My Blog List

Thursday, November 29, 2007

MALKIA ALIVYOFURAHIA UGANDA

Leo nataka tuone ni wapi Malkia Elizabeth alilala na ni jinsi gani aliandaliwa na kufurahi maisha ya kiafrika alipokuwa nchini Uganda.

KAMATI YA MADINI--NI SARAKASI ZA KISIASA ZISIZO NA TIJA SANA

Katika makala yangu ya mwezi September, tarehe 9, mwaka huu,katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili: “Bunge letu ni jumba la Sanaa”, ukurasa wa 12—13 , nilieleza kuwa demokrasia ya Tanzania ni ya kipekee duniani na kusema hivi: “kwa misingi kwamba tuna serikali isiyozingatia mihimili mitatu: Watawala, Bunge na Mahakama. Tanzania ya leo, serikali inaendeshwa kwa mihimili miwili: watawala na mahakama.” Hapa nilionesha wasiwasi wangu jinsi gani Bunge linafanya kazi ya kubariki na kuisemea serikali (rubber stamping) mijadala ya serikali badala ya kuihoji.

Hii niliona kama chanzo cha Bunge, kupitia wabunge wengi (majority) wa CCM walivyohakikisha wanaizima hoja ya Zito Kabwe na kumfungia kama adhabu kwa kile walichodai ni uzushi na utafutaji wa umaarufu kirahisi (cheap popularity).

Leo nataka niendelee nilipokomea kwani kutokana na mada ile ile ya Zitto Kabwe, rais Kikwete kaja na mpya. Kuunda kamati ya raisi kuchunguza ama kuipitia mikataba ya madini ni jambo zuri japo ninapata wasiwasi na utashi wa kweli wa hatua yake. Yaani raisi kama mkuu wa mhimili wa utawala na pia sehemu ya Bunge, ni wazi maamuzi ya awali ya kumuadhibu Zitto hayakuanzia tu kwa wabunge bali yalipangwa na raisi pia kupitia baraza la mawaziri, alafu waziri mkuu akawafunda wabunge wa CCM na maamuzi yakawa jinsi ilivyokuwa.

Mpango mzima wa kuzima madai yale ulishindwa na ukaleta matokeo isivyotarajiwa (backfire) na ikadhihirisha aibu kubwa ya kifikra kwa wabunge wa CCM na serikali kwa ujumla. Raisi anapong’amua hili alafu anawageuka wabunge baada ya kuwaaibisha kwa kuwashurutisha wafikiri visivyo. Ni kichekesho kikubwa; hebu fikiri Bunge letu limejaa wasomi, maprofesa, madaktari wa falsafa lukuki wa fani mbalimbali. Ni hatari kwa nchi kubwa kama yetu yaani mafanikio yote haya ya kitaaluma hawawezi kufikiri sahihi wala kusoma alama za nyakati.

Ukiacha hilo, raisi anajaribu kukiuka ahadi yake ya Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya. Raisi anaturudisha kulekule kufanya mambo kwa mazoea kitu ambacho amekuwa akikipinga. Uundwaji wa tume ya raisi wala si ya Bunge unanifanya nianze kukosa imani na raisi kwa hili. Swali: Inakuwaje Bunge, linaamua kufanya kazi ya mhimili wa watawala na kuacha wajibu wake wa kuhoji au kuchunguza madai halali ya Zitto kwa kisingizio cha Spika eti tungepoteza pesa bure baada ya kupoteza zile za tume ya madai ya Mengi awali. Pili, hivi hii tume ya raisi ya leo hii haitumii pesa?

Wajuzi wa masuala ya kiuchunguzi wanasema tume ya raisi haina meno kisheria kama ile ya kibunge. Ni wazi raisi anajaribu kutuchezea mchezo wa kisiasa katika kujaribu kuifuta ile kashfa ya Buzwagi. Hoja ya Kabwe ilikuwa juu ya uvunjaji wa taratibu kusaini mkataba wa Buzwagi kule hotelini Churchil. Raisi kaiteka nyara ile hoja na akageuza kuunda kamati kuchunguza mapitio ya mikataba yote ya madini. Hapa nashangazwa na utashi wa kupambana na ufisadi kama ni kiini macho tu. Najiuliza: hivi zile juhudi zote sa Spika na Wabunge wa CCM kutumia kanuni halali za Bunge na kuzima kwa msisitizo mkubwa hoja ya Buzwagi zilikuwa za kuwalinda akina nani?

