My Blog List

Wednesday, September 21, 2005

MKAPA ATAFUNGUA MASIKIO JUU YA MAPURI?

Kama ni shinikizo basi hili linatakiwa likazaniwe kabisa. Nilisema wiki iliyopita kwamba kuna wanasiasa wanachezea wananchi wa Tanzania.
Huu ni wakati wa Mapuri kung'oka kabisa; hatuwezi kuwa na waziri asiyejua nini maana ya utu.Nawapongeza wananchi kwa kuonesha bofya hapa jinsi gani mlivyochoka na huyu mheshimiwa.

Sunday, September 18, 2005

MANCHESTER YAKWAA KISIKI ANFILD

Nimetoka kuitizama mechi kali kati ya Manchester na Liverpool bofya hapa muda mfupi uliopita. Kusema kweli kama mpenzi wa Liverpool nimefurahishwa angala mwaka huu tuna timu nzuri. Tatizo leo ilikuwa ni umaliziaji mbovu hasa uchezaji usioridhisha wa Luis Garsia. Kwa kweli mimi sipendi uchezaji wa huyu mspaniola kwani hawezi kumiliki mpira inavyopaswa na hana pasi za uhakika.

Nadhani Benitez anafanya makosa kumpanga hasa kwenye mechi kubwa kama ya leo. Nilichogundua zaidi ni kwamba Manchester kweli hawana chochote. Sio timu imara sana kama wengi wanavyoamini. Nafikiri tusubiri watakapokutana na Chelsea ndio tutajua nani mwamba.

Ningependa wale wapenzi wa Manchester watoe maoni yao wanaonaje?

Mkutano wa Umoja wa Mataifa


Mkutano wa kilele wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,umemalizika mjini New York.Kwa maoni ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa uliotimiza miaka 60 tangu kuundwa kwake,sasa kuna haja ya kufanywa mabadiliko muhimu katika Umoja huo.Vile vile yale malengo yaliowekwa miaka mitano ya nyuma kuwasaidia mabilioni ya watu walio masikini sehemu mbali mbali za dunia yapaswa kuzingatiwa kwa dhati.

Miaka mitano ya nyuma,wakati wa sherehe za kuikaribisha Milenia mpya,wanachama wa Umoja wa Mataifa walikubaliana kupambana na umasikini na njaa kote duniani.Waliamua kuwa katika kipindi cha miaka 15,njaa na umasikini upunguzwe kwa nusu,watoto wa kike na wa kiume wahakikishiwe elimu ya msingi,magonjwa mabaya yaliosambaa duniani yapigwe vita,idadi ya watoto na akina mama wanaofariki wakati wa uzazi ipunguzwe, wanawake wapatiwe haki sawa na vile vile hatua zichukuliwe kuzuia hasara ya mali-asili inayotokea kila siku.Sasa basi theluthi moja ya ule muda uliowekwa kutimiza malengo hayo ndio imeshapita.Na kila siku inayopita,bila ya lo lote lile kutendeka,huufanya wajibu huo kuwa mgumu zaidi.

Mkutano wa kilele mjini New York,miongoni mwa masuala mengine umetaka kutazama yale yaliotekelezwa na kwa wakati huo huo kuimarisha na kuchangamsha upya azma za milenia.Lakini ilidhihirika tangu hapo awali kuwa itakuwa vigumu kuyatimiza malengo yaliowekwa.Kwani Marekani ambayo pia ilikubaliana na malengo ya Milenia,kwa ghafla ikajiweka mbali kabisa na mpango huo.Ikaanza upya kutoa madai;kwa mara nyingine tena imetaka kuuweka Umoja wa Mataifa katika hali ya udhaifu na mtengano.Lakini yote hayo ni ya kale,kwani Umoja wa Mataifa ulisimama kidete.Mkutano wa kilele mjini New York umeonyesha kuwa malengo shujaa yaliowekwa kupunguza umasikini na njaa hayawezi kuwaya-waya. Anaetaka kwenda kinyume na malengo hayo,basi atajitenga na wengine,kwani azma ya kutaka kupunguza kwa nusu umasikini na njaa hadi mwaka 2015,haiwezi tena kuondolewa kutoka ajenda ya kimataifa,hata na dola kuu kama Marekani.

Ni dhahiri kuwa Marekani,kwa sababu zinazoeleweka hutoa umuhimu mkubwa kwa masuala ya usalama na vita dhidi ya ugaidi.Katika hali hiyo basi Marekani ingeanza kwa dhati kupambana na umasikini,kwani umasikini husababisha mambo ya chuki,wivu na vurugu.Si hayo tu bali umasikini ni mbolea ya vitendo vya kigaidi.Marekani hutoa Dola bilioni 80 kuilinda Iraq,bila ya kufanikiwa.Idadi hiyo ya pesa,ingeongeza kwa mara mbili uwezo wa kutekeleza misaada ya maendeleo na hivyo umasikini ungepigwa vita kwa mafanikio.

Nchi zinazoendelea katika Hati ya Milenia ziliridhika na ahadi ya nchi tajiri kutoa asili mia 0,7 ya pato lao.Kwa kweli,hiyo ni punje ndogo sana kwa madola tajiri.Lakini Marekani,haipo tayari kutia saini makubaliano ya kutimiza pendekezo hilo.

KURA YA MAONI KENYA VURUGU TU

Huko Kenya kuna harakati nyingi hasa za kupiga kura ya maoni juu ya kuundwa katiba mpya. Tanzania bado tunatumia katiba ya zamani na tutaendelea kuijaza viraka ili iendelee kufaa. Tahadhari lakini kama mtu anafikiri kuunda katiba mpya ni jambo jrahisi basi soma hapa uone ni jinsi gani wanasiasa wa Kenya wanavyotapatapa. Nakwambia kuwa mwanasiasa Afrika ni sawa na kuamua kushusha hadhi yako kabisa.Yanayotokea huko si mambo ya kutia moyo sana.

KURA YA MAONI KENYA VURUGU TU

Huko Kenya kuna harakati nyingi hasa za kupiga kura ya maoni juu ya kuundwa katiba mpya. Tanzania bado tunatumia katiba ya zamani na tutaendelea kuijaza viraka ili iendelee kufaa. Tahadhari lakini kama mtu anafikiri kuunda katiba mpya ni jambo jrahisi basi soma hapa uone ni jinsi gani wanasiasa wa Kenya wanavyotapatapa. Nakwambia kuwa mwanasiasa Afrika ni sawa na kuamua kushusha hadhi yako kabisa.Yanayotokea huko si mambo ya kutia moyo sana.

HUYU NI HATARI ZAIDI YA MAPURI

Eti mtendaji mkubwa tu serikaliniBOFYA HAPA anafanya mambo machafu kama haya na bado hachukuliwi hatua. Inawezekana raisi Mkapa hajui hili. Ndio maana huwa nafikiri watanzania bado tuko gizani kabisa kuendana na mabadiliko ya dunia ya leo. Hebu niambie mtu anadhalilishwa yeye na mkewe alafu bado analala sero alafu mambo yanakwisha hewani.
Hili halinihusu kabisa ila kwa mtindo huu kale kanchi kanakofikiriwa kana nidhamu kanakwisha kabisa. La kushangaza vyombo vya habari kama kioo cha jamii ni kimya, vinaficha jina la mheshimiwa. Jamii ya usiri,hivi kweli tuna haja ya kuwa na vyombo vya habari?
Kuna haja ya wanahabari Tanzania kufikiri ni namna gani watafanya ili kuondoa hali hii. Najua ni woga kwa vigogo lakini tukiendelea namna hii haisaidii. Jamani gazeti la majira lituambie ni nani huyo kigogo mchafu kimaadili?

MAPURI APELEKWE MAHAKAMANI JAMANI.

Nafikiri wanachofanya wanahabari wa Tanzania bofya hapa hapa ni sahihi kabisa. Ili kupambana na uongozi wa kimabavu, usiojali watu wala utu ni lazima kumfunza huyu Mheshimiwa Mapuri adabu.
Huyu bwana jeuri sana, ningeshauri wanahabari waache mambo ya kumwomba Raisi Mkapa amfukuze kazi; nani kakwambia Tanzania tuna utaratibu wa viongozi kuwajibishana? Haiwezekani hata kidogo Mkapa akamfukuza kazi huyu bwana Mapuri. Kama Paul Kagame angelikuwa ni Rais wa Tanzania basi hili lingewezekana. Na kwasababu sio rais wetu basi acheni kulaani na kutegemea Mkapa atafanya lolote.
Jaribuni mahakamani tafadhali.

Tuesday, September 13, 2005

VIJANA NA UCHAGUZI HUKO UJERUMANI

Tunapokaribia uchaguzi mkuu: je vijana kweli wako tayari kushiriki siasa? Hebu tuangalie huko Ujerumani vijana wanajiandaaje na uchaguzi mwisho wa wiki hii. Bofya hapa uelewe nafasi ya vijana katika demokrasia.

SUMMIT YA UMOJA WA MATAIFA-- POROJO TENA

Kuanzia kesho siku ya Jumatano, mjini New York kutakuwa na mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa ambao utajihusisha zaidi na mageuzi ya umoja huu.Maraisi wapatao mia moja themanini watakutana. Kwenye mkutano huu wa siku tatu, Umoja wa Mataifa unatarajiwa kupitisha malengo ya Milenya uliyojiwekea miaka mitano iliyopita. Zaidi ya hapo wahusika wanatarajia kupitisha mageuzi ya ndani ya umoja huu ili kwa mfano kuboresha kazi zinazofanywa na Umoja wa Mataifa kwenye upande wa kulinda amani na haki za binadamu. Lakini kwa mara nyingine tena Marekani imekuja na mapendekezo mapya ambayo inataka yazingatiwe kwenye maazimio ya mkutano huu.

Kwenye mkutano huu wa kilele wa Umoja wa mataifa, Marekani itawakilishwa na waziri wake wa mambo ya nchi za nje, Bi. Condoleeza Rice. Mwanasiasa huyu wa ngazi ya juu kwenye serikali ya Rais Bush tangu wiki iliyopita ameonyesha wazi utayarifu wa Marekani kuunga mkono mageuzi ya ndani ya Umoja wa Mataifa.

Lakini kwa mara nyingine tena Marekani ina mapendekezo yake ambayo ingependa sana yazingatiwe kwenye maazimio yatakayopitishwa kwenyse mkutano huu wa siku tatu mjini New York.

Tangu mwezi wa Agosti, balozi wa Marekani kwenye uMoja wa Mataifa amewasilisha maependekezo ya marekebisho 700 hivi. Kwa mfano Mfano kipengee kinachozungumzia malengo ya Millenya.

Itakumbukwa kuwa malengo haya yalipitishwa na nchi zote wanachama miaka mitano iliyopita. Miongoni mwa malengo yaliyopitishwa ni kupunguza umaskini duniani kote kwa asilimia 50. Serikali ya Bush inataka kuondoa mwanya wa kuendelea kuziwajibisha nchi za viwanda kutoa misaada mikubwa zaidi ya maendeleo, kama ilivyokuwa imenuiwa hapo awali. Badala yake Marekani inadai masoko ya kimataifa yanaweza kutoa mchango mkubwa zaidi, hususani mageuzi ya ndani katika nchi zinazoendelea. Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Bi Condoleeza Rice akizungumzia uzizo wa biashara na masoko ya kimatafa alisema: “Tunataka kusisiziza uzito wa biashara duniani ili kuwanasua watu kutokana na umaskini. Baada ya kuongeza msaada tunaotoa kwa nchi zinazoendelea, tunataka sasa kuhakikisha sasa mifumo ya utawala inabadilishwa ili misaada tunayotoa itumiwe ipasavyo. Hapa tunamaanisha hususani utawala wa kisheria, mageuzi ya mfumo wa uchumi na vita dhidi ya ulaji rushwa”

Kwa mantiki hii hakuna tena uhakika kama kwenye azimio la mkutano wa kilele wa Umoja wa Mataifa kutakuwa na kipengee cha kuziwaibisha nchi tajiri za viwanda kutoa silimia 0.7 ya pato jumla la ndani kwa ajili ya misaada ya maendeleo. Lengo hili halijafikiwa na Marekani wala hakuna matarajio ya kulifikia hivi karibuni.

