Hii ni globu iliyovumbuliwa nchini Uganda inajaribu kukazia matumizi ya lugha ya kiswahili na kuhabarishana kuhusu maswala mbalimbali ya kijamii hasa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kat na kwingineko. Siasa na mambo ya michezo na kijamii kwa ujumla ndio itakayokuwa mada kuu hapa.Nitakaribisha maoni yenu.
My Blog List
Friday, June 15, 2007
MAMBO?
Leo nimeona niwaoneshe hasa wabongo kwanini wanapenda sana tamthiliya za TV ambazo ni za muda mrefu?Alafu je ni sawa kwa mtu mwenye akili kubaki kimya au kuunga mkono uchaguzi wa Nigeria hivi majuzi?Pia hivi kweli Iddi Amin alikuwa hatari isemavyo?
Saturday, June 09, 2007
kumbuku
http://www.monitor.co.ug/score/score06092.php(Uganda prep)
http://www.monitor.co.ug/health/health06073.php(Madhara ya AC)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Iddi Amin)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Musevei speech)
http://www.monitor.co.ug/health/health06073.php(Madhara ya AC)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Iddi Amin)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Musevei speech)
Wednesday, June 06, 2007
Uganda Yashinda Nigeria
Mafuta yaligunduliwa Uganda, je nchi kuwa na mafuta ndio laana?Je kukuwa kwa China ni baraka Afrika?Leo nakumbushia pia juu ya Mayombo tena, huyu mtu alikuwa na mengi ya kueleza yasiyojulikana.Nigeria yashindwa.
Saturday, June 02, 2007
Soka
Kwanza nikumbushe tu kuwa watawala wetu wanafunga midomo a wananchi tusizungumze. Nilionehsha makala moja wiki mbili zilizopita lakini Ndesanjo akaniambia nimekosea viungo vyake.Nataka niseme sikukosea nadhani jamaa walifunga kiungo kisifanye kazi lakini alieandika yuko hapa kaandika ni kwanini nilitaka msome mjue uhuru wa habari unavyoogopwa.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.
Kwanza nikumbushe tu kuwa watawala wetu wanafunga midomo a wananchi tusizungumze. Nilionehsha makala moja wiki mbili zilizopita lakini Ndesanjo akaniambia nimekosea viungo vyake.Nataka niseme sikukosea nadhani jamaa walifunga kiungo kisifanye kazi lakini alieandika yuko hapa kaandika ni kwanini nilitaka msome mjue uhuru wa habari unavyoogopwa.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.
Wednesday, May 30, 2007
RUSHWA UGANDA
Inasemekana eti Serikali ya MU7 iliingia madarakani 1986 ikiwa na mawazo ya kimapinduzi ambayo sasa yanadaiwa yamepotea njia.Huko Uganda kashfa kubwa ya rushwa imesababisha mawaziri vigogo kuwwekwa ndani, ni kisa kinachofanana na kile cha mheshimiwa Dito kupewa dhamana kwa kesi ya mauaji.Kisa hiki ni mfano hai wa siasa za kulindana zinapofika ukingoni.
Monday, May 21, 2007
MAUAJI YA SUMU KWA WANASIASA
Sasa waganda wameanza kuuana kwa sumu, siasa si mchezo.Kama ulishasikia mwanasiasa anayeogopeka ndiye huyu Uganda.
Uganda ni nchi iliyojaa vifo visivyoelezeka.
Wale wajasiriamali
Leo kwa wale wanasikiliza BBC Swahili, basi kila mara utamsikia msemaji wa jeshi la Uganda,ni muwajibikaji na msomi wa kileo jeshini ambaye hakusita kuandika makala juu ya kifo cha yule askari aliyefariki majuzi bila woga au mficho, ndie huyu Meja Kulayige. Mwisho kuna kashfa kubwa ya fedha Uganda tena.
Uganda ni nchi iliyojaa vifo visivyoelezeka.
Wale wajasiriamali
Leo kwa wale wanasikiliza BBC Swahili, basi kila mara utamsikia msemaji wa jeshi la Uganda,ni muwajibikaji na msomi wa kileo jeshini ambaye hakusita kuandika makala juu ya kifo cha yule askari aliyefariki majuzi bila woga au mficho, ndie huyu Meja Kulayige. Mwisho kuna kashfa kubwa ya fedha Uganda tena.
Saturday, May 12, 2007
JANET MUSEVENI KATIKA KASHFA YA GLOBAL FUND
Nchi ya Uganda imeshuhudia kashfa kubwa ya wizi na matumizi mabaya ya fedha za wafadhili hasa zile za fuko maalum(Global Fund). Iliundwa tume kuchunguza na matokeo yake ni kwamba hata mke wa Rais anahusika.Ni kashfa kubwa kwani inawahusu askari jeshi wa vyeo vya juu ambao ni vigumu kwa Museveni kuwagusa.
Upande wa michezo, timu ya taifa ya soka hapa tayari inaanza maandalizi dhidi ya Nigeria.Tanzania kwa sasa maneno mengi juu uteuzi wa timu hapa chama cha soka kimejipanga vizuri sana.Kwenye mambo ya kisiasa zaidi hebu soma juu ya ule msemo wa kiingereza usemao: Like Father like.....
Upande wa michezo, timu ya taifa ya soka hapa tayari inaanza maandalizi dhidi ya Nigeria.Tanzania kwa sasa maneno mengi juu uteuzi wa timu hapa chama cha soka kimejipanga vizuri sana.Kwenye mambo ya kisiasa zaidi hebu soma juu ya ule msemo wa kiingereza usemao: Like Father like.....
Saturday, May 05, 2007
WIKI HII UGANDA
Ni vyema tuanze na juu ya nini chanzo cha kifo cha Brigedia maarufu na kijana aliyefariki Uganda siku za karibuni manake inadaiwa labda ni sumu.
Tuachane na kifo na tuendelee na siasa juu ya utawla bora.
Na mwisho eti mtoto wa Iddi Amin kaanzisha wavuti kuweka kumbukumbu za baba yake. Ila kama watu wanafikiri JK wa bongo ni rais wa karibu na watu Museveni ndio usiseme kwani ana kawaida ya kutembelea vyombo vya habari yaani redio za FM na kufanya malumbano ya simu na wtu kdhaa.
Tuachane na kifo na tuendelee na siasa juu ya utawla bora.
Na mwisho eti mtoto wa Iddi Amin kaanzisha wavuti kuweka kumbukumbu za baba yake. Ila kama watu wanafikiri JK wa bongo ni rais wa karibu na watu Museveni ndio usiseme kwani ana kawaida ya kutembelea vyombo vya habari yaani redio za FM na kufanya malumbano ya simu na wtu kdhaa.
NOBLE MAYOMBO-ASKARI SHUJAA UGANDA
| NEWS | |||||||
| |||||||
Uganda mwanzoni mwa wiki hii ilimpoteza askari, mpiganaji na msomi mahiri kabisa.Noble Mayombo ni wazi alikuwa ni kati ya vijana wanaoaminiwa sana na Rais Museveni.Jamaa kafariki baada ya kuugua ghafla na inasemekana huenda kategewa sumu.Pia ni kwamba alikuwa kati ya maafisa wanaoeneza utawala wa ubabe wa Museveni na sumu yake katika ukanda mzima wa maziwa makuu.
Ni wazi alikuwa na maadui wengi saana na alikuwa na msimamo thabiti dhidi ya wapinzani akiamini mateso(torture) kama njia muafaka dhidi ya wahalifu na wapinzani kama Kiiza Besigye.Licha ya uaskari alikuwa pia ni katibu mkuu wa wizara ya ulinzi.Mengi yatasemwa lakini kashaondoka ila lazima tumkumbuke, kwani jamaa wengine wanadai hivi mashujaa tunawakumbukaje?
Jamaa kaagwa kiana yaani mwili wake kuwekwa Bungeni, mie nauliza hivi shujaa kama huyu mbona hajulikani njee ya Uganda?Mie kama msikilizaji wa redio za Uganda niliwahi kumsikia akifanya malumbano na pia nukuhu kadhaa zinamwonesha kama mtu mwenye kujidai sana; na kweli nadhani alikuwa mahiri japo nafikiri alikuwa akitetea tu utawala.
Jamaa kama kawaida mtu akifa, mkewe kamsifia kweli!
Andrew Mwenda ni mwandishi maarufu wa habari Uganda anamwelezeaje huyu bwana?Pia kifo hiki kinatukumbusha ni nini maana ya maisha.
Mwisho yuko Mhindi anatukumbusha juu ya umuhimu wa wahindi katika uchumi wa afrika.
Saturday, April 28, 2007
Thursday, April 26, 2007
UTAWALA WA KIBOKO UGANDA
Makamu wa Rais wa Uganda bado anaandamwa na kashfa ya uzinzi. Uganda imeanzisha kikosi maalum: KIBOKO SQUAD kutokana na kuongezeka kwa fujo na maandamano kila kukicha dhidi ya maamuzi dhalimu ya serikali.Watu wanachapwa viboko wakijaribu kuandamana.
Uganda pia wiki iliyopita yule bondia maarufu wa nchi hilyo alirefjea nchini humo.
Baada ya uchaguzi kule Nigeria Raila Odinga wa Kenya anaeleza woga wake juu ya nguvu kubwa alizzonazo Rais wanchi na athari zake za uchaguzi ujao.
Uganda pia wiki iliyopita yule bondia maarufu wa nchi hilyo alirefjea nchini humo.
Baada ya uchaguzi kule Nigeria Raila Odinga wa Kenya anaeleza woga wake juu ya nguvu kubwa alizzonazo Rais wanchi na athari zake za uchaguzi ujao.
SAYARI NYINGINE KAMA DUNIA
Wanasayansi wamegundua sayari mpya inayoaminika ina maisha ya viumbe hai kama dunia. Huko Uganda pia yuko jamaa mmoja mchungaji mwenye kipaji kwelikweli, mjue Sempa.
Nigeria imempata Rais mpya kwa uchaguzi uliolalamikiwa sana, je nini kitarajiwe?
Raisi Museveni wa Uganda kasababisha sakata kubwa la uuzaji wa msitu wa asili kwa Wahindi.Hebu tuujue undani wa tatizo hili la MABIRA FOREST kwa dhati.Wengine wamependekeza kuwe na MAPINDUZI YA SUKARI.Iko pia barua ya wazi kwa rais Museveni kutoka kwa mwananchi wa kawaida.Yapo maoni ya Mhindi juu ya dhahama hili na anajaribu kufananisha na hali ya wakat wa Iddi Amin.Mwingine katupa kanuni ya kubalansi mazingira na uchumi bila athari.
Nigeria imempata Rais mpya kwa uchaguzi uliolalamikiwa sana, je nini kitarajiwe?
Raisi Museveni wa Uganda kasababisha sakata kubwa la uuzaji wa msitu wa asili kwa Wahindi.Hebu tuujue undani wa tatizo hili la MABIRA FOREST kwa dhati.Wengine wamependekeza kuwe na MAPINDUZI YA SUKARI.Iko pia barua ya wazi kwa rais Museveni kutoka kwa mwananchi wa kawaida.Yapo maoni ya Mhindi juu ya dhahama hili na anajaribu kufananisha na hali ya wakat wa Iddi Amin.Mwingine katupa kanuni ya kubalansi mazingira na uchumi bila athari.
Tuesday, April 10, 2007
UZINZI HALALI UGANDA?-MAHAKAMA
Museveni hatimaye kaanza kuzungumzia mipango ya kuondoka.
Mahakama ya Uganda imefafanua juu ya sheria ya ukahaba au uzinzi kwa mwanamke na mwanaume, hata hivyo bado akina mama wengi wa Kampala wanataka talaka waachane na mabwana zao.Amanya Mushega, katibu mkuu wa EAC wa zamani anazungumzia juu ya utawala bora. Hotuba yake inatoa historia ya siasa za Uganda.
Ule msitu wa Mabira ni kielelezo cha rushwa nchini Uganda kwa miongo mingi anasema Andrew Mwenda.
Mahakama ya Uganda imefafanua juu ya sheria ya ukahaba au uzinzi kwa mwanamke na mwanaume, hata hivyo bado akina mama wengi wa Kampala wanataka talaka waachane na mabwana zao.Amanya Mushega, katibu mkuu wa EAC wa zamani anazungumzia juu ya utawala bora. Hotuba yake inatoa historia ya siasa za Uganda.
Ule msitu wa Mabira ni kielelezo cha rushwa nchini Uganda kwa miongo mingi anasema Andrew Mwenda.
Saturday, April 07, 2007
MZUKA WA IDD AMIN BADO
Watu wanamjua Iddi Amin kama mtu mnyama kuwahi kutokea Afrika. Lakini ni lazima tumtizame huyu bwana kwa undani hasa kuwa hata waliomfuatia ni wanyama pia, je unajua kwanini? Tunaambiwa eti serikali ya Museveni ni tishio kwa wapinzani kama alivyokuwa Idi Amin.
Amanya Mushega alikuwa katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki, yeye anapinga kuuzwa kwa msitu wa Mabira. Tunakumbushwa jinsi vyama vya siasa visivyo na nidhamu. Na je nini chanzo cha matatizo ya Afrika, Museveni alishasema ila leo hii anavunja aliyowahi kunena.
Amanya Mushega alikuwa katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki, yeye anapinga kuuzwa kwa msitu wa Mabira. Tunakumbushwa jinsi vyama vya siasa visivyo na nidhamu. Na je nini chanzo cha matatizo ya Afrika, Museveni alishasema ila leo hii anavunja aliyowahi kunena.
HERI YA PASAKA
Ni Pasaka hivyo hatuna budi kujua sikukuu hii husheherekewa vipi na jamii mbalimbali duniani?
Huko Uganda bado kasheshe la uuzaji wa msitu wa Mabira linaendelea.Limesababisha mfalme wa kabila la Baganda Ronald Mutebi kuja juu na kukataa uuzaji huo ndani ya Mahakama ya Kikatiba ya Uganda.Hii inasababishwa pia na tishio la hali ya hewa kuchafuka duniani. Wanasiasa ni watu wa ajabu kwelikweli, Museveni aliwahi kusema atalinda mazingira lakini leo hii anayabomoa kwa kuuza msitu huu.
Ujumbe wa pasaka eti Mbeki.
Huko Uganda bado kasheshe la uuzaji wa msitu wa Mabira linaendelea.Limesababisha mfalme wa kabila la Baganda Ronald Mutebi kuja juu na kukataa uuzaji huo ndani ya Mahakama ya Kikatiba ya Uganda.Hii inasababishwa pia na tishio la hali ya hewa kuchafuka duniani. Wanasiasa ni watu wa ajabu kwelikweli, Museveni aliwahi kusema atalinda mazingira lakini leo hii anayabomoa kwa kuuza msitu huu.
Ujumbe wa pasaka eti Mbeki.
Tuesday, March 27, 2007
MAKAMU WA RAIS UGANDA NA HAWARA!
Zile harakati za kutia nyongo harakati za Makamu wa Rais wa Uganda ili asimrithi Museveni zinaendelea, hapa kajitokeza Mwanamama mmoja na kudai eti yeye mke wa pili wa Profesa Bukenya.
Haya yote ni kule kuonesha kuwa viongozi wetu na jamii kwa ujumla kuna tatizo la kimaadili. Zaidi ya maadili pia eti kuna maadui wa Bukenya wanataka kumuangusha. Yeye anadai eti ni mafia ndani ya serikali, je ni kweli?
Tunalojiuliza ni hivi kweli atapona na kashfa hii huyu bwana?Na je kuna uwezekano wa Mganda kuwa Raisi?
SIASA ZIMBABWE SAWA NA UGANDA?
Hali ya kisiasa ya Zimbabwe inalinganishwa na Uganda kwa kiasi fulani.Je Waingereza wajinyonge atakavyo Mugabe? Wiki hii Bunge ndani ya harakati za Jenet Museveni,(mke wa rais) lilizima juhudi za kumjadili na kumlaani Mugabe.
Museveni naye inasemekana anao mawaziri ambao hawatakaa waachishwe nyadhifa zao.Tunakumbushwa pia umuhimu wa nidhamu katika siasa.
Mwisho hebu tujisomee kwanini demokrasia imeichafua Afrika kwa sana? Andrew Mwenda, ni mwandishi maarufu na makini ana mengi ya kutuambia. Ndio maana Museveni anadaiwa kuwa kibaraka wa Bush huko Somalia.
Museveni naye inasemekana anao mawaziri ambao hawatakaa waachishwe nyadhifa zao.Tunakumbushwa pia umuhimu wa nidhamu katika siasa.
Mwisho hebu tujisomee kwanini demokrasia imeichafua Afrika kwa sana? Andrew Mwenda, ni mwandishi maarufu na makini ana mengi ya kutuambia. Ndio maana Museveni anadaiwa kuwa kibaraka wa Bush huko Somalia.
Monday, March 26, 2007
NINA WASIWASI KAMA TUTAKWENDA GHANA.
Nilisema juzi kuwa tutafungwa na kweli tulifungwa. Sina hakika kama tutafuzu kwani ninahakika kibarua ni kigumu kwa hali ya mchezo ilivyokuwa juzi ni kwamba sisi tuko kwenye ligi ya kiwango kingine kabisa na wapinzani wetu Senegali au Burkinafaso.
Leo nataka nieleze hisia zangu kwa jinsi nilivyotizama mechi ile. Kwanza kabisa sina matatizo na kocha Marcio Maximo japo nashangazwa ni kwanini aliamua wachazaji wetu wacheze kwa kutafuta ushindi na si kujihami ugenini siku ile kitu ambacho kiliwachosha sana na tukafungwa.Magoli yote yalisababishwa na mapungufu ya walinzi wetu. Tangu mwamuzi Mourad kuanzisha mechi, ndani ya dakika tatu za mwanzo tayari Senegali walipata kona ambayo nadhani mlinsa lango wetu angetakiwa azuie mpira ule usitoke lakini kwasababu azijuazo yeye aliuacha mpira utoke huku akijua ingekuwa kona. Wachezaji wetu lazime waelewe kona ni goli kwa wazoefu kama Senegali nadhani.
