My Blog List

Wednesday, November 24, 2010

BARAZA LA MAWAZIRI LATANGAZWA



Hatimaye Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr.Jakaya Kikwete amelitangaza baraza lake la mawaziri. Taarifa kutoka Mawasiliano Ikulu imesomeka kama ilivyo hapo chini.

Katika Muundo wa Serikali hakuna mabadiliko makubwa isipokuwa yafuatayo:

1. Idara ya Umwagiliaji tumeiunganisha na Kilimo ambako ndipo ilipokuwa zamani.

a. Imeonekana upangaji wa maendeleo ya kilimo unakuwa hauna hakika bila ya umwagiliaji kuwa sehemu ya kilimo. Tuliihamishia maji kurahisisha pia upangaji na hasa kwa vile maji ndiyo wanaotoa haki ya matumizi ya maji.

b. Kwa kuwa tatizo la uhaba wa maji ya binadamu ni kubwa sana na tunataka tuongeze kasi ya kukabiliana na tatizo hilo tumeona tuiondolee wizara hii mzigo wa umwagiliaji ili ibaki na kazi moja tu ya kuhakikisha kuwa watu wanapata maji safi na salama mita 400 kutoka wanapoishi.

2. Idara ya Vijana tumeihamisha kutoka Wizara ya Kazi na kuihamishia Wizara ya Habari kwa sababu kuu 2.

a. Kwanza inashabihiana na michezo na utamaduni.

b. Tunataka Wizara ya Kazi ipate muda wa kutosha wa kushughulikia masuala ya ajira na wafanyakazi ambayo sasa yamepanuka.

3. Shughuli za Uwezeshaji wa Wananchi zilizokuwa Wizara ya Fedha na Wizara ya Kazi zitahamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu.

4. Marekebisho mengine ni madogo:

a. Katika Ofisi ya Rais tunairudisha shughuli ya mahusiano na jamii hivyo tunaongeza Waziri wa Nchi ambaye pia atashughulikia shughuli zilizopanuka za Tume ya Mipango, MKURABITA na TASAF.

b. Katika Ofisi ya Waziri Mkuu tutakuwa na Waziri wa Nchi wa kushughulikia Uwekezaji na Uwezeshaji wa Wananchi.

c. Katika Ofisi ya Waziri Mkuu Wizara ya TAMISEMI tumeongeza Naibu Waziri wa kushughulikia masuala ya Elimu.

Baada ya kusema hayo nitangaze orodha yetu:

MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

Ofisi ya Rais

1. WN – OR – Utawala Bora
Mathias Chikawe
2. WN – OR – Mahusiano na Uratibu
Stephen Wassira
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Hawa Ghasia
Ofisi ya Makamu wa Rais
1. Muungano
Samia Suluhu
2. Mazingira
Dr. Terezya Luoga Hovisa
Ofisi ya Waziri Mkuu
1. Sera, Uratibu na Bunge
William Lukuvi
2. Uwekezaji na Uwezeshaji
Dr. Mary Nagu

Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
George Huruma Mkuchika
1.Aggrey Mwanri
2. Kassim Majaliwa

Wizara ya Fedha
Mustapha Mkulo
1. Gregory Teu
2. Pereira Ame Silima
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Shamsi Vuai Nahodha
1. Balozi Khamis Suedi Kagasheki
Wizara ya Katiba na Sheria
Celina Kombani
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Bernard K. Membe
1. Mahadhi Juma Mahadhi
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Dr. Hussein Ali Hassan Mwinyi
Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. Mathayo David Mathayo
1. Benedict Ole Nangoro
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
1. Charles Kitwanga
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Prof. Anna Tibaijuka
Goodluck Ole Madeye

Wizara ya Maliasili na Utalii
Ezekiel Maige

Wizara ya Nishati na Madini
William Mganga Ngeleja
1. Adam Kigoma Malima

Wizara ya Ujenzi
Dr. John Pombe Magufuli
1. Dr. Harrison Mwakyembe
Wizara ya Uchukuzi
Omari Nundu
1. Athumani Mfutakamba

Wizara ya Viwanda na Biashara
Dr. Cyril Chami
Lazaro Nyalandu

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru Kawambwa
1. Philipo Mulugo

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Haji Hussein Mpanda
1. Dr. Lucy Nkya

Wizara ya Kazi na Ajira
Gaudensia Kabaka
Makongoro Mahanga

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Sophia Simba
Umi Ali Mwalimu

Wizara ya Habari, Vijana na Michezo
Emmanuel John Nchimbi
1. Dr. Fenella Mukangara

Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Samuel John Sitta
Dr. Abdallah Juma Abdallah

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika
Prof. Jumanne Maghembe
1. Christopher Chiza

Wizara ya Maji
Prof. Mark James Mwandosya
Eng. Gerson Lwinge

Nitawaapisha Jumamosi tarehe 27 Novemba, 2010 saa 05:00 asubuhi

Sunday, November 21, 2010

VITI MAALUM - ITAFUTWE FOMULA NYINGINE

Binafsi sipendi kabisa kusikia mtu anatambulishwa kama Mbunge wa Viti maalum. Sidhani kna manufaa yoyote ya umma kutoka kwa wabunge hawa. Hii ni upotezaji wa fedha za umma kwa wabunge ambao sijaona wana tija gani bungeni.
Naomba nipewe jina la mbunge wa viti maalum ambaye amewahi kuwa agitative enough kuonesha anawakilisha kundi fulani la jamii. Itafutwe fomula nyingine ya kupata wabunge hawa, kwa mfano kuwe kuna uchaguzi wa mbunge mwanamke kila mkoa kwa kushindanisha kila chama kutoa mgombea wakati wa uchaguzi.Hii itasaidia kupunguza matumizi yasiyo na tija.

Ndio maana nashangaa kwa nini wako zaidi ya 100 sasa bungeni, je hii ni nzuri kwa mwanamke wa kawaida ama ni mradi wa kifisadi?

DU! CHADEMA AU CCM, NANI YUKO SAHIHI?

Eti Jakaya Kikwete alichaguliwa kwa udini au siasa? Je ni kweli kuna udini Tanzania? Kuna jamaa kajadili hapa, kasheshe kwelikweli. Hii demokrasia yetu bwana, ina vituko sana,yaani kama ni kweli Raisi anajiandaa kufanya uteuzi huku baadhhi ya wabunge wanamshinikiza ni wizara ipi awape. Hapa Rais wa nchi ni yupi? Anayejichagulia cheo au anayetoa cheo? Jiulizeni.

Kuna madai kuwa wabunge wa chadema wamegawanyika wengine wakiona kuwa walikosea. Huu ni wakati wabunge waelewe kuwa in order to prevent the country not been thrown to the dogs completely, ni wakati wa ujasiri. Kama ni kweli Chadema wako makini na wana dhamira basi tutarajie kuwa tanaweza shuhudia maandamano na hata mikutano ya hadhara tena siku si nyingi. Nchi imefika mahali panapohitaji mkombozi na ni vyema wajiandae, kwani kuwa upinzani si kupiga makofi tu mjengoni bali ni kazi haswa.

Kitendo cha Chadema kina asili ya kihistoria.

Saturday, November 20, 2010

CHADEMA WANA KAZI KUITHIBITISHIA JAMII JUU YA UHALALI WA KUSUSA BUNGE

Watu wameendelea kuilamu Chadema kumgomea Raisi Kikwete Bungeni.
Inaelekea CCM watazua hoja binafsi Bungeni kuwaadhibu wabunge wa Chadema. Hapa napo ni utata mtupu, kwani yatatokea yaleyale ya Zitto Kabwe.
Mtizamo wangu ni kuwa nadhani ni vyema Chadema watoe maelezo ya kina kwanini waliamua kufanya vile. Manaake watanzania wengi wanalitizama tukio lile kama vile kukosa adabu.Inashangaza sana kuwa watanzania wengi hawaelewi njia mbalimbali ambazo ni sehemu ya kuwasilisha ujumbe kuwa kuna tatizo linahitaji ufumbuzi.
Inaonekana nchi imejaa "laymen" wengi sana ambao kwao wanaaona nchi yetu inatawaliwa vizuri. Ukisoma makala hii katika "The Citizen" la leo ni wazi hata wasomi wengi wanahimiza eti kuwe na dialogue, maridhiano. Hivi kweli tunahitaji maridhiano hapo ama ni Katiba ibadilishwe?

KATIBA MPYA NDIO SULUHISHO
Watu kadhaa wanatoa maoni na mitizamo yao kuwa Katiba kama
sheria mama
, ni wakati wa kutengenezwa upya.

SPIKA MWANAMKE - ILIKUWA SAHIHI?
Unajua wengi wamesema na hata mimi naamini kilichotokea ni ubaguzi wa kijinsia. Kinachobakia ni mama kuhakikisha she has to prove wrong that she's an agents of the mafisadi. Ningependa tumsome huyu mzee hapo chini ana mtizamo wake juu ya hili:

Is the procedure to elect House Speaker fundamentally flawed?

digg
By Karl Lyimo
Last Friday, Tanzania came into a newly constituted National Assembly – ‘Bunge’ – and a new Speaker, Anna Makinda. The significance of this is three-fold… One: almost a third of the 339-seat House is from Opposition political parties. Two: a goodly proportion of the new MPs are youngish…


But, perhaps the most important aspect of the whole shebang is that, for the first time in the country’s 49-year Independence History, the Speaker is a woman. This has thrown a spanner in the gender-inequality works.
At long last, the Legislature – one of the three statutory Estates of the Realm… Or four, if you take into account the de facto the Independent Press Estate – is headed by a daughter of the soil.

For better or for worse, this – taken together with the fact that nearly a third of the august House is also ‘manned’ by Lady Members – is another major step in the way forward to entrenching gender equality in Tanzania.
Of course, the Lady Speaker didn’t fall like manna from Heaven. She was tactically maneouvred into the scoring position by her ‘Nambari Wan’ patron, the veteran ruling party CCM. The top party caucus axed ten of its members who’d come forward to contest the post, leaving three aspirants – all women, as it ‘conveniently’ happened!
The field included Samuel Sitta, the immediate past Speaker, and Andrew Chenge – a decoy if I ever saw one! But, that’s another story…

Considering that gender equality’s a fashionable clarion call, there was no better vehicle to convey one of the three into the Wool Sack (House-of-Lords pardon!). In the event, Ms Makinda easily won the post with 265 votes against 53 for his formal rival from the Opposition, Mabere Marando.
This wasn’t surprising – especially considering that her party already had 251 MPs as of November 12, compared with a combined total of 82 ‘Opposition’ MPs… as well as scores of fellow women MPs!

However, what’s surprising – if that’s the correct word – is that Marando could only muster 53 of the votes… One would’ve naturally expected him to garner all the ‘Opposition’ votes! What happened to the other 29?
Of course, the easy answer’s that ‘they virtually crossed the floor,’ going to their political rivals who were already heavily fortified, anyways! But, this wasn’t necessarily the case – or she’d have won by 280 votes (251-CCM-plus-29 Opposition ‘defectors’).
Equally interesting is that some CCM MPs may’ve also voted for the Opposition candidate – thereby reducing Makinda’s ideal total from 280 to 265.

That’s if only because among them must be ‘male chauvinist pigs’ (Angela Davis pardon); disappointed Sitta-supporters, Opposition Camp followers-at-heart…
(Would you believe it? Nine ballots were spoiled!)
Confused? Let’s leave that and move on! Ideally, such crucial voting shouldn’t be secret… MPs should’ve the courage of their convictions, stand up and be counted as supporting who – and may the best candidate win!
(Indeed, the best candidate, Samuel Sitta, was jettisoned via caucus fiat. In my view, Sitta did much to put Tanzania in the good books of the comity of nations than most any other person – bar Mwalimu Nyerere… But, again, that’s another story).

Finally, regardless of what the Constitution says in the rider to Article 68, the Speaker wasn’t elected by MPs in the real sense of the term.
One really doesn’t become an MP unless and until one formally takes and subscribes the Oath of Allegiance…


Only then can we nail them to the masts if, say, it is found that they had sold their vote for a mess of pottage!
Then there’s the small matter of the Public Leaders Ethics Code… Is the Speaker (Article 84(5) and her MPs (Article 70(1) able, willing and ready to publish formal statements regarding their property… Sorry. Cheers!
[ Israellyimo@yahoo.com

Ukishaisoma hiyo makala nataka uniambie unaonaje? Mie nampa shavu mzee kwa kujenga hoja.

Thursday, November 18, 2010

JK AFUNGUA BUNGE LA 10 - CHADEMA WAMSUSIA

Nimemtizama Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia Bunge mjini Dodoma. Lilikuwa ni tukio la aina yake kwani serikali ya CCM ilijitahidi kuonesha kuwa kwa sasa ni wazi kule Zanzibar CCM na CUF ni kitu kimoja. Maridhiano yamekuwa ni machungu kwa kambi ya upinzani kwani kwa sasa itapata wakati mgumu kwa idadi kinyume na watu walivyofikiri awali kuwa upinzani Bungeni ungekuwa umeimarika kumbe wapi.
Kuhudhuria kwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, kumeonesha wazi kuwa kwa sasa CUF kama mshirika mkuu wa CCM Zanzibar ni wazi kuwa serikali ya CCM imefanikiwa kuleta amani Zanzibar na hapo hapo kudumaza nguvu ya upinzani katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.

1. CHADEMA WAMSUSA RAISI
Baada ya Raisi kukaribishwa na Spika wakati akianza kumshukuru Spika, nilimwona mbunge wa Hai, na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akitizamana na mwenzake na mara moja wabunge wote wa Chadema ambao wanaunda Kambi ya Upinzani bungeni walisimama na kutoka nje huku wakizomewa na wenzao wa CCM kwa makofi ya kejeli. Rais alibakia akitabasamu; Rais wa Zanzibar alionesha uso wenye kutaharuki na kuwaza sana wakati huo. Nilitegemea rais Kikwete azungumzie hali iliyojitokeza lakini alijifanya hajali na akamaliza hotuba yake bila kusema lolote lakini hakuacha kupiga mkwara kuwa wapinzani watambue kuwa yeye ndiye Rais wao.