Kwa hiyo, msimamo huu wa Marekani unaweza kuzifanya nchi zinazoendelea nazo zikatae kupitisha mambo ambayo Marekani inaona ni muhimu. Kwa mfano vita dhidi ya ugaidi wa kimataifa au marekebisho ya tume ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa. Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani alisema nchi yake inataka tume hii ifanyiwe marekebisho. Alisema: “Tume ya haki za binadamu inayotaka kuundwa lazima iwe na uwezo wa kutekeleza mambo na ifuate misingi tuliyojiwekea. Hatuwezi kuwa na tume ya haki za binadamu inayojumuisha nchi kama vile Sudani ambayo inatuhumiwa kwa mauaji ya wananchi”.

Upande mwingine ambao Marekani unataka ufanyiwe marekebisho ya kina ni kazi zinazofanywa na vikosi vya kulinda amani vya umoja wa Mataifa. Mageuzi ya Umoja wa Mataifa yanataka kuuwajibisha zaidi Umoja wa Mataifa, na ikiwezekana uwe na uwezo wa kuingilia kati katika nchi nyingine ili kulinda haki za binadamu na hivyo kuzuia mauaji ya halaiki kama yake yaliyotokea Rwanda. Marekani haifikiani na mageuzi haya, kwani italazimika kutoa majeshi yake kwa kazi za kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa.

KICHAPO KWA WANAHABARI KITAENDELEA

Waandishi wa habari Tanzania wataendelea kubomondwa mpaka pale watakapoamua kwa dhati kutumia kalamu zao inavyopaswa. Sitashangaa kama waziri na baadhi ya vigogo waliohusika na kitendo cha unyanyaswaji wa wanahabari watabaki huru wala sheria haitawagusa kwani tumezoea Tanzania tunapiga mdomo kwa muda alafu tunasahau.
Mpaka wanahabari watakapoamua kuleta mapinduzi ndipo mambo kama haya(bofya hapa)yatakwisha.

CUF HILI MNATUDANGANYA SASA

Kama kawaida watanzania kutokana na sijui niseme ni kuonekana mbumbumbu sana au vipi ila mimi sidhani kama kuna serikali ya Tanzani itakayoweza kusomesha bure elimu ya sekondari. Ukizingatia idadi kubwa ya wanafunzi tunahitaji shule nyingi sana na hapa kwa kutumia mbinu za kileo nafikiri chama cha CUF kinadanganya. Bofya hapa uniambie je inawezekana?

Sunday, September 11, 2005

UNENE--UTIPWATIPWA KUUA WATANZANIA WENGI.

Jamani watanzania tunakula hovyo sana. Inasemekana kwa sasa kuna hatari hasa kwa wale watanzania wanajioweza kupata matatizo yanayotokana na unene au utipwatipwa.
Kuna umuhimu elimu ya jinsi gani ya kula itolewe na vyombo vya habari manake siku za usoni badala ya Ukimwi kuchukua roho za watu wengi itakuwa ni unene. Soma tathmini iliyotolewa juu ya hali ya utipwatipwa nchini Tanzania. Bofya hapa kwa habari zaidi.

Saturday, September 10, 2005

DISSAPOINTING SPEECH FOR ME THIS YEAR.


This was what I heard with a lot of uncertainity on that day when Bush was about to beggin his crusade for Democracy: “America sees you for who you are: the future leaders of your free country”. He even mentioned countries like North Korea, Burma, Iran and Zimbabwe that they need freedom from America. These were some of many sentences I found remained in my mind following inauguration speech on 20th of January by US president Bush. His speech was full of statements that signalled a fundamental change in US foreign policy.As an African, staunch support of democracy, I heard him say that the United States under Bush would be actively engaged in Africa’s struggle for democracy. I heard him say that the US—Africa relations under his second term would not be business as usual. Happily I thought, really, if carried through, the Bush Doctrine should have a seismic effect on African politics and government.However, my delight with Bush’s speech was tempered by a scepticism born of disappointment. I decided to surf on American history a bit and I discovered: this is not the first time American President to commit himself to the struggle for freedom. Others were President Woodrow Wilson in 1916 and Truman in 1947. For example, Truman addressing Congress said: “It must be the policy of US to support free peoples who are resisting attempted subjugation by armed minorities or by outside pressures” But funny enough US supported Apartheid in South Africa for many years. It supported dictators: Mobutu, Banda, Mubarak and even currently Musharaf for serving their interests. What a cynical America politics.For opposition activists in Zimbabwe the speech was good news. But my fear is: if Mugabe is out of politics of Zimbabwe and opposition—MDC took over; will it serve Zimbabweans or Americans who seems ready to do whatever possible to ensure Mzee Bob is out. I think, obviously we should not expect Bush and America to deliver democracy in Africa. It is the African people who must accomplish the goal of successful democratisation. Africa must peacefully organize themselves into very active, brave and focused political organizations that transcend petty cleavages.Here I mean: We must not underestimate the role of a country such as US in sustaining dictatorships and pseudo-democracies through diplomatic cover, financial and material support. As we—Tanzanians—are heading for the election later this year, we should not just vote blindly. Are we really asking where do political parties get their funds? I know Conservative Party of Britain somehow funds one party. Another one is from various powerful communist states like China and Korea. Knowing source of fund can help us to identify to whom a certain party will serve: either for us citizen or to the colonialists.So when we see Bush is promising the opposition politician as future leaders of their country, do not think America is Messiah. Neo—Colonialism will finish us-Africans-as we shall continue to rely on the Western world for the improvement of our democracy.
2/6/2005.

UGOMVI KATI YA MUSEVENI NA KAGAME.

Monday, June 13, 2005

Mambo si mambo hapa Uganda, huwezi kuamini maraisi wawili wa nchi jirani hawapatani kabisa; zamani walikuwa marafiki ila hivi karibuni mambo yao si mazuri kabisa. Kwa mfano wiki chache zilizopita wakati wa mkutano Comesa, kasheshe kubwa lilijitokeza.

Wednesday, May 25, 2005

SIR ALEX NA WENGER WAMEKWISHA KIMBINU.

Makala yangu iliyopita niligusia juu ya kuporomoka kwa Man United kama timu imara barani Ulaya. Leo labda niseme kuingia kwa Roman Abramovich katika soka la Uingereza kumechangia kuporomosha timu hii. Tangu msimu uliopita, kombe la FA limekuwa ndio kitulizo cha timu kwa mashabiki wake lukuki duniani. Msimu uliopita ikumbukwe ndilo lililolinda kibarua cha Sir Alex; msimu huu amelikosa, hatakuwa salama tena kwani kuingia kwa Malcolm Glazer, tajiri la kimarekani kama mpinzani rasmi wa Abramovich hakutaruhusu meneja asiye na mafanikio.

Nifananishe na yaliyomkuta meneja wa Chelsea—Claudio Raniere—baada ya kuja kwa Abramovich ilibidi atafutwe Morinho haraka sana baada ya udhaifu wa Ranieri kuwa dhahiri. Nani asiyejua hawa jamaa wataka hela yao ipate mafanikio ya haraka sana. Hawazimiliki timu kwa misingi ya kuwafurahisha mashabiki; ni watu wako katika biashara na wanataka kila ndururu inayowekezwa izae na sio hasara. Na ndipo hapa Sir Alex yuko hatarini nathubutu kusema. Japo wapenzi wa timu hii hawamtaki Glazer ila watagundua umuhimu wake siku za usoni. Sasa hivi wana mawazo kama wapenzi wa Simba na Yanga hapa nchini Tanzania wanapopinga kila kukicha kwa klabu zao kuendeshwa kisasa.

Kwa klabu inayoendeshwa kama taasisi ya kibiashara ni dhahiri imekuwa kibonde. Inaongoza kwa kulipa mishahara ya juu kwa wachezaji nchini Uingereza, ina meneja anayelipwa ghali zaidi Uingereza hadi siku za hivi karibuni na inapata fedha nyingi zaidi katika makusanyo ya mlangoni na hata kutoka picha za runinga. Najua hakuna mpenzi wa Man United atakayeamini kuwa kushidwa huku msimu huu ni mwanzo wa kuporomoka kwa mbinu za kiufundi za Sir Alex. Huu ndio ukweli uliopo; na hali hii inazikabili timu zote mbili zilizocheza fainali ya FA mwaka huu.


Nikizingatia pia kiwango cha Arsenal katika fainali ya FA hivi majuzi ni dhahiri Arsenal haitaweza kucheza kombe la mabingwa msimu ujao kwa mafanikio zaidi ya hatua za makundi. Wenger naye hana jipya; ni wakati muafaka kwa Ashley Cole Viera na Henry kuamua kujiunga na timu za ushindi kama wanataka mafanikio katika soka. Kwa hali ilivyo sasa, tutarajie yaliyomkuta kocha mzoefu Ottmar Hitzfeld na kukatisha kibarua chake Bayern Munich mwaka jana ndiyo yatakayowakuta Sir Alex na Wenger.

WANAHABARI TANZANIA WANAKOSEA KWA HILI.


Ijumaa, tarehe ishirini mwezi huu wa tano, hatimaye Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania alikipiga mkwara chama tawala, CCM, kuacha kumtambulisha mgombea uraisi wake nchi nzima akifananisha na kitenda cha kupiga kampeni kabla ya wakati. Msemaji wa CCM, alijibu eti huyu msajili ana kimbelembele; mimi nikaona hapa CCM wanadhihirisha na kuturudisha katika enzi zile; eti bado tuko kwenye chama kimoja. Mbaya zaidi, katika fafrija moja ya utambulisho, Raisi mstaafu Ali Hassan Mwinyi alinistaajabisha pale aliposhauri utambulishi huu uendelee nchi nzima.

CCM wanaonesha kutojali kabisa uwepo wa vyama vingine vya siasa hasa katika suala la haki sawa za mchezo wa kisiasa. Hii inanikumbusha moja ya tawala dhalimu zilizopita miongo kadhaa huko Jamhuri ya watu wa China: mwanamapinduzi—De Xio Peng—alipokuja na kauli mbiu: “Haijalishi kama paka ni mweusi au mweupe bali kama anaweza kukamata panya”. Ni mbinu ya kidhalimu na kizandiki isiyojali sheria na taratibu za mchezo haki kisiasa zinatumiwa na chama tawala. Ili mradi mgombea wao atangazwe kwa wananchi katika staili ya kupiga kampeni kwa kutumia rasilimali za serikali naweza kuhisi.

Baadhi ya magazeti yalifananisha na mikutano ya kuimarisha chama ambayo inafanywa pia na vyama vingine kila siku. Lakini mimi najiuliza: nimeona mheshimiwa Kikwete akitambulishwa na mgombea mwenza, mheshimiwa Ali Shein na hata raisi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mheshimiwa Karume. Panakuwepo lundo la askari karibu wa kila aina, utaona rasilimali mbalimbali za serikali pale na hata baadhi ya viongozi wa asasi za serikali. Haijalishi hiki ni chama tawala ila kama nikifananisha na mikutano ya uimarishaji chama ya hivi vyama vya siasa vya upinzani naona kabisa hakuna usawa.

