Hii ni globu iliyovumbuliwa nchini Uganda inajaribu kukazia matumizi ya lugha ya kiswahili na kuhabarishana kuhusu maswala mbalimbali ya kijamii hasa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kat na kwingineko. Siasa na mambo ya michezo na kijamii kwa ujumla ndio itakayokuwa mada kuu hapa.Nitakaribisha maoni yenu.
My Blog List
Tuesday, September 25, 2007
SHIRIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI KUREJESHA ENZI ZA FALME YA BUNYORO KITARA
Hivi majuzi jumuiya ya Afrika Mashariki ilipigwa butwaa baada ya kuripotiwa kuna juhudi za kichinichini kuanzisha shirikisho kati ya Uganda na Kenya na kuiacha Tanzania kwani inaonekana kuzuia mawazo ya rais Yoweri Museveni ya kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki ifikapo mwaka 2013. Ghafla kama wiki mbili zilizopita kumeripotiwa eti Museveni anaendeleza ushawishi na Kenya ili Uganda iungane na iunde Shirikisho na kuiacha Tanzania ambayo inaonekana bado inasita kwa mujibu wa ripoti ya kamati ya maoni ya wananchi wake.
Asilimia 80% ya watanzania hawakuunga mkono wazo la Shirikisho kuharakishwa ingawa asilimia 97% waliunga mkono wazo la Shirikisho hatua kwa hatua. Habari hizi za juhudi za chinichini za Museveni hazikunishangaza hata kidogo bali zimenisukuma kuandika makala ya leo hii.Leo nataka tushirikishane ndugu wasomaji wetu ni kwa vipi haiba ya rais Museveni inaashiria ni mtu wa kuburuza mambo yake yafanyike hata pale inapohitaji watu kushirikiana na kuheshimu maamuzi ya pamoja. Ningependa tutafakari kama kweli Museveni ana malengo yenye tija kwa watu wa Afrika Mashariki au ni janja ya maslahi binafsi? Je watanzania tunamfahamu mtu huyu hasa au ni jujuu tu?Pia ni lazima tuone kama kweli mtindo wake wa uongozi wa Uganda kwa miaka zaidi ya ishirini unampa sifa kutuongoza katika utengamano? Nitaanza kwa maoni juu ya kikao cha mwisho cha viongozi wetu pale Arusha mwezi uliopita.
Kwanza kabisa, viongozi wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki walipokutana Arusha mwezi uliopita walifanya maamuzi kamambe ili kuokoa juhudi za ufufuaji wa jumuiya ambapo ilishaanza kupingwa na wananchi katika kura za maoni hasa Tanzania. Kubwa lilikuwa juu ya kuharakisha uundaji wa shirikisho ifikapo mwaka 2013.
Nilipokea maamuzi ya viongozi wetu kama tukio la aina yake kwa viongozi wetu kwa mara ya kwanza baada ya maberamu dhidi ya kuharakisha shirikisho kuzidi sana wameamua waanze kusikiliza sauti ya watu. Nakumbuka niliwahi kuwafananisha na kondoo ambaye anapelekwa machinjioni asiyejua kuna kifo katika makala yangu ya tarehe 26/08/2007 dhidi ya uharakishaji huu. Viongozi wetu walikubaliana kubaki na lengo la kufikiwa kwa Shirikisho ila kwa sasa ni lazima taasisi nyeti ziundwe kwanza. Kwa maana nyingine tuanze kuungana kiuchumi--kibiashara na shughuli kadhaa za kijamii. Ila serikali moja si wakati muafaka. Mimi ni muumini wa hili waliloamua kule Arusha mwezi uliopita. Yaani muungano wa Ushuru wa Forodha, Soko la Pamoja na hata Sarafu Moja, uhuru wa watu kuvuka mipaka kama wafanyabiashara, wafanyakazi na hata bidhaa bila vipingamizi visivyo vya lazima pamoja na mambo mengi chungu mbovu ambayo tayari yanafanyika hadi sasa.
Binafsi, ninaamini kabisa Shirikisho halina tija kwa jamii ya Afrika Mashariki ila tu mashirikiano ya kiuchumi ndiyo yenye tija. Tukiharakisha shirikisho bila kuwa na taasisi (institutions) zenye nguvu kukabili nyanja mbalimbali za mahusiano ni bure na ndio hapa panaponifanya niamini kuna mizengwe ya wazito fulani wenye mkakati binafsi usiozingatia maslahi ya wananchi kwa ujumla wao. Malengo ya utawala bora katika nchi zetu bado hayajafikiwa hasa nchini Uganda sasa je kweli mtu ambaye hajafanikiwa kuleta utawala bora ana nini kipya katika Shirikisho? Je ni kwanini nina wasiwasi sana na juhudi za raisi Museveni?
KUTOKA MCHAKATO MMOJA HADI MIWILI (FAST TRACKING TO DOUBLE TRACKING)
Baada ya kikao kile cha Arusha, tarehe 20, August 2007, ni wazi mwelekeo wa muundo wa Shirikisho umekumbwa na wimbi jipya. Raisi Museveni inaripotiwa, na gazeti la 'Sunday Monitor' la tarehe 23, September 2007, alimtuma mjumbe maalum kwa mwenzake wa Kenya akimhimiza rais Kibaki kuunda Shirikisho jingine lisilojumuisha Tanzania lakini litakalotoa mwanya kwa Tanzania kujiunga itakapokuwa tayari. Ni mchakato mpya ambao wachunguzi wa mambo ya siasa za jumuiya ya Afrika Mashariki, wanadai ni mpango utakaoendeshwa kwa staili tofauti ya uharakishaji kutoka ile ya "Fasttracking hadi Double Tracking". Serikali ya Uganda haijakanusha haya kwa hivyo ni wazi juhudi hizi ni za kweli. Hapa Museveni anaonesha ni jinsi gani asivyopenda kusikiliza maoni ya watu wengi; au kwa maana nyingine anamaanisha lile zoezi zima la ukusanyaji maoni halikustahili labda. Watu wameamua sivyo na yeye anaamua kuja na mkakati mpya.
Kwa maana nyingine, Kenya na Uganda zinatangulia na Shirikisho wakati Tanzania nayo ikija kwa mwendo wa pole.(Double Tracking). Tayari jina la Shirikisho hilo limebuniwa, nalo ni "Muungano wa Wenye Nia" (Coalition of the Willing). Hata makao makuu mapya inasemekana yanatajwa kama yatakuwa ya muda kule Entebbe Uganda wakati wakisubiri ya kudumu kule katika mji wa vilima wa Tororo Uganda. Hii yote inaaminika itashinikiza Tanzania kufikiri na kubadili msimamo. Wachunguzi wa jinsi juhudi za Museveni zinavyohakikishwa zinafanikiwa, ni kwamba baada ya ugunduzi wa mafuta katika ukanda wa eneo la ziwa Albert (Albertine) basi inapanga kutumia nguvu ya fedha ya mafuta hayo kuhakikisha siku za usoni ndio inakuwa na ushawishi mkuu katika eneo zima la maziwa makuu. Mafuta yatatumika kama rungu ama silaha ya kidiplomasia kuhakikisha mradi wowote wa mashirikiano ukibuniwa na Uganda unafanikiwa kwa vyovyote vile.
Binafsi Museveni kaamua kuihujumu Tanzania kiaina kwani kama kweli ana nia njema ni kwanini tayari wana mawazo ya makao makuu mapya? Na kama ni kweli wamefikia hatua hii ina maana tayari Museveni alikuwa na mipango tayari kwani si mambo rahisi tu kuamua ni wapi pa kujenga makao makuu ya muda na pia ya kudumu bila kuhusisha maamuzi ya taasisi kama Bunge.
MASLAHI YA NCHI NDANI YA SHIRIKISHO
Inaripotiwa pia kuwa katika kuishawishi Kenya iunde Shirikisho jipya-Wenye Nia-Uganda imeihakikishia Kenya itafaidika 'kiuchumi' kwa kupanua soko la bidhaa zake hadi Rwanda, Burundi, Uganda, Sudan ya Kusini na hata Kongo-DRC. Kwa upande wa Uganda, yenyewe imebainisha maslahi yake ni ya 'kisiasa' ikimaanisha hapa ni wazi Museveni anawaza zaidi utawala. Ni katika mtizamo huu najiuliza je kama Tanzania tunajiunga na mchakato huu wa Shirikisho, je maslahi yetu ni nini?
Ni wazi iwe isiwe, Kenya ina uchumi mkubwa na imara kuliko nchi zote na ndio itakayofaidika zaidi. Lakini sisi kama Tanzania ili tuamue kujiunga na wenye nia, ni lazima tuwe makini na tujue maslahi yetu ni yapi la sivyo hakuna haja ya sisi kuwa kwenye shirikisho.
WASIWASI--CHUKI ZA KIKABILA UGANDA
Kuna tatizo kubwa sana la chuki kali sana za kikabila nchini Uganda na ni vizuri ieleweke kuwa hii ni sababu ya kihistoria katika nchi hiyo kwa kiasi fulani. Ikumbukwe kuwa Uganda ilipata uhuru wake Waziri mkuu wake wa kwanza na baadaye Raisi alikuwa ni Dr. Milton Obote mzaliwa wa Kaskazini mwa Uganda. Huyu aliwajaza jeshini wazaliwa wa kaskazini kwani ndio waliokuwa wakitumika shughuli za jeshi tangu wakati wa ukoloni. Baadaye alipinduliwa na Iddi Amin ambaye alitoka kaskazini pia na akaendeleza utawala wa watu wa kaskazini katika kila nyanja.