Nawapongeza Taifa Stars kwa dakika thelathini za mwanzo ila baada ya hapo pumzi ziliwaisha kabisa. Vijana wakawa wazito kuziba nafasi hasa sehemu ya kiungo na mzigo ukabaki kwa ngome kuelemewa na ndiyo maana hata makosa yalikuwa ni lazima kwa wachezaji wa nyuma kwani walikuwa wakiucheza mpira muda mwingi.Ndipo dakika ya 87 jamaa wakapata kona; sijui kama wenzetu wanajufunza kulinda lango wakati wa kona. Goli la kwanza lilitokea hapa kwa kichwa cha Mamadou Niang. Sitaki kuhoji kwanini mchezaji yule aachwe kupiga kichwa huru ila nadhani kama nguzo ya goli ya upand wa kushoto kungekuwa na mtu basi angeokoa mpira ule kirahisi.
Sielewi nahodha, Mecky Mexime, aliyetakiwa kuwa pale alikuwa wapi kwani hata kona nyingine iliyofuata katika dakika ya 44 pia nguzo ya kushoto ilikuwa tupu. Kwa ujumla kipindi cha kwanza tulijitahidi sana kwani angalau Abdi Kassim aliweza angalau kupiga shutu moja zuri langoni mwa Senegali na pia Mwaikimba na Said Maulidi(SMG) walikuwa wakipasiana vizuri japo Smg alikuwa na tatizo la uzubaifu wa kurejea pazi za mbadilishano(return). Mapungufu mawili yalikuwa ni: moja, mipira ya kurusha tulishindwa kuitumia kabisa. Sielewi kwanini hatukuwa tunarusha mipira mirefu langoni mwa adui. Pili, kiungo chetu kilichezwa na wachezaji wadogo kiumbo ambao wasingeweza kumudu maumbo makubwa na kimo kirefu cha viungo wa Senegali kama tulivyoona.
Mara kadhaa niliona Nizar Khalfan akijaribu kukokota mpira kama vile anacheza chandimu mchangani. Ni lazima Maximo afundishe wachezaji wetu watumbue eneo la katikati ndilo linaloamua mechi. Wenzetu wanajipanga kwa eneo lenye ukubwa fulani hivyo kupenya si rahisi kwani wanaziba matundu yote katikati huku wakisaidiwa na uwezo wao mkubwa wa kuteleza na kuzuia kwa nguvu wakitumia ulizaji vibuyu(tackling) wa nguvu za ajabu.Ni vigumu kiungo chetu kingetamba siku ile. Ningependekeza Maximo aanzishe mfumo wa kutumia kiungo wa mbele ya walinzi(defensive shield) kule Brazil wanamuita "Burukutu" na awe ni mtu mwenye nguvu na mapafu haswa. Nasema hivi kwani siku ile niliona viungo wote wanacheza kama walinzi na hakuna aliyekuwa akichezesha kuunganisha washambuliaji.
Hapa napenda nipingane kabisa na Zamoyoni Mogella alipokuwa akichambua medhi ile runingani alipotupilia mbali kuwa umbo si hoja.Umbo ni kigezo hasa kwa wachezaji wa kiungo cha kati katika mpira wa kileo kwani hawa ni watu wanatakiwa kuwa na nguvu nyingi na uwezo mkubwa wa kuzunguka eneo kubwa la kati hadi mbele(zones).Nimshauri kabisa Maximo, kuwa kuna haja ya kusaka wachezaji warefu wenye nguvu wa eneo la katikati kama kweli tunataka kwenda Ghana.Hawa wapo sio lazima watoke Simba au Yanga.Wapo mikoani na wana uwezo wa kufundishika kiufundi.Nikumbushe kuwa mchezaji wa zamani wa Ushirika ya Moshi na Yanga, Willy Martin alitokea namna hii, mwanzoni akiwa mtu goigoi tu kimpira lakini Dan Koroso alimpika na akaja kuwa mahiri ajabu.
Sasa niendelee na kipindi cha pili cha mechi ile ya jumamosi: kilianza kwa mabao ya haraka haraka. Goli la pili la Diomasy Kamara ni magoli wanayofungwa wadosi katika ligi za ulaya kama Charlton, Wartford na hata West Ham siku hizi. Mara nyingi yanakuwa makosa ya mabeki wasioelewa vizuri. Nilifikiri mabeki wetu walikuwa bado hawajajua nini kinatokea kiwanjani, ilinishangaza sana. Ni makosa ambayo mpira wa kimataifa hutakiwi kuyafayanya kabisa.
Dakika mbili baadaye, Niang alifunga japo alinawa lakini refa hakuona ila mabeki wetu walionekana kumuacha Niang acheze wakinyanyua mikono kwa refa kama walivyozoea hapa Bongo. Ushamba wa mpira wa ridhaa ulijionesha wazi kwani filimbi haijalia wewe unatakiwa ucheze mpira.Ni mambo ya kujifunza haya kwa wachezaji wetu hasa wanapokuwa ugenini kwani wakumbuke mara nyingine huenda refa kalishwa mlungula dhidi ya wageni.
Goli la nne katika dakika ya 61 lilisababishwa na uzembe wa Nsajigwa ambaye hakuruhusiwa kupanda mbele siku hiyo kwani aliwekewa winga teleza ambaye hakumpa mwanya wa kupanda na plani nzima ya Taifa Stars ikaingia mtimanyongo.Nsajigwa alijaribu kumpiga chenga msenegali na akakosea na ndipo krosi ikatumwa na Niang akaunganisha kwa kichwa cha nguvu baada ya kumzidi kipa Ivo aliyetoka vizuri na kuchelewa. Ila hapa pia lazima niwalaumu walinzi wetu jpale kipa alipotoka hakuna mtu alibakia nyuma yake kulinda lango.
Kuanzia hapa nilitaraji goli la tano lakini Mungu akaweka mkono kwani Wasenegali walikuwa wanatutega tuende mbele watushtukize jambo ambalo halikufanikiwa.Nilimwonea huruma Maximo wakati Costa anapiga chenga alafu akanyang'anywa manake Maximo alishika kichwa akijua tumekwisha. Kwa ujumla Senegali walitumia 3-5-2 na sisi sikuona 4-4-2 ila muda mwingi ilikuwa5-3-2 kitu ambacho ingekuwa vigumu kupata bao na pia kufungwa japo pia tulifungwa. Hii nadhani ilisababisha viungo wetu wazidiwe na viungo wengi wa Senegali. Na hivyo mpira kuchezwa na mabeki kwa muda mrefu hali iliyosababisha wafanye makosa mengi. Kimsingi nafasi ya Ghana bado ipo ila Maximo afanye kazi kwenye ufundi(technique) hasa kiungo na pia ningependa tuone wanaitwa vijana kadhaa wapya wenye mbio kali katika wingi zote mbili. Pia ninataka Maximo atafute mchezaji wa mguu wa kushoto kucheza beki ya kushoto kwani siamini Mecky anafaa nafasi ile; hana spidi na hajui kulinda ipasavyo.
Leo nataka nieleze hisia zangu kwa jinsi nilivyotizama mechi ile. Kwanza kabisa sina matatizo na kocha Marcio Maximo japo nashangazwa ni kwanini aliamua wachazaji wetu wacheze kwa kutafuta ushindi na si kujihami ugenini siku ile kitu ambacho kiliwachosha sana na tukafungwa.Magoli yote yalisababishwa na mapungufu ya walinzi wetu. Tangu mwamuzi Mourad kuanzisha mechi, ndani ya dakika tatu za mwanzo tayari Senegali walipata kona ambayo nadhani mlinsa lango wetu angetakiwa azuie mpira ule usitoke lakini kwasababu azijuazo yeye aliuacha mpira utoke huku akijua ingekuwa kona. Wachezaji wetu lazime waelewe kona ni goli kwa wazoefu kama Senegali nadhani.
Nawapongeza Taifa Stars kwa dakika thelathini za mwanzo ila baada ya hapo pumzi ziliwaisha kabisa. Vijana wakawa wazito kuziba nafasi hasa sehemu ya kiungo na mzigo ukabaki kwa ngome kuelemewa na ndiyo maana hata makosa yalikuwa ni lazima kwa wachezaji wa nyuma kwani walikuwa wakiucheza mpira muda mwingi.Ndipo dakika ya 87 jamaa wakapata kona; sijui kama wenzetu wanajufunza kulinda lango wakati wa kona. Goli la kwanza lilitokea hapa kwa kichwa cha Mamadou Niang. Sitaki kuhoji kwanini mchezaji yule aachwe kupiga kichwa huru ila nadhani kama nguzo ya goli ya upand wa kushoto kungekuwa na mtu basi angeokoa mpira ule kirahisi.
Sielewi nahodha, Mecky Mexime, aliyetakiwa kuwa pale alikuwa wapi kwani hata kona nyingine iliyofuata katika dakika ya 44 pia nguzo ya kushoto ilikuwa tupu. Kwa ujumla kipindi cha kwanza tulijitahidi sana kwani angalau Abdi Kassim aliweza angalau kupiga shutu moja zuri langoni mwa Senegali na pia Mwaikimba na Said Maulidi(SMG) walikuwa wakipasiana vizuri japo Smg alikuwa na tatizo la uzubaifu wa kurejea pazi za mbadilishano(return). Mapungufu mawili yalikuwa ni: moja, mipira ya kurusha tulishindwa kuitumia kabisa. Sielewi kwanini hatukuwa tunarusha mipira mirefu langoni mwa adui. Pili, kiungo chetu kilichezwa na wachezaji wadogo kiumbo ambao wasingeweza kumudu maumbo makubwa na kimo kirefu cha viungo wa Senegali kama tulivyoona.
Mara kadhaa niliona Nizar Khalfan akijaribu kukokota mpira kama vile anacheza chandimu mchangani. Ni lazima Maximo afundishe wachezaji wetu watumbue eneo la katikati ndilo linaloamua mechi. Wenzetu wanajipanga kwa eneo lenye ukubwa fulani hivyo kupenya si rahisi kwani wanaziba matundu yote katikati huku wakisaidiwa na uwezo wao mkubwa wa kuteleza na kuzuia kwa nguvu wakitumia ulizaji vibuyu(tackling) wa nguvu za ajabu.Ni vigumu kiungo chetu kingetamba siku ile. Ningependekeza Maximo aanzishe mfumo wa kutumia kiungo wa mbele ya walinzi(defensive shield) kule Brazil wanamuita "Burukutu" na awe ni mtu mwenye nguvu na mapafu haswa. Nasema hivi kwani siku ile niliona viungo wote wanacheza kama walinzi na hakuna aliyekuwa akichezesha kuunganisha washambuliaji.
Hapa napenda nipingane kabisa na Zamoyoni Mogella alipokuwa akichambua medhi ile runingani alipotupilia mbali kuwa umbo si hoja.Umbo ni kigezo hasa kwa wachezaji wa kiungo cha kati katika mpira wa kileo kwani hawa ni watu wanatakiwa kuwa na nguvu nyingi na uwezo mkubwa wa kuzunguka eneo kubwa la kati hadi mbele(zones).Nimshauri kabisa Maximo, kuwa kuna haja ya kusaka wachezaji warefu wenye nguvu wa eneo la katikati kama kweli tunataka kwenda Ghana.Hawa wapo sio lazima watoke Simba au Yanga.Wapo mikoani na wana uwezo wa kufundishika kiufundi.Nikumbushe kuwa mchezaji wa zamani wa Ushirika ya Moshi na Yanga, Willy Martin alitokea namna hii, mwanzoni akiwa mtu goigoi tu kimpira lakini Dan Koroso alimpika na akaja kuwa mahiri ajabu.
Sasa niendelee na kipindi cha pili cha mechi ile ya jumamosi: kilianza kwa mabao ya haraka haraka. Goli la pili la Diomasy Kamara ni magoli wanayofungwa wadosi katika ligi za ulaya kama Charlton, Wartford na hata West Ham siku hizi. Mara nyingi yanakuwa makosa ya mabeki wasioelewa vizuri. Nilifikiri mabeki wetu walikuwa bado hawajajua nini kinatokea kiwanjani, ilinishangaza sana. Ni makosa ambayo mpira wa kimataifa hutakiwi kuyafayanya kabisa.
Dakika mbili baadaye, Niang alifunga japo alinawa lakini refa hakuona ila mabeki wetu walionekana kumuacha Niang acheze wakinyanyua mikono kwa refa kama walivyozoea hapa Bongo. Ushamba wa mpira wa ridhaa ulijionesha wazi kwani filimbi haijalia wewe unatakiwa ucheze mpira.Ni mambo ya kujifunza haya kwa wachezaji wetu hasa wanapokuwa ugenini kwani wakumbuke mara nyingine huenda refa kalishwa mlungula dhidi ya wageni.
Goli la nne katika dakika ya 61 lilisababishwa na uzembe wa Nsajigwa ambaye hakuruhusiwa kupanda mbele siku hiyo kwani aliwekewa winga teleza ambaye hakumpa mwanya wa kupanda na plani nzima ya Taifa Stars ikaingia mtimanyongo.Nsajigwa alijaribu kumpiga chenga msenegali na akakosea na ndipo krosi ikatumwa na Niang akaunganisha kwa kichwa cha nguvu baada ya kumzidi kipa Ivo aliyetoka vizuri na kuchelewa. Ila hapa pia lazima niwalaumu walinzi wetu jpale kipa alipotoka hakuna mtu alibakia nyuma yake kulinda lango.
Kuanzia hapa nilitaraji goli la tano lakini Mungu akaweka mkono kwani Wasenegali walikuwa wanatutega tuende mbele watushtukize jambo ambalo halikufanikiwa.Nilimwonea huruma Maximo wakati Costa anapiga chenga alafu akanyang'anywa manake Maximo alishika kichwa akijua tumekwisha. Kwa ujumla Senegali walitumia 3-5-2 na sisi sikuona 4-4-2 ila muda mwingi ilikuwa5-3-2 kitu ambacho ingekuwa vigumu kupata bao na pia kufungwa japo pia tulifungwa. Hii nadhani ilisababisha viungo wetu wazidiwe na viungo wengi wa Senegali. Na hivyo mpira kuchezwa na mabeki kwa muda mrefu hali iliyosababisha wafanye makosa mengi. Kimsingi nafasi ya Ghana bado ipo ila Maximo afanye kazi kwenye ufundi(technique) hasa kiungo na pia ningependa tuone wanaitwa vijana kadhaa wapya wenye mbio kali katika wingi zote mbili. Pia ninataka Maximo atafute mchezaji wa mguu wa kushoto kucheza beki ya kushoto kwani siamini Mecky anafaa nafasi ile; hana spidi na hajui kulinda ipasavyo.
Saturday, March 24, 2007
TAIFA STARS NADHANI TUTAFUNGWA LEO
Nianze na huu mchuano wa leo kati ya Taifa Stars na Senegali. Maoni yangu ni kwamba haddi wakati naandika makala hii nadhani Senegali wana nafasi ya kushinda: uzoefu, vipaji vilivyoiva,mbinu bora na ufundi mwingi pamoja na uenyeji.Hizi ndizo sifa zinazonifanya niamini watatufunga angalau mabao matatu bila majibu.
Timu yetu itategemea ngome na golikipa angalau tupate sare. Ni wazi kwenye kiungo patatuangusha kama hatutakuwa makini na ufungaji sitaki kusema chochote kwani sioni kama kuna mtu atakayeweza kufunga japo kidogo labda Saidi Maulid na mkongwe
Nigusie pia habari za siasa wiki hii Komredi Mugabe anaanza kudondoka ni wazi siku zake zinahesabika; pia huko Uganda wanasiasa wameamua kuuza msitu maarufu na muhimu wa Mabira japo yuko mfalme wa Buganda kaamua kuipa serikali ardhi ili isiuze.
Uganda bado inabakia ni nchi yenye waasi wengi, hebu wajue.
Timu yetu itategemea ngome na golikipa angalau tupate sare. Ni wazi kwenye kiungo patatuangusha kama hatutakuwa makini na ufungaji sitaki kusema chochote kwani sioni kama kuna mtu atakayeweza kufunga japo kidogo labda Saidi Maulid na mkongwe
Nigusie pia habari za siasa wiki hii Komredi Mugabe anaanza kudondoka ni wazi siku zake zinahesabika; pia huko Uganda wanasiasa wameamua kuuza msitu maarufu na muhimu wa Mabira japo yuko mfalme wa Buganda kaamua kuipa serikali ardhi ili isiuze.
Uganda bado inabakia ni nchi yenye waasi wengi, hebu wajue.
Saturday, March 17, 2007
AFYA ZETU TWAZIJALI?
Kabla ya kuangalia afya hebu tuone Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki anasemaje juu ya muungano huu?Na ni jinsi gani majeshi ya Uganda yana umuhimu huiko Somalia?
Leo tuangalie afya, hasa juu ya mambo ambayo wengine twafikiri ni urembo kumbe liipo jambo hasa kwa wanawake ambao hawatakiwi kuvaa mini skirt.Pia je kutoa mimba sawa?Pia ni jinsi gani kusevu pesa kunawezekana?
Siasa je unajua ile report ya tatizo la PRA?Maajabu ya maadili kwenda likizo, hata Mufti Mkuu mdanganyifu?Ni vizuri pia tujue wanasiasa maarufu wana historia gani?
Mwisho juu ya wazazi wetu, je kuna haja ya kuwajali?
Leo tuangalie afya, hasa juu ya mambo ambayo wengine twafikiri ni urembo kumbe liipo jambo hasa kwa wanawake ambao hawatakiwi kuvaa mini skirt.Pia je kutoa mimba sawa?Pia ni jinsi gani kusevu pesa kunawezekana?
Siasa je unajua ile report ya tatizo la PRA?Maajabu ya maadili kwenda likizo, hata Mufti Mkuu mdanganyifu?Ni vizuri pia tujue wanasiasa maarufu wana historia gani?
Mwisho juu ya wazazi wetu, je kuna haja ya kuwajali?
