My Blog List

Wednesday, August 30, 2006

SIKU YA GLOBU DUNIANI

Kesho ni siku ya blogu duniani. Nimerudi nyumbani Tanzania hivi karibuni na kwa sasa ninajaribu kutulia na kufuatilia hali huku nikijizatiti kutafuta kazi ya kufanya. Kazi ni shida sana kupata kama hauna baba au mjomba na akina shangazi serikalini au hata katika taasisi za binafsi. Lililopo mbele yangu ni kujiajiri mwenyewe nadhani niko sahihi.
Katika siku hii sina raha kabisa na ninaisikitikia Tanzania hasa katika sekta ya habari kwani hakuna majadiliano ya maana sana katika magazeti na redio zetu. Inaonekana ari mpya na nguvu mpya imeturudisha katika enzi za "Zidumu fikra za Mwenyekiti wa Chama cha........". Habari nyingi hapa ni kusifia utendaji wa wanasiasa na kutokuwakosoa kabisa.
Redio za FM kibao lakini wao dili ni kupiga mziki, vipindi vya majadiliano sio sana ila kama unataka ukweli kuhusu nchi hii soma globu. Tatizo ni watanzania wachache wanasoma globu.
Ziko globu tano ambazo nadhani ni bora kwangu na ningependa watu wasizikose kabisa: kwanza, ni hii ya Mpiga Picha Issa Michuzi ambapo tukio kuhusu Tanzania utalipata hata kama hauko nyumbani utafurahi sana na pia kwa kumbukumbu zote za nchi zipo. Pili ni Pambazuka kwani utapata habari kiuchambuzi na kiyakinifu kuhusu mauzauza yote ya wataanzania haswa wanasiasa na viongozi wake. Alafu kuna Miruko, yeye bwana anazungumza ukweli bila uficho, si mwoga kama walivyo watanzania wengi.Huyu si bendera fuata upepo.Blogu ya nne ni Kasri la Mwanazuoni, hapa huwa napata habari za upande ambao hutapata magazetini wala redioni.Huyu bwana ni kiboko huwa napenda nimsome tu. Mwisho kabisa ni globu kutoka Nigeria, hapa kuna mijadala ya kusisimua sana.

Monday, August 28, 2006

MWISHONI MWA WIKI ILIYOKWISHA

Ukisikia serikali inapinga ukweli alafu anatokea mtu anaandika kujibu mapigo ndio haya ya Uganda.Kwenye kandanda wakati hatuna mechi yeyote ya kujipima nguvu Uganda itacheza na wapinzani wetu Burkinafaso. Matokeo wametoka sare, nasikia Tanzania tulimtuma mtu akapeleleze, sijui itakuwaje jumamosi.
Kwenye siasa nako unajua kuna waafrika mawakala wa mabepari?Kama unamfahamu profesa Maamdani ambaye alimfunda pia raisi wetu JK basi soma anasemaje juu ya umuhimu wa elimu na vyuo vikuu katika nchi?Profesa mwingine, Ali Mazrui yeye ana mengi juu Jumuiya ya Afrika Mashariki, eti tunahitaji miaka mingine arobaini.Kuna haja ya Bunge la vyama vya upinzani kuwa na malengo au visheni, je Uganda wanalo bunge la aina hii?Si hayya tu, ila huu ung'ang'anizi wa Museveni madarakani una uhusiano sana na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pia mapigano yamesimamishwa na waasi wa Uganda rasmi, je ni nani shujaa katika dhahama hili la miongo miwili?
Uchaguzi wa Congo DRC utatoa rais ambaye ana maslahi tofauti kwa Uganda awe Kabila au Bemba.
Huko Burundi kama kawaida jamaa wameanza kufungana jela eti watnataka kupinduana.Huku Jumuiya ya Afrika mashariki ikisuasua
Kama unataka kujua jinsi ya kuwa tajiri na kuishi raha mustarehe bila kukopakopa.
Mambo ya akina mama pia tunakumbushwa ni jinsi gani wanafurahia mabwana jua siri

