My Blog List

Wednesday, July 25, 2007

SHIRIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI NI UTAPELI WA WATAWALA

Kamusi ya Kiingereza na Kiswahili inafafanua neno "MYTH" kama uwongo, jambo lililobuniwa na pia likimaanisha ngano. Mimi napenda nitumie neno 'ngano' kujenga mada yangu.

Kwa wale waumini wa dini mbalimbali neno 'Ngano" halitakuwa jipya kwani misaafu ya dini zote imejaa ngano za kila aina ambazo zinasaidia hasa wahubiri kufikisha ujumbe pale wanapohitajika kuhakikisha kuwa kondoo wa bwana hawapotei njia. Ninatizama Shirikisho la Afrika Mashariki ambalo hivi majuzi watanzania takriban 75% wameamua kulikataa hasa ule mpango wa wanasiasa wetu wa kuharakisha kufikia shirikisho itakapofika mwaka 2013. Binafsi siamini kuwa ni busara kuwa na shirikisho ila tu naunga mkono wazo la Jumuiya kama ilivyo sasa hivi ikiimarika kila kukicha kama taasisi itakayosaidia sekta ya uchumi kukua na urahisaji wa biashara miongoni mwa nchi zetu.

Shirikisho la Afrika Mashariki sio la lazima wala jibu toshelezi katika kupambana na umaskini. Kama lilivyokuwa tukio la uhuru katika miaka ya 1960 ambapo tunashuhudia nchi zetu zikiendelea kuwa katika kundi la nchi masikini zaidi ulimwenguni. Hali ya uchumi ni mbaya na nafikiri tutegemee pia ndivyo itakavyokuwa katika muungano wa kisiasa; kwani kwa mawazo ya uongozi tulionao hadi leo hii, kifikra si watu wa kutufikisha katika maendeleo. Bado mawazo yetu wengi tunafikiri kuwa kiongozi basi ni kujilimbikizia mali binafsi na familia pamoja na rafiki zetu.

Kwa kipindi chote cha ukusanyaji maoni ya wananchi juu ya kuharakishwa na pia kujua kama wazo la shirikisho ni muafaka, nimejaribu kutafakari maoni ya watu wengi na nikajiuliza swali: Hivi ni kwanini wanasiasa wetu wanatudanganya sana wanapotetea shirikisho au hata jumuiya kama ni jibu la umasikini,eti wigo wa soko utaongezeka na maisha bora yataibuka?Ndio hapa ngano ya Shirikisho inapoanzia; ni kweli, Shirikisho litakuwa na soko takriban la watu zaidi ya milioni mia moja. Hili ni soko la pili kwa ukubwa nadhani hapa Afrika ukiacha lile ya shirikisho la Nigeria lenye watu zaidi ya milioni mia moja arobaini na ushehe.

Pamoja ukubwa wa soko la Nigeria, bado watu wengi-wateja wa soko-ni masikini wa kutupwa sawa na hapa kwetu. Kimahesabu, "sifuri ukijumlisha sifuri ni sawasawa na sifuri". Unategemea masikini anunue nini kama tunatetea hoja ya wigo wa soko? Bila hatua madhubuti kwa kila nchi kuwezesha wananchi wake kuwa na nguvu za kushiriki kwenye soko ni bure kabisa. Hatuhitaji shirikisho manake hao wanaongoza nchi zao ambao wameshindwa kuwawezesha wananchi wengi kutoka kwenye umasikini, ndio haohao watakaotuongoza katika shirikisho. Je wana lipi jipya kukabiliana na dola kubwa la shirikisho ukiachilia mbali kushindwa kwao kwenye serikali zao ndogo?

Nadhani tunahitaji tu jumuiya kama ilivyo sasa ili ichochee kuondoa umasikini na wala si shirikisho. Naamini kuwa si sahihi kuwa ukubwa wa eneo au wingi wa watu ni kigezo cha kuwa na nguvu za kiuchumi. Turejee vitaifa vidogo vidogo kama Uingereza, Ufaransa, Japan na tujiulize je wana ukubwa wa hata Tanzania? Au yapo mataifa yenye hadhi ya kuitwa bara kama vile: Antarctica na Australia pamoja na ukubwa wao bado si mataifa namba moja kwa utajiri au maisha bora ulimwenguni. Nasema hii ni ngano ya wanasiasa kutafuta ofisi za kuendeleza maisha yao labda.

Nikitizama upande wa faida ya uwekezaji kutoka nje (FDI) ambazo tayari zinajionesha katika kila nchi kwa sasa ni wazi kuna faida bila kutegemea shirikisho. Tuangalie mashirika mbalimbali ya kikanda kama vile ASEAN la bara Asia, COMESA na hata SADC utaona ongezeko la uwekezaji na ukuaji wa uchumi na biashara bila mfumo wa shirikiso katika nchi husika. Hivi Botswana au Mauritius chumi zao zinastawi sana kwa ajili ya Shirikisho au utawala bora? Ni wazi tuna tatizo la utawala na usimamizi wa rasilimali zetu na kama ni hivyo hata lije Shirikisho ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu. Inaonekana hatujui tatizo letu Afrika Mashariki sio kuongeza soko; tujitizame kwanza, la sivyo tutahamisha matatizo ya utawala mbovu kutoka vijinchi vyetu hadi kwenye Shirikisho.

Naamini hata kama Shirikisho litaundwa, bado serikali za ndani za nchi zetu zitabakia na hatamu ya kuvutia uwekezaji ili kutoharibu hali ya uchumi wa nchi zetu. Kwa mantiki hii tuturajie serikali hizi kuendelea kutoa misamaha ya kodi na hata ruzuku kuvutia wawekezaji ili kuzuia kuachwa nyuma. Sasa hapa Shirikisho ni kama mzigo tu wa kuongeza gharama za kiuendeshaji. Ninapowaza jinsi viongozi wetu wanavyopenda minjonjo ya ukubwa napata taabu sana kuelewa ni nini hasa lengo la kupigia mbiu Shirikisho. Naona kama vile ni kwa matakwa yao binafsi na wanatudanganya wananchi ndio maana naliona wazo la Shirikisho kama "ngano".

Jambo la msingi ni kuwa hata katika jumuiya nyamafu kama ya sasa ya EAC, haitawezekana kuleta maendeleo ya kiuchumi na kufuta umasikini katika jamii ambayo asilimia hamsini ya wananchi bado wanaathiriwa na malaria; nusu ya watoto wana kwashakoo na theluthi moja ya wanawake wanakufa kwa gonjwa la kuepukika kama ukimwi. Sioni ni kwa vipi shirikisho la kisiasa litaweza kuondoa madhila haya. Hatari iliyopo ni kutuongezea gharama za kuendesha shirikisho hasa za viongozi --mamwinyi--waliopania kujipandikiza ili kutawala eneo hili kama himaya yao na watoto na marafiki zao.

Kabla sijamaliza mada yangu, hebu tujiulize juu ya faida za Shirikisho la Afrika Mashariki kama zipo? Je Shirikisho hili linalotakiwa na watawala wetu litampa faida mwananchi wa kawaida? Na je katika "anga za kimataifa" tutakuwa na sauti kubwa ya kisiasa katika kada na duru za kisiasa za ulimwengu huu wa utandawazi? Je shirikisho litaweza kutukwamua dhidi ya "utegemezi wa wafadhili au wahisani?" Jibu naliona ni hapana: kwa taarifa tu ni kwamba yale mashirika makuu ya kiuchumi ulimwenguni kama Benki ya Dunia (World Bank), Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF), Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO) na hata Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) yanatoa mgawanyo wa nguvu za maamuzi kwa nchi au mataifa kupiga kura katika kufanya maamuzi mbalimbali kwa kuzingatia GDP.

Tukilitizama Shirikisho kama litaundwa ni kwamba litakuwa na GDP ya kama dola 30 bilioni sawa na asilimia 8% ya nchi ya Afrika Kusini. Kimsingi na kiutaratibu haitaweza hata kutimiza sharti la kutoa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia (WB). Tutaendelea kushikilia kiti kimoja katika Benki ya Dunia pamoja na nchi nyingine ishirini na mbili (22) za Afrika kwa kupokezana. Dunia ya leo bila kuwa na nguvu ya maamuzi ni kwa vipi tutajikwamua hali kandamizi kadhaa ambazo mataifa yenye nguvu yananyanyasa mataifa makubwa? Ni kutokana na muono wangu huu napatwa na hisia labda viongozi wetu hasa wanavyopigia debe hii ngano iharakishwe basi ni uzushi tu na usanii na si kwa maslahi ya uchumi bali ni maslahi binafsi labda.

Nawaona wanasiasa wetu katika mtizamo wa mnyama kondoo; hasa pale anapokuwa anapelekwa machinjioni na wala hajui kifo chake. Wanasiasa wetu hawatizami mbali katika utendaji wao mara nyingi. Nchi zetu tusipokuwa makini nahisi tumetekwa nyara na sera za kizamani za kiuchumi ambazo hazikidhi haja ya jamii kwa ujumla bali kwa matakwa binafsi zaidi. Wenye kuona mbali wamebaki tumechanganyikiwa ni kwa vipi bado barabara zetu ni mbovu, hakuna huduma bora hospitalini na bado kuna wanakijiji wanalala nyumba za majani na udongo miaka zaidi ya arobaini ya uhuru.

Je tiba ya haya ni shirikisho? Mimi siamini kabisa, ndio maana sitaki Shirikisho naona hii ni ngano ya wanasiasa katika kutudanganya kama watoto kwa maslahi yao zaidi; ni 'utapeli wa watawala' ila tu Jumuiya tuliyonayo hadi sasa ni hatua muafaka.

NANI ATAMRITHI MUSEVENI?

Kama kuna mtu pekee ambaye anaweza kumruthi rais Museveni siku za usoni ni mheshimiwa Amama Mbabazi. Museveni aliwahi kusema huyu ndie pekee 'presidential material' na sasa yeye mwenyewe kathibitisha. Lakini inasemekana Museveni kukaa madarakani muda mrefu kunamfanya sasa kununua umaarufu kwa kutumia pesa kuwarubuni wapinzani warejee NRM.Hata aliyekuwa katibu mkuu wa EAC, Amanya Mushega ambaye wametofautiana kwa muda mrefu sasa anatafuta njia za kurejeana japo inasemekana ni vigumu. Lakini pia rafiki na swahiba wa Museveni naye kaanza kumtenga bosi wake.

Kufuatia kuibuliwa kwa kashfa ya ngono ya yule askofu mkosoaji sana kule Zimbabwe, Pius
Ncube, inasemekana huu ni mtindo wa "Big Brother". Chama tawala Uganda kimependekeza kuanzishwa kwa mafunzo ya kijeshi kwa kila mwananchi kwa lazima; je ndio mwanzo wa vita Uganda?
Nchini Uganda kumetokea walokole ambao wanajitajirisha kwa jina la Yesu. Je umasikini ni kujitakia?

Mwisho kweli Uganda bado nchi ya kijeshi, makada wa chama tawala walikutana majuzi; ona mambo yaliyojiri na vituko vya waziri mmoja msomi.

Saturday, July 21, 2007

Kweli haya ni mambo makubwa, yaani Robert Mugabe anatumia mbinu chafu za akina Museveni kumchafua Askofu Ncube ambaye anampinga sana.

MU 7 HANA LENGO LA URAIS WA EAC

Rais Museveni ameamua kukanusha eti ana maslahi katika jumuiya ya Afrika Mashariki, yaani anataka kuwa Rais wa kwanza kama inavyosemkana licha ya hivi majuzi kufanya ziara kwa gari katika nchi zote tatu.
Pili kuhusu jumuiya ni vyema tukamfahamu spika wa sasa wa bunge la jumuiya.

Monday, July 16, 2007

HATUHITAJI SHIRIKISHO ILA JUMUIYA INATOSHA--EAC

Ripoti ya maoni ya wananhi wa Tanzania imetoka na ni wazi wananchi wengi wana woga mkubwa na hawataki shirikisho.Binafsi sitaki shirikisho ila tu napenda tuwe na jumuiya kwani nadhani Shirikisho ni maslahi ya wanasiasa tu na kwa mwananhi wa kawaida si tija.

