My Blog List

Friday, December 22, 2006

MASLAHI YA NCHI NI ZAIDI YA SIASA NA HISIA ZA WATU

Unaposikia tofauti kati ya siasa na maslahi ya nchi mfano mzuri uko hapa kwenye maziwa makuu.
Pia kuna hili la kalenda ya uendeshaji wa ligi ya soka.
Pia huko Kenya rais Kibaki atakuwa Mombasa kama kawa.

Thursday, December 21, 2006

HAKUNA HAJA YA MIKOPO ELIMU YA JUU-PROF: MAAMDANI

Wakati wabongo tunalia na JK kuhusu mikopo ya elimu ya juu, yule profesa maaarufu, Maamdani kachapisha kitabu akisema eti serikali isilipie ila wote tulipie elimu

Tuesday, December 19, 2006

JK NA JINAMIZI LA CCM NDANI YA MWAKA MMOJA IKULU

JK sasa anaanza kuona ukweli halisi wa bongo kuwa tatizo liko kwenye CCM. Hili ni jinamizi ambalo JK ana kazi ngumu kuliondoa manake ncchi imeoza na itagharimu Taifa sana kuweza kuondoa hayo ambayo JK kakemea jana.

SALAM ZA CHRISTMAS

Tunasherehekia Krismas soma jinsi makasisi wa dini mbalimbali(mapadiri na wachungaji na mashehe pia) walivyobadilika siku hizi na tunakkumbushwa je Yesu wa wakristu angezaliwa leo ingekuwaje Afrika?Alafu nataka uone ni jinsi gani wabunge wa Afrika hasa Uganda walivyo na ulafi na mapenzi na MABENZI na si wananchi, yaani wanatishia serikali pale inapotaka kuwakata usawa.
Mwisho, ona jinsi Jaji Kiongozi Uganda hisia zake juu ya utawala bora.Alafu mkuu wa Jeshi la polisi Uganda naye anaamua kumjibu na kumkosoa ikibidi Jaji Kiongozi, patamu hapa.
Alafu wajue watu kumi waliotingisha Uganda mwaka huu.

Friday, December 15, 2006

MKE WA MUSEVENI KATIKA UGOMVI KUMTETEA MUMEWE

Mke wa rais Museveni ambaye ni mbunge jana inasemekana karushiana maneno makali na mwanamama mmoja wa shoka wa chama cha upinzani katika kile kinachoonekana kutetea rekodi mbovu ya mumewe ndani ya bunge.
Alafu unajua kwanini maprofesa wa Makerere wamegoma? Soma haya.

Wednesday, December 13, 2006

UDIKTETA-SIRI YA KUISHI MUDA MREFU

Eti madikteta hawafi mapema, tunahimizwa tuwe majitu korofi na dhalimu ili tuishi muda mrefu.

Thursday, December 07, 2006

JK AIGE KUTOKA KWA CALDERON WA MEXICO

Kama kweli Tanzania inapenda maendeleo tunahitaji kiongozi kama huyu aliyechaguliwa huko Mexico majuzi. JK angekuwa namna hii na akatekeleza basi tunaweza kufanikisha "Maisha bora kwa kila Mtanzania".
Vinginevyo JK anatania tu.

UHURU BONGO--BONGE LA PATI SAWA AU DHIHAKA?

Kama mtanzania sina budi kujumuika na watanzania wenzangu kuadhimisha siku hii ya miaka 45 ya uhuru wa Tanzania bara(Tanganyika).Huu ni wajibu wa mzalendo yeyote kutathmini je uhuru wetu umeleta tija kwa watanzania wote au kwa kukundi fulani ndani ya jamii tu?Sisherehekei manake kwa hali ilivyo si muafaka kwa hili bali ni wakati wa kujiuliza kwa nini tunaendelea kuharibu uchumi wetu namna hii?Sherehe tuwaachie wanaoona matunda ya uhuru kama akina JK na Ngoyai: hawa kwao hakuna tatizo la umeme, maji wala usafiri au barabara mbovu. Kwao wanazo njia mbadala kutatua haya.
Nimefuatilia sherehe za uhuru leo kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) kwani wakati ndio sherehe inaanza hawa jamaa wa Tanesco wakakata umeme alafu ikaw ndio mwisho wa kuangalia Runinga yangu.Matanzgazo ya RTD hayasikiki vizuri nashangaa kwanini RTD wasiweke mtambo wa FM manake hizi FM radio nyingi ni muziki kwa kwenda mbele utadhani siku ya leo ni sawa na zingine. Ni Radio Free Afrika ya Mwanza na Sauti ya Injili ya Moshi angalau leo wamekuwa na vipindi kuwahoji watu ambao walihusika na uhuru wetu wakati ule na wametoa mawazo murua kweli. Nakwambia tukio hili hapa Moshi si la muhimu kama siku ya jumapili au sikukuu ya Idd El Fitri kwani siku hizo umeme ni bwerere.Hasira imenishika kwani baada ya sherehe kumalizika hawa jamaa wanawasha umeme, nakwambia Tanesco hapa Moshi hawajui uhuru kabisa. Hayo tuyaache, ila JK hotuba yake ilikuwa nzuri nampongeza sana. Ila aliangalia tu mafanikio nchi iliyojipatia tu tangu 1961, ameacha kuzungumzia matatizo kama haya ya Umeme.