Nafikiri kipindi cha kampeni kila chama kinapewa fungu la shughuli hiyo na angalau kunakuwa na usawa ambao nafikiri msajili kauona. Nimesoma matangazo mengi yenye salam za pongezi kwa mheshimiwa Kikwete; haya yanatolewa na makampuni, mashirika, na hata idara za serikali. Profesa Lipumba alipohoji anaonekana kama mwehu na vyombo vya habari. Hakuna chombo chochote cha habari kilichoandika juu ya athari za kitendo hiki cha pongezi kutoka taasisi mbalimbali. Uwezekano wa michezo michafu kati ya mgombea anayepongezwa na asasi zilizompongeza tuutizame iwapo atachaguliwa. Vyombo vya habari labda kwa minajili ya kupata fedha za matangazo vimeona hii itawaathiri kimapato. Uandishi makini upo hapa kweli?Labda nimpongeze msajili kwa kuionya CCM dhidi ya tabia ya kuturudisha katika enzi ya chama kimoja ambapo haya yanayotokea ilikuwa ni utamaduni.

Yanayoandikwa sana na magazeti hapa ni juu ya kutabiriwa ushindi wa kizilzala—yaani Tsunami wa mheshimiwa Kikwete. Changamoto kwa vyombo vyetu vya habari ni hii: jamani hivi hamwoni huu ni wakati wa kuwakumbusha watanzania—wadanganyika—juu ya mengi yaliyotokea katika muongo huu unaokwisha wa mheshimiwa Mkapa? Kwa mfano, ile habari ya umeme ya IPTL, mkataba wa Network Solution, Ajali za MV Bukoba na Treni Dodoma pamoja na huu uvunjaji wa mkataba kati ya serikali na kampuni ya City Water kama dhihirisho la utendaji mbovu ambao wananchi wanapashwa waeleweshwe kwa kina ili waweze kuitumia kura yao kwa utashi makini?

Upinzani wetu ni dhahiri ni hoi ila ni lazima tuhakikishe katika serikali ijayo ya CCM wale wote waliohusika kwa njia moja au nyingine hawapewi dhamana tena ndani ya serikali. Katika madhila nilizotaja hapo juu ni wazi wapo mawaziri au hata wabunge; ni jukumu la vyombo vya habari kutoa habari za upelelezi za kina juu ya matukio hayo kwa wananchi ile nao wawajibishe kupitia kisanduku cha kura hapo mwishoni mwa octoba.

Nimegundua kwamba CCM kutuletea mgombea kijana imefunika rekodi zote chafu za CCM. Vyombo vya habari naviona vimeamua ‘kufunika kombe mwanaharamu apite’. Japo vyama vya upinzani viko hoi, lakini ipo haja ya ukosoaji unaozingatia haki. Kwani ni wazi kama CCM ingekuwa safi tungetarajia nchi yenye maendeleo makubwa kuliko sasa. Nasema hivi kwasababu nchi ya Uganda pamoja na kuwa vitani kwa muda mrefu iko karibu sawa kiuchumi na nchi yetu. Hatutofautiani sana, nashindwa kuelewa sisi na amani yetu ya muda mrefu kunani jamani? Wanahabari amkeni jamani, igeni wenzenu kwa mfano wa Nation Media na The Standard wa Kenya, The Monitor, Vision na The Observer wa Uganda. Wanakosoa kwa manufaa ya umma.

DALILI ZA MANCHESTER UNITED KUPOROMOKA.


Hakuna atakayebisha, Arsenal na Man United zinaelekea kuporomoka. Fainali ya jumamosi—kombe la FA—iliyopita ilionesha udhaifu mwingi katika timu zote mbili. Kwanza nikumbushie rekodi kadhaa ziliwekwa: moja, Arsenal ilifanikiwa kusawazisha rekodi ya kulitwa kombe la FA mara ya kumi na moja kama Man United. Sir Alex Ferguson alishindwa kuweka rekodi ya kulitwa kombe hilo kwa mara ya sita baada ya kuiogoza Man United katika fainali saba.Pili, Arsene Wenger aliweza kushinda kombe la FA kwa mara ya nne miongoni mwa fainali tano kama meneja.

Kwa bahati Arsenal ilishida fainali hiyo kwa sababu ya udhaifu wa Man United katika idara ya kiungo na umaliziaji. Kama nilivyowahi kuandika (www. ) Wenger hana uwezo wa kupambana na Sir Alex; hili lilijidhihirisha. Arsenal walishindwa kuonesha mchezo wake wa kawaida dhidi ya Man United. Hili ndilo limekuwa likiwanyima ushindi mara zote msimu huu walipokutana na Man United. Ndio maana baada ya dakika mia na ishirini ni mashuti kumi na tisa ya Man United dhidi ya moja la Arsenal yalielekeza golini.

Ukiacha Jens Lehman, Rooney alikuwa mchezaji bora wa fainali ile. Ni dhahiri Scholes na Keane walionesha kuchoka. Idara ya kiungo ilizidiwa na akina Viera na Gilberto wa Arsenal. Wakati fulani ilibidi Keane abadilishane nafasi na Fletcher ili kuleta uwiano. Ni lazima Man United isaini wachezaji wapya katika nafasi hizi la sivyo meli itaendelea kuzama. Ronaldo kama kawaida mchezo wake unatabirika; mbinafsi sana, hajui mpira wa kileo wa kitimu. Japo alifanikiwa kupiga krosi kadhaa ila zote zilikuwa pofu. Haelekezi mipira kwa mtu (pin-point) bali mara nyingi yeye ni majalu golini. Nelstoroy bado ni hazina ya Man United ila siku ile hakuwekewa mipira mizuri; ilimbidi mara kadhaa kushuka sana katikati kuanzisha mashambulizi.

Kama klabu tajiri kabisa duniani, mtu huwezi kuamini ile klabu iliyozoea kushika nafasi mbili za mwanzo na sio chini ya hapo kwa miaka kumi iliyopita sasa inategemea kuwafurahisha mashabiki wake kwa kujaribu kushinda kombe la FA kwa miaka miwili iliyopita. Hii ni klabu baada ya kushinda vikombe vyote vitatu mwaka 1999—Klabu Bingwa, Premia na FA—ilijiona iko mbinguni. Mwaka uliofuatia 1999/2000 ikajitoa kushiriki FA kwa maringo ya Sir Alex; haya yalikuwa matusi kwa utamaduni wa soka la Uingereza. Leo hii timu imetoka kapa: hakuna ubingwa wa ligi, FA na hata ile tabia ya angalau kufika robo fainali ya Klabu bingwa Ulaya timu haikuweza. Nini kama sio kuporomoka?

Thursday, May 19, 2005

HIZI NI HEKAYA ZA KIKWETE.

Nimesoma juu ya Kikwete kuahidi vijana wa kitanzania nafasi lukuki za ajira iwapo atachaguliwa kuw raisi wa Tanzania hapo mwezi wa octoba. Mimi nina wasiwasi mkubwa juu ya udanganyifu wa huyu bwana. Tukumbuke tatizo la ajira si la Tanzania tu, kila mahali dunia nzima limeenea.Kwa hiyo mheshimiwa Kikwete anapotuambia eti ajira zitakuwa bwerere napenda atueleze atafanya nini ili hili liweze kutokea. Ni wazi atakuwa anaendeleza sera za utandawazi ambazo hazikwepeki. Katika hili ndio tunashuhudia na tutaendelea kushuhudia ushindani mkubwa wa ajira sio tu miongoni mwa watanzania ila hata watu kutoka nje ya nchi. Kwa utafiti wangu binafsi tu: hadi leo kuna raia wengi wa Uganda na Kenya ambao wako Tanzania na wanafanya kazi wakilipwa mapesa lukuki kutokana na elimu waliyonayo inayowafanya waajirike.Katika hali hii ya ushindani nilitegemea mheshimiwa Kikwete atueleze ataboreshaje elimu yetu ili vijana wetu waweze kuajirika. Sio kusimama majukwaani na kudanganya umma eti ajira zitaongezeka; haiwezekani hivi. Nchini Kenya, serikali ya Narc iliingia madarakani na ahadi lukuki za ajira lakini leo ni miaka mitatu ajira ndio zinapotea kabisa. Tanzania pekee haitaweza kutokomeza tatizo la ajira, ila kupitia utandawazi ni wajibu wa Taifa kutoa elimu bora kwa wananchi wake ili waweze kuchangamka wenyewe kutafuta ajira iwe nchini Tanzania au nje ya nchi. Ndio maaana naweza nikaziita hekaya hizi mbwembwe za mheshimiwa Kikwete.Ingekuwa vyema tuelezwe ni mkakati gani utatumika?
9/5/2005.

TFF BOMU?

Niliwahi kuandika masikitiko yangu juu ya uoza unaokabili sekta ya michezo Tanzania hasa mchezo wa mpira wa miguu. Nilielezea masikitiko yangu juu ya uzembe wa hali ya juu uliosababisha timu yetu ya soka ya vijana kuzuiwa kucheza fainali zinazoanza kesho huko Gambia.Basi wiki hii nilicheka sana; kama mtanzania mzalendo sikupaswa kucheka ila ni pale niliposikia eti shirikisho la mahakama ya kimichezo, CAS, imeitupilia mbali rufaa soma hapa ya timu yetu iliyokuwa inadhani ingeshinda rufani hiyo. Sina hakika kama kweli TFF chini ya rais, Leodgar Tenga inawakilisha kundi la viongozi makini au ni yale yale ya zamani. Jaribio la kukata rufani linanifanya niamini kuwa hawa mabwana wapya pale TFF ni wababaishaji tu.Yaani udanganyifu ulishajulikana lakini bado walikuwa wanahangaika kubembeleza hii ni hatari kwa maendeleo ya soka nchini. Nikifikri naona bado itatuchukua miongo kadhaa hadi kizazi kingine ndipo tupate walau mafanikio katika michezo hususan soka.Kwa mpenda soka yeyote wa kitanzania, hebu tizama ushiriki wa timu za Tanzania katika michuano ya Kagame huko mwanza alafu uniambie inaonesha nini.Aibu tupu,hebu fikiria tumewakilishwa na timu tatu lakini wapi. Hivi tunakwenda mbele au ndio bado tuko kwenye usingizi wa pono? Haya! ngoja nisilonge sana ila nafikiri ndio maana Rais Mkapa atakapoacha madaraka ataweka historia ya kuwa Rais pekee wa Afrika ambaye hajawahi kuhudhuria mechi ya kandanda. Unafikiri kwa nini haudhurii? Hakuna cha kutizama.Nimalizie kwa kueleza furaha yangu kwa mafanikio ya klabu niipendayo-Liverpool-katika michuano ya kombe lamabingwa Ulaya.Wiki iliyopita nilitabiri tutafungwa ila Mungu alikuwa upande wetu.Nina matumaini tutashinda kikombe hiki mwaka huu.
6/5/2005.
posted by Kesi Inno. at 2:38 AM | 0 comments

KWELI KIKWETE TSUNAMI.


Baada ya moshi uliovuma huko Dodoma juzi jumatano, binafsi nimeridhika na chaguo la CCM. Kikwete atatufaa watanzania kama raisi wa awamu ya nne. Ni mgombea ambaye nafikiri atapata ushindi mkubwa sana hapo uchaguzi wa mwezi wa kumi utakapowadia.Kama vile watanzania wengi walivyofurahishwa na Kikwete basi ni matarajio yangu huyu bwana akishinda ataunda serikali mpya yenye sura mpya, za vijana kama yeye na sio wale wale tuliowazoea tangu uhuru. Ni wazi mheshimiwa Kikwete ana kazi kubwa katika ile vita iliyomshinda Mkapa: mdudu rushwa .Basi nasubiri wapinzani wataibuka na mbinu gani ya kuzuia hii Tsunami ya Kikwete manake mwaka huu kuna aibu itawakumba wapinzani wasipoangalia. Uungaji mkono huu kwa wingi miongoni mwa wananchi ni kielelezo tosha kuna kazi.
6/5/2005.