Hadi anakuja kupinduliwa na majeshi ya Tanzania yakisaidiana na wakombozi wa Uganda chini ya watu kama Yoweri Museveni na wengine Uganda ilikwishatawaliwa na watu wa kaskazini kwa miongo zaidi ya mitatu tangu uhuru. Obote alirudi madarakani kwa uchaguzi uliojaa mizengwe ya kitanzania inavyodaiwa ambayo ilimfanya Yoweri Museveni kuamua kurudi msituni kwani alidai uchaguzi kuendeshwa kimizengwe. Ikumbukwe aligombea urais wakati huo-1980 na kushindwa vibaya. Ila baadaye Obote alipinduliwa na Tito Okello; hali yote hii ikiendeleza utawala wa watu wa kaskazini. Tito Okello akapinduliwa mwaka 1986 na Yoweri Kaguta Museveni akachukua hatamu kuifufua nchi ambayo ilikwisha poromoka kiuchumi hadi kufikia hatua mbaya (failed state).
Kwa umahiri mkubwa kabisa Museveni akaweza kuifufua nchi na kuisimamisha hadi kuwa sawa na majirani zake kwa sasa. Ni jambo ambalo atajivunia hadi kaburini; ila uongozi wake ulikuwa wa mabavu, yaani mfumo wa "vuguvugu-movement"ambao haukuruhusu vyama vya siasa. Katika kipindi chake cha uongozi ni wazi serikali ya NRM imekuwa ikiongozwa chini ya viongozi kutoka makabila ya magharibi (westerners) katika nyadhifa zote za juu. Hali hii imejenga chuki kati ya watu wa kaskazini na kusini kwani inaaminika baada ya Museveni kuingia madarakani basi ulikuwa ni mwisho wa wakati wa watu wa kaskazini kutesa.
Hisia hizi pia ziko kwa watu wanaounga mkono hata ule uasi wa LRAkule kaskazini. Hali inamfanya Museveni kuwa mwoga na maisha baada ya urais na hivyo kuharakisha uundwaji wa Shirikisho ili aendelee kuwa kwenye hatamu za uongozi wa juu na asiyeweza kuguswa na vyombo vya sheria.
Kama sijakosea ni wazi wazo la kuharakishwa kwa shirikisho lilianzishwa na Rais Museveni na mara moja aliweza kuwashawishi wenzake na likapewa kipaumbele na ndio ikaundwa kamati ya kukusanya maoni ambayo kwangu ulikuwa ni ubadhirifu mkubwa iwapo ni kweli Museveni anaishawishi Kenya kuendelea na juhudi za kuharakisha baada ya Tanzania kutokuunga mkono wazo lake. Inaonekana alitegemea serikali ya Tanzania ingefanya mizengwe na kutosikiliza sauti ya wananchi.
Moja ya udhaifu wa Museveni ni mtu anayependa ubabe na anapokuwa na nia ni lazima itekelezwe. Kwa mfano, amekwamisha suluhu ya vita ya LRA kwani anawafananisha na majangili (thugs) akidai ni kikundi kidogo cha wahuni lakini la kushangaza ni miaka zaidi ya ishirini ameshindwa kuwamaliza. Wakosoaji wake wanadai hawajali sana watu wa kaskazini dhidi ya mateso ya vita na hapa pamemjengea chuki kubwa dhidi ya watu wa kaskazini. Binafsi nina marafiki kadhaa wanaotoka kaskazini mwa Uganda ukiwasikiliza hawafichi chuki zao dhidi ya makabila ya magharibi na kusini kama ndio chanzo cha madhila ya kaskazini. Ikumbukwe tangu Museveni aingie madarakani, Uganda iko chini ya watu wa magharibi wanaojulikana kama (westerners): wanyankole, watooro, wachiga, na wanyoro. Niliwahi kuzungumza na jamaa mmoja wa kabila la la magharibi 'mtooro', akaniambia "acha jamaa wateseke, walitutesa sana nyakati za Amin na Obote". Ni wazi kuna chuki za kisirisiri dhidi ya watu wa sehemu fulani ya nchi (xenophobia) ambapo Museveni hajafanya juhudi za kutosha kuziondosha ingawa ana uwezo huo. Ni nadra sana kwa watu wa kaskazini kuoana na watu wa magharibi.
Kwa mantiki hii, Rais Museveni lazima abebe lawama kama mtu asiye na haiba ya kuunganisha jamii kuishi kwa utengamano; na ndiye mtu anayedai anaweza kuiongoza Shirikisho la nchi tano kuishi kwa utangamano. Ni kiroja na siamini kama kweli anatufaa.
KUCHIPUA KWA MBEGU YA CHUKI
Baada ya mapinduzi ya mwaka 1986, mbegu ya chuki za kikabila ndipo ilipoanza kuchipua hasa. Museveni akampindua Tito Okello; askari wa Okello walikimbilia Kaskazini wakipita Jinja, Tororo hadi Lango na Acholi--kaskazini na kuanzisha uasi ambao hata hivyo haukuwa na nguvu. Baadaye Museveni aliwashawishi waasi na kukaa mezani na baadhi ya makamanda wao wakakubali yaishe na wakazawadiwa nyadhifa serikalini. Mmojawapo alikuwa Jenerali Moses Ali ambaye alikuwa mmoja wa vigogo wa vyeo vya juu kabisa hadi uchaguzi wa mwaka jana. Askari ambao hawakutaka suluhu walibaki msituni na ndio ukawa mwanzo wa uasi chini ya mama Alice Lakwena na baadaye Joseph Kony hadi leo.
Wote hawa wamekuwa na madai mengi mojawapo kuchukizwa na 'unyanyapaa' dhidi ya makabila ya kaskazini. Kuthibitisha haya, taasisi zote nyeti za serikali na idara zake ziko chini ya watu kutoka magharibi-kusini ukiacha spika wa Bunge. La kushangaza kama ni wasomi waliobobea wengi wanatoka Kaskazini na Mashariki--Lango, Pakwach, Acholi, Pader, Teso, Tororo n.k. Hawa wapo nchi za nje kama Marekani, Canada, Uingereza, Australia huku kukiwa na tetesi miongoni mwao ni wafadhili wakubwa wa LRA.
Kwa maelezo hapo juu, hii ndio jamii iliyo chini ya mtu anayetaka kwa nguvu za ushawishi mkubwa tuunde Shirikisho; tujiulize je kweli ana jipya kama kashindwa kuunganisha nchi yake? Je nchi tano ataziweza? Ni wazi ni kiongozi anayeongoza sehemu moja ya nchi kama vile eneo lililotekwa kivita (conquered territory). Yaani watu wa kaskazini kwa miongo kadhaa wamekuwa wakiishi katika makambi (IDPs) chini ya hali ya hatari kwa muda wote. Kisa ni serikali kukosa busara za kumaliza vita; yaani kushindwa kukang'amua njia bora ya kutatua tatizo la LRA na badala yake kusisitiza njia za kijeshi ambazo zimeshindwa kabisa. Ni hivi majuzi baada ya uchaguzi ambao ulionesha mgawanyiko mkubwa wa wananchi ndipo angalau Museveni akakubali kukaa mezani japo inaonekana huenda akarudi msituni.
JE NI LAZIMA AWE RAIS WA KWANZA WA SHIRIKISHO?
Ukiacha sababu ya woga wa maadui asiyewafahamu (paranoia), Rais Museveni ana tabia ya usaliti kwa wale anaoshirikiana nao hasa watu makini wenye misimamo. Hii inajionesha wazi baada ya Museveni kuwaahidi wanachi mwaka 2001 kuwa alikuwa akigombea kwa mara mwisho alikuja kugeuka na kuwahonga wabunge shilingi millioni tano kila mmoja ili wabadili katiba kuondoa ukomo wa rais kugombea vipindi viwili vya miaka mitano.
Hii ilimruhusu kugombea kipindi cha tatu maarufu kama "third term" kitu ambacho kilimtenganisha na watu waliokuwa nae karibu sana tangu harakati za msituni. Wale wote katika baraza la mawaziri ambao hawakumuunga mkono aliwafukuza kazi kwa kisingizio cha kutokuheshimu utendaji kazi wa pamoja(collective responsibility). Kwa mfano, alikuwepo mtu wake wa karibu tangu utotoni, Eriya Kategaya, ambaye alikuwa waziri mkuu na ambaye sasa hivi amemrudisha tena kama waziri wa Afrika Mashariki na naibu waziri mkuu. Meja Amanya Mushega, katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki aliyepita pia alifukuzwa uwaziri na amekuwa akisimamia misimamo thabiti ya kidemokrasia. Hali hii ni kitu kilichompotezea marafiki wa karibu kwa kipindi kuelekea uchaguzi mkuu uliopita.
Pili, uchaguzi mkuu uliopita aligombea kwa mara ya tatu baada ya kubadili katiba na upinzani ulikuwa mkali ajabu ambao ulihitaji mahakama ya kijeshi "Court Martial" iliyokuwa chini ya Jenerali Elly Tumwine, mzaliwa pia wa kabila moja na rais kutumika kumuundia mashtaka ya bandia mpinzani wake mkuu. Hii ilimnyima mpinzani wake kupata muda wa kutosha kupiga kampeni na badala yake kukimbizana na kesi muda wote. Hali hii iliongeza ukinzani au mbinyo wa mataifa wafadhili kwa Museveni. Ni wakati huu alipoona ndoto ya kuendelea kung'ang'ania madaraka siku za usoni itakuwa ngumu sana na akaanzisha wazo la kuharakisha shirikisho "fasttracking". Inawezekana kabisa anaamini atakapomaliza uraisi wake 2011, atakuwa na mwaka mmoja wa kampeni na mwaka unaofuata anachukua hatamu za uongozi.
