My Blog List

Thursday, June 28, 2007

AMINA CHIFUPA KAUAWA--KIFO HIKI KICHUNGUZWE


Juzi usiku saa tatu na dakika kumi napokea sms kutoka kwa mtu fulani wa karibu aliyepo Dar es salaam ikiwa na maandishi ya herufi kubwa: AMINA CHIFUPA KATUTOKA, AMINI USIAMINI. Mara nasikia pia tangazo redio free afrika juu ya hili. Basi naamua kumuuliza huyu bwana ninini maoni yake?

Anajibu: WAMEMUONDOA KISAIKOLOJIA. TANZANIA HAIHITAJI MAJASIRI!NCHI HII NI BORA KUWA KIMYA TU! KAA NA FAMILIA YAKO KAMA UKIONA WATU WANA ISHU CHAFU ACHANA NAO! HAIKUHUSU. LEO NDIO MAADHIMISHO YA AGAINST DRUGS NA SHUJAA AMEONDOKA! IPO SIKU WATU WATACHOKA NA HAPATAKALIKA! IMENIUMA KUPITILIZA.Ni maneno mazito ambayo hata mimi yaliniingia hasa lakini naamini ni lazima wapiga filimbi(whistle blowers) waendelee kuwepo. Hisia zangu ni nyingi hasa kulihusu bunge letu. Nitaeleza kwa mujibu wa mambo yaliyojitokeza baada ya msiba huu.

Amina ni mtu anaelezewa na walomfahamu kama mtu aliekuwa na upeo ambao ulihitajika nchi hii.Ila wengine kuona anafariki katika hali isiyoelezeka kwa mtu mwenye akili timamu wanathubutu hata kukilaani chama cha mapinduzi japo mie nadhani tuna tatizo la utamaduni wa kutokubali kuelezwa ukweli.Wengine wamemfananisha na Princes Diana hata pia wengine wakafikia kusema siku ya madawa ya kulevya iitwe jina lake kitu ambacho sidhani kitasaidia kwa nchi kwani ni zaidi ya hapo ndio tutaweza kumuenzi: yaani kuwa mashujaa kupambana na umafia bila kuogopa ufa hadi bila kujali kufa kama Amina ndipo tutaikomboa nchi yetu dhidi ya umafioso wa baadhi ya watu.

Kwa ufupi nafikiri mhariri wa gazeti la serikali hakukosea,AminaChifupa alikuwa ni taa iliyopotea.Huko Dodoma wabunge wetu walionekana kwenye runinga wenye simanzi ila sina hakika kama ilijkuwa ni kweli ama ni unafiki tu. Nasema hivi kwani mimi naamini chombo kama bunge kingeweza kutoa msaada mkubwa sana wa ushauri nasaha wa kitaalam kumuokoa dada hyu dhidi ya hali ngumu aliyokuwa akikabiliana nayo.

Sijui kama kuna akina mama wabunge walijipenyeza hadi kuona Mbunge huyo alikuwa akiendeleaje hadi alipozidiwa.Wananchi wengi nikiwa mmojawapo naamini kabisa ile kauli ya Amina dhidi ya uuzaji wa dawa za kulevya ndio chanzo cha hii sukari tunayoambiwa imemwondoa, kwani imemsababishia mahangaiko na fedheha (depression) mengi ya ndani hasa pale ilipopelekea hata ndoa yake kuingia matatizo.Spika wa bunge na katibu wa bunge nadhani wana deni kutueleza: je walichukua hatua gani kumsaidia mbunge huyu hasa baada ya matatizo yake ya ndoa?

Sipendi sana kusikia hizi kauli za oh ni Mungu kaamua basi hatuwezi kufanya kitu, tufike mahali nchi hii tujifunze kuhoji matukio sio kuleta habari ya Mungu kwani ni dhihirisho nchi hii watu hatupendi kufikiri labda.Ukiweka suala la Mungu tayari unazuia uwezekano wa mtu kuchunguza, napenda sana serikali ianzishe uchunguzi mara moja.

