Wiki iliyopita mbunge mmoja mwanamama aliamua kupeleka muswaada bungeni ili kudhibiti ubakaji nchini humo. Matokeo yake inaonekana kagonga mwamba manake wabunge wanaume wamekuja juu na inasemekana muswaada hautapitishwa kuwa sheria.
Mwanamama mmoja kasema hii ni sababu za umangimeza wa wanaume wa Afrika. Ila kuna sababu imetolewa ni kwanini Wabunge waliamua kuzichachamalia hoja mbalimbali ndani ya muswaada huo. Vifungu mbalimbali vya muswaada huo vilikuwa na utata. Mkwamo huu dhidi ya kuwaadhibu wabakaji kwa kiasi kikubwa unachangiwa na kutobadilika kwa jamii nyingi za kiafrika hususan nchini Kenya ambapo wengine wanaamini hawawezi kuishi bila kufuata mila zenye kukandamiza wanawake kwani mababu wa zamani watachukia.
Hii ni globu iliyovumbuliwa nchini Uganda inajaribu kukazia matumizi ya lugha ya kiswahili na kuhabarishana kuhusu maswala mbalimbali ya kijamii hasa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kat na kwingineko. Siasa na mambo ya michezo na kijamii kwa ujumla ndio itakayokuwa mada kuu hapa.Nitakaribisha maoni yenu.
My Blog List
Sunday, April 30, 2006
URAFIKI WA TZ NA CHINA UMEFIFIA?
Mambo yamebadilika dunia ya leo. Sijui kama kuna umuhimu sana kwa Tanzania kutembelewa na kiongozi wa China ila niseme tu ziara ya rais Hu Jintao huko Nigeria na katika kituo chake cha mwisho nchini Kenya imenifanya niwaze vipi, kulikoni Tanzania.
Si tulikuwa washirika wakubwa sana wa China wakati wa Mwenyekiti Mao?Jibu nimelipata eti mwelekeo umebadilika duniani na China ya ujamaa sio hii ya leo. Zipo sababu kwanini China ni mshirika mzuri kwa nchi kama Kenya.
Kwa Wachina ziara ya hii Hu sehemu mbalimbali ni muhimu sana na hatuna haja ya kusikiliza kelele za Magharibi. Unajua kwa mfano sekta ya mafuta barani Afrika ambayo ilitawaliwa na magharibi sasa China nayo imeamua kuingia kwa nguvu hasa barani Afrika.
Si tulikuwa washirika wakubwa sana wa China wakati wa Mwenyekiti Mao?Jibu nimelipata eti mwelekeo umebadilika duniani na China ya ujamaa sio hii ya leo. Zipo sababu kwanini China ni mshirika mzuri kwa nchi kama Kenya.
Kwa Wachina ziara ya hii Hu sehemu mbalimbali ni muhimu sana na hatuna haja ya kusikiliza kelele za Magharibi. Unajua kwa mfano sekta ya mafuta barani Afrika ambayo ilitawaliwa na magharibi sasa China nayo imeamua kuingia kwa nguvu hasa barani Afrika.
LEO MAGAZETINI
Leo kuna mambo ya lugha yameandikwa jinsi jamii ilivyogawanyika na kama mtu hauko makini unaweza shindwa muelewa mwenzako katika mazungumzo. Alafu Madaraka Nyerere anatukumbusha juu ya hii dhahama ya silaha za nyuklia kati ya Marekani na Iran na anasema kuwa na silaha hizi ni sababu ya kupunguza mizozo duniani. Mwanazuoni Ali Mazrui anatukumbusha jinsi ilivyo vigumu kwa nchi za Afrika kuungana. Ugomu ambao umejionesha pia katika muungano wa Tanzania ni dalili ya ugumu wa kuunganisha bara la Afrika ukiachilia mbali hii gumzo ya kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki ambapo mwandishi mmoja kaonya nini labda kifanyike ili kufikia mafanikio.
Hapa Uganda tatizo ni umeme hakuna na hakuna mtu anayejali. Ila inasemekana ziko sababu kwanini kwa waganda hili sio tatizo la kulalamikiwa. Si umeme tu ila Uganda ina mambo kwelikweli: kwa mfano, Uganda inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi za jumuiya ya Madola mwakani ambapo Malkia wa Uingereza atakuwa ndio mgeni mkubwa kabisa. La kushangaza kuna juhudi kubwa za baadhi ya Wapinzani za kupinga mkutano huo kufanyika hapa kabisa. Ila yuko Bibie mmoja kaandika labda ni nini kinagaubaga juu ya hili.
Mwisho ni hili la hiki kitabu Da Vince Code, mengi ya msingi yameandikwa juu ya ubishi ambao umegubika toleo hili. Pia tunaulizwa hivi ni kwanini tunasoma?
Hapa Uganda tatizo ni umeme hakuna na hakuna mtu anayejali. Ila inasemekana ziko sababu kwanini kwa waganda hili sio tatizo la kulalamikiwa. Si umeme tu ila Uganda ina mambo kwelikweli: kwa mfano, Uganda inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa nchi za jumuiya ya Madola mwakani ambapo Malkia wa Uingereza atakuwa ndio mgeni mkubwa kabisa. La kushangaza kuna juhudi kubwa za baadhi ya Wapinzani za kupinga mkutano huo kufanyika hapa kabisa. Ila yuko Bibie mmoja kaandika labda ni nini kinagaubaga juu ya hili.
Mwisho ni hili la hiki kitabu Da Vince Code, mengi ya msingi yameandikwa juu ya ubishi ambao umegubika toleo hili. Pia tunaulizwa hivi ni kwanini tunasoma?
Friday, April 28, 2006
JOJI KICHAKA MAMBO MRAMA?
Leo nimesoma blog moja kutoka huko Amerika kwa Joji Kichaka. Kwa mfano hata hili shirika la ujasusi, CIA, mambo si shwari kwani Joji Kichaka kamfuta kazi bosi wa shirika hilo. Halafu hali ya mzozo wa silaha za nyuklia na Iran ndio inafanya mambo yawe magumu kwa Kichaka.