UCHAGUZI VATICAN UTAKUWA KAMA ULE WA VATICANO.

Kwanza leo ni siku ya wafanyakazi duniani, napenda kutoa pongezi kwa wafanyakazi wote nchini Tanzania hasa nitoe pole kwa wale ambao wanapata taabu katika kipindi hiki cha ubinafsishaji. Ila leo sitaki niongelee juu ya hii sera mpya ya ubinafsishaji, nitatafuta wakati. Hii itakuwa wiki ya kukumbukwa kihistoria katika Tanzania. Ni wiki ambapo atakayekuwa Rais wa awamu ya nne atateuliwa na mkutano mkuu wa chama tawala-CCM. Natarajia mizengwe kutawala zoezi hili kwani hisia zangu sidhani kama yule anayedhaniwa kushinda nafasi hii atashinda. Kumekuwa na kejeli na vijembe vingi hadi sasa miongoni mwa wagombea; mwingine akimwita mwenzake kuwa uraisi sio sura nzuri na mwingine akijigamba eti funguo za nchi kashakabidhiwa. Najua wajumbe tayari wanajua watamchagua nani; mimi napenda leo nibashiri kwani kutokana na Siasa za Tanzania nilivyozizoea nafikiri huu utakuwa mpambano kati ya Sumaye na Kikwete. Ni hivi majuzi tu moja ya taasisi kubwa kabisa ulimwenguni ilimchagua kiongozi wake mkuu baada ya kufariki dunia kwa aliyekuwepo.Hili ni kanisa katoliki ambapo kwa sasa lina kiongozi mpya—Papa Benedict XXVI. Kanuni kuu katika uchaguzi ule ambao ulifanywa na wajumbe wapatao 115 ilikuwa ni kuhakikisha anawekwa mtu wa kuendeleza pale marehemu Papa Paulo II alipoachia. Ni hali hii ndio ninayoiona itatawala uchaguzi huu wa CCM wiki hii huko Dodoma. Nani asiyejua kuwa kati ya watu rais Mkapa anaowaamini ndani ya serikali yake kwa miaka kumi iliyopita wa kwanza kabisa amekuwa ni Fredrick Sumaye. Kuwa mtendaji mkuu serikalini sio kitu kidogo kwa miaka kumi. Kikwete ukizingatia alimshinda Mkapa katika Konklave iliyopita sidhani kama atakuwa na ushawishi ndani ya chama kama Sumaye. Katika gazeti la serikali hapa Uganda leo, makala moja inadai eti pamoja na kufanya kazi za kimataifa kwa miaka kumi, Kikwete hakubaliki na jumuiya ya kimataifa. Na inasemekana Mkapa hamuungi mkono. Kwa upande wa Salim, inaonekana ni vigumu kukubalika hasa ukizingatia historia yake na chama cha UMMA. Pia nafikiri ushirikiano wake na kampuni ya NICO umeshamrabia. Hawa ni watu tishio kwa sera za ubinafsishaji na ndio hapa Mkapa hatamuunga mkono.Waziri mkuu kama alivyokuwa Kardinali Ratzinger ndiye kiranja mkuu wa serikali; wakuu wote wa wilaya na mikoa wako chini yake. Ni rahisi sana kwake kushawishi wajumbe wanatoka mikoani kuliko mgombea yeyote. Ni kwa maana hii mimi nampa dau langu kwa dhati. Si kwamba napenda awe raisi lakini nitake nisitake atakuwa ndie mgombea wa chama tawala nadhani. Ingawa Sumaye anatuhumiwa sana, hii ndio sifa kwa kiongozi shupavu. Nani asiyejua kiwango cha juu cha kuchukiwa kwa Papa Benedict XXVI. Dunia ya leo inahitaji watu wasioogopa kuchukiwa na wasioyumbishwa na nadhani Sumaye ameweza kuonesha ujasiri kwa hili kama kweli mtu unafuatilia siasa za Tanzania. Hebu tusubiri hili Konklave la CCM katika Sistine Chapel yao—Chimwaga litaibuka na jina gani. Hayo ni maoni yangu kutokana na mtizamo wangu ninavyouona mimi. Mwisho mgombea wa kiti cha Zanzibar inaonekana CCM inataka kuitupa demokrasia chooni. Nilichukizwa sana wiki hii kusikia eti Dr. Bilali analazimishwa aondoe jina lake ili amwachie Karume bila pingamizi. Sasa Zanzibar naifananisha na Togo. Hii inaonesha ni jinsi gani Tanzania bado tunaabudu siasa za umangimeza. Kuna haja ya Chama tawala kuchuja wajumbe wote wenye mawazo na mitizamo hii. Hii ningependa iwe changamoto kwa vijana kujihusisha na siasa. Tumewaacha wazee kwenye siasa kwa muda mrefu. Huu ni wakati wa Zanzibar kuondoa huu uongozi wa kurithishana kama vile huu ni ufalme.
1/5/2005.

ANFIELD KUAMUA NANI ACHEZE FAINALI.

Mourinho amekwenda mbali zaidi kwa kukiri kuwa suluu waliyoipata Stanford Bridge wiki iliyopita imerahisisha kazi katika mpambano ujao wiki hii. Sasa ataelewa kwamba Anfield—Liverpool inacheza mchezo tofauti kabisa. Aulize Monaco, Olympiakos, Bayern Leverkusen na Juventus. Lakini pia ameshau Chelsea imepoteza mechi zake muhimu za ugenini katika michuano hii: Bayern, Barcelona na Porto. Hii inanipa matumaini kuwa ushindi kwa Liverpool sio ndoto, inawezekana kabisa.Hakuna timu iliyowahi kuzuru Stanford Bridge bila kuruhusu wavu wake kutikiswa msimu huu katika michuano hii. Lakini nakumbuka Jerzy Dudek wiki iliyopita alikuwa na mapumziko sana kuliko mechi yeyote aliyowahi kucheza msimu huu. Tukitizama rekodi baada ya michuanno ya makundi kati ya timu hizi mbili, Liverpool imefika nusu fainali bila kupoteza mechi yeyote kinyume na Chelsea. Tukitumia sababu hii basi tuamini kuna uwezekano wa Liverpool kushinda kinyume na matarajio ya asilimia kubwa ya wapenda soka ambao tayari wamekwisha fifisha matumaini ya Liverpool kushinda. Hadi sasa, ukweli unabakia: Chelsea ni timu bora kabisa kwa sasa nchini Uingereza; Liverpool in timu yenye rekodi ya mafanikio kuliko klabu yeyote hapo Uingereza. Ni timu mbili zenye rekodi za aina yake. Tusubiri tuone mpambano wa marudiano tuone je kutokuwepo kwa Biscan na Alonso kutaiathiri vipi Liverpool katika mpambano wa marudiano?
1/5/2005.

NUSU FAINALI MABINGWA ULAYA--UTABIRI WANGU.

Ipo haja nizichambue na kuweka ubashiri wangu juu ya mechi mbili wiki hii katika ligi ya Mabingwa Ulaya. Ni nusu fainali ambapo bila kutarajia moja ya mechi hizo inazikutanisha timu kutoka nchi moja. Chelsea, mabingwa watarajiwa wa ligi kuu ya premier watapepetana na Liverpool. Tangu Man United itwae ubingwa huo mwaka1999, ni mara ya kwanza tuna hakika ya kushuhudia fainali itakayohusisha timu moja kutoka Uingereza. [if !supportEmptyParas] [endif] Wengi wanaamini itakuwa mechi kali sana kwasababu timu hizi zimekutana mara tatu msimu huu. Chelsea ilishinda mechi zote; kikawaida kwa wapenda soka hapana shaka si kawaida kwatimu kufungwa mara nne na timu hiyo hiyo katika msimu mmoja. Ni dhahiri kuna uwezekano mkubwa kwa Liverpool kuibuka na ushindi katika nngwe hii.Lakini Mourinho na wachezaji wake tayari walishasema ni afadhali wamepangwa na Liverpool kuliko AC Milan au Juventus kama ingevuka robo fainali. Mourinho anaziogopa timu za Italia, aliwahi kunukuliwa akisema FC Porto ilikuwa na bahati msimu uliopita kutokukutana na timu za Italia. [if !supportEmptyParas] [endif] Hii inaashiria mchezo utakuwa mgumu sana kwa timu zote mbili. Liverpool ikiwa na Xabi Alonso na Djibril Cisse waliopona hivi karibuni mambo yatakuwa magumu kwa Chelsea. Liverpool itakapomsahau Lampard na kumpa mwanya wa kupiga mpira itakuwa ni balaa kwao. Ni dhahiri huu utakuwa ni mpambano wa makocha zaidi; Mourinho na Benitez watapambana kimbinu; na ni timu itakayocheza bila kufanya makosa ndio itakayoibuka kidedea. [if !supportEmptyParas] [endif] Upande mwingine, AC Milan na PSV: mchuano huu unaonekana kama ushindi bwerere kwa Milan. Meneja Guus Hiddink wa PSV ana uzoefu wa hali ya juu kuwa na mbinu za kuizuia Milan. Ila tu Milan itakuwa ni mfupa mkubwa sana kwa PSV. Ni timu iliyokamilika kila idara; ulinzi imara, kiungo ndiio usiseme na washambuliaji ni wa kutisha sana. Sioni ni vipi PSV itaibuka na ushindi hapa. [if !supportEmptyParas] [endif] Mwisho, sifikiri yaliyotokea miaka iliyopita katika michuano hii yanaweza kutokea tena. Timu ndogo isiyodhaniwa kushinda kombe hili tusahau. Ile habari ya Monaco au Bayern Leverkusen kufika fainali na kushindwa ndio itakayojitokeza. Nafikiri fainali itakuwa Chelsea dhidi ya Milan. Kama Liverpool itavuka na kuingia fainali basi yale ya Porto ya mwaka jana yatajitokeza tena msimu huu.Ila ni vigumu kwa Liverpool kushinda nngwe hii ya nusu fainali.
26/4/2005.

WANAWAKE USINGIZINI TANZANIA?

Ni maajabu manake hata kugombea kwa wanawake ni taabu. Hebu shangaa, hakuna wanawake zaidi ya watatu katika Tanzania nzima wanao angalau kutajwa kugombea uraisi kupitia chama tawala au hata vyama vya upinzani.Mimi nafikiri kule Beijing mlikwenda kutalii tu. Amkeni jamani.
11/3/2005.

HAWA NI WAZEE BWANA.

Kuingia kwa John Malecela na Salim Ahmed Salilm kumenisikitisha kwa kiasi fulani. Hawa ni watu kama ni uongozi wameshiriki kwa muda mrefu sana. Uoza wote wa rushwa na madhila mbalimbali wao wameshiriki kwa dhati kabisa. Bwana Salim pamoja na kukaa nje kwa muda mrefu nafikiri angepumzika. Hawa si chaguo langu kabisa. Nilizaliwa nikakutana na msemo: "Vijana Taifa la Kesho". Leo mimi ni kijana nakaribia uzee, je wale waliokuwa vijana ndio wameachwa kabisa?Jamani naomba Mungu hawa wazee wafe kwa uzee manake bila kuiama dunia hii, hawataachia madaraka.
11/3/2005.

NDOA BILA HARUSI.