Tatu, kuna kanuni ya hila "conspiracy theory" inayodai kuwa Museveni kama mtoto wa chifu wa kabila la Wanyankole-Hima, ana tabia za kutawala kwa kujitanua kupitia uvamizi wa mataifa jirani "expansionism". Hii ni tabia ambayo ameshaionesha tangu asaidie kuikomboa Rwanda, na baadae akaivamia Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo. Utaona baada ya kusaidia juhudi za ukombozi alitaka pia kuzitawala nchi hizo kwa kuwageuza viongozi wa nchi hizo kama vikaragosi wake (puppets) kitu ambacho kilimgombanisha na watu kama raisi Kagame na hata sasa hana uhusiano mzuri na rais Kabila. Kwani anajulikana anaunga mkono mpinzani mkuu wa Kabila, Jean Pierre Bemba. Ni hisia hizi zinadhaniwa na wengi labda ndizo zinazomsukuma ili atakapokuwa chifu wa Shirikisho si ajabu akatunisha misuli yake na kuteka nguvu za serikali za nchi shirika. Kitu ambacho kinaweza kuja leta matatizo sana.
Kanuni hii ya hila za Museveni inachangiwa na muundo halisi wa serikali yake kama nilivyokwisha eleza awali imejaa watu wa kabila lake hasa. Mwandishi mmoja, aliwahi kusema ni serikali inajionesha katika mantiki ya muungano wa kikabila yaani akaiita "Kinyoro Kitara Kingdom". Ikumbukwe kihistoria Bunyoro Kitara ilikuwa falme kubwa ilijomuisha makabila kadhaa chini ya Mfalme mmoja. Makabila haya ni kama Wanyankole (kabila la Museveni), Watooro, Wabusoga, Wanyoro, Karagwe na hata Wabaganda. Katika mtizamo huu si ajabu historia inaweza kujirudia kupitia kinara mkuu--Museveni. Ni kama serikali ya kifalme hivi kwani hata vigogo wa juu kabisa ni ndugu wa damu. Kwa mfano, binti wa Museveni kaolewa na kijana wa Waziri wa mambo ya nje--Sam Kutesa. Kwa mujibu wa tamaduni zao, watoto wa vigogo wanaoana wao kwa wao kutoka kabila moja: wanyankole. Ni kama serikali ya kifalme hivi (monarchy)
Jambo lingine ni hatua ya mama Janet Museveni, mke wa Museveni, kugombea ubunge uchaguzi mkuu uliopita. Inasemekana Museveni alipinga sana hatua za mkewe kugombea ubunge japo familia nzima iliunga mkono. Tetesi ni kuwa Mama anajiandaa kurithi nafasi ya mzee alafu na yeye ajikite kwenye shirikisho. Kwa maana nyingine familia itakamata hatamu za nchi na shirikisho kwa ujumla. Kama si hivi basi inahisiwa mtoto wake pekee wa kiume, Meja Kainerugaba ambaye sasa yupo masomoni majuu anaandaliwa kumrithi baba yake. Kwani amekuwa akipelekwa kuhudhuria masomo ya kijeshi katika vyuo maarufu vya kijeshi Uingereza na Marekani. Hadi anakwenda masomoni mwaka jana ndie aliyekuwa mkuu wa kikosi cha ulinzi wa rais (Presidential Guard Brigade).
SHIRIKISHO KWA NJIA YEYOTE ILE
Awali nimesema kuwa siku za karibuni Raisi Museveni karipotiwa kuanzisha juhudi mpya kwa siri za kuishawishi Kenya iungane na Uganda na kuikacha Tanzania ambayo bado haiko tayari. Mimi naiona hatua hii kama kiashirio cha dhati kuwa Museveni anatafuta mahali pa kutokea "Exit Strategy" na iliyobakia ni Shirikisho kuharakishwa.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la Uganda, Museveni aliwahi kunukuliwa hapo November 29, 2005 akiwahutubia waandishi wa habari: "Tutakapokuwa kwenye awamu yangu ya tatu (third term) sala yangu kuu ni kuanzishwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki. Ifikapo mwaka 2010, tuwe na uraisi wa kupokezana na 2013 tuwe na raisi mmoja wa kuchaguliwa. Kama msomaji una akili timamu lazima ujiulize suala la muda hapa (timing) . Aliongeza zaidi: "Hilo likitokea utaona mtu aking'ang'ania kustaafu hata kama mnaleta tingatinga kunilazimisha nibakie madarakani, nitaenda kuchunga ng'ombe". Inaonekana hapa si kwamba Museveni alimaanisha kustaafu siasa za Uganda ataenda kijijini, ila atapenda ahamishe ikulu yake kutoka pale "Nakarero" hadi Arusha. Hii kwenda kuchunga ng'ombe kijijini kwake kule 'Rwakitura' wilayani Mbarara ni janja tu.
Mwisho, jambo la msingi ni wazi kuwa rais Museveni ni kiongozi shupavu na mwenye kuthubutu kufanya mambo makubwa bila kujali mbinyo wa wapinzani. Hii ni sifa ambayo viongozi wengi hawana na ni silaha yake kubwa. Ila tu tatizo mara nyingi maamuzi yake si kwa ajili tu ya nchi bali maslahi binafsi.
Wasiwasi wangu unaanzia hapa: Mwanzoni alidai Shirikisho kwa misingi ya 'Wigo mpana wa Soko', kutokana na idadi ya watu wa nchi tatu na baadaye tano. Sasa anapoiacha Tanzania, tena yenye watu wengi kuliko nchi mwanachama yeyote.
Tujiulize: je wigo wa soko unaongezeka au unapungua? Hapa ananiacha hoi; kama si ukubwa unatafutwa ni nini hasa? Nitaendelea kuwajuza siku zijazo.
Saturday, September 22, 2007
MUSEVENI NA HILA DHIDI YA TANZANIA?
Pia hebu tujionee ni vipi Uganda na Kenya zina mbinu za kichinichini dhidi ya Tanzania juu ya Shirikisho?
Saturday, September 15, 2007
KENYA UGANDA KUUNDA SHIRIKISHO-EAC
Saturday, September 01, 2007
MFUMO WA KISIASA TANZANIA NI MBOVU SANA
Tusipobadili katiba hatufiki popote hata kama CCM itashindwa.
Leo nikiandikia ndani ya "Tanzania Daima" napenda nigusie juu ya mfumo wetu wa kisiasa niuonavyo nadhani una tatizo na tusipoweka tafakuri za kina sio ajabu tukawa tunalaumu wanasiasa wetu--hasa wabunge wa chama tawala-- na baadaye kitakapokuja shinda chama kingine mambo yakawa kama sasa. Naliona bunge letu kama si chombo kinachotekeleza yale yaliyokusudiwa; yaani mhimili wa kutunga na kuipa changamoto serikali bila kuingiliwa na serikali. Labda nianze kwa kuonesha wasiwasi wangu juu ya uhuru wa kusema usivyozingatiwa hasa na taasisi hii.
Kanuni hii inanisukuma kueleza hisia zangu juu ya tatizo kubwa la mfumo wetu wa kisiasa ambao nadhani una madhara mengi sana juu ya udhaifu wa Bunge letu. Nina fikra kuwa kwa ujumla watawala wetu bado hawajaweza kutoka katika fikra za umungu mtu; yaani kuwa tayari kusikiliza mawazo ya upande mwingine kwa moyo wa dhati. Bali yanayotokea mengi inaonekana ni 'bezo' kila serikali ama taasisi zake zinapokosolewa. Hawajui bado kama kwa kila watakachosema lazima kitapata wazo mbadala. Masikini, wamesahau hiyo kanuni ya fizikia!
Ni katika muono wangu huu wa kifizika ninaamini ingawa tumekuwa chini ya mfumo wa kisiasa wa vyama vingi ila bado hatujaweza kufaidi matunda ya mfumo huo kwa kiasi cha kukidhi haja ya kisiasa kuiletea nchi yetu utawala bora. Je ni kwanini nimeona hivyo? Nitaanza moja kwa moja kuangalia mfumo wetu wa kisiasa na kuoanisha na mambo kadhaa ambayo yanatokea nchini kwetu kuthibitisha kuwa bado tuna mambo ya msingi kuyafanyia kazi ili tufikie angalau demokrasia yenye tija kwa maendeleo ya nchi na wananchi wetu.
Mfumo wa siasa unaweza kuwa ule wa Chama kimoja, vyama vingi, au hata usio na vyama vya siasa bali wa kikundi cha askari (junta) kama uliokuwa nchini Uganda kipindi cha nyuma kidogo yaani ule wa vuguvugu-movement. Katika mifumo yote hii kama uhuru wa kusema na kuvumiliana hauzingatiwi basi jamii haiwezi kupiga hatua katika maendeleo. Ni katika mtizamo huu, kikao cha bunge la bajeti kilichomalizika hivi karibuni kwa kiasi kikubwa kimedhihirisha kuwa taasisi nyeti kama Bunge haizingatii sana uhuru wa kusema na kuvumiliana.
Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania la awamu ya nne lilianza na kauli mbiu za Spika Samweli Sitta eti litakuwa la 'viwango na kasi' na kutupa faraja watanzania wengi kama mimi. Ninasikitika mijadala ya hivi karibuni bungeni imeonesha badala ya kwenda mbele tumeamua kurudi nyuma (reverse gear); kuna dalili kubwa za uoza wa kujadili; na inaonesha bunge sasa ni taasisi isiyofaa (irrelevant) hasa mtu unapozingatia mambo ya uzalendo au maslahi ya Tanzania. Spika wa Bunge ndio chanzo cha uoza kwa kiasi fulani kwani jinsi anavyoadhibu wabunge inatia shaka. Anafikia kusema mbunge fulani anahitaji ushauri nasaha kwa hiyo asamehewe pale alipotenda kosa; mtu unajiuliza ni kanuni gani inasema haya unashangaa manake sidhani kama bunge letu lina watoa ushauri nasaha.