Mwenye akili za kizamani atadai hii ni maisha binafsi, ila naamini katika dunia ya leo taasisi kubwa kama bunge inaendeshwa kisasa. Ni wajibu wa watendaji wakuu wa bunge kujua hali na matatizo mbalimbali ya kisaikolojia ya watu waliochini yao na jinsi ya kuwasaidia. Haitoshi tu kupigiwa simu na kulitangazia bunge fulani ni mgonjwa.Ilipashwa spika na katibu wajue maendeleo ya mbunge Amina kila kukicha, huu ndio wajibu wa kiongozi au mtendaji wa taasisi yeyote ya kileo ukizingatia tuko katika serikali iliyokuja na kauli mbiu: Ari Mpya na Nguvu Mpya na Kasi Mpya.Hapa taasisi ya bunge ninashawishika kuilamu kwa kuuliza: Je spika na katibu mlimsaidiaje mbunge Amina?Je bunge letu lina idara ya kutoa ushauri nasaha?

Labda nikumbushe kuwa Amina ni kielelezo cha mbunge ambaye anathubutu kusema jambo ambalo viongozi wetu wengi hawako tayari kusema kwa woga na pia labda maslahi wanayopata huko.Unafiki utailetea balaa nchi hii siku za usoni, kwani nakumbuka miaka miwili iliyopita aliuawa kule nchini Uganda Makamu wa Rais wa Sudan, John Garang, kwa ajali ya ndege ambayo inaaminika ilipangwa. Lakini waandishi jasiri waliposema ukweli kuwa kulikuwepo namna Raisi Museveni aliwakamata na kusema wanahatarisha amani.

La ajabu wiki iliyopita, mke wa Garang mwenyewe kadai mumewe aliuawa na anataka uchunguzi haraka. Mama huyu alitumiwa na Rais Museveni wakati wa kampeni za uraisi kumpigia debe Museveni na kudai Museveni ni mtu safi ambaye anasaidia hata nchi jirani kama ilivyokuwa kwa mumewe.Unafiki ni hatari ila leo anasema anaamini mumewe aliuawa.Tufike mahali tuseme ukweli ndio tutajua na kuzuia mafioso ya watu fulani ambao wanafanya wapiga filimbi kama Amina wafunge midomo yao.

Kwangu inauma na ninaamini ni pigo hasa kwa akina mama wa Tanzania kwani hata wale jasiri kama Anne Kilango watafunga midomo yao sasa. Nashangazwa pia na vyombo vya habari havina vipindi vya mijadala kuhusu kifo kama hiki; navisihi vituo vya redio na Televisheni vipite mitaani kuonesha hisia halisi za watu wengi sio kutuwekea mahojiano na watu kama waziri mkuu, sijui meya wa Kinondoni na watu wengine kwenye serikali unadhani watasema nini kama si tu kutuambia Mungu kamtwa kwa sababu anampenda. Vyombo vya habari kwa mwendo huu wa kutokuwa na utamaduni wa kuhoji, nchi hii itaendelea kuwa juu ya watu mafioso.

Natia shaka uwezekano wa kuwekewa sumu hata kusababisha sukari mwilini kushindwa hata kudhibitiwa kidaktari. Kwanini uchunguzi usifanyike?Mbona serikali ya Uganda majuzi ilimpoteza pia kiongozi kijana na katibu mkuu wa wizara ya ulinzi ambaye alikuwa tishio kwa vigogo wengi na pia mtu wa karibu wa Museveni. Baada ya kupinga uwezekano wa kifo kuwa sumu sasa serikali ya Uganda imeamua kufanya uchunguzi. Kenya ulifanyika uchunguzi wa kifo cha Ouko ila sisi watu wanaondoka tunabaki kusema oh!Mungu kampenda kuliko sisi, Bwana ametwaa! Ujinga gani huu jamani? Inatia uchungu tusivyopenda kuchunguza. Tangu Kolimba, Mwaikambo na wengine ambao hawasemwi sana.
Tumekwisha watanzania, naomba nifunge hoja kwa kuomba maelezo ya taasisi ya Bunge na pia kifo hiki kichunguzwe. Mungu amlaze pema peponi, Amina.