Hili la utambuzi nadhani Raisi bado hajalielewa; hapa kuna swala la kupinga utaratibu mzima wa uchaguzi wa Raisi na hasa muundo na utendaji wa Tume ya Uchaguzi kama kiini cha hali tata na kasoro ambazo hazielezeki kimantiki kwa mtu yeyote mwenye akili ya kufikiri kimakini. Tatizo ambalo limejitokeza nadhani ni “legitimacy” ya uraisi wa Kikwete. Ni kweli tayari ameapishwa lakini suala wabunge kumgomea si la mzaha ni suala lenye kuhitaji kujiuliza hivi tumefikaje katika hali hiyo?

2. UTAWALA BORA – UFA WA KIDINI
Raisi katika hotuba yake ya ufunguzi wa bunge la tisa miaka mitano iliyopita alidhamiria kuimarisha taasisi za kidemokrasia ili zifanye kazi kisasa. Hadi leo unapoona kuna mapungufu mengi sana katika suala zima la uchaguzi ni wazi raisi kashindwa kutimiza ahadi yake. Taasisi zote za kidemokrasia kuanzia msajili wa vyama hadi Takukuru, haziko huru na zinaendeshwa kama vile bado tuko katika nchi za kikomunisti. Huo kwa Rais Kikwete ndio usasa anaoutaka alafu anashangazwa na aibu hii ya wabunge kumsusa.

Nimefuatilia hotuba ya Rais Kikwete anasema eti nchi ina ufa wa kidini ambao unatishia mgawanyiko wa kitaifa. Kila hili linaposemwa na viongozi wetu tangu wakati wa Kampeni linanishangaza sana. Ikumbukwe kuwa uchaguzi wa mwaka huu umekuja kipindi ambacho demokrasia imekuwa hadi asasi na viongozi wa kidini tayari wameanza kushiriki katika kushawishi masuala ya kisiasa. Hali hii haikwepeki katika maendeleo ya kidemokrasia na kwa wahafidhina “conservatives”, kwao wanadhani viongozi wa dini wameamua kumpigia chapuo mgombea Fulani. Ni vyema Raisi pamoja na wanaomshauri wafuatilie maendeleo ya demokrasia kule Amerika ya Kusini ambapo pamewahi kuwa na udikteta sana hapo nyuma. Lakini tangu kuibuka kwa wimbi la “ Theolojia ya Ukombozi” viongozi wa dini waliamua kuungana na waumini wao kupigia chapua katika kutoa elimu ya uraia wakibainisha sifa za kiongozi bora. Matokeo yake walichaguliwa viongozi bora na leo uchumi wa nchi hizo umeimarika na utawala bora ndio usiseme.
Kipindi chote cha kampeni sikuwahi kusikia viongozi wa kidini wakiendesha kampeni au mahubiri dhidi ya mgombea Fulani kwa kuvutia watu wao wachague muumini wao. Ila viongozi wa dini wengi wa kikristo walikazia sana sifa za kiongozi bora ambazo kwa kiasi Fulani ziliwagusa wagombea Fulani bila kujali dini zao. Huu ndio ulikuwa msisitizo na ni wazi kwa mtanzania yeyote mwenye akili timamu atakubaliana na mimi kuwa, katika sifa za kiongozi bora ambazo ziliainishwa na viongozi wa dini hasahasa zilikuwa zikitaja kiongozi atakayechaguliwa awe na sifa ambazo zitasaidia Taifa kuepukana na changamoto ambazo serikali ya Kikwete iliyopita ilikuwa imeshindwa kuzishughulikia.

Ni wazi viongozi wengi wa dini walionesha kuwa hawakuwa wanaridhishwa na utendaji kazi wa serikali ya awamu iliyopita. Bahati mbaya sana viongozi wengi wa aina hiyo walikuwa wa dini za kikristo. Hali hii ya kuelezwa hisia za ukweli ndizo zinamfanya Raisi Kikwete na wapambe wake kutafsiri hali ile kama vile kuna ufa wa kidini. Ninaamini kwa viongozi wengi wa kidini wa kikristo ambao naamini wamekwenda shule vizuri, hata kama leo hii Tanzania ingekuwa chini ya raisi mkristu, na uongozi kuwa wenye mapungufu kama ya awamu iliyopita bado wangepiga kampeni katika mwelekeo ambao ulijitokeza. Siamini kabisa kuwa kuna ufa wa kidini Tanzania wala hakuna chuki dhidi ya kiongozi wa Taifa ambaye ni muislamu bali tatizo ni aina ya uongozi uliokuwepo.

4. AHADI
Kama kawaida yake Raisi Kikwete ametoa ahadi lukuki kupitia mpango wa Maendeleo 2025. Kazungumza mengi matamu masikioni juu ya ndoto yake kichwani juu ya Taifa hili. Kwa mazoea na rais Kikwete sidhani kama ni kweli ana dhamira ya dhati kwani ili tuifikie ndoto hiyo, ni wazi inambidi abadili staili yake ya utawala.

Huku tukisubiri Baraza la Mawaziri kutangazwa, ni wazi tayari serikali atakayoiunda imeshaonesha kuwa haina dhamira ya kupambana na ufisadi kwani uchaguzi wa Spika mpya wa Bunge kwa kumuengua Spika aliyekuwepo umeonesha kuwa Bunge limetekwa nyara na Chama tawala. Serikali yake inataka Spika ambaye ataminya haki ya Wabunge kuhoji serikali katika baadhi ya mambo ambayo yana maslahi ya Chama. Bunge kwa kutumia kisingizio cha “ni wakati wa mwanamke kuongoza mhimili mmoja wa dola” limeonesha wazi halitaki Spika ambaye ataruhusu kila jambo lenye maslahi ya umma kujadiliwa kwa undani. Majadiliano ya aina hii tayari yamewaumbua baadhi ya vigogo wenye fedha ndani ya chama katika Bunge lililopita. Hali hii inaonekana imeleta migawanyiko na hivyo ni afadhali wezi wa mali za umma wasizungumzwe kwani Chama kitachafuka.

5. SERIKALI NA WOGA ISIOUJUA “PARANOIA”
Maadam serikali itakayoundwa itaendeshwa kwa kuhakikisha mambo yote ya kifisadi yanafichwa basi ile “moral authority” mamlaka ya kimaadili ya Raisi Kikwete kuahidi kkuwa atapambana na ufisadi inakuwa haina mashiko kabisa. Nchi imefika hatua inaendeshwa kwa staili ya “Kleptocracy” badala ya “Democracy” alafu watu wanafanya mzaha kwa kusingizia kuna ufa wa kidini au waziri Mkuu Pinda anaonya kuwa kuna Chama Fulani kinatishia amani na umoja wa kitaifa. Hivi hata Pinda haoni ilivvyo vigumu kutumika katika serikali ambayo maslahi ya umma yanashika nafasi ya tatu? Ya kwanza ikiwa ni maslahi ya makundi Fulani ya wakwasi, la pili ni chama na mwisho wananchi. Maadam viongozi wengi wameamua kuchagua “unafiki” kutumika, basi sitashangaa hata yule Spika aliyechinjiwa baharini atapewa zawadi ya uwaziri na atakubali kutumika kwa kufuata misingi ambayo haiamini bali ili mradi mkono unaenda kinywani. Aina hii ya viongozi ndio ambao wamelifikisha Taifa hili kwa sasa halina viwango katika kila kitu ni usanii tu “mediocrity”.

Ukitizama elimu inazalisha wahitimu mediocrity kuanzia ngazi zote hadi vyuo vikuu. Asilimia kubwa ya watanzania hawana uwezo wa kufikiri kwa kina katika mambo mbalimbali. Tumefika mahali sasa Bunge linakuwa na wawakilishi karibu mia mbili wa viti maalum ambao hawana tija kwa Taifa zaidi ya kula fedha za bure tu. Yako mengi nikiyatizama naogopa hivi watoto wangu wataishi Tanzania ya aina gani? Waama! Mungu aepushe mbali, kwa kweli sioni kama tunaelekea kuzuri huko mbele kama Raisi Kikwete asipobadilisha namna ya kuongoza Taifa hili.

HAYA NI MAFANIKIO
Hotuba ya Raisi imedhihirisha mafanikio katika ukusanyaji kodi kumeongezeka, utegemezi wa wafadhili kumeshuka hadi 28% kutoka 42% nadhani. Si haba hapa serikali imejitahidi. Lakini napo pananishangaza sana; hebu fikiria mbona hali za maisha ya watu wa chini ziko hoi bado? Ile “trickle down effect” mbona haipo? Hapa sitasita kusema ufisadi, anasa na matumizi holela ni tatizo ambalo linaondoa ile umaana wa makusanyo lukuki.

Si hilo la makusanyo tu, bali kkuna hili la “mfumuko wa bei umeshuka”, Raisi Kikwete katoa sababu nyingi sana kuhusu misukosuko ya kiuchumi iliyoikumba nchi yetu. Juhudi zilifanyika na tukamudu lakini pia amesema eti mauzo ya nje yameongezeka sana hasa kupitia sekta ya madini. Mimi mwenyewe wakati namsikiliza nilipitia bei ya dhahabu nikaona imeongezeka zaidi sokoni lakini nikashangaa kama wazalishaji mbona bado mfumuko wa bei ni tatizo kwetu ilihali “export” ni kubwa? Kuna nini hapa? Hayo madola ya madini yanaingia serikalini au yapo mifukoni mwa mafisadi? Anajua mwenyewe, lakini sikuona mantiki katika kutetea mfumuko wa bei.

Raisi anadai eti kwa sasa Tanzania inauza zaidi bidhaa nchini Kenya kuliko Kenya inavyouza Tanzania. Imenishawishi nifuatilie mauzo ya Kenya na Tanzania nione inawezekanaje hili litokee kwa nchi ambayo bado tunaona karibu kila kitu kina chapa ya Kenya madukani? Viwanda vyetu bado vimelala, kilimo chetu anajua mungu, utendaji kazi wetu ndio huo ambapo watanzania wengi starehe ndio jambo la mbele zaidi.

6. MICHEZO
Mwisho, Raisi kagusia kuhusu michezo. Hapa alinikuna kiasi Fulani kwa kueleza jinsi ambavyo zamani wakati akiwa shuleni alivyokuwa akifundishwa michezo na mwalimu wa michezo. Ana mawazo mazuri kuhusu kuimarishwa kwa sekta ya michezo hapa nchini na anajua ni nini chanzo cha kudorora kwa michezo. Ila kuna kitu ambacho bado kama watanzania hatujakitilia maanani kama kweli tunataka maandalizi ya michezo na hata sanaa kwa ujumla.

Hapo awali nimeeleza masikitiko yangu juu ya hali mbaya Taifa lilipofikia na nikasema kuwa kwa sasa kwenye elimu hatujali viwango “quality” sisi tumebakia bora liende. “mediocrity”. Michezo na utamaduni ni kielelezo cha jambo hili pia. Ningedhani Raisi Kikwete angepaswa kuelewa kuwa sekta ya michezo imekuwa ni aibu ya Taifa kwa sasa. Michezo haizingatii elimu; na ningedhani kuna haja ya fani ya michezo katika vyuo vikuu na vile vya ualiimu ianzishwe kwa kasi ya hali ya juu. Ukitizama wawakilishi wetu kwenye michezo kama “Olimpiki, Jumuiya ya Madola na hata Soka” pamoja na kuwa na makocha ambao serikali inawalipa bado ni vituko tu. Mediocrity, hali inayosababishwa na wanamichezo wasio na uelewa wa michezo kama fani ya kielimu. Michezo imebakia kkuchezwa na wengi wa vijana walioshindwa kusoma kabisa, wahuni, wavuta bangi, watukutu na watu mbalimbali ambao ni “ant – social katika jamii.

Matokeo yake kuanzia viongozi hadi wachezaji wote hawana maono “vision” wala mtizamo wa mbali ukiacha fedha kama posho za kusafiri tu. Bahati mbaya sana kwa kuzingatia hii hali ya “mediocrity” katika fani mbalimbali hapa nchini, hata wataalamu lukuki pale wizara husika na michezo wamebakia wasindikizaji wa wanamichezo katika matamasha makubwa ya kimataifa ya michezo. Hawana jipya katika kubuni mbinu za kuendeleza michezo nchini. Raisi Kikwete anapaswa aone uendelezaji michezo katika jicho la mtizamo ninaoujadili. Kuna haja ya michezo kuanzia mashuleni na shule ndio ziwe kisima cha kuandaa vijana katika michezo mbalimbali.

Hata kwenye sanaa za maonesho, Raisi amedai kuna mafanikio. Lakini mimi nadhani yapo ya kuboresha zaidi. Ingawa mimi si mtizamaji sana wa filamu za kibongo, lakini nadiriki kusema inanishangaza kila nikitizama filamu, mada ni mapenzi tu. Mtu atasema eti ndio inayouza. Naamini kuna haja ya kuhimiza mada zingine kwenye mambo kama ufisadi, kilimo, siasa na mambo yote yanayoikumba jamii.

HITIMISHO
Taifa limepoteza tunu ya utendaji kazi wa kizalendo na uwajibikaji. Mambo yanafanywa kiujanjaujanja sana. Katika kila fani wataalam kuanzia kilimo hadi michezo wao ni kufukuzia mapato ambayo hawajayafanyia kazi. Utashangaa utawaona wataalamu wa elimu, kilimo hadi michezo wakinawiri kimaisha lakini mambo wanayoyasimamia yako hoi bin taabani. Ripoti zao ziko safi sana ila kimatendo ni bure sana.

Raisi Kikwete hajui kuwa Taifa kwa sasa ni mediocrity kila pahala. Uelewa wa mambo na kuzingatia kanuni za utendaji kazi kwa tija ya maslahi ya umma unapotea. Mfumo wa siasa na utawala una matatizo, watanzania wengi ni wagonjwa kisaikolojia. Their psyche is in disarray. Sina hakika kama hujachelewa; lakini naamini sasa tumefika point of no return. Kama Raisi wetu mpendwa hutabadilika kwa kuanza kuwawajibisha na hata kukaa mbali na mafisadi, hakika kiama cha nchi yetu kitaanza sasa. Na ndipo hapo tutajua legacy ya Kikwete. Nabakia nikisubiri Baraza la mawaziri na nitaweka waraka mwingine.