Friday, August 25, 2006

FAMILIA YA MUSEVENI YAIFANYA NCHI MALI YAKE

Vituko vya marais wa Afrika ni vingi. Nchini Uganda, Museveni naye hakosi vituko hasa vya matumizi makubwa ya fedha.Andrew Mwenda anao uelewa wa ni nani hasa ni Museveni na jinsi familia ya rais huyo inavyoiibia nchi hiyo.
Imeripotiwa pia eti ili Kony aweze kumalizwa huko misitu ya Congo basi serikali ya Uganda iilipe Congo gharama ya uporaji iliyoufanya miaka kadhaa iliyopita.
Pia tunakumbushwa tusiogope ukosefu wa ajira kwani kuna namna ya kuishi bila kuajiriwa. Pia tunaambiwa kumbe hata maaskofu wa kikatoliki na makadinali wanastaafu.
Katika siasa, NRM kama mfano wa vyama tawala vinahitaji kitu kinaitwa Matangi ya Kufikiri--think tank. Pia nchini Uganda ni vizuri tumsome na kumjua afisa mmoja wa jeshi Brigedia Jenerali Tumukunde ambaye katiwa kizuizini kwa muda sasa eti kajaribu kutikisa mkuu wa dola.
Nirudi kwenye mazungumzo ya amani huko Uganda, kauwawa kamanda wa LRA ambaye inasemekana na aliyemjua kuwa alikuwa mnyama haswa. Pia nigusie mambo ya ofisini haswa tabia ya mahusiano ya kijinsia na mabosi.
Kwenye kandanda je kuna tofauti kati ya makocha wa Ulaya na wa kwetu hapa Bongo?Pia suala la nidhamu kwenye timu za kandanda kama Taifa Stars.

Friday, August 18, 2006

MAMBO YA MSINGI

Unajua umuhimu wa michezo mashuleni? Unajua inasemekana Museveni ndio anaimaliza kabisa Uganda?
Ni vizuri pia tuelewe ni kwanini Wazungu wameamua kutunyonya kabisa. Mazungumzo ya Doha yamevunjika, kwanini lakini?

YA WIKI HII

Kuna tabia ya kuhamahama kutoka upinzani kwenda chama tawala. Alafu nchini Uganda, Raisi pekee anatumia mamilioni ya shilingi kulipa washauri wake ambao ni wengi lukuki. Soma simulizi la mwandishi maarufu nchini Uganda alipokuwa lupango.
Nchini Uganda rushwa ndio haswa, je unajua wataalam wanaeleza rushwa ni nini? Je Raisi anaweza tu kuamua kufanya ziara binafsi?

Saturday, August 12, 2006

LEO

Kuna hili la ufisadi Uganda alafu eti siasa ni mbaya kwa maendeleo. Pia unamjua Kony alivyo sasa?Alafu ona jinsi matajiri wanavyoneemeka na elimu bora Ugaanda.
Yuko jamaa anatabiri Chelsea kushinda tena taji msimu huu.Na kwa wale kapera kama mie, tunahitaji wapanga sherehe za harusi?

Friday, August 04, 2006

YALIYONIVUTIA LEO

Wakati bado timu yetu haijaanza maandallizi ya kwenda huko Ghana mwaka 2008, Uganda tayari kocha waao kaanza mambo. Tunaambiwa hata sex inataka maadili fulani yazingatiwe, unazijua?
Kuhusu politiki ni kuwa Museveni kaishiwa hana hela, rushwa imezidi na sasa chama tawala kinabidi kifunge shughuli katika ngazi za chini. Athari za Chama dola ndio hizi. Nikiwa kama bachela mzoefu basi mambo ya mapishi ni vyema niyapitie.
Angalia ukubwa wa Afrika ulivyo, hapa rais anapopita anaweza akasababisha hata mauaji.Alafu ligi ya Uingereza ndio inakaribia.
Kama unamjua Joseph Kony pata undani wa maisha yake ya sasa. Je ilikuwaje Mapinduzi yakatokea Uganda?

Saturday, July 15, 2006

SALA KUONDOA RUSHWA?

Kweli sala na mafungo ndio dawa ya Rushwa?Pia mambo ya imani yapo kweli?Na siasa mwanzo wake je?
Mpira huu ni mwaka wa Chelsea tena?Je kashfa kubwa mpirani?

Friday, July 14, 2006

KONY ATAELEWEKA?

Mambo ya Kony?

UGANDA KUNASEMAJE?

Baada ya kimya kirefu leo niangaze yanayojiri nchini Uganda: kuna huyu bwana anatuhumiwa kuuwa mkewe. Katika kesi yake anaonekana kujiamini sana kitu kinachowashangaza wengi. Alafu kama ilivyo kawaida, siku hizi tunawaza pesa tu haswa wengi wetu. Matokeo yake hata kazi zetu kwa mfano wachapishaji wa magazeti maadili ya kazi yameshuka sana. Pia nchi ya Uganda inatamani kuwa na mafuta lakini inakumbushwa kuwa hiyo ni balaa kwa Afrika na ni hatari kwa demokrasia.
Baada ya kombe la dunia hebu tujue ni nini kinasemwa pia kuhusu kosa la Zidane? Alafu kuna Padri wa Kikatoliki uzalendo umemshinda na kaamua kuvunja sheriia za useja. Pia tunakumbushwa juu ya ongezeko la ugonjwa wa moyo. Nini kifanyike?
Mwisho vipi kuhusu Kony?

