My Blog List

Saturday, November 26, 2005

NITAKAMATWA SIKU YOYOTE KUANZIA LEO

Nataka niseme kwa sasa niko hatarini kukamatwa wakati wowote. Unajua kuanzia juzi serikali imepiga marufuku kuandika, kuzungumza juu ya Dr. Kiiza Besyige, mpinzani wa Museveni ambaye yuko lupango.Kama mnavyojua hapa kila kitu ni kijeshi tu kwa hiyo mkisikia nimetiwa korokoroni msishangae kabisa.
Lakini kabla hayo hayajanikumba labda niseme tu kwamba bado hali sio shwari. Jana Besyige kapewa dhamana bonyezahapa ila bado anabakia ndani ya lupango. Kujua zaidi hebu bonyezahapa. La kushangaza zaidi hapa polisi ndio hao hao wanajeshi na kuna wanajeshi wengi sana Kampala onahapa
Katika kuhakikisha uhuru wa kusema, kuandika na kutangaza unadhibitiwa, serikali imemteua mwanajeshi bonyeza kuongoza bodi ya gazeti la serikali-New Vision. Hii inatafsiriwa kama kuhakikisha hata gazeti la serikali linamchafua mpinzani yeyote na haliandiki habari njema kumhusu.
Kwa Museveni hii ndio demokrasia.

Friday, November 25, 2005

KISA CHA WA-TWAWALA WETU

Ile stori ya wa-twawala wetu wanavyowanyonya walalahoi inaendelea kudhihirika. Huko Kenya, rais Mwai Emilio Kibaki amelifuta kazi baraza la mawaziri.
Bonyeza hapa uone ni jinsi gani walalahoi wanavyonyonywa.Hivi kweli bara la Afrika ni masikini au tunatania?Mimi nashindwa kujua wala kuamini ila inanifanya niulize wenzangu: Kwa mfano jinsi serikali ya Tanzania inavyohangaishana na madaktari je ni kiasi gani kinatumika kwa wanasiasa wetu? Je ni busara kutumia mabilioni kwenye siasa na kuwasahau madaktari wetu?

Thursday, November 24, 2005

DALILI ZA UDIKTETA ZAJIONESHA JANA KAMPALA

Watu wanasema Museveni kawa dikteta; na leo nataka niwaoneshe haswa ni kwa vipi huyu bwana kweli ameamua kuitupa demokrasia kapuni.
Jana ile kesi ya mpinzani wake mkuu, Dr.Kiiza Besigye ilikuwa itajwe na kulikuwa kumepangwa maandamano makubwa ya wafuasi wake.Kinyume chake serikali ilitumia wanajeshi na kuwavisha nguo za polisi wakiwa na magari makubwa ya kijeshi katika kona mbalimbali za kampala. Soma hapa ujione mwenyewe udikteta unavyomea.

Wednesday, November 23, 2005

MKAPA ANAVYOSHAMBULIA WAZUNGU

Haya, leo Mkapa naye ameamua kuwachachamalia hawa jamaa wa magharibi. Anadai wanapokosoa nchi zetu wanaingilia sana mambo yetu kwa maslahi yao.SOMA

Tuesday, November 22, 2005

WIVU WA WAZUNGU

Eti wamarekani na waingereza wanashangaa kwanini China inawekeza kwa kasi Afrika?soma
Jamani huu sio wivu? Naomba tuelezane je China kuwekeza Afrika ni habari njema kwetu waafrika au balaa jingine?

JAMANI HII "THANKS GIVING NI NINI?"

Hii nataka mheshimiwa Ndesanjo asome na ikiwezekana anipe muangaza. Nasikia huko Amerika kuna hii sikukuu iitwayo: Thanksgiving, hebu niambie inamaanisha nini?
Joji Kichaka kong'oli hapa nimeona akitoa salamu za siku hii.Hapa ninaishi na Wamarekani miongoni mwao ni waalimu wangu basi siku tayari wameshaanza kutoa udhuru hawatahudhuria darasani. Ni nini msingi wa siku hii?