Saturday, November 13, 2010

MWELEKEO WA SIASA ZA TANZANIA BAADA YA UCHAGUZI MKUU 2010

Ukizitizama siasa za kiafrika, UKABILA, haukwepeki. Tangu juzi nimetizama wabunge wakiapishwa huku wakiwa wamesindikizwa na ndugu na hata vikundi vya kikabila utadhani mwisho wa siku matokeo ya utendaji wao yatawafikia wanakabila wenzao. Yuko bwana mmoja amejadili jinsi siasa zetu zilivyojaa ukabila.
Huku tukiwa tumemaliza uchaguzi, ni wazi kuwa CCM imethibitisha kuwa ni chama ambacho ni nguva wa kisiasa. Pamoja na kutotegemea tena hekima za Nyerere lakini bado CCM inapeta.
Kudhihirisha kuwa CCM itaendelea kutawala kwa miongo kadhaa, hebu ona jinsi ambavyo itakavyoweza kutawala siasa za Tanzania hadi 2030.

Saturday, November 06, 2010

JAKAYA KIKWETE AAPISHWA

Nilichokiona leo uwanja wa Uhuru ni maombi ambayo yalikuwa yanaashiria mawazo na mitizamo ya viongozi wa dini.
Kwa mfano huyu shehe wa waislamu, yeye alikazia kwa ufupi sana juu ya:

Ee Mola wetu, tunaomba wakinge viongozi wetu na fitna ya uongozi

Uiepushe na siasa za kidini *3

2.Mtu wa pili alikuwa Askofu Valentino Mokiwa akiwakilisha Umoja wa Makanisa Tanzania. Yeye alisisitiza katika sala yake yafuatayo:

Eti Raisi JK apewe na kujaliwa Nguvu katika kuongoza na hekima kutawala
Eti Mungu atuepushe na Tofauti za kisiasa na za itikadi, kidini,
Mungu aepushe dhidi ya Machafuko, pia Mungu ampe JK nguvu za akili, roho, mwili, hekima, busara, na uwezo wa kutafakari mbele.

3. Maombi ya tatu yalitoka kwa kanisa mama: Baraza la maaskofu Tanzania , Askofu Michael

Akiwa na karatasi alisoma sala yake kama ifuatavyo:
Aliamua kuitumia sala ya Nabii Suleiman akimuomba Mungu amtie JK yafuatayo:
Moyo wa hekima na akili, uwajibikaji, baraza la mawaziri, bunge na mahakama na vyombo vya ulinzi waweze kuongoza kuleta heri ya milele mbinguni.

4. Baadaye ikafuata hotuba ya shukrani ya JK na hakusema mengi kwani ameahidi atasema sana siku ya uzinduzi wa Bunge.rais amesema tutembee kwa kifua mbele kwani bado watanzania wengi wanakipenda chama cha mapinduzi.Amewashukuru watu wawili: Dr. Gharib Billali na Mke wake mpendwa Salma Kikwete kkusaida kutafuta ushindi CCM.
Mama Ngangari kutafuta ushindi, lakini pia amewashukuru wagombea wenzake waliowania uongozi na akakiri changamoto zao na ni lazima CCM igangamale kwani huko mbele kutakuwa kugumu.

5. Ameahidi kutibu majeraha ya kampeni ambayo yamegawa watu na jamii za nchi yetu kidini, rangi, jinsia na umaeneo. Amewaomba vyama vya upinzani visaidiane naye kudumisha amani na kuondoa nchi kugawanyika. Hapa atawategemea viongozi wa dini na wanahabari wasaidie kuifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani.

6. Jk hakuisahau Tume ya Uchaguzi kwa kazi bora iliyofanya. Ila kazi kubwa iliyo mbele yetu ni kufanya tathmini kujua ni yapi yaimarishwe kuleta chaguzi zijazo zenye ufanisi zaidi.

7. Watu wa ulinzi na usalama nao hawakubaki nyuma kushukuriwa na amewaomba waendelee kusimamia utulivu na pia kwa gwaride zuri ambalo walilifanya mbele ya umati wake.

8. Pia ameshukuru UNDP kwa msaada wao katika kufanikisha uchaguzi, Katibu Mkuu kiongozi kwa kuandaa sherehe na pia viongozi wa dini kwa dua zao.

Monday, November 01, 2010

UCHAGUZI MKUU KWISHA KWA HASIRA ZA BAADHI YA WANANCHI WA MIJINI

Uchaguzi mkuu ndio leo na ninaamini watanzania watapiga kura kumchagua kiongozi wanayemhitaji katika wakati tulionao kama Taifa. Ni wazi kama kuna haja ya mabadiliko basi wapiga kura hawatasita kutumia wasaa mfupi katika chumba cha kkupigia kura na kuhakikiksha kuwa ile karatasi ya kupigia kura haitumiki vibaya. Binafsi sipigi kura leo kwa sababu za msingi kabisa kwangu ingawa ni wazi ninapoteza haki yangu ya kiraia. Nitaeleza baadaye kwanini sipigi kura.

Katika uchaguzi huu watanzania watahitaji kupiga picha ya miaka mitano iliyopita na wajionee wenyewe kama kweli Taifa la Tanzania linahitaji mtu mbadala na vilevile chama mbadala. Ni kipindi kigumu kuamua kwani si rahisi kwa watanzania wengi kuamua kutaka mabadiliko na wala si rahisi pia kwa watanzania wengi kuchukua uamuzi kuendelea na aina ya uongozi ambao umemaliza muda wake. Nitajadili mambo haya mawili kuona ni kwanini wapiga kura leo wako njia panda?

Moja, wapiga kura wengi leo hii watapenda kuendelea na chama pamoja na viongozi wa chama kilekile ambacho wamekizoea kwa miaka nenda rudi. Ni chama ambacho kwao kimekuwa ndio kinachohakikisha uwepo na upatikanaji wa mahitaji yao. Nitatoa mifano kadhaa kuonesha uzuri wa chama hiki kikongwe: Hebu fikiria mfanyakazi wa serikali, mtumishi wa umma ambaye anafika kazini muda anaotaka kama vile yeye ndiye mwenye mali. Haulizwi kwanini amechelewa na mara nyingine hata asipofika kazini haulizwi.

Mwingine anafika kazini lakini hafanyi kazi yeyote na mwisho wa mwezi analipwa mshahara na pia anapandishwa cheo. Si hili tu, pia hebu fikiria wako watanzania kibao ambao kitaaluma ni sawa na bure kabisa, mbumbumbu kabisa, yaani hata kuandika vizuri hawawezi kabisa, mtu hajui hata kuandika barua au taarifa yoyote ikaeleweka na kupeleka ujumbe. Aliajiriwaje? Ni mfumo wa chama na serikali iliyopo. Pakitokea mabadiliko mtu huyu atakuwa hatarini sana.

Si hayo ya wafanyakazi wengi wa kada za chini. Nenda kada za juu. Hapo napo ni kasheshe tu. Wako wengi wamegawiwa vyeo na nafasi walizonazo katika ngazi mbalimbali. Kwao urafiki na uswahiba wao kwa wenye chama ndio njia pekee ya kufaidika na nafasi na vyeo katika taasisi mbalimbali. Hawa ni wengi sana na sidhani kama watakubali kupiga kura kukiondoa chama cha ccm madarakani. Hawa wote, ni kutetea maslahi yao kibinafsi zaidi pamoja na tabaka tawala na kuendeleza hali iliyopo “status quo”.

Kwa upande mwingine kuna watanzania wengine ambao kwao kura yao itataka mabadiliko. Kwao kuendelea na utawala uliopo si hatua muafaka. Kwao wanataka Tanzania mpya wakiamini yako mambo mengi ambayo yanapaswa kubadilika. Kwa mfano, habari ya ufisadi iliyokithiri hapa nchini kwa takriban katika serikali inayomaliza muda wake ni hadithi ambayo kwao ni chungu ambayo haivumiliki. Kwa mfano, wizi wa fedha za EPA, Kashfa za Meremeta, Richmond, na nyingine nyingi hazina majibu.

Kwa wapenda mabadiliko wanashangaa jinsi ambavyo chama kilichopo madarakani kilivyoshindwa kutoa majibu ya msingi juu ya hatua madhubuti kuondoa ufisadi nchini. Wanakasirishwa zaidi na hatua ya chama kuwapiga marufuku wagombea wake wote kushiriki midahalo ambayo ingeruhusu wahojiwe na watoe maelezo kwa wananchi juu ya mapungufu yanayoonekana katika utendaji wao kwa miaka mitano iliyopita.

Wanaopenda mabadiliko wanashangazwa na jeuri iliyooneshwa na chama kilichopo madarakani wakati wa kampeni. Hii ni jeuri ya fedha katika matumizi ya vifaa vya kampeni wakati wananchi wengi wakipata shida juu ya huduma mbovu na kupanda sana kwa gharama za maisha kunakosababishwa na kushuka kwa thamani ya shilingi. Wanapotaka majibu hawapewi na wanapoleta majukwaa kama vile midahalo pia wenye nchi hawako tayari kutoa ushirikiano. Hali hii ni wazi kuwa watawala hawataki kuwa “accountable” na kwa wapenda mabadiliko hili si jambo la enzi hizi.

Kwa ufupi makundi haya mawili ya wapiga kura: Lile la kuendeleza hali iliyokuwepo “statua quo”, na lingine la mabadiliko yaani kuhimiza “accountability” ndiyo yanayoshindana leo. Litakaloshinda litakuwa na wajibu wa kuhakikisha jamii ya watanzania inaendeshwa kwa kufuata matakwa yake. Nitaendelea kumsubiri mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi amtangaze mshindi na ndipo tutajua hatima ya nchi yetu. Hapo tutajua tutajua nchi itaenda kwa staili ipi kati ya kifisadi fisadi ama ile ambayo tunaahidiwa tu lakini hatuna hakika kwa dhati kama kweli itatimizwa ama inatekelezeka.

Mwisho niseme tu kwanini sijapiga kura leo: kwanza kabisa sijawahi kujiandikisha kwa makusudi kabisa kwa kuzingatia kuwa siamini kuwa kwa muundo wa Tume ya uchaguzi tuliyonayo haiwezi kuwa huru katika utendaji wake wa kusimamia zoezi la uchaguzi. Mpaka hapo Tume huru kwa kuzingatia matakwa ya demokrasia itakapokuwa imeundwa ndipo nitakaposhawishika kupiga kura.

Sunday, September 19, 2010

KAMPENI ZA UCHAGUZI TANZANIA

Nilikuwa kimya sana kwa muda mrefu, sasa nitajaribu kuwalisha watu juu ya yanayojiri juu ya Kampeni za uchaguzi mwaka huu 2010. Tayari Moshi tumeshuhudia bonge la kampeni la kitajiri na vimbwanga vya kila aina vya mgombea uraisi ambaye pia ni raisi wa Jamhuri ya Muungano JK. Hiyo ilikuwa ni wiki hii. Sidhani kama kutakuwa bonge lingine la mkutano kama ule kwa habari nilizozipata.
Wacha hayo, sasa hivi stori kuu ambayo ni ya msingi ni hii kuendelea kukamatwa pembe za ndovu kule Hong Kong kutokea Tanzania. Jamani, mimi nataka niulize, hivi, si ndio sisi tulikuwa tunataka turuhusiwe kuziuza pembe tukawekewa uzibe na majirani zetu majuzi tu, sasa kwa jeuri tumeamua tunaziuza kinyemela au ndio nisemeje?

Pili, kuna hili la Mke wa Raisi jamaa hawataki ampigie mumewe kampeni, mimi naona kama vile kuna ka wivu hivi, hivi ina maana mke wa raisi kutumia mali za serikali dhambi? kwani si ndio mama namba moja eti? Sasa kama yeye ndiye namba moja kwanini makelele wajameji? Hebu someni wake wengine wa maraisi wanavyofanyaga alafu tujiulize hivi kwani mama yetu ana shida gani, si tumuache atumbue kanchi haka masikini?

Wadau nawasikilizia kwa haya mawili.

Monday, August 02, 2010

DEMOCRASIA NI MBAYA AU NZURI?

Tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi, jiulize swali hili: Je tunahitaji democrasia au la?

Tuesday, June 08, 2010

KWAHERI MAXIMO

MAXIMO NA WABRAZIL NA KIELELEZO CHA UCHANGA WA SOKA LA BONGO

Nimeitizama mechi ya Taifa Stars dhidi ya Brazil iliyochezwa tarehe 7/06/2010 siku ya jumatatu na ikanifurahisha sana. Furaha yangu si kufungwa bao 5 – 1 kwani tangu awali nilitarajia tungefungwa 3 – 0 lakini matarajio yangu hayakuwa hivyo. Ilikuwa ni mechi ya mwisho kwa Marcio Maximo na zawadi nzuri ya kocha huyo kuonesha kielelezo cha kazi aliyoifanya takriban kwa miaka isiyopungua mitatu na ushehe.

Marcio Maximo alianza kazi yake kwa kupokea timu ambayo ilikuwa haina misingi yeyote ya soka la kisasa. Ni timu iliyokuwa inaendeshwa kienyeji sana, timu ambayo nina hakika ilikuwa haina tofauti na timu za vijijini hapa Tanzania. Kimsingi timu hii kwa kipindi chote cha Maximo imekuwa katika kujengwa ingawa wadau wengi wa soka wamekuwa wakimlaumu kocha huyo mbrazili kuwa hana mafanikio yeyote. Kimsingi hawajui kuwa kujenga timu yenye wachezaji wa kiwango cha chini kama ya kwetu inahitaji kizazi “generation” kuandaliwa tangu utotoni katika timu za makundi tofauti ya umri ili kufikia timu kamili ya kisasa.

