My Blog List

Wednesday, May 30, 2007

RUSHWA UGANDA

Inasemekana eti Serikali ya MU7 iliingia madarakani 1986 ikiwa na mawazo ya kimapinduzi ambayo sasa yanadaiwa yamepotea njia.Huko Uganda kashfa kubwa ya rushwa imesababisha mawaziri vigogo kuwwekwa ndani, ni kisa kinachofanana na kile cha mheshimiwa Dito kupewa dhamana kwa kesi ya mauaji.Kisa hiki ni mfano hai wa siasa za kulindana zinapofika ukingoni.

Monday, May 21, 2007

MAUAJI YA SUMU KWA WANASIASA

Sasa waganda wameanza kuuana kwa sumu, siasa si mchezo.Kama ulishasikia mwanasiasa anayeogopeka ndiye huyu Uganda.
Uganda ni nchi iliyojaa vifo visivyoelezeka.
Wale wajasiriamali
Leo kwa wale wanasikiliza BBC Swahili, basi kila mara utamsikia msemaji wa jeshi la Uganda,ni muwajibikaji na msomi wa kileo jeshini ambaye hakusita kuandika makala juu ya kifo cha yule askari aliyefariki majuzi bila woga au mficho, ndie huyu Meja Kulayige. Mwisho kuna kashfa kubwa ya fedha Uganda tena.

Saturday, May 12, 2007

Harusi za gharama muhimu?

Wale wanaooa je mnataka harusi ya gharama?

JANET MUSEVENI KATIKA KASHFA YA GLOBAL FUND

Nchi ya Uganda imeshuhudia kashfa kubwa ya wizi na matumizi mabaya ya fedha za wafadhili hasa zile za fuko maalum(Global Fund). Iliundwa tume kuchunguza na matokeo yake ni kwamba hata mke wa Rais anahusika.Ni kashfa kubwa kwani inawahusu askari jeshi wa vyeo vya juu ambao ni vigumu kwa Museveni kuwagusa.
Upande wa michezo, timu ya taifa ya soka hapa tayari inaanza maandalizi dhidi ya Nigeria.Tanzania kwa sasa maneno mengi juu uteuzi wa timu hapa chama cha soka kimejipanga vizuri sana.Kwenye mambo ya kisiasa zaidi hebu soma juu ya ule msemo wa kiingereza usemao: Like Father like.....

Saturday, May 05, 2007

WIKI HII UGANDA

Ni vyema tuanze na juu ya nini chanzo cha kifo cha Brigedia maarufu na kijana aliyefariki Uganda siku za karibuni manake inadaiwa labda ni sumu.
Tuachane na kifo na tuendelee na siasa juu ya utawla bora.
Na mwisho eti mtoto wa Iddi Amin kaanzisha wavuti kuweka kumbukumbu za baba yake. Ila kama watu wanafikiri JK wa bongo ni rais wa karibu na watu Museveni ndio usiseme kwani ana kawaida ya kutembelea vyombo vya habari yaani redio za FM na kufanya malumbano ya simu na wtu kdhaa.

NOBLE MAYOMBO-ASKARI SHUJAA UGANDA

NEWS




Uganda mwanzoni mwa wiki hii ilimpoteza askari, mpiganaji na msomi mahiri kabisa.Noble Mayombo ni wazi alikuwa ni kati ya vijana wanaoaminiwa sana na Rais Museveni.Jamaa kafariki baada ya kuugua ghafla na inasemekana huenda kategewa sumu.Pia ni kwamba alikuwa kati ya maafisa wanaoeneza utawala wa ubabe wa Museveni na sumu yake katika ukanda mzima wa maziwa makuu.
Ni wazi alikuwa na maadui wengi saana na alikuwa na msimamo thabiti dhidi ya wapinzani akiamini mateso(torture) kama njia muafaka dhidi ya wahalifu na wapinzani kama Kiiza Besigye.Licha ya uaskari alikuwa pia ni katibu mkuu wa wizara ya ulinzi.Mengi yatasemwa lakini kashaondoka ila lazima tumkumbuke, kwani jamaa wengine wanadai hivi mashujaa tunawakumbukaje?
Jamaa kaagwa kiana yaani mwili wake kuwekwa Bungeni, mie nauliza hivi shujaa kama huyu mbona hajulikani njee ya Uganda?Mie kama msikilizaji wa redio za Uganda niliwahi kumsikia akifanya malumbano na pia nukuhu kadhaa zinamwonesha kama mtu mwenye kujidai sana; na kweli nadhani alikuwa mahiri japo nafikiri alikuwa akitetea tu utawala.
Jamaa kama kawaida mtu akifa, mkewe kamsifia kweli!
Andrew Mwenda ni mwandishi maarufu wa habari Uganda anamwelezeaje huyu bwana?Pia kifo hiki kinatukumbusha ni nini maana ya maisha.
Mwisho yuko Mhindi anatukumbusha juu ya umuhimu wa wahindi katika uchumi wa afrika.