Saturday, June 23, 2007

MACHUNGU YA LRA

Kama unataka kujua ubaya wa vita kule Uganda kaskazini basi msome huyu mama alivyoathiriwa na waasi wa LRA.
Museveni kaanza kubadilika, anathubutu sasa kuwakamata mawaziri wala rushwa ambao waliaminika kama wasioshikika(untouchable), je unajua kwanini?Wiki iliyopita jumuiya ya Afrika Mashariki imezipokea Rwanda na Burundi, je kuna manufaa?

Wednesday, June 20, 2007

RIO FERDINAND -KAMPALA

Rio Ferdinand wa Man United alikuwa Kampala wiki iliyopita kuona maendeleo ya kituo cha michezo ya vijana anachofadhili yeye na baba yake.Nimecheka kumsoma baba wa Ferdinand haiba yake.Uganda nayo yachemsha kuna hatari isifuzu kwenda Ghana.
Tunakumbushwa pia ni nini changamoto za jumuiya ya Afrika Mashariki?Pia je ni kweli juhudi zote za kuunda jumuiya ya Afrika Mashariki zitaondoa umasikini?
Pia serikali ya Sudan imeanza uchumguzi dhidi ya mauaji ya John Garang.

MALKIA WA UINGEREZA HATANG'ATWA NA MBU UGANDA NG'O!

Ama kweli tuna kazi Afrika, yaani Malkia wa Uingereza-Elizabeti atazuru Uganda na serikali imeanza juhudi kusafisha kwa kupulizia dawa maeneo ya karibu na atakapolala ili asijeambukizwa Malaria. Kumbe tunaweza zuia Malaria Afrika?
Vita dhidi ya Rushwa Uganda inaongozwa na mwanamama matata kwelikweli.Pendekezo ni kwamba waheshimiwa wetu wanapohusishwa na rushwa basi wajiuzulu.Soma pia mapendekezo ya nnini Uganda ifanye ili iepuke dhahama baada ya kugundua mafuta.

Friday, June 15, 2007

MAMBO?

Leo nimeona niwaoneshe hasa wabongo kwanini wanapenda sana tamthiliya za TV ambazo ni za muda mrefu?Alafu je ni sawa kwa mtu mwenye akili kubaki kimya au kuunga mkono uchaguzi wa Nigeria hivi majuzi?Pia hivi kweli Iddi Amin alikuwa hatari isemavyo?

Saturday, June 09, 2007

kumbuku

http://www.monitor.co.ug/score/score06092.php(Uganda prep)
http://www.monitor.co.ug/health/health06073.php(Madhara ya AC)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Iddi Amin)
http://www.monitor.co.ug/oped/oped06092.php(Musevei speech)

Wednesday, June 06, 2007

Uganda Yashinda Nigeria

Mafuta yaligunduliwa Uganda, je nchi kuwa na mafuta ndio laana?Je kukuwa kwa China ni baraka Afrika?Leo nakumbushia pia juu ya Mayombo tena, huyu mtu alikuwa na mengi ya kueleza yasiyojulikana.Nigeria yashindwa.

Saturday, June 02, 2007

Soka

Kwanza nikumbushe tu kuwa watawala wetu wanafunga midomo a wananchi tusizungumze. Nilionehsha makala moja wiki mbili zilizopita lakini Ndesanjo akaniambia nimekosea viungo vyake.Nataka niseme sikukosea nadhani jamaa walifunga kiungo kisifanye kazi lakini alieandika yuko hapa kaandika ni kwanini nilitaka msome mjue uhuru wa habari unavyoogopwa.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.
Kwanza nikumbushe tu kuwa watawala wetu wanafunga midomo a wananchi tusizungumze. Nilionehsha makala moja wiki mbili zilizopita lakini Ndesanjo akaniambia nimekosea viungo vyake.Nataka niseme sikukosea nadhani jamaa walifunga kiungo kisifanye kazi lakini alieandika yuko hapa kaandika ni kwanini nilitaka msome mjue uhuru wa habari unavyoogopwa.
Leo ni kandanda hapa Afrika Mashariki, Kampala Uganda inaavaana na Nigeria mechi ambayo ni lazima waganda washinde kocha maarufu Ugannda anasema hivyo. Na huko Mwanza Taifa Stars ni lazima washinde la sivyo ni kusahau safari ya Ghana. Sina matumaini sana kwani kiwango cha timu yetu ukilinganisha na Senegali tutegemee maajabu ili kushinda.