Kuna harufu ya rushwa hapa, kwani kama tunapitia sheria zote za madini basi labda tunataka kuondoa akili ya watanzania wote kutoka Buzwagi na kuzika madai ambayo Spika ama kwa utashi wake ama kwa maagizo hakutaka kabisa iundwe kamati ya Bunge.

Hata hii kamati ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa Richmond inatia wasiwasi sana juu ya utashi wa kweli kama upo. Ukifikiri sana unajiuliza: kwanini imeundwa leo hii na si wakati ule ambapo ilipingwa kwa nguvu zote? Hata taasisi nyeti ya uchunguzi wa rushwa (Takukuru) ilishaisafisha Richmond lakini mara tunaona mabadiliko ya bunge letu (U-turn) na sasa bunge linakubali kamati ya Bunge iundwe. Hapa nina wasiwasi sasa wahusika wameshaandaa nakala-vielelezo mpya za kufuta ushahidi wa rushwa na maadam wameshajihami basi wana hakika Kamati ya bunge itawakuta ni wasafi.

Jambo lingine kwenye hii kamati ya raisi kupitia sheria za madini: vipi miongoni mwa wajumbe wa tume ya raisi ni wabunge wawili wa CCM ambao kwa nguvu kubwa walipiga makelele kwa kupiga meza katika kuzima kabisa hoja ya Buzwagi? Kama hawakuona kabisa utata katika mkataba ule hivi kweli ni watu wenye utashi wa kuchunguza mikataba ya madini? Hapa ndio pananitoa imani na uamuzi huu wa kuunda kamati ya raisi.

Wasiwasi wangu mwingine, nakumbuka wakati anaongea na Sauti ya Amerika (VOA) akihojiwa na Shaka Sally kupitia kipindi cha Straight Talk Afrika kutoka Chamwino Dodoma, raisi alisema mikataba yote ya madini imeshapitiwa na sasa inaendana na viwango vinavyokubalika kimataifa. Nakumbuka alizungumzia mambo kama ya mirabaha inayolipwa na kampuni za madini na hata lile suala nyeti la mgawanyo wa kodi wa asilimia 3% kwa 97% na akasema sasa ni 30% kwa 60% kama sijakosea kukunukuu. Sasa kuunda kamati kupitia tena sheria za mikataba kunamaanisha alikuwa anadanganya? Nilitegemea raisi aunde kamati kuchunguza Buzwagi—kiini cha madai ya Zitto. Sasa hii upitiaji wa mikataba ambayo raisi amewahi kusema imepitiwa na wataalamu ni nini tena?

Hapa raisi mimi binafsi nadhani tumwamini kwa maamuzi yake japo utashi unatutia wasiwasi. Nampa imani ya kidhahania tu (benefit of doubt) na tusubiri tuone kweli kama tume yake itapendekeza nini na kama atafanyia kazi mapendekezo hayo. Mambo haya ya kufunikafunika ni mbinu za kisiasa zilizopitwa na wakati. Nina wasiwasi raisi hajui kuwa nchi yetu ipo katika kipindi cha kiongozi mkuu kufanya maamuzi magumu la sivyo umaarufu wa chama na serikali yako utagharimika sana. Ni wakati wa “Utawala Bora” kuachiwa ufanye kazi. Mihimili mitatu ya dola isipoachiwa ifanye kazi kwa kujitegemea bila kuingiliwa na watawala basi ndio tunashuhudia usanii kila kukicha hasa tangu awamu ya nne ianze.

Ule wakati wa kuwachukulia watanzania kama watu wa mawazo finyu (gullible) umekwisha. Ni wazi kama rais na chama chake hawakutaka kamati ya bunge kuchunguza Buzwagi ila anaamua kuunda kamati chini ya mamlaka yake. Lengo linaweza kuwa ni kuweza kudhibiti uchafu wote utakaoibuliwa usishughulikiwe kwa mujibu wa sheria. Tume aliyoiunda inawajibika kwake na wala haina nguvu za kisheria kuwezesha mapendekezo yake yafuate mkondo wa kisheria iwapo itathibitika kuna haja ya kuwawajibisha vigogo fulani.

Ndio maana ikiwa tume itawakilisha ripoti kinyume na matarajio ya Raisi, tusishangae yale yaliwahi kumkumba Jaji Robert Kisanga wakati wa enzi za uwazi na ukweli yakamkumba pia Jaji Mark Bomani. Binafsi nimeitafakari hatua ya kuunda kamati ya raisi na si ya Bunge kama sarakasi za raisi katika kufunika kashfa ya Buzwagi. Ni dhihirisho jinsi Bunge lilivyotekwa na mhimili wa watawala (executive’s hijack of the legislature). Raisi anafanya kila juhudi kuendeleza hali tata iliyopo (Status Quo) yaani kuzuia mabadiliko ya kifikra na hata jinsi mpya ya kiutendaji ili kuikwamua nchi yetu katika umasikini wa kujitakia.