Wadau wengi walisahau kuwa Maximo amekuta timu ya kuokoteza mitaani ya wachezaji wasiojua kuwa kwenye mpira kuna nidhamu ya mpira ili uweze kufanikiwa. Wadau wetu wa soka hawakuzingatia mambo mengi ya msingi ambayo Maximo kailetea nchi yetu lakini ukweli utabakia pale pale kuwa huyu bwana kwa kiasi kikubwa kawafumbua macho watanzani na TFF juu ya jinsi ya kuendesha timu ya soka kisasa. Lililobakia ni kazi hiyo kuendelezwa na mrithi wake kutoka Dernmak ambaye ametangazwa hapo jana.

Kilichoonekana katika kipigo cha jana ni kielelezo tosha kuwa wachezaji wetu bado sana. Ni wachezaji ambao kimpira bado wako chini sana, uwezo wao kiufundi ni mdogo sana. Ni wachezaji ambao naweza kusema kuwa hawafundishiki kirahisi na wala hawajifunzi. Inashangaza kuwa pamoja na kuwa na kocha wa hadhi ya Maximo, bado wachezaji hawa wanapata fursa nyingi za kutizama mechi kupitia runinga lakini sidhani kama wanajifunza kitu. Ndio maana nasema Tanzania inahitaji kizazi kipya cha soka kiandaliwe ili kuweza kufikia angalau mafanikio ya timu kama Ivory Coast.

Kama watanzania tutaendelea kutaka kushawishi na kuwapangia makocha wachezaji wa kuita kambini kamwe hatutafika popote. Umefika wakati tuheshimu kazi kitaalamu badala tu ya kufuata hisia zetu mioyoni mwetu. Kama tutafanya hivyo ni lazima tu soka letu litapiga hatua.

Jambo pekee ambalo ningetaka kumshauri kocha mpya ni kuwa kuna haja ya kuibua vipaji vya soka kutoka mikoani. Ninaamini kuna vipaji vya soka vimejificha mikoani na haviibuliwi kwani soka letu limebakia ni la Dar es salaam tu. Makocha wa mikoani wanatakiwa kuwatambulisha vipaji vilivyopo huko mikoani.

Mwisho, naamini soka ya Tanzania inaelekea kuzuri, nimshukuru Maximo kwa kututoa tongotongo.

Tuesday, May 04, 2010

DU! RAIS JK AMEKASIRIKA KWA HOJA NYEPESI

Hatimaye Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliamua kuhutubia Taifa mwisho wa mwezi wa Aprili kwa kutumia mtindo tofauti na mazoea. Hapa alibadili hadhira, badala ya kuhutubia Taifa, Raisi Jakaya Kikwete aliamua kuwahutubia wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam. Wengi wao walionekana ni wanachama wa CCM kwa mavazi yao hali ambayo sidhani kama iliwakilisha taswira ya utaifa kwa mtu yeyote makini.

Raisi wa nchi anapoamua kubadili hadhira, ni wazi anazo sababu za msingi na ndio hapa binafsi nadhani ukakazi unakoanzia kwa kuzingatia yote aliyoyasema katika hotuba ile huku akishangiliwa kwa kelele na makofi lukuki. Ushangiliaji huu wa kishabiki hata katika mambo ya msingi kabisa unatia shaka dhamira ya dhati ya raisi pamoja na watu wake wa karibu kwa ustawi wa Taifa letu. Ninasema hivi kwa maono yangu kwani kuna kila sababu ya kufikiri kwa kina ambayo imenifanya niione hotuba ile kama lengo lake kuu ilikuwa ni kuwajibu TUKTA dhidi ya azma yao ya kuwahamasisha wafanyakazi kugoma.

Moja ya wasiwasi wangu kuhusu dhamira ya kiongozi wetu mkuu ni ile hali iliyojitokeza kwa yeye kutumia muda mrefu kuponda na kukebehi madai ya TUKTA kutaka kima cha chini kiwe ni shilingi laki tatu. Binafsi kwa serikali yetu ninayoifahamu ni kweli haiwezi kulipa kiwango hicho kamwe lakini naamini inaweze kulipa kiwango cha juu zaidi ingawa chini ya hapo kama kima cha chini. Raisi hawatendei haki TUKTA kwa kuwaponda ilihali wamejaribu kumuamsha kutoka lindi la udhaifu wa serikali yake katika kukusanya kodi. Naamini kama kweli nchi hii kodi itakusanywa kwa dhati ni wazi serikali yetu ina uwezo wa kulipa wafanyakazi wake kwa mujibu madai ya TUKTA.

Serikali yetu haikusanyi kodi kuendana na rasilimali na biashara zilizopo; serikali yetu inasamehe sana kodi, mtu makini arejee taarifa ya CAG iliyotolewa hivi majuzi, angalia misamaha ya kodi inavyoathiri mapato ya serikali yetu. Raisi anapotuambia kuwa mapato ya serikali ni madogo sana nashindwa kumuelewa kabisa. Angalia viongozi wa ngazi za juu wanavyoikwangua hazina ya nchi yetu kupitia wabunge, mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa na wilaya kwa malipo lukuki ya posho mbalimbali ambazo hazilipwi kodi lakini mfanyakazi wan chi hii anakatwa kodi katika kila apatacho. Hapa nadhani Raisi wa Jamhuri angekuwa anapaona na ana dhamira ya dhati ya kupagusa ili kuleta haki na usawa wa kugawana keki ya Taifa basi asingelithubutu kung’aka kama alivyokuwa katika hotuba yake.

Raisi ameonesha kung’ang’ania sana mambo madogo katika kutia nguvu hoja yake na akaacha mambo makubwa ambayo ndiyo msingi wa wafanyakazi wa nchi hii kudai haki yao. Kwa mfano, sidhani kama ni sahihi sana kwa raisi kuongelea kuwa TUKTA inadai kima cha chini cha laki tatu kwa wafanyakazi wa majumbani (house girls) au kwenye mabaa (bar maids). Hivi kwa kazi wafanyakazi hawa wazifanyazo, ina maana hawastahili kulipwa malipo stahili kuliko wanayolipwa sasa? Sioni mantiki kama mtu ni tajiri, anakwenda kijijini anamchukua mtoto wa masikini ambaye ameshindwa kupelekwa shule alafu anakuja kumfanyisha kazi kwa kipato ambacho si haki kibinadamu. Hapa raisi ameonekana kuwatetea sana matajiri; kwake wenye viwanda kwa mfano alionekana kusisitiza kiwanda cha Maji, hapa nachukulia mtu kama Mengi, eti ukimlazimisha alipe kima cha chini cha juu hatapata faida. Inatia shaka inawezekana raisi ana ubia na watengeneza maji mpaka anajua faida yao, kwani mie naamini biashara ya Maji kwa sasa ina faida kubwa sana.

Raisi ameonekana kutowajali wafanyakazi wa Tanzania kabisa kwa kuwatisha eti kama mtu hataki kazi aache kuna wengine watajiunga. Hapa imeonesha jinsi gani raisi kama mwajiri mkuu asivyojua kabisa misingi ya utawala wa wafanyakazi. Ukiwa kama meneja mkuu, Raisi hapaswi kutumia kauli kama ile kwani moja kwa moja raisi analazimisha kuwa na wafanyakazi wa umma wanaofanya kazi bila msukumo chanya, waliokatishwa tamaa, wanafanya kazi bora liende. Ni katika mfumo huo, sitegemei maendeleo ya kweli kufikiwa katika kipindi tunaongozwa na sera za vitisho na kutojali. Ina maana raisi wetu haelewi madhara ya kisaikolojia watakayoyapata wafanyakazi ambao kwa ukweli wanafanya kazi kwa vipato vidogo sana lakini wanaona serikali yao ikisema haina fedha huku ikiruhusu mabilioni ya fedha kuliwa na vijikundi vidogovidogo vya mafisadi kupitia kashfa kama “Richmond, Meremeta, IPTL, mikataba ya Rites na vijimambo vingi ambavyo kamwe watanzania wamebaki gizani huku fedha zikipotea alafu watu wanaambiwa hatuna uwezo wa kulipa mnachotaka.

Raisi alizungumza jambo zuri sana kuwa kama serikali italipa kwa mujibu wa madai ya TUKTA, basi ina maana wafanyakazi 355,000 wa serikali watakuwa wanawanyonya wananchi wapatao milioni 39. Raisi anafikiri ukilipa wafanyakazi hao aliowataja basi inaishia hapo, kiuchumi hapa kuna “domino effect”, naamini kwa idadi ya wafanyakazi wa serikali wanategemewa sana na watu wengi. Malipo yao yanakwenda mpaka kwa watoto, wajukuu na hata wazee wa wafanyakazi hawa. Hapa naona raisi alighafilika kidogo lakini hapaswi kubeza idadi ya wafanyakazi eti ni ndogo. Kama kweli ana dhamira ya kuondoa unyonyaji basi asitumie wafanyakazi wa serikali bali atumie kundi dogo tu ambalo ndilo msingi wa unyonyaji hapa nchini. Nitaeleza:

Kundi hili ambalo naamini linatumia fedha nyingi sana ambayo kama ikidhibitiwa kwa utaratibu mzuri unaojali haki sawa katika jamii ya kitanzania ni kundi la wateule wachache wa nyadhifa mbalimbali za kitaifa pamoja na wawakilishi wa wananchi. Hapa naongelea wabunge takriban mia tatu na ushehe, nina hakika hawa ni mzigo kwa Taifa letu. Wengi wao hawana chochote wanachochangia bungeni ni kupiga usingizi, ama kukaa kimya na kila siku kujichukuliwa posho ambazo nadhani hazikatwi kodi. Nina wasiwasi hata kama mbunge hajahudhuria kikao bado analipwa. Siamini katika kipindi tunaelekea katika uchaguzi ni vyema wabunge wanaomaliza muda wao wakalipwa mafedha lukuki ya Mfuko wa Jimbo (CDF) kama si matumizi mabaya? Busara ingekuwa kuwasubiri wachaguliwa wapya, je kwa nini tusiamini kuwa hii itakuwa fedha ya uchaguzi? Bado tena mbunge huyuhuyu atalipwa mafao yake ya miaka mitano, mamilioni ya shilingi ambayo yanazidi kabisa mafao ya mfanyakazi wa serikali aliyeitumikia nchi hii kwa miaka zaidi ya thelathini. Hivi Mheshimiwa Raisi anajua vipaumbele vyetu halisi ni vipi?

Orodha ya wanyonyaji ni ndefu ikijumuisha waheshimiwa mbalimbali wa ngazi za kitaifa, wizara, mikoa hadi wilayani. Mtindo ni mmoja tu, kazi kidogo mapato ni makubwa tena bila kodi. Kama kweli Raisi angelikuwa ni muungwana basi angelijadili hili tuone mtizamo wake badala ya kutuletea mambo madogo kama ya “mahouse girls na mabar maids”. Nasema hivi nikitambua kuwa kama hili tabaka la viongozi ambalo ni mzigo kwa hazina yetu “parasitic class” kama litaangaliwa na serikali basi angalau itasaidia kuwezesha serikali kuwalipa wafanyakazi wake mshahara wenye heshima na utu. Hapa lazima niseme wazi kuwa sidhani kama mshahara wa laki tatu na kumi na tano ndio ulipwe kwani hata mie nadhani kwa maisha ya Kitanzania hii inaweza chochea mfumoko wa bei kama wa Zimbabwe. Naamimi panahitajika kiasi zaidi ya kinacholipwa kwa sasa.

Hapa lazima nimkumbushe Raisi kuwa alijisahau na hili angelizungumzia basi wafanyakazi wangeliridhika. Hakuwa na haja ya vitisho kwani mwisho wake Raisi anakuwa ndio chanzo cha tabaka la wafanyakazi wa umma ambao hawana tija kwani wanafanya bila kupenda wakifanyacho. Kwa maana nyingine, Raisi kupitia hotuba yake amedhoofisha ari ya wafanyakazi wake.

Nilipokuwa ninamsikiliza mheshimiwa Raisi JK, nilijikuta nikitafuta nakala ya magazeti ya nyuma ambayo iligusa ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) ya mwaka 2009 nakwambia nilijiuliza hivi raisi anapoongea na wananchi kweli anakuwa anatafakari mapungufu ya serikali yake katika kuhakikisha fedha za serikali zinatunzwa na kutumiwa vizuri ambapo kwa kiasi fulani ingesaidia kuboresha maslahi ya wafanyakazi? Kwa mfano ripoti hiyo inaonesha kuwa kwa mwaka 2009, serikali kupitia TRA ilitoa misamaha ya kodi shilingi 752.4 bilioni. Hii ni sawa na asilimia 18% ya mapato ya serikali yalisamehewa. Hapo hapo taarifa inaonesha kuwa TRA ilishindwa kukusanya kodi kwa kutimiza lengo kwa shilingi bilioni 426.4. Hapa ni wazi uwezo wa kukusanya kodi una walakini na ukiongeza na misamaha kuna kama takriban shilingi Bilioni moja inaachwa tu kupotea. Kwa ufupi taarifa hiyo naweza nikainyumbulisha kama ifuatavyo:

i) Matumizi ya hovyo kununua magari: 4 bilioni.
ii) Upotevu wa fedha katika manunuzi (procurements):12.9 bilioni
iii) Fedha zilizotumika nje ya bajeti iliyokusudiwa: 67. 4 bilioni
Ukitazama mashirika ya umma ndio hatari pia:
i) Bodi ya mikopo Elimu ya Juu (HESLB) imegeuka kuwa chombo cha kutoa zawadi kwa watanzania. Kwa mfano, taarifa inaonesha kuwa kutoka 1994 – 2004/05, imekopesha wanafunzi 113,240 lakini haijaweza kufuatilia fedha zake kwa wengi ni wachache sana wameanza ama wamerudisha mikopo. Bodi imetumia shilingi 51.1 bilioni ambazo kinadharia zinakuwa kama zawadi kwa walengwa, hakuna ufuatiliaji.
ii) Kuna hili la wafanyakazi hewa ambapo kutokana na udhaifu katika usimamizi wa malipo, shilingi bilioni 3 zilipotea mwaka 2009.