Wednesday, May 30, 2007

RUSHWA UGANDA

Inasemekana eti Serikali ya MU7 iliingia madarakani 1986 ikiwa na mawazo ya kimapinduzi ambayo sasa yanadaiwa yamepotea njia.Huko Uganda kashfa kubwa ya rushwa imesababisha mawaziri vigogo kuwwekwa ndani, ni kisa kinachofanana na kile cha mheshimiwa Dito kupewa dhamana kwa kesi ya mauaji.Kisa hiki ni mfano hai wa siasa za kulindana zinapofika ukingoni.

Monday, May 21, 2007

MAUAJI YA SUMU KWA WANASIASA

Sasa waganda wameanza kuuana kwa sumu, siasa si mchezo.Kama ulishasikia mwanasiasa anayeogopeka ndiye huyu Uganda.
Uganda ni nchi iliyojaa vifo visivyoelezeka.
Wale wajasiriamali
Leo kwa wale wanasikiliza BBC Swahili, basi kila mara utamsikia msemaji wa jeshi la Uganda,ni muwajibikaji na msomi wa kileo jeshini ambaye hakusita kuandika makala juu ya kifo cha yule askari aliyefariki majuzi bila woga au mficho, ndie huyu Meja Kulayige. Mwisho kuna kashfa kubwa ya fedha Uganda tena.

Saturday, May 12, 2007

Harusi za gharama muhimu?

Wale wanaooa je mnataka harusi ya gharama?

JANET MUSEVENI KATIKA KASHFA YA GLOBAL FUND

Nchi ya Uganda imeshuhudia kashfa kubwa ya wizi na matumizi mabaya ya fedha za wafadhili hasa zile za fuko maalum(Global Fund). Iliundwa tume kuchunguza na matokeo yake ni kwamba hata mke wa Rais anahusika.Ni kashfa kubwa kwani inawahusu askari jeshi wa vyeo vya juu ambao ni vigumu kwa Museveni kuwagusa.
Upande wa michezo, timu ya taifa ya soka hapa tayari inaanza maandalizi dhidi ya Nigeria.Tanzania kwa sasa maneno mengi juu uteuzi wa timu hapa chama cha soka kimejipanga vizuri sana.Kwenye mambo ya kisiasa zaidi hebu soma juu ya ule msemo wa kiingereza usemao: Like Father like.....

Saturday, May 05, 2007

WIKI HII UGANDA

Ni vyema tuanze na juu ya nini chanzo cha kifo cha Brigedia maarufu na kijana aliyefariki Uganda siku za karibuni manake inadaiwa labda ni sumu.
Tuachane na kifo na tuendelee na siasa juu ya utawla bora.
Na mwisho eti mtoto wa Iddi Amin kaanzisha wavuti kuweka kumbukumbu za baba yake. Ila kama watu wanafikiri JK wa bongo ni rais wa karibu na watu Museveni ndio usiseme kwani ana kawaida ya kutembelea vyombo vya habari yaani redio za FM na kufanya malumbano ya simu na wtu kdhaa.

NOBLE MAYOMBO-ASKARI SHUJAA UGANDA

NEWS




Uganda mwanzoni mwa wiki hii ilimpoteza askari, mpiganaji na msomi mahiri kabisa.Noble Mayombo ni wazi alikuwa ni kati ya vijana wanaoaminiwa sana na Rais Museveni.Jamaa kafariki baada ya kuugua ghafla na inasemekana huenda kategewa sumu.Pia ni kwamba alikuwa kati ya maafisa wanaoeneza utawala wa ubabe wa Museveni na sumu yake katika ukanda mzima wa maziwa makuu.
Ni wazi alikuwa na maadui wengi saana na alikuwa na msimamo thabiti dhidi ya wapinzani akiamini mateso(torture) kama njia muafaka dhidi ya wahalifu na wapinzani kama Kiiza Besigye.Licha ya uaskari alikuwa pia ni katibu mkuu wa wizara ya ulinzi.Mengi yatasemwa lakini kashaondoka ila lazima tumkumbuke, kwani jamaa wengine wanadai hivi mashujaa tunawakumbukaje?
Jamaa kaagwa kiana yaani mwili wake kuwekwa Bungeni, mie nauliza hivi shujaa kama huyu mbona hajulikani njee ya Uganda?Mie kama msikilizaji wa redio za Uganda niliwahi kumsikia akifanya malumbano na pia nukuhu kadhaa zinamwonesha kama mtu mwenye kujidai sana; na kweli nadhani alikuwa mahiri japo nafikiri alikuwa akitetea tu utawala.
Jamaa kama kawaida mtu akifa, mkewe kamsifia kweli!
Andrew Mwenda ni mwandishi maarufu wa habari Uganda anamwelezeaje huyu bwana?Pia kifo hiki kinatukumbusha ni nini maana ya maisha.
Mwisho yuko Mhindi anatukumbusha juu ya umuhimu wa wahindi katika uchumi wa afrika.