Thursday, June 08, 2006

VIROJA KATIKA VIAPO UGANDA

Hebu ona jinsi mawaziri wapya walivyoonesha manjonjo wakati wakiapishwa wiki iliyopita.Pia unaweza ukasoma uswahiba kati ya mmojawapo wa mawaziri walioteuliwa na Museveni hivi majuzi.

Wednesday, May 24, 2006

BARAZA LA MAWAZIRI LA MUSEVENI HILO!

Hatimaye Rais Museveni kachagua baraza la mawaziri na kama ilivyotarajiwa kamchagua mdogo wake ambaye ni ofisa wa jeshi aliyeishia kidato cha sita kuwa waziri wa fedha. Huko nyuma Museveni aliwahi kumtimua kazini kwa kisingizio cha ulevi kupindukia.
Mambo ya ufalme labda ndiyo yanaanza hebu tusubiri. Maajabu ni huyu Eliya Kategaya ambaye alimpinga sana juu ya kung'ang'ania madaraka sasa kawa waziri.
Yamesemwa mengi juu ya sababu za uteuzi wa mawaziri mbalimbali. Pia kama kawaida ya Uganda, uongozi umekwenda kwa watu wa mashariki, yaani kule alikozaliwa Museveni. Hata jamaa mmoja kadai eti anaota mji mkuu wa Uganda ukahamia "RWAKITURA" kijijini kwa Museveni siku chache zijazo.
Mawaziri ni wapya wengi na hasa vijana.

Monday, May 22, 2006

Thursday, May 18, 2006

MARAISI "SUPA GLUU"-AFRIKA

Kuna malalamishi ambayo yanafurahisha juu ya hatua ya marais wa Afrika kuunga mkono wenzao wanaong'ang'ania madaraka.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.

MARAISI "SUPA GLUU"-AFRIKA

Kuna malalamishi ambayo yanafurahisha juu ya hatua ya marais wa Afrika kuunga mkono wenzao wanaong'ang'ania madaraka.
Mwandishi mmoja kalaani ni kwa nini hata JK wetu alihudhuria kuapishwa kwa Museveni?
Alafu Obasanjo alifika Uganda baada ya Museveni kuapishwa inasemekana alikuja kumfunza Museveni jinsi ya kutawala ukiwa haupendwi. Demokrasia bado inaendelea kuchezewa hapa na Museveni kwani sasa hivi yuko tayari kutumia hela za walipa kodi kumfunga mpinzani wake.

Saturday, May 13, 2006

IGIZO LA KIAPO CHA MFALME MUSEVENI WA UGANDA

Kama ilivyotarajiwa jana Rais Kaguta Museveni aliapishwa na jaji mkuu kwa mara nyingine kuendelea na ngwe nyingine ya miaka mitano katika viwanja vya Kololo jijini Kampala. Ametoa rai kwa vyama vya upinzani viwe makini ili kuweza kushirikiana naye.
Pia alipata wasaa wa kuelezea mipango ya baadaye na hata mafanikio aliyoyapata kwa miaka ishirini iliyopita.Katika sherehe za jana vyama vya upinzani hasa vile vyenye wafuasi wengi havikuhudhuria katika kile kinachoonekana kama kutomkubali Museveni kama rais halali. Pamoja na kung'ang'ania madaraka kwa Museveni lakini huwezi kuamini hadi leo ni miaka miwili Uganda ina mgao wa Umeme usiokwisha na watu wanaanza kumlalamikia sana.
Mwanzoni kabla ya kula kiapo ilisemekana hata rais Hu Jintao wa China angehudhuria katika kile kinachodaiwa kama mkakati mpya wa Museveni katika kujikita katika siasa za nchi za ukanmda wa maziwa makuu.

Sunday, May 07, 2006

J 2 YA LEO

Kama kawaida kila jumapili ninaangaza magazeti ya hapa Uganda na kwingineko. Kwa akina mama wajawazito ipo makala ya jinsi ya kujipendezesha. Alafu kuna hili la mameneja wa kiume kuongoza kwa kuwachukulia wafanyakazi wao kama wanawake.

Saturday, May 06, 2006

WAGOMBEA BINAFSI WAJA

Kwa mara nyingine mahakama nchini Tanzania imeruhusu wagombea binafsi. Huu ni ushindi wa demokrasia lakini sina hakika kama una mantiki yeyote ukizingatia demokrasia yetu changa.
Wengi wamefurahia ila ni lazima turuhusu muda tuone kwani hata nchini Uganda katika uchaguzi uliokwisha hivi majuzi pia wamechaguliwa wagombea binafsi.