Lakini pia, kama mtanzania, mimi ni mmojawapo wa wale wasioridhishwa bado kama kweli tunahitaji kuwa na shirikisho la Afrika Mashariki (EAC) .Ukiusoma mkataba wa kuanzishwa kwa EAC unaeleza kinagaubaga mtiririko mzima unaopaswa kufuatwa na nchi wanachama ili kufikia shirikisho.

Yanayotokea kwa kipindi hiki, kidogo yananishangaza hasa "uharakishwaji wa kupata shirikisho" fast traking.Kwenye mkataba wa jumuiya-mataifa shirika-Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi-yanawajibika hatua kwa hatua, taratibu; yaani kwanza, muungano wa mapato(custom union), pili, soko la pamoja(common market), tatu, sarafu moja(monetary union) na mwisho Shirikisho la Kisiasa(Federation).

Lengo la mchakato huo ni ili kupata ushirikiano makini wa kiuchumi ambapo watu wenngi masikini wataweza kuishi na kumudu maisha ya kiwango cha juu katika eneo hili. Inapowezekana kunyanyua kiwango cha maisha cha raia wengi masikini basi shirikisho linakuwa linawezekana. Shirikisho lingetakiwa lifikiriwe katika kipindi kifupi hadi 2013 kuweza kuzibadili taasisi mbalimbali za kitaifa katika mataifa shirika ziwe chini ya mtandao mmoja wa shirikisho.
Sioni itawezekanaje katika kipindi kifupi hadi 2013 kuweza kuzibadili taasisi mbalimbali za kitaifa katika mataifa shirika ziwe chini ya mtandao mmoja wa shirikisho. Hebu nitoe mifano michache:

Moja, Nchi ya Kenya iko tayari kwa shirikisho kwani ni njia mojawapo ya kuimarisha zaidi nguvu yake ya kiuchumi na kibiashara. Uchumi wa Kenya inasemekana ni karibu asilimia 50% ya uchumi wa Uganda na Tanzania kwa pamoja. Pili, ukienda Uganda na Tanzania hapa pia kuna kiini macho. Taarifa za kiuhumi zinaonesha kiwango kidogo cha biashara kati ya nchi hizi mbili. Kwa mfano, Uganda Bureau of Statistis-2004 zinaonesha mwaka 2003 Uganda iliuza bidhaa za thamani ya dola 78 millioni kwa Kenya, alafu ikauza dola 5.8 milioni kwa Tanzania.
La kushangaza kabisa ni kwamba mwaka huohuo Uganda iliuza bidhaa za thamani ya dola 13.7 milioni kwenda Sudan ambayo sio nchi mwanahama wa EAC.

Ninachokiona hapa kuna hatari inakuja hapo baadaye: Uganda inafanya biashara zaidi na Sudan kuliko Tanzania. Tukumbuke mwaka 2003, Sudan ya Kusini bado ilikuwa itani; sasa hii hali imebadilika kabisa hali ni shwari, na mpaka 2011 upo uwezekano wa Kusini mwa Sudan kuwa taifa huru.

Na kwa hali iliyo sasa biashara kati ya Uganda na Sudan itakuwa sana na wala Uganda haitahitaji nchi kama Tanzania kibiashara kabisa. Haya yote yameshaanza kutokea sasa. Kwa ushahidi tu, mtu aende kushuhudia ni malori mangapi yanapita usiku na mhana yakiwa na shehena ya bidhaa kutoka Uganda na Kenya katika barabara ya Yei hadi Juba.

Uchumi mzuri unapimwa na biashara, na kama ni hivyo je shirikisho la nini?Jumuiya inatosha kwani vikwazo vyote ya biashara vitaondolewa. Shirikisho ni mzigo kwa wanasiasa kutafuna kile kinachozalishwa na faida ya jumuiya kwa kuwakirimu wanasiasa na misafara yao ya kifahari.Nawaunga mkono wananchi kukataa shirikisho ila nasisitiza Jumuiya ni muafaka.

Saturday, July 14, 2007

LEO NI "BASTILE DAY"

Nchini Ufaransa leo ni siku ya kukumbukwa na kutafakari: "BASTILE DAY"

Wednesday, July 11, 2007

KAMPENI ZA MUSEVENI EAC ZAANZA?

Katika kile kinachoelezewa na baadhi kama kampeni ya Rais Museveni kuzunguka kwa gari nchi za Afrika Mashariki ni kampeni za kutawala eneo hili, basi jana Museveni alidhuru kaburi la Mwalimu Nyerere, nadhani kupata baraka za mzee.

Museveni kapita miji ya Busia, Kisii, Migori, Isbania, Mwanza hadi Butiama katika juhudi za kujitambulisha kama mfalme mpya wa kaya ajaye.Inasemekana hata mkewe aliwahi kusafiri kwa basi kutoka Kampala hadi Nairobi.Kuna hisia jamaa amepania uraisi wa Shirikisho la EAC na mkewe atamrithi kule Uganda. Ziara yake haikuweza kumalizika kwani kutoka Musoma ilimbidi apande ndege ya serikali ya Tanzania kurejea kwao kwani barabara hazifai.

Haya yakitokea, kwenye chama chake NRM, kuna makundi ya kisirisiri kama yale ya mitandao ya CCM.


Ama kweli duniani kuna mambo, kumbe bado usodoma na ugomora upo makanisani?

Mwisho nimalize na tahariri ya kuitetea NGO : HAKI ELIMU kwani waheshimiwa wetu na akili zao mgando hawaitaki kabisa. Napenda sana kazi yake.

Saturday, July 07, 2007

UJAMBAZI SASA UGANDA

Tanzania ni nchi ya usiri sana hasa juu ya masuala ya ujambazi lakini Uganda ni wazi kwani mtu unaweza kuwajua hata kwa sura majambazi gazetini.

Wednesday, July 04, 2007

UNITED STATES OF AFRICA-KIINI MACHO

Bara la Afrika kuwa nchi moja itabaki kuwa kiini macho milele.Mkutano uliomalizika karibuni viongozi wetu hawakuwa tayari kukubali wazo hili linalopigiwa chapuo na Ghadafi. Wengine wanatuambia kuwa ni wazi waafrika tumepotea njia hadi tutakapokubali kuwa na namna yetu ya kufanya mambo dhidi ya wazungu.

Hivi kuna sababu na haja ya kuharakisha jumuiya ya Afrika Mashariki?Pia ni vizuri tujue ile ripoti ya kiuchumi ya nchi za Mashariki ya Afrika inasemaje.
Habari ya kuvuti huko Uganda ni hii ya kubadilishwa kazi yule mlinzi au msaidizi wa Rais Museveni baada ya kumuumiza rais na sasa kuna mlinzi mpya.Hiyo ni burudani tosha ila kuna hii hadithi juu ya yale mapinduzi ya mwaka 1971 yaliyofanywa na Idd Amin.

Monday, July 02, 2007

MUSEVENI MTOTO MAFUNZO ZAID YA KIJESHI MAREKANI

Museveni anazidi kumuongezea ujuzi wa kijeshi mwanaye, je anamuandaa kumrithi?

Thursday, June 28, 2007

AMINA CHIFUPA KAUAWA--KIFO HIKI KICHUNGUZWE


Juzi usiku saa tatu na dakika kumi napokea sms kutoka kwa mtu fulani wa karibu aliyepo Dar es salaam ikiwa na maandishi ya herufi kubwa: AMINA CHIFUPA KATUTOKA, AMINI USIAMINI. Mara nasikia pia tangazo redio free afrika juu ya hili. Basi naamua kumuuliza huyu bwana ninini maoni yake?

Anajibu: WAMEMUONDOA KISAIKOLOJIA. TANZANIA HAIHITAJI MAJASIRI!NCHI HII NI BORA KUWA KIMYA TU! KAA NA FAMILIA YAKO KAMA UKIONA WATU WANA ISHU CHAFU ACHANA NAO! HAIKUHUSU. LEO NDIO MAADHIMISHO YA AGAINST DRUGS NA SHUJAA AMEONDOKA! IPO SIKU WATU WATACHOKA NA HAPATAKALIKA! IMENIUMA KUPITILIZA.Ni maneno mazito ambayo hata mimi yaliniingia hasa lakini naamini ni lazima wapiga filimbi(whistle blowers) waendelee kuwepo. Hisia zangu ni nyingi hasa kulihusu bunge letu. Nitaeleza kwa mujibu wa mambo yaliyojitokeza baada ya msiba huu.

Amina ni mtu anaelezewa na walomfahamu kama mtu aliekuwa na upeo ambao ulihitajika nchi hii.Ila wengine kuona anafariki katika hali isiyoelezeka kwa mtu mwenye akili timamu wanathubutu hata kukilaani chama cha mapinduzi japo mie nadhani tuna tatizo la utamaduni wa kutokubali kuelezwa ukweli.Wengine wamemfananisha na Princes Diana hata pia wengine wakafikia kusema siku ya madawa ya kulevya iitwe jina lake kitu ambacho sidhani kitasaidia kwa nchi kwani ni zaidi ya hapo ndio tutaweza kumuenzi: yaani kuwa mashujaa kupambana na umafia bila kuogopa ufa hadi bila kujali kufa kama Amina ndipo tutaikomboa nchi yetu dhidi ya umafioso wa baadhi ya watu.

Kwa ufupi nafikiri mhariri wa gazeti la serikali hakukosea,AminaChifupa alikuwa ni taa iliyopotea.Huko Dodoma wabunge wetu walionekana kwenye runinga wenye simanzi ila sina hakika kama ilijkuwa ni kweli ama ni unafiki tu. Nasema hivi kwani mimi naamini chombo kama bunge kingeweza kutoa msaada mkubwa sana wa ushauri nasaha wa kitaalam kumuokoa dada hyu dhidi ya hali ngumu aliyokuwa akikabiliana nayo.

Sijui kama kuna akina mama wabunge walijipenyeza hadi kuona Mbunge huyo alikuwa akiendeleaje hadi alipozidiwa.Wananchi wengi nikiwa mmojawapo naamini kabisa ile kauli ya Amina dhidi ya uuzaji wa dawa za kulevya ndio chanzo cha hii sukari tunayoambiwa imemwondoa, kwani imemsababishia mahangaiko na fedheha (depression) mengi ya ndani hasa pale ilipopelekea hata ndoa yake kuingia matatizo.Spika wa bunge na katibu wa bunge nadhani wana deni kutueleza: je walichukua hatua gani kumsaidia mbunge huyu hasa baada ya matatizo yake ya ndoa?

Sipendi sana kusikia hizi kauli za oh ni Mungu kaamua basi hatuwezi kufanya kitu, tufike mahali nchi hii tujifunze kuhoji matukio sio kuleta habari ya Mungu kwani ni dhihirisho nchi hii watu hatupendi kufikiri labda.Ukiweka suala la Mungu tayari unazuia uwezekano wa mtu kuchunguza, napenda sana serikali ianzishe uchunguzi mara moja.

Mwenye akili za kizamani atadai hii ni maisha binafsi, ila naamini katika dunia ya leo taasisi kubwa kama bunge inaendeshwa kisasa. Ni wajibu wa watendaji wakuu wa bunge kujua hali na matatizo mbalimbali ya kisaikolojia ya watu waliochini yao na jinsi ya kuwasaidia. Haitoshi tu kupigiwa simu na kulitangazia bunge fulani ni mgonjwa.Ilipashwa spika na katibu wajue maendeleo ya mbunge Amina kila kukicha, huu ndio wajibu wa kiongozi au mtendaji wa taasisi yeyote ya kileo ukizingatia tuko katika serikali iliyokuja na kauli mbiu: Ari Mpya na Nguvu Mpya na Kasi Mpya.Hapa taasisi ya bunge ninashawishika kuilamu kwa kuuliza: Je spika na katibu mlimsaidiaje mbunge Amina?Je bunge letu lina idara ya kutoa ushauri nasaha?