Saturday, April 28, 2007

Thursday, April 26, 2007

UTAWALA WA KIBOKO UGANDA

Makamu wa Rais wa Uganda bado anaandamwa na kashfa ya uzinzi. Uganda imeanzisha kikosi maalum: KIBOKO SQUAD kutokana na kuongezeka kwa fujo na maandamano kila kukicha dhidi ya maamuzi dhalimu ya serikali.Watu wanachapwa viboko wakijaribu kuandamana.
Uganda pia wiki iliyopita yule bondia maarufu wa nchi hilyo alirefjea nchini humo.

Baada ya uchaguzi kule Nigeria Raila Odinga wa Kenya anaeleza woga wake juu ya nguvu kubwa alizzonazo Rais wanchi na athari zake za uchaguzi ujao.

SAYARI NYINGINE KAMA DUNIA

Wanasayansi wamegundua sayari mpya inayoaminika ina maisha ya viumbe hai kama dunia. Huko Uganda pia yuko jamaa mmoja mchungaji mwenye kipaji kwelikweli, mjue Sempa.
Nigeria imempata Rais mpya kwa uchaguzi uliolalamikiwa sana, je nini kitarajiwe?

Raisi Museveni wa Uganda kasababisha sakata kubwa la uuzaji wa msitu wa asili kwa Wahindi.Hebu tuujue undani wa tatizo hili la MABIRA FOREST kwa dhati.Wengine wamependekeza kuwe na MAPINDUZI YA SUKARI.Iko pia barua ya wazi kwa rais Museveni kutoka kwa mwananchi wa kawaida.Yapo maoni ya Mhindi juu ya dhahama hili na anajaribu kufananisha na hali ya wakat wa Iddi Amin.Mwingine katupa kanuni ya kubalansi mazingira na uchumi bila athari.

Tuesday, April 10, 2007

UZINZI HALALI UGANDA?-MAHAKAMA

Museveni hatimaye kaanza kuzungumzia mipango ya kuondoka.
Mahakama ya Uganda imefafanua juu ya sheria ya ukahaba au uzinzi kwa mwanamke na mwanaume, hata hivyo bado akina mama wengi wa Kampala wanataka talaka waachane na mabwana zao.Amanya Mushega, katibu mkuu wa EAC wa zamani anazungumzia juu ya utawala bora. Hotuba yake inatoa historia ya siasa za Uganda.
Ule msitu wa Mabira ni kielelezo cha rushwa nchini Uganda kwa miongo mingi anasema Andrew Mwenda.

Saturday, April 07, 2007

MZUKA WA IDD AMIN BADO

Watu wanamjua Iddi Amin kama mtu mnyama kuwahi kutokea Afrika. Lakini ni lazima tumtizame huyu bwana kwa undani hasa kuwa hata waliomfuatia ni wanyama pia, je unajua kwanini? Tunaambiwa eti serikali ya Museveni ni tishio kwa wapinzani kama alivyokuwa Idi Amin.
Amanya Mushega alikuwa katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki, yeye anapinga kuuzwa kwa msitu wa Mabira. Tunakumbushwa jinsi vyama vya siasa visivyo na nidhamu. Na je nini chanzo cha matatizo ya Afrika, Museveni alishasema ila leo hii anavunja aliyowahi kunena.