Kwa mtizamo wa haraka, kuna kama shilingi 890.8 bilioni, karibu Trilioni moja zimepotea katika kipindi cha mwa ka wa 2009. Kwa mantiki hii, nilipomsikiliza rais akilalama kama vile serikali yake ni masikini sana, ripoti ilinijia nikajiuliza labda ingelikuwa vyema kwa raisi kuwapa picha halisi ya changamoto zinazoikabili serikali yake na angeliwaomba wafanyakazi wajitoe mhanga ili kuepusha upotevu wa mapato ili serikali iboreshe makusanyo ndipo TUKTA ifikirie suala la kuomba maslahi. Badala ya kuwalaumu akina Mgaya, angeliwaomba wamsaidie kuwafunda wafanyakazi juu ya kujali kazi zao kwani upotevu mkubwa wa mafedha hayo au kutofikiwa kwa lengo la makusanyo ni matokeo ya wafanyakazi kuzembea majukumu yao. Ndio maana naamini kabisa raisi Kikwete pamoja na hotuba yake ndefu bado hakuwa na mantiki kabisa siku ile. Ile si hotuba ya Kitaifa, kama ni kwa wazee tu basi ilikuwa muafaka lakini kwa wafanyakazi ambao wengi wao wana akili na wanaona mapungufu kibao serikalini, rais hakututendea haki wafanyakazi.

Pamoja na mapungufu yote ya hotuba ile ya Raisi, lakini lazima nikiri kuwa, ni wajibu wa kiongozi wa serikali kama raisi kuhakikisha nchi haikumbani na migomo. Serikali haina budi kuwazoesha watu wake na masuala ya migomo kama njia ya kutatua matatizo yao. Katika kutimiza hili, raisi amefanikiwa kwani naamini kabisa hakuna mtu atakayegoma kama TUKTA wataendelea kuitisha mgomo mwingine baada ya kusitisha huu wa sasa. Hakuna mtanzania ambaye yuko tayari kufukuzwa kazi au kuandamana akumbane na rungu la dola. Kufanikiwa huko kuepusha mgomo ni ushindi kwa raisi lakini tija na weledi miongoni mwa wafanyakazi vitabakia vikishuka badala ya kuboreka.

Mwisho nimalizie kwa kusema tu kuwa Raisi alipoamua kuzungumza na wazee labda kwa kuwa wote wale enzi zao zimepita labda aliamua aongee katika lugha watakayoilewa ndio maana akaamua kujadili hoja kwa kutumia dhana nyepesi ambazo kimsingi hazikuwa madai makuu ya TUKTA. Naamini kama niliwasikiliza vizuri viongozi wa TUKTA, yapo mambo matatu ya msingi ambayo sikuona Raisi akiyagusa. Mambo hayo ni: Kodi kubwa kwa Makato ya Mishahara, Mishahara midogo sana, Mazingira bora ya Kazi. Hebu fikiria, kuna wafanyakazi lukuki wa serikali wanalazimika kufanya kazi zaidi ya muda wa saa za kazi lakini hawalipwi stahili zao kwa mujibu wa utaratibu.

Na ndipo hapa pamenifanya nijiulize: “Hivi kweli, Raisi wetu anajua athari za kisaikolojia za kauli zake hasi dhidi ya wafanyakazi na viongozi wake katika kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye mafanikio kutoka kwa wafanyakazi wake? Naachia hapa lakini niseme tu hii ni “ Food for Thought”.

Saturday, May 01, 2010

NAREJEA NA YALIYOTOKEA

Huko Uganda, Museveni anabanwa kwa kutumia milioni 300 kwa siku.

Tuesday, March 23, 2010

MNYIKA ANAGOMBEA UBUNGE

Mara nyingi nawaona watu hasa vijana wakionesha dhamira hasa ya kuwa viongozi wa umma. Leo nimekutana na kijana mwenzangu, wa Chama cha Chadema, anatangaza rasmi kugombea ubunge.
Kwa mazingira ya Tanzania, sina hakika kweli kama dhamira yake itafanikiwa iwapo atachaguliwa. Bado mindset/mawazo mtizamo ya watanzania vijana kwa wazee haitamruhusu mtu wa haiba yake kuweza kufanikisha azma yake kirahisi. Kizazi kipya cha vijana wa Tanzania ya leo kimeamua kurithi mtizamo wa wazazi wao: yaani kufanya mambo kwa kufuata hisia zaidi kuliko kwa kufanya uchambuzi wa kina katika kila jambo. Kwa maana nyingine, kama mtu unafikiri sana katika kila jambo unalofanya kama ninavyomfahamu Bwana Mnyika, sidhani kama kweli Bw. Mnyika ataweza Bunge la Tanzania. Watanzania wa leo ni wavivu sana kutumia ubongo, mara nyingi tunatumia mioyo katika kufikiri. Ni jambo la hatari sana na ndio maana watu kama Mnyika wanaonekana na baadhi ya watu kama vile ni vichaa.

Si kwamba ninamchukia ama sipendi Mnyika awe mbunge, ila nataka ajue tu kuwa itakuwa vigumu sana kufikia malengo yake ya kuleta mabadiliko katika Taifa hili changa la Tanzania. Ninamtakia harakati njema.

Tuesday, February 23, 2010

ONA MAMBO YA SERIKALI ZA MITAA MANISPAA YA MOSHI

Baada ya kukaa muda mrefu, leo nataka niwaombe mwanajamii yeyote anayefuatilia globu hii aweze kujaribu kupitia globu hizi mbili ambazo ni kielelezo cha kazi za jamii ninazojihusisha nazo kwa sasa.
Globu ya kwanza ni juu ya shughuli za Kata ya Kaloleni katika Manispaa ya Moshi ambayo mie nafanya kazi hapo katika Manispaa ya Moshi. Hapa utaona kila kinachofanyika hapo. Ipo pia globu nyingine ya lugha ya kiingereza yenye kuonesha mambo hayo hayo. Napenda msome na muweke maoni.

Sunday, February 21, 2010

MTANZANIA AWA MWANAFUNZI BORA MAKERERE

Ni msichana wa Kitanzania ambaye amekuwa miongoni mwa wanafunzi bora kabisa waliohitimu katika Chuo kikuu cha Makerere. Jamani huyu naye ni shujaa wa kuipeperusha bendera ya Taifa letu.

Anaitwa, JOSEPHINE SERUHERE, ni vyema msome hapa na muone ni vipi katutoa kimasomaso.

Monday, January 25, 2010

MPIRA AFRICA ROBO FAINALI ZINAFURAHISHA

Jana yamepigwa mapambano ya kukata shoka. Algeria imeiondoa timu ya Ivory Coast mashindanoni. Ni wazi kwa mchezo wa Ivory Coast, Kombe la dunia Bara la Africa tumelamba garasha.Sioni ni vipi itaweza kuvuka raundi ya Kwanza.

Huko Uganda nataka tujikumbushe enzi za Sadik Wassa aliyekuwa golikipa ambaye hajawahi kutokea.

Friday, January 08, 2010

WAZIRI WA SERIKALI NA KUJALI WENGINE, NINI MAONI YAKO?

Mwaka huu nataka niwe napata maoni ya watu juu ya vikasumba kadhaa ambavyo vinafanywa na wakubwa ama watu wa heshima katika jamii. Leo naanza na hili la waziri mmoja wa serikali ambaye kaingia katika mzozo wa kiaina na mlinzi mmoja wa ATM katika kile nachokiona ni kuendelea kwa tabia ya watanzania kutojua maana ya kuwajali wengine katika huduma ya umma.

Mimi nina swali, hebu soma hiyo habari hapo chini na uniambie je waziri alikuwa sahihi kupokea simu katika wakati aliofanya tendo hilo? Na hata kama kulikuwa hakuna watu, je alikuwa sahihi? Na je ni sahihi kwa mlinzi kumuamuru awapishe wengine wakati yeye ni bwana mkubwa?

Tatu je ni sawa kwa mlinzi kuomba msamaha baada ya kugundua huyu ni mteule wa rais na pia mchaguliwa wa wananchi?

SOMA STORI HII:

WAZIRI WA SERIKALI NA USTAARABU
Sadick Mtulya

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja amesema mlinzi wa kampuni ya Ultimate Security, Pascal Mnaku kwenye mashine za kuchukulia fedha, ATM, alikuwa chanzo cha mtafaruku uliotokea juzi baina ya wawili hao.

Mwananchi iliripoti jana kuwa waziri huyo alikaribia kuzichapa na mlinzi huyo kwenye mashine hiyo ya ATM iliyo kwenye jengo la Harbour View (zamani J.Mall) baada ya Ngeleja kuombwa asogee pembeni kupisha wateja wengine baada ya kumaliza shida zake, lakini akakataa na kuanza kubwatukiana naye.

Jana, akizungumza na Mwananchi kwenye ofisi yake iliyo Barabara ya Samora jijini Dar es Salaam, Ngeleja alisema ni kweli mtafaruku huo ulitokea wakati akichukua fedha kutoka kwenye ATM hiyo ya benki ya Standard Chartered.

Ngeleja alisema alipowasili hakukuwa na mteja mwingine bali aliwakuta watu watatu wakiwa karibu na ATM nyingine ya Barclays iliyo karibu na akaingia kuchukua fedha.

"Katika ATM za Standard Chartered mteja anaweza kuchukua hadi shilingi milioni moja, lakini mteja anaweza kuchukua Sh 400,000 kwa mkupuo mmoja nami nilikuwa nimeshachukua mikupuo miwili wakati nasubiri kuchukua mkupuo wa tatu, simu yangu ikaita nikaipokea huku nikisubiri fedha zitoke," alisema Waziri Ngeleja.

Alisema wakati anasubiri ATM hiyo itoe fedha mkupuo wa tatu huku akisikiliza simu, mlinzi huyo aliingia ndani na kumtaka atoke nje ili kuwapisha wengine waliokuwa wakisubiri huduma hiyo.

Ngeleja alizidi kueleza kuwa baada ya kumaliza kuzungumza kwenye simu huku akisubiri fedha, alimsihi mlinzi huyo kutoka kwenye kibanda hicho ili ampishe aendelee kupata huduma na mlinzi huyo akaanza kupandisha hasira na kusema maneno mengi huku akipiga ukuta kuonyesha hasira zake.

"Nina uhakika yule mlinzi wakati wote huo alikuwa hanijui mimi ni nani kwani wakati akiendelea kutoa maneno makali mteja mmoja alimsihi kuwa aliyekuwa akizungumza naye ni waziri, lakini mlinzi huyo aliendelea kufoka," alisema.

Ngeleja alisema baada ya kupata fedha zake za mkupuo wa tatu aliondoka kwenye eneo hilo na kurejea ofisini kuendelea na kazi zake ndipo walipokuja watu watatu waliojitambulisha kuwa ni kutoka kampuni ya Ultimate Security ambao walikwenda ofisini kwake kuomba radhi kwa tukio lililomhusisha mlinzi wao katika jengo la JM Mall.

"Sikuwaita kuja ofisini kwangu kwa sababu tukio hilo nililichukulia kama ni la kibinadamu na kwamba maelezo yaliyotolewa na mlinzi huyo kuwa siwezi kumsamehe mpaka atakapopewa adhabu kali si kweli," alisema.

Alisema kimsingi mtafaruku huo kati yake na mlinzi huyo uliisha alipoletwa ofisini kwake na mabosi wa Ultimate Security na hasa baada ya mlinzi huyo kumwomba radhi mbele ya wakuu wake wa kazi.

Wakati huohuo, Mnaku ameliambia gazeti hili jana kwamba baada kuchukuliwa na uongozi wa kampuni hiyo na kupelekwa ofisini kwa Ngeleja majira ya saa 9:30 jioni, waziri huyo alilisisitiza apewe adhabu kali.

"Nilipofikishwa tu kwa waziri Ngeleja alisema siwezi kudhalilishwa kwa kuwa nimechaguliwa na watu wengi na pia Rais (Jakaya) Kikwete. Nitakusamehe tu hadi hapo utakapopewa adhabu kali, ili iwe fundisho kwa wengine," alidai Mnaku.

Mnaku alidai kuwa amedokezwa na mmoja wa wapelelezi wanaochunguza sakata hilo kuwa wamepanga kumfungulia mashtaka ya kumtukana Waziri Ngeleja.

"Kwanza nimetakiwa na uongozi wa Ultimate kuwepo ofisini bila kutoka ndani ya saa nane kila siku na pia nimedokezwa kuwa ninaandaliwa mashtaka ya kumtukana waziri," alidai Mnaku.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, sakata hilo lilijitokeza baada ya Mnaku kuwahamishia wateja kutoka katika mashine ya ATM ya Barclays iliyoko katika jengo hilo baada ya kuishiwa fedha.

"Baada ya Mnaku kuona mashine ya ATM ya Barclays kuwa haina fedha, ndipo akalazimika kuwaambia wateja wakatumie ATM ya Standard Chartered ambayo wakati huo Waziri Ngeleja alikuwa anaitumia na huku akizungumza na simu," alisema shuhuda mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe.

Shuhuda huyo alisema baada ya Mnaku kumtaka waziri kuwapisha wengine, ghafla na huku akiwa na hasira, Waziri Ngeleja alisema: "Ina maana hunijui mimi, hujui nafasi yangu, halafu...tusi," alisema shuhuda huyo

Shuhuda huyo aliongeza kusema: "Kutokana na maneno hayo, Mnaku akamjibu kwa kujitetea kwamba mimi nimekuomba uwapishe wateja wengine, sikuwa na jingine". Juhudi za kuupata uongozi wa Ultimate Security kuzungumzia suala hilo zilishindikana.

Wednesday, December 30, 2009

HERI YA MWAKA MPYA -2010

Mwaka Mpya 2010 ndio huo unakaribia, yamebaki masaa

Saturday, December 26, 2009

CHRISTMAS NA ZAWADI

Your Step-by-Step Guide to Returning Gifts

If you weren’t busy telling everyone exactly what you wanted this holiday season, you may find yourself on the receiving end of a couple of gifts you’d rather not keep. No one wants to hurt anyone’s feelings or get into a heated conversation with a sales associate at the store, so here are a few tried and true tricks to make the process of returning gifts as smooth as possible.