Ila ukiangalia hili la majuzi la mheshimiwa Zitto Kabwe, maamuzi ya bunge letu yanakanganya. Napata hisia spika kazidiwa na hisia za chama chake-CCM anapokuwa anataka kutoa maamuzi na anashindwa kutumia busara kama alivyoweza kuzitumia na kusema mbunge wa chama chake anahitaji ushauri nasaha. Natambua kwa kanuni za Bunge, ambazo hata Spika amekiri mara nyingi zimepitwa na wakati, kuna uhalali wa mheshimiwa Zitto Kabwe kuadhibiwa. Ila nashangaa kwanini busara haikutumika hapa? Ina maana hoja alizotoa mheshimiwa Zitto Kabwe hazina chembe ya kuona umuhimu wa kuunda kamati kuchunguza mambo yenye maslahi kwa nchi? Hivi kama ni kweli mkataba ulisainiwa nje ya nchi tena ndani ya hoteli ya Churchil na wala si angalau ubalozi kwetu London, kwani tusichunguze kama sheria zilifuatwa?
Hivi wabunge wa maeneo yenye migodi kama huko Buzwagi, Bulyanulu, North Mara, Mwadui na Nzega hawashangai ni kwanini watu wao bado wako nyuma kimaendeleo katika nyanja nyingi wakati wana utajiri mkubwa? Historia itawahukumu wabunge wa mikoa yenye rasilimali zinazoibiwa na wao kubariki bungeni kwa kile kinajionesha kama mapenzi ya chama zaidi ya wananchi waliowachagua. Hapa upande mmoja ninawalaumu wabunge wa sehemu hizo lakini kwa upande mwingine sitaki walaumiwe kabisa na ndio ningependa nizungumzie kuwa tuna tatizo. Tangu mwaka 1992, tumeanzisha mfumo wa vyama vingi tukiiga uendeshaji wake kutoka nchi za magharibi kama Marekani. Mfumo wetu naamini ni tatizo na unawalazimisha waheshimiwa wabunge wa chama tawala kuzima mfumo wa kufikiri waliojaliwa na maulana wanapokuwa bungeni.
Ninadhani bunge, kama mhimili muhimu katika kuhakikisha dola inakuwa na tija, lina tatizo na inabidi lirekebishwe sana maana kwa hali ilivyo sasa kuna hatari hiki ni chombo au kinaelekea kuwa ni chombo kisichokuwa cha maslahi yeyote kwa nchi, bali kwa maslahi ya vigogo wachache na marafiki zao wenye mitaji kutoka nje ya nchi. Kuna athari kadhaa lazima tuzing'amue kama watanzania ili tuweze kuja na mkakati hasa wakati wa kupiga kura. Tuna mfumo wa siasa wenye chama kimoja chenye maguvu mengi kutokana na kuwa na wabunge wengi. Madhara yake tunakuwa na demokrasia ya vyama vingi wenye bunge dhaifu na butu; ni Bunge lisilofanya kazi kama mhimili unaojitegemea bali linalowakilisha watawala.
Kwa maana nyingine demokrasia ya Tanzania ni ya aina yake na kipekee duniani kwa misingi kwamba tuna serikali ya awamu ya nne isiyozingatia mihimili mitatu: 'watawala, bunge na mahakama'. Tanzania ya leo, serikali inaendeshwa kwa mihimili miwili: watawala na mahakama. Bunge kupitia chama tawala limejikita katika kufanya kazi za watawala kwa kuisemea na kubariki (rubber stump) mijadala ya serikali badala ya kuihoji. Ni mfumo ambao ama unaambatana na shuruti kwa wabunge wa chama tawala au ni utashi wao kutenda watendavyo, mimi nashindwa kuelewa ila nionavyo tuna tatizo la mfumo wa kisiasa.
Nionavyo labda tunahitaji mfumo wa vyama vingi wenye chama tawala dhaifu, kwa maana kisicho na viti vingi sana ndani ya Bunge. Yaani, chama tawala ambacho kinaweza kushindwa kwa kura na wabunge wengine wa upinzani linapokuja suala lenye kuhitaji watu kufikiri kwelikweli kama la kupigia kura maamuzi kadhaa kama haya ya juzi ya kumuadabisha Zito Kabwe.
Ni kutokana na kuwa na bunge la chama kimoja chenye wabunge lukuki, bunge letu sasa limebakia kama "Sanaa za maonesho-majukwaani za kitaifa" (Nationa Theatre). Nathubutu kusema kama mtu amefuatilia kikao cha bunge hivi karibuni kwenye televisheni ni wazi tulikuwa mara kwa mara tunashuhudia sanaa za maonesho. Kwanini ninasema hivi?
Mosi, kwa mfumo wa demokrasia tulionao ni wazi wabunge wanajumuika katika makundi yao tofauti yaani kambi (CAUCUS). Kabla ya kujadili jambo bungeni, wabunge katika kambi zao wanakuwa wameshajadili ni vipi watajadili au hata kupigia kura hoja ili zipite au la. Kwa mantiki hii tunachoshuhudia pale Bungeni ni marudio ya kile kilichokwishajadiliwa ndani ya vikao vya kambi (caucus) za wabunge. Kwa maana nyingine kwa mfumo huu Bunge linakuwa chombo cha kisanii kwani ni sawa na kupoteza fedha za umma wa watanzania wengi masikini kuja kukaa na kujadili mambo ambayo yameshajadiliwa na kuamuliwa uamuzi ndani ya vikao maalum vya kambi ya chama tawala (caucus) na upinzani pia. Napata hisia wanachi tunaibiwa na wabunge kwani hakuna cha maana wanachofanya. Ingekuwa bora Spika akishirikiana na kila kiranja (Chief whip) wa kambi hizo mbili bungeni wawakilishe maamuzi, idadi ya kura za wabunge kama zilivyopigwa ndani ya kambi (caucus) zao badala ya watu wazima, wasomi waliobobea kwenda kupasha viti moto na kula fedha za walipa kodi wa nchi hii bila jasho.
Pili, ndio maana kwa mfumo huu wa kujali zaidi nidhamu ya chama na kupuuza maslahi ya kitaifa basi ni bora hata watoto wadogo wa chekechea, mangumbaru (wasio na elimu ya kiwango cha kutoa maamuzi ya msingi) waruhusiwe kuwa wabunge. Binafsi nadhani Bunge letu limefikia mahali nalifananisha na kusanyiko la watoto wa chekechea. Pamoja na ukweli kuwa serikali inaongozwa kwa kuzingatia ilani ya uchaguzi ya CCM, kinachogomba ni kwanini utekelezaji hauzingatii kanuni za msingi za uwajibikaji kwa wanachi na Taifa kwa ujumla? Hoja za wabunge wa chama tawala katika sakata la Zitto Kabwe zilionesha kabisa ilikuwa ni katika kutekeleza agizo la chama na si utashi wa dhati wa wazungumzaji. Na ndio maana wale wabunge makini wa CCM hawakuchangia hoja; inaonekana hawakuwa tayari kutuonesha ni kwa jinsi gani mfumo wa bunge ulivyoteka (hijack) akili zao.
Tatu, pamoja na spika kusisitiza kanuni mpya zinakuja karibuni, ni wazi huu si muarubaini kwani bila katiba mpya hatufiki mahali. Kuna haja ya watanzania tuwe na kongamano la kitaifa tujadili namna tunavyoweza kujiundia taratibu mpya za mustakabali wa Taifa letu bila kuzingatia sana hii mifumo ya kisiasa ya kimagharibi. Demokrasia ya magharibi kwa kiasi fulani nadhani ina matatizo kwa mazingira ya kiafrika hususan Tanzania. Nikiangalia jinsi bunge letu linavyoendeshwa na linavyotumiwa kufanya kazi za mhimili wa utawala (executive) badala ya wajibu wake halisi (legislative) nashindwa kumlaumu mbunge yeyote manake naamini kwa mfumo tulionao hata kama chama cha upinzani kinashika hatamu leo, sanaa za maonesho hazizuiliki. Nimejaribu kuitizama hii kasheshe ya hivi majuzi ya mheshimiwa Zitto Kabwe, binafsi, napata hisia kuwa mfumo wetu wa demokrasia ya vyama vingi wa kimagharibi labda pia ni tatizo.
Kuna mambo yanayoambatana na mfumo huu ambayo inabidi tuyafanyie mabadiliko katika sheria zetu. Kwa mfano, ukizingatia mfumo tulionao wa kibunge wa jumuiya ya madola: yaani unaruhusu chama chenye wabunge wengi kiamue kila kitu bila kujali hata nadhiri binafsi (conscience) ya wabunge. Yaani chama tawala kinakuja na hoja inayotetea maslahi ya chama na viongozi wake wala si Taifa. Na wabunge wa chama hicho wanaagizwa na kushinikizwa kwa mfumo wa nidhamu ya chama (party discipline) kuunga mkono jambo kama hilo hata kama nafsini mwao sivyo wanavyofikiri basi ni hatari sana. Yaani mfumo wa kisiasa tulionao unaruhusu taasisi nyeti kama Bunge kutumika kama chombo cha kuvunja Katiba; kwani, ibara ya kumi na nane (18) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa haki ya uhuru wa mawazo katika vipengele vyake vinne: a, b, c na d. Bunge letu haliheshimu vipengele viwili hapa:
Kwa mfano, kifungu (a) kinazungumzia: 'uhuru wa mtu kuwa na maoni na kueleza fikra zake', lakini Bungeni kwetu mfumo unaruhusu maamuzi ya wabunge katika kambi (caucus) zao hata kama yana upofu basi lazima yapitishwe bila kuhojiwa kwa uchambuzi makini. Kinyume cha hapo mbunge ataadhibiwa na kamati ya nidhamu ya chama husika pindi akijaribu kuhoji au kuonesha kutoridhishwa na jambo husika. Mfumo huu ndio tunaotakiwa tuondokane nao, la sivyo kama tutaiga kila kitu kutoka demokrasia ya nchi za magharibi basi nchi yetu haitatoka katika lindi hili la wabunge waliotekwa fikra. Na hii haijali tunatawaliwa na CCM au chama kingine chochote.