Tuesday, April 25, 2006
Ile sheria kandamizi-TAKRIMA-dhidi ya makabwera imefutiliwa mbali na mahakama ya katiba nchini Tanzania. Sijui watu kama Fredrick Sumaye na Andrew Chenge watakuwa na mawazo gani. Unajua nilifuatilia hotuba zao bungeni wakati wa kuundwa sheria hii nikachukizwa sana na maoni yao.
La msingi nimefurahi sana kwani angalau maana ya demokrasia inajionesha. Kuna utafiti nimefanya kuhusu hali ya kisiasa ya jimbo la Vunjo kule Moshi Tanzania ninatarajia kuuweka mtandaoni siku chache zijazo na pia nimejadili madhara ya sheria hii.
La msingi nimefurahi sana kwani angalau maana ya demokrasia inajionesha. Kuna utafiti nimefanya kuhusu hali ya kisiasa ya jimbo la Vunjo kule Moshi Tanzania ninatarajia kuuweka mtandaoni siku chache zijazo na pia nimejadili madhara ya sheria hii.
TFF NA SOKA LA TANZANIA USINGIZINI.
Wakati bado TFF haijampata kocha wa kuinoa timu ya Taifa-Taifa Stars-hapa Uganda viongozi wapya wa shirikisho la soka hapa Uganda-FUFA- tayari wamemleta mwalimu mpya wa timu hiyo kutoka Serbia. Kocha huyo ni Tomislav Sicic kutoka Serbia.
Viongozi wapya wa FUFA wameingia madarakani mapema mwaka huu tu na tayari wanafikiria juu ya safari ya timu hiyo ya Kombe la dunia na lile la Mataifa ya Africa.
Kama tunavyojua TFF walishaadiwa ushirikiano na Rais JK. Nataka tuwaulize hawa mabwana mbona wamelala? September si mbali wajameni. Nataka niangalie hii mikakati Tenga anayodai ipo je itafanikiwa?
Si soka tu ila Tanzania chini ya JK ni lazima ichukue hatua madhubuti ili kuendeleza michezo. Mimi ninaamini kama tutaendeleza michezo basi tutawainua vijana wengi ambao hawana ajira na hawatakaa waipate kutokana na fursa chache. Ninaunga mkono juhudi za serikali kufanikisha ziara ya timu ya ndondi wiki hii kwenda nchini Uhispania.
Hii ifanyike pia kwenye soka kwani ikiwa kombe la dunia litafanyika hapa Afrika hatuna budi tuanze leo kama wenzetu wa Uganda. Hainifurahishi kwa viongozi wa TFF kutuambia eti timu inakwenda Ushelisheli kwa mechi za kirafiki baada ya kualikwa huko. Pia eti Malawi imetualika kwa michezo ya kirafiki. Nasema hivi kwani inaonesha kwamba labda TFF hawana mipango madhubuti ila wanasubiri mialiko na kama isipokuja itakuwaje? Pia nataka nitoe rai ya makocha wazalendo hawakidhi haja ni muhimu tukawa na makocha kutoka Ulaya kwani tunahitaji mambo ambayo watanzania wenzangu hawana katika suala zima la kuiandaa timu ya Taifa. Kwa mfano, nina hakika kwa aina ya makocha tulionao nchini Tanzania si makini sana kwenye masuala ya kudhibiti wachezaji kinidhamu. Nidhamu ni msingi wa wachezaji kutekeleza wajibu wao na kama wachezaji wetu hawakai kambini na kufuata taratibu za kambi tusitarajie kufuzu kwenda Ghana au Afrika kusini 2010. Tayari hata katibu mkuu wa TFF, Tenga kakiri wachezaji wa Stars ni kama "chokaraa". Sijafurahishwa kabisa na hali ya sasa ambapo inabidi Tenga awakumbushe makocha akina Msola juu ya kutoa ruhusa. Hivi kweli tuna makocha wenye taaluma ya kutosha kuongoza timu ya Taifa? Jibu ni hatuna, hebu tujaribu kufuatilia timu kadhaa zitakapoanza kupiga kambi kwa ajili ya kombe la dunia kama utakuwa unasikia mchezaji kaomba ruhusa eti akachukue begi lake nyumbani kama wachezaji wetu wanavyofanya.
Alafu ni lazima tucheze na wapinzani wenye kutumia staili ya uchezaji kama ya wale tunaotarajia kukutana nao.Nionavyo mimi hii TFF bado ni kama FAT ya akina Rage na Ndolanga kwani bado sioni mabadiliko yenye kasi na ari mpya.
Viongozi wapya wa FUFA wameingia madarakani mapema mwaka huu tu na tayari wanafikiria juu ya safari ya timu hiyo ya Kombe la dunia na lile la Mataifa ya Africa.
Kama tunavyojua TFF walishaadiwa ushirikiano na Rais JK. Nataka tuwaulize hawa mabwana mbona wamelala? September si mbali wajameni. Nataka niangalie hii mikakati Tenga anayodai ipo je itafanikiwa?
Si soka tu ila Tanzania chini ya JK ni lazima ichukue hatua madhubuti ili kuendeleza michezo. Mimi ninaamini kama tutaendeleza michezo basi tutawainua vijana wengi ambao hawana ajira na hawatakaa waipate kutokana na fursa chache. Ninaunga mkono juhudi za serikali kufanikisha ziara ya timu ya ndondi wiki hii kwenda nchini Uhispania.