Saturday, March 10, 2007
MAJAJI WAMALIZA MGOMO
Baada ya ile sinema ya Iddi Amin kushinda Oscar, hali ya kisiasa nchini Uganda inaonesha wazi sinema nyingine tayari imeanza kutengenezwa. Kwanza soma ni vipi mwanaye Iddi Amin alivyomfahamu baba yake?Imeshangaza sana hata majaji wanaweza kugoma.Unaambiwa mgomo umekuwa na athari zake kwelikweli. Waganda inabidi waje tena MOSHI kwa majadiliano upya.
Ni vizuri tujue kasheshe lililosababisha majaji kugoma Uganda na ni jinsi gani demokrasia imechafuliwa?
Mwisho ni hii simu mpya ya I Pod.
Ni vizuri tujue kasheshe lililosababisha majaji kugoma Uganda na ni jinsi gani demokrasia imechafuliwa?
Mwisho ni hii simu mpya ya I Pod.
Wednesday, March 07, 2007
HATA MAJAJI WANAGOMA UGANDA?
Uganda inaongozwa kwa miujiza ya Mungu kwa mujibu wa Museveni. Athari zake ni kama ifuatavyo: moja, majaji wamegoma kwani wamechoka kuingiliwa na serikali na pia hata mawakili(wanasheria) nao wamejiunga na mgomo wa kuidhalilisha taasisi ya mahakama.Museveni ndiye atakayekuwa rais wa kwanza wa jumuiya ya Afrika Mashariki, lakini haya ya kutuma askari kuingilia maamuzi ya majaji tuyararajie?
Tunaambiwa hakuna utumwa wa hali ya juu kama ule wa kuwa na Rais mmoja kwa muda mrefu. Uganda kama Tanzania inafanya kila juhudi kukandamiza haki ya kupata habari.
Jambo moja linachekesha Museveni ameisifia sana ile sinema ya Iddi Amin iliyoshinda Oscar majuzi, je unajua kwanini?Yanayotokea uganda yanatakiwa kuepushwa ni aibu.Uganda na nchi nyingine Afrika zimebakia hakuna maelewana kati ya serikali na wapinzani.
Tuje mambo ya Makerere, na pia tuone ni jinsi gani wanawake wamefanikiwa kisiasa? Pia nini kinakwamisha mazungumzo ya LRA Uganda?
Tunaambiwa hakuna utumwa wa hali ya juu kama ule wa kuwa na Rais mmoja kwa muda mrefu. Uganda kama Tanzania inafanya kila juhudi kukandamiza haki ya kupata habari.
Jambo moja linachekesha Museveni ameisifia sana ile sinema ya Iddi Amin iliyoshinda Oscar majuzi, je unajua kwanini?Yanayotokea uganda yanatakiwa kuepushwa ni aibu.Uganda na nchi nyingine Afrika zimebakia hakuna maelewana kati ya serikali na wapinzani.
Tuje mambo ya Makerere, na pia tuone ni jinsi gani wanawake wamefanikiwa kisiasa? Pia nini kinakwamisha mazungumzo ya LRA Uganda?
Wednesday, February 21, 2007
LEO SIASA ZA UGANDA
Uganda ina siasa mbili: ya nchi na ya Jadi ambayo sasa kuna waka moto huko Lubiri.
Kuna fununu Makamu wa Rais wa Uganda atang'olewa madarakani.Je inawezekana?na je ni nani huyu Profesa Bukenya? Yeye mwenyewe kaamua kuwa ngangari na anasema haendi kokote, je hili tishio kwa Museveni na ndio maana anamng'oa kwani kwa Uganda, kuna imani kuwa mtu wa kabila la BUGANDA hawezi kuwa rais kamwe kwani hiki ni cheo cha watu wa anakotokea Museveni tu: Mashariki.
Kuna maoni juu ya filamu ya Iddi Amin; na pia unajua uwongo wa picha hiyo?
Kuna fununu Makamu wa Rais wa Uganda atang'olewa madarakani.Je inawezekana?na je ni nani huyu Profesa Bukenya? Yeye mwenyewe kaamua kuwa ngangari na anasema haendi kokote, je hili tishio kwa Museveni na ndio maana anamng'oa kwani kwa Uganda, kuna imani kuwa mtu wa kabila la BUGANDA hawezi kuwa rais kamwe kwani hiki ni cheo cha watu wa anakotokea Museveni tu: Mashariki.
Kuna maoni juu ya filamu ya Iddi Amin; na pia unajua uwongo wa picha hiyo?
Saturday, February 17, 2007
UASI NI RUKSA--KANALI BESYIGYE
Kanali Besigye bado anaendeleza tambo zake za kumng'oa Museveni. Hapa anafikia hatua ya kuhalalisha uasi kama njia halali ya kujipatia madaraka. Alafu mjue shujaa wa Uganda.
WANASIASA NI FEDHULI KULIKO NYANI
Tabia za mwanasiasa yeyote hazina ukweli wala uaminifu, inasemekana wanasiasa ni wadhalimu kuliko hata nyani.
Bado mammbo ya Rwanda nayaona kama kizungumkuti. Ninapata hisia labda akina Kagame wanamsingizia tu mke wa Habyarimana. Sina imani kuwa kuna chuki za magharibi dhidi ya Rwanda.
Museveni ni bingwa wa siasa kwa kuweza kuchanganya siasa na utawala wa kifalme kufanya kazi bila matatizo.Lakini pia zipo gharama za kuzuia matatizo yaliyotarajiwa mfano haya.
Huwa napenda KANDANDA pia;eti meneja wa Chelsea anadai watatwaa ubingwa, je inawezekana?
Kwa wale makapera kama mie: je kuna ulazima wa kuoa?
Bado mammbo ya Rwanda nayaona kama kizungumkuti. Ninapata hisia labda akina Kagame wanamsingizia tu mke wa Habyarimana. Sina imani kuwa kuna chuki za magharibi dhidi ya Rwanda.
Museveni ni bingwa wa siasa kwa kuweza kuchanganya siasa na utawala wa kifalme kufanya kazi bila matatizo.Lakini pia zipo gharama za kuzuia matatizo yaliyotarajiwa mfano haya.
Huwa napenda KANDANDA pia;eti meneja wa Chelsea anadai watatwaa ubingwa, je inawezekana?
Kwa wale makapera kama mie: je kuna ulazima wa kuoa?
Wednesday, February 14, 2007
ETI LEO NI SIKUKUU YA VALENTINE?
Wakati nikiwa masomoni Uganda nilijifunza juu ya Demokrasia na mhadhiri wangu kaandika juu alichotufunza gazetini kuhusu siasa za Uganda hasa juu ya majadiliano yasiyokwisha. Hapa anajibiwa na mwandishi eti kakosea. Mjadala unaendelea juu ya siasa haswa. Jua siri ya serikali ya Rwanda kuhusu matumizi bora ya magari ya serikali.Huko Uganda kuna mgogoro bungeni juu ya kuyaruhusu majeshi ya nchi hiyo yaende ama la nchini Somalia. Wapinzani wamegomea bunge kwani hawataki majeshi yande Somalia kitendo kinachoonekana ni kuiunga mkono serikali bila kujijua; je ni kwanini?
Hili ni la muhimu sana juu ya kufungiwa hivi majuzi kwa kituo kipya cha televisheni-NTV-kwani ni juhudi za udhibiti wa vyombo vya habari Afrika Mashariki kama zile za kudhibiti wanaharakati kama HAKI ELIMU nchini Tanzania.Lakini pia tunakumbushwa ipo mijpaka ya kusema na kuandika hasa kwa vyombo vya habari-THE FOURTH STATE.
Hili ni la muhimu sana juu ya kufungiwa hivi majuzi kwa kituo kipya cha televisheni-NTV-kwani ni juhudi za udhibiti wa vyombo vya habari Afrika Mashariki kama zile za kudhibiti wanaharakati kama HAKI ELIMU nchini Tanzania.Lakini pia tunakumbushwa ipo mijpaka ya kusema na kuandika hasa kwa vyombo vya habari-THE FOURTH STATE.
WIZI WA MITIHANI UGANDA
Wakati nchini Tanzania tuna wabunge na mawaziri wenye tuhuma nzito za kudanganya juu ya masomo au shahada zao huko nchini Uganda wabunge hawako tayari kufanya hayo ama kuruhusu watu kuiba mitihani. Wanachukua hatua inapobidi.
Soma juu ya jinsi siasa ulivyo mchezo wa kufanyiziana: kuanzia Afrika mpaka India na hata Ulaya. Ni mchezo mchafu sana ninavyoamini. Pia niliwahi kuandika juu ya Profesa Mamdani akitusihi Wabongo tuachane na mikopo ya kusoma chuo kikuu, leo kaja na makala nyingine juuu ya hili. Na mwisho kafunga mjadala wa elimu chuo kikuu.
Pia ni vipi ilivyo muhimu kusaidia Wasomalia: unajua PAN Africanism?
Soma juu ya jinsi siasa ulivyo mchezo wa kufanyiziana: kuanzia Afrika mpaka India na hata Ulaya. Ni mchezo mchafu sana ninavyoamini. Pia niliwahi kuandika juu ya Profesa Mamdani akitusihi Wabongo tuachane na mikopo ya kusoma chuo kikuu, leo kaja na makala nyingine juuu ya hili. Na mwisho kafunga mjadala wa elimu chuo kikuu.
Pia ni vipi ilivyo muhimu kusaidia Wasomalia: unajua PAN Africanism?
Saturday, February 10, 2007
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE--2006
Eti waafrika ni watu wasiweza kuendelea hata wafanye nini, je ni kweli?
Kuhusu elimu huu ndio msimu wa wale wa shule kufurahia mavuno yao.Matokeo ya mwaka huu ni haya hapa.
Pia je unajua kuonesha uwazi wa sehemu zako ni makosa hadharani?
Wakati Wabunge wa Uganda wanabishana juu ya kupeleka askari huko somalia inasemekana ni faida kwa Uganda.\\Pia ni kwawaida kwa walarushwa kulindana, kama uliwahi kusikia kashfa kubwa ya waziri wa Uganda sasa kaula, kapewa tenda na rafikie Museveni.
Kuhusu elimu huu ndio msimu wa wale wa shule kufurahia mavuno yao.Matokeo ya mwaka huu ni haya hapa.
Pia je unajua kuonesha uwazi wa sehemu zako ni makosa hadharani?
Wakati Wabunge wa Uganda wanabishana juu ya kupeleka askari huko somalia inasemekana ni faida kwa Uganda.\\Pia ni kwawaida kwa walarushwa kulindana, kama uliwahi kusikia kashfa kubwa ya waziri wa Uganda sasa kaula, kapewa tenda na rafikie Museveni.
Thursday, February 01, 2007
JINSI MAJESHI YA BONGO YALIVYOWATIA KIZUIZINI WAGANDA TZ.
Ninapenda sana mambo ya uhusiano yanavyochambuliwa na wengine hebu soma hili.Je unajua mambo ambayo watanzania wengi hatuyajui wakati wa vita ya Iddi Amin?
Unamjua bingwa wa uandishi habari aliyekufa?
Unapaswa kujua pia yuko Rais wa nchi moja ya Afrika(Guinea) bado yuko kwenye zile zama za kung'ang'ania madaraka.Pia soma juu ya jinsi vyama tawala, au vyama dola kama CCM vinavyofanya katiba ya nchi kama mali yao.
Hili ni la muhimu sana kujua juu ya Uganda manake baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana wapinzani walilalamika mahakamani na majaji wa mahakama kuu wakatoa uamuzi kuwa Museveni alikuwa mshindi halali.Jua ni kwanini majaji walitoa uamuzi huo,
Pia ni vyema usome uamuzi wao ulisemaeje?
Soma pia ni jinsi gani bara letu Afrika lilivyo na wabunge ghali sana juu ya uwezo wa nchi.Pia huko Uganda eti ubinafsishaji umegeuka kuwa kama ugaidi.
Pia tunakumbushwa ni kwanini hatuna sababu ya kukumbuka siku ya uhuryu wa nchi zetu?Alafu mwisho kabisa:SOMA JUU YA BLOOD DIAMOND, sinema ambayo inaelezea juu ya umafia ulivyokithiri Afrika.
Unamjua bingwa wa uandishi habari aliyekufa?
Unapaswa kujua pia yuko Rais wa nchi moja ya Afrika(Guinea) bado yuko kwenye zile zama za kung'ang'ania madaraka.Pia soma juu ya jinsi vyama tawala, au vyama dola kama CCM vinavyofanya katiba ya nchi kama mali yao.
Hili ni la muhimu sana kujua juu ya Uganda manake baada ya uchaguzi mkuu mwaka jana wapinzani walilalamika mahakamani na majaji wa mahakama kuu wakatoa uamuzi kuwa Museveni alikuwa mshindi halali.Jua ni kwanini majaji walitoa uamuzi huo,
Pia ni vyema usome uamuzi wao ulisemaeje?
Soma pia ni jinsi gani bara letu Afrika lilivyo na wabunge ghali sana juu ya uwezo wa nchi.Pia huko Uganda eti ubinafsishaji umegeuka kuwa kama ugaidi.
Pia tunakumbushwa ni kwanini hatuna sababu ya kukumbuka siku ya uhuryu wa nchi zetu?Alafu mwisho kabisa:SOMA JUU YA BLOOD DIAMOND, sinema ambayo inaelezea juu ya umafia ulivyokithiri Afrika.
Wednesday, January 03, 2007
FUNGUA MWAKA 2007
Mwaka 2006 umemalizika na makala kadhaa ambazo zimegusia ni jinsi gani ulimwengu wetu ulivyo na changamoto. Kifo cha Saddam pia kimegusa hisia za wengi na hasa jinsi udikteta mpya ulivyozaliwa na kinyongo hiki cha dikteta. Hata waliokuwa wanamtetea inasemekana serikali ya sasa inawatisha sana.
Mwaka mpya ni wakati wa kugusia juu ya taasisi za kiserikali zinavyopaswa kufanya kazi hasa Afrika Mashariki. Pia tujifunze zaidi nini mchango wa China katika uchumi wa Afrika?
Pia ni vizuri tujifunze juu ya changamoto za SACCOS.
Mwaka mpya ni wakati wa kugusia juu ya taasisi za kiserikali zinavyopaswa kufanya kazi hasa Afrika Mashariki. Pia tujifunze zaidi nini mchango wa China katika uchumi wa Afrika?
Pia ni vizuri tujifunze juu ya changamoto za SACCOS.
Friday, December 22, 2006
MASLAHI YA NCHI NI ZAIDI YA SIASA NA HISIA ZA WATU
Unaposikia tofauti kati ya siasa na maslahi ya nchi mfano mzuri uko hapa kwenye maziwa makuu.
Pia kuna hili la kalenda ya uendeshaji wa ligi ya soka.
Pia huko Kenya rais Kibaki atakuwa Mombasa kama kawa.
Pia kuna hili la kalenda ya uendeshaji wa ligi ya soka.
Pia huko Kenya rais Kibaki atakuwa Mombasa kama kawa.
Thursday, December 21, 2006
HAKUNA HAJA YA MIKOPO ELIMU YA JUU-PROF: MAAMDANI
Wakati wabongo tunalia na JK kuhusu mikopo ya elimu ya juu, yule profesa maaarufu, Maamdani kachapisha kitabu akisema eti serikali isilipie ila wote tulipie elimu
Tuesday, December 19, 2006
JK NA JINAMIZI LA CCM NDANI YA MWAKA MMOJA IKULU
JK sasa anaanza kuona ukweli halisi wa bongo kuwa tatizo liko kwenye CCM. Hili ni jinamizi ambalo JK ana kazi ngumu kuliondoa manake ncchi imeoza na itagharimu Taifa sana kuweza kuondoa hayo ambayo JK kakemea jana.
SALAM ZA CHRISTMAS
Tunasherehekia Krismas soma jinsi makasisi wa dini mbalimbali(mapadiri na wachungaji na mashehe pia) walivyobadilika siku hizi na tunakkumbushwa je Yesu wa wakristu angezaliwa leo ingekuwaje Afrika?Alafu nataka uone ni jinsi gani wabunge wa Afrika hasa Uganda walivyo na ulafi na mapenzi na MABENZI na si wananchi, yaani wanatishia serikali pale inapotaka kuwakata usawa.
Mwisho, ona jinsi Jaji Kiongozi Uganda hisia zake juu ya utawala bora.Alafu mkuu wa Jeshi la polisi Uganda naye anaamua kumjibu na kumkosoa ikibidi Jaji Kiongozi, patamu hapa.
Alafu wajue watu kumi waliotingisha Uganda mwaka huu.
Mwisho, ona jinsi Jaji Kiongozi Uganda hisia zake juu ya utawala bora.Alafu mkuu wa Jeshi la polisi Uganda naye anaamua kumjibu na kumkosoa ikibidi Jaji Kiongozi, patamu hapa.
Alafu wajue watu kumi waliotingisha Uganda mwaka huu.
Friday, December 15, 2006
MKE WA MUSEVENI KATIKA UGOMVI KUMTETEA MUMEWE
Mke wa rais Museveni ambaye ni mbunge jana inasemekana karushiana maneno makali na mwanamama mmoja wa shoka wa chama cha upinzani katika kile kinachoonekana kutetea rekodi mbovu ya mumewe ndani ya bunge.
Alafu unajua kwanini maprofesa wa Makerere wamegoma? Soma haya.
Alafu unajua kwanini maprofesa wa Makerere wamegoma? Soma haya.
Wednesday, December 13, 2006
UDIKTETA-SIRI YA KUISHI MUDA MREFU
Eti madikteta hawafi mapema, tunahimizwa tuwe majitu korofi na dhalimu ili tuishi muda mrefu.
Thursday, December 07, 2006
JK AIGE KUTOKA KWA CALDERON WA MEXICO
Kama kweli Tanzania inapenda maendeleo tunahitaji kiongozi kama huyu aliyechaguliwa huko Mexico majuzi. JK angekuwa namna hii na akatekeleza basi tunaweza kufanikisha "Maisha bora kwa kila Mtanzania".
Vinginevyo JK anatania tu.
Vinginevyo JK anatania tu.
UHURU BONGO--BONGE LA PATI SAWA AU DHIHAKA?