Itachukua muda mrefu hadi hapo wanakandanda wa kiafrika wanaocheza soka huko Ulaya watakapoienzi heshima wanayotunikiwa kila mwaka na shirikisho la soka barani Afrika. Kwani ni wazi wamesahau bara la Afrika kama nyumbani. [if !supportEmptyParas] [endif] Ninasema kwa machungu kwasababu kukosekana kwa mastaa hawa isipokuwa mmoja tuu tena mwanamama mwanasoka bora wa mwaka kutoka Nigeria—Pertpetua Nkocha—katika tafrija ya kuwazawadia iliyoandaliwa na kampuni ya simu MTN ikishirikiana na Shirikiksho la kandanda barani Afrika huko Durban wiki hii ilikuwa ni upotezaji wa fedha na muda. Hebu fikiria waandishi wa habari kutoka kila pembe ya dunia na bara la Afrika walikuwepo; matangazo ya television yalirushwa moja kwa moja Afrika nzima. Lakini yote hii niliiona kama ni sawa na “Ndoa bila bibi harusi”. [if !supportEmptyParas] [endif] Ilikuwapo mechi ya kusaidia wahanga wa Tsumami ambayo ilimzuia Samuel Eto’o kufika na akamtuma mkewe. L abda kwasababu ilifanyika jijini Barcelona sielewi. Kwa baadhi ya wachezaji ilikuwa ni ili angalau wajpate nafasi ya kucheza na wachezaji wenye majina. Obafemi Martin aliona ni afadhali acheze na akina Ronaldino, tena chini ya dakika kumi, kuliko asafiri aje katika bara mama kupokea tuzo yake ya mchezaji mdogo wa mwaka. [if !supportEmptyParas] [endif] Si hao tu, ila nashindwa kuelewa golikipa—Enyeama—wa Enyimba aliyeshinda tuzo ya golikipa bora au kocha wake aliyeshinda kocha bora wa mwaka kwanini hawakufika? Jamani kunani soka la Afrika? Mwisho, kwa ufadhili huu wa MTN ni matumaini yangu katika miaka michache ijayo, itapendeza tu iwapo watakaoshinda tuzo mbalimbali wanajitokeza. Sherehe za tuzo za mwaka huu ilikuwa aibu tupu; ni sawa na sherehe ya ndoa bila bibi harusi.
27/2/2005.

Miezi mitatu iliyopita Man United iliisimamisha ile rekodi ya muda mrefu ya Arsenal kutokufungwa mechi arobaini na tisa katika ligi kuu nchini Uingereza. Alafu hivi majuzi—wiki mbili zilizopita—Man United, siyo tu ilivunja rekodi nyingine ya Arsenal ya kutokufungwa mara arobaini na tano katika uwanja wao wa nyumbani-Highbury- tangu ilipofungwa na Chelsea katika robo fainali ya ligi ya mabingwa mwaka jana, bali iliisukuma Arsenal katika nafasi ya tatu baada ya kufuta pengo la pointi kumi na moja tangu October mwaka jana.Man United iko mbele ya Arsenal kwa pointi mbili. Tukumbuke mwaka jana Arsenal ilizuiwa na Man United kufika fainali ya kombe la FA. Kama Arsenal wangeishinda Man United mechi iliyopita angalau wangeamsha hisia za ubingwa. Lakini Man United imehakikisha itabakia ndoto kwa Arsenal kuwa bingwa msimu huu.Naweza kusema Wenger ni kocha dhaifu hasa unapompima na Sir Alex Ferguson. Lililobakia sasa ni kumuondoa Wenger miongoni mwa makocha mahiri katika ligi ya Uingereza hasa katika mbinu na upikaji wa nidhamu ya wachezaji. Kwa sasa Alex tumpe wapinzani wapya. Wapo tayari wanajongea taratibu kuchukua nafasi ya Wenger: Jose Mourinho na Raphael Benitez tusubiri tuwaone.Kihistoria, Man United ina sifa ya kupangua pointi na kuifukuza timu iliyo mbele yake kama ilivyo Chelsea sasa. Tayari imemaliza pengo la pointi kumi na moja dhidi ya Arsenal na sasa shughuli ni kwa Chelsea. Kama Man United watatwaa ubingwa basi Alex atakuwa hana mpinzani.Ila Chelsea wakiutwaa kama inavyoelekea basi Morinho atakuwa ndio mpinzani mpya wa Sir Alex.
13/2/2005.

SIR ALEX NI KIBOKO YA WENGER.

Miezi mitatu iliyopita Man United iliisimamisha ile rekodi ya muda mrefu ya Arsenal kutokufungwa mechi arobaini na tisa katika ligi kuu nchini Uingereza. Alafu hivi majuzi—wiki mbili zilizopita—Man United, siyo tu ilivunja rekodi nyingine ya Arsenal ya kutokufungwa mara arobaini na tano katika uwanja wao wa nyumbani-Highbury- tangu ilipofungwa na Chelsea katika robo fainali ya ligi ya mabingwa mwaka jana, bali iliisukuma Arsenal katika nafasi ya tatu baada ya kufuta pengo la pointi kumi na moja tangu October mwaka jana.Man United iko mbele ya Arsenal kwa pointi mbili. Tukumbuke mwaka jana Arsenal ilizuiwa na Man United kufika fainali ya kombe la FA. Kama Arsenal wangeishinda Man United mechi iliyopita angalau wangeamsha hisia za ubingwa. Lakini Man United imehakikisha itabakia ndoto kwa Arsenal kuwa bingwa msimu huu.Naweza kusema Wenger ni kocha dhaifu hasa unapompima na Sir Alex Ferguson. Lililobakia sasa ni kumuondoa Wenger miongoni mwa makocha mahiri katika ligi ya Uingereza hasa katika mbinu na upikaji wa nidhamu ya wachezaji. Kwa sasa Alex tumpe wapinzani wapya. Wapo tayari wanajongea taratibu kuchukua nafasi ya Wenger: Jose Mourinho na Raphael Benitez tusubiri tuwaone.Kihistoria, Man United ina sifa ya kupangua pointi na kuifukuza timu iliyo mbele yake kama ilivyo Chelsea sasa. Tayari imemaliza pengo la pointi kumi na moja dhidi ya Arsenal na sasa shughuli ni kwa Chelsea. Kama Man United watatwaa ubingwa basi Alex atakuwa hana mpinzani.Ila Chelsea wakiutwaa kama inavyoelekea basi Morinho atakuwa ndio mpinzani mpya wa Sir Alex.
13/2/2005.

NITAKAVYOMKUMBUKA MT. VALENTINE.

Siku inayojulikana kama ya wapendanao inakaribia huku watu wakiwa na matarajio ya kila aina. Mipango ni mingi: mavazi gani siku hiyo, kununua kadi, kujumuika na wapenzi( wapendanao) katika kumbi na sehemu mbalimbali za starehe na wengine wanafikiria kufanya mapenzi siku hiyo.Haya yote ni kuikumbuka siku ya Mtakatifu Valentini, padri aliyekufa akijaribu kutoa maana mpya ya mapendo, alipochagua kufa kupinga amri ya mtawala dhalimu wa Roma-Claudis II. Huyu bwana aliamua kuoa mmoja wa wanawake waliokuwa wameathiriwa na amri ya mfalme wa Roma pale alipokataza wanaume wote wasioe kwani kapera walikuwa ni watu muhimu katika kampeni ya kivita iliyokuwa ikifanyika wakati huo. Aliuawa kwa kukatwa kichwa tarehe kumi na nne ya mwaka 269A.D.Katika barua zake nyingi alizoandika kwa mpenzi wake, alikuwa akizisaini kama: “Wako Valentini” na ndio hapo watu wameamua kuikumbuka siku hii kwa jina la Valentini kama mpenzi. Huyu bwana hakuwa na haja ya kuvaa nguo nyekundu; alikuwa na upendo wa dhati wala sio kutuma kadi au kula katika mahoteli makubwa ya kifahari. Tunaweza kuona alikuwa anafanya kazi ya Mungu katika kuwaondolea kiu ya mapenzi wanawake ambao walikuwa wameathiriwa na amri ya mfalme ya wanaume kukatazwa kuoa.Tukumbuke katika kumsaidia mwanamke shida kama hizi, sio tu katika masuala ya ngono ni pamoja na mambo yote yanayohusu familia kwa ujumla. Ndio maana kwangu siungi mkono hizi mbwembwe za watu leo hii. Kwani umaana wa Valentini ni kuonesha moyo wa kusaidia. Ingepaswa tuikumbuke hii siku kwa kusaidia watu au familia zenye shida.Kwangu siku hii haina tofauti na siku zingine. Nitatumia dakika moja kukaa kimya kumkumbuka huyu bwana alafu kama nina cha kutoa kusaidia maskikini nitafanya hivyo kila nitakapopaswa nitakapokuwa katika matembezi ya kawaida mitaani.
13/2.2003.

UGONJWA HATARI DUNIANI.

Dikteta wa miaka thelathini na nane, Gnassingbe Eyadema jumamosi iliyopita-5/2/2005 alifanikiwa kuweka rekodi nyingine ya kisiasa barani Afrika. Kwanza aliweka mtego mkali; akasubiri Spika wa Bunge la Togo, Fambare Natchaba Ouattara asafiri kwenda Ulaya kikazi basi na yeye akaamua kukata roho-kufariki. Hatua hii ililiwezesha Jeshi la Togo kufunga mipaka yote ya nchi ili Spika Ouattara ashindwe kurejea kushika hatamu kama katiba ilivyokuwa ikisema. Matokeo yake Faure Gnassingbe alipandikizwa na jeshi kumrithi Baba yake kama Raisi.Nimeitazama historia ya viongozi wa aina ya Eyadema, nikagundua tunao wengi sana duniani. Hawa wna tabia zinazofanana. Kwanza, wote wameongoza nchi zao kwa zaidi ya miaka ishirini. “Kiongozi mkuu” wa Korea ya Kaskazini-Kim II-Sung alifariki 1994 baada ya kuongoza kwa miaka thelathini na nane kama Eyadema. Alimrithisha mwanaye “Kiongozi Mpendwa”-Kim Jong II.Yupo Hafidhi Al-Assad wa Syria aliyefariki mwaka 2000 baada ya kuongoza kwa miaka thelathini. Mwanaye Bashar Al Assad alimrithi alipofariki; na inasemekana hakuwa amemuandaa bali ni baada ya kufariki kwa aliyekuwa ameandaliwa-Basil Assad hapo mwaka 1994.Kuna Hosni Mubarak wa Misri ameshakaa madarakani kwa miaka ishirini na nne; naye pia tayari amemuandaa mwanaye wa kiume –Gamal Mubarak. Ukienda Libya—Kanali Gaddafi baada ya kutawala kwa miaka thelathini na sita, kijana wake wa kiume Saif al-Islam anasubiri baba afariki naye atwae madaraka.Upo mradi wa kurithisha madaraka watoto ulishindwa huko Iraq mwaka jana. Dikteta Sadaam Hussein alishamuandaa mwanaye –Uday- kumrithi lakini rais wa Marekani katika kampeni ya kutafuta silaha za maangamizi ilifyeka kabisa wanawe Sadaam.Nafikiri majeshi ya Marekani yaliwafananisha wanawe Sadaam na silaha za maangamizi.Je ni kwanini tuna viongozi wa namna hii? Mimi nadhani ni viongozi wanaosumbuliwa na ugonjwa unaoitwa “Eyadema”.Hawa ni watu waliolewa na madaraka na wanatawaliwa na ndoto zinazowaonesha hisia watakapokuwa kaburini. Wanataka familia iendelee kulinda mali walizoiba kwa muda mrefu madarakani. Na ndio maana huu mradi hauwajali watoto wa kike. Kwani wanaweza kuolewa na utajiri ukahamia kwa familia nyingine.Hapa kwetu Tanzania, ukitizama kwa kina inatia shaka sana. Huu mradi nahisi upo na tunapoelekea katika uchaguzi mkuu ni lazima tuchague mtu asiye na hata chembe za kuuendeleza. Manake nikiangalia Zanzibar tunaye Karume; ukija katika kabineti ya raisi Mkapa yupo Hussein Mwinyi—mwanaye mzee rukhsa; Bungeni tunao Rose Mary Nyerere na Makongoro Nyerere. Swali: Wamepanda ngazi za kisiasa hadi kufikia hapa kwa nia nzuri au ni katika kutekeleza huu mradi wa viongozi niliowaelezea hapo awali? Yaani wenye ugonjwa wa Eyadema—“Eyadema disease”.
13/2/2005.