Monday, November 21, 2005

HATARI KWA UHAI WA GLOBU

Haya wanablogu jamani mimi sasa natishika. Hivi kama mmefuatilia huu mkutano wa vyombo vya mawasiliano ya kompyuta kuna habari sasa wa-twawala wanataka wadhibiti mitandao ya intaneti.
Sijui mnalionaje manake natishika sasa hapa.Kuna hatari habari zinazotokea huku zikadhibitiwa, tunaelekea wapi? Nimesoma habari bonyeza
nikashtuka sasa ule uhuru wa mawasiliano uko hatarini.Jamani tutuwaweza wa-twawala?

Sunday, November 20, 2005

MUSEVENI ALIPOCHAGULIWA TENA

UTANDAWAZI HATUWEZANI NAO-WATANZANIA

Rais anayemaliza muda wake amekuwa akisisitiza watu wenye mali Tanzania kukopa benki ili kufanya biashara.Hii ni hatua nzuri isipokuwa kama hakuna usimamizi mzuri wa fedha mambo yatakwenda kombo.
Siku za hivi karibuni ile kampuni ya mabasi Scandinavia soma imeingia katika malumbano ya madai na inavyoonekana mambo si shwari.Huwa nikija huku nasafiri na kampuni hii sasa nasikia inataka kufilisiwa. Jamani watanzania tunani?Tuna udhaifu wa kusimamia shughuli mbalimbali hebu tizama jiji la Dar limekuwa na mgawo wa umeme kwa mwezi sasa.Sio IPTL wala Netgroup Solution imekuwa jibu. soma
Tumekwisha.

Saturday, November 19, 2005

KITENDAWILI CHATEGULIWA

Rais Yoweri Kaguta Museveni hatimaye jana usiku alifanya yale yaliyokuwa yametawala vinywa vya wengi hapa Uganda kwa siku nyingi.Ametangaza rasmi kwamba atagombea urais soma tena baada ya kubadili katiba na kuruhusu agombee kwani alikuwa tayari katimiza vipindi viwili vya miaka 5.
Nilitaraji hili, ila nataka niulize hivi kweli kuna tatizo hata mtu akiitawala nchi yake kwa miaka 50?
Na kama watu, wanachama wa chama chako, tena chenye wafuasi wengi ndani ya nchi wakakusukuma ugombee, ni muhimu kweli kufuata utashi wako?
Hebu pitia makala moja soma hapa ambayo inazungumzia ni njia ipi Museveni ataifuata sasa alafu unaweza ukaelezea hisia zako.
Mimi ninabaki kumshangaa BEN MKAPA eti anaachia ofisi, mbona wenzake bado wamebaki?

EBO! MADAKTARI SI BORA KAMA WANASIASA.

Haya leo turejee Tanzania: somahapa kuna hii kasheshe ya madai ya posho za madaktari. Jamani mimi huwa nachanganyikiwa ninapoona daktari kasoma na akahitimu lakini hana mapato mazuri.
Ukipima kile wanachopata watawala wetu usiombe. Hasa wanasiasa, wabunge na madiwani ndio wanaopata pato kubwa sana. Naomba mniambie wenzangu na mie, hivi ni kwanini tuwalipe mamilioni ya shilingi wabunge alafu madaktari tuwakamue?
Tumekwisha.

Thursday, November 17, 2005

UNG'ANG'ANIZI MPAKA KWA OBASANJO?

Baada ya maneno mengi hapa Uganda, ambayo yalipelekea watu kulalama eti Museveni anang'ang'ania madaraka kwa kubadilisha katiba hatimaye yametimia.
Museveni kachukua fomu somahapa za kuomba kugombea uraisi kwa tikiti ya chama tawala NRMO. Lakini kimefanyika kiroja kimoja cha kisiasa hapa. Wanachama wa chama hicho wameamua kujifanya wamemlazimisha agombee kwani hakuna mtu mwenye kile wanachokiita "visheni" ya kuongoza Uganda.
Ung'ang'anizi huu wa madaraka unanipa wasiwasi juu ya kuwaamini viongozi wanajeshi kwani hata leo asubuhi nimesikia eti hata Obasanjo naye yuko mbioni kubadili katiba.
Jamani naomba maoni yenu nini kifanyike?Manake hawa viongozi ving'ang'anizi wakipata mpinzani wanatuma askari mipakani na wanawakamata alafu wanaigiza eti ni waasi na wanawahusisha na uasi. Ndio yanayomkuta Besigye sasa hivi.