Kama mtanzania sina budi kujumuika na watanzania wenzangu kuadhimisha siku hii ya miaka 45 ya uhuru wa Tanzania bara(Tanganyika).Huu ni wajibu wa mzalendo yeyote kutathmini je uhuru wetu umeleta tija kwa watanzania wote au kwa kukundi fulani ndani ya jamii tu?Sisherehekei manake kwa hali ilivyo si muafaka kwa hili bali ni wakati wa kujiuliza kwa nini tunaendelea kuharibu uchumi wetu namna hii?Sherehe tuwaachie wanaoona matunda ya uhuru kama akina JK na Ngoyai: hawa kwao hakuna tatizo la umeme, maji wala usafiri au barabara mbovu. Kwao wanazo njia mbadala kutatua haya.
Nimefuatilia sherehe za uhuru leo kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) kwani wakati ndio sherehe inaanza hawa jamaa wa Tanesco wakakata umeme alafu ikaw ndio mwisho wa kuangalia Runinga yangu.Matanzgazo ya RTD hayasikiki vizuri nashangaa kwanini RTD wasiweke mtambo wa FM manake hizi FM radio nyingi ni muziki kwa kwenda mbele utadhani siku ya leo ni sawa na zingine. Ni Radio Free Afrika ya Mwanza na Sauti ya Injili ya Moshi angalau leo wamekuwa na vipindi kuwahoji watu ambao walihusika na uhuru wetu wakati ule na wametoa mawazo murua kweli. Nakwambia tukio hili hapa Moshi si la muhimu kama siku ya jumapili au sikukuu ya Idd El Fitri kwani siku hizo umeme ni bwerere.Hasira imenishika kwani baada ya sherehe kumalizika hawa jamaa wanawasha umeme, nakwambia Tanesco hapa Moshi hawajui uhuru kabisa. Hayo tuyaache, ila JK hotuba yake ilikuwa nzuri nampongeza sana. Ila aliangalia tu mafanikio nchi iliyojipatia tu tangu 1961, ameacha kuzungumzia matatizo kama haya ya Umeme.
Nami naona nieleze kwa ufupi japo ninafikiri nini siku hii:
Mtizamo wangu unatia wasiwasi sana kama kweli tumefikia mafanikio ya dhati kulingana na kipindi cha miaka 45. Naanza na sekta ya barabara tumefeli kabisa. Bado hatujaweza kuunganisha nchi yetu kwani tunalazimika kupitia Kenya kusafiri kutoka Arusha kwenda Mwanza, Bukoba au hata Kampala.
Pili bado tunakumbwa na njaa kila mwaka ilihali tuna ardhi, mito kibao kuwezesha kilimo cha umwagiliaji. Ukija kwenye maji ndio usiseme kabisa. Hakuna maji kunywa ya kutosha hata katika miji kama Dar es salaam, Arusha na hata Mwanza.
Huwezi kuamini nchi yenye umri wa miaka 45, haina umeme wa kuaminika na kutosha angalau mautmizi ya majumbani achilia mbali viwandani. Viongozi, yaani wanasiasa hawana utashi wowote kwa maendeleo ya jumla ya nchi. Maslahi binafsi yamewekwa mbele kuliko uzalendo: kwa mfano, nchi inagenishwa kwa kubadilishana/bei poa kati ya watu fulani ndani ya tabaka tawala(elites) na si kwa maslahi ya mtu.
Ukija kwa watunga sheria(Wabunge) ndio basi tena. Bunge limekuwa jamvi la kila mtu siku hizi hata wendawazimu au kwa maana nyingine mbumbumbu kielimu nionavyo kutokana na matendo yao.Elimu si tija kwa mtu kuwa mbunge au diwani. Nidio maana bunge letu ni taasisi ya kubariki mambo yasiyo na maslahi kwa Taifa ila Chama(CCM) na yale ya binafsi. Chama tawala kimelimeza bunge na kutupeleka kuzimu kiuchumi. Tumefika mahali mtu akiheshimu taaluma katika kusimamia au kuamua mambo ya kiuchumi na mengine ya msingi kama hayo anaonekana mwehu na si mwenzetu. Hii ndio miaka 45 ya uhuru tunayosherehekea. Hili ni lazima tulitafakari la sivyo uhuru unakuwa hauna maana.
Kwa robo mwaka sasa nchi iko gizani, hakuna umeme na viongozi na wahusika wetu hawajali kabisa. Ufisadi na kulindana ndio umetufikisha hapa tulipo na viongozi wahujumu hawaguswi bali wanahamishwa kutoka idara au wizara moja hadi nyingine kuendeleza uharibifu. Vipaumbele vyetu ni vile visivyo; viongozi wetu wamebakia kusafiri kutembeza bakuli kwa wafadhili na kuhimiza uwekezaji katika nchi isiyokuwa na umeme wa kuaminika bila aibu. Kiongozi mkuu anadiriki kusema tatizo la umeme limerithiwa kutoka serikali iliyopita bila kung'amua alikuweko ndani ya serikali hiyo.
Kisiasa, nchi imebaki hoi kabisa; vyama vya upinzani viko hoi kabisa na havionekani kuchukua hatua madhubuti kutia changamoto kwa CCM inavyoboronga. Haya yakiendelea, CCM chini ya Makamba imebakia kuwarubuni wapinzani makini kurejea CCM kama ndio kipaumbele. CCM haitaki changamoto, kwake kuwa mpinzani ni uadui, si uzalendo kwa nchi. Kweli hapa hatutaelewa wapi tunakosea kama tutaendelea hivi na ndio maana bado tuko nyuma maeneo mengi. Demokrasia yetu ni kama vile "maonesho kwa wafadhili"(show-off) na sio demokrasia ya dhati.
Viongozi wetu kama vile Lowasa na Makamba wanaongoza kwa sera kongwe za kihafidhina. Hili ni tatizo la viongozi ndani ya chama tawala, serikalini na hata vyama vya upinzani. Tunahitaji kizazi kipya cha uongozi nadhani ili tuendelee. Hata hivyo, kama Taifa tumefanikiwa kubaki na umoja wa kitaifa kitu muhimu kwa nchi yeyote.
Amani tuliyonayo ni lazima tuikuze kwa kuziunda upya taasisi za kidemokrasia katika utawala ili muongo ujao tupige hatua kwa haraka na si kama miaka hii 45 iliyopita. Katiba ni lazima iangaliwe upya ili miundo ya mihimili mitatu ya dola ifanye kazi inavyopaswa kwa uhuru na si kama sasa kwa kulinda maslahi ya chama tawala. Hii imefanya kwa mfano bunge letu kubaki kama muhuri wa udhalimu "rubber stamp" wa serikali mara kwa mara.
Mwisho, ingawa wenzetu wa magharibi iliwachukua muda mrefu kufikia mafanikio ya demokrasia, sisi isiwe kisingizio, kwani dunia ya leo mambo yamerahisishwa ni lazima tuendelee haraka. Nitoe rai: Tuna wasomi wengi wa kila aina Tanzania ila wote wamefungwa jela ya nafsi zao(conscience) na wamekuwa bendera fuata upepo(sycophants) mbele ya wanasiasa wa chama tawala. Ujasiri unahitajika kwa wasomi wa nchi hii la sivyo kama nchi tutaendelea kusherehekea uhuru wa wachache kama tunavyofanya leo hii. Kwani mantiki ya nchi huru sidhani ina maana kwa watanzania wengi wa kama kule vijijini pembezoni mwa nchi hii. Na kwa akina JK, Ngoyai na Makamba: kumbukeni turuhusu changamoto ndani ya chama na hata serikalini kwani ikiwa tutafanya hivyo hatutaona mikataba ya kijinga kama hii ya IPTL, Richmond, Usiri wa biashara ya mihadarati na mengine mengi ambayo hayasemwi kwa kuogopa kumkosoa bwana mkubwa.
Nimefuatilia sherehe za uhuru leo kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) kwani wakati ndio sherehe inaanza hawa jamaa wa Tanesco wakakata umeme alafu ikaw ndio mwisho wa kuangalia Runinga yangu.Matanzgazo ya RTD hayasikiki vizuri nashangaa kwanini RTD wasiweke mtambo wa FM manake hizi FM radio nyingi ni muziki kwa kwenda mbele utadhani siku ya leo ni sawa na zingine. Ni Radio Free Afrika ya Mwanza na Sauti ya Injili ya Moshi angalau leo wamekuwa na vipindi kuwahoji watu ambao walihusika na uhuru wetu wakati ule na wametoa mawazo murua kweli. Nakwambia tukio hili hapa Moshi si la muhimu kama siku ya jumapili au sikukuu ya Idd El Fitri kwani siku hizo umeme ni bwerere.Hasira imenishika kwani baada ya sherehe kumalizika hawa jamaa wanawasha umeme, nakwambia Tanesco hapa Moshi hawajui uhuru kabisa. Hayo tuyaache, ila JK hotuba yake ilikuwa nzuri nampongeza sana. Ila aliangalia tu mafanikio nchi iliyojipatia tu tangu 1961, ameacha kuzungumzia matatizo kama haya ya Umeme.
Nami naona nieleze kwa ufupi japo ninafikiri nini siku hii:
Mtizamo wangu unatia wasiwasi sana kama kweli tumefikia mafanikio ya dhati kulingana na kipindi cha miaka 45. Naanza na sekta ya barabara tumefeli kabisa. Bado hatujaweza kuunganisha nchi yetu kwani tunalazimika kupitia Kenya kusafiri kutoka Arusha kwenda Mwanza, Bukoba au hata Kampala.
Pili bado tunakumbwa na njaa kila mwaka ilihali tuna ardhi, mito kibao kuwezesha kilimo cha umwagiliaji. Ukija kwenye maji ndio usiseme kabisa. Hakuna maji kunywa ya kutosha hata katika miji kama Dar es salaam, Arusha na hata Mwanza.
Huwezi kuamini nchi yenye umri wa miaka 45, haina umeme wa kuaminika na kutosha angalau mautmizi ya majumbani achilia mbali viwandani. Viongozi, yaani wanasiasa hawana utashi wowote kwa maendeleo ya jumla ya nchi. Maslahi binafsi yamewekwa mbele kuliko uzalendo: kwa mfano, nchi inagenishwa kwa kubadilishana/bei poa kati ya watu fulani ndani ya tabaka tawala(elites) na si kwa maslahi ya mtu.
Ukija kwa watunga sheria(Wabunge) ndio basi tena. Bunge limekuwa jamvi la kila mtu siku hizi hata wendawazimu au kwa maana nyingine mbumbumbu kielimu nionavyo kutokana na matendo yao.Elimu si tija kwa mtu kuwa mbunge au diwani. Nidio maana bunge letu ni taasisi ya kubariki mambo yasiyo na maslahi kwa Taifa ila Chama(CCM) na yale ya binafsi. Chama tawala kimelimeza bunge na kutupeleka kuzimu kiuchumi. Tumefika mahali mtu akiheshimu taaluma katika kusimamia au kuamua mambo ya kiuchumi na mengine ya msingi kama hayo anaonekana mwehu na si mwenzetu. Hii ndio miaka 45 ya uhuru tunayosherehekea. Hili ni lazima tulitafakari la sivyo uhuru unakuwa hauna maana.
Kwa robo mwaka sasa nchi iko gizani, hakuna umeme na viongozi na wahusika wetu hawajali kabisa. Ufisadi na kulindana ndio umetufikisha hapa tulipo na viongozi wahujumu hawaguswi bali wanahamishwa kutoka idara au wizara moja hadi nyingine kuendeleza uharibifu. Vipaumbele vyetu ni vile visivyo; viongozi wetu wamebakia kusafiri kutembeza bakuli kwa wafadhili na kuhimiza uwekezaji katika nchi isiyokuwa na umeme wa kuaminika bila aibu. Kiongozi mkuu anadiriki kusema tatizo la umeme limerithiwa kutoka serikali iliyopita bila kung'amua alikuweko ndani ya serikali hiyo.
Kisiasa, nchi imebaki hoi kabisa; vyama vya upinzani viko hoi kabisa na havionekani kuchukua hatua madhubuti kutia changamoto kwa CCM inavyoboronga. Haya yakiendelea, CCM chini ya Makamba imebakia kuwarubuni wapinzani makini kurejea CCM kama ndio kipaumbele. CCM haitaki changamoto, kwake kuwa mpinzani ni uadui, si uzalendo kwa nchi. Kweli hapa hatutaelewa wapi tunakosea kama tutaendelea hivi na ndio maana bado tuko nyuma maeneo mengi. Demokrasia yetu ni kama vile "maonesho kwa wafadhili"(show-off) na sio demokrasia ya dhati.
Viongozi wetu kama vile Lowasa na Makamba wanaongoza kwa sera kongwe za kihafidhina. Hili ni tatizo la viongozi ndani ya chama tawala, serikalini na hata vyama vya upinzani. Tunahitaji kizazi kipya cha uongozi nadhani ili tuendelee. Hata hivyo, kama Taifa tumefanikiwa kubaki na umoja wa kitaifa kitu muhimu kwa nchi yeyote.
Amani tuliyonayo ni lazima tuikuze kwa kuziunda upya taasisi za kidemokrasia katika utawala ili muongo ujao tupige hatua kwa haraka na si kama miaka hii 45 iliyopita. Katiba ni lazima iangaliwe upya ili miundo ya mihimili mitatu ya dola ifanye kazi inavyopaswa kwa uhuru na si kama sasa kwa kulinda maslahi ya chama tawala. Hii imefanya kwa mfano bunge letu kubaki kama muhuri wa udhalimu "rubber stamp" wa serikali mara kwa mara.
Mwisho, ingawa wenzetu wa magharibi iliwachukua muda mrefu kufikia mafanikio ya demokrasia, sisi isiwe kisingizio, kwani dunia ya leo mambo yamerahisishwa ni lazima tuendelee haraka. Nitoe rai: Tuna wasomi wengi wa kila aina Tanzania ila wote wamefungwa jela ya nafsi zao(conscience) na wamekuwa bendera fuata upepo(sycophants) mbele ya wanasiasa wa chama tawala. Ujasiri unahitajika kwa wasomi wa nchi hii la sivyo kama nchi tutaendelea kusherehekea uhuru wa wachache kama tunavyofanya leo hii. Kwani mantiki ya nchi huru sidhani ina maana kwa watanzania wengi wa kama kule vijijini pembezoni mwa nchi hii. Na kwa akina JK, Ngoyai na Makamba: kumbukeni turuhusu changamoto ndani ya chama na hata serikalini kwani ikiwa tutafanya hivyo hatutaona mikataba ya kijinga kama hii ya IPTL, Richmond, Usiri wa biashara ya mihadarati na mengine mengi ambayo hayasemwi kwa kuogopa kumkosoa bwana mkubwa.
Wednesday, December 06, 2006
KAGAME-MUNGU MTU- ASHTAKIWE TU
Naiangalia hali ya Rwanda kama ni tatizo ambalo waafrika hatuwezi kulitatua kwani kihistoria ni vigumu. Sina imani sana na mahakama ya Arusha kwani naiona kama mahakama iliyoundwa na washindi wa vita(RPF) ili kuwahukumu washindwa.
Ndipo hapa ninapokuwa ninamuunga mkono huyu jaji wa kifaransa kutaka pia Kagame ashtakiwe. Sidhani kuna suluhisho la kiafrika, ila naunga mkono juu ya nia ya mficho ya Ufaransa katika sakata hili. Pia nionavyo tutarajie Rwanda yenye matatizo sana hapo baadaye kwani Kagame inasemekana ni kiongozi Mungu mtu.Tatizo letu waafrika ni kutokupenda kusema ukweli na kama tutaendelea na uwongo huu wa Kagame hakuna maridhiano Rwanda.
Lakini pia ni lazima tujue pande zote mbili zilihusikaje katika kile kinachoitwa ukombozi wa Rwanda?Kwa mfano, picha halisi ya ushiriki wa Kagame na Habyarimana unaweza kuisoma na kupata hali halisi hasa hii makala ambayo mwandishi anao uelewa sana wa mambo ya Rwanda.
Ndipo hapa ninapokuwa ninamuunga mkono huyu jaji wa kifaransa kutaka pia Kagame ashtakiwe. Sidhani kuna suluhisho la kiafrika, ila naunga mkono juu ya nia ya mficho ya Ufaransa katika sakata hili. Pia nionavyo tutarajie Rwanda yenye matatizo sana hapo baadaye kwani Kagame inasemekana ni kiongozi Mungu mtu.Tatizo letu waafrika ni kutokupenda kusema ukweli na kama tutaendelea na uwongo huu wa Kagame hakuna maridhiano Rwanda.
Lakini pia ni lazima tujue pande zote mbili zilihusikaje katika kile kinachoitwa ukombozi wa Rwanda?Kwa mfano, picha halisi ya ushiriki wa Kagame na Habyarimana unaweza kuisoma na kupata hali halisi hasa hii makala ambayo mwandishi anao uelewa sana wa mambo ya Rwanda.
Tuesday, December 05, 2006
BESIGYE ALIVYOMNYANG'ANYA MUSEVENI MKE
Pamoja na kufuatilia habari za wanasiasa kadhaa ni vyema pia wakati mwingine tujue habari zao binafsi. Leo nataka nieleze habari za kiumbea ambazo niliwahi kuzisikia juu ya Museveni, Kiiza Besyige na huyu mwanamke wa chuma(iron lady) Bi Winnie Byanyima.
Inasemekana ugomvi kati ya Museveni na Besigye pia unachangiwa na kuibiana mabibi. Eti Bi. Byanyima awali alikuwa ni mtu wa karibu sana wa Museveni wakati wa vita ya msituni. Wakati huo Besigye akiwa kama daktari wa Museveni. Leo hii Bi. Byanyima ni mke wa Besyigye japo nakumbuka niliwahi kumsikia akihojiwa na redio moja Kampala na akadai kuwa eti Besigye ni mshirika wake tu(companion).
Wambeya wanadai eti siku waasi wa Museveni(NRA)wanaiteka na kuitwa Kampala, waliingia Kampala huku gari alilokuwemo Museveni likiendeshwa na Bibie huyu.