Labda nikumbushe kuwa Amina ni kielelezo cha mbunge ambaye anathubutu kusema jambo ambalo viongozi wetu wengi hawako tayari kusema kwa woga na pia labda maslahi wanayopata huko.Unafiki utailetea balaa nchi hii siku za usoni, kwani nakumbuka miaka miwili iliyopita aliuawa kule nchini Uganda Makamu wa Rais wa Sudan, John Garang, kwa ajali ya ndege ambayo inaaminika ilipangwa. Lakini waandishi jasiri waliposema ukweli kuwa kulikuwepo namna Raisi Museveni aliwakamata na kusema wanahatarisha amani.

La ajabu wiki iliyopita, mke wa Garang mwenyewe kadai mumewe aliuawa na anataka uchunguzi haraka. Mama huyu alitumiwa na Rais Museveni wakati wa kampeni za uraisi kumpigia debe Museveni na kudai Museveni ni mtu safi ambaye anasaidia hata nchi jirani kama ilivyokuwa kwa mumewe.Unafiki ni hatari ila leo anasema anaamini mumewe aliuawa.Tufike mahali tuseme ukweli ndio tutajua na kuzuia mafioso ya watu fulani ambao wanafanya wapiga filimbi kama Amina wafunge midomo yao.

Kwangu inauma na ninaamini ni pigo hasa kwa akina mama wa Tanzania kwani hata wale jasiri kama Anne Kilango watafunga midomo yao sasa. Nashangazwa pia na vyombo vya habari havina vipindi vya mijadala kuhusu kifo kama hiki; navisihi vituo vya redio na Televisheni vipite mitaani kuonesha hisia halisi za watu wengi sio kutuwekea mahojiano na watu kama waziri mkuu, sijui meya wa Kinondoni na watu wengine kwenye serikali unadhani watasema nini kama si tu kutuambia Mungu kamtwa kwa sababu anampenda. Vyombo vya habari kwa mwendo huu wa kutokuwa na utamaduni wa kuhoji, nchi hii itaendelea kuwa juu ya watu mafioso.

Natia shaka uwezekano wa kuwekewa sumu hata kusababisha sukari mwilini kushindwa hata kudhibitiwa kidaktari. Kwanini uchunguzi usifanyike?Mbona serikali ya Uganda majuzi ilimpoteza pia kiongozi kijana na katibu mkuu wa wizara ya ulinzi ambaye alikuwa tishio kwa vigogo wengi na pia mtu wa karibu wa Museveni. Baada ya kupinga uwezekano wa kifo kuwa sumu sasa serikali ya Uganda imeamua kufanya uchunguzi. Kenya ulifanyika uchunguzi wa kifo cha Ouko ila sisi watu wanaondoka tunabaki kusema oh!Mungu kampenda kuliko sisi, Bwana ametwaa! Ujinga gani huu jamani? Inatia uchungu tusivyopenda kuchunguza. Tangu Kolimba, Mwaikambo na wengine ambao hawasemwi sana.
Tumekwisha watanzania, naomba nifunge hoja kwa kuomba maelezo ya taasisi ya Bunge na pia kifo hiki kichunguzwe. Mungu amlaze pema peponi, Amina.

Saturday, June 23, 2007

MACHUNGU YA LRA

Kama unataka kujua ubaya wa vita kule Uganda kaskazini basi msome huyu mama alivyoathiriwa na waasi wa LRA.
Museveni kaanza kubadilika, anathubutu sasa kuwakamata mawaziri wala rushwa ambao waliaminika kama wasioshikika(untouchable), je unajua kwanini?Wiki iliyopita jumuiya ya Afrika Mashariki imezipokea Rwanda na Burundi, je kuna manufaa?

Wednesday, June 20, 2007

RIO FERDINAND -KAMPALA

Rio Ferdinand wa Man United alikuwa Kampala wiki iliyopita kuona maendeleo ya kituo cha michezo ya vijana anachofadhili yeye na baba yake.Nimecheka kumsoma baba wa Ferdinand haiba yake.Uganda nayo yachemsha kuna hatari isifuzu kwenda Ghana.
Tunakumbushwa pia ni nini changamoto za jumuiya ya Afrika Mashariki?Pia je ni kweli juhudi zote za kuunda jumuiya ya Afrika Mashariki zitaondoa umasikini?
Pia serikali ya Sudan imeanza uchumguzi dhidi ya mauaji ya John Garang.

MALKIA WA UINGEREZA HATANG'ATWA NA MBU UGANDA NG'O!

Ama kweli tuna kazi Afrika, yaani Malkia wa Uingereza-Elizabeti atazuru Uganda na serikali imeanza juhudi kusafisha kwa kupulizia dawa maeneo ya karibu na atakapolala ili asijeambukizwa Malaria. Kumbe tunaweza zuia Malaria Afrika?
Vita dhidi ya Rushwa Uganda inaongozwa na mwanamama matata kwelikweli.Pendekezo ni kwamba waheshimiwa wetu wanapohusishwa na rushwa basi wajiuzulu.Soma pia mapendekezo ya nnini Uganda ifanye ili iepuke dhahama baada ya kugundua mafuta.

Friday, June 15, 2007

MAMBO?

Leo nimeona niwaoneshe hasa wabongo kwanini wanapenda sana tamthiliya za TV ambazo ni za muda mrefu?Alafu je ni sawa kwa mtu mwenye akili kubaki kimya au kuunga mkono uchaguzi wa Nigeria hivi majuzi?Pia hivi kweli Iddi Amin alikuwa hatari isemavyo?

Saturday, June 09, 2007

kumbuku

http://www.monitor.co.ug/score/score06092.php(Uganda prep)
http://www.monitor.co.ug/health/health06073.php(Madhara ya AC)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Iddi Amin)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Musevei speech)

Wednesday, June 06, 2007

Uganda Yashinda Nigeria

Mafuta yaligunduliwa Uganda, je nchi kuwa na mafuta ndio laana?Je kukuwa kwa China ni baraka Afrika?Leo nakumbushia pia juu ya Mayombo tena, huyu mtu alikuwa na mengi ya kueleza yasiyojulikana.Nigeria yashindwa.

Saturday, June 02, 2007

Soka

Kwanza nikumbushe tu kuwa watawala wetu wanafunga midomo a wananchi tusizungumze. Nilionehsha makala moja wiki mbili zilizopita lakini Ndesanjo akaniambia nimekosea viungo vyake.Nataka niseme sikukosea nadhani jamaa walifunga kiungo kisifanye kazi lakini alieandika yuko hapa kaandika ni kwanini nilitaka msome mjue uhuru wa habari unavyoogopwa.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.
Kwanza nikumbushe tu kuwa watawala wetu wanafunga midomo a wananchi tusizungumze. Nilionehsha makala moja wiki mbili zilizopita lakini Ndesanjo akaniambia nimekosea viungo vyake.Nataka niseme sikukosea nadhani jamaa walifunga kiungo kisifanye kazi lakini alieandika yuko hapa kaandika ni kwanini nilitaka msome mjue uhuru wa habari unavyoogopwa.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.

Wednesday, May 30, 2007

RUSHWA UGANDA

Inasemekana eti Serikali ya MU7 iliingia madarakani 1986 ikiwa na mawazo ya kimapinduzi ambayo sasa yanadaiwa yamepotea njia.Huko Uganda kashfa kubwa ya rushwa imesababisha mawaziri vigogo kuwwekwa ndani, ni kisa kinachofanana na kile cha mheshimiwa Dito kupewa dhamana kwa kesi ya mauaji.Kisa hiki ni mfano hai wa siasa za kulindana zinapofika ukingoni.

Monday, May 21, 2007

MAUAJI YA SUMU KWA WANASIASA

Sasa waganda wameanza kuuana kwa sumu, siasa si mchezo.Kama ulishasikia mwanasiasa anayeogopeka ndiye huyu Uganda.
Uganda ni nchi iliyojaa vifo visivyoelezeka.
Wale wajasiriamali
Leo kwa wale wanasikiliza BBC Swahili, basi kila mara utamsikia msemaji wa jeshi la Uganda,ni muwajibikaji na msomi wa kileo jeshini ambaye hakusita kuandika makala juu ya kifo cha yule askari aliyefariki majuzi bila woga au mficho, ndie huyu Meja Kulayige. Mwisho kuna kashfa kubwa ya fedha Uganda tena.

Saturday, May 12, 2007

Harusi za gharama muhimu?

Wale wanaooa je mnataka harusi ya gharama?

JANET MUSEVENI KATIKA KASHFA YA GLOBAL FUND

Nchi ya Uganda imeshuhudia kashfa kubwa ya wizi na matumizi mabaya ya fedha za wafadhili hasa zile za fuko maalum(Global Fund). Iliundwa tume kuchunguza na matokeo yake ni kwamba hata mke wa Rais anahusika.Ni kashfa kubwa kwani inawahusu askari jeshi wa vyeo vya juu ambao ni vigumu kwa Museveni kuwagusa.
Upande wa michezo, timu ya taifa ya soka hapa tayari inaanza maandalizi dhidi ya Nigeria.Tanzania kwa sasa maneno mengi juu uteuzi wa timu hapa chama cha soka kimejipanga vizuri sana.Kwenye mambo ya kisiasa zaidi hebu soma juu ya ule msemo wa kiingereza usemao: Like Father like.....

Saturday, May 05, 2007

WIKI HII UGANDA

Ni vyema tuanze na juu ya nini chanzo cha kifo cha Brigedia maarufu na kijana aliyefariki Uganda siku za karibuni manake inadaiwa labda ni sumu.
Tuachane na kifo na tuendelee na siasa juu ya utawla bora.
Na mwisho eti mtoto wa Iddi Amin kaanzisha wavuti kuweka kumbukumbu za baba yake. Ila kama watu wanafikiri JK wa bongo ni rais wa karibu na watu Museveni ndio usiseme kwani ana kawaida ya kutembelea vyombo vya habari yaani redio za FM na kufanya malumbano ya simu na wtu kdhaa.

NOBLE MAYOMBO-ASKARI SHUJAA UGANDA

NEWS




Uganda mwanzoni mwa wiki hii ilimpoteza askari, mpiganaji na msomi mahiri kabisa.Noble Mayombo ni wazi alikuwa ni kati ya vijana wanaoaminiwa sana na Rais Museveni.Jamaa kafariki baada ya kuugua ghafla na inasemekana huenda kategewa sumu.Pia ni kwamba alikuwa kati ya maafisa wanaoeneza utawala wa ubabe wa Museveni na sumu yake katika ukanda mzima wa maziwa makuu.
Ni wazi alikuwa na maadui wengi saana na alikuwa na msimamo thabiti dhidi ya wapinzani akiamini mateso(torture) kama njia muafaka dhidi ya wahalifu na wapinzani kama Kiiza Besigye.Licha ya uaskari alikuwa pia ni katibu mkuu wa wizara ya ulinzi.Mengi yatasemwa lakini kashaondoka ila lazima tumkumbuke, kwani jamaa wengine wanadai hivi mashujaa tunawakumbukaje?
Jamaa kaagwa kiana yaani mwili wake kuwekwa Bungeni, mie nauliza hivi shujaa kama huyu mbona hajulikani njee ya Uganda?Mie kama msikilizaji wa redio za Uganda niliwahi kumsikia akifanya malumbano na pia nukuhu kadhaa zinamwonesha kama mtu mwenye kujidai sana; na kweli nadhani alikuwa mahiri japo nafikiri alikuwa akitetea tu utawala.
Jamaa kama kawaida mtu akifa, mkewe kamsifia kweli!
Andrew Mwenda ni mwandishi maarufu wa habari Uganda anamwelezeaje huyu bwana?Pia kifo hiki kinatukumbusha ni nini maana ya maisha.
Mwisho yuko Mhindi anatukumbusha juu ya umuhimu wa wahindi katika uchumi wa afrika.

Saturday, April 28, 2007

Thursday, April 26, 2007

UTAWALA WA KIBOKO UGANDA

Makamu wa Rais wa Uganda bado anaandamwa na kashfa ya uzinzi. Uganda imeanzisha kikosi maalum: KIBOKO SQUAD kutokana na kuongezeka kwa fujo na maandamano kila kukicha dhidi ya maamuzi dhalimu ya serikali.Watu wanachapwa viboko wakijaribu kuandamana.
Uganda pia wiki iliyopita yule bondia maarufu wa nchi hilyo alirefjea nchini humo.