MUSEVENI AANZA KUONESHA DALILI ZA UDIKTETA

Ukisikia hakuna demokrasia basi ndio hapa Uganda. Kweli Museveni amemtia kizuizini mpinzani wake mkuu ambaye amekuwa akidai Museveni ni dikteta.
Huku akiwa jela jana, washtakiwa wengine wanaoshtakiwa naye walipewa dhamana ya bei mbaya: dola elfu sita kwa kila mmoja.Pamoja na kwamba hela hiyo ililipwa lakini hawakuweza kutoka kwani wanajeshi walifika na kuiteka mahakama wakidai wanataka kuwakamata hao jamaa. somahapa Jamaa wakiongozwa na wanasheria wao walikataa kutoka na kuwa huru na wakabaki gerezani kwani haijulikani wanajeshi walitaka kuwapeleka wapi.
Nakwambia dalili za udikteta zimeanza kujionesha hapa.Lakini yote hii imemuongezea umaarufu Dr. Besyige, mpinzani mkuu wa Museveni.
Museveni jana alikutana na mabalozi wa nchi za majuu na akawatisha kwelikweli. Kuna kila dalili ya Museveni kuchokwa na waganda wengi lakini yeye sasa ameamua ni ubabe tu. somahapa
Ila ningependa pia msome makala moja nzuri sana ambayo inaeleza ni kwa vipi kumtia kizuizini Besyige kuna athari kadhaa na ni kwa vipi kunachangia demokrasia ya nchi hii iliyotawaliwa na wanajeshi. somahapa

KIROJA CHA MUSEVENI KUGOMBEA URAISI KWA MARA YA TATU

Haya wajameni, kumekucha hapa Uganda; kama nilivyoeleza mwanzon mwa wiki hii kulikuwa na vurugu sana ila mambo sasa ni shwari.
Leo nataka niwafahamishe kwamba sasa chama tawala hapa kimekuja na staili mpya yaani wajumbe wanajifanya wanamlazimisha Museveni agombee urais.Na yeye atauambia umma wa wananchi kwamba alilazimishwa: hiki ni kiroja cha karne.
Kwa ufupi Museveni kachukua fomu leo soma sasa sijui atarejesha au vipi lakini ndio hali halisi.

Tuesday, November 15, 2005

NJIA NYEUPE KWA MUSEVENI

Kama unakumbuka wakati dikteta wa Nigeria, Sani Abacha alipokuwa anajizatiti madarakani kila aliyekuwa akija mbele yake kama mpinzani aliishia lupango.Hayo yamemkuta mpinzani wa Museveni hapa Uganda jana. soma hapa

Monday, November 14, 2005

VURUGU ZA KISIASA ZATAWALA KAMPALA

Uganda ni vurugu tupu.Ule mradi wa rais Museveni tayari ameanza kuufanyia kazi.Ikitarajiwa wiki hii atajitangaza kama atagombea urais leo hii serikali ya hapa imemkamata na kumshtaki Kiiza Besigye kwa kujihusisha kwake na uasi.
Nakwambia ghasia zililikumba jiji zima la Kampala leo hii.Huu ni mwanzo wa Museveni kutimiza ndoto yake ya ushindi uchaguzi ujao.Kuanzia chuo cha Makerere hadi katikati ya mji ilikuwa ni vurugu tupu. ONA HAPA
Mapema leo katika gazeti moja hapa tayari watu walikuwa wametabiri juu ya kukamatwa kwake na wakatoa sababu kadhaa. soma hapa

Sunday, November 13, 2005

SIASA ZA KIJESHI UGANDA

Hapa Uganda kwa mara nyingine tena inaonekana wanajeshi hawatang'atuka na watafanya kila wawezalo kumlinda bwana Museveni. Wiki iliyopita, Mkuu wa Majeshi hapa alitoa mpya kudhihirisha kuwa Museveni asipingwe na atakayejaribu kumpinga atashughulikiwa.
Leo kuna uchambuzi mzuri wa athari za kauli ya mkuu wa majeshi. Somahapa uone je kweli Uganda inaelekea kwenye demokrasia?