Nami naona nieleze kwa ufupi japo ninafikiri nini siku hii:

Mtizamo wangu unatia wasiwasi sana kama kweli tumefikia mafanikio ya dhati kulingana na kipindi cha miaka 45. Naanza na sekta ya barabara tumefeli kabisa. Bado hatujaweza kuunganisha nchi yetu kwani tunalazimika kupitia Kenya kusafiri kutoka Arusha kwenda Mwanza, Bukoba au hata Kampala.

Pili bado tunakumbwa na njaa kila mwaka ilihali tuna ardhi, mito kibao kuwezesha kilimo cha umwagiliaji. Ukija kwenye maji ndio usiseme kabisa. Hakuna maji kunywa ya kutosha hata katika miji kama Dar es salaam, Arusha na hata Mwanza.
Huwezi kuamini nchi yenye umri wa miaka 45, haina umeme wa kuaminika na kutosha angalau mautmizi ya majumbani achilia mbali viwandani. Viongozi, yaani wanasiasa hawana utashi wowote kwa maendeleo ya jumla ya nchi. Maslahi binafsi yamewekwa mbele kuliko uzalendo: kwa mfano, nchi inagenishwa kwa kubadilishana/bei poa kati ya watu fulani ndani ya tabaka tawala(elites) na si kwa maslahi ya mtu.
Ukija kwa watunga sheria(Wabunge) ndio basi tena. Bunge limekuwa jamvi la kila mtu siku hizi hata wendawazimu au kwa maana nyingine mbumbumbu kielimu nionavyo kutokana na matendo yao.Elimu si tija kwa mtu kuwa mbunge au diwani. Nidio maana bunge letu ni taasisi ya kubariki mambo yasiyo na maslahi kwa Taifa ila Chama(CCM) na yale ya binafsi. Chama tawala kimelimeza bunge na kutupeleka kuzimu kiuchumi. Tumefika mahali mtu akiheshimu taaluma katika kusimamia au kuamua mambo ya kiuchumi na mengine ya msingi kama hayo anaonekana mwehu na si mwenzetu. Hii ndio miaka 45 ya uhuru tunayosherehekea. Hili ni lazima tulitafakari la sivyo uhuru unakuwa hauna maana.
Kwa robo mwaka sasa nchi iko gizani, hakuna umeme na viongozi na wahusika wetu hawajali kabisa. Ufisadi na kulindana ndio umetufikisha hapa tulipo na viongozi wahujumu hawaguswi bali wanahamishwa kutoka idara au wizara moja hadi nyingine kuendeleza uharibifu. Vipaumbele vyetu ni vile visivyo; viongozi wetu wamebakia kusafiri kutembeza bakuli kwa wafadhili na kuhimiza uwekezaji katika nchi isiyokuwa na umeme wa kuaminika bila aibu. Kiongozi mkuu anadiriki kusema tatizo la umeme limerithiwa kutoka serikali iliyopita bila kung'amua alikuweko ndani ya serikali hiyo.
Kisiasa, nchi imebaki hoi kabisa; vyama vya upinzani viko hoi kabisa na havionekani kuchukua hatua madhubuti kutia changamoto kwa CCM inavyoboronga. Haya yakiendelea, CCM chini ya Makamba imebakia kuwarubuni wapinzani makini kurejea CCM kama ndio kipaumbele. CCM haitaki changamoto, kwake kuwa mpinzani ni uadui, si uzalendo kwa nchi. Kweli hapa hatutaelewa wapi tunakosea kama tutaendelea hivi na ndio maana bado tuko nyuma maeneo mengi. Demokrasia yetu ni kama vile "maonesho kwa wafadhili"(show-off) na sio demokrasia ya dhati.
Viongozi wetu kama vile Lowasa na Makamba wanaongoza kwa sera kongwe za kihafidhina. Hili ni tatizo la viongozi ndani ya chama tawala, serikalini na hata vyama vya upinzani. Tunahitaji kizazi kipya cha uongozi nadhani ili tuendelee. Hata hivyo, kama Taifa tumefanikiwa kubaki na umoja wa kitaifa kitu muhimu kwa nchi yeyote.
Amani tuliyonayo ni lazima tuikuze kwa kuziunda upya taasisi za kidemokrasia katika utawala ili muongo ujao tupige hatua kwa haraka na si kama miaka hii 45 iliyopita. Katiba ni lazima iangaliwe upya ili miundo ya mihimili mitatu ya dola ifanye kazi inavyopaswa kwa uhuru na si kama sasa kwa kulinda maslahi ya chama tawala. Hii imefanya kwa mfano bunge letu kubaki kama muhuri wa udhalimu "rubber stamp" wa serikali mara kwa mara.
Mwisho, ingawa wenzetu wa magharibi iliwachukua muda mrefu kufikia mafanikio ya demokrasia, sisi isiwe kisingizio, kwani dunia ya leo mambo yamerahisishwa ni lazima tuendelee haraka. Nitoe rai: Tuna wasomi wengi wa kila aina Tanzania ila wote wamefungwa jela ya nafsi zao(conscience) na wamekuwa bendera fuata upepo(sycophants) mbele ya wanasiasa wa chama tawala. Ujasiri unahitajika kwa wasomi wa nchi hii la sivyo kama nchi tutaendelea kusherehekea uhuru wa wachache kama tunavyofanya leo hii. Kwani mantiki ya nchi huru sidhani ina maana kwa watanzania wengi wa kama kule vijijini pembezoni mwa nchi hii. Na kwa akina JK, Ngoyai na Makamba: kumbukeni turuhusu changamoto ndani ya chama na hata serikalini kwani ikiwa tutafanya hivyo hatutaona mikataba ya kijinga kama hii ya IPTL, Richmond, Usiri wa biashara ya mihadarati na mengine mengi ambayo hayasemwi kwa kuogopa kumkosoa bwana mkubwa.