Baada ya uchaguzi kule Nigeria Raila Odinga wa Kenya anaeleza woga wake juu ya nguvu kubwa alizzonazo Rais wanchi na athari zake za uchaguzi ujao.

SAYARI NYINGINE KAMA DUNIA

Wanasayansi wamegundua sayari mpya inayoaminika ina maisha ya viumbe hai kama dunia. Huko Uganda pia yuko jamaa mmoja mchungaji mwenye kipaji kwelikweli, mjue Sempa.
Nigeria imempata Rais mpya kwa uchaguzi uliolalamikiwa sana, je nini kitarajiwe?

Raisi Museveni wa Uganda kasababisha sakata kubwa la uuzaji wa msitu wa asili kwa Wahindi.Hebu tuujue undani wa tatizo hili la MABIRA FOREST kwa dhati.Wengine wamependekeza kuwe na MAPINDUZI YA SUKARI.Iko pia barua ya wazi kwa rais Museveni kutoka kwa mwananchi wa kawaida.Yapo maoni ya Mhindi juu ya dhahama hili na anajaribu kufananisha na hali ya wakat wa Iddi Amin.Mwingine katupa kanuni ya kubalansi mazingira na uchumi bila athari.

Tuesday, April 10, 2007

UZINZI HALALI UGANDA?-MAHAKAMA

Museveni hatimaye kaanza kuzungumzia mipango ya kuondoka.
Mahakama ya Uganda imefafanua juu ya sheria ya ukahaba au uzinzi kwa mwanamke na mwanaume, hata hivyo bado akina mama wengi wa Kampala wanataka talaka waachane na mabwana zao.Amanya Mushega, katibu mkuu wa EAC wa zamani anazungumzia juu ya utawala bora. Hotuba yake inatoa historia ya siasa za Uganda.
Ule msitu wa Mabira ni kielelezo cha rushwa nchini Uganda kwa miongo mingi anasema Andrew Mwenda.

Saturday, April 07, 2007

MZUKA WA IDD AMIN BADO

Watu wanamjua Iddi Amin kama mtu mnyama kuwahi kutokea Afrika. Lakini ni lazima tumtizame huyu bwana kwa undani hasa kuwa hata waliomfuatia ni wanyama pia, je unajua kwanini? Tunaambiwa eti serikali ya Museveni ni tishio kwa wapinzani kama alivyokuwa Idi Amin.
Amanya Mushega alikuwa katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki, yeye anapinga kuuzwa kwa msitu wa Mabira. Tunakumbushwa jinsi vyama vya siasa visivyo na nidhamu. Na je nini chanzo cha matatizo ya Afrika, Museveni alishasema ila leo hii anavunja aliyowahi kunena.

HERI YA PASAKA

Ni Pasaka hivyo hatuna budi kujua sikukuu hii husheherekewa vipi na jamii mbalimbali duniani?
Huko Uganda bado kasheshe la uuzaji wa msitu wa Mabira linaendelea.Limesababisha mfalme wa kabila la Baganda Ronald Mutebi kuja juu na kukataa uuzaji huo ndani ya Mahakama ya Kikatiba ya Uganda.Hii inasababishwa pia na tishio la hali ya hewa kuchafuka duniani. Wanasiasa ni watu wa ajabu kwelikweli, Museveni aliwahi kusema atalinda mazingira lakini leo hii anayabomoa kwa kuuza msitu huu.
Ujumbe wa pasaka eti Mbeki.

Tuesday, March 27, 2007

MAKAMU WA RAIS UGANDA NA HAWARA!

Ms NAKKU, Prof. BUKENYA AND THE MAFI
Zile harakati za kutia nyongo harakati za Makamu wa Rais wa Uganda ili asimrithi Museveni zinaendelea, hapa kajitokeza Mwanamama mmoja na kudai eti yeye mke wa pili wa Profesa Bukenya.
Haya yote ni kule kuonesha kuwa viongozi wetu na jamii kwa ujumla kuna tatizo la kimaadili. Zaidi ya maadili pia eti kuna maadui wa Bukenya wanataka kumuangusha. Yeye anadai eti ni mafia ndani ya serikali, je ni kweli?
Tunalojiuliza ni hivi kweli atapona na kashfa hii huyu bwana?Na je kuna uwezekano wa Mganda kuwa Raisi?

SIASA ZIMBABWE SAWA NA UGANDA?

Hali ya kisiasa ya Zimbabwe inalinganishwa na Uganda kwa kiasi fulani.Je Waingereza wajinyonge atakavyo Mugabe? Wiki hii Bunge ndani ya harakati za Jenet Museveni,(mke wa rais) lilizima juhudi za kumjadili na kumlaani Mugabe.
Museveni naye inasemekana anao mawaziri ambao hawatakaa waachishwe nyadhifa zao.Tunakumbushwa pia umuhimu wa nidhamu katika siasa.
Mwisho hebu tujisomee kwanini demokrasia imeichafua Afrika kwa sana? Andrew Mwenda, ni mwandishi maarufu na makini ana mengi ya kutuambia. Ndio maana Museveni anadaiwa kuwa kibaraka wa Bush huko Somalia.

Monday, March 26, 2007

NINA WASIWASI KAMA TUTAKWENDA GHANA.

Nilisema juzi kuwa tutafungwa na kweli tulifungwa. Sina hakika kama tutafuzu kwani ninahakika kibarua ni kigumu kwa hali ya mchezo ilivyokuwa juzi ni kwamba sisi tuko kwenye ligi ya kiwango kingine kabisa na wapinzani wetu Senegali au Burkinafaso.
Leo nataka nieleze hisia zangu kwa jinsi nilivyotizama mechi ile. Kwanza kabisa sina matatizo na kocha Marcio Maximo japo nashangazwa ni kwanini aliamua wachazaji wetu wacheze kwa kutafuta ushindi na si kujihami ugenini siku ile kitu ambacho kiliwachosha sana na tukafungwa.Magoli yote yalisababishwa na mapungufu ya walinzi wetu. Tangu mwamuzi Mourad kuanzisha mechi, ndani ya dakika tatu za mwanzo tayari Senegali walipata kona ambayo nadhani mlinsa lango wetu angetakiwa azuie mpira ule usitoke lakini kwasababu azijuazo yeye aliuacha mpira utoke huku akijua ingekuwa kona. Wachezaji wetu lazime waelewe kona ni goli kwa wazoefu kama Senegali nadhani.
Nawapongeza Taifa Stars kwa dakika thelathini za mwanzo ila baada ya hapo pumzi ziliwaisha kabisa. Vijana wakawa wazito kuziba nafasi hasa sehemu ya kiungo na mzigo ukabaki kwa ngome kuelemewa na ndiyo maana hata makosa yalikuwa ni lazima kwa wachezaji wa nyuma kwani walikuwa wakiucheza mpira muda mwingi.Ndipo dakika ya 87 jamaa wakapata kona; sijui kama wenzetu wanajufunza kulinda lango wakati wa kona. Goli la kwanza lilitokea hapa kwa kichwa cha Mamadou Niang. Sitaki kuhoji kwanini mchezaji yule aachwe kupiga kichwa huru ila nadhani kama nguzo ya goli ya upand wa kushoto kungekuwa na mtu basi angeokoa mpira ule kirahisi.
Sielewi nahodha, Mecky Mexime, aliyetakiwa kuwa pale alikuwa wapi kwani hata kona nyingine iliyofuata katika dakika ya 44 pia nguzo ya kushoto ilikuwa tupu. Kwa ujumla kipindi cha kwanza tulijitahidi sana kwani angalau Abdi Kassim aliweza angalau kupiga shutu moja zuri langoni mwa Senegali na pia Mwaikimba na Said Maulidi(SMG) walikuwa wakipasiana vizuri japo Smg alikuwa na tatizo la uzubaifu wa kurejea pazi za mbadilishano(return). Mapungufu mawili yalikuwa ni: moja, mipira ya kurusha tulishindwa kuitumia kabisa. Sielewi kwanini hatukuwa tunarusha mipira mirefu langoni mwa adui. Pili, kiungo chetu kilichezwa na wachezaji wadogo kiumbo ambao wasingeweza kumudu maumbo makubwa na kimo kirefu cha viungo wa Senegali kama tulivyoona.
Mara kadhaa niliona Nizar Khalfan akijaribu kukokota mpira kama vile anacheza chandimu mchangani. Ni lazima Maximo afundishe wachezaji wetu watumbue eneo la katikati ndilo linaloamua mechi. Wenzetu wanajipanga kwa eneo lenye ukubwa fulani hivyo kupenya si rahisi kwani wanaziba matundu yote katikati huku wakisaidiwa na uwezo wao mkubwa wa kuteleza na kuzuia kwa nguvu wakitumia ulizaji vibuyu(tackling) wa nguvu za ajabu.Ni vigumu kiungo chetu kingetamba siku ile. Ningependekeza Maximo aanzishe mfumo wa kutumia kiungo wa mbele ya walinzi(defensive shield) kule Brazil wanamuita "Burukutu" na awe ni mtu mwenye nguvu na mapafu haswa. Nasema hivi kwani siku ile niliona viungo wote wanacheza kama walinzi na hakuna aliyekuwa akichezesha kuunganisha washambuliaji.
Hapa napenda nipingane kabisa na Zamoyoni Mogella alipokuwa akichambua medhi ile runingani alipotupilia mbali kuwa umbo si hoja.Umbo ni kigezo hasa kwa wachezaji wa kiungo cha kati katika mpira wa kileo kwani hawa ni watu wanatakiwa kuwa na nguvu nyingi na uwezo mkubwa wa kuzunguka eneo kubwa la kati hadi mbele(zones).Nimshauri kabisa Maximo, kuwa kuna haja ya kusaka wachezaji warefu wenye nguvu wa eneo la katikati kama kweli tunataka kwenda Ghana.Hawa wapo sio lazima watoke Simba au Yanga.Wapo mikoani na wana uwezo wa kufundishika kiufundi.Nikumbushe kuwa mchezaji wa zamani wa Ushirika ya Moshi na Yanga, Willy Martin alitokea namna hii, mwanzoni akiwa mtu goigoi tu kimpira lakini Dan Koroso alimpika na akaja kuwa mahiri ajabu.
Sasa niendelee na kipindi cha pili cha mechi ile ya jumamosi: kilianza kwa mabao ya haraka haraka. Goli la pili la Diomasy Kamara ni magoli wanayofungwa wadosi katika ligi za ulaya kama Charlton, Wartford na hata West Ham siku hizi. Mara nyingi yanakuwa makosa ya mabeki wasioelewa vizuri. Nilifikiri mabeki wetu walikuwa bado hawajajua nini kinatokea kiwanjani, ilinishangaza sana. Ni makosa ambayo mpira wa kimataifa hutakiwi kuyafayanya kabisa.
Dakika mbili baadaye, Niang alifunga japo alinawa lakini refa hakuona ila mabeki wetu walionekana kumuacha Niang acheze wakinyanyua mikono kwa refa kama walivyozoea hapa Bongo. Ushamba wa mpira wa ridhaa ulijionesha wazi kwani filimbi haijalia wewe unatakiwa ucheze mpira.Ni mambo ya kujifunza haya kwa wachezaji wetu hasa wanapokuwa ugenini kwani wakumbuke mara nyingine huenda refa kalishwa mlungula dhidi ya wageni.
Goli la nne katika dakika ya 61 lilisababishwa na uzembe wa Nsajigwa ambaye hakuruhusiwa kupanda mbele siku hiyo kwani aliwekewa winga teleza ambaye hakumpa mwanya wa kupanda na plani nzima ya Taifa Stars ikaingia mtimanyongo.Nsajigwa alijaribu kumpiga chenga msenegali na akakosea na ndipo krosi ikatumwa na Niang akaunganisha kwa kichwa cha nguvu baada ya kumzidi kipa Ivo aliyetoka vizuri na kuchelewa. Ila hapa pia lazima niwalaumu walinzi wetu jpale kipa alipotoka hakuna mtu alibakia nyuma yake kulinda lango.
Kuanzia hapa nilitaraji goli la tano lakini Mungu akaweka mkono kwani Wasenegali walikuwa wanatutega tuende mbele watushtukize jambo ambalo halikufanikiwa.Nilimwonea huruma Maximo wakati Costa anapiga chenga alafu akanyang'anywa manake Maximo alishika kichwa akijua tumekwisha. Kwa ujumla Senegali walitumia 3-5-2 na sisi sikuona 4-4-2 ila muda mwingi ilikuwa5-3-2 kitu ambacho ingekuwa vigumu kupata bao na pia kufungwa japo pia tulifungwa. Hii nadhani ilisababisha viungo wetu wazidiwe na viungo wengi wa Senegali. Na hivyo mpira kuchezwa na mabeki kwa muda mrefu hali iliyosababisha wafanye makosa mengi. Kimsingi nafasi ya Ghana bado ipo ila Maximo afanye kazi kwenye ufundi(technique) hasa kiungo na pia ningependa tuone wanaitwa vijana kadhaa wapya wenye mbio kali katika wingi zote mbili. Pia ninataka Maximo atafute mchezaji wa mguu wa kushoto kucheza beki ya kushoto kwani siamini Mecky anafaa nafasi ile; hana spidi na hajui kulinda ipasavyo.