Hii ifanyike pia kwenye soka kwani ikiwa kombe la dunia litafanyika hapa Afrika hatuna budi tuanze leo kama wenzetu wa Uganda. Hainifurahishi kwa viongozi wa TFF kutuambia eti timu inakwenda Ushelisheli kwa mechi za kirafiki baada ya kualikwa huko. Pia eti Malawi imetualika kwa michezo ya kirafiki. Nasema hivi kwani inaonesha kwamba labda TFF hawana mipango madhubuti ila wanasubiri mialiko na kama isipokuja itakuwaje? Pia nataka nitoe rai ya makocha wazalendo hawakidhi haja ni muhimu tukawa na makocha kutoka Ulaya kwani tunahitaji mambo ambayo watanzania wenzangu hawana katika suala zima la kuiandaa timu ya Taifa. Kwa mfano, nina hakika kwa aina ya makocha tulionao nchini Tanzania si makini sana kwenye masuala ya kudhibiti wachezaji kinidhamu. Nidhamu ni msingi wa wachezaji kutekeleza wajibu wao na kama wachezaji wetu hawakai kambini na kufuata taratibu za kambi tusitarajie kufuzu kwenda Ghana au Afrika kusini 2010. Tayari hata katibu mkuu wa TFF, Tenga kakiri wachezaji wa Stars ni kama "chokaraa". Sijafurahishwa kabisa na hali ya sasa ambapo inabidi Tenga awakumbushe makocha akina Msola juu ya kutoa ruhusa. Hivi kweli tuna makocha wenye taaluma ya kutosha kuongoza timu ya Taifa? Jibu ni hatuna, hebu tujaribu kufuatilia timu kadhaa zitakapoanza kupiga kambi kwa ajili ya kombe la dunia kama utakuwa unasikia mchezaji kaomba ruhusa eti akachukue begi lake nyumbani kama wachezaji wetu wanavyofanya.
Alafu ni lazima tucheze na wapinzani wenye kutumia staili ya uchezaji kama ya wale tunaotarajia kukutana nao.Nionavyo mimi hii TFF bado ni kama FAT ya akina Rage na Ndolanga kwani bado sioni mabadiliko yenye kasi na ari mpya.
Sunday, April 23, 2006
RUBANI MLEVI--CHANZO CHA AJALI KENYA
Wajameni eti ile ajali ya ndege kule Kenya siku chache zilizopita ilisababishwa na ulevi wa rubani. Hii inaonesha ni jinsi gani sisi waafrika siku hizi hatujali nidhamu ya kazi. Inawezekanaje rubani mlevi aruhusiwe kupanda ndege?
HABARI ZA JUMAPILI YA LEO
Kila jumapili napata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbali na kuangalia kuna nini cha maana. Leo nimeona mengi: moja, kuna hili la wabunge kupenda kulipwa mishahara mikubwa, mwandishi mmoja katuhusia kuwa hili ni janga kwa mataifa ya kiafrika kama Kenya. Nafikiri pia hata kwa Tanzania makala hii itakuwa ina maana.
Pili pia kutoka Kenya, mara baada ya ajali ya ndege ambayo iliyamaliza maisha ya wabunge kadhaa wiki mbili zilizopita, mara Rais Kibaki anatangaza siku maalum ya maombi kwa Taifa.Mwandishi anatuhabarisha zaidi kunani mpaka maombi kwenye mambo ya kiserikali? Alafu kama ulinifuatilia wiki iliyopita niligusia juu ya ile Injili mpya ya Yuda Iscariot, yule anayedaiwa kuwa alimuuza Yesu kristu kwa fedha.Mwandishi anatuambia hata mapadri wamebaki kimya juu ya hili kama kweli Yuda ni msaliti au shujaa.
Alafu lililonifurahisha kabisa ni hii ziara ya Rais wa China huko Marekani na hasa juu ya nishati ya Nuklia ambayo inasemekana China ni mshikadau anayepaswa kuzingatiwa. Nafikiri ukisoma makala hii ni muhimu; utaelewa haya mambo ya mashindano ya silaha hizi kwa undani.
Kuna pia hili la maraisi wa Afrika kutaka kugombea urais zaidi ya kipindi kilichowekewa ukomo ili kukaa madarakani mpaka kifo.Iko habari moja huko Marekani, jamaa wanajiuliza vipi tena hivi hata kama hujawahi kuwa Raisi pia kuna ukomo wa kugombea.Jamani simnajua watu kama akina Mrema na Lipumba na akina Maalim Seif wataendelea kugombea sijui mpaka lini.
Hapa Uganda, inasemekana vyama vya upinzani vimeshindwa kutekeleza yale ambayo vinapaswa kufanya. Hali hapa si tofauti sana na upinzani wa kule Tanzania.
Mwisho kabisa nimeshangazwa kiasi fulani eti vijana wengi wa Kimarekani hawana habari na mambo ya msingi ya serikali yao. Hii imenifanya nivute pumzi na kuangalia huku kwetu na kwa kiasi fulani hata kwetu Tanzania na hata hapa hali ni moja tu.
Pili pia kutoka Kenya, mara baada ya ajali ya ndege ambayo iliyamaliza maisha ya wabunge kadhaa wiki mbili zilizopita, mara Rais Kibaki anatangaza siku maalum ya maombi kwa Taifa.Mwandishi anatuhabarisha zaidi kunani mpaka maombi kwenye mambo ya kiserikali? Alafu kama ulinifuatilia wiki iliyopita niligusia juu ya ile Injili mpya ya Yuda Iscariot, yule anayedaiwa kuwa alimuuza Yesu kristu kwa fedha.Mwandishi anatuambia hata mapadri wamebaki kimya juu ya hili kama kweli Yuda ni msaliti au shujaa.
Alafu lililonifurahisha kabisa ni hii ziara ya Rais wa China huko Marekani na hasa juu ya nishati ya Nuklia ambayo inasemekana China ni mshikadau anayepaswa kuzingatiwa. Nafikiri ukisoma makala hii ni muhimu; utaelewa haya mambo ya mashindano ya silaha hizi kwa undani.
Kuna pia hili la maraisi wa Afrika kutaka kugombea urais zaidi ya kipindi kilichowekewa ukomo ili kukaa madarakani mpaka kifo.Iko habari moja huko Marekani, jamaa wanajiuliza vipi tena hivi hata kama hujawahi kuwa Raisi pia kuna ukomo wa kugombea.Jamani simnajua watu kama akina Mrema na Lipumba na akina Maalim Seif wataendelea kugombea sijui mpaka lini.