Research Return Policies
Check in with each store you need to return gifts to before you begin the process to learn their return parameters. You may have limited time (if any) to receive cash back before you may only opt for credit, or there may be a no-returns policy in place. Banana Republic, for example, will allow you to return for cash (or other method of payment) for only 30 days even if you bought the product yourself. After 30 days you will only receive a store credit—if they allow you to return at all. You may also want to know stores’ policies for returning gifts without a receipt. Generally, you will only get the current selling price, so it may not be worth returning something at all if the item’s price has recently been deeply discounted.

Get Receipts, If Possible
If you don’t know where a gift came from, don’t have a receipt, and have learned you can’t return or exchange it without one, you can always ask the gift-giver for a receipt. However, consider whether it’s worth it before inquiring. If the gift is inexpensive (like these awesome gifts under $25) and you’re worried about offending the giver, you might want to let it go. But, if it’s right up there with the most expensive gifts ever and you know the giver won’t be offended, or you can use a solid excuse like the need for a different size or color, pull the person aside, after all the presents have been unwrapped, and gingerly request the proof of purchase.

Make a Plan
Don’t hit the shops blindly. If you’ve got a bunch of stuff to offload, create an itinerary for hitting all the stores in an order that allows you the least amount of backtracking and the most timesaving. Also, try to show up right when the stores open or when they are about to close to avoid the midday returns rush.

Be Nice
While waiting in customer service lines can be a hassle and there is the occasional surly salesperson, most folks who work retail are more than accustomed to customers making returns. Be polite, honest, and matter-of-fact and be willing to accept the store’s policy and you shouldn’t have any problems returning or exchanging your item—even without a receipt.

Make the Best of Things
Don’t sweat what you can’t return. There are other worthy uses for even the most unwanted gifts. You can re-gift an item (but only if it’s in brand new condition!), donate it to charity, or save it in a special place and show it off the next time the gift-giver comes over to visit (which will make him or her feel extra special).

Monday, October 26, 2009

KIMBEMBE CHA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Ilikuwa ni kivumbi na jasho katika Uchaguzi wa serikali za mitaa jana.Uchaguzi wa serikali za Mitaa niliushuhudia mwenyewe katika Kata moja iitwayo Kaloleni katika Manispaa ya Moshi. Katika uchaguzi huo, ningependa niulezee kwa kadri nilivyouona tanga hatua za awali, yaani uandikishaji wa wapiga kura hadi siku ya kupiga kura.

Mosi, kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi ambazo zilitangazwa na wizara ya Tamisemi, kulikuwa na siku saba (7) za kujiandikisha kwa wapiga kura. Kwa Kata ya Kaloleni, kulikuwa na Mitaa miwili: Kaloleni na Kalimani. Katika mitaa yote hii walijiandikisha watu wachache sana hasa ikizingatiwa kuwa hata theluthi ya wakazi wa Mitaa hii miwili wanaostahili kupiga kura hawakujiandikisha. Hii inamaanisha kuwa, katika Mitaa yote ya Kata hii, viongozi ambao wamepatikana, si wanaotokana na kukubalika na asilimia kubwa ya wakazi. Ila kwa misingi ya kidemokrasia, mtu halazimishwi kujiandikisha, hivyo viongozi hawa ni halali kwa mujibu wa demokrasia.

Pili, kwa muono wangu naamini kuwa zoezi la uandikishaji wapiga kura lilikwenda vizuri sana kwani katika kila kituo cha kujiandikisha, kulikuwepo mawakala wa kila chama cha siasa ambacho kilikuwa kinashiriki katika uchaguzi huo. Kila wakala alionekana akiwa bize na kalamu wakati wote katika eneo la kujiandikishia kitu ambacho kilinifanya niamini kuwa baada ya zoezi hilo la uandikishaji basi ningelipata malalamiko ya pingamizi dhidi ya walioandikishwa.

Kabla sijaendelea, labda niseme tu kuwa katika uchaguzi huu, mimi nilikuwa ni msimamizi msaidizi msaidizi wa uchaguzi katika Kata husika. Kwa nafasi yangu nilipaswa kuratibu zoezi zima jambo ambalo nililifanya kwa weledi wangu wote. Baada ya kueleza ushiriki wangu katika zoezi hili, nigusie juu ya jambo la tatu, nalo ni yale mapingamizi ambayo niliyategemea sana kutoka vyama vyote baada ya uandikishaji. Kanuni zilitoa kipindi cha siku kadhaa kwa kila chama kuwasilisha mapingamizi dhidi ya wale wote waliokuwa hawakutimiza masharti ya kujiandikisha. Katika kipindi chote kilichotolewa, hakuna hata pingamizi moja liliwasilishwa na hivyo nikaamini basi zoezi la uandikishaji lilikwenda vizuri ajabu.

Ikumbukwe pia, wakati zoezi la uandikishaji likiendelea, wagombea wa nafasi za mwenyekiti wa Mtaa, wajumbe wa serikali ya Mtaa pamoja na wale wa Viti Maalum walichukua fomu za kugombea na kwenda kuzijaza kwa mujibu wa utaratibu na kuzirejesha. Baada ya urejeshaji wa fomu, wasimamizi wasaidizi wa kila Mtaa walizipitia na kuhakikisha zinatimiza masharti ya kugombea. Baadaye, wale wagombea wote walithibitika kuwa wamekidhi matakwa ya sheria na hivyo wote waliteuliwa wawe wagombea. Fomu zao zilibandikwa katika mbao za Matangazo ya Ofisi ya Kata na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wa Mitaa yote husika. Pia wagombea wote walipewa nakala ya fomu hizo na siku tatu zilitolewa kwa mapingamizi dhidi yao kuwasilishwa.

Katika siku hizo tatu, wagombea wote wa chama cha Chadema waliwekewa mapingamizi hasa wakilalamikiwa kuwa hawakuthibitishwa na Ofisi ya ngazi ya chini kabisa ya chama chao yaani Tawi. Katika fomu zao, wote walikuwa wamethibitishwa na ngazi ya Kata ambayo viongozi wa chama hicho tayari walikuwa wamewajulisha wasimamizi wasaidizi kuwa hiyo ndiyo ngazi ya chini ya chama chao kupitia barua maalum ya kuwasilisha majina ya wagombea. Maadam kila chama cha siasa kina utaratibu wake wa kiutawala, ilionekana dhahiri hili si tatizo la msingi kwani kuthibitishwa na Ofisi ya Kata, ama wilaya ama Taifa na hata Tawi hakumuongezei au kumpunguzia mgombea sifa za kugombea kama raia mwema. Hivyo pingamizi hili lilitupwa mara moja lakini pia lilipelekwa hadi ngazi ya juu zaidi na likatupwa pia.

Baada ya mapingamizi haya kutupwa, uchaguzi ulikuwa umewadia na hivyo vyama vyote vilisahau kuhusu pingamizi na vikabakia vikijiimarisha na kushiriki katika uchaguzi siku ya tarehe 25/10/2009.

SIKU YA UCHAGUZI
Siku moja kabla ya uchaguzi nililala mapema ili niweze kuamka mapema kutekeleza jukumu la kitaifa. Na kweli niliweza kuamka mapema muda wa saa 12:00 asubuhi, kulikuwa kumenyesha mvua hivyo ili niweze kuwahi, ilinibidi nichukue teksi na nikafika katika Ofisi ya Kata asubuhi ya saa 12:50 nikamkuta Msimamizi Msaidizi Mkuu kutoka Halmashauri akiwa na vyombo vya uchaguzi tayari amefika. Mara moja kazi ya kusambaza vyombo ilianza kwa kutumia gari la Halmashauri katika eneo langu la kazi ili ifikapo saa 2:00 asubuhi upigaji kura uweze kuanza.

Mungu alisaidia, ilipofika saa 2:00 asubuhi upigaji kura ulianza na mara moja kulikuwa na vitimbi. Kwanza katika kituo kimoja, Ofisi ya Kata, alifika mpiga kura mmoja akapiga kura kimakosa na kugundua kuwa alitumia karatasi za aina moja tu kupiga kura zote tatu: mwenyekiti Mtaa, mjumbe wa Mtaa na Viti Maalum. Wakati tayari ameshatumbukiza karatasi ya kupigia kura kwenye visanduku husika, mara akawa mbogo na kuniita kama Msimamizi Mkuu akiwa na mawakala wa chama chake wakisisitiza tufungue sanduku la kura ili arekebishe. Hili nilimwambia kuwa haliwezekani na kama kweli amekosea basi kura hizo zitakuwa zimeharibika.

Baada ya jaribio hili kushindikana, huyu bwana akiwa na mawakala wake walisisitiza kuwa basi wakati wa kuhesabu kura tuzitambue kura hizo. Hapa pia niliwajibu hatutaweza kujua kama kweli ndizo zitakuwa kura zilizopigwa na bwana huyu. Baada ya mimi kuonesha ugumu wa kuwasikiliza, busara iliwaingia mawakala pamoja na mpiga kura wao, na alikubali yaishe na akaaga kwa amani. Zoezi likaendelea; ila pia katika Kituo kingine katika Mtaa wa pili wa Kalimani, kitimbi cha kwanza kabisa ilikuwa ni pale kabla hata ya upigaji kura kuanza, mawakala wa chama Fulani na wapenzi wao, walinijia kwa jazba sana wakidai kuwa kabla ya zoezi kuanza ni lazima mawakala wote na wasimamizi wote wakaguliwe.

Hali hii ilijitokeza kuwa Msimamizi Mkuu wa Kituo hiki, ambaye alikuwa ni mwanamama, alikuwa amebeba begi la mkononi, yale mabegi ya fasheni za kisasa kwa akina mama, lakini kelele zilipigwa zikidai kuwa mama huyu amebeba kura ndani ya begi lake. Kuona hivyo mama huyu kwa weledi wa hali ya juu alikabidhi begi lake kwa askari wa mgambo aliyekuwepo alikague na akaguliwa mbele ya wananchi. Hakukuwa na kitu ingawa binafsi nilisikitika wananchi wanalazimisha mwanamama akaguliwe na askari wa kiume kwani kulikuwa hakuna askari wa kike. Pia sikupendezwa sana kwa begi kukaguliwa hadharani, kwani kikawaida, mabegi haya yanakuwa na vitu vya faragha. Lakini maadam ndiyo tafsiri ya demokrasia wananchi wetu wanayoijua isiyojali sana haki za kibinafsi basi sikuwa na njia kwani kulikuwa na kila dalili ya dhahama kutokea.

Mungu aliepusha mbali ukaguzi ulifanywa, wananchi wakaridhika na hamasa ikabakia katika kuhesabu kura na kupata mshindi.

KUHESABU KURA NA KUPATA WASHINDI

Kwa mujibu wa taratibu, ilipotimu saa 10:00 kamili zoezi la upigaji kura lilifungwa rasmi na shughuli za kuhesabu kura zilianza mara moja. Hapa napo hapakukosekana vitimbi kama si vimbembe. Katika kituo cha Kaloleni, mawakala wa vyama vilivyogombea: CCM na Chadema waliruhusiwa kuwepo wakati wa kuhesabu kura ndani ya chumba maalum pamoja pia na wagombea waliruhusiwa kushuhudia. Katika hali isiyo ya kawaida ama isiyoeleweka, mgombea wa CCM hakuwepo ilisemekana kuwa amekwenda kuswali huku wengine wakidai alikwenda kupumzika nyumbani. Mgombea wa Chadema aliruhusiwa kuingia katika chumba cha kuhesabia kura kitu ambacho kiliibua kelele nyingi dhidi ya Msimamizi Msaidizi kuwa anapendelea chama cha Chadema.

Hata pale wapenzi na viongozi wa CCM walipoelezwa kuwa mgombea wao hajakatazwa ana haki ya kuingia katika chumba cha kuhesabia kura, bado walilazimisha zoezi lisimamishwe na asubiriwe mgombea wa CCM arejee ndipo zoezi liendelee. Nikiwa kama Msimamizi Msaidizi, niliamua kuwa ili kutimiza haki ya msingi bila kuminya nyingine, na kwa kuzingatia kuwa haikujulikana ni saa ngapi mgombea wa CCM angelirejea basi ni vyema nimwombe mgombea wa Chadema atoke nje ili mawakala wasalie ndani na zoezi la kuhesabu liendelee ili kuokoa muda. Nilipomuomba aliridhia maelezo yangu na akatoka nje na zoezi likaendelea.

Kiroja kingine juu ya hili kilijitokeza muda mfupi baadaye wakati niliposikia kelele za wapenzi wa CCM wakisogelea eneo kuhesabia kura huku wakiwa wamemzingira mgombea wao ambaye walikuwa wamekwenda kumleta ili aje ashiriki zoezi la kuhesabu kura. Kama msimamizi msaidizi nilitoka kuona kunani? Wapenzi wenye jazba walikuwa wanapiga kelele kuwa mgombea wao aruhusiwe kuingia ndani ya chumba cha kuhesabia kura. Mara moja nilipomueleza mgombea huyo juu ya kilichotokea aliniambia kuwa yeye kamwe hawezi kuingia ndani ya chumba cha kuhesabia kura. Alianza kunilaumu kuwa mbona sikumjulisha kuwa ni haki yake kuwepo katika zoezi hilo? Mimi nilishangazwa kidogo kwani haikuniingia akilini eti mtu anagombea nafasi wakati hajui taratibu za uchaguzi. Hii ilinikumbusha kuwa kuna tatizo katika vyama vyetu katika kuwaandaa wagombea wetu.