MAALIM SEIF NI WAKUJA UNGUJA

Unaambiwa Zanzibar kama nilivyosema juma lililopita haitakaa itawaliwe na wapemba.Ndio maana nilishauri chama cha CUF kujifute alafu watu wa CUF wajiunge CCM siasa ziendelee, upinzani ndani kwa ndani. Ila leo nimevutwa na maandishi kabambe katika the gurdian la leo. soma hapa
Huyu bwana kanifurahisha nafikiri watanzania wakimsoma huyu mwandishi kuna msisimko fulani utaupata, unaweza kuamini Seif ni wakuja tu pale Unguja?Je ingewezekanaje awe raisi?
Angekubalika kweli?Kamwe nafikiri ndio maana kashindwa kwa mizengwe. Naiona hali sawa tu kwa upande wa Pemba kwani Karume naye hakubaliki huko. soma

Thursday, November 10, 2005

MUSEVENI KUTHIBITISHA KAMA ATAGOMBEA WIKI HII.

Mwishoni mwa wiki hii rais Museveni wa hapa Uganda atahitimisha yale mabishano ya muda mrefu iwapo atagombea urais tena kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.Chama tawala kinatarajia kuteua mgombea uraisi na tutajua je kweli huyu ni mpenda madaraka na je yale mabadiliko ya katiba kuondoa ukomo wa vipindi vya urais yaani miaka mitano mara mbili ilikuwa ni kwa ajili ya maslahi yake au la.bonyeza hapa
Huku umoja wa mataifa ukiwa umethibitisha kuwa kile kikundi cha waasi PRA kinachodaiwa kuongozwa na mgombea uraisi wa upinzani ambaye ni tishio kwa Museveni, inaonekana serikali hapa itamfungulia mashtaka mgombea huyo na hii itaondoa uwezekano wa Besyigye kushiriki uchaguzi.Je hii ni mbinu ya serikali au nini?Soma habari hii BONYEZA uone bonyeza Besigye anasema nini?

MGOGORO WA ZANZIBAR--SIASA MBOVU ZA NYERERE NA KARUME

Mgogoro wa siasa za Zanzibar kwa mara nyingine ni kielelezo kwamba Rais Benjamen Mkapa amefeli kuvirejesha visiwa hivi katika amani iliyopotea kwa muda mrefu.Inavyoelekea tunakwenda kumchagua Kikwete kuwa rais wetu kwa miaka mingine mitano au hata kumi kwani CCM ni utamaduni mtu hang'oki mpaka apige miaka kumi hata kama uchumi unakwenda kombo.
Katika pitia zangu za magazeti basi nikakutana na makala moja ndani ya East African, mwandishi anajaribu kuelezea mchango mkubwa wa hayati Mwalimu Nyerere katika siasa za muungano.Ni makala nzuri bonyezahapa ambayo kwangu imenifanya nione chanzo cha matatizo yote haya ni Mwalimu Nyerere na Karume kutuunganisha katika misingi mibovu.Kama unavyojua ukijenga nyumba katika msingi mbovu basi ujue utakuwa ukifanya ukarabati wa mara kwa mara.
Nimalizie tu kwamba Muungano huu ulijengwa katika msingi mbovu na ndio maana Mwalimu aling'ang'ania Mkapa awe rais ili aendeleze sera zake za kutoruhusu wapemba katika nafasi za uongozi kirahisi.Je Kikwete atafanya nini?Mimi nafikiri ni yaleyale tu.Dawa ni Wapemba waache siasa au wajiunge na CCM ili watoe upinzani wakiwa ndani ya CCM kwani tukumbuke upinzani ndani ya Bunge na Baraza la Wawakilishi ulikuwa mkubwa sana kabla ya siasa za vyama vingi kulinganisha na sasa.
Kweli tumekwisha.