Hapa Uganda, inasemekana vyama vya upinzani vimeshindwa kutekeleza yale ambayo vinapaswa kufanya. Hali hapa si tofauti sana na upinzani wa kule Tanzania.
Mwisho kabisa nimeshangazwa kiasi fulani eti vijana wengi wa Kimarekani hawana habari na mambo ya msingi ya serikali yao. Hii imenifanya nivute pumzi na kuangalia huku kwetu na kwa kiasi fulani hata kwetu Tanzania na hata hapa hali ni moja tu.
Sunday, April 16, 2006
NI PASAKA-ETI YUDA HAKUMSALITI YESU?
Nimepitia habari leo jumapili ya pasaka nikakunwa kuhifadhi haya: Moja Eti Yuda Eskarioti, yule mtume wa Yesu inasemekana ni shujaa na hakuna haja sisi waumini kumfikiria kama msaliti.bonyezahapa Eti inasemekana kuna injili ya Yuda ambayo kanisa limeikataa ambayo inaeleza kinagaubaga juu ya hili. Papa Benedict tayari ameikana ripoti iliyotolewa hivi karibuni juu ya injili ya Yuda. Nakwambia haya mambo mtu unaweza usiwe muumini wa dini yoyote. Sijui wanaglobu mnasemaje, mmeshafikiria hili? bonyeza hapa
Pia nikamsoma Papa Benedict-16 ana ujumbe gani leo hii. Ameushangaza umma kwa kubadilika kama kinyonga kinyume na alivyodhaniwa atakuwa Papa Ngangari.bonyeza
Pili, kuna huyu mtoto wa Mwalimu Nyerere, basi nikaamua nimsome nijue anaandika juu ya nini unajua inawezekana ana falsafa za baba yake. bonyezahapa
Alafu nikakunwa na umuhimu wa kuheshimu na kuilewa demokrasia, mwanamama mmoja kaandika kweli hapa Uganda. bonyeza
TUNAHITAJI SHIRIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI?
Jumuiya ya Afrika Mashariki imeingia katika hatua ya kuwa shirikishio. Ili kujua ni nini kinatarajiwa kufanyika, bonyezahapa ili umsome mwanamama ambaye atatuletea shirikisho. Pia kuna machache aliyoyasema Katibu mkuu wa jumuiya Bw Mushega wakati akiaga ili kuhitimisha muhula wake. Amemponda sana Bw Njonjo, waziri wa zamani wa Kenya kwa kuiponda jumuiya.Hebu soma mahojiano kamili ya mwanadiplomasia huyo aliyemaliza muda wake.Pia kuna ripoti maalum ambayo itatolewa hivi karibuni juu ya kama kweli hii jumuiya inawezekana.Hapa nataka tusome taarifa tangulizi ya ripoti hiyo.
Mimi sio muungaji mkono sana Shirikisho ila tu jumuiya manake najua ni ndoto. Hata JK bado anaweka msisitizo zaidi kwenye SADC. Ila kwa baadhi ya wananchi wana wasiwasi juu ya hizi nchi za Rwanda na Burundi kwani zitatuletea balaa.
Mimi sio muungaji mkono sana Shirikisho ila tu jumuiya manake najua ni ndoto. Hata JK bado anaweka msisitizo zaidi kwenye SADC. Ila kwa baadhi ya wananchi wana wasiwasi juu ya hizi nchi za Rwanda na Burundi kwani zitatuletea balaa.
Friday, April 14, 2006
TANZANIA KUWA BORA KULIKO UGHAIBUNI--JK.
Unajua mara nyingi nikisoma anayosema JK kila anapopewa nafasi huwa ninacheka alafu ninajaribu kufikiri hivi kweli itawezekana?
Leo anaripotiwa eti ataondoa ile kasumba ya wasomi kukimbilia ughaibuni.somahapa
Haya hebu ngoja tuishi kwa matumaini manake huyu jamaa anafurahisha sana. Ila nimefurahishwa na makala moja hapa Uganda juu ya tatizo la utegemezi wetu waafrika huko ughaibuni.Nimeona ni vizuri tulinganishe yaliyojadiliwa hapa na hayo JK anayosema alafu tuamue je kweli JK ataweza kuboresha na kuzuia tamaa ya kwenda Ughaibuni?somahapa
Leo anaripotiwa eti ataondoa ile kasumba ya wasomi kukimbilia ughaibuni.somahapa
Haya hebu ngoja tuishi kwa matumaini manake huyu jamaa anafurahisha sana. Ila nimefurahishwa na makala moja hapa Uganda juu ya tatizo la utegemezi wetu waafrika huko ughaibuni.Nimeona ni vizuri tulinganishe yaliyojadiliwa hapa na hayo JK anayosema alafu tuamue je kweli JK ataweza kuboresha na kuzuia tamaa ya kwenda Ughaibuni?somahapa
Sunday, April 09, 2006
MTANZANIA KASHIKWA UGONI HOTELINI NA MWANABALOZI
Ni wiki moja sasa ambapo mwanadiplomasia mmoja wa Rwanda alizusha sekeseke kama sio kasheshe pale alipokamatwa ndani ya hoteli moja ya kitalii akijinjiri na mwanamama mmoja ambaye ni mke wa mtu. somahapa
Mengi yamesemwa ila pia kumekuwa na utata juu ya kukamatwa kwa mwanadiplomasia anavunja sheria za nchi ikimaanisha ni kuvunja mkataba wa Vienna.Ila hili limefanunuliwa vizuri na msomi mmoja hapa Uganda somahapa
Sina hakika kama ninavunja Azimio la Dodoma, ila napenda nieleze kushtushwa kwangu eti mwanamama huyo alikuwa ni Mtanzania.
La msingi nataka nitoe hoja na ijadiliwe: Hivi kuwa mwanabalozi ndio tiketi ya kufanya maovu? Eti ukifanikiwa kuhodhi au kumiliki kile kitambulisho cha uanadiplomasia basi ndio mwisho wa kubughudhiwa na wakora-mapolisi na wanausalama wengine?