Hayo yote tisa, kumi leo hii Dr. Besigye kaamua kuyaanika yote yaliyojiri kule msituni na ni jinsi gani walikutana na bibie huyu.
Kama kawaida, Uganda ni nchi iliyojaa visa vya kisiasa vya kiume kweli si kama Tanzania, soma huyu mpinzani madhila aliyokwishapitia.
Inasemekana ugomvi kati ya Museveni na Besigye pia unachangiwa na kuibiana mabibi. Eti Bi. Byanyima awali alikuwa ni mtu wa karibu sana wa Museveni wakati wa vita ya msituni. Wakati huo Besigye akiwa kama daktari wa Museveni. Leo hii Bi. Byanyima ni mke wa Besyigye japo nakumbuka niliwahi kumsikia akihojiwa na redio moja Kampala na akadai kuwa eti Besigye ni mshirika wake tu(companion).
Wambeya wanadai eti siku waasi wa Museveni(NRA)wanaiteka na kuitwa Kampala, waliingia Kampala huku gari alilokuwemo Museveni likiendeshwa na Bibie huyu.
Hayo yote tisa, kumi leo hii Dr. Besigye kaamua kuyaanika yote yaliyojiri kule msituni na ni jinsi gani walikutana na bibie huyu.
Kama kawaida, Uganda ni nchi iliyojaa visa vya kisiasa vya kiume kweli si kama Tanzania, soma huyu mpinzani madhila aliyokwishapitia.
RAIS NA GAVANA UGANDA--WAWAKAMUA WALIPAKODI KWA BIASHARA BINAFSI
Mimi ni kati ya wasioamini adhabu ya kifo hata kama mtu kafanya nini. Ila nimeshangazwa sana na nchini Uganda hata katiba inaruhusu kama ilivyo pia kwetu Tanzania. Lingine ni hili la Rais Museveni na gavana wa benki kuu wameamua kutumia pesa za wali pakodi kumsaidia mfanyabiashara mmoja asifilisike.Ila inasemekana huyo mfanyabishara ni jamaa tu anasimamia shughuli za mzee.
Kama kawaida yangu napenda sana kujua inakuwaje watu wengine wanafanikiwa kimaisha wangali wadogo?
Kama kawaida yangu napenda sana kujua inakuwaje watu wengine wanafanikiwa kimaisha wangali wadogo?
Monday, November 27, 2006
MJUE GENERAL SALEH WA UGANDA
Leo nataka watu musome juu ya jamaa ambaye anajulikana kama shujaa hapa Uganda na ambaye ndie aliyesababisha kuanguka kwa serikali ya Obote.
Wednesday, November 22, 2006
MGAO WA UMEME UGANDA NI MIAKA MITATU SASA JE BONGO?
Huku tukiwa tunalaumu wanasiasa wetu juu ya labda hujuma au rushwa juu ya matatizo ya umeme nchini Tanzania kwa sasa, huko Uganda mgao wa umeme umekuweko kwa miaka mitatu sasa na ahadi kama hizi za hapa Bongo ni kawaida.
Mgao umeendelea hata pale serikali ya Uganda ilipobinafsisha shirika la Umeme kwa jamaa wale wa Afrika kusini kama tulivyofanya sisi.
Pia msome jinsi Museveni na Besyige walivyofanana.
Mgao umeendelea hata pale serikali ya Uganda ilipobinafsisha shirika la Umeme kwa jamaa wale wa Afrika kusini kama tulivyofanya sisi.
Pia msome jinsi Museveni na Besyige walivyofanana.
Saturday, November 18, 2006
NIMEKOSA MKUTANO
Wanaglobu nilijaribu kuingia ukumbini mambo yakashindikana na hivyo nikakosa kikao, inasikitisha sana.
Bassi leo nikasoma haya:Soma zaidi juu ya historia ya mtu mweusi, je kalaaniwa na Mungu? Pia hebu tujue zaidi ni kwa vipi chama tawala nchini Uganda kinavyoruhusu demokrasia?
Alafu huyyu jamaa namzimia kweli kashinda tuzo ya UN.
Bassi leo nikasoma haya:Soma zaidi juu ya historia ya mtu mweusi, je kalaaniwa na Mungu? Pia hebu tujue zaidi ni kwa vipi chama tawala nchini Uganda kinavyoruhusu demokrasia?
Alafu huyyu jamaa namzimia kweli kashinda tuzo ya UN.
Friday, November 17, 2006
JOJI KICHAKA ANASAIDIWA NA BABA YAKE
Baba yake Joji Kichaka karudi kumkomboa mwanaye.pIA soma jinsi mpanga mikakati wa Bush alivyochemsha.
Thursday, November 16, 2006
UKIMWI, MADEREVA WALEVI-FAIDA KWA UCHUMI
Leo nawapa vituko vya jamaa mmoja mcheshi kwelikweli. Eti anadai Ukimwi ni dili kwa bara la Afrika na ukiangamizwa, bara letu halitapata misaada.Alafu anaongeza zaidi kwamba uendeshaji magari wakati mtu ni mlevi ni faida kwa uchumi wa nchi.
KUPINDISHA HABARI(SPIN) KUNA MWISHO WAKE
Yuko jamaa mmoja alikuwa ni mwandishi mpambe haswa wa Raisi Museveni. Nakwambia alijua kazi yake haswa ya kupindisha habari (spin).Inasemekana ukweli umemsuta kaachana na Museveni sasa.
Ukiacha mambo ya habari tuangalie ni kwanini wanafunzi wanagoma haswa kule Makerere?Leo pia niwaletee hadithi juu ya mapambano ya msituni wakati Museveni alipozimia vitani kama inavyoelezewa na Dk. Kiiza Besyige aliyekuwa daktari wa Museveni. Alafu ni jinsi gani ukabila ulichangia kuuawa kwa waheshimiwa kadhaa hapa Uganda wakati ule wa vita kila kukicha.
Ukiacha mambo ya habari tuangalie ni kwanini wanafunzi wanagoma haswa kule Makerere?Leo pia niwaletee hadithi juu ya mapambano ya msituni wakati Museveni alipozimia vitani kama inavyoelezewa na Dk. Kiiza Besyige aliyekuwa daktari wa Museveni. Alafu ni jinsi gani ukabila ulichangia kuuawa kwa waheshimiwa kadhaa hapa Uganda wakati ule wa vita kila kukicha.
Wednesday, November 08, 2006
OMBAOMBA WA AFRIKA CHINA
Eti marais wa afrika kule China walikuwa makini au ombaomba tu?Alafu huko China tunaambiwa Museveni alifanya mambo ya kihistoria.Wakati Tanzania tumemaliza kipindi cha jeshi letu la polisi kupoteza mwelekeo kutokana na Kamanda wa polisi wa hovyo, huko Uganda hebu msome IGP wa kule ni mtu gani na umfananishe na alipita kwetu "MAHITA".
Alafu kuhusu dini kuna wanaoamini watu weusi tumelaaniwa na Mungu. Ila huyu anakataa katakata.Pia kama mtu wa ukanda huu wa afrika, je jumuiya yetu tuianze?
Mwisho waafrika eti tumezidi kupenda watoto wadogo visivyo?
Alafu kuhusu dini kuna wanaoamini watu weusi tumelaaniwa na Mungu. Ila huyu anakataa katakata.Pia kama mtu wa ukanda huu wa afrika, je jumuiya yetu tuianze?
Mwisho waafrika eti tumezidi kupenda watoto wadogo visivyo?
KUWAJIBIKA TANZANIA MPAKA UTOE ROHO YA MTU--JK
Hapa Tanzania wanasema "hapa ndipo patamu" yaani Anko Dito, naye yuko maabusu baada ya kutuhumiwa kuua raia mwema.Natizama tukio hili kama dhihirisho la wanasiasa wamangimeza wa kiafrika. Ulevi wa ukubwa unamfanya mtu kujichukulia madaraka mikononi mwake, kwani atafanywa nini?
Dito, ni mzalendo wa hali ya juu ninavyofikiri ndio maana JK hata aliweza kumpa madaraka.Ni kati ya vigogo wasioshikika nchi hii naweza kusema"untouchable".Ndio maaana nina wasiwasi sidhani kama atapatikana na hatia baada ya sheria kufuata mkondo wake.
Jana kasifiwa eti kujiuzulu ni kitendo bora kutokana na tuhuma anazokabiliana nazo. Kauli ya JK katika kukubali kujiuzulu kwake imenifanya nipate swali moja kwa wanaglobu wote: JE NI MPAKA MTU ATUHUMIWE KUTOA ROHO YA MWANANCHI MWENZAKE NDIO ANAJIUZULU? Nauliza hivi kwani hivi majuzi wako wakuu wa wilaya: HAWA NGULUME na Mheshimiwa fulani SABAYA wanatuhumiwa kupiga wananchi makofi na vyombo vya habari vimeamua kulamba miguu na kutovalia njuga ukiukaji huu wa haki za binadamu.
Yuko pia muheshimiwa mpendwa sana, POMBE MAGUFULI, tayari ana tuhuma kibao za ukiukaji wa maadili ya kazi, naye pia rais haoni kuna haja ya kumuwajibisha.
Tukiendelea hivi tutafika? Au mpaka mtu aue tu ndio tutawajibika?Wanablog mnasemaje hapa?
Dito, ni mzalendo wa hali ya juu ninavyofikiri ndio maana JK hata aliweza kumpa madaraka.Ni kati ya vigogo wasioshikika nchi hii naweza kusema"untouchable".Ndio maaana nina wasiwasi sidhani kama atapatikana na hatia baada ya sheria kufuata mkondo wake.
Jana kasifiwa eti kujiuzulu ni kitendo bora kutokana na tuhuma anazokabiliana nazo. Kauli ya JK katika kukubali kujiuzulu kwake imenifanya nipate swali moja kwa wanaglobu wote: JE NI MPAKA MTU ATUHUMIWE KUTOA ROHO YA MWANANCHI MWENZAKE NDIO ANAJIUZULU? Nauliza hivi kwani hivi majuzi wako wakuu wa wilaya: HAWA NGULUME na Mheshimiwa fulani SABAYA wanatuhumiwa kupiga wananchi makofi na vyombo vya habari vimeamua kulamba miguu na kutovalia njuga ukiukaji huu wa haki za binadamu.
Yuko pia muheshimiwa mpendwa sana, POMBE MAGUFULI, tayari ana tuhuma kibao za ukiukaji wa maadili ya kazi, naye pia rais haoni kuna haja ya kumuwajibisha.
Tukiendelea hivi tutafika? Au mpaka mtu aue tu ndio tutawajibika?Wanablog mnasemaje hapa?
Saturday, October 28, 2006
ETI MKAPA AANZE KUPOKEA TUZO YA UTAWALA BORA?
Wengi nadhani Tumesikia eti Maraisi wa Afrika sasa watapewa zawadi kama watatawala kwa ubora.
Jamaa huko Uganda kapendeza eti Mkapa apewe tuzo hiyo kama kifuta jasho.
Jamaa huko Uganda kapendeza eti Mkapa apewe tuzo hiyo kama kifuta jasho.
Friday, October 27, 2006
NILICHOSOMA
Yuko bibie Kampala hapa inaelezwa ni wanaume wenye sifa zipi watamfaa?
Kisiasa, kuna kitabu juu ya udanganyifu wa Marekani hapa duniani.
Kisiasa, kuna kitabu juu ya udanganyifu wa Marekani hapa duniani.
MAMBO YA JAMII LEO
Napenda Chuo hiki cha elimu ya juu Nkozi University. Kuna jamaa kaoa ndugu yake wa damu, yaani dada yake.Ulishasikia haya? Wanawake wa Uganda na malove.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.
MAMBO YA JAMII LEO
Napenda Chuo hiki cha elimu ya juu Nkozi University. Kuna jamaa kaoa ndugu yake wa damu, yaani dada yake.Ulishasikia haya? Wanawake wa Uganda na malove.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.
Kuhusu yule fashisti Idi Amin alipompindua Obote alitoa sababu kumi na moja za mapinduzi. Pia nchi ya Uganda inaye askari mkakamavu na msomi, msome hapa.
Mambo ya maisha ya ndoa ni misuguano mitupu; kwenye siasa napo Kagame bado anamuumbua Museveni.
Sunday, October 15, 2006
Saturday, October 14, 2006
HANA MFANO
Nyerere haenziwi kabisa.Je tunajua asili ya waafrika ni wapi?
Alafu wale wanaoanza gemu la penzi, unajua ya muhimu hapo awali?Kwa wanaume je twajua akina mama na dada siku hizi wanapennda sana pesa?
Huu ni wasifu wa mtu ninayemhusudu sana.
Alafu wale wanaoanza gemu la penzi, unajua ya muhimu hapo awali?Kwa wanaume je twajua akina mama na dada siku hizi wanapennda sana pesa?
Huu ni wasifu wa mtu ninayemhusudu sana.
Friday, October 13, 2006
UGANDA NA SALA ZA KILOKOLE
Yuko Jaji Mmoja maarufu nchini Uganda ambaye anakerwa sana na wanasiasa wa nchi hii. Basi katunga shairi babu kubwa juu ya uzandiki wa wanasiasa wa Uganda.
Kituko kingine cha wanasiasa ni tabia ya akina Museveni na mkewe kupenda kuhudhuria sala za kilokole kuiombea nchi kitu kinachoonekana hakina msaada wowote kwa nchi.Sala inaonekana ni ulevi wa wanasiasa.
Je wajua kuwa soko huria ndio balaa kuu la umasikini uliokithiri Africa? Alafu gazeti la serikali Uganda, hatimaye lamfukuza kazi meneja wake mzungu.
Kituko kingine cha wanasiasa ni tabia ya akina Museveni na mkewe kupenda kuhudhuria sala za kilokole kuiombea nchi kitu kinachoonekana hakina msaada wowote kwa nchi.Sala inaonekana ni ulevi wa wanasiasa.
Je wajua kuwa soko huria ndio balaa kuu la umasikini uliokithiri Africa? Alafu gazeti la serikali Uganda, hatimaye lamfukuza kazi meneja wake mzungu.
KUMBUKUMBU YA OBOTE BAADA YA MWAKA.
Hii ni wiki kubwa sana ya kuwakumbuka waasisi wa Afrika Mashariki. Kwanza jana imekuwa siku ya kumkumbuka Milton Obote, rais wa kwanza wa Uganda. Mkewe kaongea juu ya mumewe hasa ni yapi yanayomfanya amkumbuke.Obote kama binadamu anazo pande mbili hebu zisome:Pia ujue hivi ni upi mchango wa Obote katika siasa za Uganda na Afrika na alikuwa ni mtu wa aina gani?
Ukiacha kumbukumbu, huko Uganda baraza la mawaziri wanakosoana sio kama hapa kwetu Tanzania tunaoneana aibu na kufunika kombe mwanaharamu apite.Pia Uganda tunakumbushwa kuwa panapokuwa na amani sana basi ujue haki hakuna kabisa.
Mambo ya mahusiano, je una mpango wa kuchumbia siku za karibuni?Mwisho soma juu ya wanamuziki wa Uganda.
Ukiacha kumbukumbu, huko Uganda baraza la mawaziri wanakosoana sio kama hapa kwetu Tanzania tunaoneana aibu na kufunika kombe mwanaharamu apite.Pia Uganda tunakumbushwa kuwa panapokuwa na amani sana basi ujue haki hakuna kabisa.
Mambo ya mahusiano, je una mpango wa kuchumbia siku za karibuni?Mwisho soma juu ya wanamuziki wa Uganda.
Saturday, October 07, 2006
WABUNGE WA UGANDA NA MAGARI YA KIFAHARI
La msingi kabisa ni Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kuna mpango umeandaliwa wa kukusanya maoni ya watu.Je ni sahihi kuutekeleza?
Leo soma haya ya wabunge wa Uganda wamehongwa na serikali yao. Wale wapenda kandanda soma uone ni timu gani angalau zinahisiwa kushinda kombe la mabingwa.
Alafu inaaminika eti Waafrika tumelaaniwa:
Leo soma haya ya wabunge wa Uganda wamehongwa na serikali yao. Wale wapenda kandanda soma uone ni timu gani angalau zinahisiwa kushinda kombe la mabingwa.
Alafu inaaminika eti Waafrika tumelaaniwa:
Friday, October 06, 2006
Eti JK kadhihakiwa?
Kuna ile katuni ambayo serikali pamoja na wanahabari wa TZ wanadai ni dhihaka kwa JK na watanzania kwa ujumla.
Eti siasa Uganda ni ndege iliyo safarini, itafika. Alafu jisomee ujichekee vituko vya vigogo wa Uganda.
Eti siasa Uganda ni ndege iliyo safarini, itafika. Alafu jisomee ujichekee vituko vya vigogo wa Uganda.
Wednesday, October 04, 2006
Leo
Kuna watu na mafanikio yao pamoja na malengo.Ili kupambana na ukimwi tunaambiwa eti jibu ni ABC je hili kweli?
Pia unapoona vichaa wengi siku hizi ni dalili za umasikini eti.
Pia unapoona vichaa wengi siku hizi ni dalili za umasikini eti.
Sunday, September 10, 2006
LEO NI SIASA CONGO NA UGANDA
Mambo ya kupambana na rushwa sio mcezo, hapa kuna njia mbadala zinapendekezwa. Pia magari ya wabunge ni ulaji mtupu wa vigogo nchini Uganda, je umasikini utakwisha kweli? Hili la kushangaza manake inasemekana si Kabila wala Bemba anayestahili kugombea urais nchini Jamhuri ya kidmokrasia ya Congo. Si Congo tu ila eti hata Uganda sasa iko chini ya serikali ya maharamia, unajua?
Alafu kuna mtu kasema "Ushoga na Ufirauni" haukubaliki Afrika. Alafu soma ilivyo ngumu kuzuia uvunjaji wa haki za binadamu serikalini.
Alafu kuna mtu kasema "Ushoga na Ufirauni" haukubaliki Afrika. Alafu soma ilivyo ngumu kuzuia uvunjaji wa haki za binadamu serikalini.