ZANZIBAR--CUF KIJIFUTE CHENYEWE

Uchaguzi Zanzibar umemalizika, kasheshe kama zilivyotabiriwa tumeziona. Kama kawaida ule uadui wa miongo kadhaa umejionesha. Sikuamini wanasiasa wetu ni wajinga kiasi hiki.Nasema hivi kwa sababu pamoja na miafaka kadhaa kati ya vyama vikuu viwili, ambayo ilichukua pesa nyingi za watanganyika na wazanzibara bado imeonesha ilikuwa ni suala la kulipana mafedha tu alafu ghasia mtindo mmoja.
Mengi sitaki kusema ila nawashauri CUF wavunje chama tu manake hawatakaa washinde uchaguzi.Seif inasemekana anataka kuwa rais ona hapa kwa kila hali.Sina hakika kama ni kweli ila nadhani.Baada ya hali ilivyokuwa Zanzibar najiuliza hivi ni kwanini Seif tua au Lipumba tu ndio wagombea wa urais wa CUF kwa mwongo mmoja sasa?Kuna demokrasia ya kweli ndani ya chama au chama ni kama mali ya watu au kikundi fulani?
Wasiwasi wangu unanifanya nisijali sana juu ya mbinu chafu za uchaguzi za CCM huko Zanzibar kwani ni hatari kama Seif angelishinda uchaguzi sio ajabu asingeng'atuka kwa mujibu wa sheria.
Sijui wengine mnasemaje ila nafikiri baada ya uchaguzi huu ni wakati wa Lipumba, Seif, Mrema kupumzika. Inaelekea mtashindwa na hivyo waachieni vijana jamani.
Mwisho sijui nisemeje kuhusu uchaguzi wa Zanzibar, sina haja ya kumpongeza Karume kwani sidhani kama ni mwanademokrasia halisi lakini ndio hivyo: "Mwenye nguvu mpishe".

Sunday, November 06, 2005

DEMOKRASIA UGANDA NI NDOTO

Pamoja na kwamba mwanasiasa wa upinzani wa Uganda, Dr. Kiiza Besyigye amerudi hapa baada ya kuishi uhamishoni, nchini Afrika kusini kwa miaka minne, tayari kuna wasiwasi baada ya chama chake cha FDC kufanya uteuzi wa viongozi wake na kupanga safu ya uongozi kupambana na Museveni.
Chama tawala hapa NRMO cha Museveni, kimejengwa chini ya jina la mtu kama mali yake na sio kama taasisi ya watu.Ila la kushangaza nimegundua hata hiki chama cha Besyige, FDC, ni kama cha Museveni tu.Soma hapa uone ni kwa jinsi gani Uganda ina safari ndefu kupata demokrasia.

RAISI ANAYEPENDA UJIKO HUYU HAPA

Tunaelekea katika uchaguzi wa hapa Uganda mwaka ujao.Rais Museveni ni dhahiri atashinda, baada ya kufanikisha mradi wake wa kufuta katiba ili awe huru kugombea tena.
Huyu ni mtu mwenye jina haswa hapa Uganda, ingawa siku za karibuni amepoteza sifa na haiba miongoni mwa watu makini baada ya kuonesha dhahiri anapenda madaraka kuliko demokrasia. Sasa hivi ameanza wazi kampeni za kupita na kusalimia wananchi huku binyahapa akiendesha gari mwenyewe. Huwezi kuamini lakini ndio katika njia moja ya kuonesha ukaribu na wananchi.Wengine watasema anajikomba lakini ndio siasa.
Mimi sina maoni sana isipokuwa nilifurahi kuona rais anaendesha mwenyewe, sijawahi kuona kabisa.Nafikiri hii mambo ya kutembea kwa misafara ni utumwa fulani ndio maana nimevutwa na hili.