Serikali ya Rwanda imelalamika sana juu ya kukamatwa mwanadiplomasia wao. Ila zaidi ni kwamba kuna hali tete sana katika tukio hili: Unajua kuna uadui mkubwa sana kati ya Museveni na Kagame na hali hii imepelekea mwanamama, ndugu yetu mtanzania mwenzetu kuhusishwa katika kuendeleza sokomoko kati ya wakubwa wawili hawa.
Unaambiwa udikteta wa Museveni sasa unaingilia starehe za watu bonyezahapa na kuzihusisha katika kuaibishana kati ya serikali hizi mbili. Mambo si mambo hapa. bonyeza hapa
Mengi yamesemwa ila pia kumekuwa na utata juu ya kukamatwa kwa mwanadiplomasia anavunja sheria za nchi ikimaanisha ni kuvunja mkataba wa Vienna.Ila hili limefanunuliwa vizuri na msomi mmoja hapa Uganda somahapa
Sina hakika kama ninavunja Azimio la Dodoma, ila napenda nieleze kushtushwa kwangu eti mwanamama huyo alikuwa ni Mtanzania.
La msingi nataka nitoe hoja na ijadiliwe: Hivi kuwa mwanabalozi ndio tiketi ya kufanya maovu? Eti ukifanikiwa kuhodhi au kumiliki kile kitambulisho cha uanadiplomasia basi ndio mwisho wa kubughudhiwa na wakora-mapolisi na wanausalama wengine?
Serikali ya Rwanda imelalamika sana juu ya kukamatwa mwanadiplomasia wao. Ila zaidi ni kwamba kuna hali tete sana katika tukio hili: Unajua kuna uadui mkubwa sana kati ya Museveni na Kagame na hali hii imepelekea mwanamama, ndugu yetu mtanzania mwenzetu kuhusishwa katika kuendeleza sokomoko kati ya wakubwa wawili hawa.
Unaambiwa udikteta wa Museveni sasa unaingilia starehe za watu bonyezahapa na kuzihusisha katika kuaibishana kati ya serikali hizi mbili. Mambo si mambo hapa. bonyeza hapa
MPASUKO WA KISIASA PEMBA
Nimesoma makala moja kwenye IPP Media ikanikuna sana. Unajua hii siasa ya Pemba watanzania wengi hatuifahamu kabisa. Ule MPASUKO wa kisiasa JK aliodai upo eti inasemekana hata yeye hajui kuuziba.
Kujua zaidi hebu soma makala hii: bonyeza
Zaidi ya hapo, mwandishi kaongeza makala yake katika sehemu ya pili akichambua zaidi hasa baada ya kiongozi wa chama pinzani, CUF, kufika pia Pemba na kumsifia JK. bonyezahapa
Lakini inafurahisha zaidi kwani JK kasifiwa na wasomi wa Bongo juu ya jinsi ambavyo analifuatilia suala la Muungano.
Kujua zaidi hebu soma makala hii: bonyeza
Zaidi ya hapo, mwandishi kaongeza makala yake katika sehemu ya pili akichambua zaidi hasa baada ya kiongozi wa chama pinzani, CUF, kufika pia Pemba na kumsifia JK. bonyezahapa
Lakini inafurahisha zaidi kwani JK kasifiwa na wasomi wa Bongo juu ya jinsi ambavyo analifuatilia suala la Muungano.
Sunday, April 02, 2006
JK SIKU 100
Eti rais Jakaya Kikwete kafikisha siku mia moja madarakani. bonyeza hapa Binafsi nafikiri anastahili pongezi.
Ila leo kanifurahisha zaidi katika kupambana na majambazi kwani kaanzisha kikosi maalum dhidi ya ujambazi; bonyezahapa ni hatua ya muhimu nainga mkono.
Ila tahadhari imetolewa leo hii juu ya utendaji mzima wa serikali ya JK kama inataka iendeleze mafanikio zaidi ya haya yaliyotokea kwa siku mia moja. somahapa
Ila leo kanifurahisha zaidi katika kupambana na majambazi kwani kaanzisha kikosi maalum dhidi ya ujambazi; bonyezahapa ni hatua ya muhimu nainga mkono.
Ila tahadhari imetolewa leo hii juu ya utendaji mzima wa serikali ya JK kama inataka iendeleze mafanikio zaidi ya haya yaliyotokea kwa siku mia moja. somahapa
Sunday, March 19, 2006
HABARI ZA LEO MAGAZETINI
Katika pitiapitia yangu ya habari leo nimekunwa na jinsi wanaume wa siku hizi wanavyochagua wanawake wanaowapenda wawe wenza wao. Mwandishi kaandika kwelikweli na akaonya sana juu ya makosa tufanyayo sisi wanaume. somahapa . Kuna hili la haki za ukombozi wa wanawake: inasemekana wengine wamejisahau na wakavuka mipaka. soma
Habari nyingine ni kuwa eti dunia ya leo mambo ya elimu sio tena msingi wa kufanikiwa kimaisha. Ukisoma mwandishi wa makala ile ameniacha nikipigwa butwaa ni kwanini ninasoma sasa? bonyezahapa
Alafu ningependa tumsome raisi wa hapa Yoweri Museveni katika mahojiano yake ya kwanza tangu achaguliwe kuwa raisi hivi majuzi. bonyeza
Habari nyingine ni kuwa eti dunia ya leo mambo ya elimu sio tena msingi wa kufanikiwa kimaisha. Ukisoma mwandishi wa makala ile ameniacha nikipigwa butwaa ni kwanini ninasoma sasa? bonyezahapa
Alafu ningependa tumsome raisi wa hapa Yoweri Museveni katika mahojiano yake ya kwanza tangu achaguliwe kuwa raisi hivi majuzi. bonyeza
Saturday, March 18, 2006
HISTORIA KUJIRUDIA KOMBE LA MABINGWA ULAYA?