Kifungu cha (d) kinazungumzia: 'haki ya mtu kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii'. Tukizingatia mjadala wa Zitto Kabwe juu ya kuundwa kwa kamati ya uchunguzi ya Bunge napata hisia mheshimiwa alikuwa akiegemea haki ya kikatiba ambayo imeainishwa katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yaani waziri anaweza kusaini mkataba bila kutaarifu Bunge kama taasisi ya uwakilishi wa wananchi. Hili ni suala muhimu kwa jamii kwa hivyo kama lina utata ni vyema uchunguzi ungefanywa. Ila mfumo wetu una mwanya wa kuruhusu katiba ivunjwe kutokana tu na "uwingi wa wabunge wa chama tawala" ambao inawalazimu wafuate agizo la chama kupitia kambi (caucus).
Wabunge wa chama tawala wanajinyima haki ya kupewa taarifa juu ya suala muhimu la jamii kwa kuunga mkono hakuna haja ya uchunguzi wa madai ya mheshimiwa Zitto. Hii ni sababu ya mfumo wa siasa tulionao unawalazimisha wabunge wenye akili timamu wasizitumie pale inapobidi. Sitaki niwalaumu wabunge wa chama tawala manake naona mfumo wa kisiasa unatoa mwanya na kuwalazimisha wasihoji na waunge mkono maamuzi ya chama ambayo si yakinifu. Na usipohoji unaadhibiwa na chama chako.
Hapa inamaanisha wabunge wengi wa chama tawala kwa ishu kama ile ya Karamagi na Zitto naamini si wote walikuwa na msimamo waliouchukua kuunga mkono adhabu iliyotolewa. Ila naamini tayari kulikuwa na agizo ndani ya kambi ya chama tawala kuamua vile. Ni wazi wabunge wetu wametekwa kiakili, yaani chama cha Mapinduzi kinawasaidia kufikiri na kuamua mambo kadhaa yenye maslahi kwa umma na kuwafanya wayaamue kwa kufuata maelekezo ya watawala. Na hapa maamuzi yanakuwa si kwa ajili ya umma bali dhidi ya wachache, yaani wanasiasa mafia fulani ambao ni wateule wanaostahili kufaidi keki ya nchi hii.
Ndio maana mwanataaluma mmoja hivi karibuni katika gazeti la 'The Citizen' tarehe 22 August 25, 2007, kanena kuwa yaliyomkuta Zitto ni Bunge kutenda kosa la "Crime against Logic", yaani "Kosa/hatia dhidi ya Kufikiri sahihi". Pamoja na lawama zinazoelekezwa kwa wengi wa vigogo hasa kule bungeni kama Spika na wabunge kadhaa na hata mheshimiwa Karamagi, nadhani maoni yangu tukae chini kama Taifa tuunde demokrasia ya kitanzania, yenye kuzingatia maslahi ya nchi ambayo itakuwa na Bunge lisiloruhusu mwanya wowote wa mbunge kufungwa mdomo hata kama anatoka kwenye chama kinachotawala. Ikibidi tusiwe na mawaziri ambao ni wabunge au hata wakuu wa mikoa ambao ni wabunge. Mianya inayoingilia uhuru wa mbunge wa kufikiri inatokana na mfumo wa kibunge unaowapa wabunge wengi (majority) bungeni kutuamulia mambo kama watoto wa chekechea.
Tukiachia mfumo tulionao wa kibunge wa Jumuiya ya Madola uendelee basi hata kama siku za usoni kitashinda kwa kishindo chama kingine zaidi ya CCM, bado kitatumia mianya iliyopo sasa kupitisha na kujadili maamuzi katika hali ya kitoto kama tunavyoshuhudia sasa. Wanasiasa wetu waanzie kwenye vyama vyao kuweka taratibu za uwazi na uhuru wa viongozi na wabunge wanaowakilisha vyama wawe huru kuzungumzia hata mambo yanayogusa maslahi ya vyama vyao na kukinzana na maslahi ya Taifa bila kubanwa na kamati za nidhamu za vyama vyao. Tusipoacha mfumo wa kuadabishana ndani ya vyama vyetu, hata Bungeni hatutaruhusu wabunge wetu wazungumze kwa uwazi. Na ndio kinachotokea kwa sasa.
Na ndio tatizo lililotufikisha hapa tulipo leo ambapo Bunge la bajeti lililokwisha majuzi lilikuwa sawa na 'Sanaa ya Maigizo', mahali ambapo wabunge kwa ujumla wao na kwa makusudi kabisa hawajali maslahi ya nchi ila tu kujali fedha na posho, huu ni ulafi wa hali ya juu (collective greed of the highest degree) kuunga mkono na kupitisha maamuzi kadhaa yasiyozingatia maslahi ya nchi yetu na wananchi kwa ujumla wao. Inanikumbusha mwanafalsafa wa kifaransa, Jean-Francois Bayart anavyoiona hali kama hii kama siasa za tumboni (politics of the belly) akihusisha na mkakati wa wanasiasa kujitajirisha pamoja na kuimarisha utamaduni wa kung'ang'ania madarakani tu. Ni kama vile kwao wanaangalia maslahi yao na chama chao tu; wananchi na nchi kwa ujumla si hoja. Nionavyo hii inasababishwa na mfumo holela wa kiunyanyasaji (irregular coercive mechanism) tulionao ambao tunafikiri ndio demokrasia makini kumbe ni mfumo wa vyama vingi wa hali ya chini sana (primitive multipartism)
Nahitimisha kama nilivyoanza makala hii juu ya kukubali kukosolewa hata kama kunauma kiasi gani lazima kukubaliwe kama changamoto. Kukichukuliwa ni kama kudhalilisha utawala ama ni kudanganya basi ujue maendeleo ya jamii husika hayatafikiwa. Ni wakati tubadili mfumo wetu wa kisiasa ili uendane na wakati na mahitaji ya wote na si wachache tu kwa kuondoa mianya yote inayotulazimu tufikiri kama watoto katika maamuzi ya kimsingi ya nchi yetu na kutuadabisha pindi tunapojaribu kufikiri kwa umakini.
Tukibadili mfumo wetu wa kisiasa tutaweza kuondoa ile nguvu ya chama tawala kuwa na nguvu ya kudhibiti Bunge kama ilivyo sasa hata kama kuna wingi wa wabunge. Hii ni lazima ianzie kwenye vyama vya siasa; manake leo ni CCM kesho ikiwa DP au Chadema kwa mfumo huu wa kibunge wa jumuiya ya Madola sitashangaa kumwona mtu kama Zitto au Mtikila akifanya kwa mbwembwe ndani ya Bunge haya haya yaliyokuwa yakifanywa na wabunge wa chama tawala bila aibu.
Kama tunadhani tuna mfumo bora wa kidemokrasia barani Afrika, ni wakati wa kutafakari; la sivyo tutakuwa tunatupiana lawama bila sababu za msingi kwani mfumo wa kisiasa unaruhusu taasisi ya Bunge kuonekana kama tamthiliya kwa yeyote mwenye uchungu na nchi yetu. Na tujiulize: Ili ile kanuni ya fizikia izingatiwe bila kukwepeka, je wabunge wenye kutoa hoja zinazofanana na watoto wa chekechea, je ni nani wa kulaumiwa, wabunge hasa wa chama tawala au ni mfumo mzima wa kisiasa?
Wednesday, August 15, 2007
VITA YA MAFUTA CONGO DRC--UGANDA?
Kama ni kweli mafuta ni chanzo cha ugomvi na Kongo, je ni nini nafasi ya Uganda katika biashara ya mafuta barani Afrika.
Ni lazima watu tutambue kuwa Ituri ni eneo lenye utajiri wenye balaa sana kwani ni chanzo cha mgogoro wa sasa kati ya nchi hizi mbili.
Saturday, August 11, 2007
SHIRIKISHO LA AFRICA MASHARIKI-- SI HATUA MUAFAKA
Baadhi ya wanaofuatilia mtizamo wangu ni wazi nimekuwa napinga Shirikisho la Afrika Mashariki ila nikiunganga mkono hatua ya Jumuiya tu kwani naamini Shirikisho la Afrika Mashariki itakuwa ni hatua ya kisiasa isiyokuwa na manufaa yeyote kwa mwanachi wa kawaida.
Moja, mwaka 1958, Osagyefo Kwame Nkrumah alifanya juhudi sana kuinganisha Afrika kwa kuanzia na Ghana na Guinea, ikafuatiwa na Ghana-Guinea-Mali ambazo zote hazikudumu. Pili, kukaja Shirikisho la Senegambia kati ya mwaka 1981 na 1989. Zote hizi hazikudumu sana wala kuweza kusimama; kwa ujumla mashirikisho ya kisiasa yaliyojaribiwa katika karne iliyopita hayakufanikiwa pia si tu Afrika bali hata sehemu nyingine za ulimwengu na mifano ipo mingi: kwa mfano, Shirikisho la India Magharibi (West Indies Federation) kati ya mwaka 1952 hadi 1962.
Nyingine ikawa ni Shirikisho la Kijamaa la Mataifa ya Kiarabu (Federation of Socialist Arab States) kati ya mwaka 1972 hadi 1977 ambapo msisitizo ulikuwa wa kizalendo yaani Pan Arabinism; alafu likawepo lile shirikisho la Yugoslavia kati ya mwaka 1945 hadi 1992; na mfano wa mwisho kabisa ni lile shirikisho kubwa kubwa kabisa la kisiasa wakati wa vita baridi la Urusi ( Union of Socialist States of Russia) la mwaka 1922 hadi 1991.