Alipokataa kuingia ndani kwa kisingizio kuwa mawakala wake wafanye hilo, huku nyuma mgombea wa Chadema alikuwa yuko tayari aingie ndani. Kutokana na hali kuwa tete, ilibidi nimsihi mgombea wa Chadema asiingie ndani ingawa ni haki yake, kwani niling’amua kuwa maadam tayari kuna dalili za kuonesha kuwa ninampendelea mgombea wa Chadema nilidhani ni vyema nikawanyima wote wakae tu nje na wawaachie mawakala wao kuhesabu kura. Nilimnyima mgombea wa Chadema haki ya kushuhudia zoezi la kuhesabu kura kwani niliamini kuwa pindi matokeo yatakapotangazwa inawezekana kabisa uwepo wake mwenyewe ndani ya chumba cha kuhesabia kura ikawa ni chanzo cha kuibua sintofahamu juu ya ushawishi wake katika matokeo. Sikutaka kamwe matokeo ya uchaguzi ule yawe na mashaka. Mungu alisaidia na uchaguzi ulikwenda shwari na mwishoni baada ya kuhesabu kura, wagombea wote wawili waliitwa ndani ya chumba na wakaoneshwa matokeo yao wakiwa na mawakala wao na kupewa fomu maalum kusaini kukubali ama kukataa matokeo.

Wagombea wote walikubali matokeo na kusaini fomu kabla ya Msimamizi Msaidizi kuyatangaza hadharani kwani ilibidi ifanyike hivyo ili kuweza kuwadhibiti wapenzi wao ambao walikuwa nje na shauku kubwa. Hali hii ilikuwa inatishia amani hivyo, ilibidi tuwaombe kuwa wagombea watusaidie kuwadhibiti wapenzi wao ili mshindi atakapowekwa wazi basi kuwe na utulivu huku wakiwa wamekwishawaonesha hali ya kukubali matokeo hayo. Hili lilifanyika na mwisho matokeo yaliwekwa hadharani na zoezi lilifungwa kwa amani baada ya mgombea wa CCM kushinda.

KUHESABU KURA MTAA WA KALIMANI

Ikumbukwe kuwa katika Mtaa wa Kalimani, zoezi la upigaji kura lilianza kwa kimbembe cha wasimamizi na mawakala kukaguliwa pochi zao na hata maungoni (mifukoni) pale watu walipoamini kulikuwa na uwezekano wa kura kufichwa. Imani hapa ilikuwa ni ndogo sana dhidi ya watumishi wa serikali. Wafuasi wa chama cha Chadema walikuwa na hamasa na hali ya kutowaamini kabisa watendaji wa serikali.

Kabla ya kura kuhesabiwa, tayari wananchi kadhaa akiwemo Diwani wa Kata ya Kaloleni walinifikishia malalamiko yao kwa mdomo na kwa njia ya simu kuhusu kuwepo kwa wapiga kura wasio kuwa na sifa, yaani watoto. Binafsi niliwajibu kuwa kuleta pingamizi siku hiyo si sahihi kwani kulikuwa na muda wake ambao hawakuutumia. Lakini pia niliwasihi kuwa mawakala wao si wapo eneo la kupigia kura, basi kwanini wasiwazuie na zifanyike juhudi za kuwatambua kiumri? Ni wazi majibu yangu haya dhahiri hayakuwaridhisha walalamikaji hawa wa chama cha CCM lakini sikuwa na njia nyingine ya kuwasaidia zaidi ya kutembelea vituo vyote vilivyolalamikiwa na kukuta zoezi la kupiga kura likiendelea huku wasimamizi pamoja na mawakala wa vyama vyote wakiwa wametulia wakiniambia hakuna taabu wala shida yeyote. Nilifanya upitiaji huu mara tatu kabla ya zoezi la kupiga kura kufungwa na sikukuta jambo hili likisemwa na wakala yeyote kama ni tatizo.

Kwa hali hiyo niliridhika kuwa labda hili ni hali ya homa ya uchaguzi miongoni mwa wapenzi wa CCM. Uchaguzi uliendelea vyema hadi kufungwa na zoezi la kuhesabu kura lilianza ambapo lilikwenda hadi mnamo saa sita za usiku. Hapa palitokea vimbembe kadhaa: Kwa mfano, wakati kura za nafasi ya uenyekiti zikihesabiwa mara baada ya zile za wajumbe na viti maalum kukamilika, ilikuwa tayari imeonesha kuwa wagombea wa Chadema walikuwa na mwelekeo wa kushinda karibu viti vyote. Hesabu ya kura ya nafasi ya mwenyekiti ilijaa hamasa, jazba na hofu miongoni mwa mawakala na wagombea wote. Ikiwa ni karibu zoezi la kuhesabu kura limalizike, nje ya chumba cha kuhesabu kura wananchi walijawa na bashasha na hamasa kubwa zikiambatana na jazba ya kupata matokeo. Kelele ziliongezeka sana na walinzi (mgambo na polisi) walipata taabu sana kuwadhibiti vijana hao.

Mara taa za chumba hicho cha kuhesabia kura zilizimwa na mawe yalianza kurushwa juu ya paa kwa wingi na makelele ya kila aina. Hali ya mkanganyiko ilijitokeza wengi tukidhani ni umeme umekatika. Kumbe la, kuna mmoja miongoni mwa mawakala ama wagombea waliokuwa ndani ya chumba cha kuhesabia kura alikuwa amezima taa. Mimi pamoja na Msimamizi Msaidizi wa Halmashauri tulikuwa nje tukijaribu kuwatuliza wananchi ambao walikuwa wakivurumisha mawe na kupiga makelele.

Baada ya muda mfupi, taa iliwashwa na mara mawakala wawili ambao pia ni mke na mume walionekana wakihimiza wenzao kuwa haitawezekana tena zoezi la kuhesabu kura liendelee kwani kuna mtu (mmoja wa msimamizi aliyekuwa akiendesha zoezi la kuhesabu kura ambaye pia ni mwalimu kitaaluma amechukua kura za mgombea wao na kuzihamisha). Kutokana na hali ile, wasimamizi wote watatu tuliokuwemo ndani ya chumba kile tulijaribu kuwatuliza watu wote na tukaamuru kuwa zoezi la kuhesabu kura za nafasi ya mwenyekiti wa Mtaa lianze upya.

Nilisisitiza kuwa ni lazima zoezi lianze upya kwani wakati taa zilipozimika, alikuwepo mgombea mmoja ambaye alikuwa na tochi na alikuwa ameiwasha kuelekea katika eneo la kuhesabia na ilionekana dhahiri kuwa kila mtu eneo lile alikuwa ametulia na hakuna aliyekuwa akifanya lolote hadi pale taa zilipowaka. Nilijiridhisha na hili na ndio maana niliamua kuamuru kuhesabu kura kurejewe kwani nilikuwa nina uhakika kuwa hakuna aina yeyote ya ukiukwaji wa utaratibu ulifanyika wakati taa zimezimika kwani kwa mwanga wa tochi na mimi nikiwa dirishani niliweza kuona kila kitu katika eneo la kuhesabia. Niliamini kuwa mawakala hawa wawili walikuwa ni chanzo cha uvurugaji wa zoezi zima la uchaguzi na hivyo sikutaka kuwapa mwanya. Kama Afisa Mtendaji wa Kata tayari nilikwishasikia tetesi kuwa wafuasi wa chama Fulani walikuwa wamekutana kwenye nyumba Fulani siku mbili kabla ya siku ya kupiga kura na kupanga nini cha kufanya pale itakapodhihirika wanashindwa. Hivyo, niliamini kuwa huenda kuzimwa taa ndiko kulikokuwa chanzo cha utekelezaji wa tetesi nilizokuwa nimezisikia.

Kwa kutumia ushawishi wa kimamlaka, zoezi zima la kuhesabu kura za nafasi ya mwenyekiti wa Mtaa lilirejewa na hadi mwisho mgombea wa Chadema pamoja na wajumbe wanne waliibuka washindi huku CCM ikipata mgombea mmoja. Mara baada ya matokeo kuwa dhahiri, wagombea wote wa CCM walikataa kusaini fomu za matokeo kwa ushawishi mkubwa wa wale wavurugaji wawili ambao nimewaelezea hapo awali. Pamoja na kukataa huko, ilibidi tuombe ulinzi wa FFU ili kuwakaribia wapenzi wa Chama cha Chadema waliokuwa na shauku ya matokeo wakiwa na jazba ya ajabu. Mgombea aliyeshinda wa Chadema aliombwa awatulize wapenzi wake na matokeo yakatangazwa na watu wakaondoka zao. Muda wa saa saba usiku tuliyafikisha matokeo ya uchaguzi pamoja na vyombo vya uchaguzi Halmashauri na siku ikawa imekwisha.

CHANGAMOTO ZA UCHAGUZI HUU:

Uchaguzi huu ambao kwa kiasi Fulani uliboreshwa umeonesha kuwa bado watanzania wengi hawajiandikishi kupiga kura kwani wengi hawaoni umuhimu wa serikali za mitaa. Na wengi wa wananchi wala hawajui nini ni wajibu wa serikali ya mitaa.
Pili, wengi hamtaamini lakini ukweli ni kuwa wananchi wengi wa Tanzania hawajui kusoma wala kuandika. Wananchi wengi wamepigiwa kura, huku hili likiwa ni mwanya wa baadhi ya kura kupigwa kwa mgombea ambaye si chaguo halisi la mpigaji aliyepaswa; kwani vyama viliwaandaa vijana kuwadanganya wasiojua kusoma wala kuandika kwa kupigia kura wagombea wa vyama vyao.

Tatu, pamoja na serikali kutoa miongozo mingi ya uchaguzi huu, lakini uchunguzi binafsi unaonesha kuwa vyama vya siasa havikushirikishwa kwa dhati. Kwa mfano utakuta Msimamizi Msaidizi unalumbana na wagombea na wapenzi wao kutokana na hali ya wao kutokujua taratibu za uchaguzi. Kuna haja ya makabrasha yote ya uchaguzi kugawanywa kwenye vyama vyote ili viweze kuyatumia kwa kuyasoma na kuwafunza wafuasi wao na hata wagombea wao. Hili likifanyika, tutapunguza sana mizozo inayoibuka ama hisia mbaya na potofu za kupendelea zinatojitokeza kwa wasimamizi.

Nne, ni wazi kuwa kutokujitokeza kwa wapiga kura wengi kunatokana na Serikali za Mitaa kutokuwa hai vya kutosha. Sehemu nyingi serikali za Mitaa imebaki jina zaidi na si vitendo ndio maana watu wengi hawajui umuhimu wake.

Tano, kutokana na kukuwa kwa demokrasia nchini mwetu, umefika wakati watu kufundishwa kuaminiana hata kama mtu mmoja yuko chama pinzani. Uchaguzi wa Kaloleni ulikuwa umejaa kutokuaminiana miongoni mwa vyama viwili; na pia ni vyema misingi ya kidemokrasia ya kushindwa na kushinda ikafundishwa zaidi kwani bado kuna watu wanaoamini kuwa katika kila kinyang’anyiro lazima washinde tu.

Sita, hatua ya chama cha CCM kuweka pingamizi dhidi ya wagombea wa Chadema katika eneo nililokuwa nalisimamia ilileta picha kuwa CCM ilitaka wagombea wake watangazwe washindi bila uchaguzi kufanyika. Sidhani na wala siamini ni sahihi kutegemea zaidi ushindi wa mezani kwani mara nyingine tunaweza kuwa na viongozi waliopendekezwa tu na wanachama Fulani na wala si wakazi kwa maslahi yao. Pia ningedhani kuwa ni vyema kama mgombea aliyebakia ni mmoja basi iwepo ile sheria ya “proportional representation” yaani uwiiano,kura zipigwe na mgombea ashinde kwa kufikia kiwango fulani cha kura ndipo atangazwe halali ni mshindi. Naamini tabia ya kupenda kupata kiongozi aliyepita bila kupingwa si demokrasia makini bali ni “primitive politics” au siasa za porini. Ni lazima kila kiongozi katika jamii ya kidemokrasia achujwe kwa wapiga kura wake na wala si tu kupitia chama chake.

Jambo la saba, kuna haja ya wanasiasa kutenganisha nafasi ya wanasiasa na watendaji wa serikali katika chaguzi zetu. Kwa mfano, wasimamizi wa uchaguzi wanapata shida sana kutokana na mibinyo ya wanasiasa na hata wapenzi wa vyama vya siasa. Wanasiasa wa CCM katika ngazi za chini wanaamini kabisa kuwa Afisa Mtendaji wa Kata au Mtaa ni Kada wa chama kitu ambacho si sahihi. Wanaamini kabisa uwepo wa Afisa huyu ana wajibu wa kuweka mazingira mazuri ili washinde. Haya ni mawazo ya watu wasiosoma, wenye mawazo ya kale “primitive thinking”.

Kutokana na hali hii, pia upande wa vyama vya upinzani, wao wanaamini kuwa maafisa wa serikali wanaosimamia uchaguzi ni sehemu ya Chama Tawala na hivyo si rahisi watende haki. Hali hii inasababisha mikwaruzano mingi isiyo ya lazima. Kuna haja ya serikali na hata asasi mbalimbali kuliweka hili vizuri. La sivyo bado tutabaki tukifikiri katika mitizamo ya Chama kushika hatamu kitu ambacho kilishapitwa na wakati.

Jambo la nane, ni vyema wakati wa kuandaa karatazi za kupigia kura, basi kwa upande wa wajumbe, kuwe na karatasi za kupigia kura kwa idadi ya wajumbe badala ya kuweka majina yote ya wajumbe katika karatasi moja. Hii itarahisisha zoezi la kuhesabu kwani muda mwingi ulitumika sana katika kupata idadi ya kila kura za mgombea kutoka katika karatasi moja. Ni vyema hapa pakawa na karatasi tano zilizo tupu anapewa mpiga kura na yeye mwenyewe anazijaza kwa kuweka majina ya wagombea anaowataka kwa Wajumbe na kwa Viti maalum. Kupigia wajumbe kwenye karatasi moja kumefanya zoezi la kuhesabu kuwa gumu na la muda mrefu.

Jambo la mwisho, ningewashauri wale wote wanaofanya mafunzo ya utafiti wajaribu kuandika tafiti zao juu ya Serikali za Mitaa kwani panahitajika marekebisho mengi sana kiutendaji ili Serikali za Mitaa ziweze kuwa kweli kioo cha jamii katika maendeleo yao. Sehemu nyingi nchini bado Serikali za Mitaa ziko chini sana kiutendaji. Hili ndilo linalochangia kwa wananchi wengi hadi leo hasa wasomi hawajui ni nini umuhimu wa serikali za Mitaa.