Saturday, March 24, 2007

TAIFA STARS NADHANI TUTAFUNGWA LEO

Nianze na huu mchuano wa leo kati ya Taifa Stars na Senegali. Maoni yangu ni kwamba haddi wakati naandika makala hii nadhani Senegali wana nafasi ya kushinda: uzoefu, vipaji vilivyoiva,mbinu bora na ufundi mwingi pamoja na uenyeji.Hizi ndizo sifa zinazonifanya niamini watatufunga angalau mabao matatu bila majibu.
Timu yetu itategemea ngome na golikipa angalau tupate sare. Ni wazi kwenye kiungo patatuangusha kama hatutakuwa makini na ufungaji sitaki kusema chochote kwani sioni kama kuna mtu atakayeweza kufunga japo kidogo labda Saidi Maulid na mkongwe
Nigusie pia habari za siasa wiki hii Komredi Mugabe anaanza kudondoka ni wazi siku zake zinahesabika; pia huko Uganda wanasiasa wameamua kuuza msitu maarufu na muhimu wa Mabira japo yuko mfalme wa Buganda kaamua kuipa serikali ardhi ili isiuze.
Uganda bado inabakia ni nchi yenye waasi wengi, hebu wajue.

Saturday, March 17, 2007

AFYA ZETU TWAZIJALI?

Kabla ya kuangalia afya hebu tuone Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anasemaje juu ya muungano huu?Na ni jinsi gani majeshi ya Uganda yana umuhimu huiko Somalia?
Leo tuangalie afya, hasa juu ya mambo ambayo wengine twafikiri ni urembo kumbe liipo jambo hasa kwa wanawake ambao hawatakiwi kuvaa mini skirt.Pia je kutoa mimba sawa?Pia ni jinsi gani kusevu pesa kunawezekana?
Siasa je unajua ile report ya tatizo la PRA?Maajabu ya maadili kwenda likizo, hata Mufti Mkuu mdanganyifu?Ni vizuri pia tujue wanasiasa maarufu wana historia gani?
Mwisho juu ya wazazi wetu, je kuna haja ya kuwajali?

Saturday, March 10, 2007

MAJAJI WAMALIZA MGOMO

Baada ya ile sinema ya Iddi Amin kushinda Oscar, hali ya kisiasa nchini Uganda inaonesha wazi sinema nyingine tayari imeanza kutengenezwa. Kwanza soma ni vipi mwanaye Iddi Amin alivyomfahamu baba yake?Imeshangaza sana hata majaji wanaweza kugoma.Unaambiwa mgomo umekuwa na athari zake kwelikweli. Waganda inabidi waje tena MOSHI kwa majadiliano upya.
Ni vizuri tujue kasheshe lililosababisha majaji kugoma Uganda na ni jinsi gani demokrasia imechafuliwa?
Mwisho ni hii simu mpya ya I Pod.

Wednesday, March 07, 2007

HATA MAJAJI WANAGOMA UGANDA?

Uganda inaongozwa kwa miujiza ya Mungu kwa mujibu wa Museveni. Athari zake ni kama ifuatavyo: moja, majaji wamegoma kwani wamechoka kuingiliwa na serikali na pia hata mawakili(wanasheria) nao wamejiunga na mgomo wa kuidhalilisha taasisi ya mahakama.Museveni ndiye atakayekuwa rais wa kwanza wa jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini haya ya kutuma askari kuingilia maamuzi ya majaji tuyararajie?
Tunaambiwa hakuna utumwa wa hali ya juu kama ule wa kuwa na Rais mmoja kwa muda mrefu. Uganda kama Tanzania inafanya kila juhudi kukandamiza haki ya kupata habari.
Jambo moja linachekesha Museveni ameisifia sana ile sinema ya Iddi Amin iliyoshinda Oscar majuzi, je unajua kwanini?Yanayotokea uganda yanatakiwa kuepushwa ni aibu.Uganda na nchi nyingine Afrika zimebakia hakuna maelewana kati ya serikali na wapinzani.
Tuje mambo ya Makerere, na pia tuone ni jinsi gani wanawake wamefanikiwa kisiasa? Pia nini kinakwamisha mazungumzo ya LRA Uganda?

Wednesday, February 21, 2007

LEO SIASA ZA UGANDA

Uganda ina siasa mbili: ya nchi na ya Jadi ambayo sasa kuna waka moto huko Lubiri.
Kuna fununu Makamu wa Rais wa Uganda atang'olewa madarakani.Je inawezekana?na je ni nani huyu Profesa Bukenya? Yeye mwenyewe kaamua kuwa ngangari na anasema haendi kokote, je hili tishio kwa Museveni na ndio maana anamng'oa kwani kwa Uganda, kuna imani kuwa mtu wa kabila la BUGANDA hawezi kuwa rais kamwe kwani hiki ni cheo cha watu wa anakotokea Museveni tu: Mashariki.
Kuna maoni juu ya filamu ya Iddi Amin; na pia unajua uwongo wa picha hiyo?

Saturday, February 17, 2007

UASI NI RUKSA--KANALI BESYIGYE

Kanali Besigye bado anaendeleza tambo zake za kumng'oa Museveni. Hapa anafikia hatua ya kuhalalisha uasi kama njia halali ya kujipatia madaraka. Alafu mjue shujaa wa Uganda.

WANASIASA NI FEDHULI KULIKO NYANI

Tabia za mwanasiasa yeyote hazina ukweli wala uaminifu, inasemekana wanasiasa ni wadhalimu kuliko hata nyani.
Bado mammbo ya Rwanda nayaona kama kizungumkuti. Ninapata hisia labda akina Kagame wanamsingizia tu mke wa Habyarimana. Sina imani kuwa kuna chuki za magharibi dhidi ya Rwanda.
Museveni ni bingwa wa siasa kwa kuweza kuchanganya siasa na utawala wa kifalme kufanya kazi bila matatizo.Lakini pia zipo gharama za kuzuia matatizo yaliyotarajiwa mfano haya.
Huwa napenda KANDANDA pia;eti meneja wa Chelsea anadai watatwaa ubingwa, je inawezekana?
Kwa wale makapera kama mie: je kuna ulazima wa kuoa?

Wednesday, February 14, 2007

ETI LEO NI SIKUKUU YA VALENTINE?

Wakati nikiwa masomoni Uganda nilijifunza juu ya Demokrasia na mhadhiri wangu kaandika juu alichotufunza gazetini kuhusu siasa za Uganda hasa juu ya majadiliano yasiyokwisha. Hapa anajibiwa na mwandishi eti kakosea. Mjadala unaendelea juu ya siasa haswa. Jua siri ya serikali ya Rwanda kuhusu matumizi bora ya magari ya serikali.Huko Uganda kuna mgogoro bungeni juu ya kuyaruhusu majeshi ya nchi hiyo yaende ama la nchini Somalia. Wapinzani wamegomea bunge kwani hawataki majeshi yande Somalia kitendo kinachoonekana ni kuiunga mkono serikali bila kujijua; je ni kwanini?
Hili ni la muhimu sana juu ya kufungiwa hivi majuzi kwa kituo kipya cha televisheni-NTV-kwani ni juhudi za udhibiti wa vyombo vya habari Afrika Mashariki kama zile za kudhibiti wanaharakati kama HAKI ELIMU nchini Tanzania.Lakini pia tunakumbushwa ipo mijpaka ya kusema na kuandika hasa kwa vyombo vya habari-THE FOURTH STATE.

WIZI WA MITIHANI UGANDA

Wakati nchini Tanzania tuna wabunge na mawaziri wenye tuhuma nzito za kudanganya juu ya masomo au shahada zao huko nchini Uganda wabunge hawako tayari kufanya hayo ama kuruhusu watu kuiba mitihani. Wanachukua hatua inapobidi.
Soma juu ya jinsi siasa ulivyo mchezo wa kufanyiziana: kuanzia Afrika mpaka India na hata Ulaya. Ni mchezo mchafu sana ninavyoamini. Pia niliwahi kuandika juu ya Profesa Mamdani akitusihi Wabongo tuachane na mikopo ya kusoma chuo kikuu, leo kaja na makala nyingine juuu ya hili. Na mwisho kafunga mjadala wa elimu chuo kikuu.
Pia ni vipi ilivyo muhimu kusaidia Wasomalia: unajua PAN Africanism?

Saturday, February 10, 2007

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE--2006

Eti waafrika ni watu wasiweza kuendelea hata wafanye nini, je ni kweli?
Kuhusu elimu huu ndio msimu wa wale wa shule kufurahia mavuno yao.Matokeo ya mwaka huu ni haya hapa.
Pia je unajua kuonesha uwazi wa sehemu zako ni makosa hadharani?
Wakati Wabunge wa Uganda wanabishana juu ya kupeleka askari huko somalia inasemekana ni faida kwa Uganda.\\Pia ni kwawaida kwa walarushwa kulindana, kama uliwahi kusikia kashfa kubwa ya waziri wa Uganda sasa kaula, kapewa tenda na rafikie Museveni.

Thursday, February 01, 2007

JINSI MAJESHI YA BONGO YALIVYOWATIA KIZUIZINI WAGANDA TZ.

Ninapenda sana mambo ya uhusiano yanavyochambuliwa na wengine hebu soma hili.Je unajua mambo ambayo watanzania wengi hatuyajui wakati wa vita ya Iddi Amin?
Unamjua bingwa wa uandishi habari aliyekufa?
Unapaswa kujua pia yuko Rais wa nchi moja ya Afrika(Guinea) bado yuko kwenye zile zama za kung'ang'ania madaraka.Pia soma juu ya jinsi vyama tawala, au vyama dola kama CCM vinavyofanya katiba ya nchi kama mali yao.
Hili ni la muhimu sana kujua juu ya Uganda manake baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana wapinzani walilalamika mahakamani na majaji wa mahakama kuu wakatoa uamuzi kuwa Museveni alikuwa mshindi halali.Jua ni kwanini majaji walitoa uamuzi huo,
Pia ni vyema usome uamuzi wao ulisemaeje?
Soma pia ni jinsi gani bara letu Afrika lilivyo na wabunge ghali sana juu ya uwezo wa nchi.Pia huko Uganda eti ubinafsishaji umegeuka kuwa kama ugaidi.
Pia tunakumbushwa ni kwanini hatuna sababu ya kukumbuka siku ya uhuryu wa nchi zetu?Alafu mwisho kabisa:SOMA JUU YA BLOOD DIAMOND, sinema ambayo inaelezea juu ya umafia ulivyokithiri Afrika.