Unaweza kuona mashirikisho niliyoyataja hapo juu yalianza na kufa kwa sababu mbalimbali ambazo pia zipo hapa Afrika Mashariki. Lakini pia mtu anaweza kujiuliza mbona yapo mashirikisho ya kisiasa ambayo bado wamo na yanaendelea? kwa mfano, Shirikisho la Nigeria lenye watu takriban millioni mia moja na kumi (110) au lile la Ethiopia lenye wakazi takriban milioni sabini na nane (78). Kama kweli Mashirikisho haya mawili ya kiafrika yana tija hasa kwa wananchi wa kawaida ni kwanini basi nchi zote hizi mbili bado ziko katika kundi la nchi zinazoendelea na si nchi zilizoendelea?
Hii ni sababu inayonifanya mimi kutokuunga mkono wazo la Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki. Nikihakikishiwa ni dawa ya kutuondoa kutoka katika nchi zinazoendelea, au zile masikini sana ulimwenguni (LDCs) basi nitaunga mkono; ila kwa hali ya sasa nafikiri shirikisho halina maslahi makini ukiacha matakwa binafsi ya wachache.
Nimejaribu kutizama pia lile shirikisho ambalo nadhani ni mfano wa mafanikio ulimwenguni, nalo ni ule Muungano wa Mataifa ya Amerika ( United States of America) ambalo kisiasa ni mfano wa kuigwa kimafanikio. Je hiki ni kielelezo cha Shirikisho la Afrika Mashariki kufikiwa? Mimi sioni kama ni kweli kabisa: nikumbushe kihistoria ilihitajika takriban miaka mia moja (100)--1776 hadi 1865 pamoja na vita kali na kubwa ya kiraia ya mwaka 1861 hadi 1865 ndipo Marekani ikakomaa na kuweza hata kustawi kama taifa lenye nguvu kabisa ulimwenguni.
Ni wazi kuundwa kwa Shirikisho sio mchakato wa kuharakishwa kama akina Museveni, Kibaki na Kikwete wanavyotaka. Kuna mambo mengi ya kuzingatia hasa ukiangalia EAC ni jumuiya yenye nchi zenye historia ya kupiganapigana katika kila jambo la kisiasa.
Labda nisisitize kuwa si Marekani tu ambapo mambo hayakuwa rahisi kama vile maraisi wetu wanavyotaka tuharakishe kufikia Shirikisho. Niwapeleke katika jumuiya ya Ulaya--(European Union). Kuanzia juhudi za mwanzo kabisa pale uliposainiwa mkataba wa Roma- 1957, kuanzisha Jumuiya ambayo mpaka leo mchakato wa kuunda Shirikisho la Kisiasa umebaki kiini macho. Mwaka juzi tu wanachi wa Ufaransa na Uholanzi walikataa kuunga mkono Katiba mpya ya Jumuiya ya Ulaya kwenye kura ya maoni, ambapo lilikuwa ni pigo katika kukwamisha mchakato mzima wa kufikia Shirikisho la Kisiasa. Tunaweza kuona ni miaka zaidi ya hamsini sasa Ulaya inashindwa kuunda Shirikisho la Kisiasa.
Mambo yote haya niliyoyataja yananifanya niamini kuwa muungano ya kiuchumi ni hatua muafaka ambayo itatufaidisha kiuchumi baada ya kipindi fulani. Nionavyo, Shirikisho la Kisiasa halitaweza kwa jinsi yeyote kuleta faida yeyote kwa mwananchi wa kawaida zaidi ya kuwafaidisha wanasiasa wetu. Wanasiasa wetu waache mawazo eti ile kuwa tu na idadi kubwa ya watu basi utakuwa na soko kubwa ambayo ni kielelezo cha nguvu za kiuchumi. Kwa Jumuiya yetu kweli soko litakuwa kubwa ila ni dhaifu sana kiuchumi; ni soko la wateja wengi ila ni masikini sana na ndio hapa nadhani zifanyike juhudi kuendeleza wananchi kielimu na kiuchumi hasa kiujasiriamali (entreprenuership) ndipo tutegemee soko lenye tija. Kinyume chake, hii "uharakishaji" ni usanii mwingine wa watawala kama walivyowahi kujaribu hapo nyuma na kutofanikiwa.
Mwisho ni vyema tuangalie historia ya mashirikisho ya kisiasa katika sehemu kadhaa za dunia ili tuweze kung'amu tufanye nini katika juhudi zetu za kujumuika kimataifa; lisiwe suala la kuharakisha bila kujiuliza je ni kwa maslahi ya nani? Je watawala wanawaza juu ya mwananchi wa kawaida katika jumuiya? Mimi nashangazwa sana na hili zoezi la kukusanya maoni juu ya Shirikisho kufanyika wakati tayari wameshatia saini kuruhusu "kuharakisha mchakato" mzima wa kuunda Shirikisho. Zoezi zima la kukusanya maoni naamini ilikuwa ni ufujaji wa fedha kwani viongozi wetu walishaamua jambo walilotaka kutuuliza; sasa sijue kwanini wanakusanya maoni kwa kitu walichokwisha kitolea maamuzi. Ama kweli tusipokuwa makini tutaburuzwa bila kutafakari.
UMOJA WA AFRIKA--USA NI NDOTO NYINGINE ZA ALINACHA
Leo hii, karibu miongo mitano, bado tuko palepale hatujaweza kuamua tufuate hoja ya Asgyefo au Julius. Mwaka 2002, October 15, ikiwa ni miaka 38 ya OAU, viongozi wetu walikutana
Mkutano wa maraisi wa Afrika kule
Mwishoni mwa mkutano ule, ni wazi ilijionesha wazi kuwa Umoja wa Afrika (AU) tulionao umefeli kabisa. Raisi wa kamisheni ya AU, Alpha Oumar Konare wa
Je tumuenzi Julius Nyerere au Kwame Nkrumah? Hadi sasa wazo la Nyerere linaungwa mkono na wengi wa viongozi waliokutana kule Ghana.
YAWEZEKANA RAISI KIKWETE NI MWOGA!
Kama sijakosea Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mwoga katika kuwachukulia hatua watendaji kadhaa pale panapotokea tuhuma zenye kustahili mtu kuadhibiwa. Hii kusema bei ya mafuta kushindwa kudhibitiwa na serikali ni udhaifu wa Ewura kunanitia wasiwasi sana, kwani raisi anajaribu kutupa mpira. Ninahisi wauza mafuta ni kundi linaloendesha mambo kimafia mafia hivi na lina uswahiba na baadhi ya vigogo wenye nguvu (untouchables).
Serikali inaogopa kuwagusa na inarusha mpira kwa Ewura iwashughulikie situ ambacho nadhani Ewura hawataweza. Kuna uwezekano serikali yetu imeshanunuliwa na hawa mafia wa mafuta ndio maana wanaogopwa na wanajipangia bei watakavyo. Kama sivyo, basi serikali ijaribu kufanya yale iliyofanyiwa Shirika la ndege la Uingereza wiki hii kwa kupigwa faini dhidi ya kupanga bei ghali kuwanyanyasa wasafiri. Nitaeleza juu ya muono wangu huu wa labda raisi wetu ni mwoga mwishoni mwa waraka wangu wa leo; ila kwanza nigusie hisia zangu kadhaa pale nilipobahatika kumuuliza Raisi Kikwete maswali mawili wakati akihojiwa na shirika la utangazaji la VOA la Marekani hivi majuzi.
Kwa miaka sita sasa nimekuwa mfuatiliaji wa kipindi cha mahojiano cha redio na televisheni "Straight Talk Africa" kinachorushwa na shirika la utangazaji la Sauti ya America (VOA) na kuendeshwa na mtangazaji Shaka Sally. Hivi karibuni pia nimekuwa pia mshiriki na nimepata nafasi kutoa ama kuuliza maswali juu ya mada zilizokuwa zikijadiliwa. Wiki hii, yaani tarehe 1/8/2007, Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa ndiye mgeni akihojiwa kutoka Dodoma. Washiriki tulitakiwa tutume maswali mapema kwa barua pepe. Nilifanya hivyo ili nipate nafasi ya kipekee kumuuliza Raisi swali juu ya mustakabali wa nchi yetu. Na kwa bahati nzuri kabisa, maswali mawili ya kwanza yalitoka kwangu; yalihusu wasiwasi wangu juu ya mchango wa sekta ya madini kwa uchumi wetu. Mheshimiwa Raisi alinijibu na nikaridhika hasa swali la kwanza ila sehemu ya pili kidogo kutokana na uhariri uliofanywa na Shaka Sally, sikuridhika na jibu la mheshimiwa Raisi.
Swali langu la kwanza nilitaka mheshimiwa Raisi lilikuwa ni kwa vipi ametimiza ahadi yake ya kuipitia upya mikataba ya madini iliyosainiwa na serikali iliyopita ili sasa ituletee tija? Raisi alijibu vyema kwa maoni yangu na napenda nimshukuru sana kwani alieleza makubaliano kati ya serikali na makampuni mawili: Barrick Gold na Resolute Mines, kuwa sasa yanalipa kwa takriban asilimia 33% ya kodi ikijumuisha pia na mrabaha.Na akasema kuwa kiwango cha dunia au kimataifa ndio hicho kinachotumika katika nchi nyingine. Raisi aliahidi kuwa kuanzia sasa mchango wa makampuni ya madini itakuwa asilimia 33% na si tena yale mambo ya 3%.