MWISHO
Kwa nilivyoeleza hapo juu, hiyo ndiyo picha halisi ya kimbembe cha uchaguzi katika Kata ya Kaloleni. Kama matokeo yanavyoonekana, ni wazi kuwa sasa vyama viwili: CCM na Chadema vitaongoza mtaa mmoja kwa mmoja. Kama Mtendaji nasubiri nione ni changamoto zipi za kiuongozi na kiutawala zitajitokeza katika kufanya kazi na serikali ya Mtaa ulio chini ya Chama cha Upinzani.

Kama mfanyakazi wa serikali ambaye nina uelewa wa taratibu za kiserikali za utawala bora naamini shughuli zitatekelezeka kama tutafuata misingi ya kidemokrasia. Ni imani yangu kwa watu wengi hawaamini itakuwaje ila naamini kwa kuzingatia sheria na kwa kuzisimamia sheria bila kuzipindisha, mambo yatakwenda shwari.

Thursday, October 22, 2009

Vyama tawala Africa ni wizi mtupu.

Wednesday, October 21, 2009

UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA -2009 UMEDODA

Jumapili, tarehe 25th October 2009, ni siku ya uchaguzi wa serikali za Mitaa hapa nchini Tanzania. Nataka nitoe tathimini fupi tu juu ya zoezi zima hili kabla ya siku ya uchaguzi. Niseme tu, tathmini yangu inaanzia tangu siku ya kujiandikisha miongoni mwa wapiga kura. Nitaonesha ni nini hasa chanzo cha tatizo la wananchi wengi kutojiandikisha na pia ni jinsi gani vyama vya siasa vimeandaa wagombea wao pamoja na kasoro kadhaa ambazo zitachangia tuchague viongozi bomu miongoni mwa wagombea tunaopaswa kuwachagua mwaka huu.

Mosi, kwa uchunguzi wangu, wananchi wengi hawakujiandikisha kabisa katika zoezi la kuchagua viongozi wa serikali ya mitaa. Hali hii haijashangaza kabisa kwani ni wazi watanzania wengi sana hasa wasomi hawaelewi kabisa ni nini maana na wala umuhimu wa serikali za Mitaa. Wala hawajui wajibu wa serikali za mitaa na ndio maana wengi wa wananchi hawakwenda kujiandikisha na wala hawana mpango wa kupiga kura.

Pili, kuna sababu nyingine ambayo ni ya msingi sana inayochangia wananchi wengi kutozingatia wala kutokupenda kutegemea ofisi ya serikali ya mtaa. Ukiangalia, kwa kupitia mazoea ya utendaji kazi katika Halmashauri mbalimbali hapa nchini, ni wazi serikali za Mitaa ni hafifu sana hapa nchini Tanzania; na kwa uhalisia Ofisi hizi zinaendeshwa kienyeji sana kwa kutozingatia taratibu za “Utawala bora” huku rushwa ndogondogo zikibakia kama ndio tegemeo kuu la watendaji wakuu wa Ofisi hizi.

Tatu, labda nitoe mifano michache hapa: nenda Ofisi za Vijiji au Kata pamoja na Mitaa, hapa utawakuta maafisa mbalimbali ambao wameajiriwa na serikali za Mitaa kupitia halmashauri mbalimbali hapa nchini. Kwa mfano, kuna Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa ambao ndio waratibu wakuu wa shughuli za serikali katika Mitaa na Kata. Wapo maafisa waratibu wa elimu, maafisa afya, maafisa kilimo, na maafisa maendeleo ya jamii. Lakini katika Ofisi hizi nyingi hapa nchini ukijiuliza kama kweli maafisa hawa wanafanya kazi zao kwa kuwajibika au la, unapata jibu kuwa hamna kitu. Ni wizi mtupu nchi hii. Mara nyingi maafisa hawa wako pale kwa ajili ya kuibia serikali fedha kupitia mishahara bila kufanya kazi.

Ninasema hivi kwani kiutaratibu ili wananchi waweze kuona thamani “value”, ya serikali za Mitaa ni kupitia shughuli ambazo maafisa hawa wanapaswa kushirikiana na wananchi katika utekelezaji. Uzoefu na uchunguzi wangu umenionesha kuwa wananchi wengi hawajui kabisa ni nini wajibu wa maafisa hawa katika Kata au mitaa yao. Kuna pia utaratibu wa kuitisha mikutano ya hadhara kwa kila Mtaa ama Kijiji, lakini utashangaa, hakuna juhudi zozote zinazofanyika kuhakikisha taratibu hii inafanyika.

Changamoto kubwa hapa inakuwa ni kuwa hata wananchi huwa hawapatikani katika kuhudhuria mikutano hii. Lakini pia hata pale wananchi wanapopatikana, maafisa hawa hawako tayari kuhudhuria kwani huwa hawalipwi marupurupu ambayo wangestahili kwani hii huwa ni kazi nje ya muda wa kazi na hasa siku za wikendi. Kwa hili ni dhahiri kuwa Halmashauri nyingi hapa nchini pamoja na kuwa zinasifiwa kwa kufanya mikutano ya hadhara, mara nyingi mikutano hii haifanyiki na inaandikwa mihutasari ya gagari na kuonekana kama vile inafanyika. Na ndio maana hadi tunapofanya uchaguzi huu unakuta kuwa wananchi wengi wala hawana habari na Serikali za Mitaa.

Kwa ufupi ni kuwa kuna haja kubwa kwa serikali za mitaa kuamka hasa kwa upande wa watendaji wa sekta hii kwani kama hali itaachwa hivyo, basi tusishangae hali hii ya kutojitokeza katika kupiga kura itaendelea.

Jambo la nne ambalo lazima niliweke wazi: nimejionea kasumba fulani ya chama fulani kujitokeza katika kuwawekea pingamizi wagombea wa vyama vingine na kujaribu kung’ang’aniza uchaguzi huu uendeshwe ukiwa na mgombea mmoja tu wakiamini kuwa angelitangazwa kuwa hana mpinzani na hivyo kuwa ni mshindi. Kasumba hii kama itaachwa tu iendelee basi ni wazi bado nchi yetu ina watu ambao bado wana mawazo ya chama kimoja na kwao demokrasia ya ushindani hawaitaki kabisa. Pia hata waliotunga kanuni za uchaguzi huu ni lazima waipitie tena kanuni ya wagombea kwani imedhihirika wazi kuwa hawakuzungumzia nini kifanyike pale ambapo mgombea anapobakia ni mmoja kama wengine wakijitoa. Hili nimeliona kwani nadhani kidemokrasia si sahihi kwa mgombea kutangazwa mshindi wakati hajapigiwa kura.

Kwa mantiki hiyo, naamini uchaguzi huu tutapata wagombea ambao hakuna ushahidi wa dhati unaoonesha kukubalika kwao miongoni mwa wananchi watakaowaongoza. Nasema hivyo kwani naamini kulihitajika iwapo mgombea ni mmoja, basi apigiwe kura na kuwe na kiwango ambacho atastahili akifikie ili aonekane anakubalika kuwa mshindi. Hii habari ya kusema eti huyo amepitwa bila kupingwa kwa kiasi fulani ni dhihirisho kuwa nchi yetu bado tuna tatizo la kufikiri sahihi na kwa mantiki. Kwa maelezo yangu kwa hili, uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu utazalisha viongozi haramu kwa kiasi Fulani kwani inawezekana kabisa mtu akatumia ama nguvu za fedha au vitisho vya ushirikina ili achaguliwe kilaini bila kupigiwa kura kwani wale ambao wangeweza kujaribu kupingana naye wataogopa. Na hii si demokrasia.

Pia nimeshuhudia kuwa vyama vya upinzani pamoja na kujua kuwa uchaguzi huu ulikuwepo, vimekurupuka sana katika kuweka wagombea wanaofaa. Sehemu kadhaa nimeona wagombea waliowekwa ni wa kuokoteza tu, si watu makini ambao wana uwezo wa kuongoza. Ni dhahiri, vyama vya upinzani vikiendelea na hali hii basi vitakuwa kama chanzo cha demokrasia ambayo haina tija. Haiwezekani watu wanaokotezwa tu, watu ambao jana tu walikuwa hawana itikadi yeyote leo wanakuwa na itikadi fulani na wanapewa uongozi. Huwezi kwenda kumuokota mpiga debe katika vituo vya mabasi au jitu lisilokuwa na shughuli yeyote ya maana zaidi ya kuendesha shughuli zinazojulikana kama “mission town” kuwa mgombea katika zama hizi licha ya kuwa kila mwananchi ana haki ya kugombea na kuchaguliwa. Tunavyolifanya hili ni dhihirisho kuwa vyamba vyetu vya siasa bado vina tatizo. Hili nimeliona sana katika vyama vyote vya upinzani na nadhani kama kweli tutakwenda hivi basi tusishangae uchaguzi huu hautakuwa na tija tarajiwa.

Si vyama vya upinzani tu, Chama tawala nacho kimeonesha mapungufu sana katika zoezi la kuweka wagombea. Chama hiki bado hakijafika mahali kikaona kuwa uchaguzi ni wakati muafaka kuleta mabadiliko. Kwa chama hiki, hata kama aliyekuwa kiongozi wao alikuwa mzembe na asiye mtendaji bora, wao hawakuchuja. Ule mfumo ambao ulisifiwa kuwa ni wa uwazi kupata wagombea umechezewa. Kura za maoni katika chama hiki ziliendeshwa kienyeji. Kadi za chama hiki ziligawanywa kama njugu huku kila mgombea akizinunua na kuzigawa kwa wapiga kura ambao aliamini wangemchagua. Ni kwa mtizamo huu bado unaona hata chama tawala bado hakijakuwa na mfumo bora na wa kisayansi kupata wagombea.

Kwa ujumla, vyama vyote, vile vya upinzani na mtindo wa kuokoteza wagombea pamoja na CCM kuendesha zoezi la kura za maoni lisilo la kisayansi wameboronga katika kupata wagombea bora. Hapa simaanishi kuwa wagombea wote si bora ila kuna mwanya mkubwa wa kuwa na wagombea bomu katika uchaguzi wa serikali za Mitaa mwaka huu. Uchaguzi wa mwaka huu basi uwaamshe viongozi wetu kutizama upya uendeshaji wa serikali za Mitaa hapa nchini, na kuzingatia umuhimu wa kuwa na viongozi waadilifu na wenye weledi na akili timamu zinazoendana na alama za nyakati tulizonazo. La sivyo, nchi hii haitabadilika kamwe.

Umefika wakati akina Mizengo Pinda wajue kuwa Serikali za Mitaa zikiendeshwa kwa kujali maafisa wakuu katika ngazi za juu tu katika Halmashauri zetu basi kamwe hata siku moja, wananchi hawatakaa waelewe umuhimu wa serikali za Mitaa. Kwa hali ilivyo sasa, juhudi kubwa za kiuwezeshaji zinalengwa kwa maafisa katika makao makuu ya Halmashauri ambao wao ni kukaa ofisini zaidi na kuhudhuria vikao visivyokwisha na baadaye kutoa amri za utekelezaji kwa simu kwa maafisa wa chini huko kwenye Kata, Mitaa na Vijiji. Maafisa hawa wadogo kutokana na kutokupewa mtizamo chanya kiuwezeshaji ili watekeleze kazi zao mara nyingi wamedoda na hawatekelezi lile wanalopaswa na ndipo hapa wananchi wengi wala hawana habari kama kuna serikali za Mitaa.

Ni wazi kwa mtizamo wangu ambao nimeufanyia uchunguzi na kujiuliza sana kwanini wananchi wengi hawazijali Serikali za Mitaa, ni wazi kuna tatizo la kiutendaji bado katika kuziendesha Halmashauri zetu pamoja na kudhani kuwa tayari tuna mafanikio. Ni lazima tukubali mafanikio tulionayo lakini tukubali pia kuwa kuna changamoto kedekede ambazo ni lazima tuzifanyie kazi na uchaguzi utakaokuja basi watu wawe na ushiriki zaidi ya sasa. Kwangu mimi, kutokujiandikisha miongoni mwa wananchi wengi ni dhihirisho la wazi la utendaji dhaifu, usiokuwa na tija wa miongoni mwa Halmashauri zetu.

Monday, October 19, 2009

MWALIMU NYERERE NA MAFANIKIO

Mwalimu Nyerere kama wanadamu wengine alipata sapoti kubwa sana kwa waliomzunguka hadi kufikia mafanikio. Pia ni vyema kujua je, Nyerere alikuwa mwana wa Africa nzima ama tu ile Afrika kusini mwa jangwa la sahara?
Kama baba wa Taifa alikuwa na mtizamo juu ya hali ya Elimu ya Juu. Alitaka Elimu ya Juu iwe ya kiwango cha juu pia si ya bora liende tu. Si elimu tu, ila alipigania hasa, Uhuru wa Mwafrika.

MWALIMU AWA MTAKATIFU: Kanisa katoliki limeanza mchakato wa kumfanya mwalimu kuwa ni mtakatifu.
Mwisho, yuko bwana mmoja anampenda sana mwalimu, hebu soma barua yake.

Saturday, October 17, 2009

SIKU YA CHAKULA DUNIANI NA VIMBWANGA VYAKE

Ugh! kwa wasomaji wangu, nimekuwa kimya sasa narejea kwa kuwapa machache niyasoayo. Huko Uganda Mambo ya MDGs juu ya Ukimwi, je inawezekana?
Wanasema pia tusishangazwe na Uganda kuendelea kuwa chini ya kutokuwa na amani kwa miaka mingi, ni kuwa chuki ilipandwa tangu wakati wa uhuru.
Pia kwa kuwa jana ilikuwa siku ya chakula duniani, ni wazi kuna watu wanapata taabu sana kwani wanahitaji kula vizuri lakini hakuna chakula hasa wale wanaotumia dawa za kuwaongezea maisha.

Kwa wale wanaopenda kuwa na akina dada karibu, ni wakati mtu kujiuliza, unajua makundi ya akina dada hasa katika maeneo ya shule? Huko huko mashuleni, je tunajua maprofesa wanafanya nini?