KLABU MAARUFU YA MARAISI AFRICA


Naanza kwa kutoa buriani kwa hayati Gnansibe Eyadema aliyetutoka mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuwakandamiza wananchi wa Togo kwa miongo isiyopungua minne. Niliposikia juu ya kifo cha huyu bwana sikusikitika nikiwa kama mpenda demokrasia.Ingawa natambua wajibu kama mwaafrika ni lazima niheshimu marehemu. Hasira zangu ziliongezeka pale nilipobaini eti mwanaye kamrithi kama Raisi wa Togo. Umoja wa Afrika umelaani kitendo hiki na hapa nimpongeze rais wake, Alfa Konare, kwa ujasiri.Leo nataka nieleze kwamba ukiacha Swaziland, Moroko na Lesotho ambazo ni nchi chini ya himaya za kifalme, ziko nchi ambazo kimantiki ni sawa tu na za kifalme ingawa zina chaguzi kila baada ya kipindi fulani. Hapa nataka nijadili juu ya aina fulani ya viongozi waliopo hapa barani Afrika ambao wanafanana kitabia. Kwa maana nyingine wameunda timu (klabu) yao. Bahati nzuri Tanzania haina aina hii ya viongozi na hakuna dalili za kuwepo.Mojawapo ya wajihi wa wachezaji wa timu hii ni kwamba wanaongoza wananchi masikini wakati wao ni matajiri sana. Ni watu ambao kwao madaraka ni mpaka kifo ndio wataachia wengine. Uchaguzi ni wakati wa kuwadanganya wahisani kuwa kuna demokrasia. Hawapotezi uchaguzi hata siku moja. Wakishindwa uchaguzi ina maana hakuna demokrasia. Katika uchaguzi wowote, hawa hushinda ushindi wa aina yake. Hapa ndugu msomaji lazima usahau ile habari ya chama tawala nchini Tanzania—Ushindi wa Kishindo. Hawapati ushindi wa chini ya asilimia themanini na tano.Labda nitoe ufafanuzi zaidi: Hii timu sijui ni ya mchezo gani; lakini haina wachezaji wengi kwa sasa. Kwa mfano, ina watu kama ajulikanavyo na wananchi wake: Monsieur(monsie) Paul Biya wa Cameroon. Huyu amekuwa raisi tangu mwaka 1982 mpaka leo tangu alipomrithi Ahmadou Ahidjou aliyestaafu. Mwishoni mwa mwaka jana alichaguliwa kwa kipindi kingine cha miaka saba kama raisi. Mwingine ni Jenerali Lansana Conte wa Guinea ya Conakri. Alijipatia asilimia 95.6 katika uchaguzi wa mwaka 2003. Wiki mbili zilizopita aliponea kuuwawa na waviziaji. Ni mgonjwa kwa muda mrefu sasa; kuna kila dalili ndiye atakayemfuatia Eyadema kuzimu. Kabla ya uchaguzi inasemekana aliingizwa kwa baiskeli ya kukokotwa katika mkutano wa chama tawala na akapitishwa bila kupingwa kama mgombea uraisi. Baadaye iliripotiwa aliwaambia wajumbe kwamba: “Mmenichagua, kwahiyo endeleeni na yaliyobakia wenyewe.” Hapa alimaanisha kampeni: kwani hasingeweza kupiga kampeni kwani ingeongeza maumivu ya miguu yake. Amini usiamini alishinda kwa kishindo mwishoni bila hata ya kushiriki kampeni.Wengine katika klabu hii ni Jenerali Paul Kagame wa Rwanda, mchezaji mpya aliyejiunga na timu hii mwaka juzi baada ya kushinda uchaguzi kwa asilimia 95.1. Mwingine ni Dennis Sassou Nguesso wa Jamhuri ya Congo aliyeshinda uchaguzi mwaka 2002 kwa asilimia 89.4. Yupo pia hapa Ben Ali wa Tunisia ambaye baada ya kuzoea kushinda kwa asilimia 94 mwaka jana kama kipindi chake cha nne.Ukiacha wachezaji niliowataja wapo wengine ambao nao imani yao ni moja tu: “Uraisi ni taasisi ya kuongozwa na familia kutoka kizazi kimoja hadi kingine.” Kwao uchaguzi ni sehemu ya kuwaendeleza madarakani hadi kufa ambapo huwarithisha watoto wao. Hapa yuko Kanali Gaddafi wa Libya ambaye kwa sasa anamwaandaa mwanaye wa kiume Sayf al-Islam Gaddafi. Hosni Mubarak ambaye amekuwa madarakani tangu miaka ya sitini; kwasasa anamuandaa kijana wake wa kiume Gamal Mubarak kumrithi. Linalonisikitisha zaidi kwenye timu hii ni hasa kuhusu hapa kwetu Afrika ya Mashariki. Kuna kila dalili mmoja wa maraisi wa nchi moja atajiunga na timu hii siku za karibuni. Wakati ukiwadia nitawaambia; maajabu ni kwamba Robert Mugabe hayuko hapa. Huyu anasumbuliwa na ugonjwa wa kung’ang’ania madaraka bila sababu za msingi.Swali nililonalo ni hili: Jinsi timu hii ilivyo hatari kama silaha za maangamizi, kuna haja ya kuiangamiza. Je, itawezekana kweli? Mwenye jibu ajitose uwanjani; kwani nina wasiwasi hakuna njia ya kuondokana nayo. Nabakia nikiitazama hali ya Togo kwa siku kadhaa zijazo ndipo nitajua kama kweli waafrika tunaweza kujikwamua na timu hii. Generali Gnansibe Eyadema amefariki na kumrithisha mwanaye kama ilivyotarajiwa. Inakuwaje namna hii?Sipati jibu kabisa.
2/6/2005.

Tuesday, May 17, 2005

SERENGETI BOYS KATIKA STAILI YA KIMACHIAVELI.

Ilikuwa saa kumi na mbili na dakika hamsini na nane jioni, tarehe thelathini, siku ni jumapili, ninasikiliza kipindi cha michezo kupitia idhaa ya kiswahili ya redio BBC. Kiongozi mmoja wa zamani wa TFF anakanusha kabisa juu ya makosa yake kama mtendaji juu ya Tanzania kuondolewa katika michuano ya Kombe la vijana chini ya miaka kumi na nane.Anatoa kauli ya kijinga kabisa eti huu sio wakati wa kutafuta mchawi; ninajiuliza: hivi tusipomjua aliyefanya makosa haya, ni lini tutajirekebisha? Kwanini watanzania hatuna tabia ya kuwajibika? Hivi kweli huko TFF orodha za wachezaji wetu zinahifadhiwa katika teknolojia ya kisasa kweli? Sasa inawezekanaje Simba na TFF zipingane katika orodha ya wachezaji?Hisia zangu zinanituma kuamini kuwa staili ya maisha ya watanzania-uliberali wa hali ya juu- kama taifa leo hii ndiyo iliyotufikisha katika hali hii: Timu ya Taifa ya vijana—Serengeti Boys—inafuzu mashindano yatakayofanyika huko Gambia mwezi Mei isivyo halali, alafu inapigwa kumbo nje na shirikisho la mchezo wa soka barani Afrika-CAF. Ni habari iliyonisikitisha kwa upande mmoja na pia kunifurahisha kwa upande mwingine.Masikitiko ni kuwa tumejikuta wtanzania wote tulikuwa tunashangilia na kuchangia kitu haramu. Ni kitu haramu kwa misingi kwamba tulikuwa tunazionea timu zingine. Hivi hawa walioichagua timu hii walikuwa na lengo la kuinua kiwango cha mchezo huu nchini au kupata ushindi kwa njia yeyote ile. Mwanafalsafa Niccolo Machiavelli naweza kumtumia kumfananisha na viongozi wa michezo nchini Tanzania. Alisema: “Kufanikiwa maana yake ni kutekeleza malengo yako kwa njia yeyote itakayowezekana”. Alisahau kabisa kuwa kuna mipaka katika kila unalofanya. Na ni lazima uizingatie mipaka hiyo ili ufanikiwe.Bahati mbaya Tanzania, viongozi wetu wa michezo-soka-wengi ni wafuasi wa Kimachiavelli. Kung’ang’ana kupata matokeo mazuri bila kujali mipaka na njia madhubuti zinazostahili. Hivi kweli ile michango yote iliyokuwa ikikusanywa, tena na viongozi wakubwa tu kama Waziri Mkuu eti bila kuchunguza uendeshaji wa timu ulikuwa madhubuti au la; la kushangaza zaidi timu imekwenda Harare ikiambatana na viongozi wakubwa tu serikalini na wale wa TFF. Aibu gani hii, soka itaendelea kudorora kama hatutaachana na viongozi hawa wa kimachiaveli. Haya ndiyo masikitiko yangu.Upande wa furaha, ni kwamba huu ni wakati mwingine kwa watanzania kujifunza mabadiliko ya dunia ya kileo. Kuheshimu kanuni na kufanya kazi kwa misingi—kiprofeshenali. Hii mambo ya njia za mkato tusahau jamani. TFF natumaini hili ni darasa tosha. Labda nikumbushe: mwaka juzi huko Kenya, waziri wa michezo—Najib Balala—alilaumiwa sana na wananchi baada ya kuiomba FIFA iiondoe Kenya katika michuano ya kufuzu ya vijana baada ya Kenya kuiondoa Ghana kwa kutumia wachezaji waliozidi umri uliotakikana. Ilikuwa ni katika kuhakikisha rushwa inaondoka michezoni. Na kweli FIFA iliiondoa Kenya; wafuasi wa Machiavelli kama walivyo watanzania wengi wa leo walimwona waziri Balala kama msaliti.Tutakavyoendelea kufanya mambo mbalimbali bila kujali maadili na kanuni kadhaa basi huu mkasa wa Serengeti Boys ndio mwanzo wa mingine lukuki itakayofuata.
31/1/2005.

CHELSEA INA UHAKIKA WA UBINGWA HATA IJE MVUA AU JUA.