Wednesday, January 03, 2007

FUNGUA MWAKA 2007

Mwaka 2006 umemalizika na makala kadhaa ambazo zimegusia ni jinsi gani ulimwengu wetu ulivyo na changamoto. Kifo cha Saddam pia kimegusa hisia za wengi na hasa jinsi udikteta mpya ulivyozaliwa na kinyongo hiki cha dikteta. Hata waliokuwa wanamtetea inasemekana serikali ya sasa inawatisha sana.
Mwaka mpya ni wakati wa kugusia juu ya taasisi za kiserikali zinavyopaswa kufanya kazi hasa Afrika Mashariki. Pia tujifunze zaidi nini mchango wa China katika uchumi wa Afrika?
Pia ni vizuri tujifunze juu ya changamoto za SACCOS.

Friday, December 22, 2006

MASLAHI YA NCHI NI ZAIDI YA SIASA NA HISIA ZA WATU

Unaposikia tofauti kati ya siasa na maslahi ya nchi mfano mzuri uko hapa kwenye maziwa makuu.
Pia kuna hili la kalenda ya uendeshaji wa ligi ya soka.
Pia huko Kenya rais Kibaki atakuwa Mombasa kama kawa.

Thursday, December 21, 2006

HAKUNA HAJA YA MIKOPO ELIMU YA JUU-PROF: MAAMDANI

Wakati wabongo tunalia na JK kuhusu mikopo ya elimu ya juu, yule profesa maaarufu, Maamdani kachapisha kitabu akisema eti serikali isilipie ila wote tulipie elimu

Tuesday, December 19, 2006

JK NA JINAMIZI LA CCM NDANI YA MWAKA MMOJA IKULU

JK sasa anaanza kuona ukweli halisi wa bongo kuwa tatizo liko kwenye CCM. Hili ni jinamizi ambalo JK ana kazi ngumu kuliondoa manake ncchi imeoza na itagharimu Taifa sana kuweza kuondoa hayo ambayo JK kakemea jana.

SALAM ZA CHRISTMAS

Tunasherehekia Krismas soma jinsi makasisi wa dini mbalimbali(mapadiri na wachungaji na mashehe pia) walivyobadilika siku hizi na tunakkumbushwa je Yesu wa wakristu angezaliwa leo ingekuwaje Afrika?Alafu nataka uone ni jinsi gani wabunge wa Afrika hasa Uganda walivyo na ulafi na mapenzi na MABENZI na si wananchi, yaani wanatishia serikali pale inapotaka kuwakata usawa.
Mwisho, ona jinsi Jaji Kiongozi Uganda hisia zake juu ya utawala bora.Alafu mkuu wa Jeshi la polisi Uganda naye anaamua kumjibu na kumkosoa ikibidi Jaji Kiongozi, patamu hapa.
Alafu wajue watu kumi waliotingisha Uganda mwaka huu.

Friday, December 15, 2006

MKE WA MUSEVENI KATIKA UGOMVI KUMTETEA MUMEWE

Mke wa rais Museveni ambaye ni mbunge jana inasemekana karushiana maneno makali na mwanamama mmoja wa shoka wa chama cha upinzani katika kile kinachoonekana kutetea rekodi mbovu ya mumewe ndani ya bunge.
Alafu unajua kwanini maprofesa wa Makerere wamegoma? Soma haya.

Wednesday, December 13, 2006

UDIKTETA-SIRI YA KUISHI MUDA MREFU

Eti madikteta hawafi mapema, tunahimizwa tuwe majitu korofi na dhalimu ili tuishi muda mrefu.

Thursday, December 07, 2006

JK AIGE KUTOKA KWA CALDERON WA MEXICO

Kama kweli Tanzania inapenda maendeleo tunahitaji kiongozi kama huyu aliyechaguliwa huko Mexico majuzi. JK angekuwa namna hii na akatekeleza basi tunaweza kufanikisha "Maisha bora kwa kila Mtanzania".
Vinginevyo JK anatania tu.

UHURU BONGO--BONGE LA PATI SAWA AU DHIHAKA?

Kama mtanzania sina budi kujumuika na watanzania wenzangu kuadhimisha siku hii ya miaka 45 ya uhuru wa Tanzania bara(Tanganyika).Huu ni wajibu wa mzalendo yeyote kutathmini je uhuru wetu umeleta tija kwa watanzania wote au kwa kukundi fulani ndani ya jamii tu?Sisherehekei manake kwa hali ilivyo si muafaka kwa hili bali ni wakati wa kujiuliza kwa nini tunaendelea kuharibu uchumi wetu namna hii?Sherehe tuwaachie wanaoona matunda ya uhuru kama akina JK na Ngoyai: hawa kwao hakuna tatizo la umeme, maji wala usafiri au barabara mbovu. Kwao wanazo njia mbadala kutatua haya.
Nimefuatilia sherehe za uhuru leo kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) kwani wakati ndio sherehe inaanza hawa jamaa wa Tanesco wakakata umeme alafu ikaw ndio mwisho wa kuangalia Runinga yangu.Matanzgazo ya RTD hayasikiki vizuri nashangaa kwanini RTD wasiweke mtambo wa FM manake hizi FM radio nyingi ni muziki kwa kwenda mbele utadhani siku ya leo ni sawa na zingine. Ni Radio Free Afrika ya Mwanza na Sauti ya Injili ya Moshi angalau leo wamekuwa na vipindi kuwahoji watu ambao walihusika na uhuru wetu wakati ule na wametoa mawazo murua kweli. Nakwambia tukio hili hapa Moshi si la muhimu kama siku ya jumapili au sikukuu ya Idd El Fitri kwani siku hizo umeme ni bwerere.Hasira imenishika kwani baada ya sherehe kumalizika hawa jamaa wanawasha umeme, nakwambia Tanesco hapa Moshi hawajui uhuru kabisa. Hayo tuyaache, ila JK hotuba yake ilikuwa nzuri nampongeza sana. Ila aliangalia tu mafanikio nchi iliyojipatia tu tangu 1961, ameacha kuzungumzia matatizo kama haya ya Umeme.

Nami naona nieleze kwa ufupi japo ninafikiri nini siku hii:

Mtizamo wangu unatia wasiwasi sana kama kweli tumefikia mafanikio ya dhati kulingana na kipindi cha miaka 45. Naanza na sekta ya barabara tumefeli kabisa. Bado hatujaweza kuunganisha nchi yetu kwani tunalazimika kupitia Kenya kusafiri kutoka Arusha kwenda Mwanza, Bukoba au hata Kampala.

Pili bado tunakumbwa na njaa kila mwaka ilihali tuna ardhi, mito kibao kuwezesha kilimo cha umwagiliaji. Ukija kwenye maji ndio usiseme kabisa. Hakuna maji kunywa ya kutosha hata katika miji kama Dar es salaam, Arusha na hata Mwanza.
Huwezi kuamini nchi yenye umri wa miaka 45, haina umeme wa kuaminika na kutosha angalau mautmizi ya majumbani achilia mbali viwandani. Viongozi, yaani wanasiasa hawana utashi wowote kwa maendeleo ya jumla ya nchi. Maslahi binafsi yamewekwa mbele kuliko uzalendo: kwa mfano, nchi inagenishwa kwa kubadilishana/bei poa kati ya watu fulani ndani ya tabaka tawala(elites) na si kwa maslahi ya mtu.
Ukija kwa watunga sheria(Wabunge) ndio basi tena. Bunge limekuwa jamvi la kila mtu siku hizi hata wendawazimu au kwa maana nyingine mbumbumbu kielimu nionavyo kutokana na matendo yao.Elimu si tija kwa mtu kuwa mbunge au diwani. Nidio maana bunge letu ni taasisi ya kubariki mambo yasiyo na maslahi kwa Taifa ila Chama(CCM) na yale ya binafsi. Chama tawala kimelimeza bunge na kutupeleka kuzimu kiuchumi. Tumefika mahali mtu akiheshimu taaluma katika kusimamia au kuamua mambo ya kiuchumi na mengine ya msingi kama hayo anaonekana mwehu na si mwenzetu. Hii ndio miaka 45 ya uhuru tunayosherehekea. Hili ni lazima tulitafakari la sivyo uhuru unakuwa hauna maana.
Kwa robo mwaka sasa nchi iko gizani, hakuna umeme na viongozi na wahusika wetu hawajali kabisa. Ufisadi na kulindana ndio umetufikisha hapa tulipo na viongozi wahujumu hawaguswi bali wanahamishwa kutoka idara au wizara moja hadi nyingine kuendeleza uharibifu. Vipaumbele vyetu ni vile visivyo; viongozi wetu wamebakia kusafiri kutembeza bakuli kwa wafadhili na kuhimiza uwekezaji katika nchi isiyokuwa na umeme wa kuaminika bila aibu. Kiongozi mkuu anadiriki kusema tatizo la umeme limerithiwa kutoka serikali iliyopita bila kung'amua alikuweko ndani ya serikali hiyo.
Kisiasa, nchi imebaki hoi kabisa; vyama vya upinzani viko hoi kabisa na havionekani kuchukua hatua madhubuti kutia changamoto kwa CCM inavyoboronga. Haya yakiendelea, CCM chini ya Makamba imebakia kuwarubuni wapinzani makini kurejea CCM kama ndio kipaumbele. CCM haitaki changamoto, kwake kuwa mpinzani ni uadui, si uzalendo kwa nchi. Kweli hapa hatutaelewa wapi tunakosea kama tutaendelea hivi na ndio maana bado tuko nyuma maeneo mengi. Demokrasia yetu ni kama vile "maonesho kwa wafadhili"(show-off) na sio demokrasia ya dhati.
Viongozi wetu kama vile Lowasa na Makamba wanaongoza kwa sera kongwe za kihafidhina. Hili ni tatizo la viongozi ndani ya chama tawala, serikalini na hata vyama vya upinzani. Tunahitaji kizazi kipya cha uongozi nadhani ili tuendelee. Hata hivyo, kama Taifa tumefanikiwa kubaki na umoja wa kitaifa kitu muhimu kwa nchi yeyote.
Amani tuliyonayo ni lazima tuikuze kwa kuziunda upya taasisi za kidemokrasia katika utawala ili muongo ujao tupige hatua kwa haraka na si kama miaka hii 45 iliyopita. Katiba ni lazima iangaliwe upya ili miundo ya mihimili mitatu ya dola ifanye kazi inavyopaswa kwa uhuru na si kama sasa kwa kulinda maslahi ya chama tawala. Hii imefanya kwa mfano bunge letu kubaki kama muhuri wa udhalimu "rubber stamp" wa serikali mara kwa mara.
Mwisho, ingawa wenzetu wa magharibi iliwachukua muda mrefu kufikia mafanikio ya demokrasia, sisi isiwe kisingizio, kwani dunia ya leo mambo yamerahisishwa ni lazima tuendelee haraka. Nitoe rai: Tuna wasomi wengi wa kila aina Tanzania ila wote wamefungwa jela ya nafsi zao(conscience) na wamekuwa bendera fuata upepo(sycophants) mbele ya wanasiasa wa chama tawala. Ujasiri unahitajika kwa wasomi wa nchi hii la sivyo kama nchi tutaendelea kusherehekea uhuru wa wachache kama tunavyofanya leo hii. Kwani mantiki ya nchi huru sidhani ina maana kwa watanzania wengi wa kama kule vijijini pembezoni mwa nchi hii. Na kwa akina JK, Ngoyai na Makamba: kumbukeni turuhusu changamoto ndani ya chama na hata serikalini kwani ikiwa tutafanya hivyo hatutaona mikataba ya kijinga kama hii ya IPTL, Richmond, Usiri wa biashara ya mihadarati na mengine mengi ambayo hayasemwi kwa kuogopa kumkosoa bwana mkubwa.

