My Blog List

Saturday, April 28, 2007

Thursday, April 26, 2007

UTAWALA WA KIBOKO UGANDA

Makamu wa Rais wa Uganda bado anaandamwa na kashfa ya uzinzi. Uganda imeanzisha kikosi maalum: KIBOKO SQUAD kutokana na kuongezeka kwa fujo na maandamano kila kukicha dhidi ya maamuzi dhalimu ya serikali.Watu wanachapwa viboko wakijaribu kuandamana.
Uganda pia wiki iliyopita yule bondia maarufu wa nchi hilyo alirefjea nchini humo.

Baada ya uchaguzi kule Nigeria Raila Odinga wa Kenya anaeleza woga wake juu ya nguvu kubwa alizzonazo Rais wanchi na athari zake za uchaguzi ujao.

SAYARI NYINGINE KAMA DUNIA

Wanasayansi wamegundua sayari mpya inayoaminika ina maisha ya viumbe hai kama dunia. Huko Uganda pia yuko jamaa mmoja mchungaji mwenye kipaji kwelikweli, mjue Sempa.
Nigeria imempata Rais mpya kwa uchaguzi uliolalamikiwa sana, je nini kitarajiwe?

Raisi Museveni wa Uganda kasababisha sakata kubwa la uuzaji wa msitu wa asili kwa Wahindi.Hebu tuujue undani wa tatizo hili la MABIRA FOREST kwa dhati.Wengine wamependekeza kuwe na MAPINDUZI YA SUKARI.Iko pia barua ya wazi kwa rais Museveni kutoka kwa mwananchi wa kawaida.Yapo maoni ya Mhindi juu ya dhahama hili na anajaribu kufananisha na hali ya wakat wa Iddi Amin.Mwingine katupa kanuni ya kubalansi mazingira na uchumi bila athari.

Tuesday, April 10, 2007

UZINZI HALALI UGANDA?-MAHAKAMA

Museveni hatimaye kaanza kuzungumzia mipango ya kuondoka.
Mahakama ya Uganda imefafanua juu ya sheria ya ukahaba au uzinzi kwa mwanamke na mwanaume, hata hivyo bado akina mama wengi wa Kampala wanataka talaka waachane na mabwana zao.Amanya Mushega, katibu mkuu wa EAC wa zamani anazungumzia juu ya utawala bora. Hotuba yake inatoa historia ya siasa za Uganda.
Ule msitu wa Mabira ni kielelezo cha rushwa nchini Uganda kwa miongo mingi anasema Andrew Mwenda.

Saturday, April 07, 2007

MZUKA WA IDD AMIN BADO

Watu wanamjua Iddi Amin kama mtu mnyama kuwahi kutokea Afrika. Lakini ni lazima tumtizame huyu bwana kwa undani hasa kuwa hata waliomfuatia ni wanyama pia, je unajua kwanini? Tunaambiwa eti serikali ya Museveni ni tishio kwa wapinzani kama alivyokuwa Idi Amin.
Amanya Mushega alikuwa katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki, yeye anapinga kuuzwa kwa msitu wa Mabira. Tunakumbushwa jinsi vyama vya siasa visivyo na nidhamu. Na je nini chanzo cha matatizo ya Afrika, Museveni alishasema ila leo hii anavunja aliyowahi kunena.

HERI YA PASAKA

Ni Pasaka hivyo hatuna budi kujua sikukuu hii husheherekewa vipi na jamii mbalimbali duniani?
Huko Uganda bado kasheshe la uuzaji wa msitu wa Mabira linaendelea.Limesababisha mfalme wa kabila la Baganda Ronald Mutebi kuja juu na kukataa uuzaji huo ndani ya Mahakama ya Kikatiba ya Uganda.Hii inasababishwa pia na tishio la hali ya hewa kuchafuka duniani. Wanasiasa ni watu wa ajabu kwelikweli, Museveni aliwahi kusema atalinda mazingira lakini leo hii anayabomoa kwa kuuza msitu huu.
Ujumbe wa pasaka eti Mbeki.