Arsenal ndio timu pekee kutoka ligi kuu ya Uingereza iliyobakia katika ligi ya mabingwa Ulaya. Sikutarajia hili kabisa ila napenda niwasifu wapiga bunduki wa London kwa hili. Waingereza huwa wanasema ‘due credit’.
Hii siyomara ya kwanza Arsenal kufikia hatua hii ya robo fainali ila emeweka rekodi ya ulaya kuiondoa Real Madrid. Hii, kwa kuzingatia misingi ya kihistoria katika soka la Ulaya, Arsenal itafika fainali kama kweli historia hujirudia. Nimechambua historia ya mashindano haya inaonesha kila timu iliyoweza kuondoa Real Madrid ilifika fainali. Hebu tujitahidi kukumbuka Bayern Munich, AC Milan, Juventus na Monaco katika miaka kadhaa michache iliyopita.
Ushindi wa Benfica dhidi ya Liverpool ni historia nyingine katika soka la Ulaya. Sio tu ni timu ya kwanza kuiondoa Liverpool katika vikombe vya Ulaya bali pia ni timu ya kwanza barani Ulaya kuifunga Liverpool ugenini na nyumbani tangu mwaka 2001/ 2002. Hii inanifanya niamini kuwa timu yeyote yenye uwezo wa kuiondoa Man United na Liverpool katika mashindano ni bora kufikia fainali. Labda hapa niwakumbushe kuwa Bayer Leverkusen iliiondoa Liverpool mwaka 2001/ 2002 na ikatinga fainali. Porto chini ya mtaalam Mourinho iliiondoa Man United mwaka 2003/ 2004 na wakafika fainali na kushinda.
Hadi sasa Arsenal wana rekodi bora kabisa ya kufungwa magoli mawili tu na ni timu pekee pamoja na Barcelona hazijapoteza mchezo wowote. Timu imebadilika ikicheza kwa umoja na nidhamu ya mchezo katika kulinda na kushambulia.
Kwa upande wa Chelsea, iliaminika na wengi kwamba ingeondolewa tu. Barcelona ni timu yenye vipaji asili (natural) pamoja na ufundi wa hali ya juu. Ukizingatia timu ya Mourinho inayotegemea ufundi wa kisayansi—yaani mtizamo wa kibinadamu (artificial) niwazi njia za asili zingeshinda tu. Kushinda ligi ya mabingwa unahitaji wachezaji wenye vipaji vya asili ambavyo vituvizidi vile vya kufundishwa na walimu wa timu pinzani. Mourinho alikosa jibu la Lionel Messi na Ronaldino katika timu yake.
Liverpool haina wafungaji magoli na ndio maana ikatolewa. Unapopata nafasi nyingi za kufunga alafu hufungi magoli ninachoweza kusema ni kuwa timu ni mbovu. Magoli ndio kiashirio cha ushindi na wala sio chati ya vielelezo vya umilikaji au majaribio mangapi timu imefanya golini mwa timu pinzani.
Mwisho, Liverpool kuondolewa katika ligi ya mabingwa ni sheria wala sio jambo la kustaajabisha. Hakuna bingwa mtetezi aliyewahi kutetea kombe hili. Arsenal wanalihitaji kombe hili na inaonekana matumaini yapo. Kwani nina hakika Juventus watapata shida sana kuenda na kasi na ari ya Arsenal. Hebu tusubiri robo fainali tuone.
Hii siyomara ya kwanza Arsenal kufikia hatua hii ya robo fainali ila emeweka rekodi ya ulaya kuiondoa Real Madrid. Hii, kwa kuzingatia misingi ya kihistoria katika soka la Ulaya, Arsenal itafika fainali kama kweli historia hujirudia. Nimechambua historia ya mashindano haya inaonesha kila timu iliyoweza kuondoa Real Madrid ilifika fainali. Hebu tujitahidi kukumbuka Bayern Munich, AC Milan, Juventus na Monaco katika miaka kadhaa michache iliyopita.
Ushindi wa Benfica dhidi ya Liverpool ni historia nyingine katika soka la Ulaya. Sio tu ni timu ya kwanza kuiondoa Liverpool katika vikombe vya Ulaya bali pia ni timu ya kwanza barani Ulaya kuifunga Liverpool ugenini na nyumbani tangu mwaka 2001/ 2002. Hii inanifanya niamini kuwa timu yeyote yenye uwezo wa kuiondoa Man United na Liverpool katika mashindano ni bora kufikia fainali. Labda hapa niwakumbushe kuwa Bayer Leverkusen iliiondoa Liverpool mwaka 2001/ 2002 na ikatinga fainali. Porto chini ya mtaalam Mourinho iliiondoa Man United mwaka 2003/ 2004 na wakafika fainali na kushinda.
Hadi sasa Arsenal wana rekodi bora kabisa ya kufungwa magoli mawili tu na ni timu pekee pamoja na Barcelona hazijapoteza mchezo wowote. Timu imebadilika ikicheza kwa umoja na nidhamu ya mchezo katika kulinda na kushambulia.
Kwa upande wa Chelsea, iliaminika na wengi kwamba ingeondolewa tu. Barcelona ni timu yenye vipaji asili (natural) pamoja na ufundi wa hali ya juu. Ukizingatia timu ya Mourinho inayotegemea ufundi wa kisayansi—yaani mtizamo wa kibinadamu (artificial) niwazi njia za asili zingeshinda tu. Kushinda ligi ya mabingwa unahitaji wachezaji wenye vipaji vya asili ambavyo vituvizidi vile vya kufundishwa na walimu wa timu pinzani. Mourinho alikosa jibu la Lionel Messi na Ronaldino katika timu yake.
Liverpool haina wafungaji magoli na ndio maana ikatolewa. Unapopata nafasi nyingi za kufunga alafu hufungi magoli ninachoweza kusema ni kuwa timu ni mbovu. Magoli ndio kiashirio cha ushindi na wala sio chati ya vielelezo vya umilikaji au majaribio mangapi timu imefanya golini mwa timu pinzani.