Wednesday, December 06, 2006

KAGAME-MUNGU MTU- ASHTAKIWE TU

Naiangalia hali ya Rwanda kama ni tatizo ambalo waafrika hatuwezi kulitatua kwani kihistoria ni vigumu. Sina imani sana na mahakama ya Arusha kwani naiona kama mahakama iliyoundwa na washindi wa vita(RPF) ili kuwahukumu washindwa.
Ndipo hapa ninapokuwa ninamuunga mkono huyu jaji wa kifaransa kutaka pia Kagame ashtakiwe. Sidhani kuna suluhisho la kiafrika, ila naunga mkono juu ya nia ya mficho ya Ufaransa katika sakata hili. Pia nionavyo tutarajie Rwanda yenye matatizo sana hapo baadaye kwani Kagame inasemekana ni kiongozi Mungu mtu.Tatizo letu waafrika ni kutokupenda kusema ukweli na kama tutaendelea na uwongo huu wa Kagame hakuna maridhiano Rwanda.
Lakini pia ni lazima tujue pande zote mbili zilihusikaje katika kile kinachoitwa ukombozi wa Rwanda?Kwa mfano, picha halisi ya ushiriki wa Kagame na Habyarimana unaweza kuisoma na kupata hali halisi hasa hii makala ambayo mwandishi anao uelewa sana wa mambo ya Rwanda.

Tuesday, December 05, 2006

BESIGYE ALIVYOMNYANG'ANYA MUSEVENI MKE

Pamoja na kufuatilia habari za wanasiasa kadhaa ni vyema pia wakati mwingine tujue habari zao binafsi. Leo nataka nieleze habari za kiumbea ambazo niliwahi kuzisikia juu ya Museveni, Kiiza Besyige na huyu mwanamke wa chuma(iron lady) Bi Winnie Byanyima.
Inasemekana ugomvi kati ya Museveni na Besigye pia unachangiwa na kuibiana mabibi. Eti Bi. Byanyima awali alikuwa ni mtu wa karibu sana wa Museveni wakati wa vita ya msituni. Wakati huo Besigye akiwa kama daktari wa Museveni. Leo hii Bi. Byanyima ni mke wa Besyigye japo nakumbuka niliwahi kumsikia akihojiwa na redio moja Kampala na akadai kuwa eti Besigye ni mshirika wake tu(companion).
Wambeya wanadai eti siku waasi wa Museveni(NRA)wanaiteka na kuitwa Kampala, waliingia Kampala huku gari alilokuwemo Museveni likiendeshwa na Bibie huyu.
Hayo yote tisa, kumi leo hii Dr. Besigye kaamua kuyaanika yote yaliyojiri kule msituni na ni jinsi gani walikutana na bibie huyu.
Kama kawaida, Uganda ni nchi iliyojaa visa vya kisiasa vya kiume kweli si kama Tanzania, soma huyu mpinzani madhila aliyokwishapitia.

RAIS NA GAVANA UGANDA--WAWAKAMUA WALIPAKODI KWA BIASHARA BINAFSI

Mimi ni kati ya wasioamini adhabu ya kifo hata kama mtu kafanya nini. Ila nimeshangazwa sana na nchini Uganda hata katiba inaruhusu kama ilivyo pia kwetu Tanzania. Lingine ni hili la Rais Museveni na gavana wa benki kuu wameamua kutumia pesa za wali pakodi kumsaidia mfanyabiashara mmoja asifilisike.Ila inasemekana huyo mfanyabishara ni jamaa tu anasimamia shughuli za mzee.
Kama kawaida yangu napenda sana kujua inakuwaje watu wengine wanafanikiwa kimaisha wangali wadogo?

Monday, November 27, 2006

MJUE GENERAL SALEH WA UGANDA

Leo nataka watu musome juu ya jamaa ambaye anajulikana kama shujaa hapa Uganda na ambaye ndie aliyesababisha kuanguka kwa serikali ya Obote.

Wednesday, November 22, 2006

MGAO WA UMEME UGANDA NI MIAKA MITATU SASA JE BONGO?

Huku tukiwa tunalaumu wanasiasa wetu juu ya labda hujuma au rushwa juu ya matatizo ya umeme nchini Tanzania kwa sasa, huko Uganda mgao wa umeme umekuweko kwa miaka mitatu sasa na ahadi kama hizi za hapa Bongo ni kawaida.
Mgao umeendelea hata pale serikali ya Uganda ilipobinafsisha shirika la Umeme kwa jamaa wale wa Afrika kusini kama tulivyofanya sisi.
Pia msome jinsi Museveni na Besyige walivyofanana.

Saturday, November 18, 2006

NIMEKOSA MKUTANO

Wanaglobu nilijaribu kuingia ukumbini mambo yakashindikana na hivyo nikakosa kikao, inasikitisha sana.
Bassi leo nikasoma haya:Soma zaidi juu ya historia ya mtu mweusi, je kalaaniwa na Mungu? Pia hebu tujue zaidi ni kwa vipi chama tawala nchini Uganda kinavyoruhusu demokrasia?
Alafu huyyu jamaa namzimia kweli kashinda tuzo ya UN.

Friday, November 17, 2006

JOJI KICHAKA ANASAIDIWA NA BABA YAKE

Baba yake Joji Kichaka karudi kumkomboa mwanaye.pIA soma jinsi mpanga mikakati wa Bush alivyochemsha.

Thursday, November 16, 2006

UKIMWI, MADEREVA WALEVI-FAIDA KWA UCHUMI

Leo nawapa vituko vya jamaa mmoja mcheshi kwelikweli. Eti anadai Ukimwi ni dili kwa bara la Afrika na ukiangamizwa, bara letu halitapata misaada.Alafu anaongeza zaidi kwamba uendeshaji magari wakati mtu ni mlevi ni faida kwa uchumi wa nchi.

KUPINDISHA HABARI(SPIN) KUNA MWISHO WAKE

Yuko jamaa mmoja alikuwa ni mwandishi mpambe haswa wa Raisi Museveni. Nakwambia alijua kazi yake haswa ya kupindisha habari (spin).Inasemekana ukweli umemsuta kaachana na Museveni sasa.
Ukiacha mambo ya habari tuangalie ni kwanini wanafunzi wanagoma haswa kule Makerere?Leo pia niwaletee hadithi juu ya mapambano ya msituni wakati Museveni alipozimia vitani kama inavyoelezewa na Dk. Kiiza Besyige aliyekuwa daktari wa Museveni. Alafu ni jinsi gani ukabila ulichangia kuuawa kwa waheshimiwa kadhaa hapa Uganda wakati ule wa vita kila kukicha.

Wednesday, November 08, 2006

OMBAOMBA WA AFRIKA CHINA

Eti marais wa afrika kule China walikuwa makini au ombaomba tu?Alafu huko China tunaambiwa Museveni alifanya mambo ya kihistoria.Wakati Tanzania tumemaliza kipindi cha jeshi letu la polisi kupoteza mwelekeo kutokana na Kamanda wa polisi wa hovyo, huko Uganda hebu msome IGP wa kule ni mtu gani na umfananishe na alipita kwetu "MAHITA".
Alafu kuhusu dini kuna wanaoamini watu weusi tumelaaniwa na Mungu. Ila huyu anakataa katakata.Pia kama mtu wa ukanda huu wa afrika, je jumuiya yetu tuianze?
Mwisho waafrika eti tumezidi kupenda watoto wadogo visivyo?

KUWAJIBIKA TANZANIA MPAKA UTOE ROHO YA MTU--JK

Hapa Tanzania wanasema "hapa ndipo patamu" yaani Anko Dito, naye yuko maabusu baada ya kutuhumiwa kuua raia mwema.Natizama tukio hili kama dhihirisho la wanasiasa wamangimeza wa kiafrika. Ulevi wa ukubwa unamfanya mtu kujichukulia madaraka mikononi mwake, kwani atafanywa nini?
Dito, ni mzalendo wa hali ya juu ninavyofikiri ndio maana JK hata aliweza kumpa madaraka.Ni kati ya vigogo wasioshikika nchi hii naweza kusema"untouchable".Ndio maaana nina wasiwasi sidhani kama atapatikana na hatia baada ya sheria kufuata mkondo wake.
Jana kasifiwa eti kujiuzulu ni kitendo bora kutokana na tuhuma anazokabiliana nazo. Kauli ya JK katika kukubali kujiuzulu kwake imenifanya nipate swali moja kwa wanaglobu wote: JE NI MPAKA MTU ATUHUMIWE KUTOA ROHO YA MWANANCHI MWENZAKE NDIO ANAJIUZULU? Nauliza hivi kwani hivi majuzi wako wakuu wa wilaya: HAWA NGULUME na Mheshimiwa fulani SABAYA wanatuhumiwa kupiga wananchi makofi na vyombo vya habari vimeamua kulamba miguu na kutovalia njuga ukiukaji huu wa haki za binadamu.
Yuko pia muheshimiwa mpendwa sana, POMBE MAGUFULI, tayari ana tuhuma kibao za ukiukaji wa maadili ya kazi, naye pia rais haoni kuna haja ya kumuwajibisha.
Tukiendelea hivi tutafika? Au mpaka mtu aue tu ndio tutawajibika?Wanablog mnasemaje hapa?

Saturday, October 28, 2006

ETI MKAPA AANZE KUPOKEA TUZO YA UTAWALA BORA?

Wengi nadhani Tumesikia eti Maraisi wa Afrika sasa watapewa zawadi kama watatawala kwa ubora.
Jamaa huko Uganda kapendeza eti Mkapa apewe tuzo hiyo kama kifuta jasho.

Friday, October 27, 2006

NILICHOSOMA

Yuko bibie Kampala hapa inaelezwa ni wanaume wenye sifa zipi watamfaa?
Kisiasa, kuna kitabu juu ya udanganyifu wa Marekani hapa duniani.

MAMBO YA JAMII LEO

Napenda Chuo hiki cha elimu ya juu Nkozi University. Kuna jamaa kaoa ndugu yake wa damu, yaani dada yake.Ulishasikia haya? Wanawake wa Uganda na malove.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.

MAMBO YA JAMII LEO

Napenda Chuo hiki cha elimu ya juu Nkozi University. Kuna jamaa kaoa ndugu yake wa damu, yaani dada yake.Ulishasikia haya? Wanawake wa Uganda na malove.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.

Sunday, October 15, 2006

Saturday, October 14, 2006

HANA MFANO

Nyerere haenziwi kabisa.Je tunajua asili ya waafrika ni wapi?
Alafu wale wanaoanza gemu la penzi, unajua ya muhimu hapo awali?Kwa wanaume je twajua akina mama na dada siku hizi wanapennda sana pesa?
Huu ni wasifu wa mtu ninayemhusudu sana.

Friday, October 13, 2006

UGANDA NA SALA ZA KILOKOLE

Yuko Jaji Mmoja maarufu nchini Uganda ambaye anakerwa sana na wanasiasa wa nchi hii. Basi katunga shairi babu kubwa juu ya uzandiki wa wanasiasa wa Uganda.
Kituko kingine cha wanasiasa ni tabia ya akina Museveni na mkewe kupenda kuhudhuria sala za kilokole kuiombea nchi kitu kinachoonekana hakina msaada wowote kwa nchi.Sala inaonekana ni ulevi wa wanasiasa.
Je wajua kuwa soko huria ndio balaa kuu la umasikini uliokithiri Africa? Alafu gazeti la serikali Uganda, hatimaye lamfukuza kazi meneja wake mzungu.

KUMBUKUMBU YA OBOTE BAADA YA MWAKA.

Hii ni wiki kubwa sana ya kuwakumbuka waasisi wa Afrika Mashariki. Kwanza jana imekuwa siku ya kumkumbuka Milton Obote, rais wa kwanza wa Uganda. Mkewe kaongea juu ya mumewe hasa ni yapi yanayomfanya amkumbuke.Obote kama binadamu anazo pande mbili hebu zisome:Pia ujue hivi ni upi mchango wa Obote katika siasa za Uganda na Afrika na alikuwa ni mtu wa aina gani?
Ukiacha kumbukumbu, huko Uganda baraza la mawaziri wanakosoana sio kama hapa kwetu Tanzania tunaoneana aibu na kufunika kombe mwanaharamu apite.Pia Uganda tunakumbushwa kuwa panapokuwa na amani sana basi ujue haki hakuna kabisa.
Mambo ya mahusiano, je una mpango wa kuchumbia siku za karibuni?Mwisho soma juu ya wanamuziki wa Uganda.