Thursday, September 07, 2006
KUHAMAHAMA VYAMA SIASA
Kwa wale wanasiasa uchwara ambao hawaishi kuhamahama vyama basi hii ya kule Uganda ndio funzo. Jamaa alikuwa mkuu wa majeshi lakini sasa ndie kati ya wapinzani wakuu na hana mpango wa kurejea chama tawala. Alafu sisi watanzania tunafikiri ni Mkapa tu kauza nchi yetu kule Uganda Museveni pia kagenisha na wazawa hawana chao.
Pia ona jinsi Maadili yalivyoshuka na kuathiri jammi za kiafrika.
Pia ona jinsi Maadili yalivyoshuka na kuathiri jammi za kiafrika.
Wednesday, August 30, 2006
SIKU YA GLOBU DUNIANI
Kesho ni siku ya blogu duniani. Nimerudi nyumbani Tanzania hivi karibuni na kwa sasa ninajaribu kutulia na kufuatilia hali huku nikijizatiti kutafuta kazi ya kufanya. Kazi ni shida sana kupata kama hauna baba au mjomba na akina shangazi serikalini au hata katika taasisi za binafsi. Lililopo mbele yangu ni kujiajiri mwenyewe nadhani niko sahihi.
Katika siku hii sina raha kabisa na ninaisikitikia Tanzania hasa katika sekta ya habari kwani hakuna majadiliano ya maana sana katika magazeti na redio zetu. Inaonekana ari mpya na nguvu mpya imeturudisha katika enzi za "Zidumu fikra za Mwenyekiti wa Chama cha........". Habari nyingi hapa ni kusifia utendaji wa wanasiasa na kutokuwakosoa kabisa.
Redio za FM kibao lakini wao dili ni kupiga mziki, vipindi vya majadiliano sio sana ila kama unataka ukweli kuhusu nchi hii soma globu. Tatizo ni watanzania wachache wanasoma globu.
Ziko globu tano ambazo nadhani ni bora kwangu na ningependa watu wasizikose kabisa: kwanza, ni hii ya Mpiga Picha Issa Michuzi ambapo tukio kuhusu Tanzania utalipata hata kama hauko nyumbani utafurahi sana na pia kwa kumbukumbu zote za nchi zipo. Pili ni Pambazuka kwani utapata habari kiuchambuzi na kiyakinifu kuhusu mauzauza yote ya wataanzania haswa wanasiasa na viongozi wake. Alafu kuna Miruko, yeye bwana anazungumza ukweli bila uficho, si mwoga kama walivyo watanzania wengi.Huyu si bendera fuata upepo.Blogu ya nne ni Kasri la Mwanazuoni, hapa huwa napata habari za upande ambao hutapata magazetini wala redioni.Huyu bwana ni kiboko huwa napenda nimsome tu. Mwisho kabisa ni globu kutoka Nigeria, hapa kuna mijadala ya kusisimua sana.
Katika siku hii sina raha kabisa na ninaisikitikia Tanzania hasa katika sekta ya habari kwani hakuna majadiliano ya maana sana katika magazeti na redio zetu. Inaonekana ari mpya na nguvu mpya imeturudisha katika enzi za "Zidumu fikra za Mwenyekiti wa Chama cha........". Habari nyingi hapa ni kusifia utendaji wa wanasiasa na kutokuwakosoa kabisa.
Redio za FM kibao lakini wao dili ni kupiga mziki, vipindi vya majadiliano sio sana ila kama unataka ukweli kuhusu nchi hii soma globu. Tatizo ni watanzania wachache wanasoma globu.
Ziko globu tano ambazo nadhani ni bora kwangu na ningependa watu wasizikose kabisa: kwanza, ni hii ya Mpiga Picha Issa Michuzi ambapo tukio kuhusu Tanzania utalipata hata kama hauko nyumbani utafurahi sana na pia kwa kumbukumbu zote za nchi zipo. Pili ni Pambazuka kwani utapata habari kiuchambuzi na kiyakinifu kuhusu mauzauza yote ya wataanzania haswa wanasiasa na viongozi wake. Alafu kuna Miruko, yeye bwana anazungumza ukweli bila uficho, si mwoga kama walivyo watanzania wengi.Huyu si bendera fuata upepo.Blogu ya nne ni Kasri la Mwanazuoni, hapa huwa napata habari za upande ambao hutapata magazetini wala redioni.Huyu bwana ni kiboko huwa napenda nimsome tu. Mwisho kabisa ni globu kutoka Nigeria, hapa kuna mijadala ya kusisimua sana.
Monday, August 28, 2006
MWISHONI MWA WIKI ILIYOKWISHA
Ukisikia serikali inapinga ukweli alafu anatokea mtu anaandika kujibu mapigo ndio haya ya Uganda.Kwenye kandanda wakati hatuna mechi yeyote ya kujipima nguvu Uganda itacheza na wapinzani wetu Burkinafaso. Matokeo wametoka sare, nasikia Tanzania tulimtuma mtu akapeleleze, sijui itakuwaje jumamosi.
Kwenye siasa nako unajua kuna waafrika mawakala wa mabepari?Kama unamfahamu profesa Maamdani ambaye alimfunda pia raisi wetu JK basi soma anasemaje juu ya umuhimu wa elimu na vyuo vikuu katika nchi?Profesa mwingine, Ali Mazrui yeye ana mengi juu Jumuiya ya Afrika Mashariki, eti tunahitaji miaka mingine arobaini.Kuna haja ya Bunge la vyama vya upinzani kuwa na malengo au visheni, je Uganda wanalo bunge la aina hii?Si hayya tu, ila huu ung'ang'anizi wa Museveni madarakani una uhusiano sana na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pia mapigano yamesimamishwa na waasi wa Uganda rasmi, je ni nani shujaa katika dhahama hili la miongo miwili?
Uchaguzi wa Congo DRC utatoa rais ambaye ana maslahi tofauti kwa Uganda awe Kabila au Bemba.
Huko Burundi kama kawaida jamaa wameanza kufungana jela eti watnataka kupinduana.Huku Jumuiya ya Afrika mashariki ikisuasua
Kama unataka kujua jinsi ya kuwa tajiri na kuishi raha mustarehe bila kukopakopa.
Mambo ya akina mama pia tunakumbushwa ni jinsi gani wanafurahia mabwana jua siri
Kwenye siasa nako unajua kuna waafrika mawakala wa mabepari?Kama unamfahamu profesa Maamdani ambaye alimfunda pia raisi wetu JK basi soma anasemaje juu ya umuhimu wa elimu na vyuo vikuu katika nchi?Profesa mwingine, Ali Mazrui yeye ana mengi juu Jumuiya ya Afrika Mashariki, eti tunahitaji miaka mingine arobaini.Kuna haja ya Bunge la vyama vya upinzani kuwa na malengo au visheni, je Uganda wanalo bunge la aina hii?Si hayya tu, ila huu ung'ang'anizi wa Museveni madarakani una uhusiano sana na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pia mapigano yamesimamishwa na waasi wa Uganda rasmi, je ni nani shujaa katika dhahama hili la miongo miwili?
Uchaguzi wa Congo DRC utatoa rais ambaye ana maslahi tofauti kwa Uganda awe Kabila au Bemba.
Huko Burundi kama kawaida jamaa wameanza kufungana jela eti watnataka kupinduana.Huku Jumuiya ya Afrika mashariki ikisuasua
Kama unataka kujua jinsi ya kuwa tajiri na kuishi raha mustarehe bila kukopakopa.
Mambo ya akina mama pia tunakumbushwa ni jinsi gani wanafurahia mabwana jua siri
Friday, August 25, 2006
FAMILIA YA MUSEVENI YAIFANYA NCHI MALI YAKE
Vituko vya marais wa Afrika ni vingi. Nchini Uganda, Museveni naye hakosi vituko hasa vya matumizi makubwa ya fedha.Andrew Mwenda anao uelewa wa ni nani hasa ni Museveni na jinsi familia ya rais huyo inavyoiibia nchi hiyo.
Imeripotiwa pia eti ili Kony aweze kumalizwa huko misitu ya Congo basi serikali ya Uganda iilipe Congo gharama ya uporaji iliyoufanya miaka kadhaa iliyopita.
Pia tunakumbushwa tusiogope ukosefu wa ajira kwani kuna namna ya kuishi bila kuajiriwa. Pia tunaambiwa kumbe hata maaskofu wa kikatoliki na makadinali wanastaafu.
Katika siasa, NRM kama mfano wa vyama tawala vinahitaji kitu kinaitwa Matangi ya Kufikiri--think tank. Pia nchini Uganda ni vizuri tumsome na kumjua afisa mmoja wa jeshi Brigedia Jenerali Tumukunde ambaye katiwa kizuizini kwa muda sasa eti kajaribu kutikisa mkuu wa dola.
Nirudi kwenye mazungumzo ya amani huko Uganda, kauwawa kamanda wa LRA ambaye inasemekana na aliyemjua kuwa alikuwa mnyama haswa. Pia nigusie mambo ya ofisini haswa tabia ya mahusiano ya kijinsia na mabosi.
Kwenye kandanda je kuna tofauti kati ya makocha wa Ulaya na wa kwetu hapa Bongo?Pia suala la nidhamu kwenye timu za kandanda kama Taifa Stars.
Imeripotiwa pia eti ili Kony aweze kumalizwa huko misitu ya Congo basi serikali ya Uganda iilipe Congo gharama ya uporaji iliyoufanya miaka kadhaa iliyopita.
Pia tunakumbushwa tusiogope ukosefu wa ajira kwani kuna namna ya kuishi bila kuajiriwa. Pia tunaambiwa kumbe hata maaskofu wa kikatoliki na makadinali wanastaafu.
Katika siasa, NRM kama mfano wa vyama tawala vinahitaji kitu kinaitwa Matangi ya Kufikiri--think tank. Pia nchini Uganda ni vizuri tumsome na kumjua afisa mmoja wa jeshi Brigedia Jenerali Tumukunde ambaye katiwa kizuizini kwa muda sasa eti kajaribu kutikisa mkuu wa dola.
Nirudi kwenye mazungumzo ya amani huko Uganda, kauwawa kamanda wa LRA ambaye inasemekana na aliyemjua kuwa alikuwa mnyama haswa. Pia nigusie mambo ya ofisini haswa tabia ya mahusiano ya kijinsia na mabosi.
Kwenye kandanda je kuna tofauti kati ya makocha wa Ulaya na wa kwetu hapa Bongo?Pia suala la nidhamu kwenye timu za kandanda kama Taifa Stars.
Friday, August 18, 2006
MAMBO YA MSINGI
Unajua umuhimu wa michezo mashuleni? Unajua inasemekana Museveni ndio anaimaliza kabisa Uganda?
Ni vizuri pia tuelewe ni kwanini Wazungu wameamua kutunyonya kabisa. Mazungumzo ya Doha yamevunjika, kwanini lakini?
Ni vizuri pia tuelewe ni kwanini Wazungu wameamua kutunyonya kabisa. Mazungumzo ya Doha yamevunjika, kwanini lakini?
YA WIKI HII
Kuna tabia ya kuhamahama kutoka upinzani kwenda chama tawala. Alafu nchini Uganda, Raisi pekee anatumia mamilioni ya shilingi kulipa washauri wake ambao ni wengi lukuki. Soma simulizi la mwandishi maarufu nchini Uganda alipokuwa lupango.
Nchini Uganda rushwa ndio haswa, je unajua wataalam wanaeleza rushwa ni nini? Je Raisi anaweza tu kuamua kufanya ziara binafsi?
Nchini Uganda rushwa ndio haswa, je unajua wataalam wanaeleza rushwa ni nini? Je Raisi anaweza tu kuamua kufanya ziara binafsi?
Saturday, August 12, 2006
LEO
Kuna hili la ufisadi Uganda alafu eti siasa ni mbaya kwa maendeleo. Pia unamjua Kony alivyo sasa?Alafu ona jinsi matajiri wanavyoneemeka na elimu bora Ugaanda.
Yuko jamaa anatabiri Chelsea kushinda tena taji msimu huu.Na kwa wale kapera kama mie, tunahitaji wapanga sherehe za harusi?
Yuko jamaa anatabiri Chelsea kushinda tena taji msimu huu.Na kwa wale kapera kama mie, tunahitaji wapanga sherehe za harusi?
Friday, August 04, 2006
YALIYONIVUTIA LEO
Wakati bado timu yetu haijaanza maandallizi ya kwenda huko Ghana mwaka 2008, Uganda tayari kocha waao kaanza mambo. Tunaambiwa hata sex inataka maadili fulani yazingatiwe, unazijua?
Kuhusu politiki ni kuwa Museveni kaishiwa hana hela, rushwa imezidi na sasa chama tawala kinabidi kifunge shughuli katika ngazi za chini. Athari za Chama dola ndio hizi. Nikiwa kama bachela mzoefu basi mambo ya mapishi ni vyema niyapitie.
Angalia ukubwa wa Afrika ulivyo, hapa rais anapopita anaweza akasababisha hata mauaji.Alafu ligi ya Uingereza ndio inakaribia.
Kama unamjua Joseph Kony pata undani wa maisha yake ya sasa. Je ilikuwaje Mapinduzi yakatokea Uganda?
Kuhusu politiki ni kuwa Museveni kaishiwa hana hela, rushwa imezidi na sasa chama tawala kinabidi kifunge shughuli katika ngazi za chini. Athari za Chama dola ndio hizi. Nikiwa kama bachela mzoefu basi mambo ya mapishi ni vyema niyapitie.
Angalia ukubwa wa Afrika ulivyo, hapa rais anapopita anaweza akasababisha hata mauaji.Alafu ligi ya Uingereza ndio inakaribia.
Kama unamjua Joseph Kony pata undani wa maisha yake ya sasa. Je ilikuwaje Mapinduzi yakatokea Uganda?
Wednesday, August 02, 2006
Saturday, July 15, 2006
SALA KUONDOA RUSHWA?
Kweli sala na mafungo ndio dawa ya Rushwa?Pia mambo ya imani yapo kweli?Na siasa mwanzo wake je?
Mpira huu ni mwaka wa Chelsea tena?Je kashfa kubwa mpirani?
Mpira huu ni mwaka wa Chelsea tena?Je kashfa kubwa mpirani?
Friday, July 14, 2006
UGANDA KUNASEMAJE?
Baada ya kimya kirefu leo niangaze yanayojiri nchini Uganda: kuna huyu bwana anatuhumiwa kuuwa mkewe. Katika kesi yake anaonekana kujiamini sana kitu kinachowashangaza wengi. Alafu kama ilivyo kawaida, siku hizi tunawaza pesa tu haswa wengi wetu. Matokeo yake hata kazi zetu kwa mfano wachapishaji wa magazeti maadili ya kazi yameshuka sana. Pia nchi ya Uganda inatamani kuwa na mafuta lakini inakumbushwa kuwa hiyo ni balaa kwa Afrika na ni hatari kwa demokrasia.
Baada ya kombe la dunia hebu tujue ni nini kinasemwa pia kuhusu kosa la Zidane? Alafu kuna Padri wa Kikatoliki uzalendo umemshinda na kaamua kuvunja sheriia za useja. Pia tunakumbushwa juu ya ongezeko la ugonjwa wa moyo. Nini kifanyike?
Mwisho vipi kuhusu Kony?
Baada ya kombe la dunia hebu tujue ni nini kinasemwa pia kuhusu kosa la Zidane? Alafu kuna Padri wa Kikatoliki uzalendo umemshinda na kaamua kuvunja sheriia za useja. Pia tunakumbushwa juu ya ongezeko la ugonjwa wa moyo. Nini kifanyike?
Mwisho vipi kuhusu Kony?
Thursday, June 08, 2006
VIROJA KATIKA VIAPO UGANDA
Wednesday, May 24, 2006
BARAZA LA MAWAZIRI LA MUSEVENI HILO!
Hatimaye Rais Museveni kachagua baraza la mawaziri na kama ilivyotarajiwa kamchagua mdogo wake ambaye ni ofisa wa jeshi aliyeishia kidato cha sita kuwa waziri wa fedha. Huko nyuma Museveni aliwahi kumtimua kazini kwa kisingizio cha ulevi kupindukia.
Mambo ya ufalme labda ndiyo yanaanza hebu tusubiri. Maajabu ni huyu Eliya Kategaya ambaye alimpinga sana juu ya kung'ang'ania madaraka sasa kawa waziri.
Yamesemwa mengi juu ya sababu za uteuzi wa mawaziri mbalimbali. Pia kama kawaida ya Uganda, uongozi umekwenda kwa watu wa mashariki, yaani kule alikozaliwa Museveni. Hata jamaa mmoja kadai eti anaota mji mkuu wa Uganda ukahamia "RWAKITURA" kijijini kwa Museveni siku chache zijazo.
Mawaziri ni wapya wengi na hasa vijana.
Mambo ya ufalme labda ndiyo yanaanza hebu tusubiri. Maajabu ni huyu Eliya Kategaya ambaye alimpinga sana juu ya kung'ang'ania madaraka sasa kawa waziri.
Yamesemwa mengi juu ya sababu za uteuzi wa mawaziri mbalimbali. Pia kama kawaida ya Uganda, uongozi umekwenda kwa watu wa mashariki, yaani kule alikozaliwa Museveni. Hata jamaa mmoja kadai eti anaota mji mkuu wa Uganda ukahamia "RWAKITURA" kijijini kwa Museveni siku chache zijazo.
Mawaziri ni wapya wengi na hasa vijana.
Monday, May 22, 2006
Thursday, May 18, 2006
MARAISI "SUPA GLUU"-AFRIKA
Kuna malalamishi ambayo yanafurahisha juu ya hatua ya marais wa Afrika kuunga mkono wenzao wanaong'ang'ania madaraka.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.
MARAISI "SUPA GLUU"-AFRIKA
Kuna malalamishi ambayo yanafurahisha juu ya hatua ya marais wa Afrika kuunga mkono wenzao wanaong'ang'ania madaraka.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.
