My Blog List

Thursday, March 26, 2009

JINSI TANZANIA INAVYOMOMONYOLEWA NA MAFISADI

Huwa nasikia kelele kuwa mafisadi wamezidi nchini ila kwa haya ninayoyasoma katika vyombo vya habari basi hali ni mbaya sana. Kwa mfano eti serikali ya JK kumbe inashikwa na familia tisa (9) tu; huwezi amini lakini habari ndio hiyo. La kushangaza zaidi eti hata raisi Kikwete na serikali kujisifu kuwa uchumi ni mzuri kwa sasa kupitia Mkutano wa IMF hivi majuzi kumbe ulikuwa uzushi mtupu.

La kushangaza zaidi, ni kule kuendelea kumkumbatia na kumwacha katibu mkuu wa baraza la mitihani necta kubakia katika madaraka yake huku kazi na utendaji mzima ukiwa umepotea njia. Hebu shangaa eti hata vyeti vinaandikwa kwa makosa na hakuna mtu anayeguswa, hivi huyu mama ana egemeo gani pale? Mwisho kabisa inayonivunja mbavu na ninaisubiri itokee ni hili la kuwa kumbe uchaguzi ujao Mafisadi watatupa raisi.

OBAMA KUSABABISHA MKANGANYIKO UGANDA

Uganda ina wanajeshi 20,000 huko nchini Iraq; na kwa mpango wa Obama kuwaondoa askari wa Marekani siku za karibuni kunatishia hali ya usalama wa Uganda pindi askari hao wakilazimika kurejea. Kwa hali hii na huu mdororo wa uchumi, nchi ya Uganda inatarajiwa kukumbana na fedhaha katika uchumi wake siku za karibuni.

MENGINE YA KIANA NCHINI UGANDA MWEZI MARCH:
1. Raisi Museveni alidhihirisha kuwa serikali ya Uganda ni serikali ya demokrasia ya kiundugu kwani baraza la mawaziri limejaa kuanzia mke, kaka, mkwe n.k. Yaani kati ya waganda millioni 30, ni lazima mke wake awe waziri.
2. Naye Padri wa Kikatoliki, Fr. Simon Lokodo aliamua kuitoroka mimbari na kujiunga na siasa kwa kukubali kuwa waziri katika serikali ya Museveni. Amevunja sheria kuu ya kanisa (Canon Law) inayokataza kujihusisha na kanisa.
3. Pia ni vyema watu tuwajue wanawake 50 bora nchini Uganda kwa mwaka 2009
4.