Wapenzi ama mashabiki wengi wa Arsenal na Man United hawafurahishwi kabisa na mtizamo wangu eti hawatavuna ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza msimu huu. Wengine—marafiki zangu—hapa wametishia kuacha hata kusoma makala zangu.John Tany, mnazi wa Arsenal pamoja na Richard-mnazi wa Man United wananiambia eti mwaka 1995—Newcastle iliongoza kwa point kumi mwezi Disemba-Boxing Day-lakini baadaye Man United iliipiku kwa point nne mwisho wa msimu na kulinyaua kombe. Mimi nimewajibu hivi: Man United wakati ule ilikuwa na mashine-Eric Cantona. Inasemekana ukiacha George Best, hajawahi kutokea mchezaji kama yeye Old Trafford.Wakati ule Newcastle ilikuwa na washambulizi mahiri: Asprila na Shearer walikuwa hawashikiki. Ila kwenye ngome ilikuwa ni ubwete sana. Nafikiri tunamjua Kevin Keagan, kocha asiyejua jinsi ya kujenga uwiano kati ya ngome na washambuliaji. Hili ni tatizo lake mpaka leo. Leo hii Man United haina Cantona wala anayefanana naye.Mwaka 1995/96, Newcastle iliruhusu nyavu zake kutikiswa mara arobaini. Chelsea imeruhusu magoli nane hadi sasa kukiwa bado michezo kumi na tano. Ni dhahiri kwa mechi zilizobakia, uwezekano wa Chelsea kufungwa magoli thelathini na mbili haupo. Hii ni timu iliyoonesha haiba ya bingwa, hatuwezi hata kidogo kuifananisha na Newcastle ya wakati ule kwani haikustahili ubingwa. Bingwa utafungwaje magoli arobaini?Pia tukumbuke Ferguson alimshinda Keagan kisaikolojia wakati ule alipoikandia Newcastle eti yeye pekee ndiye mwenye plani ya kucheza nayo na ataifunga. Kitendo hiki kiliwachanganya Newcastle na kocha wao. Na ni wazi kwa vita ya kisaikolojia, Mourinho ndiye bingwa msimu huu. Ferguson mwenyewe anamtetemekea. Ni mdhibiti na anatisha na amehimili kukurukakara zote za ligi ya primia.Ndiyo maana vita ya kisaikolojia imebaki kati ya Ferguson na Wenger. Hawazungumzi juu ya Chelsea sana. Kwani wamekwishakiri kugombea nafasi ya pili. Labda niungane na Mourinho kwa kusema: “Chelsea ina uhakika na ubingwa hata ije mvua au jua”.Wiki iliyopita amekaririwa akisema wiki iliyopita: “Itakuwa vigumu kutokushinda ubingwa msimu huu kwani ni lazima tushinde mechi kumi na moja kati ya kumi na tano zilizosalia. Wachezaji wangu wana ari; hawahitaji mimi kuwasukuma; wanayo imani binafsi ambayo ni ya nguvu sana”. Nakubaliana naye kabisa; kwani hii ni timu ambayo inalinda lango lake vizuri na inafunga magoli, tena sio machache. Ndio maana Morinho aliwahi kuikebehi Arsenal kuwa inaruhusu nyavu zake kutikiswa sana na akaifananisha na timu ya mchezo wa magongo-Hockey. Kwani kwake mpira wa kupendeza ni timu inayolinda maridadi na inayofunga magoli.Na hii ni Chelsea hadi sasa. Timu ambayo hadi sasa inawania makombe manne; tusubiri historia iandikwe kama haya yatatimia.
31/1/2005.

CHELSEA INA UHAKIKA WA UBINGWA HATA IJE MVUA AU JUA.

Wapenzi ama mashabiki wengi wa Arsenal na Man United hawafurahishwi kabisa na mtizamo wangu eti hawatavuna ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza msimu huu. Wengine—marafiki zangu—hapa wametishia kuacha hata kusoma makala zangu.John Tany, mnazi wa Arsenal pamoja na Richard-mnazi wa Man United wananiambia eti mwaka 1995—Newcastle iliongoza kwa point kumi mwezi Disemba-Boxing Day-lakini baadaye Man United iliipiku kwa point nne mwisho wa msimu na kulinyaua kombe. Mimi nimewajibu hivi: Man United wakati ule ilikuwa na mashine-Eric Cantona. Inasemekana ukiacha George Best, hajawahi kutokea mchezaji kama yeye Old Trafford.Wakati ule Newcastle ilikuwa na washambulizi mahiri: Asprila na Shearer walikuwa hawashikiki. Ila kwenye ngome ilikuwa ni ubwete sana. Nafikiri tunamjua Kevin Keagan, kocha asiyejua jinsi ya kujenga uwiano kati ya ngome na washambuliaji. Hili ni tatizo lake mpaka leo. Leo hii Man United haina Cantona wala anayefanana naye.Mwaka 1995/96, Newcastle iliruhusu nyavu zake kutikiswa mara arobaini. Chelsea imeruhusu magoli nane hadi sasa kukiwa bado michezo kumi na tano. Ni dhahiri kwa mechi zilizobakia, uwezekano wa Chelsea kufungwa magoli thelathini na mbili haupo. Hii ni timu iliyoonesha haiba ya bingwa, hatuwezi hata kidogo kuifananisha na Newcastle ya wakati ule kwani haikustahili ubingwa. Bingwa utafungwaje magoli arobaini?Pia tukumbuke Ferguson alimshinda Keagan kisaikolojia wakati ule alipoikandia Newcastle eti yeye pekee ndiye mwenye plani ya kucheza nayo na ataifunga. Kitendo hiki kiliwachanganya Newcastle na kocha wao. Na ni wazi kwa vita ya kisaikolojia, Mourinho ndiye bingwa msimu huu. Ferguson mwenyewe anamtetemekea. Ni mdhibiti na anatisha na amehimili kukurukakara zote za ligi ya primia.Ndiyo maana vita ya kisaikolojia imebaki kati ya Ferguson na Wenger. Hawazungumzi juu ya Chelsea sana. Kwani wamekwishakiri kugombea nafasi ya pili. Labda niungane na Mourinho kwa kusema: “Chelsea ina uhakika na ubingwa hata ije mvua au jua”.Wiki iliyopita amekaririwa akisema wiki iliyopita: “Itakuwa vigumu kutokushinda ubingwa msimu huu kwani ni lazima tushinde mechi kumi na moja kati ya kumi na tano zilizosalia. Wachezaji wangu wana ari; hawahitaji mimi kuwasukuma; wanayo imani binafsi ambayo ni ya nguvu sana”. Nakubaliana naye kabisa; kwani hii ni timu ambayo inalinda lango lake vizuri na inafunga magoli, tena sio machache. Ndio maana Morinho aliwahi kuikebehi Arsenal kuwa inaruhusu nyavu zake kutikiswa sana na akaifananisha na timu ya mchezo wa magongo-Hockey. Kwani kwake mpira wa kupendeza ni timu inayolinda maridadi na inayofunga magoli.Na hii ni Chelsea hadi sasa. Timu ambayo hadi sasa inawania makombe manne; tusubiri historia iandikwe kama haya yatatimia.
31/1/2005.

MAN UNITED NAYO HOI MSIMU HUU.

Niliwahi kuandika kwanini Arsenal haitashinda ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza msimu huu. Leo nataka kujadili juu ya wapinzani wao Manchester United. Hawa nao huu ni msimu mwingine bila ubingwa. Mosi, ni wazi katika sehemu ya kiungo—injini ya timu—imekufa kwa sasa. Roy Keane amezeeka; panahitaji damu mpya ili kuweza kulisha mipira ipasavyo sehemu ya ushambulizi hasa katika winga ambako kuna wachezaji wazuri sana.Sio tatizo la kiungo tu, bali Ferguson alifanya makosa sana pale alipotumia kiasi cha paundi milioni arobaini kuwanunua Lois Saha, Allan Smith na Wyne Rooney kwani mpaka sasa hawajalipa thamani ya pesa iliyowaleta Old Traford. Ulikuwa ni uamuzi mbovu zaidi ya ule wa kutumia paundi milioni thelathini kumnunua Veron kutoka Lazio mwaka 2001. Ili kukubaliana au kutokukubaliana na mimi, hebu fuatilia maelezo yangu:Alan Smith kwa miaka saba akiwa Leeds alifunga magoli thelathini na nane ya ligi, wastani wa magoli matano kwa msimu. Hainishangazi magoli machache alikwishaifungia Man United hadi sasa. Rooney aliyenunuliwa kwa paundi milioni ishirini, kipenzi cha waingereza, lakini sio mfungaji kiasili mwenye rekodi ya kuziona nyavu. Kwa misimu miwili akiwa Everton, alifunga magoli kumi na tano ambayo ni sawa na magoli saba kwa msimu. Idadi yake ya magoli kwa sasa hainishangazi kwani atabakia kuwa mfungaji wa mechi kubwa tu. Huyu ni mtu wa matukio makubwa. Kwahiyo, tunaweza kusema amesajiliwa kwa ajili ya mechi kubwa tu.Je kuhusu Louis Saha? Huyu angalau ni bora zaidi ya Rooney na Smith. Majeraha yamemzuia asifanye machojo. Akiwa Fulham alifunga magoli hamsini na tatu kwa misimu mine ikiwa ni magoli kumi na tatu kwa wastani. Sasa tunaweza kuona Ferguson alipokosea kununua wafungaji ambao hawajawahi kufikisha idadi ya magoli angalau kumi na tano kwa msimu kwenye ligi. Ukiacha Ruud Van Nilsterooy, hawa wanabaki kama wasaidizi wasiona sifa za kucheza na mchezaji wa kiwango cha Ruud. Man United inahitaji wachezaji wenye rekodi za ufungaji kama za ule ushirikiano wa akina Andy Cole na Dwight Yorke au ule mbadala wao wa akina Sheringham na Solsksjer.Nianze na Andy Cole: Alicheza Man United kwa misimu sita na akafunga magoli tisini na tatu ya ligi kwa wastani wa magoli kumi na tano kwa msimu. Pia alifunga magoli kumi na tisa katika ligi ya Mabingwa. Ikumbukwe kabla ya hapa alikuwa Newcastle ambapo alifunga magoli hamsini na tano kwa misimu miwili, yaani wastani wa magoli ishirini na saba kwa msimu. Huyu ndiye mfungaji kiasili(natural goal poucher). Mwenzake Dwight Yorke, kwa misimu mine aliifungia Man United magoli arobaini na saba ya ligi na kumi na mbili katika ligi ya mabingwa. Kabla ya hapo alikuwa Aston Villa ambapo alifunga magoli sabini na nane katika ligi.Nistelrooy tayari kafunga magoli sabini katika misimu mitatu. Magoli zaidi ya thelathini na tano katika kombe la mabingwa na mengine kumi na mbili katika kombe la FA. Kwa ujumla amefunga zaidi ya magoli mia moja kumi na tisa hadi sasa. Huyu anatimiza sifa za kuchezea Man United. Ila anahitaji mtu mwingine wa kujenga ushirikiano naye. Kama Ferguson ataliona hili na kutafuta jibu basi ndio ubingwa utaweza kupatikana. Ila kwa hali ilivyo sasa ni wazi ubingwa Man United inapaswa kusahau. Timu yenye hadhi kama hii inahitaji wafungaji haswa wenye sifa za kiasili. Sio hawa wa kubahatisha kama Rooney, Saha na Smith.
23/1/2005.

MAN UNITED NAYO HOI MSIMU HUU.