Swali langu la pili ambalo mheshimiwa Raisi Kikwete hakuniridhisha kwa majibu na ningependa kama inawezekana atoe ufafanuzi zaidi pindi akipata wasaa niliuliza: Je ni kweli Tanzania hatuna uwezo wa ndani wa kuweza kuzalisha madini hadi hatua ya mwisho na badala yake tunauza nje madini katika hatua ya malighafi?
Raisi alijibu kuwa hatuna nibu la ndani kwa hili na imetubidi tutegemee mitaji ya nje ya kimataifa kama hali halisi inavyodhihiri. Binafsi, nilitegemea ajibu hivyo kwani si mara ya kwanza kusikia viongozi wetu wakisema hivyo. Jibu hili linanisumbua sana na litaendelea kuniuma roho labda mpaka atakapotokea mtu anipe maelezo fulani ambayo sidhani kama huwa yanazingatiwa tunaposema eti nchi ya miaka arobaini na zaidi ya uhuru haina uwezo wa kuuza rasilimali zake katika thamani stahili kupata faida halisi. Je ni kwanini nasema hivi?
Ili nimtendee haki Raisi Kikwete, labda nioneshe swali langu ambalo Shaka Sally alilihariri lilikuwa hivi: Je ni kweli Tanzania hatuna uwezo wa teknolojia au kitaaluma kutengeneza madini ya nchi yetu hadi hatua ya mwisho? Kama ni kweli, ni nini maana ya kuwa na idara ya Geolojia kwa mfano pale Chuo Kikuu cha Dar es salaam? Ina maana kwa miaka yote ya uwepo wa idara hii imekua ikifanya nini kama imeshindwa kutupatia wataalam katika sekta ya madini?
Manake kwa hoja ya kutegemea mitaji kutoka nje, inamaanisha chuo chetu kimeweza tu kutuzalishia wataalamu wa kusaini mikataba bila kuzingatia maslahi ya nchi, hii ni hatari kwa elimu yetu kwani haikidhi haja ya kuzalisha wasomi wazalendo, kweli tumekwisha. Nimpongeze mheshimiwa Raisi alishang'amua hili alipokuwa ziarani kule nchi za Nordic.
Nikiacha maswali ambayo niliyazua binafsi, niseme tu mahojiano ya Raisi yalikuwa mazuri sana na ya uwazi wa dhati. Kwa mfano, Raisi Kikwete akijibu swali la Juma Iddi, juu ya "Kupaa kwa Uchumi Wetu", Raisi aliweka wazi kuwa kwa sasa tuko kwenye mchakato tu na kusema Uchumi unapaa ni mapema sana. Alitumia kauli: "We are yet to see the trickle down". Hapa Raisi Kikwete aliifunga ile hoja ya majibizano kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu na waandishi kadhaa katika gazeti hili la Tanzania Daima.
Raisi aliulizwa na Shaka Sally juu ya Visheni yake kwa Taifa: Alisema lengo
Shaka Sally alitaka kujua kuwa tangu Raisi Kikwete awe raisi ni jambo gani au uamuzi gani mkubwa na muhimu anaweza kujivunia kati ya mengi aliyokwishafanya? Alisema ni upanuzi wa elimu ya sekondari ambapo asilimia 96% ya wanafunzi wameandikishwa shuleni. Ila alikiri kiwango cha elimu kinachotolewa hakina viwango madhubuti. Na alikiri ni changamoto iliyobakia kuboresha ubora (quality) akitumia neno 'tall order'. Hapa raisi Kikwete alinikuna kwa kuwa mkweli kwani ni kweli kabisa kunahitajika kazi ya ziada; yaani walimu bora na zana bora.
Jambo lingine Raisi Kikwete aliulizwa: je ni nini kinaichoisumbua sana roho yake tangu awe Raisi katika majukumu yake? Jibu la Raisi lilinipa hisia mchanganyiko; kwani raisi alisema kuwa pale anapomuondoa mtu kutoka kwenye madaraka yake amegundua imekuwa ikiambatana na habari za uzushi zaidi na si ukweli. Kwa maana nyingine majungu ni mengi
Hapa
Raisi amenishtua kidogo labda hana karama za kiuongozi za kutosha. Kwani kama ni kweli anaumia roho kwa kugundua baadhi ya mabadiliko ya viongozi aliyofanya hayakustahili kwa ajili ya majungu; basi inamaana kuwa hii kuongezeka kashfa kila kukicha na Raisi anakaa kimya labda pia anaumia roho?
Nitoe mifano michache ambapo kashfa zisizohitaji hata mtu kufikiri na kuchukua hatua dhidi ya wahusika: hivi waliosaini
Visheni yako haitafikiwa hata kidogo ukiumia roho kwa kupima majungu, wajibisha watu kwa ujasiri. Angalia hisia za wananchi juu ya kashfa mbalimbali alafu chukua maamuzi kuwaadhibu waliokuzunguka ambao wanakosa kila kukicha wakijua hawafanywi kitu. Woga wako utalifikisha Taifa hili katika siasa za kiushirika vikundi (patronage au cronyism)
Mwisho, nitoe hongera kwa mheshimiwa Raisi kwa mahojiano yale na VOA; Mungu Ibariki Tanzania iwe na viongozi majasiri wasio waoga na wenye kutenda badala ya kutoa sababu kwa kila jambo lililo ndani ya uwezo wao.
DRC-UGANDA VITANI?
Kuna habari za wanajeshi wa Kongo kuwavamia wa Uganda mpakani.
Saturday, August 04, 2007
LIGI YA UINGEREZA YAANZA
Sasa ligi inaanza na utabiri unaonesha ni mwaka wa timu zilezile za msimu uliopita.
Huko Hispania kuna uvumi kuwa Barcelona kumwongeza Henry haitafua dafu kiushambuliaji kabisa.
Ukiacha soka kuna mambo ya personality yamenikuna kidogo. Alafu kuna hii hali ya Zimbabwe inakuwa mbaya kila kukicha na inaonekana Robert Mugabe kaamua kukomalia urais.
Wednesday, July 25, 2007
SHIRIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI NI UTAPELI WA WATAWALA
Kwa kipindi chote cha ukusanyaji maoni ya wananchi juu ya kuharakishwa na pia kujua kama wazo la shirikisho ni muafaka, nimejaribu kutafakari maoni ya watu wengi na nikajiuliza swali: Hivi ni kwanini wanasiasa wetu wanatudanganya sana wanapotetea shirikisho au hata jumuiya kama ni jibu la umasikini,eti wigo wa soko utaongezeka na maisha bora yataibuka?Ndio hapa ngano ya Shirikisho inapoanzia; ni kweli, Shirikisho litakuwa na soko takriban la watu zaidi ya milioni mia moja. Hili ni soko la pili kwa ukubwa nadhani hapa Afrika ukiacha lile ya shirikisho la Nigeria lenye watu zaidi ya milioni mia moja arobaini na ushehe.
Pamoja ukubwa wa soko la Nigeria, bado watu wengi-wateja wa soko-ni masikini wa kutupwa sawa na hapa kwetu. Kimahesabu, "sifuri ukijumlisha sifuri ni sawasawa na sifuri". Unategemea masikini anunue nini kama tunatetea hoja ya wigo wa soko? Bila hatua madhubuti kwa kila nchi kuwezesha wananchi wake kuwa na nguvu za kushiriki kwenye soko ni bure kabisa. Hatuhitaji shirikisho manake hao wanaongoza nchi zao ambao wameshindwa kuwawezesha wananchi wengi kutoka kwenye umasikini, ndio haohao watakaotuongoza katika shirikisho. Je wana lipi jipya kukabiliana na dola kubwa la shirikisho ukiachilia mbali kushindwa kwao kwenye serikali zao ndogo?
Nadhani tunahitaji tu jumuiya kama ilivyo sasa ili ichochee kuondoa umasikini na wala si shirikisho. Naamini kuwa si sahihi kuwa ukubwa wa eneo au wingi wa watu ni kigezo cha kuwa na nguvu za kiuchumi. Turejee vitaifa vidogo vidogo kama Uingereza, Ufaransa, Japan na tujiulize je wana ukubwa wa hata Tanzania? Au yapo mataifa yenye hadhi ya kuitwa bara kama vile: Antarctica na Australia pamoja na ukubwa wao bado si mataifa namba moja kwa utajiri au maisha bora ulimwenguni. Nasema hii ni ngano ya wanasiasa kutafuta ofisi za kuendeleza maisha yao labda.
Nikitizama upande wa faida ya uwekezaji kutoka nje (FDI) ambazo tayari zinajionesha katika kila nchi kwa sasa ni wazi kuna faida bila kutegemea shirikisho. Tuangalie mashirika mbalimbali ya kikanda kama vile ASEAN la bara Asia, COMESA na hata SADC utaona ongezeko la uwekezaji na ukuaji wa uchumi na biashara bila mfumo wa shirikiso katika nchi husika. Hivi Botswana au Mauritius chumi zao zinastawi sana kwa ajili ya Shirikisho au utawala bora? Ni wazi tuna tatizo la utawala na usimamizi wa rasilimali zetu na kama ni hivyo hata lije Shirikisho ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu. Inaonekana hatujui tatizo letu Afrika Mashariki sio kuongeza soko; tujitizame kwanza, la sivyo tutahamisha matatizo ya utawala mbovu kutoka vijinchi vyetu hadi kwenye Shirikisho.
Naamini hata kama Shirikisho litaundwa, bado serikali za ndani za nchi zetu zitabakia na hatamu ya kuvutia uwekezaji ili kutoharibu hali ya uchumi wa nchi zetu. Kwa mantiki hii tuturajie serikali hizi kuendelea kutoa misamaha ya kodi na hata ruzuku kuvutia wawekezaji ili kuzuia kuachwa nyuma. Sasa hapa Shirikisho ni kama mzigo tu wa kuongeza gharama za kiuendeshaji. Ninapowaza jinsi viongozi wetu wanavyopenda minjonjo ya ukubwa napata taabu sana kuelewa ni nini hasa lengo la kupigia mbiu Shirikisho. Naona kama vile ni kwa matakwa yao binafsi na wanatudanganya wananchi ndio maana naliona wazo la Shirikisho kama "ngano".