Wednesday, December 06, 2006

KAGAME-MUNGU MTU- ASHTAKIWE TU

Naiangalia hali ya Rwanda kama ni tatizo ambalo waafrika hatuwezi kulitatua kwani kihistoria ni vigumu. Sina imani sana na mahakama ya Arusha kwani naiona kama mahakama iliyoundwa na washindi wa vita(RPF) ili kuwahukumu washindwa.
Ndipo hapa ninapokuwa ninamuunga mkono huyu jaji wa kifaransa kutaka pia Kagame ashtakiwe. Sidhani kuna suluhisho la kiafrika, ila naunga mkono juu ya nia ya mficho ya Ufaransa katika sakata hili. Pia nionavyo tutarajie Rwanda yenye matatizo sana hapo baadaye kwani Kagame inasemekana ni kiongozi Mungu mtu.Tatizo letu waafrika ni kutokupenda kusema ukweli na kama tutaendelea na uwongo huu wa Kagame hakuna maridhiano Rwanda.
Lakini pia ni lazima tujue pande zote mbili zilihusikaje katika kile kinachoitwa ukombozi wa Rwanda?Kwa mfano, picha halisi ya ushiriki wa Kagame na Habyarimana unaweza kuisoma na kupata hali halisi hasa hii makala ambayo mwandishi anao uelewa sana wa mambo ya Rwanda.

Tuesday, December 05, 2006

BESIGYE ALIVYOMNYANG'ANYA MUSEVENI MKE

Pamoja na kufuatilia habari za wanasiasa kadhaa ni vyema pia wakati mwingine tujue habari zao binafsi. Leo nataka nieleze habari za kiumbea ambazo niliwahi kuzisikia juu ya Museveni, Kiiza Besyige na huyu mwanamke wa chuma(iron lady) Bi Winnie Byanyima.
Inasemekana ugomvi kati ya Museveni na Besigye pia unachangiwa na kuibiana mabibi. Eti Bi. Byanyima awali alikuwa ni mtu wa karibu sana wa Museveni wakati wa vita ya msituni. Wakati huo Besigye akiwa kama daktari wa Museveni. Leo hii Bi. Byanyima ni mke wa Besyigye japo nakumbuka niliwahi kumsikia akihojiwa na redio moja Kampala na akadai kuwa eti Besigye ni mshirika wake tu(companion).
Wambeya wanadai eti siku waasi wa Museveni(NRA)wanaiteka na kuitwa Kampala, waliingia Kampala huku gari alilokuwemo Museveni likiendeshwa na Bibie huyu.
Hayo yote tisa, kumi leo hii Dr. Besigye kaamua kuyaanika yote yaliyojiri kule msituni na ni jinsi gani walikutana na bibie huyu.
Kama kawaida, Uganda ni nchi iliyojaa visa vya kisiasa vya kiume kweli si kama Tanzania, soma huyu mpinzani madhila aliyokwishapitia.

RAIS NA GAVANA UGANDA--WAWAKAMUA WALIPAKODI KWA BIASHARA BINAFSI

Mimi ni kati ya wasioamini adhabu ya kifo hata kama mtu kafanya nini. Ila nimeshangazwa sana na nchini Uganda hata katiba inaruhusu kama ilivyo pia kwetu Tanzania. Lingine ni hili la Rais Museveni na gavana wa benki kuu wameamua kutumia pesa za wali pakodi kumsaidia mfanyabiashara mmoja asifilisike.Ila inasemekana huyo mfanyabishara ni jamaa tu anasimamia shughuli za mzee.
Kama kawaida yangu napenda sana kujua inakuwaje watu wengine wanafanikiwa kimaisha wangali wadogo?