Saturday, May 13, 2006
IGIZO LA KIAPO CHA MFALME MUSEVENI WA UGANDA
Kama ilivyotarajiwa jana Rais Kaguta Museveni aliapishwa na jaji mkuu kwa mara nyingine kuendelea na ngwe nyingine ya miaka mitano katika viwanja vya Kololo jijini Kampala. Ametoa rai kwa vyama vya upinzani viwe makini ili kuweza kushirikiana naye.
Pia alipata wasaa wa kuelezea mipango ya baadaye na hata mafanikio aliyoyapata kwa miaka ishirini iliyopita.Katika sherehe za jana vyama vya upinzani hasa vile vyenye wafuasi wengi havikuhudhuria katika kile kinachoonekana kama kutomkubali Museveni kama rais halali. Pamoja na kung'ang'ania madaraka kwa Museveni lakini huwezi kuamini hadi leo ni miaka miwili Uganda ina mgao wa Umeme usiokwisha na watu wanaanza kumlalamikia sana.
Mwanzoni kabla ya kula kiapo ilisemekana hata rais Hu Jintao wa China angehudhuria katika kile kinachodaiwa kama mkakati mpya wa Museveni katika kujikita katika siasa za nchi za ukanmda wa maziwa makuu.
Pia alipata wasaa wa kuelezea mipango ya baadaye na hata mafanikio aliyoyapata kwa miaka ishirini iliyopita.Katika sherehe za jana vyama vya upinzani hasa vile vyenye wafuasi wengi havikuhudhuria katika kile kinachoonekana kama kutomkubali Museveni kama rais halali. Pamoja na kung'ang'ania madaraka kwa Museveni lakini huwezi kuamini hadi leo ni miaka miwili Uganda ina mgao wa Umeme usiokwisha na watu wanaanza kumlalamikia sana.
Mwanzoni kabla ya kula kiapo ilisemekana hata rais Hu Jintao wa China angehudhuria katika kile kinachodaiwa kama mkakati mpya wa Museveni katika kujikita katika siasa za nchi za ukanmda wa maziwa makuu.
Sunday, May 07, 2006
J 2 YA LEO
Kama kawaida kila jumapili ninaangaza magazeti ya hapa Uganda na kwingineko. Kwa akina mama wajawazito ipo makala ya jinsi ya kujipendezesha. Alafu kuna hili la mameneja wa kiume kuongoza kwa kuwachukulia wafanyakazi wao kama wanawake.
Saturday, May 06, 2006
WAGOMBEA BINAFSI WAJA
Kwa mara nyingine mahakama nchini Tanzania imeruhusu wagombea binafsi. Huu ni ushindi wa demokrasia lakini sina hakika kama una mantiki yeyote ukizingatia demokrasia yetu changa.
Wengi wamefurahia ila ni lazima turuhusu muda tuone kwani hata nchini Uganda katika uchaguzi uliokwisha hivi majuzi pia wamechaguliwa wagombea binafsi.
Wengi wamefurahia ila ni lazima turuhusu muda tuone kwani hata nchini Uganda katika uchaguzi uliokwisha hivi majuzi pia wamechaguliwa wagombea binafsi.
Friday, May 05, 2006
UNAMJUA RAIS AJAYE WA UGANDA?
Huku Uganda ikiwa inasubiri kwa hamu kuapishwa kwa Rais wa Maisha, Yoweri Kaguta Museveni hapo wiki ijayo ni wazi mtu huyu hapendwi ila king'ang'anizi tu.
Naona ni hivyo kwani kwa sasa hadithi kubwa ni juu ya nani atamrithi Museveni atakapoamua kung'atuka. Wako wengi ila huyu waziri wa ulinzi ndiye anayeonekana atakuwa rais ajaye wa Uganda.
Si haya tu ya kumrithi ila inaonekana bado serikali ya Museveni inatumia kila mbinu hata zile chafu kabisa kumtia hatiani mpinzani wake Kiiza Besigye. Hapo jana serikali iliamua kumleta mahakamani mmoja wa makamanda wa jeshi la waasi wa LRA kuja kutoa ushahidi. Nakwambia hii inaonekana ni hatua ya ajabu kabisa. Kwani hapa hata serikali inatumia wauaji ili kumtia hatiani bwana Besigye. Mawakili hawakuwa tayari kuendelea na kesi na wanataka kwanza shahidi asimamishwe juu ya koti ili ajibu mashtaka ya mauaji na ugaidi. Hali hii inafanya wanazuoni kuhoji labda hii vita ya waasi wa LRA haishi kwani kuna mkono wa serikali. Kuwatumia waasi kutoa ushahidi mahakamani kunachukuliwa kama dhihirisho la kuwepo na uhusiano kati ya serikali na waasi kwa kiasi fulani. Mwenyewe Rais Museveni hivi karibuni kazungumza kinagaubaga juu ya mzozo huu wa miaka ishirini.
Ni wazi ingawa Museveni alishinda uchaguzi majuzi, kwasasa ana kazi kubwa kuunda serikali yenye mvuto. Sasa ameanza kuwashawishi baadhi ya wanasiasa waliokuwa naye wakati akipambana msituni ambao walimkimbia na wengine aliwafukuza pale, walipopinga kampeni yake maarufu kama "EKISANJA" ya kubadili katiba ili aendelee kuwa rais wa maisha, anataka wajiunge serikali mpya atakayounda baada ya kuapishwa wiki ijayo.
Familia nzima ya Museveni sasa imeamua kujikita kwenye siasa za nchi hii kiasi kwamba kuna kila dalili hapa ni mambo ya kurithishana yatafuata pale Museveni atakapokuwa amemaliza muda wake. Kwa mfano, hata mwanaye wa kiume Museveni, ambaye afisa wa jeshi la hapa sasa kaanza kuandika makala za kisiasa hasa akiunga mkono shirikisho la Afrika Mashariki, kitu ambacho kinapigiwa upatu sana na Museveni.
Naona ni hivyo kwani kwa sasa hadithi kubwa ni juu ya nani atamrithi Museveni atakapoamua kung'atuka. Wako wengi ila huyu waziri wa ulinzi ndiye anayeonekana atakuwa rais ajaye wa Uganda.
Si haya tu ya kumrithi ila inaonekana bado serikali ya Museveni inatumia kila mbinu hata zile chafu kabisa kumtia hatiani mpinzani wake Kiiza Besigye. Hapo jana serikali iliamua kumleta mahakamani mmoja wa makamanda wa jeshi la waasi wa LRA kuja kutoa ushahidi. Nakwambia hii inaonekana ni hatua ya ajabu kabisa. Kwani hapa hata serikali inatumia wauaji ili kumtia hatiani bwana Besigye. Mawakili hawakuwa tayari kuendelea na kesi na wanataka kwanza shahidi asimamishwe juu ya koti ili ajibu mashtaka ya mauaji na ugaidi. Hali hii inafanya wanazuoni kuhoji labda hii vita ya waasi wa LRA haishi kwani kuna mkono wa serikali. Kuwatumia waasi kutoa ushahidi mahakamani kunachukuliwa kama dhihirisho la kuwepo na uhusiano kati ya serikali na waasi kwa kiasi fulani. Mwenyewe Rais Museveni hivi karibuni kazungumza kinagaubaga juu ya mzozo huu wa miaka ishirini.
Ni wazi ingawa Museveni alishinda uchaguzi majuzi, kwasasa ana kazi kubwa kuunda serikali yenye mvuto. Sasa ameanza kuwashawishi baadhi ya wanasiasa waliokuwa naye wakati akipambana msituni ambao walimkimbia na wengine aliwafukuza pale, walipopinga kampeni yake maarufu kama "EKISANJA" ya kubadili katiba ili aendelee kuwa rais wa maisha, anataka wajiunge serikali mpya atakayounda baada ya kuapishwa wiki ijayo.
Familia nzima ya Museveni sasa imeamua kujikita kwenye siasa za nchi hii kiasi kwamba kuna kila dalili hapa ni mambo ya kurithishana yatafuata pale Museveni atakapokuwa amemaliza muda wake. Kwa mfano, hata mwanaye wa kiume Museveni, ambaye afisa wa jeshi la hapa sasa kaanza kuandika makala za kisiasa hasa akiunga mkono shirikisho la Afrika Mashariki, kitu ambacho kinapigiwa upatu sana na Museveni.
Sunday, April 30, 2006
SHERIA DHIDI YA WABAKAJI YAKWAMA-KENYA
Wiki iliyopita mbunge mmoja mwanamama aliamua kupeleka muswaada bungeni ili kudhibiti ubakaji nchini humo. Matokeo yake inaonekana kagonga mwamba manake wabunge wanaume wamekuja juu na inasemekana muswaada hautapitishwa kuwa sheria.
Mwanamama mmoja kasema hii ni sababu za umangimeza wa wanaume wa Afrika. Ila kuna sababu imetolewa ni kwanini Wabunge waliamua kuzichachamalia hoja mbalimbali ndani ya muswaada huo. Vifungu mbalimbali vya muswaada huo vilikuwa na utata. Mkwamo huu dhidi ya kuwaadhibu wabakaji kwa kiasi kikubwa unachangiwa na kutobadilika kwa jamii nyingi za kiafrika hususan nchini Kenya ambapo wengine wanaamini hawawezi kuishi bila kufuata mila zenye kukandamiza wanawake kwani mababu wa zamani watachukia.
Mwanamama mmoja kasema hii ni sababu za umangimeza wa wanaume wa Afrika. Ila kuna sababu imetolewa ni kwanini Wabunge waliamua kuzichachamalia hoja mbalimbali ndani ya muswaada huo. Vifungu mbalimbali vya muswaada huo vilikuwa na utata. Mkwamo huu dhidi ya kuwaadhibu wabakaji kwa kiasi kikubwa unachangiwa na kutobadilika kwa jamii nyingi za kiafrika hususan nchini Kenya ambapo wengine wanaamini hawawezi kuishi bila kufuata mila zenye kukandamiza wanawake kwani mababu wa zamani watachukia.
URAFIKI WA TZ NA CHINA UMEFIFIA?
Mambo yamebadilika dunia ya leo. Sijui kama kuna umuhimu sana kwa Tanzania kutembelewa na kiongozi wa China ila niseme tu ziara ya rais Hu Jintao huko Nigeria na katika kituo chake cha mwisho nchini Kenya imenifanya niwaze vipi, kulikoni Tanzania.
Si tulikuwa washirika wakubwa sana wa China wakati wa Mwenyekiti Mao?Jibu nimelipata eti mwelekeo umebadilika duniani na China ya ujamaa sio hii ya leo. Zipo sababu kwanini China ni mshirika mzuri kwa nchi kama Kenya.
Kwa Wachina ziara ya hii Hu sehemu mbalimbali ni muhimu sana na hatuna haja ya kusikiliza kelele za Magharibi. Unajua kwa mfano sekta ya mafuta barani Afrika ambayo ilitawaliwa na magharibi sasa China nayo imeamua kuingia kwa nguvu hasa barani Afrika.
Si tulikuwa washirika wakubwa sana wa China wakati wa Mwenyekiti Mao?Jibu nimelipata eti mwelekeo umebadilika duniani na China ya ujamaa sio hii ya leo. Zipo sababu kwanini China ni mshirika mzuri kwa nchi kama Kenya.
Kwa Wachina ziara ya hii Hu sehemu mbalimbali ni muhimu sana na hatuna haja ya kusikiliza kelele za Magharibi. Unajua kwa mfano sekta ya mafuta barani Afrika ambayo ilitawaliwa na magharibi sasa China nayo imeamua kuingia kwa nguvu hasa barani Afrika.
LEO MAGAZETINI
Leo kuna mambo ya lugha yameandikwa jinsi jamii ilivyogawanyika na kama mtu hauko makini unaweza shindwa muelewa mwenzako katika mazungumzo. Alafu Madaraka Nyerere anatukumbusha juu ya hii dhahama ya silaha za nyuklia kati ya Marekani na Iran na anasema kuwa na silaha hizi ni sababu ya kupunguza mizozo duniani. Mwanazuoni Ali Mazrui anatukumbusha jinsi ilivyo vigumu kwa nchi za Afrika kuungana. Ugomu ambao umejionesha pia katika muungano wa Tanzania ni dalili ya ugumu wa kuunganisha bara la Afrika ukiachilia mbali hii gumzo ya kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki ambapo mwandishi mmoja kaonya nini labda kifanyike ili kufikia mafanikio.
Hapa Uganda tatizo ni umeme hakuna na hakuna mtu anayejali. Ila inasemekana ziko sababu kwanini kwa waganda hili sio tatizo la kulalamikiwa. Si umeme tu ila Uganda ina mambo kwelikweli: kwa mfano, Uganda inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi za jumuiya ya Madola mwakani ambapo Malkia wa Uingereza atakuwa ndio mgeni mkubwa kabisa. La kushangaza kuna juhudi kubwa za baadhi ya Wapinzani za kupinga mkutano huo kufanyika hapa kabisa. Ila yuko Bibie mmoja kaandika labda ni nini kinagaubaga juu ya hili.
Mwisho ni hili la hiki kitabu Da Vince Code, mengi ya msingi yameandikwa juu ya ubishi ambao umegubika toleo hili. Pia tunaulizwa hivi ni kwanini tunasoma?
Hapa Uganda tatizo ni umeme hakuna na hakuna mtu anayejali. Ila inasemekana ziko sababu kwanini kwa waganda hili sio tatizo la kulalamikiwa. Si umeme tu ila Uganda ina mambo kwelikweli: kwa mfano, Uganda inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi za jumuiya ya Madola mwakani ambapo Malkia wa Uingereza atakuwa ndio mgeni mkubwa kabisa. La kushangaza kuna juhudi kubwa za baadhi ya Wapinzani za kupinga mkutano huo kufanyika hapa kabisa. Ila yuko Bibie mmoja kaandika labda ni nini kinagaubaga juu ya hili.
Mwisho ni hili la hiki kitabu Da Vince Code, mengi ya msingi yameandikwa juu ya ubishi ambao umegubika toleo hili. Pia tunaulizwa hivi ni kwanini tunasoma?
Friday, April 28, 2006
JOJI KICHAKA MAMBO MRAMA?
Leo nimesoma blog moja kutoka huko Amerika kwa Joji Kichaka. Kwa mfano hata hili shirika la ujasusi, CIA, mambo si shwari kwani Joji Kichaka kamfuta kazi bosi wa shirika hilo. Halafu hali ya mzozo wa silaha za nyuklia na Iran ndio inafanya mambo yawe magumu kwa Kichaka.
Tuesday, April 25, 2006
Ile sheria kandamizi-TAKRIMA-dhidi ya makabwera imefutiliwa mbali na mahakama ya katiba nchini Tanzania. Sijui watu kama Fredrick Sumaye na Andrew Chenge watakuwa na mawazo gani. Unajua nilifuatilia hotuba zao bungeni wakati wa kuundwa sheria hii nikachukizwa sana na maoni yao.
La msingi nimefurahi sana kwani angalau maana ya demokrasia inajionesha. Kuna utafiti nimefanya kuhusu hali ya kisiasa ya jimbo la Vunjo kule Moshi Tanzania ninatarajia kuuweka mtandaoni siku chache zijazo na pia nimejadili madhara ya sheria hii.
La msingi nimefurahi sana kwani angalau maana ya demokrasia inajionesha. Kuna utafiti nimefanya kuhusu hali ya kisiasa ya jimbo la Vunjo kule Moshi Tanzania ninatarajia kuuweka mtandaoni siku chache zijazo na pia nimejadili madhara ya sheria hii.
TFF NA SOKA LA TANZANIA USINGIZINI.
Wakati bado TFF haijampata kocha wa kuinoa timu ya Taifa-Taifa Stars-hapa Uganda viongozi wapya wa shirikisho la soka hapa Uganda-FUFA- tayari wamemleta mwalimu mpya wa timu hiyo kutoka Serbia. Kocha huyo ni Tomislav Sicic kutoka Serbia.
Viongozi wapya wa FUFA wameingia madarakani mapema mwaka huu tu na tayari wanafikiria juu ya safari ya timu hiyo ya Kombe la dunia na lile la Mataifa ya Africa.
Kama tunavyojua TFF walishaadiwa ushirikiano na Rais JK. Nataka tuwaulize hawa mabwana mbona wamelala? September si mbali wajameni. Nataka niangalie hii mikakati Tenga anayodai ipo je itafanikiwa?
Si soka tu ila Tanzania chini ya JK ni lazima ichukue hatua madhubuti ili kuendeleza michezo. Mimi ninaamini kama tutaendeleza michezo basi tutawainua vijana wengi ambao hawana ajira na hawatakaa waipate kutokana na fursa chache. Ninaunga mkono juhudi za serikali kufanikisha ziara ya timu ya ndondi wiki hii kwenda nchini Uhispania.
Hii ifanyike pia kwenye soka kwani ikiwa kombe la dunia litafanyika hapa Afrika hatuna budi tuanze leo kama wenzetu wa Uganda. Hainifurahishi kwa viongozi wa TFF kutuambia eti timu inakwenda Ushelisheli kwa mechi za kirafiki baada ya kualikwa huko. Pia eti Malawi imetualika kwa michezo ya kirafiki. Nasema hivi kwani inaonesha kwamba labda TFF hawana mipango madhubuti ila wanasubiri mialiko na kama isipokuja itakuwaje? Pia nataka nitoe rai ya makocha wazalendo hawakidhi haja ni muhimu tukawa na makocha kutoka Ulaya kwani tunahitaji mambo ambayo watanzania wenzangu hawana katika suala zima la kuiandaa timu ya Taifa. Kwa mfano, nina hakika kwa aina ya makocha tulionao nchini Tanzania si makini sana kwenye masuala ya kudhibiti wachezaji kinidhamu. Nidhamu ni msingi wa wachezaji kutekeleza wajibu wao na kama wachezaji wetu hawakai kambini na kufuata taratibu za kambi tusitarajie kufuzu kwenda Ghana au Afrika kusini 2010. Tayari hata katibu mkuu wa TFF, Tenga kakiri wachezaji wa Stars ni kama "chokaraa". Sijafurahishwa kabisa na hali ya sasa ambapo inabidi Tenga awakumbushe makocha akina Msola juu ya kutoa ruhusa. Hivi kweli tuna makocha wenye taaluma ya kutosha kuongoza timu ya Taifa? Jibu ni hatuna, hebu tujaribu kufuatilia timu kadhaa zitakapoanza kupiga kambi kwa ajili ya kombe la dunia kama utakuwa unasikia mchezaji kaomba ruhusa eti akachukue begi lake nyumbani kama wachezaji wetu wanavyofanya.
