My Blog List

Tuesday, February 23, 2010

ONA MAMBO YA SERIKALI ZA MITAA MANISPAA YA MOSHI

Baada ya kukaa muda mrefu, leo nataka niwaombe mwanajamii yeyote anayefuatilia globu hii aweze kujaribu kupitia globu hizi mbili ambazo ni kielelezo cha kazi za jamii ninazojihusisha nazo kwa sasa.
Globu ya kwanza ni juu ya shughuli za Kata ya Kaloleni katika Manispaa ya Moshi ambayo mie nafanya kazi hapo katika Manispaa ya Moshi. Hapa utaona kila kinachofanyika hapo. Ipo pia globu nyingine ya lugha ya kiingereza yenye kuonesha mambo hayo hayo. Napenda msome na muweke maoni.

Sunday, February 21, 2010

MTANZANIA AWA MWANAFUNZI BORA MAKERERE

Ni msichana wa Kitanzania ambaye amekuwa miongoni mwa wanafunzi bora kabisa waliohitimu katika Chuo kikuu cha Makerere. Jamani huyu naye ni shujaa wa kuipeperusha bendera ya Taifa letu.

Anaitwa, JOSEPHINE SERUHERE, ni vyema msome hapa na muone ni vipi katutoa kimasomaso.