Niliwahi kuandika kwanini Arsenal haitashinda ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza msimu huu. Leo nataka kujadili juu ya wapinzani wao Manchester United. Hawa nao huu ni msimu mwingine bila ubingwa. Mosi, ni wazi katika sehemu ya kiungo—injini ya timu—imekufa kwa sasa. Roy Keane amezeeka; panahitaji damu mpya ili kuweza kulisha mipira ipasavyo sehemu ya ushambulizi hasa katika winga ambako kuna wachezaji wazuri sana.Sio tatizo la kiungo tu, bali Ferguson alifanya makosa sana pale alipotumia kiasi cha paundi milioni arobaini kuwanunua Lois Saha, Allan Smith na Wyne Rooney kwani mpaka sasa hawajalipa thamani ya pesa iliyowaleta Old Traford. Ulikuwa ni uamuzi mbovu zaidi ya ule wa kutumia paundi milioni thelathini kumnunua Veron kutoka Lazio mwaka 2001. Ili kukubaliana au kutokukubaliana na mimi, hebu fuatilia maelezo yangu:Alan Smith kwa miaka saba akiwa Leeds alifunga magoli thelathini na nane ya ligi, wastani wa magoli matano kwa msimu. Hainishangazi magoli machache alikwishaifungia Man United hadi sasa. Rooney aliyenunuliwa kwa paundi milioni ishirini, kipenzi cha waingereza, lakini sio mfungaji kiasili mwenye rekodi ya kuziona nyavu. Kwa misimu miwili akiwa Everton, alifunga magoli kumi na tano ambayo ni sawa na magoli saba kwa msimu. Idadi yake ya magoli kwa sasa hainishangazi kwani atabakia kuwa mfungaji wa mechi kubwa tu. Huyu ni mtu wa matukio makubwa. Kwahiyo, tunaweza kusema amesajiliwa kwa ajili ya mechi kubwa tu.Je kuhusu Louis Saha? Huyu angalau ni bora zaidi ya Rooney na Smith. Majeraha yamemzuia asifanye machojo. Akiwa Fulham alifunga magoli hamsini na tatu kwa misimu mine ikiwa ni magoli kumi na tatu kwa wastani. Sasa tunaweza kuona Ferguson alipokosea kununua wafungaji ambao hawajawahi kufikisha idadi ya magoli angalau kumi na tano kwa msimu kwenye ligi. Ukiacha Ruud Van Nilsterooy, hawa wanabaki kama wasaidizi wasiona sifa za kucheza na mchezaji wa kiwango cha Ruud. Man United inahitaji wachezaji wenye rekodi za ufungaji kama za ule ushirikiano wa akina Andy Cole na Dwight Yorke au ule mbadala wao wa akina Sheringham na Solsksjer.Nianze na Andy Cole: Alicheza Man United kwa misimu sita na akafunga magoli tisini na tatu ya ligi kwa wastani wa magoli kumi na tano kwa msimu. Pia alifunga magoli kumi na tisa katika ligi ya Mabingwa. Ikumbukwe kabla ya hapa alikuwa Newcastle ambapo alifunga magoli hamsini na tano kwa misimu miwili, yaani wastani wa magoli ishirini na saba kwa msimu. Huyu ndiye mfungaji kiasili(natural goal poucher). Mwenzake Dwight Yorke, kwa misimu mine aliifungia Man United magoli arobaini na saba ya ligi na kumi na mbili katika ligi ya mabingwa. Kabla ya hapo alikuwa Aston Villa ambapo alifunga magoli sabini na nane katika ligi.Nistelrooy tayari kafunga magoli sabini katika misimu mitatu. Magoli zaidi ya thelathini na tano katika kombe la mabingwa na mengine kumi na mbili katika kombe la FA. Kwa ujumla amefunga zaidi ya magoli mia moja kumi na tisa hadi sasa. Huyu anatimiza sifa za kuchezea Man United. Ila anahitaji mtu mwingine wa kujenga ushirikiano naye. Kama Ferguson ataliona hili na kutafuta jibu basi ndio ubingwa utaweza kupatikana. Ila kwa hali ilivyo sasa ni wazi ubingwa Man United inapaswa kusahau. Timu yenye hadhi kama hii inahitaji wafungaji haswa wenye sifa za kiasili. Sio hawa wa kubahatisha kama Rooney, Saha na Smith.
23/1/2005.

WASOMI CHANZO CHA SIASA ZA UOZA TANZANIA.

Mwaka 2005 umeanza na matukio ya kushangaza kiaina. Yaani mabaya na mazuri. Libaya kabisa ni lile la Tsunami mwisho mwa mwaka jana ambalo athari zake bado zinatesa watu hadi sasa. Zuri kwangu ni kutoka Zimbabwe ambapo Raisi, kichwangumu, jeuri ya wazungu, mwenye siasa za Kimachiavelli, Robert Mugabe, ameamua kuanza kumtenga kisiasa waziri wake wa habari, swahiba, Jonathan Moyo.Profesa Moyo ni msomi haswa, ambaye amefunza vyuo mbalimbali huko kusini mwa Afrika miaka ya nyuma. Lakini baadaye alijiingiza katika mchizo wa siasa za Mugabe na akawa moja ya nguzo muhimu katika ukandamizaji hasa wa uhuru wa vyombo vya habari. Nataka nimfananishe huyu bwana na ubumbuwazi unaowakumba wasomi wengi nchini Tanzania kwa sasa. Ubumbuwazi huo ni ile hali ninayoiona ambapo wasomi wanalazimika kujiunga na siasa na kuacha taaluma zao. Hii inawabidi kushirikiana na kuunga mkono utawala wa serikali hata pale inapokosea ili kuganga njaa zao; yaani, kupata mkate na siagi badala ya kusimama kidete kwa kutumia ujuzi wao kutetea wanyonge.Nimesema hivi nikiangalia jinsi bunge la Tanzania lilivyojaa wasomi wengi lakini utashangaa kazi yao kubwa ni kupiga makofi na kupitisha baadhi ya sheria zisizosaidia wananchi. Mara nyingine wanadiriki kuwazomea wapinzani pale ambapo wanajaribu kutetea maskini wa nchi yetu. Matokeo ya hali hii kambi ya upinzani Tanzania ni dhaifu, haina wanazuoni kwani ni dili kisiasa kujiunga na Chama tawala. Jamani dhamira haiwasuti akina Profesa…, Dokta….?Nirejee kwa Profesa Moyo, kama tujuavyo elimu na ujinga ni sawa na mafuta na maji. Kutokana na elimu yake, Profesa Moyo alijikuta akijitengenezea jeneza lake mwenyewe la kisiasa. Pale alipojaribu kuhoji hatua ya Mugabe kumteua mwanamama—Joyce Muguru—kama Makamu wa Raisi. Jamani mnajua kafanywaje huyu? Kuna uchaguzi wa bunge mwezi wa tatu. Ugombea wake kwa kiti cha ubunge kwa tiketi ya ZANU-PF umebatilishwa. Na ameondolewa katika nyadhifa zote za juu kichama. Masikini sijui atajiunga upinzani ama itakuwaje. Manake awali alikuwa akiwadhibiti sana wapinzani. Na hapendwi kabisa kambi ya upinzani.Basi tukiwa tunaelekea katika uchaguzi mwaka huu Tanzania, nawaomba wasomi wote watakaoenda Bungeni: Nina wasiwasi na aina ya wasomi nchini Tanzania, si jasiri wala wapambanaji; ni wanafiki na waoga sana. Hii tabia ya kufyata mkia kwa ajili ya kuganga njaa muache jamani. Ni njia hiyo tu itakayotuletea maendeleo nchini mwetu—kidemokrasia na kiuchumi.
23/1/2005.

GORDON BROWN- UKOLONI MWINGINE AFRIKA.

Waziri wa fedha wa Uingereza, Gordon Brown, hivi majuzi alitembelea Tanzania. Imeripotiwa ni katika juhudi za nchi yake kuzipunguzia madeni nchi masikini hata akaweza kusaini makubaliano ya kusamehe deni la nchi yetu kwa kiasi fulani. Binafsi ninatiwa shaka sana na juhudi hizi za waingereza: Huu ni utapeli mwingine wa wazungu; wanajaribu kutupumbaza tufikiri wanatujali sana. Uongo mtupu, hivi ni mikataba na misamaha mingapi ya kupunguza deni la Tanzania na nchi nyingine masikini imewahi kusainiwa? Jibu—imekuwepo mingi lakini deni limekuwa likiongezeka. Leo ni mwaka 2005, thamani ya deni letu leo hii, baada ya miaka mitano takwimu zitaongezeka.Hebu fuatilia hadithi hii: Ni imani iliyojikita mioyoni mwetu—waafrika—kihistoria kuwa madini, mafuta au dhahabu na demokrasia haviendi pamoja hata siku moja. Ukiacha nchi chache za Ulaya kama Norway inayotegemea kiasi kikubwa cha pato lake la taifa kutokana na mafuta na gesi. Nchi nyingine zaidi ya hizi ni udicteta tu uliotawala na unachangia madhila mbalimbali ya masikini.Hii waingereza wanaita ‘laana ya madini’(minerals curse). Yaliyokwishatokea na yanayoendelea kutokea kwa mfano, Sierra Leone, Angola, Guinea ya Ikweta, Mashariki ya Kati na pia katika Sovieti ya zamani-Kazakhstan ni dhihirisho.Ukweli ni kuwa pale viongozi wa kisiasa wanapogundua kuwa tegemeo la mapato ya taifa-kodi-lipo kwenye mafuta au madini na sio kutoka kwa walipa kodi-wananchi, wanakuwa mbali na wananchi waliowachagua. Kwa maana nyingine wanakuwa madikteta wa kiaina. Hi inanifanya niamini uwepo wa mafuta au madini katika nchi ni laana. Ndio maana mimi ni mmoja wa waaminio huu uchimbaji madini Tanzania usipowekewa usimamizi mzuri utatuletea matatizo. Je tusubiri hii laana itufike?Imani yangu ni kwamba moja ya sababu kuu kwanini serikali ya awamu ya tatu japo imefanikiwa kiuchumi, imepata upinzani sana katika utekelezaji wa baadhi ya sera zake na ikaonekana kutekeleza baadhi ya mambo kinyume na mategemeo ya wananchi: ununuzi wa rada, ndege ya raisi, ubinafsishaji wa Tanesco, Benki ya NBC na pia kampuni ya simu-TTCL. Hii yote ni kwasababu ya utegemezi badala ya kujitegemea.Kwa mfano, kiuongozi, Tanzania imeongozwa katika staili karibu sawa na ile ya zile nchi zilizokwishaangukiwa na balaa hilila laana ya rasilimali niliyoeleza awali. Katika nchi hizi raisi anaingia mkataba na makampuni ya kimataifa ya kibiashara kama Elf, Shell, Chevron au hata Anglo American na kuyategemea katika uendeshaji wa uchumi. Nchi kama Congo-Brazavile, Rais Paschal Lisouba alifikia mahali akawa anategemea kampuni ya Elf kulipa mishahara ya wafanyakazi. Katika hali kama hii: Ni Elf na sio wananchi watakaojaliwa na serikali yao walioichagua.Je Tanzania iko katika hali niliyoielezea? Labda niite hali hii”LAANA YA WAHISANI”—Donnor Curse. Miongoni mwetu watanzania tunajua Tanzania inaweza kukusanya pato lake kwa matumizi ya bajeti kwa asilimia 55% na inayobaki ni wafadhili.Na ndio hapa wahisani wanakuwa na sauti kwa serikali yetu. Mada yangu imekuwa ya hii laana ya utegemezi wa wafadhili ambayo umaana wa serikali katika nchi za dunia ya tatu haupo. Ndio maana najiuliza kama kweli hawa akina Brown na Blair wanatupenda, Uingereza ingefanya juhudi za kuwawajibisha waliosababisha deni hili. Alafu ilifute kabisa tuanze upya. Kwa hali ilivyo sasa ni kuwa tutakopa tena; tutafuja mkopo kwani tunajua hakuna kuwajibishwa.Binafsi niliona ziara ya huyu bwana kama ukoloni mpya ambapo Uingereza ikiwa mwenyekiti wa mataifa nane tajiri—G8—inahakikisha masikini watabakia masikini na wao-matajiri-wataneemeka zaidi siku za usoni. Kinyume na ilivyoripotiwa eti alikuja kutanzua tatizo la deni la Tanzania; lazima tukubali huyu bwana alikuja kuiongezea Tanzania deni. Kama hatuamini basi tusubiri watoto wa kizazi kijacho watasoma katika historia kwamba aliwahi kuja mzungu kusaini mikataba ambayo ilichangia umasikini nchini mwetu.Ndugu zanguni, siasa za leo ni masikini kujiuza kwa matajiri. Hatuna njia watanzania, tumekwisha, ndio basi tena.
23/1/2005.