Alafu ni lazima tucheze na wapinzani wenye kutumia staili ya uchezaji kama ya wale tunaotarajia kukutana nao.Nionavyo mimi hii TFF bado ni kama FAT ya akina Rage na Ndolanga kwani bado sioni mabadiliko yenye kasi na ari mpya.
Viongozi wapya wa FUFA wameingia madarakani mapema mwaka huu tu na tayari wanafikiria juu ya safari ya timu hiyo ya Kombe la dunia na lile la Mataifa ya Africa.
Kama tunavyojua TFF walishaadiwa ushirikiano na Rais JK. Nataka tuwaulize hawa mabwana mbona wamelala? September si mbali wajameni. Nataka niangalie hii mikakati Tenga anayodai ipo je itafanikiwa?
Si soka tu ila Tanzania chini ya JK ni lazima ichukue hatua madhubuti ili kuendeleza michezo. Mimi ninaamini kama tutaendeleza michezo basi tutawainua vijana wengi ambao hawana ajira na hawatakaa waipate kutokana na fursa chache. Ninaunga mkono juhudi za serikali kufanikisha ziara ya timu ya ndondi wiki hii kwenda nchini Uhispania.
Hii ifanyike pia kwenye soka kwani ikiwa kombe la dunia litafanyika hapa Afrika hatuna budi tuanze leo kama wenzetu wa Uganda. Hainifurahishi kwa viongozi wa TFF kutuambia eti timu inakwenda Ushelisheli kwa mechi za kirafiki baada ya kualikwa huko. Pia eti Malawi imetualika kwa michezo ya kirafiki. Nasema hivi kwani inaonesha kwamba labda TFF hawana mipango madhubuti ila wanasubiri mialiko na kama isipokuja itakuwaje? Pia nataka nitoe rai ya makocha wazalendo hawakidhi haja ni muhimu tukawa na makocha kutoka Ulaya kwani tunahitaji mambo ambayo watanzania wenzangu hawana katika suala zima la kuiandaa timu ya Taifa. Kwa mfano, nina hakika kwa aina ya makocha tulionao nchini Tanzania si makini sana kwenye masuala ya kudhibiti wachezaji kinidhamu. Nidhamu ni msingi wa wachezaji kutekeleza wajibu wao na kama wachezaji wetu hawakai kambini na kufuata taratibu za kambi tusitarajie kufuzu kwenda Ghana au Afrika kusini 2010. Tayari hata katibu mkuu wa TFF, Tenga kakiri wachezaji wa Stars ni kama "chokaraa". Sijafurahishwa kabisa na hali ya sasa ambapo inabidi Tenga awakumbushe makocha akina Msola juu ya kutoa ruhusa. Hivi kweli tuna makocha wenye taaluma ya kutosha kuongoza timu ya Taifa? Jibu ni hatuna, hebu tujaribu kufuatilia timu kadhaa zitakapoanza kupiga kambi kwa ajili ya kombe la dunia kama utakuwa unasikia mchezaji kaomba ruhusa eti akachukue begi lake nyumbani kama wachezaji wetu wanavyofanya.
Alafu ni lazima tucheze na wapinzani wenye kutumia staili ya uchezaji kama ya wale tunaotarajia kukutana nao.Nionavyo mimi hii TFF bado ni kama FAT ya akina Rage na Ndolanga kwani bado sioni mabadiliko yenye kasi na ari mpya.
Sunday, April 23, 2006
RUBANI MLEVI--CHANZO CHA AJALI KENYA
Wajameni eti ile ajali ya ndege kule Kenya siku chache zilizopita ilisababishwa na ulevi wa rubani. Hii inaonesha ni jinsi gani sisi waafrika siku hizi hatujali nidhamu ya kazi. Inawezekanaje rubani mlevi aruhusiwe kupanda ndege?
HABARI ZA JUMAPILI YA LEO
Kila jumapili napata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbali na kuangalia kuna nini cha maana. Leo nimeona mengi: moja, kuna hili la wabunge kupenda kulipwa mishahara mikubwa, mwandishi mmoja katuhusia kuwa hili ni janga kwa mataifa ya kiafrika kama Kenya. Nafikiri pia hata kwa Tanzania makala hii itakuwa ina maana.
Pili pia kutoka Kenya, mara baada ya ajali ya ndege ambayo iliyamaliza maisha ya wabunge kadhaa wiki mbili zilizopita, mara Rais Kibaki anatangaza siku maalum ya maombi kwa Taifa.Mwandishi anatuhabarisha zaidi kunani mpaka maombi kwenye mambo ya kiserikali? Alafu kama ulinifuatilia wiki iliyopita niligusia juu ya ile Injili mpya ya Yuda Iscariot, yule anayedaiwa kuwa alimuuza Yesu kristu kwa fedha.Mwandishi anatuambia hata mapadri wamebaki kimya juu ya hili kama kweli Yuda ni msaliti au shujaa.
Alafu lililonifurahisha kabisa ni hii ziara ya Rais wa China huko Marekani na hasa juu ya nishati ya Nuklia ambayo inasemekana China ni mshikadau anayepaswa kuzingatiwa. Nafikiri ukisoma makala hii ni muhimu; utaelewa haya mambo ya mashindano ya silaha hizi kwa undani.
Kuna pia hili la maraisi wa Afrika kutaka kugombea urais zaidi ya kipindi kilichowekewa ukomo ili kukaa madarakani mpaka kifo.Iko habari moja huko Marekani, jamaa wanajiuliza vipi tena hivi hata kama hujawahi kuwa Raisi pia kuna ukomo wa kugombea.Jamani simnajua watu kama akina Mrema na Lipumba na akina Maalim Seif wataendelea kugombea sijui mpaka lini.
Hapa Uganda, inasemekana vyama vya upinzani vimeshindwa kutekeleza yale ambayo vinapaswa kufanya. Hali hapa si tofauti sana na upinzani wa kule Tanzania.
Mwisho kabisa nimeshangazwa kiasi fulani eti vijana wengi wa Kimarekani hawana habari na mambo ya msingi ya serikali yao. Hii imenifanya nivute pumzi na kuangalia huku kwetu na kwa kiasi fulani hata kwetu Tanzania na hata hapa hali ni moja tu.
Pili pia kutoka Kenya, mara baada ya ajali ya ndege ambayo iliyamaliza maisha ya wabunge kadhaa wiki mbili zilizopita, mara Rais Kibaki anatangaza siku maalum ya maombi kwa Taifa.Mwandishi anatuhabarisha zaidi kunani mpaka maombi kwenye mambo ya kiserikali? Alafu kama ulinifuatilia wiki iliyopita niligusia juu ya ile Injili mpya ya Yuda Iscariot, yule anayedaiwa kuwa alimuuza Yesu kristu kwa fedha.Mwandishi anatuambia hata mapadri wamebaki kimya juu ya hili kama kweli Yuda ni msaliti au shujaa.
Alafu lililonifurahisha kabisa ni hii ziara ya Rais wa China huko Marekani na hasa juu ya nishati ya Nuklia ambayo inasemekana China ni mshikadau anayepaswa kuzingatiwa. Nafikiri ukisoma makala hii ni muhimu; utaelewa haya mambo ya mashindano ya silaha hizi kwa undani.
Kuna pia hili la maraisi wa Afrika kutaka kugombea urais zaidi ya kipindi kilichowekewa ukomo ili kukaa madarakani mpaka kifo.Iko habari moja huko Marekani, jamaa wanajiuliza vipi tena hivi hata kama hujawahi kuwa Raisi pia kuna ukomo wa kugombea.Jamani simnajua watu kama akina Mrema na Lipumba na akina Maalim Seif wataendelea kugombea sijui mpaka lini.
Hapa Uganda, inasemekana vyama vya upinzani vimeshindwa kutekeleza yale ambayo vinapaswa kufanya. Hali hapa si tofauti sana na upinzani wa kule Tanzania.
Mwisho kabisa nimeshangazwa kiasi fulani eti vijana wengi wa Kimarekani hawana habari na mambo ya msingi ya serikali yao. Hii imenifanya nivute pumzi na kuangalia huku kwetu na kwa kiasi fulani hata kwetu Tanzania na hata hapa hali ni moja tu.
Sunday, April 16, 2006
NI PASAKA-ETI YUDA HAKUMSALITI YESU?
Nimepitia habari leo jumapili ya pasaka nikakunwa kuhifadhi haya: Moja Eti Yuda Eskarioti, yule mtume wa Yesu inasemekana ni shujaa na hakuna haja sisi waumini kumfikiria kama msaliti.bonyezahapa Eti inasemekana kuna injili ya Yuda ambayo kanisa limeikataa ambayo inaeleza kinagaubaga juu ya hili. Papa Benedict tayari ameikana ripoti iliyotolewa hivi karibuni juu ya injili ya Yuda. Nakwambia haya mambo mtu unaweza usiwe muumini wa dini yoyote. Sijui wanaglobu mnasemaje, mmeshafikiria hili? bonyeza hapa
Pia nikamsoma Papa Benedict-16 ana ujumbe gani leo hii. Ameushangaza umma kwa kubadilika kama kinyonga kinyume na alivyodhaniwa atakuwa Papa Ngangari.bonyeza
Pili, kuna huyu mtoto wa Mwalimu Nyerere, basi nikaamua nimsome nijue anaandika juu ya nini unajua inawezekana ana falsafa za baba yake. bonyezahapa
Alafu nikakunwa na umuhimu wa kuheshimu na kuilewa demokrasia, mwanamama mmoja kaandika kweli hapa Uganda. bonyeza
TUNAHITAJI SHIRIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI?
Jumuiya ya Afrika Mashariki imeingia katika hatua ya kuwa shirikishio. Ili kujua ni nini kinatarajiwa kufanyika, bonyezahapa ili umsome mwanamama ambaye atatuletea shirikisho. Pia kuna machache aliyoyasema Katibu mkuu wa jumuiya Bw Mushega wakati akiaga ili kuhitimisha muhula wake. Amemponda sana Bw Njonjo, waziri wa zamani wa Kenya kwa kuiponda jumuiya.Hebu soma mahojiano kamili ya mwanadiplomasia huyo aliyemaliza muda wake.Pia kuna ripoti maalum ambayo itatolewa hivi karibuni juu ya kama kweli hii jumuiya inawezekana.Hapa nataka tusome taarifa tangulizi ya ripoti hiyo.
Mimi sio muungaji mkono sana Shirikisho ila tu jumuiya manake najua ni ndoto. Hata JK bado anaweka msisitizo zaidi kwenye SADC. Ila kwa baadhi ya wananchi wana wasiwasi juu ya hizi nchi za Rwanda na Burundi kwani zitatuletea balaa.
Mimi sio muungaji mkono sana Shirikisho ila tu jumuiya manake najua ni ndoto. Hata JK bado anaweka msisitizo zaidi kwenye SADC. Ila kwa baadhi ya wananchi wana wasiwasi juu ya hizi nchi za Rwanda na Burundi kwani zitatuletea balaa.
Friday, April 14, 2006
TANZANIA KUWA BORA KULIKO UGHAIBUNI--JK.
Unajua mara nyingi nikisoma anayosema JK kila anapopewa nafasi huwa ninacheka alafu ninajaribu kufikiri hivi kweli itawezekana?
Leo anaripotiwa eti ataondoa ile kasumba ya wasomi kukimbilia ughaibuni.somahapa
Haya hebu ngoja tuishi kwa matumaini manake huyu jamaa anafurahisha sana. Ila nimefurahishwa na makala moja hapa Uganda juu ya tatizo la utegemezi wetu waafrika huko ughaibuni.Nimeona ni vizuri tulinganishe yaliyojadiliwa hapa na hayo JK anayosema alafu tuamue je kweli JK ataweza kuboresha na kuzuia tamaa ya kwenda Ughaibuni?somahapa
Leo anaripotiwa eti ataondoa ile kasumba ya wasomi kukimbilia ughaibuni.somahapa
Haya hebu ngoja tuishi kwa matumaini manake huyu jamaa anafurahisha sana. Ila nimefurahishwa na makala moja hapa Uganda juu ya tatizo la utegemezi wetu waafrika huko ughaibuni.Nimeona ni vizuri tulinganishe yaliyojadiliwa hapa na hayo JK anayosema alafu tuamue je kweli JK ataweza kuboresha na kuzuia tamaa ya kwenda Ughaibuni?somahapa
Sunday, April 09, 2006
MTANZANIA KASHIKWA UGONI HOTELINI NA MWANABALOZI
Ni wiki moja sasa ambapo mwanadiplomasia mmoja wa Rwanda alizusha sekeseke kama sio kasheshe pale alipokamatwa ndani ya hoteli moja ya kitalii akijinjiri na mwanamama mmoja ambaye ni mke wa mtu. somahapa
Mengi yamesemwa ila pia kumekuwa na utata juu ya kukamatwa kwa mwanadiplomasia anavunja sheria za nchi ikimaanisha ni kuvunja mkataba wa Vienna.Ila hili limefanunuliwa vizuri na msomi mmoja hapa Uganda somahapa
Sina hakika kama ninavunja Azimio la Dodoma, ila napenda nieleze kushtushwa kwangu eti mwanamama huyo alikuwa ni Mtanzania.
La msingi nataka nitoe hoja na ijadiliwe: Hivi kuwa mwanabalozi ndio tiketi ya kufanya maovu? Eti ukifanikiwa kuhodhi au kumiliki kile kitambulisho cha uanadiplomasia basi ndio mwisho wa kubughudhiwa na wakora-mapolisi na wanausalama wengine?
Serikali ya Rwanda imelalamika sana juu ya kukamatwa mwanadiplomasia wao. Ila zaidi ni kwamba kuna hali tete sana katika tukio hili: Unajua kuna uadui mkubwa sana kati ya Museveni na Kagame na hali hii imepelekea mwanamama, ndugu yetu mtanzania mwenzetu kuhusishwa katika kuendeleza sokomoko kati ya wakubwa wawili hawa.
Unaambiwa udikteta wa Museveni sasa unaingilia starehe za watu bonyezahapa na kuzihusisha katika kuaibishana kati ya serikali hizi mbili. Mambo si mambo hapa. bonyeza hapa
Mengi yamesemwa ila pia kumekuwa na utata juu ya kukamatwa kwa mwanadiplomasia anavunja sheria za nchi ikimaanisha ni kuvunja mkataba wa Vienna.Ila hili limefanunuliwa vizuri na msomi mmoja hapa Uganda somahapa
Sina hakika kama ninavunja Azimio la Dodoma, ila napenda nieleze kushtushwa kwangu eti mwanamama huyo alikuwa ni Mtanzania.
La msingi nataka nitoe hoja na ijadiliwe: Hivi kuwa mwanabalozi ndio tiketi ya kufanya maovu? Eti ukifanikiwa kuhodhi au kumiliki kile kitambulisho cha uanadiplomasia basi ndio mwisho wa kubughudhiwa na wakora-mapolisi na wanausalama wengine?
Serikali ya Rwanda imelalamika sana juu ya kukamatwa mwanadiplomasia wao. Ila zaidi ni kwamba kuna hali tete sana katika tukio hili: Unajua kuna uadui mkubwa sana kati ya Museveni na Kagame na hali hii imepelekea mwanamama, ndugu yetu mtanzania mwenzetu kuhusishwa katika kuendeleza sokomoko kati ya wakubwa wawili hawa.
Unaambiwa udikteta wa Museveni sasa unaingilia starehe za watu bonyezahapa na kuzihusisha katika kuaibishana kati ya serikali hizi mbili. Mambo si mambo hapa. bonyeza hapa
MPASUKO WA KISIASA PEMBA
Nimesoma makala moja kwenye IPP Media ikanikuna sana. Unajua hii siasa ya Pemba watanzania wengi hatuifahamu kabisa. Ule MPASUKO wa kisiasa JK aliodai upo eti inasemekana hata yeye hajui kuuziba.
Kujua zaidi hebu soma makala hii: bonyeza
Zaidi ya hapo, mwandishi kaongeza makala yake katika sehemu ya pili akichambua zaidi hasa baada ya kiongozi wa chama pinzani, CUF, kufika pia Pemba na kumsifia JK. bonyezahapa
Lakini inafurahisha zaidi kwani JK kasifiwa na wasomi wa Bongo juu ya jinsi ambavyo analifuatilia suala la Muungano.
Kujua zaidi hebu soma makala hii: bonyeza
Zaidi ya hapo, mwandishi kaongeza makala yake katika sehemu ya pili akichambua zaidi hasa baada ya kiongozi wa chama pinzani, CUF, kufika pia Pemba na kumsifia JK. bonyezahapa
Lakini inafurahisha zaidi kwani JK kasifiwa na wasomi wa Bongo juu ya jinsi ambavyo analifuatilia suala la Muungano.
Sunday, April 02, 2006
JK SIKU 100
Eti rais Jakaya Kikwete kafikisha siku mia moja madarakani. bonyeza hapa Binafsi nafikiri anastahili pongezi.
Ila leo kanifurahisha zaidi katika kupambana na majambazi kwani kaanzisha kikosi maalum dhidi ya ujambazi; bonyezahapa ni hatua ya muhimu nainga mkono.
Ila tahadhari imetolewa leo hii juu ya utendaji mzima wa serikali ya JK kama inataka iendeleze mafanikio zaidi ya haya yaliyotokea kwa siku mia moja. somahapa
Ila leo kanifurahisha zaidi katika kupambana na majambazi kwani kaanzisha kikosi maalum dhidi ya ujambazi; bonyezahapa ni hatua ya muhimu nainga mkono.
Ila tahadhari imetolewa leo hii juu ya utendaji mzima wa serikali ya JK kama inataka iendeleze mafanikio zaidi ya haya yaliyotokea kwa siku mia moja. somahapa
Subscribe to:
Posts (Atom)