie kuwajua wengine wanaofaidika na sheria kama hii vita dhidi ya mafisadi itaendelezwa. Waziri wa fedha kipindi cha uborongaji wa BoT, mama Zakia Meghji ameripotiwa akimsifia marehemu ete alikuwa mchapakazi hodari. Imenishangaza yaani unakuwa kiongozi alafu mafisadi wanajichotea fedha hazina ya serikali ukiangalia tu alafu mambo yakiharibika unaandika barua kujiuzulu eti huo ni uhodari.
Mwisho, kifo cha mtu yeyote ni ukumbusho wa jinsi gani mtu aliishi kimaadili au la. Na kwa Balali ni wazi kama Gavana, uoza wake ulifichuka pale ukaguzi wa Ernst & Young ulipoanika ufisadi wa EPA. Kimaadili namwondoa katika kundi na huyu anatuachia kumbukumbu ya ufisadi. Kama si fisadi basi wanafamilia wake wamsafishe na kutujuza nini hasa zilikuwa hisia zake kabla ya kuondoka. Ila kama wataendelea kushiriki huu usiri wa serikali kuhusu kifo chake ni wazi yeye pamoja na familia yake hawatalikwepa hili limzimu la ufisadi.
Binafsi nadhani hayati Balali kafa kama mtu pekee Tanzania ambaye hakuwahi kufukuzwa kazi ila uteuzi wake ulitenguliwa. La kushangaza kwanini kujiuzulu kwake kukataliwe? Aliogopwa sana? Ama mamlaka ya uteuzi ni ya kishikaji sana na kufukuza wavunja sheria na taratibu ni vigumu kwayo au ina woga kumtia mkosaji kwenye aibu? Sina jibu hapa ila kifo hiki kwa kiasi fulani kinatupa picha halisi ya udhaifu ama uimara wa mamlaka kuu ya utawala wa nchi hii. Na kwa mwono wangu mdogo nadhani kama shahidi muhimu katika suala la BoT basi skandali hiyo imepoteza mwelekeo na ni furaha kwa mafisadi wengi waliohusika.
Mungu amlaze hayati Balali mahali pema peponi, Amina.
Thursday, May 08, 2008
UTAPELI WA WALOKOLE
Watu wanadai eti kuna walokole wenye uwezo wa kutibu Ukimwi kwa sala!Mama wee!, huyu katumiwa na walokole kudanganya aliponywa kwa miaka kadhaa.
Malimwengu bwana, yaani kumbe tunadanganywa sana, lazima tuwe macho sasa na haya madini yaliyoongezeka sana.
Malimwengu bwana, yaani kumbe tunadanganywa sana, lazima tuwe macho sasa na haya madini yaliyoongezeka sana.
Friday, May 02, 2008
Thursday, May 01, 2008
MEI MOSI ILIVYOFANA MOSHI
Sunday, April 27, 2008
Subscribe to:
Posts (Atom)