Jambo la msingi ni kuwa hata katika jumuiya nyamafu kama ya sasa ya EAC, haitawezekana kuleta maendeleo ya kiuchumi na kufuta umasikini katika jamii ambayo asilimia hamsini ya wananchi bado wanaathiriwa na malaria; nusu ya watoto wana kwashakoo na theluthi moja ya wanawake wanakufa kwa gonjwa la kuepukika kama ukimwi. Sioni ni kwa vipi shirikisho la kisiasa litaweza kuondoa madhila haya. Hatari iliyopo ni kutuongezea gharama za kuendesha shirikisho hasa za viongozi --mamwinyi--waliopania kujipandikiza ili kutawala eneo hili kama himaya yao na watoto na marafiki zao.
Kabla sijamaliza mada yangu, hebu tujiulize juu ya faida za Shirikisho la Afrika Mashariki kama zipo? Je Shirikisho hili linalotakiwa na watawala wetu litampa faida mwananchi wa kawaida? Na je katika "anga za kimataifa" tutakuwa na sauti kubwa ya kisiasa katika kada na duru za kisiasa za ulimwengu huu wa utandawazi? Je shirikisho litaweza kutukwamua dhidi ya "utegemezi wa wafadhili au wahisani?" Jibu naliona ni hapana: kwa taarifa tu ni kwamba yale mashirika makuu ya kiuchumi ulimwenguni kama Benki ya Dunia (World Bank), Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF), Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO) na hata Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) yanatoa mgawanyo wa nguvu za maamuzi kwa nchi au mataifa kupiga kura katika kufanya maamuzi mbalimbali kwa kuzingatia GDP.
Tukilitizama Shirikisho kama litaundwa ni kwamba litakuwa na GDP ya kama dola 30 bilioni sawa na asilimia 8% ya nchi ya Afrika Kusini. Kimsingi na kiutaratibu haitaweza hata kutimiza sharti la kutoa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia (WB). Tutaendelea kushikilia kiti kimoja katika Benki ya Dunia pamoja na nchi nyingine ishirini na mbili (22) za Afrika kwa kupokezana. Dunia ya leo bila kuwa na nguvu ya maamuzi ni kwa vipi tutajikwamua hali kandamizi kadhaa ambazo mataifa yenye nguvu yananyanyasa mataifa makubwa? Ni kutokana na muono wangu huu napatwa na hisia labda viongozi wetu hasa wanavyopigia debe hii ngano iharakishwe basi ni uzushi tu na usanii na si kwa maslahi ya uchumi bali ni maslahi binafsi labda.
NANI ATAMRITHI MUSEVENI?
Kufuatia kuibuliwa kwa kashfa ya ngono ya yule askofu mkosoaji sana kule Zimbabwe, Pius
Ncube, inasemekana huu ni mtindo wa "Big Brother". Chama tawala Uganda kimependekeza kuanzishwa kwa mafunzo ya kijeshi kwa kila mwananchi kwa lazima; je ndio mwanzo wa vita Uganda?
Nchini Uganda kumetokea walokole ambao wanajitajirisha kwa jina la Yesu. Je umasikini ni kujitakia?
Mwisho kweli Uganda bado nchi ya kijeshi, makada wa chama tawala walikutana majuzi; ona mambo yaliyojiri na vituko vya waziri mmoja msomi.
Saturday, July 21, 2007
MU 7 HANA LENGO LA URAIS WA EAC
Pili kuhusu jumuiya ni vyema tukamfahamu spika wa sasa wa bunge la jumuiya.
Monday, July 16, 2007
HATUHITAJI SHIRIKISHO ILA JUMUIYA INATOSHA--EAC
Lakini pia, kama mtanzania, mimi ni mmojawapo wa wale wasioridhishwa bado kama kweli tunahitaji kuwa na shirikisho la Afrika Mashariki (EAC) .Ukiusoma mkataba wa kuanzishwa kwa EAC unaeleza kinagaubaga mtiririko mzima unaopaswa kufuatwa na nchi wanachama ili kufikia shirikisho.
Yanayotokea kwa kipindi hiki, kidogo yananishangaza hasa "uharakishwaji wa kupata shirikisho" fast traking.Kwenye mkataba wa jumuiya-mataifa shirika-Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi-yanawajibika hatua kwa hatua, taratibu; yaani kwanza, muungano wa mapato(custom union), pili, soko la pamoja(common market), tatu, sarafu moja(monetary union) na mwisho Shirikisho la Kisiasa(Federation).
Lengo la mchakato huo ni ili kupata ushirikiano makini wa kiuchumi ambapo watu wenngi masikini wataweza kuishi na kumudu maisha ya kiwango cha juu katika eneo hili. Inapowezekana kunyanyua kiwango cha maisha cha raia wengi masikini basi shirikisho linakuwa linawezekana. Shirikisho lingetakiwa lifikiriwe katika kipindi kifupi hadi 2013 kuweza kuzibadili taasisi mbalimbali za kitaifa katika mataifa shirika ziwe chini ya mtandao mmoja wa shirikisho.
Sioni itawezekanaje katika kipindi kifupi hadi 2013 kuweza kuzibadili taasisi mbalimbali za kitaifa katika mataifa shirika ziwe chini ya mtandao mmoja wa shirikisho. Hebu nitoe mifano michache:
Moja, Nchi ya Kenya iko tayari kwa shirikisho kwani ni njia mojawapo ya kuimarisha zaidi nguvu yake ya kiuchumi na kibiashara. Uchumi wa Kenya inasemekana ni karibu asilimia 50% ya uchumi wa Uganda na Tanzania kwa pamoja. Pili, ukienda Uganda na Tanzania hapa pia kuna kiini macho. Taarifa za kiuhumi zinaonesha kiwango kidogo cha biashara kati ya nchi hizi mbili. Kwa mfano, Uganda Bureau of Statistis-2004 zinaonesha mwaka 2003 Uganda iliuza bidhaa za thamani ya dola 78 millioni kwa Kenya, alafu ikauza dola 5.8 milioni kwa Tanzania.
La kushangaza kabisa ni kwamba mwaka huohuo Uganda iliuza bidhaa za thamani ya dola 13.7 milioni kwenda Sudan ambayo sio nchi mwanahama wa EAC.
Ninachokiona hapa kuna hatari inakuja hapo baadaye: Uganda inafanya biashara zaidi na Sudan kuliko Tanzania. Tukumbuke mwaka 2003, Sudan ya Kusini bado ilikuwa itani; sasa hii hali imebadilika kabisa hali ni shwari, na mpaka 2011 upo uwezekano wa Kusini mwa Sudan kuwa taifa huru.
Na kwa hali iliyo sasa biashara kati ya Uganda na Sudan itakuwa sana na wala Uganda haitahitaji nchi kama Tanzania kibiashara kabisa. Haya yote yameshaanza kutokea sasa. Kwa ushahidi tu, mtu aende kushuhudia ni malori mangapi yanapita usiku na mhana yakiwa na shehena ya bidhaa kutoka Uganda na Kenya katika barabara ya Yei hadi Juba.
Uchumi mzuri unapimwa na biashara, na kama ni hivyo je shirikisho la nini?Jumuiya inatosha kwani vikwazo vyote ya biashara vitaondolewa. Shirikisho ni mzigo kwa wanasiasa kutafuna kile kinachozalishwa na faida ya jumuiya kwa kuwakirimu wanasiasa na misafara yao ya kifahari.Nawaunga mkono wananchi kukataa shirikisho ila nasisitiza Jumuiya ni muafaka.
Saturday, July 14, 2007
Wednesday, July 11, 2007
KAMPENI ZA MUSEVENI EAC ZAANZA?
Museveni kapita miji ya Busia, Kisii, Migori, Isbania, Mwanza hadi Butiama katika juhudi za kujitambulisha kama mfalme mpya wa kaya ajaye.Inasemekana hata mkewe aliwahi kusafiri kwa basi kutoka Kampala hadi Nairobi.Kuna hisia jamaa amepania uraisi wa Shirikisho la EAC na mkewe atamrithi kule Uganda. Ziara yake haikuweza kumalizika kwani kutoka Musoma ilimbidi apande ndege ya serikali ya Tanzania kurejea kwao kwani barabara hazifai.
Haya yakitokea, kwenye chama chake NRM, kuna makundi ya kisirisiri kama yale ya mitandao ya CCM.
Ama kweli duniani kuna mambo, kumbe bado usodoma na ugomora upo makanisani?
Mwisho nimalize na tahariri ya kuitetea NGO : HAKI ELIMU kwani waheshimiwa wetu na akili zao mgando hawaitaki kabisa. Napenda sana kazi yake.
Saturday, July 07, 2007
UJAMBAZI SASA UGANDA
Wednesday, July 04, 2007
UNITED STATES OF AFRICA-KIINI MACHO
Hivi kuna sababu na haja ya kuharakisha jumuiya ya Afrika Mashariki?Pia ni vizuri tujue ile ripoti ya kiuchumi ya nchi za Mashariki ya Afrika inasemaje.
Habari ya kuvuti huko Uganda ni hii ya kubadilishwa kazi yule mlinzi au msaidizi wa Rais Museveni baada ya kumuumiza rais na sasa kuna mlinzi mpya.Hiyo ni burudani tosha ila kuna hii hadithi juu ya yale mapinduzi ya mwaka 1971 yaliyofanywa na Idd Amin.