Saturday, October 07, 2006

WABUNGE WA UGANDA NA MAGARI YA KIFAHARI

La msingi kabisa ni Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kuna mpango umeandaliwa wa kukusanya maoni ya watu.Je ni sahihi kuutekeleza?
Leo soma haya ya wabunge wa Uganda wamehongwa na serikali yao. Wale wapenda kandanda soma uone ni timu gani angalau zinahisiwa kushinda kombe la mabingwa.
Alafu inaaminika eti Waafrika tumelaaniwa:

Friday, October 06, 2006

Eti JK kadhihakiwa?

Kuna ile katuni ambayo serikali pamoja na wanahabari wa TZ wanadai ni dhihaka kwa JK na watanzania kwa ujumla.
Eti siasa Uganda ni ndege iliyo safarini, itafika. Alafu jisomee ujichekee vituko vya vigogo wa Uganda.

Wednesday, October 04, 2006

Leo

Kuna watu na mafanikio yao pamoja na malengo.Ili kupambana na ukimwi tunaambiwa eti jibu ni ABC je hili kweli?
Pia unapoona vichaa wengi siku hizi ni dalili za umasikini eti.

Sunday, September 10, 2006

LEO NI SIASA CONGO NA UGANDA

Mambo ya kupambana na rushwa sio mcezo, hapa kuna njia mbadala zinapendekezwa. Pia magari ya wabunge ni ulaji mtupu wa vigogo nchini Uganda, je umasikini utakwisha kweli? Hili la kushangaza manake inasemekana si Kabila wala Bemba anayestahili kugombea urais nchini Jamhuri ya kidmokrasia ya Congo. Si Congo tu ila eti hata Uganda sasa iko chini ya serikali ya maharamia, unajua?
Alafu kuna mtu kasema "Ushoga na Ufirauni" haukubaliki Afrika. Alafu soma ilivyo ngumu kuzuia uvunjaji wa haki za binadamu serikalini.

Thursday, September 07, 2006

KUHAMAHAMA VYAMA SIASA

Kwa wale wanasiasa uchwara ambao hawaishi kuhamahama vyama basi hii ya kule Uganda ndio funzo. Jamaa alikuwa mkuu wa majeshi lakini sasa ndie kati ya wapinzani wakuu na hana mpango wa kurejea chama tawala. Alafu sisi watanzania tunafikiri ni Mkapa tu kauza nchi yetu kule Uganda Museveni pia kagenisha na wazawa hawana chao.
Pia ona jinsi Maadili yalivyoshuka na kuathiri jammi za kiafrika.

Wednesday, August 30, 2006

SIKU YA GLOBU DUNIANI

Kesho ni siku ya blogu duniani. Nimerudi nyumbani Tanzania hivi karibuni na kwa sasa ninajaribu kutulia na kufuatilia hali huku nikijizatiti kutafuta kazi ya kufanya. Kazi ni shida sana kupata kama hauna baba au mjomba na akina shangazi serikalini au hata katika taasisi za binafsi. Lililopo mbele yangu ni kujiajiri mwenyewe nadhani niko sahihi.
Katika siku hii sina raha kabisa na ninaisikitikia Tanzania hasa katika sekta ya habari kwani hakuna majadiliano ya maana sana katika magazeti na redio zetu. Inaonekana ari mpya na nguvu mpya imeturudisha katika enzi za "Zidumu fikra za Mwenyekiti wa Chama cha........". Habari nyingi hapa ni kusifia utendaji wa wanasiasa na kutokuwakosoa kabisa.
Redio za FM kibao lakini wao dili ni kupiga mziki, vipindi vya majadiliano sio sana ila kama unataka ukweli kuhusu nchi hii soma globu. Tatizo ni watanzania wachache wanasoma globu.
Ziko globu tano ambazo nadhani ni bora kwangu na ningependa watu wasizikose kabisa: kwanza, ni hii ya Mpiga Picha Issa Michuzi ambapo tukio kuhusu Tanzania utalipata hata kama hauko nyumbani utafurahi sana na pia kwa kumbukumbu zote za nchi zipo. Pili ni Pambazuka kwani utapata habari kiuchambuzi na kiyakinifu kuhusu mauzauza yote ya wataanzania haswa wanasiasa na viongozi wake. Alafu kuna Miruko, yeye bwana anazungumza ukweli bila uficho, si mwoga kama walivyo watanzania wengi.Huyu si bendera fuata upepo.Blogu ya nne ni Kasri la Mwanazuoni, hapa huwa napata habari za upande ambao hutapata magazetini wala redioni.Huyu bwana ni kiboko huwa napenda nimsome tu. Mwisho kabisa ni globu kutoka Nigeria, hapa kuna mijadala ya kusisimua sana.

Monday, August 28, 2006

MWISHONI MWA WIKI ILIYOKWISHA

Ukisikia serikali inapinga ukweli alafu anatokea mtu anaandika kujibu mapigo ndio haya ya Uganda.Kwenye kandanda wakati hatuna mechi yeyote ya kujipima nguvu Uganda itacheza na wapinzani wetu Burkinafaso. Matokeo wametoka sare, nasikia Tanzania tulimtuma mtu akapeleleze, sijui itakuwaje jumamosi.
Kwenye siasa nako unajua kuna waafrika mawakala wa mabepari?Kama unamfahamu profesa Maamdani ambaye alimfunda pia raisi wetu JK basi soma anasemaje juu ya umuhimu wa elimu na vyuo vikuu katika nchi?Profesa mwingine, Ali Mazrui yeye ana mengi juu Jumuiya ya Afrika Mashariki, eti tunahitaji miaka mingine arobaini.Kuna haja ya Bunge la vyama vya upinzani kuwa na malengo au visheni, je Uganda wanalo bunge la aina hii?Si hayya tu, ila huu ung'ang'anizi wa Museveni madarakani una uhusiano sana na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pia mapigano yamesimamishwa na waasi wa Uganda rasmi, je ni nani shujaa katika dhahama hili la miongo miwili?
Uchaguzi wa Congo DRC utatoa rais ambaye ana maslahi tofauti kwa Uganda awe Kabila au Bemba.
Huko Burundi kama kawaida jamaa wameanza kufungana jela eti watnataka kupinduana.Huku Jumuiya ya Afrika mashariki ikisuasua
Kama unataka kujua jinsi ya kuwa tajiri na kuishi raha mustarehe bila kukopakopa.
Mambo ya akina mama pia tunakumbushwa ni jinsi gani wanafurahia mabwana jua siri

Friday, August 25, 2006

FAMILIA YA MUSEVENI YAIFANYA NCHI MALI YAKE

Vituko vya marais wa Afrika ni vingi. Nchini Uganda, Museveni naye hakosi vituko hasa vya matumizi makubwa ya fedha.Andrew Mwenda anao uelewa wa ni nani hasa ni Museveni na jinsi familia ya rais huyo inavyoiibia nchi hiyo.
Imeripotiwa pia eti ili Kony aweze kumalizwa huko misitu ya Congo basi serikali ya Uganda iilipe Congo gharama ya uporaji iliyoufanya miaka kadhaa iliyopita.
Pia tunakumbushwa tusiogope ukosefu wa ajira kwani kuna namna ya kuishi bila kuajiriwa. Pia tunaambiwa kumbe hata maaskofu wa kikatoliki na makadinali wanastaafu.
Katika siasa, NRM kama mfano wa vyama tawala vinahitaji kitu kinaitwa Matangi ya Kufikiri--think tank. Pia nchini Uganda ni vizuri tumsome na kumjua afisa mmoja wa jeshi Brigedia Jenerali Tumukunde ambaye katiwa kizuizini kwa muda sasa eti kajaribu kutikisa mkuu wa dola.
Nirudi kwenye mazungumzo ya amani huko Uganda, kauwawa kamanda wa LRA ambaye inasemekana na aliyemjua kuwa alikuwa mnyama haswa. Pia nigusie mambo ya ofisini haswa tabia ya mahusiano ya kijinsia na mabosi.
Kwenye kandanda je kuna tofauti kati ya makocha wa Ulaya na wa kwetu hapa Bongo?Pia suala la nidhamu kwenye timu za kandanda kama Taifa Stars.

Friday, August 18, 2006

MAMBO YA MSINGI

Unajua umuhimu wa michezo mashuleni? Unajua inasemekana Museveni ndio anaimaliza kabisa Uganda?
Ni vizuri pia tuelewe ni kwanini Wazungu wameamua kutunyonya kabisa. Mazungumzo ya Doha yamevunjika, kwanini lakini?

YA WIKI HII

Kuna tabia ya kuhamahama kutoka upinzani kwenda chama tawala. Alafu nchini Uganda, Raisi pekee anatumia mamilioni ya shilingi kulipa washauri wake ambao ni wengi lukuki. Soma simulizi la mwandishi maarufu nchini Uganda alipokuwa lupango.
Nchini Uganda rushwa ndio haswa, je unajua wataalam wanaeleza rushwa ni nini? Je Raisi anaweza tu kuamua kufanya ziara binafsi?

Saturday, August 12, 2006

LEO

Kuna hili la ufisadi Uganda alafu eti siasa ni mbaya kwa maendeleo. Pia unamjua Kony alivyo sasa?Alafu ona jinsi matajiri wanavyoneemeka na elimu bora Ugaanda.
Yuko jamaa anatabiri Chelsea kushinda tena taji msimu huu.Na kwa wale kapera kama mie, tunahitaji wapanga sherehe za harusi?

Friday, August 04, 2006

YALIYONIVUTIA LEO

Wakati bado timu yetu haijaanza maandallizi ya kwenda huko Ghana mwaka 2008, Uganda tayari kocha waao kaanza mambo. Tunaambiwa hata sex inataka maadili fulani yazingatiwe, unazijua?
Kuhusu politiki ni kuwa Museveni kaishiwa hana hela, rushwa imezidi na sasa chama tawala kinabidi kifunge shughuli katika ngazi za chini. Athari za Chama dola ndio hizi. Nikiwa kama bachela mzoefu basi mambo ya mapishi ni vyema niyapitie.
Angalia ukubwa wa Afrika ulivyo, hapa rais anapopita anaweza akasababisha hata mauaji.Alafu ligi ya Uingereza ndio inakaribia.
Kama unamjua Joseph Kony pata undani wa maisha yake ya sasa. Je ilikuwaje Mapinduzi yakatokea Uganda?

Saturday, July 15, 2006

SALA KUONDOA RUSHWA?

Kweli sala na mafungo ndio dawa ya Rushwa?Pia mambo ya imani yapo kweli?Na siasa mwanzo wake je?
Mpira huu ni mwaka wa Chelsea tena?Je kashfa kubwa mpirani?

Friday, July 14, 2006

KONY ATAELEWEKA?

Mambo ya Kony?

UGANDA KUNASEMAJE?

Baada ya kimya kirefu leo niangaze yanayojiri nchini Uganda: kuna huyu bwana anatuhumiwa kuuwa mkewe. Katika kesi yake anaonekana kujiamini sana kitu kinachowashangaza wengi. Alafu kama ilivyo kawaida, siku hizi tunawaza pesa tu haswa wengi wetu. Matokeo yake hata kazi zetu kwa mfano wachapishaji wa magazeti maadili ya kazi yameshuka sana. Pia nchi ya Uganda inatamani kuwa na mafuta lakini inakumbushwa kuwa hiyo ni balaa kwa Afrika na ni hatari kwa demokrasia.
Baada ya kombe la dunia hebu tujue ni nini kinasemwa pia kuhusu kosa la Zidane? Alafu kuna Padri wa Kikatoliki uzalendo umemshinda na kaamua kuvunja sheriia za useja. Pia tunakumbushwa juu ya ongezeko la ugonjwa wa moyo. Nini kifanyike?
Mwisho vipi kuhusu Kony?

Thursday, June 08, 2006

VIROJA KATIKA VIAPO UGANDA

Hebu ona jinsi mawaziri wapya walivyoonesha manjonjo wakati wakiapishwa wiki iliyopita.Pia unaweza ukasoma uswahiba kati ya mmojawapo wa mawaziri walioteuliwa na Museveni hivi majuzi.