Kwa mwendo huu kama viongozi wa bara la Afrika hawataki kuruhusu mfumo wa utawala bora ufanye kazi basi katu haisaidii juhudi za kujikwamua na umasikini. Haya ndio yananifanya niwe na wasiwasi na tume ya raisi; hebu tusubiri tuone kama itakuwa na tija. Lakini ningekumbusha mbona tunaizika kashfa ya Buzwagi? Hii ni sarakasi ya raisi; je itafanikiwa? Tusubiri tuone.

Saturday, November 17, 2007

LEO JUMAMOSI

Profesa Mazrui kaandika juu ya mapambano ya mwafrika; na pia kama kawaida napenda sana kujijuza mambo ya nyakati za Iddi Amin.

Wednesday, November 14, 2007

RAIS KIKWETE ADHIHIRISHA JINSI BUNGE LISIVYOJALI MASLAHI YA NCHI

Sijui niuite ni ukinyonga au niseme nini ila kama kuna siku rais Kikwete kanichekesha ni pale niliposikia kuwa ameunda tume ya kuchunguza na kupitia mikataba ya madini. Mshangao ulinipata baada ya kusikia eti na mheshimiwa Zito Kabwe nae ni miongoni mwa wajumbe wa tume. Kwangu hii ilikuwa ni faraja kusikia hili la kumjumuisha mpinzani ndani ya shughuli kama hii. Zaidi kumjumuisha Zito Kabwe lilinichekesha sana.

Zitto Kabwe ndie mwaanzilishi na mpiga filimbi mkuu aliyethubutu kujitoa mhanga na hatimaye kupewa adhabu ya kutohudhuria kikao cha Bunge kinachoendelea sasa ili kutaka tume ya Bunge iundwe kuchunguza haya rais anayoyaundia tume. Kama mtu unafikiri na si kimgandomgando, unapata hisia kuwa raisi Jakaya Kikwete amelipiga bunge mwereka kimawazo. Ni katika msingi huu Bunge letu hasa vinara wake: Waziri Mkuu na Spika pamoja na wabunge wote waliounga mkono Zitto apewe adhabu wanafanywa ni wajinga ajabu.

Saturday, November 10, 2007

MSONGO WA MAWAZO TATIZO KUBWA UGANDA

Jamani watu wengi wana msongo mkubwa w a mawazo au wana tatizo la kisaikolojia; Uganda eti watu wengi wamechanganyikiwa. Pia ziara y a Museveni Marekani imekuwa gumzo juu ya uswahiba m p ya na Joji Kichaka.

MUSEVENI NA UTUNZI WA VITABU

Museveni ni rais mahiri kwani huwa anaandika vitabu na hata makala magazetini. Karibuni kaandika kitabu na kimeshangaza kidogo kimtazamo. M useveni anaaminika kama kiongozi bora ila kuna haja ya mabadiliko kwa mujibu wa jaji maarufu. Pia tujiulize je Big Brother ni muhimu sana?Pia benki zimeanza kuhimiza ndoa unazijua?
Pia tunajuzwa zaidi ni vipi Iddi A min alivyowapendelea watu wa kabila lake.

Kumbe John Garang aliuawa na serikali ya Uganda? Kumbe pia uzazi bila mpango ni chanzo cha Ukimwi kuenea kwa kasi? Mwisho kabisa hii ni kali yaani kuna kesi kubwa ya aina yake nchini Uganda.Unamjua mtuhumiwa wa wizi wa f edha za Gl obal Fund?Na ugonjwa wa m araisi wa Afrika je?

Monday, November 05, 2007

KWANINI VIGOGO WANAPENDA HOSPITALI ZA MAJUU?

Ama kweli bongo kuna vituko, huwezi amini eti madaktari wanaweza kosea namna hii; mambo kama haya yanawezekana bongo tu. Inawezekana ndio maana vigogo wanaziogopa hospitali za bongo.

Saturday, November 03, 2007

IDDI AMIN MZIMU BADO HAI

Kwanza kabisa leo tukumbushane juu ya Iddi Amin; alafu tutizame waasi wa LRA Uganda wanavyojaribu kujirudi.
Alafu kuna hili gonjwa la kisukari linakuwa sugu, hali ni mbaya Uganda.

Na kwa wale mapedeje, mnajua gharama zake?