Mwisho, Liverpool kuondolewa katika ligi ya mabingwa ni sheria wala sio jambo la kustaajabisha. Hakuna bingwa mtetezi aliyewahi kutetea kombe hili. Arsenal wanalihitaji kombe hili na inaonekana matumaini yapo. Kwani nina hakika Juventus watapata shida sana kuenda na kasi na ari ya Arsenal. Hebu tusubiri robo fainali tuone.
Thursday, March 16, 2006
MKAPAISIM--LEGASI YA AWAMU YA TATU
Mimi ni mmoja wa watanzania wachache sana ambao wakati JK anaingia madarakani sikuwa namwamini kabisa. Unajua nimezaliwa nikakuwa nikiona wanasiasa wa CCM wakituongoza kwa migengwe ya kila aina. Ndio maana niliwahi kuandika JK Anatania tu. SOMA
Kama nilivyosema katika makala ile, kuwa JK anawafahamu walarushwa waliojikia mizizi ndani ya dola. Na nikahisi ataendeleza sera ya kulindana ya aliyemtanglia, mheshimiwa Mkapa. Nafurahi kusema kwa ninayoyaona sasa, JK kadhihirisha kuwa nilikosea. Kwa kiasi fulani ninaanza kuona Kasi Mpya. Na hii ni wazi kwangu ni juu ya suala la “Ujambazi”.
Ninasoma habari jinsi ambavyo serikali imewavalia njuga baadhi ya matajiri ambao wanalea majambazi nikafurahi sana. Imani yangu imeanza kumea kwani nataka niseme baadhi ya matajiri waliokamatwa ni watu ambao wamekuwa wakitawala tetesi kuwa ni majambazi tangu nikiwa mtoto nasoma shule ya msingi. Kwa hiyo mimi nimefurahishwa na hatua ya serikali.
Labda nimkumbushe kamanda Saidi Mwema kuwa tafadhali hakikisha dola inajua shughuli za wenye fedha wote. Kuna umuhimu wa serikali kujua baadhi ya wafanyabishara wanapata wapi mitaji mikubwa ya kuendeshea miradi yao feki. Utandawazi isiwe ndio mwanzo wa watu kuachiwa huru kujifanyia chochote watakacho. Nikumbushe pia hawa wafanyabiashara wanajihusisha na vigogo wa serikali; hivyo ni muhimu na vigogo kadhaa waanze kuhoiwa kama kweli tunataka kupambana na ujambazi kwa ari mpya na kasi mpya. Hii mambo ya kuhamisha baadhi ya maofisa polisi na kuwapeleka jijini makao makuu nataka niseme ni doa katika hii vita ya ujambazi. Yaani mtu anahamishwa eti kutoka mkoa unaosemekana ni kitovu cha ujambazi alafu anakwenda makao makuu? Kwa nini tusiwastaafishe watu kama hawa kwa manufaa ya umma? Hapa nimechanganyikiwa kabisa.
Katika gazeti la Nipashe toleo la tarehe 10/3 nilisoma eti kuna afisa wa polisi eti akaunti zake zimesimamishwa. Hakutajwa kwa jina na mimi naona nisimtaje ila walipoandika eti anatoka mikoa ya kaskazini hisia zangu zilinicheza. Unajua Tanzania watu wa kawaida wanaishi na kuzungumza tetesi nyingi sana. Ila tatizo ni kwamba hasa kipindi cha Mkapa alikuwa akipiga tetesi kabisa. Alikuwa anasisitiza eti wananchi walete ushahidi. Dhihirisho la jinsi ambavyo alivyokuwa anapenda kulea watendaji wake, wengi wao wakiwa wala rushwa na mafisadi wakubwa. Hii madhila ya jeshi la polisi ni dhihirisho la sera mbovu za uongozi mbovu wa awamu iliyopita.
Madhila ya ujambazi tunayoyaona leo ni matokeo ya sera: MKAPAISM—kuficha maovu, wala rushwa, mafisadi na kutochukua hatua dhidi ya maafisa wakubwa wa serikali pale walipokwenda mrama. Hii ilipelekea kwa mfano jeshi la polisi likafika mahali haliheshimu hata raia. Jeshi linaendeshwa kama mali ya mtu binafsi bwana. Nakumbuka kila mara ninapokuwa kule Moshi huwa nashangaa sana. Sina hakika kama ni watu wote wanashangaa kama mimi pale unapoona askari polisi wa usalama barabarani wanasimamisha vipanya navyo havisimami na unasikia kondakta akitumwa akawaone hawa mabwana. Huko nasikia huwa anapeleka noti ya shilingi 1500 au 2000. Huwa nabaki kujiuliza je hawa ni wafanyakazi wa umma au wakusanya ushuru? Kama unataka kuyaona haya nenda karibu na kituo cha mabasi Moshi Mjini sehemu inaitwa BORA, kuna nguzo ya umeme na utakuta askari kasimama pale mida ya asubuhi.
Hapa kamanda Saidi Mwema atajiju kwani jeshi letu la polisi lilikuwa likiendeshwa bila maadili, kizamani na kila aina ya michezo michafu. Mwisho, niulize: polisi imewatia kizuizini matajiri kadhaa lakini nikumbushe kitu kimoja: wataalam wa sosholojia wanasema wanawake pia wanajihusisha sana na uhalifu. Mbona hamjawatia lupango Wabejing? Wanalea majambazi sana pia.
Kama nilivyosema katika makala ile, kuwa JK anawafahamu walarushwa waliojikia mizizi ndani ya dola. Na nikahisi ataendeleza sera ya kulindana ya aliyemtanglia, mheshimiwa Mkapa. Nafurahi kusema kwa ninayoyaona sasa, JK kadhihirisha kuwa nilikosea. Kwa kiasi fulani ninaanza kuona Kasi Mpya. Na hii ni wazi kwangu ni juu ya suala la “Ujambazi”.
Ninasoma habari jinsi ambavyo serikali imewavalia njuga baadhi ya matajiri ambao wanalea majambazi nikafurahi sana. Imani yangu imeanza kumea kwani nataka niseme baadhi ya matajiri waliokamatwa ni watu ambao wamekuwa wakitawala tetesi kuwa ni majambazi tangu nikiwa mtoto nasoma shule ya msingi. Kwa hiyo mimi nimefurahishwa na hatua ya serikali.
Labda nimkumbushe kamanda Saidi Mwema kuwa tafadhali hakikisha dola inajua shughuli za wenye fedha wote. Kuna umuhimu wa serikali kujua baadhi ya wafanyabishara wanapata wapi mitaji mikubwa ya kuendeshea miradi yao feki. Utandawazi isiwe ndio mwanzo wa watu kuachiwa huru kujifanyia chochote watakacho. Nikumbushe pia hawa wafanyabiashara wanajihusisha na vigogo wa serikali; hivyo ni muhimu na vigogo kadhaa waanze kuhoiwa kama kweli tunataka kupambana na ujambazi kwa ari mpya na kasi mpya. Hii mambo ya kuhamisha baadhi ya maofisa polisi na kuwapeleka jijini makao makuu nataka niseme ni doa katika hii vita ya ujambazi. Yaani mtu anahamishwa eti kutoka mkoa unaosemekana ni kitovu cha ujambazi alafu anakwenda makao makuu? Kwa nini tusiwastaafishe watu kama hawa kwa manufaa ya umma? Hapa nimechanganyikiwa kabisa.
Katika gazeti la Nipashe toleo la tarehe 10/3 nilisoma eti kuna afisa wa polisi eti akaunti zake zimesimamishwa. Hakutajwa kwa jina na mimi naona nisimtaje ila walipoandika eti anatoka mikoa ya kaskazini hisia zangu zilinicheza. Unajua Tanzania watu wa kawaida wanaishi na kuzungumza tetesi nyingi sana. Ila tatizo ni kwamba hasa kipindi cha Mkapa alikuwa akipiga tetesi kabisa. Alikuwa anasisitiza eti wananchi walete ushahidi. Dhihirisho la jinsi ambavyo alivyokuwa anapenda kulea watendaji wake, wengi wao wakiwa wala rushwa na mafisadi wakubwa. Hii madhila ya jeshi la polisi ni dhihirisho la sera mbovu za uongozi mbovu wa awamu iliyopita.
Madhila ya ujambazi tunayoyaona leo ni matokeo ya sera: MKAPAISM—kuficha maovu, wala rushwa, mafisadi na kutochukua hatua dhidi ya maafisa wakubwa wa serikali pale walipokwenda mrama. Hii ilipelekea kwa mfano jeshi la polisi likafika mahali haliheshimu hata raia. Jeshi linaendeshwa kama mali ya mtu binafsi bwana. Nakumbuka kila mara ninapokuwa kule Moshi huwa nashangaa sana. Sina hakika kama ni watu wote wanashangaa kama mimi pale unapoona askari polisi wa usalama barabarani wanasimamisha vipanya navyo havisimami na unasikia kondakta akitumwa akawaone hawa mabwana. Huko nasikia huwa anapeleka noti ya shilingi 1500 au 2000. Huwa nabaki kujiuliza je hawa ni wafanyakazi wa umma au wakusanya ushuru? Kama unataka kuyaona haya nenda karibu na kituo cha mabasi Moshi Mjini sehemu inaitwa BORA, kuna nguzo ya umeme na utakuta askari kasimama pale mida ya asubuhi.
Hapa kamanda Saidi Mwema atajiju kwani jeshi letu la polisi lilikuwa likiendeshwa bila maadili, kizamani na kila aina ya michezo michafu. Mwisho, niulize: polisi imewatia kizuizini matajiri kadhaa lakini nikumbushe kitu kimoja: wataalam wa sosholojia wanasema wanawake pia wanajihusisha sana na uhalifu. Mbona hamjawatia lupango Wabejing? Wanalea majambazi sana pia.
Pamoja na kumkandia Mkapa na "Mkapaism yake" nafikiri ni bora pia tujue anaendeleaje na mapumziko yake. Hebu bonyeza hapa uone.
Sunday, March 12, 2006
USHOGA KUKUBALIKA KAMA DESTURI HIVI KARIBUNI
Nimekutana na makala moja ambayo imenikuna sana juu ya ushoga.
Ama kweli hivi majuzi katika nishani za Oskar kule kwa Joji Kichaka, walifikia mahali na kuitunza filamu ya ushoga.
Kwa kweli nina wasiwasi sasa si muda mrefu 'Ushoga utakuwa sio dhambi'. Jamani mimi nimechanganyikiwa manake sasa wazungu wanatuwekea viwango kwenye kila kitu. Na wakishapitisha kwamba kitu fulani ni bora ndio hivyo tena sisi makabwela tunaona ni fasheni. Bonyeza hapa uone yuko mzungu mmoja hapa Uganda ana maoni fulani.
Ama kweli hivi majuzi katika nishani za Oskar kule kwa Joji Kichaka, walifikia mahali na kuitunza filamu ya ushoga.
Kwa kweli nina wasiwasi sasa si muda mrefu 'Ushoga utakuwa sio dhambi'. Jamani mimi nimechanganyikiwa manake sasa wazungu wanatuwekea viwango kwenye kila kitu. Na wakishapitisha kwamba kitu fulani ni bora ndio hivyo tena sisi makabwela tunaona ni fasheni. Bonyeza hapa uone yuko mzungu mmoja hapa Uganda ana maoni fulani.
NCHI INAPOMILIKISHWA KWA MTU BINAFSI
Ama kweli kuna viongozi wanaopenda kumiliki nchi kama mali yao. soma hapa
Tuesday, March 07, 2006
MAMBO YA LUGHA NA FRED MACHA
Makala ya Fred Macha imenikosha na nimeona niifadhi ili tuisome na tujikumbushe umuhimu wa kulea lugha yetu. soma
Subscribe to:
Posts (Atom)